
Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba ukiwa unasema “Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.
Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, “Tusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote, na tuunganishe nia hizo na nia zetu sisi wenyewe, nk).
Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu.
Mojawapo ya maneno yafuatayo huweza kutumika:
“Mungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, …… Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, …… Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, …..”
Au;
“Utuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,…. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,…. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, …..” Au;
“Salamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,….. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,….. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,……”
Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina.
Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi.
Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef.
Kisha endelea na sala zinazofuata kama mpangilio unavyoonyesha hapo juu.
Kila baada ya Tendo moja na makumi ya Salamu Maria…, “Atukuzwe..”, “Ee Yesu wangu…” na “Tuwasifu milele…” kama muda unatosha wimbo ufaao wa Bikira Maria uimbwe (kama muda ni mfupi basi angalau ubeti mmoja mmoja uimbwe kila baada ya makumi hayo). Baada ya Wimbo, Tendo linalofuata litangazwe kwa sauti pamoja na tafakari fupi au ombi linaloambatana na Tendo husika kama inavyoonyeshwa hapa chini.
MATENDO YA ROZARI TAKATIFU
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA YA BIKIRA MARIA
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utusikie
- Kristo utusikilize
- Mungu Baba wa Mbinguni,…… Utuhurumie
- Mungu Mwana Mkombozi wa dunia ……… Utuhurumie
- Mungu Roho Mtakatifu …….. Utuhurumie
- Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja …….. Utuhurumie
- Maria Mtakatifu ………. utuombee
- Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
- Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee
- Mama wa Kristo ……… utuombee
- Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
- Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
- Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
- Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
- Mama usiye na doa ……….. utuombee
- Mama mpendelevu ………. utuombee
- Mama mstajabivu ………. utuombee
- Mama wa Muumba ………. utuombee
- Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
- Mama wa Kanisa……….. utuombee
- Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
- Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
- Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
- Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
- Bikra mweye huruma ………….. utuombee
- Bikra mwaminifu………….. utuombee
- Kioo cha haki ………….. utuombee
- Kikao cha hekima ………….. utuombee
- Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
- Chombo cha neema ………….. utuombee
- Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
- Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
- Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
- Mnara wa Daudi ………….. utuombee
- Mnara wa pembe ………….. utuombee
- Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
- Sanduku la Agano ………….. utuombee
- Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
- Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
- Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
- Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
- Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
- Msaada wa waKristo ………….. utuombee
- Malkia wa Malaika ………….. utuombee
- Malkia wa Mababu ………….. utuombee
- Malkia wa Manabii ………….. utuombee
- Malkia wa Mitume ………….. utuombee
- Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
- Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
- Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
- Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
- Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
- Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
- Malkia wa amani ………….. utuombee
- Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusamehe ee Bwana.
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusikilize ee Bwana
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utuhurumie.
- Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,…………..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
Karibu Vitatabu vya Kikatoliki
-
Vitabu Vya Dini
KITABU CHA SALA ZA KILA SIKU ASUBUHI NA JIONI
Original price was: Sh4,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
Kwa nini Wakatoliki wanaweka Sanamu Kanisani?
Original price was: Sh5,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Tafakari kwa Mkristu Mkatoliki (Sehemu ya I)
Original price was: Sh3,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
Biblia Takatifu Agano la Kale
Original price was: Sh7,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Novena Ya Huruma ya Mungu
Original price was: Sh2,500.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Novena ya Roho Mtakatifu
Original price was: Sh5,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Mwongozo wa kusali Rozari Takatifu ya Mama Bikira Maria
Original price was: Sh5,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
Biblia Takatifu Agano Jipya
Original price was: Sh3,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Mwongozo wa Sala na Nyimbo za Ibada ya Njia ya Msalaba
Original price was: Sh6,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
KITABU CHA NOVENA KWA MTAKATIFU RITA WA KASHIA
Original price was: Sh5,000.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart -
Vitabu Vya Dini
📕Kitabu cha Sala Muhimu: Mkusanyiko wa SALA, LITANIA NA NOVENA
Original price was: Sh12,500.Sh0Current price is: Sh0. Add to cart










🙏🌟 Mbarikiwe sana
Plunge into the expansive universe of EVE Online. Shape your destiny today. Fight alongside millions of explorers worldwide. Download free
Katika imani, yote yanawezekana
Mwamini Bwana; anajua njia
🙏🌟 Mungu akujalie amani
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Video exxxx
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rehema hushinda hukumu
Baraka kwako na familia yako.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
Neema na amani iwe nawe.
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe
🙏❤️ Mungu akubariki
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
Nakuombea 🙏
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mwamini katika mpango wake.
🙏💖 Nakusihi Mungu
Kwa Mungu, yote yanawezekana
🙏✨ Mungu atakuinua
Endelea kuwa na imani!
Mungu akubariki!
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
🙏🌟 Mungu alete amani
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
Sifa kwa Bwana!
Rehema zake hudumu milele
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Tumaini ni nanga ya roho
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Dumu katika Bwana.
🙏🙏🙏
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Nguvu hutoka kwa Bwana
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
🙏💖💫 Mungu ni mwema
🙏💖 Nakushukuru Mungu
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Imani inaweza kusogeza milima
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
Amina
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
🙏🙏🙏
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Neema ya Mungu inatosha kwako
🙏✨ Mungu atupe nguvu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie