Karibu AckySHINE
Karibu AckySHINE
Chagua Unachotaka Kusoma Hapa
Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.
Ni vizuri kujua haya
👉🏿Degree au vyeti ulivyo navyo haviwezi kukupa mafanikio.
👉🏿Uzuri ulio nao hauwezi kukupeleka kwenye ndoto zako.
👉🏿Usipobadilisha hao marafiki ulio nao hutofika mahali popote.
👉🏿Usipobadilisha vitendo unavyovifanya kila siku hivyo hivyo mafanikio utayasikia kwa wengine.
👉🏿Kazi au ajira unayoifanya usipojiongeza haiwezi kukupeleka kwenye maisha unayoyataka.
👉🏿Huo mshahara unaolipwa usipoutumia vizuri na kujiwekea akiba au kuwekeza kidogokidogo hutoacha kulalamika kila siku mshahara mdogo au hautoshi.
👉🏿Usipoacha kukopa bila malengo mafanikio ni ngumu kuyapata.
👉🏿Usipowekeza muda kwa ajili ya kujifunza na kuelewa mambo mengi ya biashara na ujasiriamali kwa ujumla na kufahamu dunia imetoka wapi,iko wapi na inaelekea wapi huytoacha kulalamika.
👉🏿Usipolipia gharama za kujifunza na ukajifunza kweli kile unachoelekezwa ikiwa ni pamoja na Pesa na muda haya mambo waachie wengine.
👉🏿Usipobadili fikra na mtazamo wako huwezi kubadilisha chochote katika maisha yako.
👉🏿Ukiacha kusikiliza kila aina ya ushauri unaopewa na ndugu zako,jamaa zako,marafiki zako,familia yako,majirani zako na kujisikiliza wewe mwenyewe utahangaika sana.
👉🏿Usipofanya bidii na juhudi na ukakubaliana na changamoto zozote utakazokutana nazo maisha yatakuwa magumu sana kwako.
Kumbuka mtu pekee Wa kuyabadilisha maisha yako na kukusaidia kufikia malengo na ndoto zako wala sio mwingine ni mmoja tu nae ni WEWE.
Badilisha fikra zako,badilisha mtizamo wako,badilisha maisha yako.
Jinsi vitunguu swaumu vinavyosaidia kuzuia wadudu shambani
Vitungu saumu vina manufaa sana katika kukabiliana na aina mbalimbali za wadudu waharibifu na baadhi ya magonjwa kutokana na kuwa na harufu kali inayosaidia kuwafukuza wadudu kama vidukari, bungo na hata panya.
Hatua za kufuata kutengeneza dawa ya kitunguu saumu
- Saga kitunguu saumu kimoja,
- Changanyakwenye lita moja ya maji
- Nyunyizia kwenye mazao.
Namna nyingine ya kutengeneza dawa
- Unaweza pia kusaga vitunguu saumu 3,
- kishachanganya na mafuta taa,
- acha ikae kwa siku tatu,
- kisha ongeza lita 10 za maji ya sabuni na unyunyizie.
Hii itaondoa aina nyingi sana ya wadudu wanaosababisha magonjwa.
Jinsi ya kufanya kupunguza mwili kwa kupanga ulaji wa chakula
Ulaji wa vyakula vingi vya wanga na mafuta ni chanzo kikubwa cha unene na uzito kuongezeka. Vyakula kama ugali,wali,mkate mweupe,bia na pombe za kienyeji zinazotokana na wanga (kimea) huchangia kuongezeka kwa uzito. Matumizi ya aina hii ya chakula ni muhimu kupunguzwa katika mlo wako.
Yafuatayo ndiyo mambo ya msingi ya kuzingatia katika ualaji wa chakula ili kupunguza mwili
Acha kula vyakula vya Sukari
Sukari inayozidi mwilini toka katika vyakula hubadilishwa na kuwa mafuta. Vyakula kama chokuleti,biskuti,keki na vinyaji kama soda vina kiwango kikubwa cha sukari. Pia usitumie sukari nyingi katika chai na juisi.
Kula mboga mboga na matunda kwa wingi
Mboga mboga ni nzuri kwa afya kwa ujumla lakini pia haina mafuta hivyo itakufanya kuingiza mafuta kidogo mwilini.
Tumia Chai ya kijani
Umesikia kuhusu chai ya kijani (Green Tea), ni chai ambayo ni ya kijani na inasaidia kuondoa sumu za mwili (antioxadation). Hii inasaidia katika kusaidia mwili kuunguza mafuta katika njia inayoitwa thermogenesis.
Tumia chai ya Tangawizi
Tangawizi kama ilivyo chai ya kijani inafahamika kuongeza mmeng’enyo wa chakula tumboni hivyo kupunguza mrundikano wa mafuta yasiyotumika
Kunywa Maji mengi
Maji yanachangia kuharakisha mfumo wa uvunjaji chakula tumboni na hivyo kupunguza mafuta yanayohifadhiwa.
Matunda halikadharika hayapunguzi uzito moja kwa moja bali yatakufanya ushibe na usitamani kula kila mara kwani yanakata hamu ya chakula. Hivyo utaokoka na tabia ya kula kila mara ambayo huchangia sana kuongezeka uzito.
Acha kula kula ovyo nje ya milo maalumu
Uzito na kula kula hovyo ni marafiki wakubwa. Ukiona mtu ni mnene ujue anapenda kula. Ile kweli anakulakula ikimaanisha anakula kila mara na kila wakati chakula kinapokuwepo.
Anza leo kujenga tabia ya kula kidogo na katika milo muhimu mitatu.
Punguza matumizi ya Chumvi
Ndiyo,chumvi inaongeza uzito. Sodiamu iliyomo katika chumvi inachangia katika mchakato wa kikemikali unaopelekea kuongezeka uzito. Tumia chumvi katika kiwango kidogo.
Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata
Wali Wa Nazi
Mpunga – 4 vikombe
Tui la nazi – 6 vikombe
Chumvi – Kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele kisha
Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi.
Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.
Mchuzi Wa Samaki Nguru
Samaki – 4
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi – 2 viijiko vya supu
Kitunguu maji kilokatwakawa – 2 slice ndogo
Nyanya/tungule – 4
Nyanya kopo – 3 vijiko vya supu
Pilipili mbichi – 2
Kotmiri ilokatwakatwa – 3 msongo (bunches)
Bizari ya mchuzi (simba 2) – I kijiko cha chai
Ndimu – 1 kamua
Mafuta – ¼ kikombe
Chumvi kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katakata samaki mkaange kwa kumtia viungo.
Weka mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu. Vinapogeuka rangi thomu na tangawizi mbichi, nyanya, nyanya kopo, kitunguu na bizari ya mchuzi endelea kukaanga.
Tia maji kiasi na ndimu, pilipili mbichi ilosagwa kisha tia kotmiri.
Mwisho tia nusu ya samaki alokaangwa ukiwa tayari
Bilingani Za Kukaanga Na Viazi
Bilingani – 4 madogodogo
Viazi/mbatata – 3
Nyanya – 3
Majani ya mchuzi/mvuje/curry leaves – kiasi 6-7
Nnyanya kopo – 2 vijiko vya supu
Methi/uwatu ulosagwa – 1 kijiko cha chia
Rai/mustard seeds – 1 kijiko cha supu
Bizari ya manjano/haldi/turmeric – 1 kijiko cha chai
Chumvi – kiasi
Mafuta ya kukaangia – kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
1. Weka mafuta ya kukaangia katika karai
2. Katakakata bilingani vipande vipande vya mraba (cubes) kaanga katika mafuta ya moto hadi yageuke rangi. Eupa weka kando.
3. Katakataka viazi/mbatata vipande vidogodogo vya mraba (cubes) Kaanga hadi viive epua weka kando.
4. Ondosha mafuta yote katika karai bakisha kidogo tu kiasi ya vijiko 2 vya supu.
5. Kaanga rai kisha majani ya mchuzi, na methi/uwatu kisha kaanga nyanya.
6. Tia nyanya ya kopo kisha changanya pamoja bilingani na viazi ikiwa tayari.
Siri ya Kuwa na Amani ya Moyoni au Rohoni
Utangulizi
Amani ya Moyoni au Rohoni ni hali ya kutokua na wasiwasi na hofu moyoni kuhusu Mambo ya Rohoni na ya kidunia.
Ili kuwa na Amani ya Moyoni unatakiwa uishi kwa kutimiza wajibu wako wa kiroho na kidunia kama inavyotakiwa na kwa uwezo wako wote, Huku ukiwa na Matumaini ya kua kile unachokifanya kitafanikiwa, ni sahihi na umekifanya vizuri.
Uwe na Matumaini na utaipata Amani.
Amani ya Moyoni au Rohoni
Amani ya Moyoni au Rohoni ni hali ya kutokua na wasiwasi na hofu moyoni kuhusu mambo ya kiroho na ya kidunia. Ni hali ya utulivu na furaha ambayo hutokana na kuishi kwa namna inayolingana na maadili na imani zako, pamoja na kujua kwamba unafanya kila uwezalo kutimiza wajibu wako.
Kutimiza Wajibu Wako wa Kiroho na Kidunia
Ili kuwa na Amani ya Moyoni, unatakiwa uishi kwa kutimiza wajibu wako wa kiroho na kidunia kama inavyotakiwa na kwa uwezo wako wote. Hii inamaanisha kuwa mkweli kwa nafsi yako, kufanya kazi kwa bidii, na kuwa na nia safi katika kila jambo unalolifanya. Huku ukifanya hivyo, unapaswa kuwa na matumaini kwamba kile unachokifanya kitafanikiwa, ni sahihi, na umekifanya vizuri.
“Na lolote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo wote, kama kwa Bwana wala si kwa wanadamu, mkijua ya kuwa mtapokea kutoka kwa Bwana urithi kama thawabu. Mnamtumikia Bwana Kristo.” (Wakolosai 3:23-24)
Matumaini na Amani
Uwe na Matumaini na utaipata Amani. Matumaini yana nafasi kubwa katika kufikia amani ya moyoni. Matumaini ni imani kwamba mambo yatakuwa sawa hata kama hali inaonekana ngumu kwa sasa. Matumaini yanakusaidia kuvumilia changamoto na kukupa nguvu ya kuendelea mbele bila kukata tamaa. Hivyo, unapokuwa na matumaini na unajua kuwa unafanya jitihada zako zote, utaweza kupata amani ya ndani.
“Kwa maana mimi najua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa tumaini katika siku zenu za mwisho.” (Yeremia 29:11)
Shukrani na Kuridhika
Zaidi ya hayo, ni muhimu kujenga tabia ya kushukuru kwa kile ulichonacho na kukubali hali halisi ya maisha yako. Shukrani husaidia kuondoa hofu na wasiwasi, na inakuza hali ya kuridhika. Unapokuwa na moyo wa shukrani, utaona mambo mazuri katika maisha yako, hata yale madogo, na utaweza kufurahia safari yako ya maisha.
“Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” (1 Wathesalonike 5:18)
Afya ya Kiroho
Kujali afya yako ya kiroho pia ni muhimu. Tafakari, sala, na kufanya mazoezi ya kiroho kama vile kutafakari kwa kina, kujisomea vitabu vitakatifu au kuzungumza na washauri wa kiroho kunaweza kusaidia kuimarisha amani yako ya ndani. Pia, kujenga mahusiano mazuri na watu wengine na kusaidia jamii kunaweza kuongeza hisia za furaha na amani ndani yako.
“Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ambayo ndio mliyoitiwa katika mwili mmoja. Tena iweni watu wa shukrani.” (Wakolosai 3:15)
Hitimisho
Kwa kifupi, Amani ya Moyoni inakuja kwa kuishi maisha yenye uwiano kati ya mambo ya kidunia na ya kiroho, kuwa na matumaini, kushukuru, na kujali afya yako ya kiroho. Ni hali inayoweza kufikiwa kwa kufanya jitihada za dhati na kuwa na mtazamo mzuri juu ya maisha.
“Amani nakuachieni; amani yangu nawapa; si kama ulimwengu utoavyo, ndivyo mimi nivyo wapa ninyi. Mioyo yenu isifadhaike, wala isikate tamaa.” (Yohana 14:27)
Matumizi ya juisi ya limao kutibu shinikizo la chini la damu
Juisi hii ni nzuri sana katika kutibu shinikizo la juu la damu.
Lakini inaweza pia kutumika kutibu shinikizo la chini la damu hasa ikiwa hili shinikizo la chini la damu limesababishwa na upungufu wa maji mwilini (dehydration).
Kutibu shinikizo la chini la damu unaweza kuchanganya juisi ya limau na chumvi kidogo na sukari au unaweza kutumia maji maji ya miwa.
Kilichotokea baada ya polisi wa kibongo kukutana na mwizi mzungu
POLISI KAKAMATA MZUNGU ‘yestaday I saw u at ze maize shop..(jana nilikuona dukani kwa muhindi) when u saw me u started 2 six six.(uliponiona ulianza ku-sitasita) u ran n decided 2 plant a car.(ulikimbia na ukaamua kupanda gari) zen u pot-cry me through ze window.(kisha ukanichungulia dirishani) now sleep down n snake well b4 I cut u a millet.(sasa lala chini kisha nyooka vizuri kabla sijakukata mtama) Chezea lugha wewe..!!!
Jinsi ya kuondoa kitambi Kitaalamu
Hapo zamani kidogo tuliona na tulishuhudia watu wakisema ya kwamba mwanaume ambaye ana kitambi ndiye ambaye mwenye fedha, hiyo ni imani ambayo ilijengeka katika fikra na mitazamo yetu. Lakini katika karne hii mambo yamebadilika baada ya kuona baadhi ya madaktari wakieleza kwa kina ya kwamba kuwepo matumbo makubwa tanatokana na uwepo wa mafuta mengi katika kuta za tumbo.
Na mafuta hayo pindi ambao yanazidi huwa na athari sana kiafya, athari hizo za kiafya hupelekea mtu kuweza kupata magonjwa mbalimbali kama vile shinikizo la damu na magonjwa mengine mbalimbali.
Hivyo ili kuepukana na athari hizo zitokanazo na kitambi nakusihi ufanye yafuatayo:
1. Chakula
Huu ni msingi mwingine muhimu sana katika harakati za kupunguza unene na tumbo, kwa kifupi unahitaji kuzingatia yafuatayo:
- Kula mboga za majani kwa wingi kwani husaidia sana kiafya.
- Kunywa maji mengi sana
- Weka chakula cha kukutia hamu mbali na nyumba yako
- Kula vyakula ambavyo vitatumika kwa kiwango kikubwa katika kujenga mwili wako ila epuka kula vyakula vyenye mafuta kwa wingi.
2. Mazoezi ya viungo husaidia kupunguza tumbo.
Kwa kiwango kikubwa Unaweza kufanya mazoezi ya aina nyingi ili kupunguza tumbo. Mazoezi yoyote ya nguvu yatapunguza mafuta ya mwili wako pamoja na mafuta ya ndani (visceral fat).
Mazoezi ambayo nayazungumzia ni mazoezi ambayo yanasaidia kukata tumbo kwa kiwango cha juu sana. Mazoezi haya kwa karne hii ya teknolojia yapo wazi katika video mbalimbali.
Hivyo jaribu kutafuta video mbalimbali ambazo zitakusaidia kwa kiwango kikubwa katika kukata tumbo.
3. Hakikisha unapata usingizi Wlwa kutosha kwa siku.
Kupata usingizi kwa muda mzuri kumeonyesha kuwa na mchango katika kudhibiti kiwango cha mafuta katika mwili wa binadamu. Katika utafiti mmoja, watu waliopata usingizi kwa saa 5 hadi 7 kwa siku katika kipindi cha miaka 5, walionyesha kuwa na mafuta mwilini kidogo zaidi ukilinganisha na wale waliopata usingizi kwa pungufu ya saa 5 kwa siku.
Hivyo hakikisha unatenga muda wa kupumzika hasa pale unapokuwa una usingizi.
Utayarishaji bora wa chakula
· Osha mikono yako kwa sabuni kabla na baada
ya kutayarisha chakula
· Tumia vyombo safi na sehemu safi kwa
kutayarisha na kula chakula
· Viporo vipashwe moto vizuri kabla ya kula
· Chemsha maji ya kunywa na kuyaacha jikoni
dakika kumi baada ya kuchemka
Mapishi ya Half cake (Keki)
Mahitaji
Unga wa ngano (self risen flour) kikombe 1na 1/2
Sukari (sugar) 1/4 kikombe
Barking powder 1/2 kijiko cha chai
Magadi soda (bicarbonate soda) 1 kijiko cha chai
Mafuta 2 vijiko vya chai
Mafuta ya kukaangia
Maji ya uvuguvugu kiasi
Matayarisho
Changanya unga na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande (hakikisha unakuwa mgumu) Baada ya hapo sukuma na ukate shape uipendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama mandazi) Baada ya hapo ziweke sehemu yenye joto na uache ziumuke. Zikisha umuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani. Zikisha iva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili zichuje mafuta. Ziache zipoe na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Kuna watu makauzu ila huyu kazidi.. Soma hii!
Kakubaliana vizuri na msichana fulani hivi kuwa aibuke gheto, mchizi kajipanga vizuri kabisa…. mara saa nne hivi mdada kasema hana nauli.
Mshkaji kajikunja kamtumia Elfu tano maana mwenye shida alikuwa ni yeye……
Baada ya nusu saa yule dada akamtumia meseji.
“Jamani mpenzi, kumbe baba hatoki nilijua atatoka… sorry bae sitaweza kuja kwa leo… sooo sorry!”
Mshkaji jiii! hajajibu kitu…..
Baada ya muda kidogo meseji ikaingia katika simu ya binti, akajua mchizi kajibu. Mh! kutazama ni meseji kutoka Mpesa.
“CA90F0511 IMETHIBITISHWA Tshs 5000 ILIYOTUMWA KIMAKOSA KATIKA ACCOUNT YAKO IMETOLEWA SALIO LAKO NI Tshs 5”
Halafu ndo ikaingia meseji ya mshkaji.
“BASI POA SIKU NYINGINE KAMA VIPI”
#dada wa watu mashavu yakamshuka… hakuamini kilichotokea…. yaani jamaa keshawapigia Voda na pesa fasta imezuiliwa……
Tusali daima
Sala sio kitu cha muhimu kufanya wakati wa shida tuu. Sala ni kitu cha muhimu zaidi kila siku katika Maisha kuwe na shida au kusiwe na shida.
Biashara ya maisha
Biashara ya maisha ni kusonga mbele tuu. Maisha hayarudi nyuma wala hayafai kurudisha nyuma. Maisha yanasonga mbele.
KICHEKESHO: Ukiona masikini Kachinja kuku
Ukiona masikin kachinja kuku basi kat ya kuku au yeye kuna mmoja atakua mgonjwa 😆😆😆😆
Maswali yanayoulizwa sana Kumhusu Bikira Maria
Ni ipi sala bora kwa Bikira Maria? Kwa nini Tunasali kwa Bikira Maria?
Kwa nini watu wengi wanaomba kwa Bikira Maria?
Bikira Maria anatuombea kwa jina na mamlaka ya nani?
Je ni halali au ni sawa kwa Bikira Maria kutuombea kwa Jina la Yesu? Na Je tunajuaje kuwa Bikira Maria anaushirika na Yesu?
Je ni kweli kwamba Bikira Maria ni Malkia wa Kipepo?
Bikira Maria kukingiwa dhambi ya asili maana yake ni nini?
Mama wa Yesu ni nani?
Bikira Maria alimzaa Yesu Kristo kwa uwezo gani?
Ni kwa nini Bikira Maria anaitwa Mama wa Mungu? Na kwa nini aheshimiwe?
Je, Bikira Maria kuitwa Mama wa Mungu maana yake ni kwamba yeye ndiye chanzo cha Yesu na Bila yeye Yesu asingekuwepo?
Je Bikira Maria anamwonaje Yesu? Bikira Maria Anamchukulia Yesu kama nani Kwake?
Kwa nini Bikira Maria anapewa Heshima kubwa
Je, Bikira Maria anastahili kuabudiwa? Je Tunamwabudu Maria?
Kwa nini tunamuheshimu Bikira maria na kusali kwake?
Ni kwa nini Bikira Maria anaitwa Mama wa Kanisa?
Bikira Maria anafaida yeyote kwa Kanisa?
Nafasi ya Heshima kwa Bikira Maria ni ipi?
Kwa nini wakatoliki wanaweka sanamu Kanisani?
Sanamu au picha sio haramu bali maana ya hiyo sanamu au picha ndio inaiharamisha.
Tofauti ya Sanamu za Kikatoliki na za kipagani ni Kwamba,
Sanamu za Kipagani: Sanamu hizi huchukuliwa kama Mungu na huabudiwa na kutolewa Sadaka kama Mungu Mwenyewe.
Sanamu za Kikatoliki: Sanamu hizi huchukuliwa kama ishara ya kile inachokiwakilisha, haiabudiwi kamwe bali inaheshimiwa tuu.
Jifunze kupitia Sanduku la Agano na Msalaba wa Yesu
Kwa nini tunasali mbele ya Picha/Sanamu na Hasa kufanya Ishara ya msalaba?
Kwa nini watu wanabusu picha na sanamu?
Hapa duniani Yesu alizaliwa na nani?
Malaika alimsalimia Maria “umejaa neema”: maana yake nini?
Kwa nini Maria anastahili kuitwa “Mama wa Mungu”?
Je, Bikira Maria ni kama Bahasha au chombo cha kumleta Yesu tuu Duniani au anayo thamani zaidi?
Je, Maria amechangia wokovu wetu?
Je, Maria ni mama yetu pia?
Je, ni vizuri kumsifu Maria?
Je, sala inaweza kuwaendea Mama na marafiki wa Yesu (Watakatifu)?
Je, Bikira Maria alikua na watoto wengine Mbali na Yesu?
Je, Bikira Maria ni Bikira Daima au alizaa watoto wengine?
Tunaweza kuthibitisha kuwa Bikira Maria hakuzaa watoto wengine kwa kunukuu Biblia Kama ifuatavyo;
1. Bikira Maria Alikuwa Bikira Kabla ya kumzaa Yesu
2. Biblia Haiwataji ndugu wa Yesu wakati Yosefu na Maria walipokimbilia Misri kumficha Yesu na wakati waliporudi
3. Biblia haituambii kuwa Yesu alikua na wadogo zake alipokuwa na miaka 12
4. Kukosekana kwa neneo “Binamu” kwenye lugha ya Yesu
5. Biblia haitumii neno Ndugu, kaka au dada ikimaanisha ndugu wa kuzaliwa mama mmoja na baba mmoja
6. Undugu wa Yakobo, Simoni, Yosefu na Yuda kwa Yesu Sio wa mtu na kaka zake
7. Yesu alimwacha Mama yake kwa Yohane kwa kuwa hakuwa na Kaka na dada wakumwachia mamaye
Wazazi wa Bikira Maria ni nani?
Mafundisho kuhusu Neema
2. Neema ya msaada
1. Kwanza kwa Sakramenti ya Ubatizo
2. Sakramenti ya Kitubio
3. Kwa majuto kamili (majuto ya mapendo)
5. Kwa Sala
6. Kwa Ibada Takatifu
7. Kwa matendo mema
2. Na kupokelewa kwake mbinguni baada ya kufa
Huyu kashauzwa!! Angalia kilichomkuta sasa
Jamaa alionekana Mnyooooonge sana ikabidi mpita njia amuulize…
Kaka, mbona u mnyonge hivyo?”
Jamaa : ‘aaaaah we niache tu, kuna rafiki yangu nimemkopesha laki tano akafanye PLASTIC SURGERY ya uso, Mwanaharamu sasa nashindwa kumtambua!!!
😂😂😂😂😂😂
Mke anamwambia mme wake kuwa angetamani mme wake awe tajiri cheki alichojibiwa
Mke; mme wangu ungekuwa tajiri ningefurahi
Mimi; kwa nini?
Mke; ungekuta na sisi tuna gari nzuri hatutembeu kwa mguu
Mimi; ah wap,unadhani ningekuwa tajiri ningekuwa na wewe?ungekuta natoka na kina wema,zari…
😁😁😁
naona anakusanya nguo zake itakuwa anaenda kufua
Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nazi Wa Nyanya Chungu/Mshumaa/Ngogwe Na Bamia, Mboga Ya Matembele Na Samaki Wa Kukaanga
Vipimo Vya Ugali
Unga wa mahindi – 4
Maji – 6 kiasi kutegemea na aina ya unga
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Weka maji katika moto.
Tia unga kidogo katika kibakuli, koroga ufanye uji.
Maji yakichemka tia kwenye maji uwe uji.
Ujii ikiiva punguza kidogo tia unga kidogokidogo na usonge ugali. Ikiwa unga ni mgumu utaongeza maji ya ule uji ulopunguza usonge hadi uive ukiwa tayari.
Vipimo Vya Mchuzi Wa Nazi Kwa Nyanya Chungu/Mshumaa/Ngogwe Na Bamia
Nyanya chungu/mshumaa/Ngogwe – 7
Bamia – 10
Kitunguu maji – 2
Nyanya/tungule – 2
Tui la nazi jepesi – 2 viwili
Tui la nazi zito – 2
Chumvi – kiasi
Ndimu – 2 mbili kamua
Bizari manjano/haldi/turmeric – ½ kijiko cha chai
Pilipili mbuzi – 3
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katakata kitunguu maji na nyanya vipande vidogodogo sana kisha weka katika sufuria.
Iache ichemke kwa maji yake ya nyanya, ikishachemka tia maji kidogo kama robo kikombe.
Tia nyanya chungu, bamia na koleza ndimu, chumvi.
Iache ichemke. Inapokuwa tayari imeiva tia tui jepesi endelea kuacha katika moto huku unakoroga kidogo kidogo.
Tui jepesi likipungua kiasi chake, tia tui zito, kisha usiachie mkono koroga ikichemka kidog kiasi cha kuiva tui mchuzi tayari.
Vipimo Vya Mboga Ya Matembele
Matembele – 5 mafungu
Mafuta – ¼ kikombe
Kitunguu maji kilokatwakatwa – 1
Nyanya/tungule – 4
Chumvi – 1
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Punguza miche ya matembele kwa kuikata ncha kisha osha majani yake. Acha yachuje maji .
Weka mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji na nyanya hadi viivie.
Tia mboga, Iache ichemke kwa maji yake hadi iive. Ukiona bado haikuiva tia maji kidogo tu.
Ukipenda unatia ndimu kiasi cha kipande kimoja ukamue .
Samaki Wa Nguru Wa Kukaanga
Samaki Wa Nguru – 4 vipande
Kitunguu saumu(thom/galic) na tangawizi ilosagwa – 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi – 4
Ndimu – 2 kamua
Bizari ya samaki – 1 kijiko cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Mwoshe samaki kisha mtie kitunguu thomu, tangawizi ilosagwa, chumvi, pilipilimbichi ilosagwa, ndimu na bizari ya samaki.
Mwache akolee viungo kwa muda kidogo.
Makaange katika mafuta hadi aive akiwa tayari.
Recent Comments