Viambaupishi: Wali
Mchele 3 Magi
Mafuta 1/4 kikombe
Karoti unakata refu refu 3
Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa 1 kikubwa
Pilipli manga 1/2 kijicho chai
Hiliki 1/2 kijiko chai
Karafuu ya unga 1/4 kijiko cha chai
Mdalasini wa unga 1/2 kijiko cha chai
Zaafarani (ukipenda) roweka katika maji 1 kijiko cha chai
Zabibu kavu (ukipenda) 1/4 kikombe
Chumvi kiasi
Jinsi ya kuandaa na kupika
1. Kwenye sufuria tia mafuta na kaanga karoti kidogo.
2. Tia vitunguu kisha tia bizari zote.
3. Tia maji kiasi (kutegemea aina ya mchele) na chumvi
4. Tia mchele upike uwive.
5. Karibu na kuwvia tia zabibu ukipenda.
6. Funika endelea kuupika hadi uwive.
Viambaupishi kwa Nyama
Nyama 2 Ratili (LB)
Chumvi Kiasi
Mafuta 1/4 kikombe
Kitunguu (kata virefu virefu) 1 Kikubwa
Pilipili mboga kubwa 2
(ukipenda moja nyekundu moja kijani)
unazikata vipande virefu virefu.
Figili mwitu (celery) kata vipande Miche miwili
virefu virefu
Jinsi ya kuandaa na kupika
1. Chemsha nyama hadi iwive
2. Ikaange kwa mafuta hadi iwe nyekundu
3. Weka vitunguu, pilipili mboga na figili mwitu
4. Kaanga kidogo tu kama dakika moja.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE