Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Angalia mchezo wa kutuma message mara zikubali mara zikatae.. Lilishakukuta hili???

GARLFREND»»hellow sweetheart

BOYFREND»»hellow darling(SENDING FAILED)

GARLFREND»»kwanin hutaki kujibu sms yangu,au huna mda»??

BOYFREND»>najitahid kukujibu lakin mtandao unasumbua,imefika??(SENDING FAILED)

GARLFREND»»kama hunipend bhas usinijbu,kama unanipenda kwel bhas nijibu

BOYFREND»»i love you (SENDING FAILED)
GALFREND»»do you lov me????

BOYFREND»»i lov you baby(SENDING FAILED)

GARLFREND»»usiongee na mimi tenaaaaa

BOYFREND»»i love you sweetieeee(SENDING FAILED)

GARLFREND»»unataka mim na wew tuachaneee????

BOYFREND»»nshachoka mie na huu upUmbavu,shenz (MESSAGE SENT)

👆👆👆👆👆😄😄😄😄😄😄😄😄👆👆👆👆😄😄😄😄👆👆😄😄👆👆

Kilichompata huyu jamaa mroho wa nyama, Hata kaa arudie tena

Jamaa kaenda kumtembelea rafiki yake Levi, kule sehemu za kwetu, akakaribishwa bonge ya ugali na nyama nyingi tu, wakati anakula akagundua kuwa shemeji yake, mke wa rafiki yake hali nyama;

JAMAA: Aise hili ni bonge ya lanchi hii, lakini Levi mbona sisi tu tunakula nyama shemeji Gulo hagusi kabisa anaishia mchicha tu? Tabia gani hii?
LEVI: Hapana sijamkataza, ila shemeji yako Mngoni halagi nyama ya FISI kama sisi

Mbinu za kumfanya mwanamke akukubali

Njia za kumfanya akukubali ni kama ifuatavyo

Uwe na muonekano mzuri

Wanawake wanapenda wanaume wasafi na watanashati kwa hiyo ukiwa msafi na mtanashati utakua na mvuto kwake. Hivyo utakapoamua kumshawishi kufanya mapenzi itakua rahisi yeye kuwa rahisi kukubali.

Mfanye ajisikie huru

Ni rahisi mwanamke kufanya mapenzi na mtu anayejisikia huru mbaele zake na ambaye yupo huru kuongea na kufanya nae mambo mengine ya kawaida katika maisha. Kwa hiyo ili uweze kumshawishi mwanamke kufanya mapenzi na wewe njia nzuri ni kumfanya ajisikie yupo huru mbele yako na kasha atakua huru kufanya mapenzi na wewe.

 

Mfurahishe

Mfanye ajisikie mwenye furaha kila anapokuwa na wewe na atamani kuwa na wewe. Akishajiskia mwenye furaha kila anapokuwa na wewe ni rahisi kushawishika kuwa na wewe kimapenzi.

Mfanye ajione kuwa yeye ni mzuri

Mwanamke anapenda sana na anavutiwa na mwanamme anayeona ubora wake au anayemsifia kuwa ni mzuri.

Mfanye akuamini

Mfanye aamini kwamba hata baada ya kufanya mapenzi bado mtakua pamoja na sio mwisho wa mahusiano yenu au urafiki wenu.

 

Usiwe na haraka, Mpe muda

Usiwe na haraka ya kumwambia kuwa unataka kufanya mapenzi na yeye bali subiri mpaka utakapoona yupo tayari au anaelekea kukuhitaji.

Mfanye akuone mwaminifu

Mfanye akuone mwaminifu kwa kutomchanganya na wanawake wengine. Usimuonyeshe kuwa una mahusiano na wanawake wengine. Mfanye aamini kuwa unamuhitaji yeye tuu.

 

Mjali kama mwanamke

Mfanye ajiskie kuwa mwanamke. Jaribu kuonyesha kuwa mwelewa, onyesha kuwa unajali, mkarimu na muonyeshe kuwa wewe ni msaada kwake. Mfungulie mlango, mbebee begi au pochi yake n.k.

Onyesha kuwa unapenda kila kitu kutoka kwake

Muonyeshe kuwa unampenda yeye na vyote vyake. Onyesha kuwa umevutiwa na yeye na mambo yake yote na sio mwili wake tuu.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Jamaa mpenda michepuko kapatikana

…Upo kazini umeacha familia yako nyumbani mara ghafla unapigiwa simu kutazama unakutana na no ngeni na kuamua kuipokea ndipo unakutana na Sauti ya msichana ya kuvutia lakin kabla hajasema shida yake anaamua kukata simu. Unashikwa na hamu ya kujua ni nani. Tamaa ya mchepuko inakujia ghafla na kuamua kuipiga ile no tena kwa mara nyingine inakuwa haipatikani.

Siku hiyo hiyo usiku ukiwa umelala chumba kimoja na mkeo meseji inaingia tena kwenye cm yako kwa ile namba iliyokupigia mchana ikikuomba umpigie kwa mida ule na kusisitiza kuwa ana hamu ya kukufahamu. kila ukimtumia meseji ya kumdanganya upo sehemu mbaya hasikii anakubipu mara nyingi. Uzalendo unakushinda, unamuangalia pembeni mkeo kalala fofofo kajifunika shuka hadi usoni. Unaamua kuondoka kwa kunyata mpaka sebuleni kwenda kuipiga Ile namba kwa lengo la Kumwambia kesho mkutane. Ile unafika sebuleni na kuanza kuipiga ile cm ndipo unakutana na sauti hii:- MUME WANGU ACHA MCHEPUKO, NILIKUWA NAKUPIMA TU RUDI TU CHUMBANI TULALE 😋😋😋😋😋😋😋😋 Hapo ndo utajua kwann bata hata ale kokoto anaharisha 😂😂😂😂😂😂😂😂

Kwa nini tarehe ya Pasaka hubadilika

KALENDA za mwanzo ziliutumia mwezi wa
angani kama kipimo cha muda. Ziliitwa
“Lunar calender” au Kalenda-Mwezi. Tarehe 1
ya Mwezi ilikuwa ni siku ulipoandama yaani
Mwezi-Mdogo (Crescent Moon).
Mwezi unapofika siku ya 15 unakuwa
umefikia ukubwa wa juu na huitwa Mwezi-
Mkubwa (Full Moon). Hivyo kwa kalenda ile
tarehe 15 ilikuwa ni siku ya Mwezi-Mkubwa.
Mwaka 45KK, Julius Caesar alitangaza
kalenda mpya ikaitwa “Julian Calender” iwe
na siku 365. Wakati huo ikijulikana kwamba
jua huzunguka kwa siku 365.25. Hivyo pengo
la kalenda na mzunguko likabaki robo siku.

Robo hiyo ifidiwe kila baada ya miaka minne
mwishoni mwa mwezi Februari ambayo sasa
ulifanywa kuwa wa pili baada ya January.
Inapofanyika hivyo, huo ukaitwa mwaka-
mrefu (Leap year).
Mwaka mrefu ukachaguliwa kuwa ni ule tu
unaogawanywa kwa nne mfano miaka
ifuatayo 1700, 1800, 1900, 2100, 2200, 2300.
Baadaye iligundulika kuwa jua huzunguka
kwa siku 365.24218967 ziitwazo “Tropical
year”. Hizi ni chache kuliko siku 365.25
zilizokadiriwa mwanzoni. Uchache huu
husababisha kuwe na pengo la dakika 11 na
sekunde 14.812512 kwa mwaka.
Pengo hili ni dogo, lakini hupanuka hadi kuwa
siku nzima kila baada ya miaka 128.0355.
Mwaka 1545 lilivuka siku 9.25.
Kuondoa tatizo hili, Papa Gregory XIII
aliamuru iundwe kalenda mpya na akachagua
Oktoba 04, 1582 iwe siku ya mwisho
kutumika “Julian Calender”. Kesho yake,
kalenda mpya ikaanza kutumika.
Ungetegemea hiyo kesho iwe ni Oktoba 05,
1582. Lakini ili uzibe pengo lile lililofikia siku
kumi, ilibidi kalenda mpya kuziruka siku hizo
siku kumi. Hivyo hii mpya iliyoitwa
“Gregorean Calender” ikaanza kama Oktoba
15 badala ya Oktoba 05.
Ndiyo sababu katika historia ya nchi nyingi
Ulaya, hakuna tarehe za Oktoba 05, 1582
hadi Oktoba 14, 1582. Watu walilala Oktoba
04, 1582 kesho yake wakaamka ikiwa ni
Oktoba 15, 1582.
Teresa Alonso huandikwa kwamba alifariki
Oktoba 1582, kwenye usiku wa tarehe NNE
kuamkia tarehe KUMI NA TANO!
Alipotangazwa kuwa Mtakatifu, Kanisa
Katoliki likaifanya Oktoba 15 kuwa siku ya
kumkumbuka, yaani siku ya Mtakatifu Teresa
wa Avila.
Usipofahamu kwamba Mtakatifu Teresa
alifariki siku kalenda zinabadilishwa, utadhani
aliyeandika vile tarehe za kifo chake
amekosea!
Waandishi, William Shakespeare wa
Uingereza na Miguel de Cervantes wa Spain
huandikwa kwamba wote walifariki Aprili 23,
1616. Lakini ukweli ni kwamba hawakufa siku
moja bali walipishana siku kumi kwani
England ilichelewa kwa karibu miaka 200
kuikubali “Gregorean Calender”!
“Gregorean Calender” haikuundwa ili kuishia
kuliziba lile pengo. Bali pia, kuhakikisha
halitokei tena. Tumeshaona kuwa lile pengo
ni dakika 11 na sekunde 14.812512. Hivyo,
linapanuka na kuwa siku tatu ndani ya miaka
400.
Hivyo kuliziba inatakiwa kupunguza siku tatu
kila baada ya miaka 400.

Je, zipunguzweje?

Kipande cha miaka 400 kina miaka mitatu ya
karne inayogawanyika kwa 4 lakini
haigawanyiki kwa 400.
Ikakubalika kwamba unaogawanyika kwa 4,
lakini haugawanyaiki kwa 400, usiendelee
kuwa mrefu. Humo siku moja ichomolewe na
uwe mfupi.
Ndipo miaka 1700, 1800, 1900 haikuwa tena
mirefu. Ndivyo pia miaka 2100, 2200, 2300
nayo haitakuwa mirefu. Kwa sababu ni miaka
ambayo “Gregorean Calender” inachomoa
siku moja ili kutosababisha pengo tena.
Kipande hiki cha miaka 400 kikaleta wastani
mpya wa siku 365.2425 kwa mwaka. Sasa
lile pengo lile la siku moja si rahisi kufikiwa.
Kwenye “Julian Calender” tumeona lilikuwa
miaka 128.0355 lakini sasa limekuwa miaka
3,222.
Sasa tuijadili tarehe ya siku ya Pasaka
tukiwa na ufahamu wa kalenda zile. +++ Je, tarehe ya Pasaka imetajwa ndani ya Biblia?

Kuna kifungu kinasema hivi:
“..Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya
mwezi, wakati wa jioni, ni Pasaka ya BWANA.
Na siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni
sikukuu ya BWANA, ndiyo siku ya mikate
isiyotiwa chachu. (Walawi 23:5)..”. Hivyo
Pasaka ni tarehe 15 ya mwezi wa Kwanza.
Lakini Biblia pia inautaja mwezi wa kwanza
kwa jina la Nisan (Esta 3:7, Nehemia 2:1).
Yesu alisulubiwa mwaka ambao Ijumaa
iliitangulia sikukuu ya Pasaka kwa siku moja
(Yohana 18: 28, Marko 15:42-43). Hivyo
tarehe ya Yesu kusulubiwa ni Ijumaa, Nisan
14. Siku moja kabla ya Nisan 15. Siku moja
kabla ya Mwezi-Mkubwa.
Baada ya Yesu, Wakristo wengi Pasaka
waliiadhimisha Jumapili, lakini utata
ulijitokeza kuhusu tarehe ya kuiweka hiyo
Jumapili ya Pasaka. Ilifika wakati jimbo moja
la Wakristo linaadhimisha siku tofauti na
jingine na kwa njia wanayoijua wao.
Utata huu uliondolewa kule Nicaea mwaka
325 ambapo Kanisa Katoliki lilipoamua kuwa,
tarehe ya Pasaka iwe moja tu duniani kote,
yaani iwe ni Jumapili inayokuja baada ya
Mwezi-Mkubwa (Full Moon) unaotokea baada
ya siku ya Ikweta, yaani baada ya Machi 21
(Equinox).
Baada ya uamuzi huu, wataalamu walipania
kuunda chati maalum zenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa zitazokasaidia kuitambua tarehe ya
Pasaka kwa mwaka wowote.
Mwezi huizunguka dunia kwa siku
29.5305891203704 (Synodic Month), wakati
dunia hulizunguka jua kwa siku
365.24218967 (Tropical year).
Mizunguko hii miwili ikianza safari siku moja,
itapishana kila mwaka, lakini itakutana tena
mwezi unapokamilisha mizunguko 235. Dunia
nayo inakuwa imekamilisha mizunguko 19,
yaani miaka 19.
Wataalamu wakaitumia hii miaka 19
kutengeneza chati yenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa unaotokea March 22 hadi April 18.
Tarehe zile zikaitwa tarehe za Mwezi-
Mkubwa Wa Pasaka au Ecclesiastical Full
Moon (EFM).
Ndani ya ile miaka 19, kila mwaka ukapewa
tarakimu iitwayo Golden Number
inayosimama badala ya mwaka ikiwa na
tarehe zile ziliorekodiwa za Mwezi Mkubwa
wa Pasaka. Chati yenyewe ya Golden
Number na tarehe zake (siku/Mwezi) ni hii
ifuatayo: {1=5/4, 2=25/3, 3=13/4, 4=2/4,
5=22/3, 6=10/4, 7=30/3, 8=18/4, 9=7/4,
10=27/3, 11=15/4, 12=4/4, 13=24/3, 14=12/4,
15=1/4, 16=21/3, 17=9/4, 18=29/3, 19=17/4}
Golden Number ya mwaka inapatikana
kuanza kuugawa mwaka kwa 19.
Tulifundishwa mashuleni kuwa namba
inayosalia baada ya kugawa huitwa “Baki” .
Hii “Baki” ukiijumlisha na 1 unapata Golden
Number (GN).
Mfano unatafuta GN ya 27. Hatua ya kwanza
ni kutafuta “Baki” baada ya kugawa 27 kwa
19. Hizi ni hesabu za “modulo” , yaani
zinahitaji tu namba inayobaki baada ya
kugawa.
Ikiandikwa hivi: (27 mod 19) inatakiwa
namba inayobaki baada ya kuigawa 27 kwa
19. Jibu ni 8. Hivyo tulipaswa tuandike hivi:
(27 mod 19=8). “Baki” 8 tuliyoipata, ndiyo
tunaihitaji ili tuijumlishe na 1 ili tupate GN
ambayo hapa ni 9 kwani (8+1=9).
Tungeweza pia kuandika hivi : 27 mod 19 +
1=9. Hivyo kanuni ya kupata GN kwa mwaka
wowote ni hii:
(MWAKA mod 19 + 1). Yaani, ugawe huo
mwaka kwa 19, kisha namba itakayobaki
ijumlishe na moja.
Ukishaipata GN, itafute kwenye ile chati
ambapo utaiona ikiwa na mwezi na tarehe.
Jumapili inayofuata baada ya tarehe hii ndiyo
tarehe ya Pasaka ya mwaka huo.
Tutumie chati ile na kanuni hii kujua tarehe
ya Pasaka ya mwaka 1474. GN ni (1474 mod
19 + 1=12). Hivyo GN ni 12.
Kwenye chati, 12 inaonyesha ni tarehe 4/4.
Hivyo, mwaka 1474 Mwezi-Mkubwa wa
Pasaka ulikuwa tarehe 4/4/1474. Hiyo ilikuwa
ni Jumatatu. Hivyo Pasaka ilikuwa ni
Jumapili iliyofuata yaani tarehe 10/4/1474.
Lakini, Kanisa Katoliki liliikubali kanuni hii
karne ya sita. Hii ndiyo sababu, tarehe za
Pasaka zinazojulikana ni zile tu zinazoanza
mwaka 533.
Ndivyo Pasaka ilivyotafutwa miaka ile. Sasa
tuone Pasaka ya kizazi chetu. Kizazi cha
“Gregorean Calender” iliyoanza mwaka 1582.
Tumelijadili lile pengo la siku lililofikia ambalo
mwaka 1582 lilishafika siku 10. Ukweli ni
kwamba kabla halijazibwa, Pasaka ilikuwa
inawadia lakini uhalisi ni kwamba inakuwa
tayari imepitwa siku 10. Kinyume kabisa na
maamuzi ya Kanisa kule Nicaea!
Ili kulizuia lisitokee tena, tumeona uchomoaji
wa siku moja toka kwenye miaka inayofunga
karne, isiyogawanyika kwa 400. Uchomoaji
huu umewekwa kwenye kanuni (formula)
iitwayo “Solar Equation”.
Kama mwendo wa kuzunguka jua
umezingatiwa na “Gregorean Calender”, vipi
kuhusu mwendo wa mwezi?
Tumeuona kwamba mizunguko ya mwezi na
dunia hukutana kila baada ya miaka 19.
Kadirio la dunia kuzunguka kwa siku 365.25

linafanya ikizunguka kwa miaka 19 zinakuwa
siku 6,939.75. Mwezi utakuwa nao
umezunguka mara 235, huku kila mzunguko
ukitumia siku 29.5305891203704.
Hivyo, kukutana kule ndani ya kila miaka 19,
huleta pengo dogo la saa 1, dakika 28,
sekunde 38.5.
Mapengo madogo haya tunayoyapuuza
mwanzoni, yameshatugharimu vya kutosha.
Pengo hili kwa mwaka ni dogo lakini kwa
miaka 2500 linakuwa hadi kufika siku nane.
Kwenye hesabu za kutafuta Pasaka
urekebishaji wa hili pengo hutokea kwenye
kanuni iitwayo “Lunar Equation”. Lakini kwa
sababu ya tofauti ya uelekeo wa mzunguko
wa mwezi na dunia, “Lunar Equation”
hujumlisha mara nane kila baada ya miaka
2500.
Hivyo, mahesabu yoyote ya kuitafuta tarehe
ya Pasaka hayakosi kanuni hizi mbili “Solar
Equation” na “Lunar Equation” .
Tumeona kwamba kalenda ilianza mwaka
1582. “Solar Equation” inaondoa siku moja
toka kwenye miaka 1700, 1800, 1900. Hivyo,
ni kujidanganya kusema kwamba miaka yote
inayogawanyika kwa nne ni mirefu, jambo
ambalo hata mimi nilifundishwa shuleni.
Hapa tumeona kwamba “Solar Equation”
imeondoa siku moja kwenye mwaka 1900 na
hivyo haukuwa mwaka mrefu ingawa
unagawanyika kwa nne.
“Lunar Equation” huongeza siku moja kwenye
miaka 1800, 2100, 2400. Mwaka 1800
unaguswa na vyote “Solar Equation” na
“Lunar Equation”. Hivyo hauathiriki.
Kanuni zote za kuitafuta Pasaka huzingatia
zaidi ya niliyoyaeleza, lakini cha muhimu
zaidi ni hizi mbili yaani “Solar Equation” na
“Lunar Equation” ambazo sijawahi kuzisikia
kwa kiswahili.
Ni vigumu kuepuka hesabu za “modulo” au
“mod” unapotafuta tarehe ya Pasaka. Lakini
ukiwauliza wanafunzi wa darasa la nne
kwamba machungwa 2011 yakipangwa
kwenye mafungu 19, ni mangapi yatakosa
fungu?

Wapo watakaopata jibu sahihi kwamba ni
machungwa 16. Kimahesabu swali hilo
linaandikwa hivi: (2011 mod 19) na jibu lake
ni 16, yaani (2011 mod 19=16).
Ifuatayo ni moja ya kanuni zinazotumika
kuipata tarehe za Pasaka ya mwaka wowote
kuanzia 1700 hadi 2099:
(1) : a=MWAKA mod 19;
(2) : b=MWAKA \ 100;
(3) : c=MWAKA mod 100;
(4) : d=b \ 4;
(5) : e=b mod 4;
(6) : f=c \ 4;
(7) : g=c mod 4;
(8) : h=(b + 8)\25;
(9) : i=(b – h + 1)\3;
(10) : j=(19xa + b – d – i + 15) mod 30;
(11) : k=(32 + 2xe + 2xf – j – g) mod 7;
(12) : m=(a + 11xj + 22xk) \ 451;
(13) : n=j + k – 7xm + 114;
(14) : Tarehe=(n mod 31) + 1
(15) : Mwezi =n\31;
Penye neno MWAKA, andika mwaka
unaotafuta kujua tarehe yake ya Pasaka.
Panapotokea alama (\) ni kugawanya
ambako hata kama jibu litaleta desimali, basi
hiyo desimali unatakiwa kuachana nayo ili
jibu libaki namba nzima. Penye alama (x)
hiyo ni ya kuzidisha.
Yafuatayo ni majibu niliyopata kwa hatua
zote baada ya kuuingiza mwaka 2015 ili
kujua siku ya Pasaka ya mwaka huu: (1): 1,
(2): 20, (3): 15, (4): 5, (5): 0, (6): 3, (7): 3,
(8): 1, (9): 6, (10): 13, (11): 1, (12): 0, (13):
128, (14): 5, (15): 4.
Tarehe imepatikana kwenye hatua ya 14
ambako jibu ni “5”. Mwezi umepatikana
kwenye hatua ya 15 ambako jibu ni “4”. Hivyo
Pasaka ya mwaka (2015) huu ni Tarehe 5,
mwezi wa 4.
Hivyo, kwa njia hii, unaweza kujua tarehe za
Pasaka kwa miaka ijayo kama unavyoijua
tarehe ya Krismas. Kama kuna tukio
lilifanyika siku ya Pasaka miaka iliyopita na
hukumbuki tarehe, basi tumia kanuni hii.
Zifuatazo ni siku zinazoitangulia Pasaka kwa
idadi ya siku zilizoandikwa kwenye mabano:
Jumatano Ya Majivu (46), Jumapili ya
Matawi (7), Ijumaa Kuu (2).
Zinazotanguliwa na Pasaka ni hizi zifuatazo:
Kupaa (42), Pentekoste (49), Utatu Mtakatifu
(56), Ekaristi (63).
Mwanzo tuliona kwamba Mwezi-Mkubwa wa

Pasaka au “Ecclesiastical full Moon” ni ule wa
March 22 hadi April 18. Ukitokea March 22
basi kuna uwezekano siku hiyohiyo ikawa
Pasaka na ikawa imevunja rekodi ya kuwahi
mapema.
Ukitokea April 18, kuna uwezekano wa
Pasaka kuwa siku saba zaidi ya hapa yaani
April 25, na hiyo ikawa ni tarehe ya juu mno
ya Pasaka. Hivyo, Pasaka yoyote haiwezi
kuwa chini ya Machi 22, wala haiwezi
kuwazaidi ya April 25.
Pasaka tuliyoiona mwaka 2008 ndiyo ya
mwisho kwa kizazi chetu kuiona ikiwahi
mapema kiasi kile, kwani ilitokea Machi 23 na
itairudia tena tarehe hiyo mwaka 2160!

by JOSEPH MAGATA

Jinsi ya kupika Biskuti Za Kopa Za Kunyunyuziwa Sukari Za Rangi

MAHITAJI

Unga vikombe 2 ¼

Siagi 250g

Sukari kukaribia kikombe ½ (au takriban vijiko 10 vya kulia)

Baking powder ½ kijiko cha chai

Ute wa yai 1

Vanilla 1 kijiko cha chai

Sukari Ya Kunyunyizia na rangi mbali mbali.

MATAYARISHO

Kagawa sukari katika vibakuli utie rangi mbali mbali uweke kando.
Changanya siagi na sukari katika mashine ya kusagia keki upige mpaka ilainike iwe nyororo.
Tia ute wa yai vanilla uhanganye vizuri.
Tia unga na baking powder kidogo kidogo uchanganye upate donge.
Sukuma donge ukate kwa kibati cha shepu ya kopa.
Pakaza siagi katika treya ya kupikia kwenye oveni upange biskuti
Nyunyizia sukari za rangi rangi kisha pika katika oven moto mdogo wa baina 180 – 190 deg F kwa takriban robo saa.
Epua zikiwa tayari.

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Samaki Wa Kuchoma

Vipimo Vya Ugali

Unga wa mahindi – 4 vikombe

Maji – 6 kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria wacha yachemke hasa

Tia unga kidogo kidogo huku ukikoroga mpaka ukamatane

Punguza moto huku ukiendelea kuusonga

Endelea kusonga kwa dakika kadhaa mpaka uanze kuchambuka

Kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari

Vipimo Ya Upishi Wa Mchuzi Wa Samaki Wa Kuchoma Wa Nazi

Samaki:

Samaki wa Nguru – kiasi vipande 5 – 6

Pilipili mbichi – 3

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 5 chembe

Tangawizi mbichi – 1 kipande

Bizari ya samaki – 1 kijiko cha supu

Pilipili nyekundu ya unga – 1 kijiko cha chai

Ndimu – 3 kamua

Chumvi – kiasi

Ukipenda mkate samaki vipande kiasi.
Saga vipimo vyote vinginevyo katika mashine. Mchanganyiko ukiwa mzito ongezea ndimu
Changanya pamoja na samaki upake vizuri vipande vya samaki
Acha kwa muda wa nusu saa vikolee mchanganyiko
Panga samaki katika treya ya kupikia ndani ya oveni, kisha mchome (grill) samaki huku ukigeuza hadi viwive.
Epua weka kando.

Kuandaa Mchuzi:

Nyanya/tungule – 3

Kitunguu – 2

Bizari ya manjano/haldi – ¼ kijiko cha chai

Mafuta – 3 vijiko vya supu

Tui la nazi zito – 3 vikombe

Chumvi – kiasi

Katakata vitunguu na nyanya vidogodogo (chopped) weka kando

Weka mafuta katika karai au sufuria, kaanga vitunguu hadi vianze kugeuka rangi

Tia nyanya kaanga pamoja na tia bizari ya njano/haldi .

Tia tui la nazi, chumvi koroga .

Mwishowe tia vipande vya samaki na rojo lake litakalobakia katika treya, mchuzi uko tayari

Mungu ni mwenye upendo, Huruma na Rehema hasa kwa Wenye dhambi

Mungu ni mwenye upendo Huruma na Rehema hasa kwa Wenye dhambi.
Mungu yupo tayari kumsikiliza mtu yeyote mwenye dhambi kama ameutambua, amekiri na Kutubu makosa yake.

Mungu akishamsamehe mtu uovu wake anambariki.

Hakuna mtu ambaye hatasamehewa na Mungu kama Ametubu, amekiri na Kuomba msamaha wa makosa yake.

Mungu wakati wote yupo akisubiri wenye dhambi waende kwake kwa Toba ili awasemehe.

Lakini tatizo ni la watu wengi wanazani kua wakati wakiwa dhambini Mungu anakua amewakasirikia, Ukweli ni kwamba unapokua dhambini Mungu anakuonea Huruma na anatamani umrudie yeye.

Unaweza ukawa umetenda dhambi lakini hujamuasi Mungu, Kumuasi Mungu ni pale Unapoona kuwa Mungu hana nafasi katika maisha yako tena. Lakini ukiwa dhambini huku unamtumaini Yeye basi bado upo katika njia yake kwa kuwa yeye ni sawa na Baba kwako na kumkosea Baba yako sio kumuasi kama tuu utarudi Kuomba msamaha na Kuheshimu nafasi yake katika maisha yako.

Upendo wa Mungu Kwa Wenye Dhambi

Mungu ni mwenye upendo, huruma, na rehema hasa kwa wenye dhambi. Biblia inatufundisha kwamba Mungu hachoki kuwakaribisha wenye dhambi wanaotubu kwa dhati. Mungu yupo tayari kumsikiliza mtu yeyote mwenye dhambi ambaye ameutambua, amekiri, na kutubu makosa yake. Huruma na rehema zake haziishi kamwe, na anasubiri kwa shauku kubwa kuona wanae wakirudi kwake kwa toba.

“Basi, Bwana, Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli.” (Kutoka 34:6)
“Acha waovu na watu wanaodharau sheria wamrudie Bwana, naye atawahurumia. Warudi kwa Mungu wetu, maana atawasamehe kabisa.” (Isaya 55:7)
“Wote wanaokuja kwangu sitawatupa nje kamwe.” (Yohana 6:37)

Msamaha na Baraka za Mungu

Mungu akishamsamehe mtu uovu wake, anambariki. Hakuna mtu ambaye hatasamehewa na Mungu kama ametubu, amekiri, na kuomba msamaha wa makosa yake. Hii inaonyesha upendo wa ajabu wa Mungu kwa wanadamu wake, upendo ambao haujali ukubwa wa dhambi, bali ukubwa wa toba ya mtu.

“Tubu basi, geuka ili dhambi zako zifutwe.” (Matendo 3:19)
“Na dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kamwe.” (Waebrania 10:17)
“Maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitakumbuka tena.” (Yeremia 31:34)

Mungu Anasubiri Wenye Dhambi Warudi Kwake

Mungu wakati wote yupo akisubiri wenye dhambi waende kwake kwa toba ili awasamehe. Huu ni ujumbe wa matumaini kwa kila mtu anayehisi ameanguka mbali na neema ya Mungu. Mungu ni kama baba anayesubiri mwanae mpendwa arudi nyumbani. Ana shauku ya kumsamehe na kumrejesha kwenye familia ya kiroho.

“Bwana si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili, husamehe uovu na makosa, lakini hatahesabu kuwa hana hatia mwenye hatia.” (Hesabu 14:18)
“Mkiungama dhambi zenu, yeye ni mwaminifu na mwenye haki, atasamehe dhambi zenu na kuwasafisha na udhalimu wote.” (1 Yohana 1:9)
“Furahini pamoja nami, kwa sababu mwana wangu alikuwa amekufa, naye amerudi tena kuwa hai; alikuwa amepotea, naye ameonekana.” (Luka 15:24)

Wakati wa Dhambi: Huruma ya Mungu

Tatizo ni kwamba watu wengi wanadhani kuwa wakati wakiwa dhambini Mungu anakua amewakasirikia. Ukweli ni kwamba unapokuwa dhambini, Mungu anakuonea huruma na anatamani umrudie yeye. Unaweza ukawa umetenda dhambi lakini hujamuasi Mungu, Kumuasi Mungu ni pale unapomkataa kabisa na kuona kuwa hana nafasi katika maisha yako tena.

“Nanyi mtarudi, na kuona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.” (Malaki 3:18)
“Hata kama dhambi zenu ni nyekundu sana zitakuwa nyeupe kama theluji.” (Isaya 1:18)
“Bwana ni mwingi wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, ana wingi wa fadhili. Hata mshika hasira yake daima, wala hatawakemea milele.” (Zaburi 103:8-9)

Kurejea kwa Mungu kwa Toba

Ukiwa dhambini huku unamtumaini Mungu, basi bado upo katika njia yake kwa kuwa yeye ni sawa na baba kwako. Kumkosea Baba yako sio kumuasi kama tu utarudi kuomba msamaha na kuheshimu nafasi yake katika maisha yako. Toba ya kweli inarejesha uhusiano wetu na Mungu, na anatupokea kwa mikono miwili.

“Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao.” (Zaburi 103:13)
“Nikaribieni mimi, nami nitawakaribia ninyi, asema Bwana.” (Yakobo 4:8)
“Heri wenye huruma, maana hao watapata rehema.” (Mathayo 5:7)

Kwa hivyo, tunapokuwa dhambini, tunapaswa kukumbuka kwamba Mungu anatuona kwa macho ya huruma na upendo. Yupo tayari kutusamehe na kutubariki, mradi tu tutambue dhambi zetu, tukiri, na kutubu kwa dhati. Tunapomrudia Mungu kwa toba, tunapokea huruma na neema zake zisizo na kipimo.

Mafundisho na mapokeo Katika Kanisa Katoliki yanapopatikana kwenye Biblia

Wakatoliki wengi huyumbishwa kwa kuambiwa huamini mambo ambayo hayako au ni kinyume na Biblia. Aya zifuatazo zitakusaidia wewe mkatoliki kuelewa au kujua mistari ya Biblia inayofafanua imani katoliki.
1) KUOMBEA MAREHEMU:
2 Mak. 12:38-46
Hek. 3:1
Tob 4:17
2) MATUMIZI YA SANAMU NA VISAKRAMENTI
2Fal 3:20-21
Hes. 21:8-9
Kut. 25:17-22
Kol. 1:20, 2:14
Yn. 12:32
Mt. 19:11-12
3) USAHIHI WA MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI KAMA CHANZO CHA IMANI
2 The 2:15
2 Kor. 10:10-11
Yn 21-25
2 Yoh. 1:12
3 Yoh. 1:13
4) KUABUDU JUMAPILI BADALA YA JUMAMOSI(SABATO)…. Hasa ni kwa sababu Yesu aliitukuza siku ya kwanza ya juma kwa ufufuko wake na kwa kuwatokea wanafunzi wake siku hiyo.
Ufu 1:10
Mdo 20:7
Mt 28:1-8
Lk. 24:1-7
Lk. 24:13ff
1 Kor. 16:1-2
Yn. 20:1-22
5) MAMLAKA YA PAPA KAMA MFUASI AU MRITHI WA MT. PETRO
Yn. 21:15-17
Mt 16:18-19
W 2:1-14
6) MAPADRI KUITWA BABA WAKATI BABA NI MMOJA ALIYEKO MBINGUNI
Mwa 17:4
Yer. 7:7
Hes. 12:14
Yn. 6:49
Mt 23:30
Lk. 1:73
7) JE BIBLIA INATAMBUA MUUNDO WA UONGOZI WA KANISA?
Efe. 4:11-13
1Tim 5:17-25
1Tim 3:1-7,8-18
8) JE BIBLIA INASEMAJE KUHUSU TOHARANI.
Isa 35:8, 52:1
Zek 13:1-2
1Kor 3:15
Lk 12:47-48, 58-59
Ufu 21:27
Ebr 12:22-23
Ayu 14:13-17
9) KUHUSU MATUMIZI YA UBANI
Kut 30:34-37
Hes 16:6-7
Law 16:12-13
Lk 1:10
Ufu 8:32
10) ROZARI IKO KATIKA BIBLIA?
Lk 1:28
Lk 1:42
11) JE KUTUMIA MAJI YA BARAKA NI MAPENZI YA MUNGU?
2Fal 2:19-22
Yn 5:1-18
Yn 7:37
Hes 19:1-22
12) KWANINI TUNAOMBA WATAKATIFU WATUOMBEE?
Mit 15:8, 15:29
Ayu 42:8
Yak 5:16
Mt 16:19
13)KWANINI TUNATUMIA MEDALI, MISALABA, SCAPURALI NA MIFUPA YA WATAKATIFU?
2Fal 13:20-21
14) KWANINI TUNAUNGAMA DHAMBI ZETU KWA PADRI
Mt 16:19,1-20
Yak 5:15-16
15) UBATIZO WA WATOTO WACHANGA UKO KATIKA BIBLIA
Mdo 16:15-33
Mdo 18:8
Mt 28:19
Mdo 10:47-48
16) KUSIMIKWA KWA UTUME
Kut 28:4-43
17) RANGI ZA KANISA
Kut 27:9-29
18) MATUMIZI YA MISHUMAA
Kut 25:31-40; 27:20-21
Hes 8:1-4
19) MPAKO WA MAFUTA YA KRISMA
Kut 30:22-32
20) MPAKO WA MAFUTA YA WAGONJWA
Yak 5:14-15

Cheki huyu jamaa anavyoungama kwa padri sasa

JAMAA: Baba Padri nimekuja kuungama
PADRI: Haya
JAMAA: Niliiba kamba
PADRI: Kamba?
JAMAA: Ndio, kamba lakini kule mwisho kulikuwa kumefungwa ng’ombe
PADRI: Kwa hiyo uliiba ng’ombe?
JAMAA: Kiukweli nilikuwa nina lengo la kuiba kamba, kwa bahati mbaya mwisho kulikuwa na ng’ombe
PADRI: Mi naona mueleze Mungu direct, mi sikuelewi kabisaaa

🙈😃😃😃😀😀😀😂🙊

Utajuaje kama una upungufu wa maji mwilini? Dalili ni hizi

Upungufu wa maji ni pale mwili unapopoteza kiasi kingi cha maji kwa njia mbalimbali, ikiwemo jasho na mkojo, mwili hupungukiwa maji na hivyo mtu huyo huambiwa ana upungufu wa maji. Tunaelezwa kuwa karibu theluthi mbili ya miili yetu imejaa maji.

Ili mwili uweze kufanya kazi yake vizuri, kiwango cha maji mwilini hakipaswi kupungua hata kidogo, hivyo kila mtu ana wajibu wa kunywa maji ya kutosha kila siku ili kulinda kiwago chake cha maji kisipungue na kinapopungua ndipo hapo mwili huanza kuonesha dalili za kukaukiwa maji (dehydration).

Zifutazo ndizo dalili za upungufu wa maji mwilini;

Dalili za upungufu wa maji kwa mtoto.

Kwa kawaida, dalili za upungufu wa maji mwilini hujitokeza zaidi kwa watoto wadogo kuliko watu wazima au wazee. Dalili za upungufu wa maji mwilini kwa watoto huweza kusabababishwa ama na kuharisha, kutapika, kutokunywa maji au vimiminika vingine vya kutosha.

Mtoto mwenye dalili za upungufu wa maji huweza kuonesha dalili zifutazo:

  1. Kukojoa mara chache sana
  2. Mdomo na ulimi kukauka
  3. Mtoto kulia mara kwa mara na anapolia machozi hayatoki.
  4. Mtoto kutokuwa mchangamfu
  5. Macho, tumbo au mashavu kubonyea

Dalili za upungufu wa maji kwa wazee.

Dalili za upungufu wa maji kwa wazee ni tofauti na watu wazima. Wazee wa umri zaidi ya miaka 60 huwa na ngozi iliyosinyaa na hata ukiiminya, hubaki katika hali hiyo kwa muda na unapoikwaruza alama hubaki.
Halikadhalika, wazee hukosa haja ndogo kwa muda mrefu, hupungukiwa uzito kwa kiasi kikubwa na hupatwa na homa.

Dalili za upungufu wa maji kwa wajazito.

Upungufu wa maji mwilini kwa waja wazito ni hatari kwa mama pamoja na mtoto. Dalili zinazoweza kujitokeza kwa waja wazito ni pamoja na:

  1. Kukojoa mkojo wa njano nyeusi
  2. Kuumwa na kichwa.
  3. Mwili kukosa nguvu.
  4. Kichefuchefu na kutapika.
  5. Kukaukwa na mdomo.

Ili kujiepusha na matatizo ya upungufu wa maji na hatimaye kujikuta unakumbwa na dalili kadhaa zilizoelezewa hapo, ambazo ziko pia kwa watu wazima wengine, ni kuwa na mazoea ya kunywa maji ya kutosha kila siku. Hata utakapozidiwa na kukimbizwa hospitali, hakuna dawa nyingine utakayopewa zaidi ya maji (re-hydrating solution) . Kwa nini usubiri hali hiyo ikutokee wakati unaweza kuizuia kwa kunywa maji tu?

Hivyo wito wetu kwako kuendelea kunywa maji mengi ya kutosha kadri uwezavyo hii itakusaidia sana kwa namna moja ama nyingine kuwa na afya bora

Shopping Cart
0
    0
    Your Cart
    Your cart is emptyReturn to Shop
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About