Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

JINSI YA KUANDAA VILEJA

MAHITAJI

Unga wa mchele – 500g

Samli – 250g

Sukari – 250g

Hiliki iliyosagwa – 1/2 kijiko cha chai

Arki (rose flavour) – 1/2 kijiko cha chai

Baking powder – 1 kijiko cha chai

Mayai – 4

Maji ya baridi – 1/2 kikombe cha chai

MAANDALIZI

Saga sukari iwe laini kiasi, changanya unga wa mchele, baking powder, hiliki na sukari.
Pasha moto samli mpaka iwe nyepesi kama maji mimina kwenye ule mchanganyiko wa unga wa mchele, kisha uchanganye pamoja na arki.
Ongeza mayai yaliopigwa endelea kuchanganya mpaka unga umeanza kuchanganyika vizuri.
Ongeza maji ya baridi sana kama nusu kikombe tu ili uchanganyike vizuri.
Kata kwa design unayotaka viwe vinene visiwe kama cookies za kawaida kama ilivyo kwenye picha na ukipenda utaweka kidoto kwa kutumia zaafarani katikati ya kileja kama inavyoonesha hapo juu.
Choma kwa moto wa baina ya 300F na 350F kwa dakika 15 mpaka 20 visiwe vyekundu toa na tayari kwa kuliwa.

Huyu mtoto kaongea point kweli, angalia anachomwambia baba yake

Mtoto alimwuuliza baba yake,
Mtoto: Baba unaweza kumwachia hilo gari lako house boy/girl akaliendesha?
Baba: siwezi kumwachia gari langu hili aliendeshe ni ghali sana.
Mtoto: je mnaweza kumwachia chumba chenu house boy/girl kikiwa wazi na mkaenda kazini?
Baba: haiwezekani kamwe kuna vitu vya gharama na pia heshima haitakuwepo.

Mtoto: unaweza ukampa house boy/girl ATM CARD yako na namba ya siri ukakuchulie pesa?

Baba: mtoto unatafuta balaa sasa, unataka siku akiiba hii card akachukue pesa zote tuwe maskini, sithubutu.

Mtoto: aahaaaaaa, kumbe hauwezi kumkabidhi chochote chenye thamani house boy/ girl, sasa kwa nini mnanikabidhi mimi kwa house boy/girl na nyie mnaenda kazini mpaka mnarudi kumbe mimi sina thamani kwenu eeeeh!

Mapishi ya Wali, samaki wa nazi na kisamvu

Mahitaji

Mchele
Kisamvu kilichotwangwa
Samaki
Mbaazi
Nyanya chungu
Vitunguu
Nyanya ya kopo
Tangawizi
Kitunguu swaum
Vegetable oil
Curry powder
Tui la nazi (kopo 2)
Chumvi
Pilipili
Limao

Matayarisho

Safisha samaki kisha wamarineti na kitunguu swaum, tangawizi, pilipili, chumvi na limao kwa muda wa masaa 3.Baada ya hapo wakaange na usiwakaushe sana na uwaweke pembeni kwa ajili ya kuungwa.Katakata vitunguu maji, saga tangawizi na kitunguu swaum. Baada ya hapo injika sufuria ya mchuzi jikoni na mafuta kiasi ya kupikia, mafuta yakisha pata moto, tia vitunguu maji na vikaange mpaka viwe vya rangi ya brown. kisha tia kitunguu swaum na tangawizi.kaanga kidogo kisha tia nyanya ya kopo moja na ufunike. acha mpaka nyanya ziive. Kisha tia chumvi na curry powder na uache ikaangike kwa muda wa dakika 2 kisha tia samaki na nyanya chungu nakisha kamulia nusu ya limao. Geuza mpaka mchanganyiko uchanganyike vizuri kisha tia tui la nazi kopo moja na uache ichemke mpaka mchuzi uive.

Baada ya hapo chemsha kisamvu pamoja na mbaazi Kikisha iva, kaanga kitu na nyanya pembeni mpaka ziive kisha tia kisamvu. geuza mchanganyiko mpaka uchanganyike vizuri kisha tia tui la nazi na chumvi na aacha ichemke mpaka tui liive kisha ipua.malizia kwa kupika wali ambapo utachemsha maji kisha tia mafuta,chumvi na mchele na uupike mpaka uive kisha sevu na mboga ulizopika na mlo wako utakuwa tayari kwa kuliwa.

Jinsi ya kumshawishi mwanamke kufanya mapenzi

Zifuatazo ni njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke. Njia hizi zimegawanyika katika hatua mbili kuu, kwanza ni kumfanya akukubali na kisha kuamsha hisia zake.

 

Mfanye akukubali

Njia za kumfanya akukubali ni kama ifuatavyo

Uwe na muonekano mzuri

Wanawake wanapenda wanaume wasafi na watanashati kwa hiyo ukiwa msafi na mtanashati utakua na mvuto kwake. Hivyo utakapoamua kumshawishi kufanya mapenzi itakua rahisi yeye kuwa rahisi kukubali.

Mfanye ajisikie huru

Ni rahisi mwanamke kufanya mapenzi na mtu anayejisikia huru mbaele zake na ambaye yupo huru kuongea na kufanya nae mambo mengine ya kawaida katika maisha. Kwa hiyo ili uweze kumshawishi mwanamke kufanya mapenzi na wewe njia nzuri ni kumfanya ajisikie yupo huru mbele yako na kasha atakua huru kufanya mapenzi na wewe.

 

Mfurahishe

Mfanye ajisikie mwenye furaha kila anapokuwa na wewe na atamani kuwa na wewe. Akishajiskia mwenye furaha kila anapokuwa na wewe ni rahisi kushawishika kuwa na wewe kimapenzi.

Mfanye ajione kuwa yeye ni mzuri

Mwanamke anapenda sana na anavutiwa na mwanamme anayeona ubora wake au anayemsifia kuwa ni mzuri.

Mfanye akuamini

Mfanye aamini kwamba hata baada ya kufanya mapenzi bado mtakua pamoja na sio mwisho wa mahusiano yenu au urafiki wenu.

 

Usiwe na haraka, Mpe muda

Usiwe na haraka ya kumwambia kuwa unataka kufanya mapenzi na yeye bali subiri mpaka utakapoona yupo tayari au anaelekea kukuhitaji.

Mfanye akuone mwaminifu

Mfanye akuone mwaminifu kwa kutomchanganya na wanawake wengine. Usimuonyeshe kuwa una mahusiano na wanawake wengine. Mfanye aamini kuwa unamuhitaji yeye tuu.

 

Mjali kama mwanamke

Mfanye ajiskie kuwa mwanamke. Jaribu kuonyesha kuwa mwelewa, onyesha kuwa unajali, mkarimu na muonyeshe kuwa wewe ni msaada kwake. Mfungulie mlango, mbebee begi au pochi yake n.k.

Onyesha kuwa unapenda kila kitu kutoka kwake

Muonyeshe kuwa unampenda yeye na vyote vyake. Onyesha kuwa umevutiwa na yeye na mambo yake yote na sio mwili wake tuu.

 

Amsha Hisia zake

Baada ya kumvutia, sasa amsha hisia zake. Njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke au Hatua za kufuata kuamsha hisia za mwanamke ni kama ifuatavyo

Andaa mazingira

Andaa mazingira ya kuamsha hisia zake, fanya kitu kitakachowasogeza karibu na kuamsha hisia zake Kwenye akili yake kabla ya kugusa mwili. Mfano, weka mziki au muvi nzuri n.k. Kisha tengeneza mazingira ya kuwa karibu kimwili na kugusana.

 

Kaa kwa kubanana naye

Unapokuwa na mwanamke ambaye umemzimia, tafuta kisababu cha kukaa na yeye karibu. Toa simu muangalie pamoja videos kama vile za kuchekesha, ama unaweza kuchukua kitabu/gazeti umuonyeshe habari ambazo anapenda ilimradi tuu muwe karibu.

Usimwonyeshe/usiongee wazi kile unachotaka

Usijaribu kutumia lugha ya kutongoza ama utamfanya aanze kukushuku. Tayari anajua kuwa miguso ya mikono yako ya mara kwa mara inaashiria kitu fulani. Kile unachotakiwa kufanya ni kuivuruga akili yake kwa kuleta mada ambayo itamvutia huku ukiendelea gusa mwili wake

 

Anza kutumia lugha ya kumsuka

Wakati mtakuwa mnaendelea unaweza kutumia maneno ya kumsuka lakini yawe ya kichini chini. Mfano unaweza kumwambia “Unanukia utamu”, “nimependa kitambaa cha nguo yako”,”nishawahi kukuambia kuwa macho yako yanapendeza? Nimependa vile yanang’aa nikiwa karibu yako.” Maneno kama haya unaweza kumrushia mwanamke huyu bila hata yeye kusongea mbali na wewe. Mwanzo atakuwa anapenda kuyaskia.

Isome miondoko yake

Ukianza kumuona anazungumza polepole na kukusongelea karibu yako, ishara kuu ni kuwa yupo tayari. Kwa hiyo kufikia hapa unaweza kurudia hatua za kumsuka, kumgusa na kujaribu kufikia viungo vyake vingine vya mwili ilimradi nyote wawili mnafurahia.

 

Mbusu

Baada ya kuandaa mudi au mazingira na kuamsha hisia zake sasa tafuta namna ya kumbusu. Mbusu taratibu kwa namna ambayo haitamshtua na kumfanya aogope au akatae.

Mhikeshike

Wakati wa kumbusu mshike mwili wake ili kuamsha hisia zake. Anza na mikono kasha rudi kichwani Kwenye nywele zake na kisha maliza sehemu nyingine za kuamsha hisia zake

Usimlazimishe bali mbembeleze

Kama hataki usimlazimishe bali mbembeleze au muache mpaka wakati mwingine atakapokuwa tayari.

 

NB: Ni makosa makubwa na ni dhambi kufanya mapenzi kabla ya ndoa. Mbinu hizi zitumie kwa mwenzi wako wa ndoa

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Kutibu chunusi kwa ute mweupe wa yai

Hii inaweza kuchukuliwa kama njia rahisi na isiyo na gharma katika kutibu chunusi. Kwa mjibu wa wanasayansi kutumia mchanganyiko wa ute mweupe wa yai na maji maji ya limau ni namna nzuri ya kutibu chunusi.

Changanya ute mweupe wa mayai matatu na kijiko kidogo kimoja cha maji maji ya limau na ukoroge vizuri. Pakaa mchanganyiko huu usoni na uache kwa dakika 15 hivi kisha jisafishe na maji moto.

Fanya zoezi hili mara 1 au 2 tu kwa wiki

Madhara ya kisukari kwa nguvu za kiume

Kulingana na baadhi ya chunguzi zilizofanywa na wanasayansi asilimia 60 โ€“ 70 ya wanaume hupoteza nguvu za kiume kutokana na ugonjwa wa kisukari.

Sababu ni ngumu sana kuelewa lakini hutokana na mabadiliko ya mwili ambayo hutokea baada ya mtu kupata kisukari.

Ukiachana na kupata hamu ya kufanya tendo la ndoa mara kwa mara unatakiwa kuwa na mtiririko mzuri wa damu kwenye mishipa ya uume ili uweze kusimamisha uume kwa muda mrefu.

Unahitaji mishipa ya fahamu yenye afya na pia unahitaji homoni za kiume zakutosha.

Ugonjwa wa kisukari husababisha kudhoofu kwa mishipa ya damu, misuli pamoja na mishipa ya fahamu.

Uharibifu huu hupelekea mwanaume kupoteza uwezo wa kusimamisha uume kwa muda mrefu na baadae husababisha kushindwa kusimamisha uume kabisa.

Lakini pia ugonjwa wa kisukari hupelekea maradhi ya moyo na kusababisha matatizo makubwa mwilini.

Faida za matumizi ya Ukwaju kiafya

Faida kuu za ukwaju ni kama ifuatavyo:

Huondoa sumu Mwilini

Chanzo kizuri cha viua sumu mwilini ‘antioxidants’ ambavyo huzuia Saratani (cancer)

Una Vitamin B na C

Chanzo cha Vitamini B na C vile vile “carotentes”

Huondoa homa

Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya malaria na homa ya matumbo

Huzuia mafua

Huulinda mwili dhidi ya mafua na kero za mafua kooni

Husaidia mmengenyo wa chakula

Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula na kuondosha kuvimbiwa

Hutibu nyongo

Husaidia kutibu matatizo ya nyongo (bile disorders)

Husaidia kurahisisha choo (laxative)

Hupunvuza Lehemu

Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na hivyo kuimarisha moyo

Husaidia Ngozi

Husaidia ngozi kuwa nyororo, vile vile husaidia ngozi inayopona baada ya kuungua au yenye vidonda

Huua minyoo

Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo

Jifunze kitu Kwenye mfano huu kuhusu Maombi na kuomba

Nabii mmoja aliumwa
na Jino, lilimtesa sanaโ€ฆ
Akapiga magoti kumlilia
Mungu ili amponye..
Mungu akamuonesha mti
flani ili majani yake
Yapate kumtibu..
Akaenda kwenye mti ule,
Akachukua majani yake
akatumia na kweli
akaponaโ€ฆ
Baada ya Muda Mrefu
Kupita, nabii yule aliumwa
na Jino tenaโ€ฆ
Safari Hii alienda
moja kwa moja kwenye mti
Na kuchuma majani yake
na kuyatumia,Lakini
hakupona..
Akaja tena Kwa Mungu
na kumwambiaโ€ฆ
“Mbona ule mti niliutumia
Haukuniponyesha kama
Wakati ule? “
Mungu akamjibuโ€ฆ
“Mara ya Mwanzo ulipona
Kwa kuwa
ulinitegemea mimi, mara ya
Pili hakupona kwa kuwa
Uliutegemea Mti”..

KILA WAKATI TUNAPASWA
KUMUOMBA NA
KUMTEGEMEA MUNGU,
HATA KAMA KWA JAMBO
AMBALO ALISHATUJIBU..
KWA KUTOKUFANYA HIVYO
NDIYO MAANA MARA
KADHAA
TUNAKOSA MAFANIKIOโ€ฆ

โœ”Tulipooomba mchumba
Tulipompata
Hatukuombea Ulinzi wa
ndoa zetu, matokeo yake
Ni vilio kwenye ndoa
Karibu zote..

โœ” Tuliomba watoto,
Tulipowapata
muda mwingi tukatumia
Akili zetu kuwalea
Na kusahau kumshirikisha
Mungu katika malezi yao,
mwisho wa yote
Tunaishia kusema
Watoto wa siku hiziโ€ฆ

โœ” Tuliomba kazi kwa Mungu ,
Tulipopata tukaanza
Kutumia akili zetu katika
Kazi hizo na kuanza
Kudharau wenzetu na
Kuzisaliti ndoa
na familia zetu..
โ–ช Familia zinaliaโ€ฆ
โ–ช Watoto wanalia
Baraka zitatoka wapi?

โ–ช Kabla ya Kupata kazi
Tulikuwa Hatukosi
Kanisani,
Hakukosi kwenye
Maombiโ€ฆ
TUMEPATA KAZI
TUMEKUWA BIZE
HAKUNA MAOMBI
WALA KANISANI..
Baraka zitokee wapi?
Mafanikio yatoke wapi?
Mshahara mkubwa
Lakini madeni kila siku,
Tena tunakopeshwa na
Tuliowazidi mshaharaโ€ฆ

Wapendwa tustuke..
Tumrudie Munguโ€ฆ
Tusisingizie uchawi..
Tumejiroga wenyewe..

Tumuweke Mungu mbele..

Tafakari chukua hatua

Cheki kilichonipata sasa, ungekua wewe ungefanyaje?

Siku moja katika pitapita zangu nikakutana na mtoto mmoja mkali balaa yaani ni mzuri sanaaaa, moyo ukanituma nimuimbishe mtoto akakubali kwamba nitafute siku tukae tuongee vizuri akasema nimpe namba yangu ya simu.

ย 

Ebwana si akatoa simu hiyo inauzwa laki sita mimi hapa nina kisimu cha tochi tena nimefunga na rababendi
Je, wewe ungeendelea kumtajia namba zako!!!

Baada ya kumkuta mwanamme mwingine chumbani kwake na mke wake cheki huyu anachokifanya

NAKUA(BABA) karudi kazini mwanae mdogo akamuwahi,
DOGO: Baba usiingie ndani kina jini chumbani kwenu
NAKUA: Hakuna kitu kama hicho
DOGO: Kweli baba kuna jini liko kwenye kabati lenu la nguoโ€ฆ.

NAKUA kaingia ndani kamkuta mkewe kalala kitandani kajifunika shuka gubigubi hadi kichwani. Kaenda kwenye kabati kufungua mlango , akamkuta rafiki yake wa miaka mingi yuko uchi ndani ya kabati
NAKUA: Aise unajua we fala sana, we rafiki yangu miaka yote hiyo halafu unamtisha mwanangu eti wewe jini, hebu toka huko nenda kwenu kacheze michezo hiyo na mwanao.

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini Ya Pilipili Mbichi

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama

Nyama ya ngโ€™ombe vipande vidogo – 2lb

Nyanya – 1

Kitunguu Kilichoktwa katwa – 1

Mafuta – 2 vijiko vya supu

Paprika (bizari ya masala ya rangi) – ยฝ kijiko cha chai

Kidonge cha supu – 1

Chumvi – Kiasi

Ndimu – Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha nyama kwa chungio ili itoke maji. Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwerangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.
Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.

Vipimo Vya Mboga

Mchicha ulio katwa katwa 400 gm

Nyanya 1

Kitunguu kilicho katwa 1

Nazi ya unga kiasi

Pilipili mbichi 2

Mafuta ยฝ kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha na Kupika

Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.
Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.
Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji
Tia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa
tayari kuliwa

Vipimo Vya Maharage

Maharage – 1 kopo

Kitunguu – 1

Nazi – 1 mug

Nyanya (itowe maganda) – 1 kiasi

Pilipili mbichi – 2

Mafuta – 1 kijiko cha supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.
kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.
Tia chumvi, maharage na nazi uwachie
moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.

Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi

Pilipili mbichi – 4/5

Kotmiri – 1 Kijiko cha supu

Ndimu – kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 1 chembe

Mafuta ya zaituni – 2 vijiko Vya supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha

Kwenye blender, tia vipimo vyote na sage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Vipimo Vya ugali

Maji – 4 Vikombe kiasi inategemea na unga

Unga wa sembe – 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.

Jinsi ya kung’arisha sura yako kwa kutumia Asali, Sukari, Maziwa, na Limao

Usafi wa uso ni moja ya mambo muhimu sana kwa mwanamke au mwanaume yeyote yule ambaye anapenda kuwa nadhifu na mwenye mvuto. Kumbuka โ€œreception ndio kila kitu โ€œ. Unapokutana na mtu sura yako na mwonekano wa sura yako ndio kitu cha kwanza kinachomtambulisha kwamba wewe ni nani na upo kwenye hali gani.

Kuna njia nyingi za kuufanya uso wako uvutie na kupendeza. Leo tutaongelea zaidi jinsi ya kusafisha uso kwa njia ya asili. Mie hupenda kutumia njia ya asili sababu ni rahisi kupata vifaa na ni nafuu . Pia mtu anaweza kufanya kwa mazingira yoyote yale. Na matumizi ya vitu vya asili kwenye mwili husaidia kupunguza sumu mwilini kwani kutumia vipodozi vyenye kemikali husababisha miili yetu kujaaa sumu.

Njia ya asili ya kusafisha na kupendezesha mwili ninayokueleza leo inahitaji vitu vikuu vinne : asali, sukari, maziwa, na limao.

Haijalishi aina gani ya ngozi unayo , njia hii ya asili inaweza kutumika kwa aina yoyote ile ya ngozi iwe ngozi yenye mafuta au ngozi kavu.

Kiasi cha mahitaji yanayohitajika:

  • Kijiko kimoja cha asali
  • Kijiko kimoja cha sukari
  • Kijiko kimoja cha maziwa
  • Kijiko kimoja cha limao

Utaratibu wa kusafisha uso

Weka mahitaji hapo juu kwenye chombo kilicho kisafi, changanya vitu vyako mpaka vilainike, viache kwa muda wa dakika 10 ili viweze kuchanganyikana vizuri na na sukari iweze kuyayuka vizuri.

Baada ya mchanganyiko wako kuwa tayari chukua kipande cha pamba kilicho kisafi tumia kupakia mchanganyiko wako usoni . Na kumbuka ni vizuri uso ukiwa mchafu na upaswi kuosha uso alafu ufanye zoezi hili. Baada ya kupaka mchanganyiko wako usoni kaa kwa dk 15 .

Baada ya hapo chukua maji ya uvuguvugu, kitaulo kisafi na sabuni ya kipande โ€œvizuri kutumia sabuni ya kipande maana haina kemikali nyingiโ€ tumia kitambaa kuoshea uso wako pamoja na sabuni.

Basi baada ya hapo umekuwa umemaliza zoezi lako la usafi wa ngozi yako
Kumbuka njia hii aina madhara yoyote na haibadilishi rangi au muonekano wa ngozi yako na unashauliwa kufanya mara kwa mara ili kukupa mvuto zaidi.

Angalia haya mazungumzo ya msichana na mvulana, mapenzi ya ajabu haya

Demu: Hny mambo jamani!
Man: Safi nipe habari wangu wa moyo
Demu:Wafanya kazi gani vile wangu?
Man: Ni fundi wa kufunga ATM
Demu: Wow dont tel me i love you myn mwa mwa mwaaaaah

Man: Mbona wafurahia?
Demu: Nami natamani kuja kufanya kazi za kibenki.
Man: Itakua poa sana nami natamani pia
Demu: Hee si umesema wafanya kazi ya kufunga ATM?
Man: Hukunielewa mie ninafunga mashine na za kunulia condom kwenye bar
Demu: nipishe huko

Mapishi ya Ndizi za nazi na utumbo

Mahitaji

Ndizi mshale 10
Utumbo wa ng’ombe 1/2 kilo
Nazi ya kopo 1
Nyanya 1
Kitunguu kikubwa 1
Tangawizi/ swaum 1 kijiko cha chakula
Olive oil kiasi
Limao 1
Chumvi
Curry powder 1 kijiko cha chai
Turmaric 1/2 kijiko cha chai
Coriander ya powder 1/2 kijiko cha chai
Pilipili ya unga 1/2 kijiko cha chai
Pilipili kali nzima (usiipasue)

Matayarisho

Safisha utumbo kisha uweke ktk pressure cooker pamoja na chumvi kiasi, limao, tangawizi, swaum na maji kiasi kisha uchemshe kwa muda wa nusu saa. Baada ya hapo menya ndizi kisha zikate vipande vidogo kiasi ili ziwahi kuiva, kisha ktk sufuria ya kupikia tia vitunguu na nyanya kisha ndizi kwa juu yake na supu ya utumbo kiasi chumvi kidogo na mafuta kiasi kisha bandika jikoni na uchemshe mpaka ndizi zikaribie kuiva. Zikisha karibia kuiva tia utumbo na spice zote, pilipili nzima na tui la nazi kisha changanya vizuri na uache vichemke mpaka ndizi na tui la nazi vitakapoiva na rojo ibaki kiasi. Baada ya hapo Ndizi zako zitakuwa tayari kwa kuliwa.

CleanUp 48 SL: Dawa Maalumu ya Kuua Magugu sumbufu. Dawa ya kuandalia Shamba. Haichagui Aina ya Majani.

Ina Glyphosate isopropylamine salt 480g/L

Hii ni dawa maalumu Kwa ajili ya kuulia Magugu. Ni dawa ya kuandalia Shamba.

Dawa hii inaangamiza Magugu Aina zote shambani. Sio Kwa ajili ya palizi.

Imetengenezwa katika Ubora wa Hali ya Juu Ili kukuhakikishia matokeo mazuri unapotumia dawa hii.

Bidhaa hii inaletwa Kwako na Kampuni ya BareFoot International Limited. Wauzaji na wasambazaji wa bidhaa Bora za Kilimo Tanzania.

Mawasiliano

Simu:

+255 756 914 936

โ€”

WhatsApp:

+255 756 914 936

โ€”

Email:

info@bfi.co.tz

โ€”

NB: Tunapatikana Mikoa Yote Tanzania

Mipango ya Mungu kwetu sisi wanadamu

Utangulizi

Mipango ya Mungu daima ni myema, Mungu anapanga Mema katika maisha ya mtu kama akifuata mapenzi yake. Tatizo ni kwamba watu wanafuata mapenzi yao wenyewe na kisha kukosa yale mema Mungu aliyopanga kwao.

Sio kila jambo jema unalofikiri kulifanya ni jema, kama halipo katika mipango ya Mungu halifai na linaweza kuzuia yale mema Mungu aliyopanga kwako.

Kwa hiyo, jitahidi kufahamu mapenzi ya Mungu na kuyafanya ili uwe katika mipango yake.

Mipango ya Mungu Daima ni Myema

Mipango ya Mungu ni kamilifu na inatufanyia mema ikiwa tutaifuata. Mungu anapanga mema kwa ajili ya maisha yetu, lakini mara nyingi tunashindwa kuona mema hayo kwa sababu tunafuata mapenzi yetu wenyewe badala ya mapenzi ya Mungu. Katika kila jambo tunalofanya, ni muhimu kutafuta kujua mapenzi ya Mungu na kuyatekeleza ili tuweze kuwa katika baraka na neema zake.

Mipango ya Mungu ni Kamilifu

Jeremia 29:11 inasema:
“Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.” (Jeremia 29:11)

Mungu anatuwazia mema na anatupangia maisha yaliyojaa amani na mafanikio. Hata hivyo, ili tuweze kuona mipango ya Mungu ikitimia katika maisha yetu, tunahitaji kumfuata na kutii mapenzi yake.

Tatizo la Kufuata Mapenzi Yetu Wenyewe

Mara nyingi, tunachagua njia zetu wenyewe na kutozingatia mapenzi ya Mungu. Hii inatufanya tukose yale mema ambayo Mungu ameyapanga kwa ajili yetu. Mithali 14:12 inasema:
“Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti.” (Mithali 14:12)

Hii inatukumbusha kwamba si kila jambo tunalofikiri ni jema linakubalika mbele za Mungu. Ni muhimu kujua mapenzi ya Mungu na kuyafuata.

Jitahidi Kufahamu Mapenzi ya Mungu

Warumi 12:2 inasema:
“Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” (Warumi 12:2)

Tunapaswa kubadili mawazo yetu na kujua mapenzi ya Mungu kwa kusoma Neno lake na kuomba mwongozo wake. Kwa njia hii, tutaweza kutambua yale yaliyo mema na kukubalika kwake.

Mifano 10 ya Watu Waliopokea Mema kwa Kufuata Mapenzi ya Mungu

  1. Noa:
    Noa alifuata mapenzi ya Mungu kwa kujenga safina kama alivyoagizwa, na akawaokoa familia yake na wanyama wakati wa gharika. (Mwanzo 6:13-22)
  2. Ibrahimu:
    Ibrahimu alitii mapenzi ya Mungu alipomtoa mwanawe Isaka kama sadaka. Kwa imani yake, alibarikiwa na kuwa baba wa mataifa mengi. (Mwanzo 22:1-18)
  3. Yusufu:
    Yusufu alitii mapenzi ya Mungu hata alipouzwa utumwani na ndugu zake. Mwisho wa yote, Mungu alimtumia kuokoa Misri na familia yake kutokana na njaa. (Mwanzo 37-50)
  4. Musa:
    Musa alifuata mapenzi ya Mungu kwa kuwaongoza Waisraeli kutoka utumwani Misri kwenda kwenye nchi ya ahadi. (Kutoka 3:1-22)
  5. Yoshua:
    Yoshua alitii mapenzi ya Mungu alipowaongoza Waisraeli kuvuka mto Yordani na kushinda mji wa Yeriko kwa kuzunguka ukuta wake kama alivyoagizwa. (Yoshua 6:1-20)
  6. Gideoni:
    Gideoni alifuata mapenzi ya Mungu alipowachagua wanaume 300 kupigana dhidi ya jeshi kubwa la Wamidiani. Kwa imani yake, walipata ushindi mkubwa. (Waamuzi 7:1-25)
  7. Samueli:
    Samueli alitii mapenzi ya Mungu alipomteua Daudi kuwa mfalme wa Israeli, ingawa Sauli alikuwa bado anatawala. (1 Samweli 16:1-13)
  8. Daudi:
    Daudi alitii mapenzi ya Mungu alipompiga na kumuua Goliathi kwa jina la Bwana, na kuokoa Israeli kutoka kwa Wafilisti. (1 Samweli 17:45-50)
  9. Elia:
    Elia alifuata mapenzi ya Mungu alipotangaza njaa na mvua katika Israeli kulingana na amri ya Mungu. (1 Wafalme 17-18)
  10. Maria:
    Maria, mama wa Yesu, alitii mapenzi ya Mungu alipokubali kuwa mama wa Masiya, licha ya changamoto na aibu ambayo ingemkabili. (Luka 1:26-38)

Hitimisho

Mipango ya Mungu daima ni myema. Mungu anapanga mema katika maisha ya mtu kama akifuata mapenzi yake. Tatizo ni kwamba watu wanafuata mapenzi yao wenyewe na kisha kukosa yale mema Mungu aliyopanga kwao. Si kila jambo jema tunalofikiri kulifanya ni jema mbele za Mungu. Kwa hiyo, jitahidi kufahamu mapenzi ya Mungu na kuyafanya ili uwe katika mipango yake. Kwa kufuata mapenzi ya Mungu, tutapata mema yote aliyoyapanga kwa ajili yetu na kuishi maisha yenye baraka na amani.

SMS nzuri ya mapenzi ya kutakia usiku mwema

Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka.
Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika.
Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka.
Kitale katikati yake ukila utaridhika.
Matamu na maji yake hukata kiu haraka.
Weupe watui lake lina ladha ukipika.
Kupaka mafuta yake mwili hulainika.
Na kwenye machicha yake kazi nying hufanyika.
Hata na upepo wake uvumapo utacheka.
Sikijui kitu chake kipi kisichotumika.usiku mwema

Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa

Mapishi ya bagia na chatney ya machicha ya nazi

Mahitaji

Kunde (Ila mimi nilitumia Nigerian brown beans 1/2 kilo)
Vitunguu maji (onion 2)
Pilipili (scotch bonnet pepper 2)
Vitunguu swaum (garlic 4 cloves)
Chumvi (salt)
Barking powder (1/2 kijiko cha chai)
Machicha ya nazi (grated coconut 1 kikombe cha chai)
Limao (lemon 1)
Mafuta (vegetable oil)

Matayarisho

Loweka kunde usiku mzima kisha ziondoe maganda na uzitie kwenye blender pamoja na vitunguu maji, vitunguu swaum, pilipili, chumvi,barking powder na maji kiasi. Visage vitu vyote mpaka viwe laini na kisha uutoe na kuweka kwenye chujio ili uchuje maji. baada ya hapo zikaange katika mafuta mpaka ziwe za brown na uzitoe na kuziweka kwenye kitchen towel ili zichuje mafuta.Baada ya hapo saga machicha ya nazi,limao, pilipili chumvi pamoja na maji kidogo na hapo chatney yako itakuwa tayari kwa kuseviwa na bagia.

Shopping Cart
17
    17
    Your Cart
    ๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About