Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

MAFANIKIO YA MAISHA SIO ELIMU TU, UTHUBUTU, KUJIAMINI NA UJASIRI WA MAAMUZI

โœ๐ŸฝUkichunguza katika jamii, utabaini kuwa sehemu kubwa ya matajiri ni wale ambao wana elimu ndogo ama hawakusoma kabisa.

๐Ÿ‘‰๐ŸพKatika miji na maeneo yote; wenye majengo ya maana, wenye makampuni makubwa, wenye utitiri wa malori na mabasi, wenye maduka makubwa ni wale wa “darasa la sabaโ€ au wale ambao hawakuingia darasani kabisa

๐Ÿ™‡๐Ÿฝ๐Ÿ“š Wasomi wengi wana maisha ya kawaida yaani yale ya kiwango cha kubadilisha mboga, wakijitahidi sana wanaishia kujenga nyumba za kuishi ๐Ÿก na ๐Ÿš— ๐Ÿš™magari mawili ya kutembelea (tena kwa mikopo!)

๐Ÿ‘‰๐ŸพWapo ๐Ÿ™‡๐Ÿฝ๐Ÿ“šwasomi wengi tu wanaoishi kimasikini, kwa lugha ya kistaarabu tunasema wana maisha ya kuungaunga. Kiukweli idadi ya wasomi walio matajiri ni ndogo sana

๐Ÿ‘‰๐ŸพLakini Umasikini wa wasomi wengi umeanzia huko shuleni na vyuoni wanakopatia usomi wao. Madarasani kuna mambo mawili wanafundishwa wasomi ambayo ndio yanayowaroga

Hii inachangiwa na mambo mawili:-
๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ
I. Wameelimishwa na kuaminishwa kwamba yule anaepata maswali yote kwa usahihi ndio anaonekana amefaulu. Ukikosea unahesabika kuwa u mjinga na wenyewe wanaita umefeli

๐Ÿ‘‰๐ŸพHata hivyo katika maisha ya kawaida hasa kwenye mchakato wa kutafuta hela, kujaribu na kukosea ni sehemu ya mafanikio

๐Ÿ‘‰๐ŸพKadiri unavyojaribu na kukosea mara nyingi ndivyo unavyojifunza na ndivyo nafasi ya kutajirika kwako inakuwa kubwa!

๐Ÿ™‡๐Ÿฝ๐Ÿ“šWasomi wengi kwa sababu ya “mentality” ya kuogopa kukosea huwa hawapendi kujaribu biashara kwa hofu ya kushindwa kuiendesha, na huamua kufa kimasikini wakitegemea mishahara pekee kwa sababu mishahara ndio pato lao la uhakika
๐Ÿ‘‡๐Ÿพ
II. Madarasani kunahimizwa ubinafsi badala ya umoja. Angalia namna mitihani inavyofanyika. Kila mwanafunzi anafanya mtihani peke yake, na ukikutwa unaangalizia ama mnasaidiana na mwenzio ndani ya chumba cha mtihani mtapata adhabu kali ikiwemo kufutiwa mtihani!

๐Ÿ‘‰๐ŸพKatika maisha ya kawaida hasa ya kusaka fedha, unahitajika ushirikiano mkubwa sana, baina yako na wadau, wateja, wafanyakazi wenzio, marafiki n.k. Kwa kifupi unatakiwa kuwa na Networking ya kutosha.

โœ‹๐ŸพHuwezi kufika mbali kiuchumi kama utakuwa na “mentality” ya ubinafsi unaosisitizwa madarasani!

๐Ÿค”Simaanishi kusoma hakuna maana, isipokuwa ninakwambia: Kama ukipata nafasi ya kusoma, soma kwa bidii; lakini usibebe kila wanachokulisha madarasani; ukakileta huku mtaani

๐Ÿ›ฃMtaani panahitaji akili ambayo ni tofauti na hiyo iliyopimwa kupitia kukariri ya vitabuni, mwishoni wanakuzawadia makaratasi yaitwayo vyeti

๐Ÿ˜ŽUkitaka kufanikiwa ungana na waliofanikiwa wakuelekeze

๐Ÿ˜€๐Ÿ™๐Ÿฝ Hii habari haitaki hasira, vumilia tu na jiongeze

Mapishi ya Wali Wa Tambi Na Kuku Wa Sosi Ya Mtindi

Vipimo Vya Wali

Mchele – 3 vikombe

Tambi – 2 vikombe

Mafuta – ยผ kikombe

Chumvi

Vipimo Vya Kuku

Kuku kidari (boneless) aliyekatwa katwa vipande – 1 Kilo

Kitunguu maji kilichokatwa katwa – 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa – 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa – 1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Paprika – 1 kijiko cha supu

Masala ya kuku (tanduri au yoyote) – 1 kijiko cha supu

Ndimu – 2 vijiko vya supu

Mtindi (yoghurt) au malai (cream) – 1 kikombe

Mafuta – ยผ kikombe

Majani ya kotmiri (coriander) – ยฝ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali:

Osha Mchele, uroweke.
Tia mafuta katika sufuria, kaanga tambi zilizokatwakatwa hadi zigeuke rangi kuwa nyekundu.
Tia mchele endelea kukaanga kidogo.
Tia maji kiasi cha wali kupikika kama unavyopika pilau. Kiasi cha maji kinategemea aina ya mchele
Funika katika moto mdogo mdogo hadi uive ukiwa tayari.

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku

Katika bakuli, changanya vitu vyote isipokuwa mtindi na kitunguu.
Tia mafuta katika karai, kisha tia kitunguu ukaange muda mdogo tu, usikiache kugeuka rangi.
Tia kuku na masala yake, endelea kukaanga, kisha tia mtindi au malai ufunike apikike na kuiva vizuri.
Nyunyuzia kotmiri iliyokatwakatwa ikiwa tayari kuliwa na wali wa tambi.

Mapishi ya Ndizi za nazi na utumbo

Mahitaji

Ndizi mshale 10
Utumbo wa ng’ombe 1/2 kilo
Nazi ya kopo 1
Nyanya 1
Kitunguu kikubwa 1
Tangawizi/ swaum 1 kijiko cha chakula
Olive oil kiasi
Limao 1
Chumvi
Curry powder 1 kijiko cha chai
Turmaric 1/2 kijiko cha chai
Coriander ya powder 1/2 kijiko cha chai
Pilipili ya unga 1/2 kijiko cha chai
Pilipili kali nzima (usiipasue)

Matayarisho

Safisha utumbo kisha uweke ktk pressure cooker pamoja na chumvi kiasi, limao, tangawizi, swaum na maji kiasi kisha uchemshe kwa muda wa nusu saa. Baada ya hapo menya ndizi kisha zikate vipande vidogo kiasi ili ziwahi kuiva, kisha ktk sufuria ya kupikia tia vitunguu na nyanya kisha ndizi kwa juu yake na supu ya utumbo kiasi chumvi kidogo na mafuta kiasi kisha bandika jikoni na uchemshe mpaka ndizi zikaribie kuiva. Zikisha karibia kuiva tia utumbo na spice zote, pilipili nzima na tui la nazi kisha changanya vizuri na uache vichemke mpaka ndizi na tui la nazi vitakapoiva na rojo ibaki kiasi. Baada ya hapo Ndizi zako zitakuwa tayari kwa kuliwa.

Mambo Mubimu kujua Kuhusu Tatizo la Shinikizo la damu (Tatizo la presha)

Ni msukumo wa damu ulio juu kuliko inavyotakiwa kwa muda mrefu. Msukumo wa damu huhitajika mwilini ili kusambaza chakula, oksijeni na kutoa uchafu. Shinikizo la damu hupimwa kwa kutumia kifaa kinachoitwa Sphygmomanometer

Shinikizo la damu husababishwa na nini?

Vitu vifuatavyo vinaweza kusababisha shinikizo la juu la damu:

  1. Uvutaji sigara
  2. Unene na uzito kupita kiasi
  3. Unywaji wa pombe
  4. Upungufu wa madini ya potassium
  5. Upungufu wa vitamin D
  6. Umri mkubwa
  7. Ongezeko la kemikali kwenye figo (renin)
  8. Kushindwa kufanyakazi kwa kichocheo kiitwacho insulin

Uanishaji wa shinikizo la damu

Presha ya kawaida <120 <80
Presha inayoelekea kupanda 120-139 80-89
Presha hatua ya 1 140-159 90-99
Presha hatua ya 2 160-179 100-109
Presha hatua ya 3 โ‰ฅ180 โ‰ฅ110

Shinikizo la damu/BP ni ugonjwa unaosumbuwa watu wengi sana duniani na hii ni kutokana na kutokujuwa ni nini hasa husababisha ugonjwa huu mwilini. Shinikizo la damu linaonekana kuwa ni ugonjwa wa kuishi kwa kufuata masharti.

Katika makala hii tutaona uhusiano mkubwa uliopo kati ya upungufu wa maji mwilini na ugonjwa huu, mwishoni utakuwa umeelewa sasa ni jinsi gani ilivyo rahisi kabisa kujiepusha na kujiponya ugonjwa huu. Endelea kusoma.

Takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) zinasema tayari watu bilioni moja duniani kote, wanaathiriwa na shinikizo la juu la damu huku likisababisha mshtuko wa moyo (Heart Attacks), kupooza na kiharusi (Strokes).

Takribani watu milioni nane hufa kila mwaka kutokana na ugonjwa huu wa kupanda kwa shinikizo la damu.

Dalili zitakazokutokea unapokuwa na ugonjwa huu ni pamoja na;

  1. Maumivu ya kichwa (Haswa nyuma ya kichwa mara nyingi nyakati za asubuhi),
  2. Kuchanganyikiwa,
  3. Kizunguzungu,
  4. Kelele sikioni (Mvumo au Mazomeo masikioni),
  5. Kutoweza kuona vizuri au
  6. Matukio ya kuzirai.
  7. Uchovu/kujisikia kuchokachoka
  8. Mapigo ya moyo kwenda haraka
  9. Kutokuweza kuona vizuri
  10. Damu kutoka puani
  11. Uonapo dalili hizi unapaswa kuwahi hospitali kupata vipimo.

Shinikizo la damu (hasa la juu) ni kiashiria cha mwili kupungukiwa maji kwa kiwango kikubwa, ni wakati ambapo mwili unajaribu kujizoesha na upungufu wa jumla wa maji wakati kunapokuwa hakuna maji ya kutosha kuijaza mishipa ya damu yenye kazi ya kusambaza maji kwenye seli mhimu.

Mishipa ya damu imebuniwa maalumu kuendana na mtiririko uliosawa wa ujazo wake wa damu na mahitaji mbalimbali ya tishu kwa kufunga na kufungua mishipa mbalimbali ya damu ndani ya mwili.

Figo hushtuka upesi kulingana na mtiririko wa damu. Hili linaposhindikana, yaani iwapo mtiririko au ujazo wa damu utapungua, basi Figo huitoa homoni iitwayo โ€˜reniniโ€™ ambayo yenyewe huzarisha kitu kiitwacho โ€˜angiotensiniโ€™ ambayo huwa na matokeo mawili; kwanza huzibana ateri na kupandisha shinikizo la damu, pili huisababisha tezi ya โ€˜adrenoโ€™ kutoa homoni iitwayo โ€˜aldosteroniโ€™ ambayo huzifanya figo kuishikilia chumvi na hivyo kusababisha kupanda kwa shinikizo la damu.

Asilimia 94 ya damu ni maji. Kwa ujumla kila seli ndani ya miili yetu ina bahari ya maji baridi ndani yake na bahari ya maji chumvi nje yake. Afya bora inategemea uwiano mzuri wa maji ya bahari hizo mbili.

Chumvi inayashikilia na kuyalazimisha baadhi ya maji kubaki nje ya seli (osmotic retention) na potasiamu inayashikilia maji ndani ya seli.

Wakati mwili unapokuwa katika upungufu wa maji (yaani haunywi maji ya kutosha kila siku) mwili utaongeza ujazo wa maji chumvi kwenye bahari ya nje ya seli.

Kupitia mfumo maalumu, homoni iitwayo โ€˜vasopressiniโ€™ hutolewa ambayo inaweza kuyachuja maji ya chumvi toka katika bahari ya nje ya seli na kuyachoma maji hayo baridi (baada ya kuwa yamechujwa) ndani katikati ya bahari ya ndani ya seli kama yanavyohitajika ili kuutunza uwiano sawa wa maji ndani na nje ya seli.

Lakini ili mbinu hii ifanikiwe, mbinu gani, mbinu ya kuyachuja maji ya chumvi toka katika bahari ya nje ya seli, vasopressini husababisha kapilari na mishipa ya damu kujikaza au kupunguza vipenyo vyake na kukupatia wewe shinikizo la juu la damu (BP) ambalo ni mhimu ili kuyachuja na kuyachoma maji baridi ndani ya seli toka katika bahari ya maji chumvi iliyopo nje ya seli.

Kama mishipa ya damu haitapunguza vipenyo vyake, baadhi ya gesi itaachana na damu ili kuziba nafasi zilizowazi kutokana na kupungua kwa umajimaji mwilini na hatimaye kukusababishia msongamano wa Gesi (Gas locks).

Sifa hii ya vipenyo vya mishipa ya damu kujirekebisha kwa ajili ya mzunguko wa damu, ndiyo mtindo unaotumika zaidi katika kanuni za kihaidroliki wakati ambapo mzunguko wa damu mwilini umejirekebisha kuendana na kiasi cha umajimaji kinachopatikana.

Wakati mwili unapokuwa katika upungufu wa maji kwa mfano kutokana na kutokunywa maji ya kutosha; asilimia 66 ya kuishiwa maji inajionesha kwa kupungua kwa ujazo wa seli, asilimia 26 inapotea toka ujazo wa umajimaji uliopo sehemu ya nje ya seli na asilimia 8 tu inapotea toka katika ujazo wa damu.

Shinikizo la juu la damu ni kiashirio cha mwili kupungukiwa maji kwa asilimia 8 tu, lakini madhara yanajitokeza sababu ya asilimia 66 ya kupunguwa kwa ujazo wa seli.

Maji na chumvi vitalirudisha shinikizo la damu katika hali yake ya kawaida.

Hii ndiyo sababu shinikizo la damu linapaswa kutibiwa kwa kuongeza unywaji wa maji pekee. Dr.Batmanghelidj anasema; Maji peke yake, ni dawa bora ya kukojosha, pekee ya asili tuwezayo kuiendea.

Kama watu wanaosumbuliwa na shinikizo la damu wangeongeza kiasi cha uchukuaji maji, hawatazihitaji dawa za kukojosha, watazarisha mkojo wa kutosha na hivyo kuiondoa chumvi iliyokuwa imezidi!. Watatakiwa pia kuacha kula vyakula visivyo na chumvi na hivyo kuepukana na mikakamao ya mishipa (cramps) kwenye miguu yao.

Madhara yanayoweza kuletwa na shinikizo la damu:

Kwa mjibu wa dr.Batmanghelidj, kutokulielewa shinikizo la damu kama moja ya ishara za mwili kupungukiwa maji na kulitibu kwa dawa za kukojosha ambazo zinaukausha mwili zaidi, baada ya muda zitasababisha;

  1. Kuzibika kwa ateri za moyo na ateri ziendazo kwenye ubongo
  2. Shambulio la moyo (heart attack)
  3. Mishtuko midogo midogo au mikubwa inayopelekea kuzimia
  4. Ugonjwa wa kibofu cha mkojo
  5. Kiharusi
  6. Kupungua kwa nguvu za kiume kwa upande wa wanaume
  7. Kuharibiwa kwa ubongo na matatizo ya akili kama vile kupoteza kumbukumbu (Alzheimer).

Daktari mwingine, Dr.David Brownstein katika kitabu chake kiitwacho; โ€œSalt Your Way to Liveโ€, anasema kwamba alifundishwa katika vyuo vya kiganga kuwa chumvi husababisha shinikizo la damu na kuwa kila mmoja lazima ale vyakula vyenye chumvi kidogo. Na hili watu wengi wamekuwa wakiamini hivi.

Wakati akiwatibu wagonjwa wake, anasema; alianza kuona kuwa wale wanaotumia vyakula vyenye chumvi kidogo wanapata matokeo ya chini au wanapata nafuu ndogo sana kutoka katika vyakula hivyo vyenye chumvi kidogo au bila chumvi kabisa na wengi wao walitokewa kuwa na uhaba mkubwa wa madini katika miili yao.

Katika utafiti wake ili kuwasaidia wagonjwa wake, ndipo akaja na jibu la chumvi ya baharini ambayo haijasafishwa (unrefined sea salt) ambayo huwa na madini mengine zaidi ya 80 ndani yake, alianza kuona kitu kigeni kinaanza kutokea. Wagonjwa wake hao wakaanza kuona mashinikizo yao ya damu yanaanza kushuka katika kiwango ambacho wanaweza kuachana kabisa na matumizi ya dawa.

Dr.Batmanghelidj anasema, ikiwa watu watajishughulisha na mazoezi hasa mazoezi ya kutembea kwa miguu, watakunywa maji halisi zaidi na kuongeza chumvi (siyo sodiamu) kidogo ya ziada kwenye vyakula vyao, mashinikizo yao ya damu yatarudi katika hali yake ya kawaida.

Swali la kujiuliza; Ni zaidi ya miongo minne sasa tangu tulipoambiwa kula vyakula vyenye chumvi kidogo ili kuepukana na shinikizo la damu, kwanini sasa Idadi ya watu wanaopatwa na ugonjwa huu inazidi kuongezeka?.

Narudia tena, mwili unapoanza kuishikilia chumvi, hufanya hivyo ili kuhifadhi maji, toka katika bahari chumvi hiyo ya nje ya seli, maji huchujwa na kutumika wakati wa mahitaji ya dharura.

Maji na chumvi kwa pamoja vitalirudisha shinikizo la damu katika hali yake ya kawaida. Kuikimbia chumvi kunasababisha shinikizo la damu (BP) kuwa sehemu ya maisha yetu, tutapata nafuu, lakini baada ya muda mfupi hali hurudi ileile na pengine kuwa watumwa wa kuchagua kula hiki au kile.

Tofauti na zamani ambapo shinikizo la juu la damu lilipokuwa ni ugonjwa wa watu wanene au wenye uzito uliozidi pekee, siku hizi wanene kwa wembamba, watoto kwa wakubwa wanaugua BP.

Vidokezo vya kukusaidia ule mboga za majani zaidi

Ulaji wa mboga za majani ni muhimu kwa sababu zina vitamini na madini mengi na viwango vidogo vya kalori. Ili uongeze mboga zaidi za majani katika milo yako, fuata vidokezi hivi vifuatavyo;

Gundua njia za kupika haraka

Pika mboga mpya za majani au zilizogandishwa kwa barafu katika wimbi mikro kwa mlo wa haraka na rahisi kuongeza kwa mlo wowote. Pika maharagwe ya kijani, karoti, au brokoli kwa mvuke katika bakuli na kiwango kidogo cha maji katika wimbi mikro kwa mlo wa haraka.

Kuwa mbele ya mambo

Katakata bechi ya pilipili hoto, karoti, au brokoli.Ziweke ili uzitumie wakati zimeadimika. Unaweza kuzifurahia kwenye saladi, na mboji au sandwichi ya mboga za majani.

Chagua mboga za majani zilizo na rangi nyingi

Ngโ€™arisha sahani yako na mboga za majani zilizo na rangi nyekundu, ya machungwa, au kijani. Ziko na vitamini na madini. Jaribu boga ya tunda la muoka, nyanya cheri, viazi vitamu, au kale (sukuma wiki). Hazionji vizuri tu bali ni nzuri kwako pia.

Angalia mpangilio wa friza

Mboga za majani zilizogandishwa kwenye barafu hutumika haraka na kwa urahisi na ziko na lishe kama mboga mpya za majani. Jaribu kuongeza mahindi, dengu, maharagwe ya kijani, spinachi, au mbaazi barafu kwa milo yako kadhaa uipendayo au au ule kama mlo wa kando.

Weka mboga nyingi za majani

Mboga za majani za mkebe ni ongezo muhimu kwa mlo wowote, kwa hivyo weka nyanya, maharagwe mekundu, uyoga, na viazisukari vya mkebe tayari. Chagua zilizo na lebo kama โ€œsodiamu iliyo punguzwa,โ€ โ€œsodiamu kidogo,โ€ au โ€œhakuna chumvi imeongezwa.โ€

Fanya saladi yako ya bustani ingโ€™ae kwa rangi

Ngโ€™arisha saladi yako kwa kutumia mboga za majani zilizo na rangi nzuri kama vile maharagwe meusi, pilipili hoho zilizokatakatwa, figili zilizokatakatwa, kabichi nyekundu iliyokatakatwa au wotakresi. Saladi yako haitapendeza tu lakini pia itaonja vizuri.

Kunywa supu ya mboga za majani

Ipashe moto na uile. Jaribu supu ya nyanya, boga kikazio, au mboga za majani za bustani. Tafuta supu iliyopunguzwa sodiamu au iliyo na kiwango cha chini cha sodiamu.

Ukiwa nje

Kama chakula cha jioni ni nje ya nyumbani, usijali. Unapoagiza, itisha mboga zaidi za majani au saladi zaidi badala ya mlo wa kawaida wa kando uliokarangwa.

Onja ladha ya mboga za majani za msimu

Nunua mboga za majani ambazo ni msimu wake kwa ladha ya kiwango cha juu kwa bei ya chini. Angalia bidhaa zilizo na bei maalumu katika duka kuu la karibu kwa ununuzi wa bei nafuu. Au tembelea soko la wakulima lililokaribu.

Jaribu kitu kipya

Huwezijua unachoweza kupenda. Chagua mboga mpya ya majani โ€“ iongeze kwa mapishi yako au tafuta mtandaoni jinsi ya kuipika.

Sababu ya meno kubadilika rangi

Wapo baadhi ya watu wanashindwa hata kuachia kicheko chenye bashasha hii ni kwa sababu meno yao yamekuwa na rangi, hivyo kuwafanya watu hao kuona aiabu. Pia watu wengi wakiona meno yana rangi ya njano hudhani ni machafu, meusi yanahitaji kusafishwa ili yawe meupe.

Meno kubadilika rangi huweza kuwa ni sababu moja au muunganiko wa sababu mbalimbali kama ifuatavyo;

Matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye kaboni, sigara na mvinyo (wine) kwa muda mrefu husababisha kubadilika kwa rangi ya meno kwa juu (extrinsic staining).

Utumiaji wa maji yenye madini mengi ya fluoride katika kipindi cha utoto (dental fluorosis).

Matumizi ya dawa aina ya tetracycline kwa mama mjamzito ambaye tayari meno ya mtoto aliye tumboni yameanza kuumbwa lakini hayapata madini ya kutosha.

Maumbile yasiyo sahihi ya sehemu ya juu ya jino (amelogenesis imperfecta). Iwapo sehemu hii imeumbwa ikiwa laini kuliko inavyotakiwa huwa rahisi kufyonza rangi na jino huota likiwa limebadilika rangi au hubadilika baada ya muda.

Kufa kwa sehemu hai ya jino hasa kutokana na kuumia kwa jino au ajali (pulp necrosis), hali hii huweza huchukua miaka mingi mpaka kutokea kubalika rangi ya jino..

Jino liliozibwa kwa kutumia material aina ya amalgam huweza kubadilika rangi na kuwa nyeusi.

Mara nyingne jino lililotibiwa kwenye mzizi wa jino (root canal treatment ) huweza kubadilika rangi baada ya miaka mingi.

Kuna njia mbalimbali ambazo hutumika kuyafanya meno yaliyo na rangi isiyo ya kawaida kuwa meupe.

Njia hizi hutofautiana kati ya mtu na mtu kutokana na jinsi alivyoathirika. Kuna njia nyingi ambazo huweza kuyangโ€™arisha kwa ndani (internal bleaching) au kuyangarisha kwa nje (external bleaching).

Endapo una tatizo la meno yaliyobadilika rangi, muone daktari wa kinywa na meno kwaajili ya ushauri na matibabu kwani kinywa kizuri na chenye afya huongeza kujiamini.

Misemo 10 bora ya kuchekesha itakayokuacha mdomo wazi

1. Mwanaume hata awe bahili vipi, hawezi kumpa mwanamke mimba nusu.

2. Hata uwe na magari mangapi chooni utaenda kwa miguu.

3. Kama ubinadamu kazi mbona hatupewi mishahara?

4. Ukichanganya wali na choroko unapata mseto, lakini hautibu malaria.

5. Hata njiwa nae ana makinda, lakini hawezi kuwa spika wa Bunge.

6. Hata uwe na haraka vipi kwenda Zenj, huwezi kupanda Jahazi ya Yusuph Mzee.

7. Umeme hauna kiuno lakini unaongoza kwa kukatika.

8. Hata uwe kauzu vipi, huwezi kujamba wakati unatongoza.

9. Hata uwe na imani kali vipi, huwezi kusali wakati unafanya mapenzi.

10. Hata kizibo ni mfuniko lakini hauwezi
kufunika sufuria.

Kumtafuta Mungu ni Jukumu lako Binafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na nafsi yake. Huwezi kumfuata Mungu kwa kufwata njia ya wengine. Njia yako ya kukuwezesha kumfikia Mungu ni tofauti na wengine, Kwa maana Mungu amemwita kila mtu kwa namna ya kipekee.

Melkisedeck Leon Shine

Kumtafuta Mungu: Jukumu la Mtu Binafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na nafsi yake. Kila mmoja wetu ana safari ya kiroho inayomwita kumtafuta Mungu kwa njia yake mwenyewe. Safari hii ni ya kipekee na haifanani na ya mwingine yeyote. Mungu anatuita kila mmoja wetu kwa namna ya kipekee, akitufundisha na kutuongoza kupitia maisha yetu binafsi. Kumtafuta Mungu si jambo la jumuia au kanisa, bali ni uamuzi wa kibinafsi unaohitaji moyo wa kujitolea na utayari wa kipekee.

“Nitajitokeza kwenu, nanyi mtaniona; nanyi mtakaponiomba, nitasikiliza.” (Yeremia 29:12-13)
“Wakati unapotaka kujua mambo ya Mungu, basi mpe nafasi, naye atakujulisha siri zake.” (Amosi 3:7)
“Ee Mungu, Mungu wangu, nakutafuta asubuhi; roho yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakutamani, katika nchi kame na yenye kuia, isiyo na maji.” (Zaburi 63:1)

Njia ya Kipekee ya Kumtafuta Mungu

Huwezi kumfuata Mungu kwa kufuata njia ya wengine. Ingawa tunaweza kupata mwongozo na msaada kutoka kwa wale walio karibu nasi katika jumuia au kanisa, ni muhimu kutambua kuwa kila mtu ana njia yake ya kumfikia Mungu. Njia yako ya kukuwezesha kumfikia Mungu ni tofauti na wengine. Hii ni kwa sababu Mungu amemwita kila mtu kwa namna ya kipekee. Katika ulimwengu huu wa tofauti na utofauti, Mungu anazungumza nasi kwa njia ambazo zinaendana na maisha yetu binafsi na hali zetu za kipekee. Hili ni jambo la kibinafsi na si suala la jumuia au kanisa.

“Kwa maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu, asema Bwana.” (Isaya 55:8)
“Pendo la Mungu limemiminwa mioyoni mwetu na Roho Mtakatifu tuliyekirimiwa.” (Warumi 5:5)
“Mmoja na mmoja wenu, ajaribu sana kutafuta kibali mbele za Bwana, kwa moyo wote, maana hatuwezi kumpendeza Mungu bila imani.” (Waebrania 11:6)

Kutembea Katika Wito Wako

Mungu anatuita kila mmoja wetu kwa namna ya kipekee. Kila wito unaambatana na vipawa, changamoto, na fursa ambazo ni za kipekee kwa kila mmoja wetu. Kwa hivyo, ni muhimu kumsikiliza Mungu katika maisha yako na kutembea katika wito wako binafsi. Hii inamaanisha kujifunza kusikiliza sauti ya Mungu katika maombi, kusoma Neno lake, na kutafakari juu ya maisha yako. Kutembea katika wito wako ni hatua ya kibinafsi inayohitaji kujitolea na uwazi wa moyo.

“Bali nyote mtakuja kwa njia ya utulivu na kunyamaza; na mtafakari kwa utulivu wa moyo, ndipo mtakapoona nuru ya Bwana.” (Isaya 30:15)
“Jitoe kwa Bwana, na umetulie mbele zake; nawe atakupatia maombi ya moyo wako.” (Zaburi 37:4)
“Naye atatenda katika njia zako, atakuongoza kwa haki na njia zake zote.” (Mithali 3:6)

Umuhimu wa Maombi na Tafakari

Kumtafuta Mungu kunahitaji muda wa maombi na tafakari. Huu ni wakati wa kuwa kimya mbele za Mungu, kumwambia mahitaji yako, na kumsikiliza. Maombi ni mazungumzo na Mungu, na ni katika mazungumzo haya tunapopata mwongozo wa kiroho. Tafakari juu ya Neno la Mungu na jinsi linavyohusiana na maisha yako binafsi ni muhimu katika safari hii ya kiroho. Hili ni jukumu la kibinafsi, ambalo linaweza kufanyika vyema wakati unapotenga muda maalumu kuwa peke yako na Mungu.

“Basi, kesheni, mkiomba kila wakati, ili mweze kuokoka mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.” (Luka 21:36)
“Kwa maana mkimtafuta kwa bidii mtampata, mkimtafuta kwa moyo wenu wote.” (Yeremia 29:13)
“Jilindeni, ninyi wenyewe, na usiache moyo wako upotee, bali mwombe Mungu kwa bidii, naye atakujulisha mapenzi yake.” (Yakobo 1:5)

Kusikiliza Sauti ya Mungu

Mungu anaweza kuzungumza nasi kwa njia nyingi tofauti. Anaweza kuzungumza kupitia Neno lake, kupitia watu wengine, au kupitia matukio katika maisha yetu. Ni muhimu kuwa na moyo wazi na kusikiliza kwa makini sauti ya Mungu. Unapokuwa na utayari wa kusikiliza na kufuata mwongozo wake, utaona njia zako zikifunguka na kupata mwanga mpya wa kiroho. Hii ni safari ya kibinafsi inayohitaji kujitoa na kuwa na moyo wa kusikiliza.

“Kwa maana Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara mbili, lakini mwanadamu hajali.” (Ayubu 33:14)
“Ee Bwana, unayenifundisha na kuniongoza kwa njia ya haki, unayenipenda kwa upendo wa milele.” (Zaburi 32:8)
“Ee Mungu, unayejua kila kitu, unayejua kwamba nakupenda. Unayejua kwamba nakutafuta kwa moyo wote.” (Yohana 21:17)

Kumtafuta Mungu ni Jukumu la Kibinafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na si suala la jumuia au kanisa. Mwisho wa siku, kila mmoja wetu atahitajika kusimama peke yake mbele za Mungu na kutoa hesabu ya maisha yake. Hatutaweza kutumia njia za wengine kama kigezo cha safari yetu ya kiroho. Ni muhimu kuchukua jukumu la kumtafuta Mungu kwa bidii na moyo wote, kwa kuwa hatimaye, ni uhusiano wetu binafsi na Mungu ndio utakaotupa uzima wa milele.

“Kwa maana kila mmoja wetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.” (Warumi 14:12)
“Usiwe na hofu, maana mimi nipo nawe; usishike, maana mimi ndimi Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia; naam, nitakushika kwa mkono wangu wa kuume wa haki.” (Isaya 41:10)
“Lakini wewe, unaposali, ingia katika chumba chako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Na Baba yako aonaye sirini atakupa.” (Mathayo 6:6)

Katika safari ya kumtafuta Mungu, kumbuka kwamba ni jukumu lako binafsi na nafsi yako. Usijaribu kufuata njia ya mwingine, bali tembea katika njia yako binafsi ambayo Mungu ameiweka mbele yako. Kwa kufanya hivyo, utaweza kumfikia Mungu kwa undani na kujenga uhusiano wa kipekee na wa kweli naye. Kumtafuta Mungu si jambo la jumuia au kanisa; ni mwito wa ndani unaohitaji kujitoa na kuwa tayari kusimama peke yako mbele za Mungu.

Ugumu wa maisha huanzia akilini mwako

Ebu fikiria Dada anayechoma mahindi maeneo ya Manzese Darajani kuanzia saa 12 jioni mpaka SAA 2 usiku, kwa siku moja anauwezo wa kuchoma mahindi .50. Kila hindi moja ananunua shambani kwa shilingi 100/- Na Anauza kwa sh.600/-

Hiyo ina maana mahindi 50 ananunua kwa shilingi 5000/- akichoma na kuuza anapata sh.30,000/-. Akitoa pesa ya mtaji (5000/- ya mahindi na 1500/- ya mkaa) anabakiwa na sh.23,500/- kwa siku.

Hivyo kwa mwezi huyu mchoma mahindi atakuwa ameingiza kiasi cha sh.705,000/-

Mwalimu mwenye Degree anayeanza kazi analipwa 584,000/- akikatwa kodi pamoja na makato mengene ya mifuko ya jamii anabakiwa na sh.425,000/.

Tofauti ya Mwalimu wa degree na Muuza mahindi ni kuwa Mwalimu kaajiriwa, muuza mahindi kajiajiri. Mwalimu anafanya kazi masaa 9 kwa siku, muuza mahindi anafanya kazi masaa matatu kwa siku (saa 12 jioni hadi 2 usiku). Mwalimu anatumia muda wake wa ziada kusahihisha mitihani na homework, mchoma mahindi anatumia muda wake wa ziada kutafuta fursa nyingine za kupata hela.

Uoga wako ndio umaskini wako.
KAMA HUNA FURAHA NA UNACHOKIFANYA BADILI MTAZAMO NA SIKUSHAURI UKAUZE MAHINDI NO HUO NI MF. KAMA SWALA NI KIPATO TU BASI KUNA FURSA NYINGI SANA KIPINDI HIKI NA WAWEZA BILA HATA YA KUWA NA MTAJI CHA MSINGI NI WEWE KUAMUA KUWAONA WATAALAMU WAKUSHAURI NI NINI CHA KUFANYA.

mafanikio yanaanza nawewe

Nini kinachokufanya udhani utashindwa sasa?

Kwa mujibu wa Biologia, baada ya tendo la kukutana kimwili takribani mbegu milioni 200 hadi 300 hutolewa na mwanaumeโ€ฆhalafu zote huanza kupiga mbizi kuogelea kwenye njia safarini kukutana na yai la kike.

Ajabu ya kwanza ni kwamba sio zote 200 – 300 ambazo hufanikiwa kulifikia yai( nyingi huchoka na kufia njiani maana si mashindano ya mchezo mchezo).
Ajabu ya pili ni kwamba kati ya hizi 300 zinazofanikiwa kufikia yai, ni moja tu..moja tu itakayoshinda nakufanikiwa kupenya na kurutubisha yai, na kwa mantiki hii ILIYOSHINDA NI WEWE HAPO.

Umewahi kuwaza kuhusu hili vizuri?
Yaani ulishindana mbio hizo ukiwa huna macho na ulishinda, ulishindana bila elimu na ukashinda,ulishindana bila hata cheti chochote wala msaada wa yeyote โ€ฆ.na UKASHINDA.

Nini kinachokufanya udhani utashindwa sasa?
Tena sasa uko na macho yote, miguu, sasa Unamjua Mungu, sasa ukiwa na mipango,ndoto na maono.
Kumbuka ULISHASHINDA toka tumboni huna sababu ya kuwa na hofu yeyote, PAMBANA

Jinsi ya kupika vizuri Wali Wa Karoti Na Nyama

MAHITAJI YA WALI

Mchele – 3 Magi

Mafuta – 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu – 3

Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa – 1 kikubwa

Pilipli manga – 1/2 kijicho chai

Hiliki – 1/2 kijiko chai

Karafuu ya unga – 1/4 kijiko cha chai

Mdalasini wa unga – 1/2 kijiko cha chai

Zaafarani (ukipenda) roweka katika maji – 1 kijiko cha chai

Zabibu kavu (ukipenda) – 1/4 kikombe

Chumvi kiasi

KUPIKA WALI

Kwenye sufuria tia mafuta na kaanga karoti kidogo.
Tia vitunguu kisha tia bizari zote.
Tia maji kiasi (kutegemea aina ya mchele) na chumvi
Tia mchele upike uwive.
Karibu na kuwvia tia zabibu ukipenda.
Funika endelea kuupika hadi uwive.

MAHITAJI KWA NYAMA

Nyama – 2 Ratili (LB)

Chumvi – Kiasi

Mafuta – 1/4 kikombe

Kitunguu (kata virefu virefu) – 1 Kikubwa

Pilipili mboga kubwa – 2 ukipenda moja nyekundu moja kijani unazikata vipande virefu virefu.

Figili mwitu (celery) kata vipande virefu virefu- Miche miwili.

KUPIKA NYAMA

Chemsha nyama hadi iwive
Ikaange kwa mafuta hadi iwe nyekundu
Weka vitunguu, pilipili mboga na figili mwitu
Kaanga kidogo tu kama dakika moja.
Tayari kuliwa na wali.

Matumizi ya juisi ya limao kutibu shinikizo la chini la damu

Juisi hii ni nzuri sana katika kutibu shinikizo la juu la damu.

Lakini inaweza pia kutumika kutibu shinikizo la chini la damu hasa ikiwa hili shinikizo la chini la damu limesababishwa na upungufu wa maji mwilini (dehydration).

Kutibu shinikizo la chini la damu unaweza kuchanganya juisi ya limau na chumvi kidogo na sukari au unaweza kutumia maji maji ya miwa.

Wakati unapitia magumu usikate tamaa

Kuna Kipindi katika maisha yako unaweza ukapitia mambo Fulani magumu hadi ukaanza kujiuliza,hivi kwa nini yote haya yananitokea?Why Me God?.Na Mimi nimeshawahi kupitia katika hali hii.

Nilichojifunza ni kuwa hakuna changamoto ya kudumu milele na katika kila kinachoonekana Leo kuwa hakina majibu,ukiamini kuwa inawezekana basi utapata majibu yake.

Watu wanaoibuka kuwa washindi kwenye maisha ni wale ambao wanapojikuta katika hali ngumu sana na tata katika maisha yao,huwa wanajiambia-“Hata hili nalo litapita”

Kuna siku utaangalia nyuma ulikotoka na hautaimi jinsi ulivyoshinda na kuvuka.Majibu yako njiani.

Tafakari Kuhusu Kipindi cha Changamoto

Kuna kipindi katika maisha yako ambapo unaweza ukapitia mambo fulani magumu hadi ukaanza kujiuliza, “Hivi kwa nini yote haya yananitokea? Why me, God?” Na mimi nimeshawahi kupitia katika hali hii. Changamoto hizi zinaweza kuwa ngumu sana na zinaweza kukufanya uhisi kama kila kitu kimeenda vibaya. Hata hivyo, ni muhimu kukumbuka kuwa kila mmoja wetu hupitia changamoto, na njia tunayochagua kushughulika nazo ndiyo inayotufanya tuwe tofauti.

“Ee Mungu, kwa nini umeniacha? Mbona uko mbali na kunisaidia, mbali na maneno ya kuugua kwangu?” (Zaburi 22:1)
“Ndivyo Roho wa Mungu anavyotusaidia katika udhaifu wetu. Kwa maana hatujui kusali ipasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa uchungu usiosemeka kwa maneno.” (Warumi 8:26)
“Nimeshikwa sana, ee Bwana niokoe; ee Bwana niokoe.” (Zaburi 40:13)

Hakuna Changamoto ya Kudumu Milele

Nilichojifunza ni kuwa hakuna changamoto ya kudumu milele. Katika kila kinachoonekana leo kuwa hakina majibu, ukikumbatia imani na matumaini, basi utapata majibu yake. Hii inamaanisha kuwa changamoto tunazokutana nazo ni za muda tu, na zinakuja na kuondoka kama vipindi vya majira.

“Kwa kila jambo kuna majira, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.” (Mhubiri 3:1)
“Naye Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, akiisha kuteseka kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuimarisha, na kuwatia nguvu.” (1 Petro 5:10)
“Hata katika hali hii tunajua kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao, kwa ajili ya mema, yaani wale walioitwa kwa kusudi lake.” (Warumi 8:28)

Hata Hili Nalo Litapita

Watu wanaoibuka kuwa washindi kwenye maisha ni wale ambao, wanapojikuta katika hali ngumu sana na tata katika maisha yao, hujiambia, “Hata hili nalo litapita.” Kauli hii ni yenye nguvu sana kwa sababu inakukumbusha kwamba hakuna hali inayodumu milele. Ni muhimu kujipa moyo na kuelewa kwamba matatizo ni ya muda tu na yatapita.

“Hata sasa najua ya kuwa kila unaloomba kwa Mungu, Mungu atakupa.” (Yohana 11:22)
“Kwa maana imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” (Waebrania 11:1)
“Basi nasi tukiwa na ushahidi mwingi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito na dhambi ituzingayo kwa upesi, na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu.” (Waebrania 12:1)

Majibu Yako Njiani

Kuna siku utaangalia nyuma ulikotoka na hautaimani jinsi ulivyoshinda na kuvuka. Majibu yako njiani. Unapokabiliana na changamoto, kuwa na imani kwamba kuna jibu na mwongozo ambao Mungu amekuwekea. Hakuna tatizo lisilo na suluhisho kwa wale wanaomwamini Mungu na kutafuta msaada wake.

“Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.” (Zaburi 46:1)
“Ujapopita katika maji mengi mimi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; ujapokwenda katika moto, hutateketea, wala mwali wa moto hautakuunguza.” (Isaya 43:2)
“Lakini watumainio Bwana watapata nguvu mpya; watapaa kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.” (Isaya 40:31)

Katika safari yako ya maisha, kumbuka kuwa changamoto ni sehemu ya kukua na kujifunza. Kwa kupitia magumu, tunakuwa na nguvu na hekima zaidi. Kwa hiyo, endelea kusonga mbele kwa imani, ukiamini kwamba Mungu yupo pamoja nawe na atakuonyesha njia katika kila hali.

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About