1. Huwezi kubadili namna watu walivyokutendea mpaka ubadili namna unavyowatendea.
Matayo 7:12;
“Basi yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo Torati na Manabii.”
2. Huwezi kubadili tabia mpaka ubadili marafiki.
1Wakorintho 15:33
“Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.”
3. Huwezi kubadili ulichovuna mpaka ubadili ulichokipanda.
Wagalatia 6:7;
“Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.”
4. Huwezi kubadili mwelekeo wa maisha yako mpaka ubadili dereva.
Kutoka 23:1-3;
“Msivumishe habari za uongo; usishirikiane na mwovu kwa kuwa shahidi wa uongo. Usiwafuate walio wengi katika kutenda uovu; wala usitie ushahidi wako katika neno lolote kwa kugeukia kando na kuandamana na mkutano ili kupotosha hukumu; wala usimpendelee mtu mnyonge katika neno lake”.
Maisha yako yaweza ongozwa na mkumbo wa watu au MSIMAMO wako BINAFSI kwa UNACHOKIAMINI.
5. Huwezi kubadili hali yako ya kifedha mpaka ubadili tabia yako ya kifedha.
Mithali 21:17;
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; yeyote apendaye mvinyo, kula na manukato hatakuwa tajiri.”
Mtindo wa maisha ya ufukara ndiyo busara kwa wengi.
6. Huwezi kunibadili mpaka ujibadili mwenyewe.
Matayo 7:3-5.
“Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huioni? Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.”
7. Huwezi kubadili mtazamo wako wa kifikra mpaka ubadilipo usikiacho.
Mithali 23:7;
“Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.
Akuambia haya kula, kunywa; lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.”
(Waache wenye Hekima wasikilize na kuongeza ufahamu wao.)
Huyo anayesikiliza, huashiria na kuamua kile anachojifunza.
Kile unachojifunza, huashiria uelewa ulio nao kichwani mwako.
Uelewa ulionao kichwani mwako, huashiria maamuzi yako.
Na maamuzi yako, huashiria mwelekeo wa maisha yako.
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Nakuombea 🙏
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Mungu ni mwema, wakati wote!
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Katika imani, yote yanawezekana
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema hushinda hukumu
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Sifa kwa Bwana!
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Baraka kwako na familia yako.
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Tumaini ni nanga ya roho
Neema na amani iwe nawe.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Neema ya Mungu inatosha kwako
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mwamini Bwana; anajua njia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema zake hudumu milele
Dumu katika Bwana.
Mungu akubariki!
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Endelea kuwa na imani!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni