Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya

Mapishi ya Pilau Ya Nyama ya Kusaga, Adesi Za Brauni Na Zabibu

Mahitaji

Mchele wa Par boiled au basmati – 5 vikombe

Nyama kondoo/mbuzi ya kusaga – 1 kikombe

Kitunguu – 2

Kitunguu saumu (thomu/galic) – 7 chembe

Adesi za brauni (brown lentils) – 1 kikombe

Zabibu – 1 kikombe

Baharaat/bizari mchanganyiko – 1 kijiko cha supu

Chumvi – kiasi

Pilipilii manga – ยฝ kijiko

Jiyra/bizari pilau/cummin – 1 kijiko cha chai

Supu ya nyama ngโ€™ombe – Kiasi cha kufunikia mchele

Mafuta – ยฝ kikombe

Namna Ya Kutayarisha

Osha, roweka masaa 2 au zaidi.

Katakata (chopped)

Menya, saga, chuna

Osha, roweka, kisha chemsha ziive nusu kiini.

Osha, chuja maji

Namna Ya Kupika:

Tia mafuta katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vianze kugeuka vyekundu.
Tia kitunguu thomu, kaanga, tia baharati/bizari zote kaanga.
Tia nyama uchanganye vizuri, ukaange iwive..
Tia mchele ukaange kidogo kisha tia supu, koroga kidogo, funika uivie mchele.
Karibu na kuiva, tia adesi, zabibu, changanya, funika uendelee kuiva kama unavyopika pilau.
Epua pakua katika chombo, ongezea zabibu kupambia ukipenda

Jinsi ya kutengeneza Cookies Za Tende Na Tangawizi

MAHITAJI

Unga vikombe vikombe 4

Baking soda 1 kijiko cha chai mfuto

Siagi 400 gms

Sukari ยฝ kikombe

Tende chambua ukatekate ifikie ยพ kikombe

Tangawizi ya unga vijiko 2 vya chai

Vanilla 1 kijiko cha chai

Yai 1

Maziwa mazito vijiko 2 vya kulia.

MAANDALIZI

Changanya siagi na sukari katika mashine usage mpaka iwe laini nyororo.
Tia yai uchanganye vizuri
Tia tende na vanilla, tangawizi uchanganye vizuri.
changanya unga na baking soda kisha, mimina kidogo kidogo huku unachanganya kwa kijiko cha ubao (mwiko).
Unga ukiwa mzito ongeza vijiko 2 vya maziwa. Fanya viduara upange katika treya uliyopakaza siagi kisha uchome (bake) katika over moto mdogo wa kiasi dakika 15 vigeuke rangi viwive.
Epua vikiwa tayari

Mapishi ya Supu Ya Maboga

Viamba upishi

Blue band vijiko vikubwa 2
Maziwa vikombe 2
Royco kijiko kikubwa 1-2
Pilipili manga (unga) kijiko cha 1
Chumvi kiasi Maji lita 2-3
Boga kipande ยฝ
Viazi mviringo 2
Vitunguu 2
Karoti 2
Nyanya 2

Hatua

โ€ข Menya boga, viazi, karoti, nyanya na kwaruza weka kwenya sufuria kubwa.
โ€ข Menya, osha na katakata vitunguu kisha ongeza kwenye mboga.
โ€ข Ongeza maji na chumvi chemshwa mpaka vilainike.
โ€ข Pekecha ikiwa jikoni na moto kidogo
โ€ข Ongeza blue band, maziwa royco na pilipili manga ukikoroga kwa dakika 5.
โ€ข Onja chumvi na pakua kama supu.
Uwezekano
Tumia siagi badala ya margarine.

Mapishi ya Mandazi Matamu

Mahitaji

Unga wa ngano (nusu kilo)
Sukari (Kikombe 1 cha chai)
Chumvi (nusu kijiko cha chai)
Hamira (kijiko kimoja cha chai)
Yai (1)
Maziwa ya unga (vijiko 2 vya chakula)
Butter (kijiko 1 cha chakula)
Hiliki (kijiko1 cha chai)
Maji ya uvuguvugu ya kukandia
Mafuta ya kuchomea

Matayarisho

Tia unga kwenye bakuli kisha tia sukari, chumvi, yai, maziwa ya unga, butter na hiliki kisha uchanganye pamoja mpaka mchanganyiko wote uchanganyike vizuri. Baada ya hapo tia maji ya uvuguvugu kiasi na uanze kuukanda. Ni vizuri ukaukanda kwa muda wa dakika 15 ili kuhakikisha donge lote la unga limelainika vizuri.
Baada ya hapo Tawanyishaa unga uliokwandwa katika madonge 4. Tia unga wa ngano kidogo katika kibao cha kusukumia na uanze kusukuma donge moja katika shape ya chapati na hakikisha haiwi nyembamba sana wala nene sana yani inatakiwa iwe ya wastani.Ukishamaliza kusukuma unatakiwa ukate shape uipendayo na uyatandaze katika kitu kilichopo flat na kiwe kimenyunyuziwa unga wa ngano ili kuyazuia yasigandie. Rudia hiyo process kwa madonge yote yaliyobakia. Baada ya hapo yaweke mandazi katika sehemu iliyokuwa na joto ili yaweze kuumuka (inaweza kuchukua masaa 3 kuumuka). Yakisha umuka unatakiwa uweke mafuta katika karai la kuchomea. Yakisha pata joto la kiasi unatakiwa utumbukize mandazi na unaze kuyachoma mpaka yawe ya brown. Yakisha iva yaipue na uyaweke kwenye kitchen towel iliyakauke mafuta. Yakisha poa yatakuwa tayari kwa kuliwa.

Jinsi ya kupika wali wa Tuna (samaki/jodari)

VIAMBAUPISHI VYA TUNA

Tuna (samaki/jodari) – 2 Vikopo

Vitunguu (kata kata) – 4

Nyanya zilizosagwa – 5

Nyanya kopo – 3 Vijiko vya supu

Viazi (vilivyokatwa vipande vidogo – cubes) – 4

Dengu (chick peas) – 1 kikombe

Kitunguu saumu(thomu/galic)&Tangawizi iliyosagwa 1 Kijiko cha supu

Hiliki – 1/4 kijiko cha chai

Mchanganyiko wa bizari – 1 kijiko cha supu

Chumvi – kiasi

Pilipili manga – 1 Kijiko cha chai

Vipande cha Maggi (Cube) – 2

VIAMBAUPISHI VYA WALI

Mchele – 3 Vikombe vikubwa (Mugs)

Mdalasini – 2 Vijiti

Karafuu – chembe 5

Zaafarani – kiasi
Jirsh (Komamanga kavu au zabibu kavu -raisins) – 1/2 Kikombe

JINSI YA KUANDAA

Kosha Mchele na roweka.
Kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi (brown) chuja mafuta uweke kando.
Kaanga viazi, epua
Punguza mafuta, kaanga nyanya.
Tia thomu/tangawizi, bizari zote, vipande vya Maggi, nyanya kopo, chumvi.
Mwaga maji ya tuna iwe kavu, changanyisha kwenye sosi.
Tia zaafarani kidogo katika sosi na bakisha ya wali.
Chemsha mchele pamoja na mdalasini na karafuu.
Karibu na kuwiva, chuja maji utie katika chombo cha kupikia katika jiko (oven)
Nyunyizia zaafarani, mwagia vitunguu, viazi, na dengu juu ya wali.
Mwagia sosi ya tuna na pambia jirshi (au zabibu).
Funika wali na upike katika jiko moto wa 450ยบ kwa muda wa kupikika wali. Epua upakue.

Mapishi ya Kachori

Mahitaji

Viazi mbatata (potato 4 vya wastani)
Nyama ya kusaga (mince beef 1 kikombe cha chai)
Kitunguu (onion 1 cha wastani)
Carrot 1
Hoho (green pepper 1/2)
Kitunguu swaum (garlic)
Tangawizi (ginger )
Binzari nyembamba (ground cumin 1/2 kijiko cha chai)
Binzari manjano (turmeric 1/2 kijiko cha chai)
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Limao (lemon 1/2)
Pilipili ya unga (chilli powder 1/2 kijiko cha chai)
Giligilani (coriander kiasi)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)
Unga wa ngano kiasi

Matayarisho

Katakata vitunguu na hoho katika vipande vidogo vidogo na kisha kwangua carrot na uweke pembeni. Chemsha viazi na chumvi kidogo vikiiva viponde na uviweke pembeni, Baada ya hapo tia nyama limao, chumvi, kitunguu swaum na tangawizi ichemshe mpaka iive na uhakikishe maji yote yamekauka. Kisha Tia binzari zote, pilipili, curry powder, giligilani, vitunguu, hoho na carrot. Pika mchanganyiko huo kwa muda wa dakika 3 na kisha ipua. Baada ya hapo changanya na viazi kisha tengeneza maduara ya kiasi na uyaweke pembeni. Chukua unga wa ngano kiasi na uchanganye na maji kupata uji usiokuwa mzito au mwepesi sana. baada ya hapo chovya madonge katika huo uji na uyachome katika mafuta. Hakikisha zinaiva na kuwa rangi ya brown na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.Unaweza ukazisevu na chatney yoyote unayopendelea.

Mapishi ya viazi mbatata Vya Nazi Kwa Nyama Ya Ng’ombe

Mahitaji

Mbatata / viazi – 2 kilo

Nyama ngโ€™ombe – ยฝ kilo

Kitunguu maji – 2

Tungule/nyanya – 2

Nazi /tui zito – 2 vikombe

Kitunguu saumu(thomu/galic) ilosagwa – 1 kijiko cha supu

Tangawizi mbichi ilosagwa – 1 kijiko cha supu

pilipili shamba/mbichi ilosagwa – kiasi

Mdalasini – 1 kipande

Bizari ya manjano – ยฝ kijiko cha chai

Bizari ya pilau/jiyrah/cummin – ยฝ kijiko cha chai

Ndimu/limau – 1

Namna Ya Kupika:

Chemsha nyama kwa kutia; chumvi, tangawizi, kitunguu thomu, mdalasini, na bizar zote.

Ipike nyama mpaka iwive na ibakishe supu yake kidogo.

Changanya tui la nazi pamoja na supu ilobakia.

Panga mbatata katika sufuria.

Tia nyama

Mwagia vitunguu na nyanya ulizotayarisha, tia pilipili.

Mwagia supu ulochanganya na tui

Funika upike mpaka viwive .

Tia ndimu

Jinsi ya kutengeneza Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

VIAMBAUPISHI

Unga – 4 Vikombe vya chai

Siagi – 1 Kikombe cha chai

Hiliki ยฝ Kijiko cha chai

VIAMBAUPISHI:SHIRA

Sukari – 2 Vikombe vya chai

Maji – 1 Kikombe cha chai

Vanilla ยฝ Kijiko cha chai

(cocoa ukipenda kugawa visheti aina mbili) 2 Vijiko vya chai.

JINSI YA KUTENGENEZA

Tia unga kwenye bakuli pamoja na siagi na hiliki.
Changanya vizuri isiwe na madonge.
Tia maji baridi vikombe viwili kasoro vya chai changanya ukiona bado ongeza maji kidogo, iwe kama chapati usikande uchanganye tu.
Halafu utakata sampuli unayopenda mwenyewe.
Unaweka karai ya mafuta yakisha kupata moto unaanza kuchoma moto usiwe mkali sana, kiasi, baadae unaweza kuongeza moto na vikaange hadi viwe rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta. .
Ukipenda gawa visheti sehemu mbili, na shira pia igawe sehemu mbili
Changanya nusu ya visheti kwa shira nyeupe.
Nusu ya shira nyingine ibandike tena motoni na tia cocoa vijiko viwili vidogo vya chai.
Inapochanganyika cocoa vizuri changanya nusu ya visheti ulivyogawa kupata visheti vya shira ya cocoa.

Mapishi ya Mlenda wa bamia na nyanya chungu

Mahitaji

Bamia (okra) 20
Nyanya chungu (garden eggs) 5
Magadi soda (Bicabonate soda) 1/4 ya kijiko cha chai
Nyanya (fresh tomato) 1
Chumvi (salt) kidogo
Pilipili 1/4

Matayarisho

Osha bamia, nyanya chungu na nyanya kisha vikatekate katika vipande vidogovidogo. Baada ya hapo vitie kwenye sufuria na vitu vyote vilivyobakia na kisha tia maji kidogo.Chemsha mpaka bamia na nyanya chungu ziive na vimaji vibakie kidogo sana. Baada ya hapo ziponde na mwiko kidogo kisha zikoroge na uipue na mlenda utakuwa tayari kwa kuliwa na ugali.

Mapishi ya Mitai

VIAMBAUPISHI

Unga wa ngano – magi 2 (vikombe vikubwa)

Hamira kijiko 1 cha chai

Sukari Vijiko 2 vya supu

Maziwa ยพ Magi

Siagi Vijiko 2 vya supu

Mafuta ya kukaangia kiasi

VIAMBAUPISHI:SHIRA

Sukari ยพ Kikombe

Maji ยพ Kikombe

Illiki ya unga kiasi

Zafarani kiasi

JINSI YA KUPIKA

Katika bakuli, changanya vipimo vyote pamoja na ukande unga usiwe mgumu wala laini sana uwe kiasi.
Kisha fanya donge moja na iache pahali penye joto mpaka iimuke.
Halafu weka mafuta ya kukaangia kwenye moto.
Sukuma donge hadi liwe duara sio nyembamba sana, kisha katakata kama maandazi.
Mafuta ya kisha pata moto choma mittai hukuunazigeuza hadi ziwive na kugeuka rangi.
Katika sufuria tia vipimo vya shira na iache ichemke isiwe nzito sana.
Mimina mitai kwenye shira na uzipepete, kisha weka kwenye sahani na zitakuwa tayari kwa kuliwa.

Jinsi ya kupika Mitai

VIAMBAUPISHI

Unga wa ngano 1ย 1/2 Kikombe

Baking powder 1 Kijiko cha chai

Baking soda ยผ Kijiko cha chai

Chumvi ยฝ kijiko cha chai

Sukari 1 kijiko cha supu

Hamira 1/2 Kijiko cha supu

Yai 1

Maziwa ยฝ Kikombe

Mafuta ya kukaangia

VIAMBAUPISHI:SHIRA

Sukari 1 Kikombe

Maji ยฝ Kikombe

Iliki au Mdalasini ยผ kijiko cha chai (ya unga)

MAANDALIZI NA JINSI YA KUPIKA

1. Kwenye bakuli, changanya pamoja unga, baking powder, baking soda, chumvi, sukari na hamira.

2. Katika kibakuli, piga mayai na maziwa pamoja.

3. Changanya mchanganyiko wa mayai na wa unga ; na ukande kama unga wa maandazi.

4. Ikisha fura, sukuma unga kama wa maandazi na ukate mitai .

5. Pasha moto mafuta na uchome hadi iwe rangi ya dhahabu, upande zote mbili.

6. Ipikie shira lakini isiwe nzito .

7. Tia mitai na upepete hadi sukari ienee kote na zitakuwa tayari kuliwa.

Mapishi ya Pilau Ya Kuku Kwa Mchele Mpya

Mahitaji

Mchele – 1 kilo

Kuku – 1

Vitunguu – 3

Viazi/mbatata – 5

Jira/bizari ya pilau nzima – 3 vijiko vya supu

Mdalasini – 1 kijiti

Pilipili manga – 1 kijiko cha supu

Hiliki – 3 chembe

Karafuu – 5 chembe

Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa – 3 vijiko vya supu

Tangawizi mbichi ilosagwa – 3 vijiko vya supu

Mafuta ya kupikia – ยฝ kikombe

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Baada ya kumsafisha kuku na kumkatakata, mchemshe kwa chumvi na ndimu, kijiko kimoja cha kitunguu thomu/somu na tangawizi yote..
Menya viazi, katakata vipande vya kiasi.
Katakata vitunguu maji kisha kaanga kwa mafuta katika sufuria ya kupikia pilau.
Tia bizari zote isipokuwa hiliki.
Saga hiliki kisha tia pamoja na kitunguu thomu/somu ukaange kidogo.
Mimina kuku na supu yake ikichemka kisha tia mchele na viazi.
Koroga kisha acha katika moto mdogomdogo wali uwive kama kawaida ya kupika pilau.

Jinsi ya kupika Biskuti Ya Keki Kavu kwa kizungu Shortcake

Viamba upishi

Unga 2 Magi (vikombe vya chai)

Sukari iliyosagwa 2/3 Magi (kikombe cha chai)

Siagi โ€… 220ย g

Unga wa mchele ยฝ Magi

Yai 1

Vanilla 1 kijiko cha chai

Jinsi ya kuandaa na kupika

1. Changanya vitu vyote hivyo kwenye bakuli mpaka unga ushikamane.

2. Paka mafuta treya ya kuchomea kisha utandaze kwenye treya ya 20cm kwa 30ย cm au (8 in kwa 12 in)

3. Choma kwenye moto 325หšC kwa muda wa saa nzima au mpaka ibadilike kuwa rangi ya dhahabu.

4. Epua acha ipoe kisha kata vipande kama mstatili, weak kwenye sahani tayari kunywewa na chai.

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Wiki Nzima cha Lishe Bora

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Wiki Nzima cha Lishe Bora ๐Ÿฅ—

Hakuna jambo bora kuliko kujihusisha na maisha yenye afya na lishe bora. Kwa wengi wetu, changamoto kubwa ni jinsi ya kujiandaa kwa chakula chetu cha wiki nzima ili tuweze kula vyakula vyenye virutubisho muhimu. Kama AckySHINE, mtaalamu wa lishe, ninafuraha kukushirikisha njia kadhaa ambazo unaweza kutumia kuandaa chakula chako cha wiki nzima cha lishe bora! ๐ŸŒฑ

Hapa kuna orodha yangu ya 15 ya hatua unazoweza kuchukua kufanikisha lengo hili:

  1. Tengeneza orodha ya ununuzi: Kupanga ni muhimu sana. Andika vyakula vyote unavyotaka kuwa nayo katika chakula chako cha wiki nzima. ๐Ÿ“

  2. Tafuta mapishi: Tafuta mapishi mbalimbali yanayokusisimua na yenye lishe bora. Kuna tovuti nyingi na programu za simu ambazo zinaweza kukusaidia kupata mapishi haya. ๐Ÿ“ฑ

  3. Nunua vyakula vyenye virutubisho muhimu: Nunua mboga mboga, matunda, nafaka na protini zenye lishe bora. Epuka vyakula vyenye sukari nyingi au mafuta mengi. ๐Ÿฅฆ๐Ÿ“

  4. Panga ratiba yako: Jijengee ratiba ya kushughulikia maandalizi ya chakula cha wiki nzima. Hii itakusaidia kuwa na mpango mzuri wa wakati na kufanya kazi yako vizuri. โฐ

  5. Fanya maandalizi ya kabla: Jitahidi kuandaa sehemu ya chakula chako kabla ya wiki kuanza. Kwa mfano, unaweza kuosha na kukata mboga mboga, na kuandaa mlo wa asubuhi kwa kuyaweka kwenye kontena. ๐Ÿ‘ฉโ€๐Ÿณ

  6. Pika mlo wa kwanza: Anza kwa kupika mlo wako wa kwanza wa wiki. Unaweza kuwa na chakula cha kiamsha kinywa, chakula cha mchana na chakula cha jioni tayari katika kontena au sahani zilizogawanyika kwa siku zote za wiki. ๐Ÿณ

  7. Tumia vyombo vya kuhifadhia: Vyombo vya plastiki au glasi vyenye sehemu tofauti vinaweza kukusaidia kuweka chakula chako salama na safi kwa muda mrefu. Hakikisha kuandika tarehe za kumaliza mlo wako kwenye vyombo hivyo. ๐Ÿฅฃ

  8. Fanya chakula kuwa kiburudisho: Hakikisha kuwa chakula chako cha wiki nzima kinakufurahisha. Jaribu mapishi mapya na ubunifu ili uweze kula vyakula tofauti kila siku. ๐Ÿฝ๏ธ

  9. Tumia vifaa vya kuongeza lishe: Kwa kuongeza lishe, unaweza kutumia viungo kama vile mbegu za chia, karanga, na tasty na vinywaji vya afya kama vile smoothies au matunda ya kuchoma. ๐ŸŒฐ๐Ÿฅค

  10. Hakikisha unakula kwa wingi: Ni muhimu kuhakikisha unapata mlo wa kutosha kwa siku nzima. Tenga sehemu yako ya kila mlo na kuzingatia uwiano sahihi wa protini, wanga na mafuta. ๐Ÿฝ๏ธ

  11. Panga vinywaji vyako: Hakikisha unakunywa maji ya kutosha kwa siku nzima. Weka chupa ya maji karibu nawe ili uweze kuinywa mara kwa mara. ๐Ÿšฐ

  12. Fikiria kuhusu uchumi: Kujiandaa kwa chakula cha wiki nzima kunaweza kukusaidia kuokoa pesa, kwani huwezi kutumia pesa nyingi kununua chakula nje. ๐Ÿช™

  13. Saidia familia na marafiki: Unaweza kuwahimiza familia na marafiki wako kujiunga na wewe katika kuandaa chakula cha wiki nzima. Inaweza kuwa ni jambo la kufurahisha na kuwapa motisha. ๐Ÿ‘จโ€๐Ÿ‘ฉโ€๐Ÿ‘งโ€๐Ÿ‘ฆ

  14. Uwepo wa akili: Kujiandaa kwa chakula cha wiki nzima kunahitaji subira na nidhamu. Kuwa na akili nzuri na uzingatia lengo lako. ๐Ÿ’ช

  15. Badilisha mapishi yako: Usiogope kubadilisha mapishi yako na kujaribu vitu vipya. Hii itakupa uzoefu mpya na kuongeza furaha yako ya kula chakula chako cha wiki nzima cha lishe bora. ๐ŸŒŸ

Kwa hivyo, kama AckySHINE, na mtaalamu wa lishe, ninaamini kuwa kujiandaa kwa chakula cha wiki nzima cha lishe bora ni njia nzuri ya kuboresha afya yako na kufurahia chakula chako kwa njia ya kipekee. Je, umeshawahi kujaribu kuandaa chakula chako cha wiki nzima? Je, unayo mbinu zako za kujiandaa? Nishirikishe mawazo yako katika sehemu ya maoni hapa chini! ๐Ÿ‘‡

Asante kwa kusoma, na kuwa na wiki njema ya lishe bora! ๐Ÿฅ—โœจ

Mapishi ya Chai ya maziwa, mandazi, uyoga na mayai

Mahitaji

Mandazi (angalia jinsi ya kupika katika recipe ya mandazi ya nyuma)
Uyoga (mashroom kikombe 1 cha chai)
Mayai (eggs 4)
Hoho (greenpepper 1/4 ya hoho)
Nyanya (fresh tomato 1)
Kitunguu (onion 1/4 ya kitunguu)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)
Hiliki nzima (cardamon 4)
Masala ya chai (tea masala 1 kijiko cha chai)
Pilipili mtama iliyosagwa (ground black pepper 1/4 ya kijiko cha chai)
Maziwa (fresh milk 1 kikombe cha chai)
Majani ya chai (tea leaves)
Maji kiasi.
Sukari (sugar)

Matayarisho

Jinsi ya kupika chai, weka maziwa, maji kiasi,hiliki, masala ya chai, pilipili mtama na majani katika sufuria. Chemsha kwa muda wa dakika 10 na chai itakuwa tayari.
Jinsi ya kupika mayai, weka mafuta kiasi katika fry pan na utie vitunguu, vikaange kidogo kisha tia nyanya, chumvi na hoho. Pika kwa muda wa dakika 4 kisha tia mayai na uyaache yaive mpaka yakauke kisha geuza upande wa pili na uyapike mpaka ya ive kisha ipua.
Jinsi ya kupika uyoga, weka mafuta kidogo katika fry pan kisha tia uyoga na chumvi na ukaange mpaka uive katika moto wa wastani. Ukisha iva breakfast yako itakuwa teyari kwa kuseviwa.

Mapishi ya Viazi vitamu na kachumbari

Mahitaji

Viazi utamu 3
Nyanya 2 kubwa
Kitunguu
Tango
Limao
Chumvi
Pilipili
Mafuta (vegetable oil)

Matayarisho

Menya viazi na kisha vikate katika vipande. Tia mafuta kwenye chuma cha kukaangia, yakisha pata moto tia viazi nauviache vikaangike mpaka upande mmoja uwe wa brown na kisha geuza upande wa pili na upike mpaka uwe wa brown. Vikisha iva ipua na uweke kwenye kitchen towel ili vikauke mafuta.
Kachumbali: Katakata vitunguu katika bakuli na kisha tia chumvi kwa ajili ya kuondoa ukali wa vitunguu. Baada ya hapo vioshe mpaka chumvi yote iishe. osha nyanya, Pilipili tango na kisha katakata slice nyembamba na uchanganye na vitunguu. Baada ya hapo tia chumvi, kamulia limao na uchanganye zote pamoja .Baada ya hapo viazi na kachumbali vitakuwa tayari kwa kuliwa.

Bisikuti Za Kokoa (Cocoa Biscuits)

Viambaupishi

Siagi 100gm

Unga wa kaukau (cocoa powder) 2 Vijiko vya supu

Maziwa mazito (condensed milk) Moja kikopo (397gm)

Bisikuti za Mary 2 Pakiti

Njugu ยฝ Kikombe

Karatasi la plastiki

Jinsi ya kuandaa na kupika

1. Vunjavunja bisikuti zote packet mbili ziwe vipande vidogo vidogo.

2. Pasha moto siagi mpaka ipate.

3. Tia kwenya siagi imoto maziwa mazito na cocoa koroga vizuri.

4. Kisha tia kwenye mchanganyiko bisikuti zilizovunjwa na njugu na uchanganye kisha epua motoni.

5. Paka karatasi la plastiki mafuta kidogo halafu tia mchanganyiko kisha kunja (roll).

6. Tia kwenye freeza muda wa saa.

7. Halafu toa karatasi na ukate kate na panga kwenye sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Upishi wa Afya kwa Kompyuta: Milo Rahisi na yenye Ladha

Upishi wa Afya kwa Kompyuta: Milo Rahisi na yenye Ladha ๐Ÿฒ๐Ÿ–ฅ๏ธ

Hivi leo, AckySHINE anataka kuzungumzia kuhusu jinsi ya kupika milo rahisi na yenye ladha kwa kutumia kompyuta. Unaweza kujiuliza, "Kwa nini AckySHINE anazungumzia upishi wa afya kwa kompyuta?" Vizuri, jibu ni rahisi. Katika dunia ya leo, teknolojia imeingia kwenye kila nyanja ya maisha yetu, ikiwemo upishi. Sasa hivi, tunaweza kutumia kompyuta zetu kupata mapishi, kununua chakula, na hata kupika kupitia programu mbalimbali za upishi. Kwa hivyo, hebu tuangalie jinsi ya kupika milo rahisi na yenye ladha kwa kutumia kompyuta!

  1. Tafuta programu za upishi kwenye kompyuta yako ๐Ÿ–ฅ๏ธ
    Kuna programu nyingi za upishi ambazo unaweza kuzipakua kwenye kompyuta yako. Programu hizi zinakupa mapishi mbalimbali kutoka kote duniani. Unaweza kupata mapishi ya vyakula vya Afrika, Asia, Ulaya na hata Marekani. Chagua programu ambayo inakidhi ladha yako na iweze kukupa mapishi rahisi kutoka kwa wataalamu.

  2. Chagua mapishi ambayo unaweza kufuata kwa urahisi ๐Ÿ“
    Wakati wa kuchagua mapishi, ni muhimu kuchagua yale ambayo unaweza kufuata kwa urahisi. Epuka mapishi yenye viungo vingi na hatua nyingi sana. Chagua mapishi ambayo yanatumia viungo rahisi kupatikana na mchakato wa kupika ni rahisi. Kwa mfano, unaweza kuamua kupika pilau ya nyama ya ng’ombe. Mapishi haya yanahitaji viungo kama vile mchele, nyama ya ng’ombe, vitunguu, pilipili na viungo vingine rahisi.

  3. Panga ni mapishi gani unataka kufanya ๐Ÿ“…
    Kabla ya kupika, ni muhimu kupanga mapishi gani unataka kufanya. Unaweza kuandaa orodha ya mapishi na kuamua ni lini utapika kila kitu. Hii itakusaidia kujiandaa vizuri na kuwa tayari na viungo vyote unavyohitaji.

  4. Nunua viungo vyote unavyohitaji ๐Ÿ›’
    Baada ya kuandaa orodha yako ya mapishi, nunua viungo vyote unavyohitaji. Hakikisha unanunua viungo vyenye ubora na safi. Unaweza kufanya hivi kwa kupitia programu yako ya upishi ambayo inaweza kukusaidia hata kununua viungo mtandaoni.

  5. Fuata hatua kwa hatua mapishi uliyochagua ๐Ÿ“–
    Sasa, ni wakati wa kuanza kupika! Fuata hatua kwa hatua mapishi uliyochagua. Hakikisha unazingatia muda unaopendekezwa na kuhakikisha kuwa unafuata kwa usahihi kila hatua. Kumbuka, upishi ni sanaa na inahitaji uvumilivu na uzingatiaji wa maelekezo.

  6. Tumia kompyuta kama rafiki yako wa upishi ๐Ÿค–
    Kompyuta yako ni rafiki yako wa upishi. Unaweza kutumia programu ya upishi ili kufuatilia muda wa kupika, kupata vidokezo na maelekezo wakati unapikia, na hata kupata mapishi ya milo mbalimbali. Kompyuta yako itakusaidia kuwa na ufanisi zaidi na kupika milo yenye ladha kwa urahisi.

  7. Jaribu mapishi mpya na ubunifu ๐ŸŒŸ
    Usiwe na hofu ya kujaribu mapishi mapya na kubadilisha ladha. Kompyuta yako inakupa fursa ya kupata mapishi kutoka kote duniani. Jaribu mapishi ya vyakula vya Kiafrika kama vile ugali na samaki, au jaribu mapishi ya vyakula vya Kichina kama vile chow mein. Kwa kufanya hivyo, utaweza kuboresha ujuzi wako wa upishi na kufurahia milo mbalimbali.

  8. Andika mapishi yako mwenyewe ๐Ÿ“
    Unapokuwa umeshajenga uzoefu na upishi kwa kutumia kompyuta, unaweza kuandika mapishi yako mwenyewe. Unaweza kuchanganya viungo mbalimbali na kubuni ladha yako ya kipekee. Kumbuka, upishi ni sanaa na wewe ni msanii wake. Andika mapishi yako na uhisi furaha na kujivunia mafanikio yako.

  9. Share mapishi yako na marafiki na familia ๐Ÿ‘จโ€๐Ÿ‘ฉโ€๐Ÿ‘งโ€๐Ÿ‘ฆ
    Unapotengeneza mapishi yako mwenyewe, usisite kushiriki mapishi hayo na marafiki na familia yako. Wanaweza kufurahia ladha yako ya kipekee na hata kukupa maoni yao juu ya mapishi yako. Hii itakusaidia kukua kama mpishi na kuboresha ujuzi wako zaidi.

  10. Jifunze kutoka kwa wataalamu ๐Ÿ‘จโ€๐Ÿณ
    Ni muhimu kujifunza kutoka kwa wataalamu wa upishi ili kuimarisha ujuzi wako zaidi. Unaweza kujiunga na madarasa ya upishi au hata kufuatilia wataalamu wa upishi kwenye mitandao ya kijamii. Hii itakusaidia kupata vidokezo na mbinu mpya za kupika.

  11. Tangaza upishi wako kwenye mitandao ya kijamii ๐Ÿ“ธ
    Mitandao ya kijamii ni njia nzuri ya kuonyesha talanta yako ya upishi. Unaweza kuchukua picha za milo yako na kuzishiriki kwenye mitandao ya kijamii kama vile Instagram au Facebook. Watu watavutiwa na milo yako yenye ladha na hata kukupa maoni chanya.

  12. Heshimu muda wa chakula ๐Ÿ•’
    Kupika kwa kutumia kompyuta kunaweza kukupa urahisi zaidi na kuokoa muda wako. Lakini ni muhimu kukumbuka kwamba chakula ni jambo muhimu na linahitaji kuheshimiwa. Tumia muda wa kufurahia milo yako na kuwa na mazungumzo mazuri na familia yako au marafiki wakati wa kula.

  13. Jitahidi kula lishe bora na afya ๐Ÿฅฆ๐Ÿ“
    Kama AckySHINE, napenda kukumbusha umuhimu wa kula lishe bora na afya. Hakikisha unachanganya aina tofauti za chakula kwenye milo yako, kama vile mboga na matunda. Epuka vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi. Vyakula vya jumla, kama vile mchele wa kahawia na mkate wa ngano, ni chaguo bora kwa afya yako.

  14. Kumbuka, upishi ni furaha na mchakato wa kujifunza ๐ŸŽ‰๐Ÿ“š
    Upishi ni furaha na mchakato wa kujifunza. Usikate tamaa ikiwa kitu hakikwendi sawa au kama una mapishi ambayo hayakufanikiwa. Kumbuka, kila mpishi huanza kutoka mwanzo na anajifunza kupitia uzoefu. Jifurahishe na upishi na ufurahie safari yako ya kuwa mpishi stadi.

  15. Je, unaonaje kuhusu upishi wa afya kwa kompyuta? ๐Ÿ˜Š
    Kama AckySHINE, nimejadili

Jinsi ya kupika pizza ya mboga mboga na cheese

MAHITAJI

1 kilo unga wa ngano
240 ml maji ya vugu vugu
2 olive oil kijiko kikubwa cha chakula
2 asali kijiko kidogo cha chai
1 chumvi kijiko kidogo cha chai
1 hamira ya chenga kijiko kidogo cha chai

JINSI YA KUPIKA

Chukua bakuli weka maji ya uvugu vugu, amira ya chenga, asali na chumvi kisha koroga ichanganyike vizuri acha itulie kwa dakika 10.
Kisha chukua olive oil na unga wa ngao mimina kidogo kidogo changanya mpaka ichanganyike safi kabisa kisha anza kukanda kama mchanganyiko wa chapati au maandazi.
Baada ya mchanganyiko wako kua mgumu safi kabisa funika bakuli lako na mfuko wa plastiki au cling film kwa muda wa saa 1 katika joto la chumba na mchanganyiko wako utaumuka baada ya muda huo. kisha ukandamize mchanganyiko huo wa unga na kua flati kama mwanzo.
Kata mafungu matano hadi saba ya ujazo sawa inategemea na ukubwa wa piza unaopenda we mlaji kisha sukuma umbo la duara.
Tengeneza mchuzi mzito wa nyanya kisha weka juu ya kitako cha piza na kuitandaza vizuri kwenye pizza yako kama unavyopaka siagi kwenye mkate. Usisahau kuweka chumvi na sukari kidogo katika mchuzi wa nyanya ili kukata uchachu.
Katakata nyanya, kitunguu, pili pili hoho, na bilinganya na kuziweka juu ya pizza yako kwa mpangilio ukitanguliza biringanya, ikifuatiwa na pili pili hoho, kitunguu maji na nyanya.
Kisha chukua mozarella cheese ikwaruze katika mkato mdogo rahisi kuyeyuka kwa kutumia kwaruzo la karoti linafaa.
kisha chukua mkwaruzo wa mozarella cheese na unyunyizie juu ya hizo mboga.
Weka pizza yako kwenye sahani ya bati au pizza pan ili isaidie kuiva upande wa chini.
Weka pizza yako kwenye oven ambayo imeshawashwa na ina joto 400 – 450ย F. Choma kwa dakika 20 hadi 25 iwe kaukau na rangi ya kahawia pia cheese itakua imyeyuka na kusambaa vizuri juu ya pizaa.

NB: Unaweza weka mchanganyiko wa nyama yeyote ile kama salami, nyama ya ngombe, nyama ya kuku au samaki kwa kufata maelekezo sawa sawa na hii piza ya mboga, tofauti yake itakua huweki mboga unaweka nyama.

Jinsi ya kupika Biskuti Za Njugu/Matunda Makavu (Rock Cakes)

Viambaupishi

Unga 4 Vikombe

Sukari 10 Ounce

Siagi 10 Ounce

Mdalasini ya unga 2 vijiko vya chai

Matunda makavu/njugu (kama lozi,
Zabibu, maganda ya chungwa,
Cherries na kadhalika 4 ounce

Maziwa ya maji 4 Vijiko vya supu

Jinsi ya kuandaa na kupika

1) Chukua siagi na sukari koroga na mixer mpaka iwe kama cream.

2) Tia vanilla mdalasini, tia yai moja mix tena endelea kuongeza yai lingine mpaka umalize yote, changanya mpaka iwe laini kama sufi (fluffy)

3) Tia unga na baking powder na dried fruits, changanya na mwiko.

4) Chota mchanganyiko na kijiko cha soup weka kwenye treya ya kupikia tandaza na uma ili upate matundu juu ya biskuti.

5) Pika (bake) kwenye oven lenye moto wa 375ย F. kwa muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama.

Shopping Cart
0
    0
    Your Cart
    Your cart is emptyReturn to Shop
    ๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About