Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu Maria,โฆ.
Ndimi Mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyonena. Salamu Maria, โฆโฆ Neno wa Bwana akatwaa Mwili, akakaa kwetu. Salamu Maria, โฆ..
Utuombee, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe:
Tunakuomba ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika, kwamba, Kristo Mwanao amejifanya mtu: kwa mateso na Msalaba wake, utufikishe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu, Amina.
Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria saba kwa kila teso.
TESO LA KWANZA
Mzee Simeoni aliagua kuwa Moyo wa Mama Maria utachomwa kwa upanga. Tuombe neema ya kuvumilia mateso. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA PILI
Maria na Yosefu walikimbilia Misri usiku ili kumficha Mtoto Yesu asiuawe na Herodi. Tuombe neema ili miili yetu iwe kimbilio lake Yesu. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TATU
Mama Maria aliona uchungu sana Mtoto Yesu alipopotea kwa siku tatu. Tuombe neema ya kudumu na Yesu mioyoni mwetu. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA NNE
Mama Maria aliona uchungu sana alipokutana na Mwanae Yesu katika njia ya Msalaba. Tuombe neema ya kudumu na Yesu siku zote. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TANO
Mama Maria aliona uchungu sana alipomwona Mwanae Yesu akisulibiwa Msalabani. Tuombe neema ya kufa mikononi mwa Yesu na Maria. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SITA
Mama Maria aliona uchungu sana alipopakata maiti ya Mwanae Yesu baada ya kushushwa Msalabani. Tuombe neema ya kutotenda dhambi. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SABA
Mama Maria aliona uchungu sana aliporudi nyumbani baada ya kumzika Mwanae Yesu Tuombe neema ya kitulizo kwa Mama Maria. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
Salamu Maria Umejaa neema Bwana yu nawe Umebarikiwa kuliko wanawake wote Na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa Maria Mtakatifu Mama wa Mungu Utuombee sisi wakosefu Sasa, na saa ya kufa kwetu. Amina.
Ee Mt. Yosefu, ambaye ulinzi wako ni mkubwa, wenye nguvu na wa haraka mbele ya Kiti cha Enzi cha Mungu, ninakukabidhi nia na haja zangu zote. Ee Mt. Yosefu, unisaidie kwa maombezi yako yenye nguvu, na unipatie kutoka kwa Mwanao Mungu, baraka zote za kiroho, kwa njia ya Kristu Bwana wetu, ili nikishapata msaada wako wa mbinguni ningali bado hapa duniani, niweze nami kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu aliye Baba mwema kabisa kushinda wote. Ee Mt. Yosefu, sichoki kamwe kufikiri moyoni kwa upendo, jinsi Mtoto Yesu alivyokuwa amesinzia mikononi mwako. Akiwa amepumzika hivyo karibu na moyo wako, sithubutu kujongea, nisije nikamsumbua, bali nakuomba wewe umkumbatie na kumbusu kwa niaba yangu na kumwambia anipe busu lake nitakapovuta pumzi yangu ya mwisho. Mtakatifu Yosefu Msimamizi wa wanaozimia roho; Utuombee. Amina.
Sala hii ilipatikana katika mwaka wa hamsini wa Bwana na Mwokozi Wetu Yesu Kristu. Mnamo mwaka 1505 Baba Mtakatifu alimtumia sala hii Mfalme Charles wakati alipokuwa anaenda vitani. Yeyote atakayeisoma sala hii, au kuisikia ikisomwa, au kuibeba, hatakufa kifo cha ghafla,hatazama majini, hatadhurika kwa sumu, wala hataanguka katika mikono ya adui zake, au kuunguzwa katika moto wowote ule, au kushindwa katika vita.
Sali sala hii kwa siku tisa mfululizo, kwa kuomba jambo lolote unalolihitaji. Haijawahi kusikika kuwa sala hii imeshindwa jambo.
Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Maria Bikira Milele, na mkubwa wa Familia Takatifu. Umechaguliwa na Mwakilishi wa Kristu kama Msimamizi wa kimbingu na mlinzi wa Kanisa alilolianzisha Kristu. Ndiyo maana ninakuomba kwa matumaini makuu usaidizi wako wenye nguvu kwa ajili ya Kanisa zima duniani.
Mlinde kwa namna ya pekee, kwa upendo wa kikweli wa ki-baba, Baba Mtakatifu na Maaskofu wote na Mapadre wenye ushirika na Kiti cha Petro. Uwe mlinzi wao wote wanaotumikia wokovu wa wanadamu kati ya majaribu na mahangaiko ya maisha haya, na utujalie kwamba watu wote wa dunia hii wamfuate Kristu na Kanisa alilolianzisha.
Mpendwa Mtakatifu Yosefu, ukubali majitoleo ya nafsi yangu ambayo sasa ninafanya. Ninajiweka wakfu kwako kwa ajili ya utumishi wako, ili daima wewe uwe baba yangu, mlinzi wangu, na kiongozi wangu katika njia ya wokovu. Unijalie usafi mkuu wa moyo na matamanio makuu ya maisha ya kiroho. Unijalie ili matendo yangu yote, kwa mfano wako, yawe kwa ajili ya sifa na utukufu wa Mungu, pamoja na Moyo wa kimungu wa Yesu, moyo safi wa Maria, na moyo wako wa ki-baba. Uniombee, nami nishiriki kifo chako cha furaha na kitakatifu. Amina.
Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe tegemeo langu na tumaini langu dhabiti. Ndiwe mwenye dawa ya maovu yangu yote, malipizi ya makosa yangu yote. Waweza kunipatia haja zangu na neema ninazoziomba mimi na wengine. Wewe uko ili kutusaidia sote, ndiwe mwanga mkuu usiozimika, ndiwe chanzo cha nguvu, uvumilivu, amani na faraja. Nina hakika kuwa maombi yangu hayatakuchosha, nawe hutaacha kunisaidia, kunilinda, kunipenda, kwani, ee Moyo Mtakatifu , upendo wako hauna mwisho. Ee Moyo Mtakatifu, unihurumie, kwa ajili ya maombi yangu, kadiri ya huruma yako. Nawe katika sisi, na kwa ajili yetu, ufanye lolote unalolihitaji, kwani tunajitoa kwako kwa imani na uhakika thabiti kwamba kamwe hautatuacha, kwa milele. Amina.
Mwongozo wa namna ya Kusali Rozari Takatifu ya Mama Bikira Maria
Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba ukiwa unasema โKwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Aminaโ.
Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, โTusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote, na tuunganishe nia hizo na nia zetu sisi wenyewe, nk).
Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu.
Mojawapo ya maneno yafuatayo huweza kutumika: โMungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, โฆโฆ Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, โฆโฆ Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, โฆ..โ
Au;
โUtuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,โฆ. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,โฆ. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, โฆ..โ Au; โSalamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,โฆ.. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,โฆ.. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,โฆโฆโ Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina.
Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi. Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef.
Kisha endelea na sala zinazofuata kama mpangilio unavyoonyesha hapo juu.
Kila baada ya Tendo moja na makumi ya Salamu Mariaโฆ, โAtukuzwe..โ, โEe Yesu wanguโฆโ na โTuwasifu mileleโฆโ kama muda unatosha wimbo ufaao wa Bikira Maria uimbwe (kama muda ni mfupi basi angalau ubeti mmoja mmoja uimbwe kila baada ya makumi hayo). Baada ya Wimbo, Tendo linalofuata litangazwe kwa sauti pamoja na tafakari fupi au ombi linaloambatana na Tendo husika kama inavyoonyeshwa hapa chini.
MATENDO YA ROZARI TAKATIFU
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuungโarisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA YA BIKIRA MARIA
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utusikie
Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni,โฆโฆ Utuhurumie
Mungu Mwana Mkombozi wa dunia โฆโฆโฆ Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu โฆโฆ.. Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja โฆโฆ.. Utuhurumie
Maria Mtakatifu โฆโฆโฆ. utuombee
Mzazi Mtakatifu wa Mungu โฆโฆ.. utuombee
Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira โฆโฆ.. utuombee
Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utusikilize ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utuhurumie.
Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,โฆโฆโฆโฆ..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utusikilize ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utuhurumie.
Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,โฆโฆโฆโฆ..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yesu./ Jina la yule msaliti aliyemwuza Yesu/ limewafanya wengi wakusahau./ Walakini Kanisa zima linakuheshimu/ na kukuomba kama Msaidizi katika mashaka makubwa,/ na katika mambo yasiyo na matumaini tena./
Uniombee mimi mnyonge./ Ninaomba utumie uwezo ule uliojaliwa/ wa kuleta upesi msaada kwa watu walioukosa./ Unisaidie sasa katika mahitaji yangu,/ ili nipate kitulizo na msaada wa mbinguni/ katika lazima zangu,/ masumbuko na mateso,/ hasa/ (taja shida yako)./ Pia ili niweze kumsifu Mungu nawe na wateule wote milele./
Mtakatifu Yuda Tadei,/ utuombee,/ na uwaombee watu wote wanaokuheshimu na kukuomba msaada./
Moyo Mtakatifu wa Yesu,/ Rafiki mpenzi wa Yuda Tadei,/ nakutumainia./
(Mwisho Sali: Baba yetu (x3), Salamu Maria (x3) na Atukuzwe(x3).
Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya shetani, Mungu amtiishe, tunaomba sana, nawe Mkuu wa Majeshi ya Mbinguni kwa nguvu ya Mungu uwaangushe motoni shetani na pepo wabaya wengine wote, wanaozunguka duniani, ili kuzipoteza roho za watu.ย Amina.
(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi) Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na mwili wangu, nikikuomba uipokee amana yangu, kuitunzia ulinzi mwema ulinzi bora, ninakuaminia na kila neno langu, matumaini na kitulizo na kisongo chote, na masumbuko na uzima na ukomo wa uzima wangu: nitakayo ndiyo unifanyizie kwa maombezi na stahili zako, ili mambo yangu yote yapate kuongoka, yakiwa na kufuata mapenzi yako, pamoja na mapenzi ya Mwanao. Amina.
Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na Mungu wangu/ ambaye ninasadiki kuwa upo hapa/ katika Sakramenti Takatifu ya Altare;/ pokea kitendo hiki cha kukuangukia kifudi fudi/ kama ishara ya tamaa niliyonayo ya kukuabudu Wewe/ bila kuchoka/ na kukushukuru kwa mapendo yako makubwa/ yasiyo na kipimo/ ambayo Moyo wako Mtakatifu sana/ unawaka katika Sakramenti Takatifu hii./ Siwezi kukushukuru vizuri zaidi/ kuliko kama ningetolea kwako/ matendo yangu yote ya kukuabudu/ unyenyekevu wangu/ uvumilivu na mapendo/ ambayo huu Moyo Mwabudiwa ulifanya,/ bado unafanya/ na utaendelea kufanya katika uzima wa milele mbinguni./ Ninaahidi kupitia Moyo huu,/ nitakupenda,/ nitakutukuza,/ na nitakuabudu kama nitakavyoweza./ Ninajiunganisha na hii Sadaka Takatifu/ ambayo unatoa kwa Baba Mungu/ na ninatolea kwako utu wangu./ Ninakuomba kuangamiza ndani yangu/ dhambi zote pamoja na majeraha yake/ na usikubali kunitenga nawe milele./ Amina.
Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi,/ mwumba mbingu na dunia./ Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee, Bwana wetu;/ aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu,/ akazaliwa na Bikira Maria,/ akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato,/ akasulubiwa, akafa, akazikwa,/ akashukia kuzimu;/ siku ya tatu akafufuka katika wafu;/ akapaa mbinguni;/ amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi;/ toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,/ Kanisa takatifu katoliki,/ ushirika wa Watakatifu,/ maondoleo ya dhambi,/ ufufuko wa miili,/ uzima wa milele. Amina.
Please note that AckySHINE Swahili Website is not active.ย
Because of unavoidable circumstances AckySHINE Swahili Website will not be updated starting from May 2018. No new post will be published from May 2018.
However, You can view/read old pages (public pages) which were created before May 2018 and shared to public.
With hundreds of old public pages, we believe Swahili Website service can still be useful to the public users.
AckySHINE is a Platform that support provision of both Online and Offline Services.
We provide the following Services
Research Consultancy– Active Offline Service We offer consultation services in Research, including research concept development, designing, data collection and processing and report writing.
Monitoring and evaluation Consultancy– Active Offline Service We offer consultation services in M&E Planning, Process Evaluation and In Impact Evaluation.
Training and facilitation Consultancy– Active Offline Service We offer consultation services inย Training and Facilitation. This include Training Planning, Session Plan and Management as well as Conduction of Training andย facilitationย session.
English – Swahili Translationย services– Active Offline Service We translate Short Texts, Documents and webpage from English to Swahili and vise versa. We provide live human support, translation is done by native speaking translators, no automatic translation.
Web designing and development– Active Offline Service We offer WordPress Set up service and Customization Services. Free Templates, SEO optimization, One Year Assistance, Responsive Design, Mobile Friendly.
AckySHINE Dedications– Pending Online Service This is a special place for sendingย dedicationsย to the person you love. Via WhatsApp and SMS.
AckySHINE Shop– Pending Online Service This is anย Digital shopping serviceย aim at sharing of knowledge and skills through soft copy books.
AckySHINE Library– Pending Online Service Welcomeย AckySHINE Libraryย where you can get unlimited Books. Feel Free to Download our Books.
English Website– Pending Online Service This isย English multi-category websiteย special designed for information, entertainment and motivation
Swahili website– Pending Online Service This isย Swahili multi-category websiteย special designed for information, entertainment and motivation
Advertising and marketing– Active Online Service We Display banner, image & links on our website. For ads we offer freeย translationย (English to Swahili), free Landing page, you can embed forms on your landing page and embed HTML Codes. You can also publish your posts on our website with unlimited words, unlimited pictures, unlimited videos and free translation service. Your posts will be intergraded in post categories.
Monitoring and Evaluation Consultancy
[rpt name=”m-e-consultancy”]
My Downloads
[woocommerce-my-downloads]
Welcome AckySHINE Charity
AckySHINE charity is a program for humanitarian campaigns and aid aimed at promoting peace and unity, protecting the environment, and maintaining the health and development of individuals and the community as a whole. These campaigns are advertised through ackyshine.com.
“๐Kitabu cha Mbinu za Kilimo Bora Cha Mboga๐ฟ๐ ” has been added to your cart. View cart
Login
Register
AckySHINE Development Changelog
Welcome AckySHINE, We are still developing AckySHINE platform. Almost all services are not available for now because of reprogramming state. However, some services might be available from time as we are occasionally testing our services before full launching. We are sorry for any inconvenience.
Share your ideas and suggestions for our services here. We will be happy to hear from you.
Because of unavoidable circumstances this website (ackyshine.com) will not be updated starting from May 2018 till further notice.
No new post will be published. However you can only view/read old pages (public pages), which are pages created before May 2018 and shared to the public.
With thousands of old public pages, this website can still be useful and active to the public users.
Contact Me
Hey, Awesome Friend!
Thanks for reaching out! Send me a message on WhatsApp via the link below or email through the form. I prefer messages over calls, so please avoid calling. Thanks!
We, the Operators of this Application, provide it as a public service to our users.
Terms of Use
Please carefully review theย Terms of Use that govern your use of the Application and Website. Please note that your use of the Application constitutes your unconditional agreement to follow and be bound by these Terms and Conditions of Use. If you (the “User”) do not agree to them, do not use the Application, provide any materials to the Application or download any materials from it.
Privacy Policy
Theย Privacy Policy explains what we may do, and will not do, with your personal data that might be collected while you use this application and its services. Please read this policy and if you do not agree with it, please do not use this application or any of the services on it.
Further
If you have questions regarding these policies pleaseย contactย us.
AckySHINE is a consultancy office operating in Tanzania and providing professional services in the areas of Community development issues, Social science research and Project planning, monitoring and evaluation.
Main Consultation Services
Research methodology
Research Design/Planning
Data collection
Data Processing and analysis
Project/Programme management and evaluation
(M&E) Monitoring and Evaluation Project/Programme
Planning and implementation
Web design and Development
And Other relating services
You are Always Welcome
We are well placed to ensure optimum solutions for numerous clientsโ projects. We prefer a relationship based on mutual trust, co-operation, and communication
For us, the trust between the consultant and client is paramount. Enjoy the friendly atmosphere of his office when visiting.
Recent Comments