Kwa jina la Baba…..
Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu.
Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,Mwana na Roho.
Nilinde tena siku hii,niache dhambi nikutii.Naomba sana Baba wee, baraka yako nipokee.
Bikira safi, Ee Maria nisipotee nisimamie.
Mlinzi mkuu malaika wee kwa Mungu wetu niombee,nitake nitende mema tu na mwisho nije kwako juu.Amina.
NIA NJEMA.
Kumueshimu Mungu wangu,namtolea roho yangu.
Nifanye kazi nipumzike ,amri zake tu nishike.
Wazo,neno,tendo lote namtolea Mungu pote Roho,Mwili chote changu.
Pendo na uzima wangu.
Mungu wangu nitampenda wala dhambi sitatenda.
Jina lako nasifia,utakalo hutimia kwa utii navumili.
Teso na matata pia,nipe Bwana neema zako, niongeze sifa yako.Amina.
SALA YA MATOLEO.
Ee Yesu kwa mikono ya Bikira Maria,na kwa maungano na sadaka yako kuu.
Ninakutolea sala,matendo,masumbuko na furaha zangu zote za leo.
Ee Yesu ufalme wako utufikie.Amina.
BABA YETU.
Baba yetu uliye mbinguni,jina lako litukuzwe.
Ufalme wako ufike.Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku.Utusamehe makosa yetu,kama tunavyo wasamehe na sisi waliyo tukosea.
Usitutie katika kishawishi,lakini utuopoe maovuni.Amina.
SALAMU MARIA.
Salamu Maria,umejaa neema Bwana yu nawe,umebarikiwa kuliko wanawake wote,na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria mtakatifu Mama wa Mungu,utuombee sisi wakosefu sasa na saa ya kufa kwetu.Amina.
KANUNI YA IMANI.
Nasadiki kwa Mungu,Baba Mwenyezi,muumba mbingu na dunia.
Na kwa Yesu Kristu Mwanaye wa pekee,Bwana wetu aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu,akazaliwa na Bikira Maria,akateswa kwa mamlaka ya ponsyo Pilato,akasulibiwa, akafa,akazikwa,akashukia kuzimu siku ya tatu akafufuka katika wafu, akapaa mbinguni amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi,toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu.
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,kanisa takatifu katoliki ushirika wa Watakatifu,maondoleo ya dhambi,ufufuko wa miili na uzima wa milele.Amina.
AMRI ZA MUNGU.
1.Ndimi Bwana Mungu wako,usiabudu miungu wengine.
2.Usilitaje bure jina la Mungu wako.
3.Shika kitakatifu siku ya Mungu.
4.Waheshimu Baba na Mama upate miaka mingi na heri duniani.
5.Usiue.
6.Usizini.
7.Usiibe.
8.Usiseme uwongo.
9.Usitamani mwanamke asiye mke wako.
10.Usitamani mali ya mtu mwingine.
AMRI ZA KANISA.
1.Hudhuria misa takatifu domonica na sikukuu zilizo amuliwa.
2.Funga siku ya jumatano ya majivu,usile nyama siku ya Ijumaa kuuu.
3.Ungama dhambi zako walau mara moja kwa mwaka.
4.Pokea Ekarist takatifu hasa wakati wa Pasaka
5.Saidia kanisa katoliki kwa zaka.
6.Shika sheria katoliki za ndoa.
SALA YA IMANI.
Mungu wangu,nasadiki maneno yote linayo sadiki na kufundisha kanisa katoliki la Roma kwani ndiwe uliye fumbuliwa hayo,wala hudanganyiki na wala hudanganyi.Amina.
SALA YA MATUMAINI.
Mungu wangu,natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristu,neema zako duniani na utukufu mbinguni.Kwani ndiwe uliyeagana hayo nasi nawe mwamini.Amina.
SALA YA MAPENDO.
Mungu wangu,nakupenda zaidi ya chochote, kwani ndiwe mwema ndiwe mwenye kupendeza.
Nampenda na jirani yangu kama nafisi yangu kwa ajiri yako.Amina.
SALA YA KUTUBU.
Mungu wangu,nimetubu sana dhambi zangu kwani ndiwe mwema,ndiwe mwenye kupendeza wachukizwa na dhambi.
Basi sitaki kukosa tena nitafanya kitubio,naomba neema yako nipate kurudi.Amina.
SALA KWA MALAIKA MLINZI.
Malaika mlinzi wangu,unilinde katika hatari zote za Roho na za Mwili.Amina.
MALAIKA WA BWANA.
K.Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria.
W.Naye akapata mimba kwa Roho mtakatifu.
Salamu Maria…..
K.Ndimi mtumishi wa Bwana.
W.Nitendewe ulivyo nena.
Salamu Maria…..
K. Neno la Mungu akatwaa Mwili.
W. Akakaa kwetu.
Salamu Maria….
K. Utuombee Mzazi Mtakatifu wa Mungu.
W. Tujaliwe ahadi za Kristu.
Tuombe.
Tunakuomba Ee Bwana utie neema yako mioyoni mwetu ili sisi tuliyojuwa kwa maelezo ya malaika kwamba, Kristu mwanao amejifanya mtu kwa mateso na msalaba wake.
Tufikishwe kwenye utukufu wa ufufuko.
Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu.Amina.
ATUKUZWE BABA.
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,kama mwanzo na sasa na siku zote na milele.Amina.
K. Moyo Mtakatifu wa Yesu
W.Utuhurumie.
K. Moyo safi wa Bikira Maria.
W. Utuombee.
K. Mtakatifu Yosefu.
W. Utuombee.
K. Watakatifu somo wa majina yetu.
W. Mtuombee.
K.Watakatifu wote wa Mungu.
W.Mtuombee.
Kwa jina la Baba…..
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
🙏🌟 Mungu akujalie amani
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Endelea kuwa na imani!
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
Amina
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu akubariki!
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
Imani inaweza kusogeza milima
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mwamini Bwana; anajua njia
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Baraka kwako na familia yako.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie
Rehema hushinda hukumu
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
🙏❤️ Mungu akubariki
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
Wakati wa Mungu ni kamilifu
🙏💖 Nakusihi Mungu
🙏💖 Nakushukuru Mungu
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Katika imani, yote yanawezekana
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
🙏💖💫 Mungu ni mwema
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
🙏🌟 Mungu alete amani
Nakuombea 🙏
🙏🌟 Mbarikiwe sana
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Neema na amani iwe nawe.
Rehema zake hudumu milele
Tumaini ni nanga ya roho
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
🙏🙏🙏
Sifa kwa Bwana!
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Mungu ni mwema, wakati wote!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
🙏✨ Mungu atupe nguvu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mwamini katika mpango wake.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Neema ya Mungu inatosha kwako
Dumu katika Bwana.
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
🙏🙏🙏
Tembea kwa imani, si kwa kuona
🙏✨ Mungu atakuinua
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu