Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi,/ mwumba mbingu na dunia./ Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee, Bwana wetu;/ aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu,/ akazaliwa na Bikira Maria,/ akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato,/ akasulubiwa, akafa, akazikwa,/ akashukia kuzimu;/ siku ya tatu akafufuka katika wafu;/ akapaa mbinguni;/ amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi;/ toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,/ Kanisa takatifu katoliki,/ ushirika wa Watakatifu,/ maondoleo ya dhambi,/ ufufuko wa miili,/ uzima wa milele. Amina.
Ee uliye Mkuu, Mt. Yosefu, uliyatii kabisa maongozi ya Roho Mt. Unijalie neema ya kufahamu aina ya maisha ambayo Mungu anapenda mimi niishi. Usiniache nidanganyike katika jambo muhimu kama hili, ambalo furaha yangu hapa duniani inalitegemea, na hata pia wokovu wa roho yangu.
Unijalie, nikiangazwa na matakwa matakatifu na nikiwa mwaminifu katika kuyatimiza, nikumbatie aina ya maisha ambayo Mungu ameniandalia na yatakayoniongoza kwenye furaha ya milele. Amina.
Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina.
Ee Utatu Mtakatifu wa Mwenyezi Mungu, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, nasadiki kuwa upo hapa na mahali pote. Ee Mungu wangu, umeniumba, umenikomboa, umenifanya mkristo, umenizidishia neema zako hapa duniani, umenitayarishia makao yangu mbinguni, umenijalia na siku hii nikutumikie. Ee Mungu wangu! Nakuabudu, nakushukuru, nakuomba toba, nakupenda! Ee Mungu wangu, nakutolea roho yangu, na mawazo, na maneno, na kazi, na furaha, na mateso yangu: uyapokee unipe neema yako nisikutende leo dhambi!
Mwongozo wa namna ya Kusali Rozari Takatifu ya Mama Bikira Maria
Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba ukiwa unasema โKwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Aminaโ.
Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, โTusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote, na tuunganishe nia hizo na nia zetu sisi wenyewe, nk).
Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu.
Mojawapo ya maneno yafuatayo huweza kutumika: โMungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, โฆโฆ Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, โฆโฆ Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, โฆ..โ
Au;
โUtuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,โฆ. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,โฆ. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, โฆ..โ Au; โSalamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,โฆ.. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,โฆ.. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,โฆโฆโ Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina.
Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi. Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef.
Kisha endelea na sala zinazofuata kama mpangilio unavyoonyesha hapo juu.
Kila baada ya Tendo moja na makumi ya Salamu Mariaโฆ, โAtukuzwe..โ, โEe Yesu wanguโฆโ na โTuwasifu mileleโฆโ kama muda unatosha wimbo ufaao wa Bikira Maria uimbwe (kama muda ni mfupi basi angalau ubeti mmoja mmoja uimbwe kila baada ya makumi hayo). Baada ya Wimbo, Tendo linalofuata litangazwe kwa sauti pamoja na tafakari fupi au ombi linaloambatana na Tendo husika kama inavyoonyeshwa hapa chini.
MATENDO YA ROZARI TAKATIFU
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuungโarisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA YA BIKIRA MARIA
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utusikie
Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni,โฆโฆ Utuhurumie
Mungu Mwana Mkombozi wa dunia โฆโฆโฆ Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu โฆโฆ.. Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja โฆโฆ.. Utuhurumie
Maria Mtakatifu โฆโฆโฆ. utuombee
Mzazi Mtakatifu wa Mungu โฆโฆ.. utuombee
Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira โฆโฆ.. utuombee
Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utusikilize ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utuhurumie.
Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,โฆโฆโฆโฆ..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
TUNAKUSHUKURU, EE MUNGU KWA MAPAJI YOTE ULIYOTUJALIA LEO AMINA
BABA YETUโฆโฆโฆโฆโฆโฆ.. SALAMU MARIAโฆโฆโฆโฆโฆโฆ.
SALA YA IMANIโฆโฆ.YA MATUMAINIโฆโฆโฆYA MAPENDO
SALA YA KUTUBU
TUWAZE KATIKA MOYO WETU MAKOSA YA LEO TULIYOMKOSEA MUNGU KWA MAWAZO,KWA MANENO, KWA VITENDO NA KWA KUTOTIMIZA WAJIBU (HUSUBIRI KIDOGO) NAKUUNGAMIA MUNGU MWENYEZI,NANYI NDUGU ZANGU,KWANI NIMEKOSA MNO KWA MAWAZO,KWA MANENO,KWA VITENDO NA KWA KUTOTIMIZA WAJIBU,NIMEKOSA MIMI,NIMEKOSA SANA.NDIYO MAANA NAKUOMBA MARIA MWENYE HERI,BIKIRA DAIMA,MALAIKA NA WATAKATIFU WOTE,NANYI NDUGU ZANGU,MNIOMBEENI KWA BWANA MUNGU WETU.
MUMNU MWENYEZI ATUHURUMIE ATUSAMEHE DHAMBI ZETU,ATUFIKISHE KWENYE UZIMA WA MILELE.AMINA
SALA YA KUOMBEA WATUโฆโฆโฆโฆโฆโฆโฆโฆ KUSIFUโฆโฆโฆโฆโฆโฆโฆโฆ
Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.// Waniangalia sana,/ siyo kwa kunipeleleza,/ lakini kwa sababu wapenda kuniona hivi karibu na wewe,/ wafurahiwa nikija kukuabudu./ Wayasikiliza maneno yangu yote/ yenye kutoka mdomoni mwangu,/ na zaidi wapokea maneno yangu yanayotoka moyoni./ Nataka kuzungumza na wewe peke yako,/ na kusahau mambo mengine yote/ na watu wengine walioko kanisani pamoja nami./
Yesu wangu,/ nakushukuru/ kwa sababu umekubali kutupa Sakramenti hii kuu kabisa,/ ukitaka kukaa pamoja na sisi,/ na hata ukakubali kuwa chakula chetu/ chenye nguvu ya ajabu./ Mfalme wangu Yesu,/ Sultani wangu Mkuu,/ naamini kabisa kwamba upo katika Altare/ na kwamba umejificha chini ya umbo la mkate./ Ulipokuwapo bado hapa duniani mbele za watu,/ ulikuwa hujifichi kama sasa;/ lakini hata siku zile/ watu hawakuweza kukuona vile ulivyo./ Hawakuweza kuutambua Umungu wako,/ ikalazimu kukuamini tu sawa kama sisi./ Wakainama kichwa wakisema,/ โBwana wangu na Mungu wanguโ./ Na mimi kadhalika naungama/ U Bwana wangu na Mungu wangu/ na Mkombozi wangu/ na salama yangu yote./ U Yesu wangu tu,/ siwezi kusema zaidi./ Nakuabudu ee Yesu./ Najua sana, mimi ni mdogo kabisa,/ sina maana hata kidogo./ Mimi ni dhaifu na maskini mno./ Lakini Wewe katika hruuma yako kubwa/ waniita nije kwako./ Wewe huuangalii umaskini wangu,/ bali wanivuta katika mapendo yako./
Nasikia maneno yako usemayo:/ โNjooni kwangu ninyi nyote mnaoelemewa na mizigo/ nami nitawasaidiaโ./ Kwa ajili ya maneno hayo/ nakuja kwako bila hofu./ Najua kwamba wanipenda,/ najua wataka kunisaidia na kuniponya,/ najua kuwa wataka kunitakasa./
Nahitaji sana msaada wako, hakika./ Unaniona katika mwendo wangu wa kila siku,/ Jinsi ninavyohangaika na vishawishi mara nyingi;/ jinsi nilivyo na lazima ya kushindana kila siku/ nikitaka kukaa mwema na safi katika utumishi wako./ Naungama mbele yako Wewe Mkombozi wangu,/ kwamba sikukaa imara siku zote vile nilivyopaswa./ Naungama kwamba nimeshindwa mara nyingine/ na kwa hivi naomba toba./ Lakini kwa nini nimeshindwa mara nyingine?/ Kwa nini nikakosa?/ Ni kwa sababu nalikuwa nimekwenda mbali nawe;/ nalianza kujitegemea mwenyewe./ Katika majivuno yangu nikajisifu mwenyewe,/ nikajiona mwema,/ nikasahau udhaifu wangu./ Na kwa ajili hiyo nikajitia katika hatari bure,/ sikujilinda tena,/ nikampa shetani nafasi ya kunishambulia kwa hila zake zote./ Unihurumie ee Yesu wangu./
Sasa nafahamu jinsi nilivyokuwa mjinga kwelikweli./ Ndiyo maana nakuabudu kwa moyo wangu wote./ Najiweka mikononi mwako/ ufanye nami vile unavyotaka./ Wewe utanitunza;/ Wewe utanilinda vema;/ Wewe utaniongoza nijue namna ya kuepa hatari zote,/ na jinsi ya kufukuza kila kishawishi./ Chukua moyo wangu kabisa,/ kwa sababu ni mali yako kamili;/ Wewe ndiwe uliyeniumba,/ ndiwe uliyenipeleka katika Ukristo,/ nawe ndiwe utakayenihukumu siku ya mbele./ Ndivyo ninavyojitolea kwako./ Ndivyo ninavyokuabudu,/ wala sijui njia nyingine ya kukusifu zaidi./
Yesu wangu mpenzi,/ naomba upokee kwa uzuri heshima hiyo yangu./ Angalia: naitolea pamoja na heshima yote/ unayopewa daima na watakatifu wako/ na malaika wako./ Nikipiga magoti hapa mbele yako sasa,/ siko peke yangu,/ nakuabudu pamoja na Mama yako Bikira Maria,/ ambaye sala zake zinakupendeza kabisa./ Sala zangu naweka pamoja na sala zake yeye,/ uzipokee zote pamoja,/ zikupendeze zote sawa./ Ee Mama Maria!/ Nifundishe maneno ya kumsifu Mwanao Yesu vizuri./ Nipeleke kwa Yesu tumwabudu pamoja./ Nifunike na utakatifu wako/ kusudi Yesu asiangalie tena umaskini wangu/ na makosa yangu,/ aniponye katika huruma yake./
Sasa najisikia vizuri, Yesu wangu./ Sasa nina moyo wa kuweza kuendelea vema/ katika njia njema./ Sasa ninatumaini kwamba/ nitakaa mkristo mwema,/ nitakuwa mtumishi wako mwaminifu./ Nasikia amani kubwa sana moyoni mwangu,/ kwa kuwa nimo mikononi mwako./ Baada ya dakika chache/ nitaondoka tena kanisani,/ nitarudi nyumbani kwangu,/ lakini hatutaachana,/ hapana./ Mapendo yetu yatatuunganisha pamoja daima./ Wewe utanikumbuka nikiwa kazini,/ nikilala usingizi,/ nikienda njiani,/ kila mahali nilipo,/ Wewe utaniona,/ utafuatana na mimi./ Kadhalika nitakukumbuka tu./ Nitafanya bidii nisikuache kabisa./ Amina.
(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi) Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na mwili wangu, nikikuomba uipokee amana yangu, kuitunzia ulinzi mwema ulinzi bora, ninakuaminia na kila neno langu, matumaini na kitulizo na kisongo chote, na masumbuko na uzima na ukomo wa uzima wangu: nitakayo ndiyo unifanyizie kwa maombezi na stahili zako, ili mambo yangu yote yapate kuongoka, yakiwa na kufuata mapenzi yako, pamoja na mapenzi ya Mwanao. Amina.
Baba Yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe; ufalme wako ufike, utakalo lifanyike duniani kama mbinguni. Utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina
Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utusikilize ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,โฆโฆโฆโฆ..Utuhurumie.
Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,โฆโฆโฆโฆ..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. A mina
Yesu, ulikufa, lakini chanzo cha uhai kilitoka kwa ajili ya watu, na bahari ya huruma ilifunguka kwa ajili ya ulimwengu mzima. Ee chemchemi ya Uhai, huruma ya Mungu isiyo na mwisho, ikafunika ulimwengu mzima na ukajimwaga mwenyewe juu yetu.
โฃโโฃ
โEe Damu na Maji, yaliyotoka moyoni mwa Yesu kama chemchemi ya Huruma kwetu. Nakutumainia.
1. NDIMI BWANA MUNGU WAKO, USIABUDU MIUNGU WENGINE. 2. USILITAJE BURE JINA LA MUNGU WAKO. 3. SHIKA KITAKATIFU SIKU YA MUNGU. 4. WAHESHIMU BABA NA MAMA, UPATE MIAKA MINGI NA HERI DUNIANI. 5. USIUE 6. USIZINI 7. USIIBE 8. USISEME UONGO 9. USITAMANI MWANAMKE ASIYE MKE WAKO 10. USITAMANI MALI YA MTU MWINGINE
Kumbuka ee Bikira mwenye rehema, haijasikika kamwe kwamba ulimwacha mtu aliyekimbilia ulinzi wako, akiomba msaada wako, akitaka umwombe.
Nami kwa matumaini hayo, nakukimbilia ee mama, mkuu wa mabikira, ninakuja kwako, ninasimama mbele yako,ย nikilalamika mimi mkosefu ewe mama wa neno la mungu, usiyakatae maneno yangu, mbali uyasikilize kwa wema na unitimizie Amina.
Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria saba kwa kila teso.
TESO LA KWANZA
Mzee Simeoni aliagua kuwa Moyo wa Mama Maria utachomwa kwa upanga. Tuombe neema ya kuvumilia mateso. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA PILI
Maria na Yosefu walikimbilia Misri usiku ili kumficha Mtoto Yesu asiuawe na Herodi. Tuombe neema ili miili yetu iwe kimbilio lake Yesu. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TATU
Mama Maria aliona uchungu sana Mtoto Yesu alipopotea kwa siku tatu. Tuombe neema ya kudumu na Yesu mioyoni mwetu. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA NNE
Mama Maria aliona uchungu sana alipokutana na Mwanae Yesu katika njia ya Msalaba. Tuombe neema ya kudumu na Yesu siku zote. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TANO
Mama Maria aliona uchungu sana alipomwona Mwanae Yesu akisulibiwa Msalabani. Tuombe neema ya kufa mikononi mwa Yesu na Maria. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SITA
Mama Maria aliona uchungu sana alipopakata maiti ya Mwanae Yesu baada ya kushushwa Msalabani. Tuombe neema ya kutotenda dhambi. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SABA
Mama Maria aliona uchungu sana aliporudi nyumbani baada ya kumzika Mwanae Yesu Tuombe neema ya kitulizo kwa Mama Maria. Mama wa mateso utuombee. Baba Yetu โฆโฆโฆ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba โฆโฆ Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.
Ee Yesu uliyesema โKweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwaโ, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba โฆโฆ.. (Taja ombi lako) Baba Yetuโฆ.., Salamu Maria โฆโฆ.., Atukuzwe Babaโฆโฆ.. Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Yesu uliyesema โKweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewaโ, tazama kwa jina lako ninaomba โฆโฆ. (Taja ombi lako) Baba Yetuโฆ.., Salamu Maria โฆโฆ.., Atukuzwe Babaโฆโฆ.. Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Yesu uliyesema โKweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamweโ, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba โฆโฆ.. (Taja ombi lako) Baba Yetuโฆ.., Salamu Maria โฆโฆ.., Atukuzwe Babaโฆโฆ.. Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.
Sali โSalamu Malkiaโ na kuongezea, โMtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombeeโ.
P.S. โ Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.
You can see how this popup was set up in our step-by-step guide: https://wppopupmaker.com/guides/auto-opening-announcement-popups/
AckySHINE Development Changelog
Welcome AckySHINE, We are still developing AckySHINE platform. Almost all services are not available for now because of reprogramming state. However, some services might be available from time as we are occasionally testing our services before full launching. We are sorry for any inconvenience.
Share your ideas and suggestions for our services here. We will be happy to hear from you.
Because of unavoidable circumstances this website (ackyshine.com) will not be updated starting from May 2018 till further notice.
No new post will be published. However you can only view/read old pages (public pages), which are pages created before May 2018 and shared to the public.
With thousands of old public pages, this website can still be useful and active to the public users.
AckySHINE is a consultancy office operating in Tanzania and providing professional services in the areas of Community development issues, Social science research and Project planning, monitoring and evaluation.
Main Consultation Services
Research methodology
Research Design/Planning
Data collection
Data Processing and analysis
Project/Programme management and evaluation
(M&E) Monitoring and Evaluation Project/Programme
Planning and implementation
Web design and Development
And Other relating services
You are Always Welcome
We are well placed to ensure optimum solutions for numerous clientsโ projects. We prefer a relationship based on mutual trust, co-operation, and communication
For us, the trust between the consultant and client is paramount. Enjoy the friendly atmosphere of his office when visiting.
If you’re enjoying yourself, please leave a comment๐ฌ.
I’d love to hear from you! ๐ฌโค๏ธ
Your Friend, Melkisedeck Leon Shine
AckySHINE Kiswahili Website
Please note that AckySHINE Swahili Website is not active.ย
Because of unavoidable circumstances AckySHINE Swahili Website will not be updated starting from May 2018. No new post will be published from May 2018.
However, You can view/read old pages (public pages) which were created before May 2018 and shared to public.
With hundreds of old public pages, we believe Swahili Website service can still be useful to the public users.
Thanks for reaching out! Send me a message on WhatsApp via the link below or email through the form. I prefer messages over calls, so please avoid calling. Thanks!
AckySHINE charity is a program for humanitarian campaigns and aid aimed at promoting peace and unity, protecting the environment, and maintaining the health and development of individuals and the community as a whole. These campaigns are advertised through ackyshine.com.
You can see how this popup was set up in our step-by-step guide: https://wppopupmaker.com/guides/auto-opening-announcement-popups/
AckySHINE is a Platform that support provision of both Online and Offline Services.
We provide the following Services
Research Consultancy– Active Offline Service We offer consultation services in Research, including research concept development, designing, data collection and processing and report writing.
Monitoring and evaluation Consultancy– Active Offline Service We offer consultation services in M&E Planning, Process Evaluation and In Impact Evaluation.
Training and facilitation Consultancy– Active Offline Service We offer consultation services inย Training and Facilitation. This include Training Planning, Session Plan and Management as well as Conduction of Training andย facilitationย session.
English – Swahili Translationย services– Active Offline Service We translate Short Texts, Documents and webpage from English to Swahili and vise versa. We provide live human support, translation is done by native speaking translators, no automatic translation.
Web designing and development– Active Offline Service We offer WordPress Set up service and Customization Services. Free Templates, SEO optimization, One Year Assistance, Responsive Design, Mobile Friendly.
AckySHINE Dedications– Pending Online Service This is a special place for sendingย dedicationsย to the person you love. Via WhatsApp and SMS.
AckySHINE Shop– Pending Online Service This is anย Digital shopping serviceย aim at sharing of knowledge and skills through soft copy books.
AckySHINE Library– Pending Online Service Welcomeย AckySHINE Libraryย where you can get unlimited Books. Feel Free to Download our Books.
English Website– Pending Online Service This isย English multi-category websiteย special designed for information, entertainment and motivation
Swahili website– Pending Online Service This isย Swahili multi-category websiteย special designed for information, entertainment and motivation
Advertising and marketing– Active Online Service We Display banner, image & links on our website. For ads we offer freeย translationย (English to Swahili), free Landing page, you can embed forms on your landing page and embed HTML Codes. You can also publish your posts on our website with unlimited words, unlimited pictures, unlimited videos and free translation service. Your posts will be intergraded in post categories.
Application Legal Notice
We, the Operators of this Application, provide it as a public service to our users.
Terms of Use
Please carefully review theย Terms of Use that govern your use of the Application and Website. Please note that your use of the Application constitutes your unconditional agreement to follow and be bound by these Terms and Conditions of Use. If you (the “User”) do not agree to them, do not use the Application, provide any materials to the Application or download any materials from it.
Privacy Policy
Theย Privacy Policy explains what we may do, and will not do, with your personal data that might be collected while you use this application and its services. Please read this policy and if you do not agree with it, please do not use this application or any of the services on it.
Further
If you have questions regarding these policies pleaseย contactย us.
Swahili Catholic Website
Please note that Swahili Catholic Website is not active.ย
Because of unavoidable circumstances Swahili Catholic Website will not be updated starting from May 2018. No new post will be published from May 2018.
However, You can view/read old pages (public pages) which were created before May 2018 and shared to public.
With hundreds of old public pages, we believe Swahili Catholic Website can still be useful to the public users.
Recent Comments