Karibu AckySHINE
Karibu AckySHINE
Chagua Unachotaka Kusoma Hapa
Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.
Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Samaki Wa Pink Salmon
Vipimo
Mchele 3 vikombe
Mboga mchanganyiko 1 kikombe
Samaki wa Pink Salmon 5 -6 vipande
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa 1 kijiko cha supu
Chumvi kiasi
Pilipili manga ya unga ยฝ kijiko cha chai
Pilipili nyekundu ya unga ยฝ kijiko cha chai
Ndimu zilokamuliwa 2
Parsley kavu (aina ya kotmiri) 2 vijiko vya supu
Bizari ya mchuzi 1 kijiko cha supu
Kidonge cha supu (stock) 2
Mafuta ยผ kikombe
Maji ยฝ kikombe
Namna ya Kutayarisha Na Kupika
Samaki:
Katika kibakuli kidogo, changanya; kitunguu thomu, tangawizi, chumvi, pilipili zote za unga, ndimu, parsely, bizari ya mchuzi na mafuta vijiko viwili vya supu.
Pakaza kwenye samaki.
Weka vipande vya samaki katika treya ya oveni kisha uchome (grill) huku ukigeuza hadi samaki awive. Epua weka kando.
Wali:
Osha mchele roweka kisha uchemshe uive nusu kiini
Mwaga maji uchuje mchele
Weka mafuta katika sufura, tia mboga mchanganyiko kakaanga kidogo
Weka vidonge vya supu, tia maji ยฝ kikombe, tia chumvi kiasi
Mimina mchele uchanganye vizuri, kisha funika hadi uive wali ukiwa tayari
Pakua katika sahani pamoja na samaki
Njia 3 rahisi za kuondoa kitambi
JE, una KITAMBI na unataka kukiondoa?
FANYA HAYA;
1. Kopa mkopo mkubwa benki
2. Nunua gari bovu la biashara
3.Oana na mke mwenye kelele.
Ukiona miezi mitatu hakijaisha basi ujue umevimba BANDAMA sio kitambi..
Madhara ya kutumia dawa bila ushauri wa Dakitari
Mara nyingi watu wanaugua maradhi mbalimbali, lakini wengi wao hawapendi kwenda hospitali kufanya vipimo au kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa daktari. Kutokana na uwepo wa maduka ya dawa baridi, watu wengi wanapojisikia kuwa wagonjwa, hununua dawa kwenye maduka hayo na kuanza kuzitumia.
Ni ukweli usiopingika kuwa dawa zimetengenezwa ili kutibu maradhi fulani ambayo yatabainika kwa mgonjwa baada ya uchunguzi wa kitaalamu.
Hivyo matumizi ya dawa bila kufanya uchunguzi wa kitaalamu yanaweza kuwa na madhara makubwa kwenye afya yako
Yafuatayo ni madhara yatokanayo na kutumia dawa bila ushauri wa dactari:
1. Huweza kusababbisha kifo.
Kama nilivyoeleza kwenye hoja zilizotangulia, dawa ni sumu zinazokabili vimelea vya magonjwa. Hivyo kutumia dawa vibaya kunaweza kusababisha kifo.
Ikumbukwe pia watu wenye matatizo maalumu kama vile maradhi ya moyo pamoja na shinikizo la damu, wanapaswa kuwa makini na dawa wanazozitumia kwani zinaweza kuchochea matatizo yao na hatimaye kifo
2. Huweza kusababisha saratani.
Dawa zinapoingia mwilini mwako kimakosa na kushindwa kufanya kazi yake, zinaweza kuharibu baadhi ya seli za mwili na kuzifanya kugeuka seli za saratani. Hivyo hakikisha dawa unayoitumia ni sahihi na inalenga ugonjwa husika.
3. Husababisha usugu wa maradhi
Mtaalamu wa afya hukupa kiwango (dosage) cha dawa kulingana na vipimo alivyovifanya; hivyo kutumia dawa bila vipimo vya kitaalamu kunaweza kusababisha vimelea vya ugonjwa vizoee dawa husika na kusababisha ugonjwa huo usitibike tena.
Hili ndilo linalosababisha maradhi kama vile malaria sugu au UTI sugu. Hivyo kabla ya kutumia dawa ni vyema ukafanya uchunguzi wa kitaalamu
4. Husababisha tatizo la mzio. Allegy.
Kuna watu wenye tatizo la mzio au wengi huita โalejiโ kwa lugha isiyo sanifu, watu hawa wanapaswa kuwa makini na kuepuka kutumia dawa bila ushauri wa kitaalamu.
Hili ni kutokana na baadhi ya dawa kutokuendana na afya zao, hivyo kusababisha tatizo lao la mzio kuibuka. Ni vyema ukamwona mtaalamu wa afya na umweleze aina ya mzio uliyo nayo ili akupe dawa stahiki.
5. Huongeza sumu mwilini.
Dawa zimetengenezwa kwa kutumia kemikali mbalimbali ambazo kimsingi ni sumu zinazoua vimelea vya magonjwa.
Hivyo kutumia dawa bila vipimo kunakusababishia kuongeza sumu za dawa hizo mwilini mwako kwani umetumia dawa ambazo mwili hauzihitaji kukabili ugonjwa husika.
Sumu hizi zinapokusanyika mwilini mwako zinaweza kukuletea athari mbalimbali za muda mfupi au hata mrefu.
Ni muhimu ukumbuke kuwa dalili za ugonjwa mmoja zinaweza kuwa dalili za ugonjwa mwingine pia. Hivyo ni muhimu kufanya uchunguzi pamoja na kutafuta ushauri wa kitabibu kabla ya kutumia dawa zozote kutibu maradhi yanayokukabili.
Wabongo ni noma! Angalia huyu mbongo anachokifanya
Basi juzi kati hapa sehemu ndogo ya ukuta wa Ikulu ya Magogoni ilianguka!..
Wakapelekwa contractors watatu ili achaguliwe mmoja atakayejenga vzr na kwa bei nafuu!..
Wakwanza alikuwa MUHINDI, wa pili MCHINA na MBONGO!โฆ
MUHINDI: “ntajenga kwa milioni 90!.., 40 za vifaa, 40 za mafundi na milioni 10 faida yangu”
MCHINA: “mi ntajenga kwa milioni 70!.., 30 za vifaa, 30 za mafundi na milioni 10 faida yangu”
MBONGO kuona vile akamvuta chemba msimamizi wa Magogoni!..
MBONGO: “mi ntajenga kwa milioni 270”
MSIMAMIZI WA MAGOGONI: “we una wazimu nn!.. yaani unathubutu kusema hivyo na unaona wenzako wametaja kiwango kidogo?!.”
MBONGO: “milioni 100 zako, 100 zangu alafu hiyo milioni 70 tunaajiri yule mchina”
Soma alichojibiwa huyu mzee baada ya kudai kutaka kumsikiliza Nyerere
Mzee: Dereva ongeza sauti tumsikilize Mwalimu Nyerere!!
Dereva: ungemsikiliza mwalimu wako miaka iyo saivi ungekua na gari yako
๐ ๐ ๐ ๐ ๐ ๐ ๐ ๐ ๐
Jinsi ya kutengeneza Wali Wa Dengu Kwa Samaki Wa Kukaanga
Mahitaji
Mchele wa basmati – 3 Vikombe
Dengu – 2 vikombe
Viazi – 3 vikubwa
Kitunguu – 2 kubwa
Nyanya – 2
Pilipili mbichi kubwa – 3
Pilipilimanga – ยฝ kijiko cha chai
Garama Masala (bizari mchanganyiko) -1 kijiko cha chai
Supu ya vidonge (stock cubes) – 2 vidonge
Chumvi – kiasi
Mafuta – ยผ kikombe
Zaafarani – 1 kijiko cha chai
Samaki wa kukaanga
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Dengu kama sio za tayari kwenye kopo, roweka na zichemshe hadi ziwive
Maandalizi ya Masala Ya Dengu:
Zaafarani โ iroweke katika maji ya dafu dafu (warm) ya chini ya robo kikombe weka kando.
Osha mchele, roweka.
Menya viazi na vitunguu, katakata vitunguu, na nyanya , weka kando.
Katakata viazi vipande vidogo vidogo kwa umbo la mchemraba (cubes).
Katika sufuria tia mafuta yakipata moto, tia viazi ukaange kidogo kwa moto mdogo mdogo hadi kukaribia kuwiva, toa weka kando.
Kaanga vitunguu hadi vigeuka rangi ya hudhurungi isiyokoza (light brown) kisha tia nyanya ukaange kidogo.
Tia vidonge vya supu (stock cubes) uvivuruge katika mchanganyiko, katakata pilipili mbichi kwa urefu tia, uendelee kukakaanga. Tia bizari, chumvi.
Zima moto, changanya dengu na viazi katika mchanganyiko huo.
Mapishi ya Wali:
Chemsha mchele kama kawaida ya kupika wali mweupe, kiini kiwe kimewiva nusu yake.
Chuja maji kisha changanya katika mchanganyiko wa dengu.
Nyunyizia zaafarani, uchanganye wali na mchanganyiko kidogo tu.
Funika acha uive katika mtoto mdogo mdogo au tia katika oveni hadi uive kama kawaida ya kupika wali.
Pakua katiha sahani na tolea na samaki yoyote wa kukaanga.
Ni herufi gani tatu zinafuata baada ya hizi?
SWALI: Ni herufi gani tatu zinafuata baada ya MMTNTSS
Onesha Jibu
MMTNTSSNTK: Herufi ya kwanza ya namba Moja mpaka Kumi. Yaani Moja, Mbili, Tatu, Nnne, Tano, Sitaโฆ
SMS nzuriiii ya kumpa mtu hai
Nakupa HAI, kwa sababu uko HAI, usingekuwa HAI, ni vigumu kupewa HAI, basi nawe wape HAI, walio HAI, maana ni bahati kuwa HAI, wengi walitamani kuwa HAI, lakini wamepoteza UHAI, Usione najidai, ila mimi naringia UHAI, Haya basi pokea HAI, ili moyo wako ufurahi. HAIIIIIIIIIIIII!!!
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Utani wa wahindi, cheka kidogo
Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili
(1) Mfa maji ?โฆโฆโฆโฆโฆโฆ.. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?โฆโฆโฆโฆ Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?โฆโฆโฆ.. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?โฆโฆโฆโฆโฆโฆ Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?โฆโฆ. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?โฆโฆโฆ Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?โฆโฆ.. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?โฆโฆ Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?โฆโฆโฆ Takosa guo ya sikukuuโฆ
(10) Kila ndege ?โฆโฆโฆโฆ.. โฆHutua Airport
(11) Bandu bandu ?โฆ.. โฆโฆ.Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?โฆ Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?โฆ.Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?โฆโฆโฆ. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?โฆโฆ.. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?โฆ. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? โฆโฆ.. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? โฆโฆโฆโฆ..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?โฆโฆ.. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?โฆ.Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?โฆโฆ.. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? โฆโฆโฆ.Taenda Chadema
(23) Bendera ?โฆโฆโฆโฆโฆ. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?โฆโฆ. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?โฆโฆโฆ. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? โฆโฆ.. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.
SMS ya kumwambia mpenzi wako kuwa bado unampenda na hujabadilika
“Japokuwa”
“Kuku” “Haogi” “Yai” “Lake” “Litabaki” “Kuwa” “Jeupe” “Tu” “Namaanisha”
“Kuwa”
“Hata” “Kama” “Ukiona”
“Nipo” “”KIMYA”” Muda”
“Mrefu” “”UPENDO”” “Wangu” “Kwako”
“””Bado”””
“Uko” Pale pale!!!!!
Usijali
“Tupo Pamoja” “Kwa” “Asilimia 100%”.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Je, glasi itakuwa vipande vingapi?
SWALI:ย Mtoto alikua amebeba glasi mkono mmoja na mkono mwingine mpira. Kwa bahati mbaya mpira ukaanguka chini na kudunda mara tatu. Je, glasi imebaki vipande vingapi?
Onesha Jibu
JIBU: Glasi bado ni nzima. Mpira ndio ulianguka. Glasi haikuanguka
Hyuyu daktari ni noma, cheki anachokisema
Kuna Daktari wa Moyo alifariki wakamchongeaa jeneza lenye umbo la Moyo. Ghafla Daktari mwingine akaanza kucheka, watu wakamuuliza “kwanini unacheka unafurahia mwenzako kufariki?” Daktari yule akajibu “hapana mimi ni Daktari wa kutahiri nafikilia nikifa mtanichongea jeneza lenye umbo la โฆ.”
Maisha ya kijijini hadi raha!!
Jamaa alimfumania mtu anazini na mkewe,
Akamtoza Faini ya sh 5000 tu,yule mtu akatoa 10000.
Jamaa akasema lala nae tena sina chenji!๐๐๐๐๐๐๐
Uwepo wa Mungu wakati wa shida
Kwa kawaida kwenye maisha unapofikia Hatua unaona Mungu hayupo kabisa na wewe basi ujue huo ndio wakati ambao Mungu yupo karibu na wewe zaidi.
Visababishi, dalili, matibabu na kinga ya presha ya kushuka
Hypotension ndio jina linalotumika kuelezea presha ya kushuka ambayo mpaka sasa chanzo chake hakijawa wazi. Kipimo cha presha huwa na namba mbili. Namba moja huwa juu na nyengine huwa chini. Hivyo basi namba ya juu kikawaida kwa mtu mzima inapaswa kuwa 100 hadi 139 na ya chini inapaswa kuwa 60 hadi 90. Hivyo basi pressure yako ikiwa chini ya 100/60 Ndio inajulikana kama Hyptension yaani pressure iko chini.
Hypotension (haipo juu). Kwa watu wengi presha hii huwatia kizunguzungu na kuwaangusha. Presha hii ikiwa ya muda mrefu husababisha mtu kupata maradhi ya mshtuko.Watu wenye afya nzuri, hasa wakimbiaji, presha ya kushuka huwa ni dalili ya uzima kwao.
Si rahisi kuziona dalili kwa mtu mwenye presha ya kushuka hata kama imedumu kwa muda mrefu. Mara nyingi matatizo ya kiafya huonekana pale mtu presha yake inaposhuka ghafla. Wakati huo wa matatizo ya kiafya, damu kidogo hufika katika ubongo. Hali hii humfanya mtu awe na kizunguzungu au kuumwa na kichwa.
Kushuka ghafla kwa presha mara nyingi humtokezea mtu pale anapofanya jambo la haraka kama mtu aliyekaa na kutaka kusimama mara moja. Kitaalamu presha hii inajulikana kama postural hypotension, orthostatic hypotension, au neurally mediated orthostatic hypotension.
Postural hypotension inachukuliwa ni hali ile ya kushindwa kwa mfumo wa mawasilianao unaojiendesha wenyewe mwilini kufanya kazi yake kikamilifu (autonomic nervous system). Mfumo huu huendesha na kuongoza vitendo visivyo vya hiari (involuntary vital actions), kama vile mapigo ya moyo kubadilika kutokana na jambo lililotokea kwa wakati uleopo.
Kwa kawaida unapoinuka, kiwango fulani cha damu yako kinakuwa kimebaki sehemu ya chini (miguuni). Kukiwa hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa na mwili wako, hali hii itasababisha presha yako kushuka. Katika hali hii mwili wako unafanya nini ?
Mwili wako unapeleka taarifa kwenye moyo na kuamuru uongeze usukumaji wa damu ambao utaizidi mishipa yako na kuifanya kuwa membamba hali itakayopelekea kuifanya presha yako kubakia ileile. Ikiwa jambo hili halikufanyika au limaefanyika polepole sana, presha yako itashuka ghafla. Hapa ndipo mtu unapomuona anaguka ghafla.
Kwa ufupi athari ya maradhi ya presha ya kushuka na ya juu huongezeka kadri mtu anapokuwa na umri mkubwa na pia kubadilikabadilika kadri umri unavyoongezeka. Jambo jingine la kufahamu ni kuwa, ufikaji wa damu kikawaida kwenye ubungo unapungua kadri umri unavyoongezeka. Inakisiwa kiasi cha asilimia 10 mpaka 20 ya watu wenye umri unaozidi miaka 65, wanapata tatizo la presha yao kushuka.
Ni kiwango gani cha presha kinapofika ndio huwa maradhi ?
Hakuna kiwango maalum kinachojulikana ambacho ni sawasawa kwa watu wote kikifika ndio kinaitwa maradhi. Kiwango ambacho kwako ndio uzima, basi huenda kwa mwenzako ikawa ni maradhi. Katika presha ya kushuka, madaktari wengi huchukulia kuwa tayari mtu ana maradhi pale aambapo kiwango chake cha presha kinafuatana na dali za maradhi yenyewe.
Hata hivyo, baadhi ya wataalamu wanachukulia tayari mtu ana maradhi ya presha ya kushika pale vipimo vinapoonyesha kiwango hichi 90/60 mm Hg. Tufahamu kuwa kiwango cha namba inayosomwa chini katika kipimo cha presha (โฆ /60 mm Hg ), hichi huonyesha tayari mtu huyu anapresha ya chini hata kama kile cha juu ( 90/โฆmm Hg) kina namba iliyozidi 100.
Mfano ikiwa umepimwa presha na ukapata kipimo hichi 115/60 mm Hg, presha yako itakuwa ipo chini. Na kama umepata kipimo hichi 115/50 mm Hg, sio kwamba presha yako itakuwa ipo chini tu, bali presha hii itakuwa si ya kawaida.
Dalili za maradhi
Kama nilivyokwisha tangulia kusema, presha inaweza kuwa sawa kati ya watu wawili lakini ikawa na matokeo tofauti. Presha hiyo inayoweza kuwa sawa na ikawa na matokeo tofauti si yenye kipimo hichi 120/80 mm Hg. Presha yenye kipimo hichi 120/80 mm Hg, ndiyo nzuri na watu wenye presha hii wanakuwa na afya nzuri. Kitu muhimu ni kujua, mabadiliko gani yanaleta tatizo katika presha hata inapelekea kuwa si ya kawaida.
Presha nyingi za watu wanapopimwa huwa zinakuwa kati ya 90/60 mm Hg (presha iliyo chini) mpaka 130/80 mm Hg (presha iliyo juu). Mabadiliko ya kushuka presha upande wa chini, hata kama kidogo kiasi cha 20 mm Hg, hupelekea matatizo kwa baadhi ya watu ( hasa watu wasiofanya mazoezi kila siku).
Mtu mwenye mazoezi ambaye presha yake nzuri (120/80 mm Hg) akapimwa presha na kupata kipimo hichi, 110/60 mm au 120/70 mm Hg, mtu huyu hatakuwa na tatizo lolote la presha
Kuna aina tatu za presha ya kushuka :
Orthostatic sambamba na postprandial orthostatic (Orthostatic hypotension, including postprandial orthostatic hypotension)
Orthostatic, hii ni aina ya kwanza ya presha inayosababishwa na kubadili mazingira uliyonayo kwa ghafla, maranyingi hutokea kwa mtu anayesimama kutoka alipolala. Presha hii haidumu muda mrefu, kiasi cha sekunde chache mpaka dakika moja. Ikiwa presha hii itatokeze. baada ya kula, basi itakuwa ni hatua ya pili (postprandial orthostatic) .
Hatua hii ya pili huwapata zaidi wazee na wenye presha ya juu.
Neurally mediated hypotension (NMH)
NMH kama ilivyo kifupisho cha presha aina ya pili, huwapata zaidi vijana na watoto. Presha hii hutokea pale mtu anaposimama kwa muda mrefu. Maranyingi huwapata sana watoto.
Aina hii ya pili ya presha ya kushuka maranyingi husababishwa na hali zifuatazo :
- Utumiaji wa pombe
- Utumiaji wa dawa za kutibu presha ya juu.
- Utumiaji wa dawa za kumtoa fahamu mtu wakati wa kufanyiwa upasuaji
Mambo mengine yanayosababisha presha kushuka ni pamoja na :
- Ugonjwa wa Kusukari
- Mtu kula kitu kinachomdhuru
- Mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida
- Maradhi ya kuharisha
- Kuzimia
- Maradhi ya moyo
- Maradhi ya kustuka
Severe hypotension hii ni aina ya tatu ya presha ya kushuka ambayo hutokana na kupoteza damu
Kwa muhtasari, dalili za presha ya kushuka ni pamoja na :
- Kuona kizunguzungu/kuumwa na kichwa kusiko kuwa kukubwa
- Kuzimia
- Kushindwa kuzingatia
- Kushindwa kuona vizuri ghafla
- Kuona baridi,
- Kujihisi kuchoka sana
- Kuvuta pumzi kwa tabu
- Kutapika
- Kuhisi kiu
Hali zinazosababisha kupata presha ya kushuka.
Kinachosababisha presha ya chini bado hakijatambulika hasa. Chanzo chake hakiko wazi. Hata hivyo mambo yafuatayo yanaweza kuhusiswa nayo :
- Kuwa na mimba
- Matatizo ya homoni mwilini, maradhi ya kisukari, au upungufu wa sukari mwilini
- Utumiaji mkubwa wa dawa
- Ulaji wa dawa za presha unaopindukia kiwango (Overdose) kwa mtu mwenye presha ya juu.
- Maradhi ya moyo
- Maradhi ya figo
Nani anapata presha ya kushuka ghafla ?
Presha ya kushuka ghafla inayompata mtu anapoinuka ghafla, inaweza kumpata mtu yeyote kwa sababu tofauti zikiwemo,
- kuharisha sana,
- kukosa chakula ( njaa kali) kwa muda mrefu,
- kusimama kwa mapigo ya moyo, au
- kuchoka kupita kiasi.
- Pia inawezekana ikawa ni urithi wa maradhi,
- Umri mkubwa,
- Matumizi ya dawa,
- Utapiamlo na mambo mengine kama kupatwa na madhara ya jambo fulani.
Nini kinaifanya presha inayoshuka iendelee ?
Pia Presha ya kushuka mara nyingi huwapata watu wanaotumia dawa kwa kutibu presha ya juu (hypertension). Pia huwapata wajawazito au wagonjwa wa kisukari. Mara nyingi wazee nao hupata maradhi haya hasa wale walio na presha ya juu wakiwa wanaendelea kutumia dawa zao za presha.
Baadhi ya maradhi ambayo yanasababisha presha kushuka kuendelea ni pamoja na;
- Ukosefu wa vitamin mwilini,
- Madhara kwenye uti wa mgongo, na
- Kansa hasa kansa ya mapafu.
Wakati gani wa kuchukua hatua za matibabu
Matibabu huanza na hatua zako wewe mwenyewe. Wakati utakapojiona presha yako inashuka, kaa chini au lala chali na unyanyue miguu yako juu. Wakati yanafanyika haya, ufanyike utaratibu wa kuonana na daktari haraka.
Pia ufanyike utaratibu wa kuonana na daktari yanapoonekana mambo yafuatayo yamemkuta mtu :
- Maumivu ya kifua
- Kizunguzungu
- Kuzimia
- Homa kali sana
- Mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida
- Kupumua kwa tabu
Pia afuatwe daktari haraka ikiwa baada ya hayo yaliyotokea, kuongezeka na haya yafuatayo :
- Mtu anapata matatizo makubwa ya mkojo
- Kushinwa kula au kunywa chochote
- Kuendelea kuharisha au kutapika kwa muda mrefu
Matibabu na Dawa
Presha ya kushuka ambayo haijulikani chanzo chake wala haileti dalili au inampa mtu kizunguzungu anaposimama, mara chache inaweza kutafutiwa matibabu. Ikiwa zipo dalili, matibabu yataendana na chanzo chenyewe na daktari atashughulikia hicho chanzo. ( kuharisha,maradhi ya moyo, kisukari). Ikiwa presha ya chini imesababishwa na matumizi ya dawa kwa matibabu, basi matibabu yake huwa kubadili dawa nyingine ua kuacha kutumia dawa kabisa.
Ikiwa hakuna uhakika wa sababu za presha ya kushuka au hayapatikani matibabu yaliyo sahihi, matibabu sahihi yatakuwa ni kuifanya presha yako ipande na kuondoa zile dalili zanazokupata inapokujia.
Kwa kutegemea umri wako, hali yako ya kiafya na aina ya presha uliyonayo, mambo haya yanaweza kukusaidia :
Kuongeza matumizi ya chumvi. Matumizi ya chumvi lazima yawe kwa kipimo, kwani chumvi nyingi hupandisha presha. Kabla hujaanza kuongeza matumizi ya chumvi, ni vizuri uwasiliane na daktari ili akupe kiwango cha matumizi.
Kunywa maji mengi. Kunywa maji mengi kunamsaidia kila mtu sio mtu mwenye presha ya chini tu. Tunapozungumzia maji tunalenga zaidi vinywaji na sio maji peke yake, lakini vinywaji vyenyewe viwe ni maji, maji ya matunda maziwa na hata kahawa au chai. Tahadhari ichukuliwe kwa vinywaji vya viwandani kwani huwaletea matatizo baadhi ya watu.
Kuvaa mavazi yenye kubana. Haya ni mavazi ya mpira ambayo yanavaliwa sehemu za miguuni. Mavazi haya yanasaidia kufanya damu yako isikae miguuni na iendelee kwenye mzonguko wake kikawaida.
Matumizi ya dawa. Zipo dawa mbalimbali ambazo zinatumika kufuatana na hali ya presha uliyonayo.
Matibabu hospitalini.
Presha ya kushuka inayomtokezea mtu mwenye afya nzuri ambayo haina dalili zozote na haimletei matatizo yeyote, hatahitajika kutumia dawa. Ikiwa zipo dalili, atahitaji matibabu kutokana na hizo dalili zilizoonekana. Ikiwa presha ulokuwa nayo inatokana na matumizi ya dawa, daktari atakubadilishia dawa nyengine au utaacha matumizi ya dawa. Wale wenye NMH pamoja na matumizi ya dawa, inabidi waache tabia ya kusimama muda mrefu. Kimtazamo presha ya chini inatibika hata kufikia mtu kuwa na presha ya kawaida.
Napenda nichukue nafasi hii kuwafahamisha kuwa, bila kubadili mfumo wa maisha ulionao, hata ukikusanyiwa dawa nzuri za dunia nzima kwa kutibu maradhi yako hutopata uzima wowote. Kubadili mfumo wa maisha si katika kuishughulikia presha tu, bali kwa maradhi yote ndio
Tiba sahihi. Nini dawa zinafanya?. Dawa zinalazimisha kuurudisha mfumo katika hali yake ya kawaida tu. Baada ya dawa kutoa msaada wake huu, kinachotakiwa kwako wewe kuendeleza mfumo huo unaofaa ambao dawa zimekurudishia tena.
Kwa kutegemea sababu za kupata presha uliyonayo, unaweza kuchukua hatua zifuatazo :
Kunywa maji mengi, kuacha kunywa pombe, Kula vyakula kiafya (kula nafaka, matunda, mbogamboga, kula mifupa ya samaki na hata ya ndege[kuku,njiwa nk]) Tupendelee kuku wa kienyeji zaidi. Ikiwa kuongeza chumvi katika chakula, basi usizidishe vijiko viwili vya chai kwa siku na ni vizuri sana upate ushauri kwa daktari.
Kujenga utamaduni wa kuinuka taratibu ulipo kaa ua kulala. kulalia mto, ikiwa unapenda kunalalia ubavu, pendelea kulalia upande wa kulia (kila unapozungumzia presha, basi jambo la kwanza la kukumbuka ni moyo, moyo wako uko upande wa kushoto, kitendo cha kulalia upande wa kushoto kinaweza kuupa tabu moyo katika utendaji wake wa kazi).
Kuwa na tabia ya kula chakula kidogo katika mlo wako. Kufanya hivyo kunasaidia presha yako kutoshuka baada ya kumaliza kula. Jipangie utaratibu wa kula mara kwa mara ili uweze kula chakula cha kutosha. Punguza kula vyakula vyenye uwanga kwa wingi kama vile, mbatata, wali na mikate. Kula chakula pamoja na chai au kahawa. Ni vizuri haya yote utakayoyafanya ukawasiliana na daktari kabla.
Kinga ya presha ya kushuka.
Ikiwa wewe ni mzima au tayari una presha ya kushuka, Daktari atakushauri hatua za kuzuia isitokee au isiendelee au kuipunguza. Hatua hizo ni pamoja na :
1. Kuacha unywaji wa pombe.
2. Kuepuka kusimama muda mrefu ( hasa ikiwa tayari una NMH)
3. Kunywa maji kwa wingi
4. Kuinuka taratibu kutoka ulipokaa ua kulala
5. Kuvaa mavazi ya kubana miguuni (ikiwa tayari unayo)
Hawa wanaume wanaopenda wanawake hovyo barabarani wamepatikana, hawatarudia ๐๐๐
Marafiki wawiliย (Jose na Ben)ย walikuwa wanatembea mtaani akatokea mwanamke akarusha busu kwa mmojawapo kupitia dirishani katika jengo la ghorofa tatu.
Wakaanza kujadiliana kama ifuatavyo:
Ben:ย Muone yule mrembo amenirushia busu
Jose:ย tafadhali achana na huyo mwanamke, usimjali..
(baadae yule mwanamke akamuashiria aende)
Ben:ย yule mwanamke ameniita!
Jose:ย Rafiki yangu, usiende. Nakutafadhalisha.
Ben:ย Kwa nini unaniambia nisiende Wakati mrembo kama yule ananiita? Huo ni wivu
Jose:ย Ben, Ninakutafadhalisha tena, usiende, tafadhali usiende kuleย (akihisi kutotiliwa maanani)
(Rafiki yake alimpuuza na alienda kwa yule mwanamke, mwanamke alishuka kukutana naye na wakapanda juu. Ghafla wakiwa wanataka kuanza taratibu za kula uroda, wakasikia mlio WA gari getini).. ๐๐
Lady:ย _(akiangalia kupitia dirishani)_
Oooh! Yule ni mume wangu!!
Ben:ย Mama yangu !
Nipo matatani, kweli ? ..!!
Lady:ย Usiwe na khofu, jifanye kuwa Dobi na anza kupiga pasi hizo nguo
(akimuonyesha lundo la nguo)
(Ben alitumia masaa matano kukamilisha kunyoosha zile nguo kwa sababu yule mume hakutoka tena siku ile)
(Siku iliyofuatia Ben alikwenda kwa Rafiki yake)
Ben:ย Kaka, unaweza kuamini Jana nimepiga pasi nguo kwa masaa matano???
Jose:ย Lakini nilikwambia usiende. Nguo zote hizo ulizonyoosha,ย Nilizifua Mimi Juzi!!
๐๐๐๐๐๐๐๐๐
When an experienced person speaks โฆ ๐you must listen..!
Meseji ya usiku mwema kwa umpendaye
Ckia ckupend, cktaki na wala ckhitji tena ww ni kikwzo
ktka maisha yangu ucnizoee! Mwmbie shtan maneno hya kabla
hjalala. g9t
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Mbinu 4 anazotumia Shetani kuteka na kurubuni Watu
1. Kutushawishi tuache kusali maaana njia kuu ya mawasiliano kati yetu na MUNGU.Hivyo akifanikiwa hapo kwisha habari yako
2. Kufanya umwogope shetani na nguvu zake kuliko unavyompenda MUNGU. Wakristo wengi leo hii husali na kuomba kwa nguvu mno siyo sababu wanampenda MUNGU mno hapana ni sababu wanamwogopa shetani na majeshi yake na muda mwingine hata watumishi wa MUNGU wanamsaidia kwa kuhubiri mno na muda mwingine kuongeza jumvi juu ya nguvu za giza kuna wahubiri huambatanisha kila kitu na vifungo vya nguvu za giza na kusahau kuhubiri uzuri na wema wa MUNGU kwetu.
3.Kutufanya tusahau uwepo wake au kuupuzia. pale tunapokuwa hatupay attention existance ya shetani yeye ndio hupata wakati mzuri wa kutupiga ,sababu ni rahisi mno kutouutambua ubaya wa dhambi kama hatutaamini uwepo wa shetani ktk uovuโฆhii hutupelekea kutenda dhambi na kuziona siyo dhambi mfano kwa wasomi wengi hupuuzia baadhi ya mambo kama kujilinda na zinaa wakiamini ni kupitwa na wkt kama utakuwa hauna mahusiano ya kingono mpaka umefika chuo kikuu tena huchukulia wasiokuwa hivyo ni wagonjwa.hapo ni kuwa wengi wameignore uwepo wa shetani “no devil no evil” hivyo watu ndio hupotea.
4.KUTUTIA MOYO WAKATI WA KUTENDA DHAMBI NA KUTUKATISHA TAMAA YA KUSAMEHEWA. nitatoa mfano huu mtu ambaaye anataka kufanya uzinzi shetani humtia moyo kuwa MUNGU anajua kuwa sisi ni binadamu dhaifu na yeye husamehe dhambi zetu daima lakini ifikiapo wakati ukataka kutubu hafanya kila njia kukukatisha tamaa ya kusamehewa na hututia aibu hata kutsmka kwa padri kuwa nimedhini maana huanza kufikiria padre atanionaje mimi.
BASI NDUGU TUSISINZIE BALI TUWE MACHO DAIMA MSHITAKI WETU YU MACHO KUTUJARIBU.
Kuomba na Kushukuru
Unapo mwomba Mungu Usisahau Kushukuru. Kushukuru ni kuomba mara ya pili. Utazidishiwa kile ulichokiomba na kupewa hata usichokiomba kwa shukrani yako.














































































I’m so happy you’re here! ๐ฅณ
Recent Comments