Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Mbinu 9 za kuwavutia na kuwateka wanawake kimapenzi

Kati ya wanawake na wanaume wote wawili wanahitaji kuvutiwa na wenza wao ili wadumu katika mahusiano. Kama mwanaume lazima upate wakati wa kujua unatakiwa kufanya nini kwa ajili ya kulifanya penzi lako lizidi kuchanua.
Hali kadhalika kama bado haupo Kwenye mahusiano kuna mambo ambayo ni ya msingi kufanya au kuwa nayo ili uweze kuwa na mvuto zaidi kwa wanawake.

Yafuatayo ni mambo yakufanya ili kumvutia mwanamke.

1. Kuonyesha kuwa unamjali

Wanawake wanapenda sana wanaume wanaojali wao kama wao, wanaojali kile wanachokifanya na watu wao wa karibu kama ndugu na wazazi. Wanapenda wanaume wanawaona wao ni kila kitu na wanaotoa kipaumbele kwao. Kama huna tabia hiyo, ujue upo katika nafasi kubwa ya kumkwaza mpenzi wako. Mwanamme anatakiwa amjali mpenzi wake kwa kila hali. Kumjulia hali kila wakati na kutaka kujua maendeleo yake, kutakupa nafasi kubwa sana ya kuendelea kudumu katika uhusiano hai. Vile vile kuonyesha kujali mambo yake na watu wake wa karibu kunamvutia mwanamke.

2. Kuonyesha kuwa karibu na kupatikana unapohitajika

Mwanamke huvutiwa sana na mtu ambaye yupo karibu nae na ambaye anapatikana wakati anapohitajika. Kati ya vitu vinavyowapa wapendeza sana wanawake ni pamoja na kusogezwa karibu. Hapa ni kuwa naye katika mambo mengi unayoyafanya kila siku na kushiriki katika mambo yake hata kwa mawazo kama ukishindwa kwa matendo. Ni vizuri kuwa naye au kuwasiliana naye wakati wa kula, ukitaka kujua aina ya chakula alichokula siku hiyo au ikiwezekana mchagulie. Ni mambo madogo sana lakini yanayoongeza nakshi katika mapenzi na ambayo ni muhimu sana kwa wanawake. Yapo mengi sana ambayo kwa kuyafanya utakuwa umemsogeza mpenzi wako karibu yako, mfano kutembea pamoja, kuangalia movie pamoja, nakadhalika. Tumia ubunifu wako ili uweze kuteka hisia za mwenzi wako kisawasawa kwani mwanamke anavutiwa sana na mtu aliye karibu nae.

3. Kumsifia na kumuonyesha kuwa ni bora

Wanawake wanapenda kusifiwa na kuonekana kuwa bora. Mwanamke akisifiwa anahisi kupendwa kupita kiasi. Anajiona kamili, peke yake na mwenye nguvu kwako. Anajiamini na unamfanya azidi kukupenda kwa kuwa anaamini yupo na mwanaume ambaye anajivunia kuwa naye. Vilevile kumsifia mwanamke kwake ni njia ya kuonyesha upendo na Ishara ya kuonyesha kumjali kupita kiasi.

4. Kupewa kipaumbele

Mwanamke anavutiwa zaidi na mtu anayeonyesha kumpa kipaumbele na kupewa nafasi. Kuna wakati wanawake huwa na mambo yao binafsi. Kazini au kifamilia. Inawezekana akatatizika katika eneo fulani ambalo kwa namna moja ama nyingine atahitaji usaidizi wako. Ikitokea mwanamke akawa katika hali hiyo, msikilize.
Mathalani ana tatizo la kifamilia, amekuambia mmoja wa wazazi wake anaumwa, msaidie. Si lazima kifedha, lakini kuonesha kujali kwako tu, kutampa matumani kwamba anaishi na mtu sahihi. Acha kupuuza mambo yake; hata yale madogo, kama ya โ€˜mtoto wa dada amerudishwa ada shuleniโ€™.
Msikilize, mshauri panapofaa kufanya hivyo na ukiweza msaidie hata kifedha. Katika upande wa pili ni hivyo hivyo. Labda una tatizo binafsi, kazini kwako au kifamilia, mshirikishe.
Unaweza kushangaa jambo ambalo uliamini unaweza kulimaliza peke yako, kwa kumshirikisha likawa jepesi zaidi na mambo yakaendelea vyema. Kipaumbele kwa namna yoyote ile, kunaongeza mapenzi zaidi kwa mwanamke.

5. Usafi binafsi

Wanawake wanapenda mwanamme ambaye ni msafi, hii ni kwa sababu kiasili wamejaliwa kupenda usafi ndio maana ni nadra sana kukutana na mwanamke asiyejipenda. Ndiyo maana wanaitwa mapambo ya nyumba au la nyumba! Ni kwa sababu ya hulka yao ya kupenda sana usafi. Mwanamke anavutiwa sana na mwanaume mtanashati. Usafi wako unamfanya ajiamini kuwa na wewe. Hata nyumbani kwako, lazima uishi katika nyumba safi. Hata anapokuja kukutembelea, anakuta mazingira masafi kuanzia sebuleni hadi chumbani. Anapokukuta katika hali ya usafi, inakuwa rahisi zaidi yeye kuanzia hapo alipokukuta na kuendelea mbele.

6. Anavutiwa na mwanamme anayejiamini

Mwanamke anajisikia salama zaidi akiwa na mwanaume ambaye anajiamini yaani mwenye uwezo wa kutetea hoja zake na kujieleza sawia pale anapotakiwa kufanya hivyo au wakati wowote ule. Siyo anayebabaika na kuyumba yumba. Suala la msimamo binafsi, kwa mwanamke ni kubwa kuliko hata kumnunulia nguo mpya.
Mwanamke anapenda kukuona ukiwa katika hali halisi ya maisha yako, usiyeyumbishwa na mwenye kutoa maamuzi yasiyoyumba.
Wakati mwingine, mwanamke anaweza kukupima hata katika jambo ambalo amekosea yeye, ataangalia unavyotoa maamuzi yako, lakini pia atafuatilia kuona kama utakuwa mwepesi wa kuyabadilisha.
Anataka kuona msimamo wako muda wote. Mwanamke hapendi mtu anayebadilikabadilika Kwenye maamuzi na misimamo yake.

7. Malengo ya maisha

Mwanamke anapenda mwanaume mwenye malengo na anayemshirikisha katika mipango yake. Mwanamke anavutiwa na mwanamke mwenye malengo katika maisha yake. Vilevile anapenda mtu anayemshirikisha katika malengo yake na kumuweka katika mipango yake. Faida ya kumshirikisha katika malengo yako ni pamoja na kunampa nguvu na nafasi ya kujiona mama katika familia yenu. Msaidizi kamili wa nyumba yenu. Mweleze juu ya malengo yako, wakati mwingine anaweza kukusaidia sehemu ambayo hukutarajia.

8. Anayeweza kujitetea

Mwanamke hupenda mwanamme anayeweza kujitetea. Mwanaume aliye โ€˜fitiโ€™ ni chaguo la wanawake wengi. Si mnyonge. Mpole kupitiliza na aliye tayari kuonewa! Huyu hana nafasi.
Wanawake hawapendi kuwa na wanaume ambao wapo tayari kuonewa. Wanataka wenye uwezo wa kusimama kidete kuona haki zao hazichukuliwi kirahisi. Hili si suala la kutetea tu haki yako pekee kama mwanaume, bali inapobidi kusimamia haki ya mwanamke wako. Nisieleweke vibaya katika hili, lakini mwanaume imara ni yule ambaye ana nguvu โ€“ anafanya mazoezi na ambaye yupo tayari kwa lolote! Inapowezekana, uwe na uwezo wa โ€˜kuzichapaโ€™ ikiwa mtakutana na vibaka au watu wabaya wenye lengo wa kukudhuru/kuwadhuru au kumdhuru mpenzi wako.

9. Anayemtosheleza tendo la ndoa

Mwanamke anavutiwa zaidi na mwanamme anayeweza kumridhisha katika tendo la ndoa. Anataka mwanamme anayeweza kufanya kile anachotaka yeye na kile anachokipenda. Mwanamke hapendi mwanamme anayemkomoa katika tendo la ndoa au anayefanya mambo asiyoyapenda. Mwanamke anataka kuridhishwa na kujaliwa katika tendo la ndoa.

Ili kufahamu mambo Mbalimbali ya muhimu kuhusu wanawake, Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Huyu jamaa kawaweza wapenda vya bure

Jamaa kaingia mgahawani kwa fujo
JAMAA :ย Nipe soda moja na kila mtu mpe yake maana ninapokunywa soda napenda kila mtu anywe
WATU :ย Ha! Ha! Ha! Haaaa!
JAMAA :ย Nipe mchemsho na kila mtu mpe wa kwake maana ninapokula mchemsho napenda kila mtu ale wake
WATU:ย Watu weweeee! Tena safari hii Na makofi juu..
JAMAA :ย Mhudumu, nipe bili na kila mtu mpe yake maana ninapolipa bili napenda kuona kila mtu analipa yake
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Tafakari ya leo kuhusu Uaminifu

Uaminifu ni kipimo na kigezo cha Ukamilifu na Utakatifu.

Uaminifu ni ishara ya Upendo na tunda la uvumilivu

Uaminifu ni alama ya ushirika na Umoja

Upendo haukamiliki bila Uaminifu.

Ni kwa kiasi cha Uaminifu wako Mungu atakuhukumu

Kama unaweza kuwa mwaminifu katika jambo dogo basi hata Makubwa utakua mwaminifu.

Uaminifu: Kipimo na Kigezo cha Ukamilifu na Utakatifu

Uaminifu ni kipimo na kigezo cha ukamilifu na utakatifu katika maisha ya kiroho. Katika safari yetu ya kiroho, uaminifu ni msingi muhimu unaoonyesha ubora wa uhusiano wetu na Mungu na wanadamu wenzetu. Uaminifu ni zaidi ya neno; ni mtindo wa maisha ambao unaakisi ndani na nje ya matendo yetu ya kila siku.

“Mtu mwaminifu atafurika baraka; bali afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.” (Mithali 28:20)
“Tena asemacho ni hiki, Kama mtu akitamani kazi ya askofu, atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, anayejizuia, anayeheshimika, mkaribishaji, ajuaye kufundisha.” (1 Timotheo 3:1-2)
“Uaminifu wako hudumu kizazi na kizazi; uliifanya imara nchi, nayo idumu.” (Zaburi 119:90)

Uaminifu: Ishara ya Upendo na Tunda la Uvumilivu

Uaminifu ni ishara ya upendo wa kweli na tunda la uvumilivu. Upendo wa kweli hauwezi kuwepo bila uaminifu. Ni kwa kupitia uaminifu ndipo tunathibitisha upendo wetu kwa Mungu na kwa watu tunaowapenda. Uaminifu unahitaji uvumilivu kwani mara nyingi tunakutana na majaribu na changamoto nyingi katika maisha yetu.

“Upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote.” (1 Wakorintho 13:7)
“Basi mnapaswa kuwa na uvumilivu, ili mweze kutimiza mapenzi ya Mungu na kupokea yale ahadi.” (Waebrania 10:36)
“Katika upendo wangu nitakuimarisha. Wakati upendo wako unapokuwa imara, ndipo uaminifu wako unapokuwa thabiti.” (Hosea 2:19-20)

Uaminifu: Alama ya Ushirika na Umoja

Uaminifu ni alama ya ushirika na umoja. Katika jamii yoyote yenye mshikamano, uaminifu unachukua nafasi kubwa. Ni uaminifu unaotuwezesha kuishi kwa amani na kuelewana. Bila uaminifu, ushirika na umoja vinaporomoka, na matokeo yake ni migawanyiko na kutoelewana.

“Ni nani awezaye kukaa katika hema yako? Ni nani atakayekaa katika mlima wako mtakatifu? Ni yeye aendaye kwa ukamilifu, atendaye haki, asemaye kweli kwa moyo wake.” (Zaburi 15:1-2)
“Mimi ni mzabibu wa kweli, nanyi ni matawi. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.” (Yohana 15:5)
“Tuzingatie basi jinsi tunavyoweza kuchocheana katika upendo na matendo mema, tusikose kuhudhuria mikutano yetu, kama wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo; na zaidi sana kwa kadri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.” (Waebrania 10:24-25)

Upendo Hauwezi Kukamilika Bila Uaminifu

Upendo haukamiliki bila uaminifu. Uaminifu ndio unaofanya upendo kuwa wa kweli na wa kudumu. Bila uaminifu, upendo unakuwa na mashaka na hauna msingi imara. Hivyo basi, ni muhimu kuzingatia uaminifu katika mahusiano yetu yote.

“Watu wawili wawezaje kwenda pamoja, wasipokubaliana?” (Amosi 3:3)
“Upendo na uaminifu hukutana pamoja; haki na amani hubusiana.” (Zaburi 85:10)
“Kila kitu mfanyacho na kiwe kwa upendo.” (1 Wakorintho 16:14)

Mungu Atakuhukumu Kwa Kiasi cha Uaminifu Wako

Ni kwa kiasi cha uaminifu wako Mungu atakuhukumu. Uaminifu ni kipimo cha uadilifu wetu mbele za Mungu. Mungu huangalia jinsi tunavyoshughulikia majukumu yetu, madogo na makubwa, kwa uaminifu. Tunapokuwa waaminifu katika mambo madogo, tunadhihirisha kwamba tunaweza kuaminiwa na mambo makubwa.

“Yeye aliye mwaminifu katika lililo dogo, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na yeye aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.” (Luka 16:10)
“Bwana asema hivi, Tumaini la mtu ni Bwana, Uaminifu wake huonyesha tumaini lake kwa Mungu.” (Yeremia 17:7)
“Bwana akasema, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.” (Mathayo 25:21)

Uaminifu Katika Mambo Madogo na Makubwa

Kama unaweza kuwa mwaminifu katika jambo dogo basi hata makubwa utakua mwaminifu. Uaminifu unajengwa hatua kwa hatua, kuanzia mambo madogo tunayofanya kila siku. Hii ina maana kwamba tunapokuwa waaminifu katika majukumu madogo, tunajijengea msingi wa kuwa waaminifu katika mambo makubwa yanayokuja mbele yetu.

“Kuwa mwaminifu hadi mauti, nami nitakupa taji ya uzima.” (Ufunuo 2:10)
“Tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu yawe ya Mungu, wala si kutoka kwetu.” (2 Wakorintho 4:7)
“Nawaambia kweli, kama hamjageuka na kuwa kama watoto wadogo, hamtaingia katika ufalme wa mbinguni.” (Mathayo 18:3)

Hitimisho

Uaminifu ni kipimo na kigezo cha ukamilifu na utakatifu. Ni ishara ya upendo wa kweli na tunda la uvumilivu, na ni alama ya ushirika na umoja. Mungu atakuhukumu kwa kiasi cha uaminifu wako, na kama unaweza kuwa mwaminifu katika mambo madogo, basi hata makubwa utakua mwaminifu. Kwa hivyo, tujitahidi kuishi maisha ya uaminifu katika yote tunayofanya, tukijua kwamba tunamtumikia Mungu mwaminifu ambaye daima yupo nasi, akitubariki na kutuongoza katika njia zake za haki.

Tafakari Upendo Mkuu wa Mungu kwa Mwanadamu

Utangulizi

Mungu alimpenda sana binadamu hata akauvaa Mwili wa Binadamu akashuka duniani na kuishi kama Binadamu ili amkomboe Mwanadamu na hata akaamua kufa kwa ajili ya Binadamu kwa malipizi ya dhambi za Binadamu na kwa maondoleo ya dhambi.

Je, ni Kitu gani ambacho Mungu angemfanyia mtu ambacho hajakifanya?

Kweli nakwambia hata kama Yesu angebaki duniani na kuwa hai mpaka leo bado watu wasinge mwamini na wapo ambao wangemchukia na kumfanya adui yao hata kumuwinda.

Ni watu wachache sana duniani wanaouona upendo huu mkuu wa Mungu, wengi hawaoni wala hawataki kuona. Wapo hata wacha Mungu lakini hawaelewi upendo huu.

Upendo Mkuu wa Mungu kwa Mwanadamu: Kwa Nini Yesu Alikuja Duniani?

Mungu alimpenda sana binadamu hata akaamua kuuvaa mwili wa binadamu na kushuka duniani ili amkomboe mwanadamu. Alishuka na kuishi kama binadamu, akakubali kuteseka na kufa kwa ajili ya malipizi ya dhambi za wanadamu. Huu ni upendo mkuu ambao Mungu ametufanyia, na ni muhimu kuelewa kwa kina ukubwa wa tendo hili la ajabu.

Mungu Alishuka na Kuishi Kama Binadamu

Mungu, kwa upendo wake usio na kifani, aliona mateso na maumivu ya wanadamu na akaamua kushuka duniani kama binadamu kupitia Yesu Kristo. Aliacha utukufu wake wa mbinguni na kuja kuishi kati yetu. Yohana 1:14 inasema:

“Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.” (Yohana 1:14)

Yesu alikuja na kuishi kama binadamu, akakutana na changamoto zote tunazokutana nazo, ili aweze kutuelewa na kutukomboa kikamilifu.

Alikufa kwa Ajili ya Dhambi Zetu

Upendo wa Mungu ulionyeshwa kwa namna ya ajabu pale Yesu alipokubali kuteseka na kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu. Alibeba mzigo wa dhambi za ulimwengu mzima na kutoa maisha yake kama sadaka takatifu. Warumi 5:8 inasema:

“Lakini Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.” (Warumi 5:8)

Yesu hakufa kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wenye dhambi, ili kutupa nafasi ya kupokea msamaha na uzima wa milele.

Je, Ni Kitu Gani Ambacho Mungu Angemfanyia Mtu Ambacho Hajakifanya?

Mungu ametufanyia kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya wokovu wetu. Alitoa mwanawe wa pekee, Yesu Kristo, ili afe kwa ajili yetu na kutuondolea dhambi zetu. Ni nini zaidi tunachoweza kumwomba Mungu ambacho hajakifanya? Hakuna upendo mkuu zaidi ya huu ambao Mungu ametufanyia. Kama ilivyoandikwa katika Yohana 15:13:

“Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.” (Yohana 15:13)

Yesu Angekuwa Hai Mpaka Leo, Bado Watu Wasingemwamini

Hata kama Yesu angeendelea kuishi duniani mpaka leo, bado kungekuwa na watu wasiomwamini na kumchukia. Hii ni kwa sababu mioyo ya watu wengi imejaa ugumu na kutokuamini. Yesu mwenyewe alisema katika Yohana 15:18:

“Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni ya kwamba ulinichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.” (Yohana 15:18)

Hii inaonyesha kwamba kuna watu ambao hata wakiweka wazi upendo wa Mungu, bado watakataa na kumwona Yesu kama adui.

Wengi Hawaoni Upendo Huu Mkuu wa Mungu

Ni watu wachache sana wanaoona na kuthamini upendo huu mkuu wa Mungu. Wengi hawaoni wala hawataki kuona. Wengine ni wacha Mungu lakini hawaelewi kabisa kina cha upendo huu. Hata hivyo, wale wanaoona upendo huu na kuukubali wanapata uzima wa milele na uhusiano wa karibu na Mungu. Yesu alisema katika Yohana 3:16:

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16)

Hitimisho

Upendo wa Mungu kwa mwanadamu ni mkubwa sana na umedhihirishwa kwa Yesu Kristo kushuka duniani, kuishi kama binadamu na kufa kwa ajili ya dhambi zetu. Mungu ametufanyia kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya wokovu wetu. Ni jukumu letu kutambua na kuthamini upendo huu, na kuishi maisha yanayodhihirisha imani na shukrani zetu kwake. Tunapoona upendo huu wa ajabu, mioyo yetu inapaswa kujazwa na furaha na amani, tukijua kwamba Mungu ametupenda sana na anataka tuwe na uzima wa milele.

Cheki tabia za kuandika vimaneno vya ajabuajabu kwenye pikipiki na bodaboda ilivyomponza huyu

Jamaa mmoja dereva wa bajaji alianguka, sasa bajaji ikawa imem’bana akawa anafurukuta bila mafanikio Cha ajabu watu wakawa wanampita bila kumsaidia, Kumbe Nyuma ya Bajaji yake alikua Kaandika “NIACHENI KAMA NILIVYO, HII NDIO STYLE YANGU”ย ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ย Mpaka sasa nimemwacha bado yuko hapoย *Sipendagi Ujinga mimi* ๐Ÿšถ๐Ÿฝ๐Ÿšถ๐Ÿฝ๐Ÿšถ๐Ÿฝ๐Ÿšถ๐Ÿฝ๐Ÿšถ๐Ÿฝ

AHADI 15 ZA ROZARI TAKATIFU

Mama Bikira Maria alitoa ahadi 15 kwa yule au wale watakaosali Rozari takatifu kila siku. Ahadi hizi aliwapa Mtakatifu Dominic na mwenye heri Alan de la Roche.

1. Yeyote yule atakayesali kwa imani rozari hii takatifu atapokea neema kuu zenye nguvu
2. Naahidi ulinzi wa kipekee na neema za kipekee kwa yule atakayesali rozari hii
3. Rozari itakuwa silaha kubwa dhidi ya nguvu za kuzimu, itaharibu maovu, itapunguza dhambi na kushinda kutofautiana
4. Itafanya fadhila kukua, kazi nzuri kuongezeka, itapatia roho huruma tele toka kwa MUNGU, itaondoa hamu ya wanadamu kupenda mambo ya dunia na majivuno yake na kufanya wapende zaidi mambo ya mbinguni. Ooh, ni kwa namna gani roho hizo zitajifurahisha na kubarikiwa kwa namna hii.
5. Roho zitakazojikabidhi kwangu kwa njia ya kusali rozari, kamwe hazitapotea.
6. Yeyote atakayesali rozari kwa uaminifu huku akiyatafakari matendo makuu ya rozari, kamwe hatashindwa na ubaya. MUNGU hatamwadhibu katika hukumu yake, hatapotea katika kifo asichopangiwa na atabaki katika neema za MUNGU na kustahili kupata uzima wa milele.
7. Yeyote atakayekuwa mwaminifu katika kusali rozari, kamwe hatakufa bila ya kupokea Sakramenti takatifu za Kanisa.
8. Wote watakaokuwa waaminifu katika kusali rozari watadumu katika mwanga wa MUNGU katika maisha yao na saa yao ya kufa na kupata neema zake tele; katika saa yao ya kufa watashiriki fadhila za watakatifu waliopo peponi
9. Nitawatoa toharani wale wote waliokuwa waaminifu katika kusali rozari
10. Watoto wangu waaminifu katika kusali rozari watapata fadhila kuu ya utukufu Mbinguni.
11. Utapata yale yote unayoniomba kwa kusali rozari
12. Wote wale wanaoeneza rozari hii takatifu nitawasaidia katika mahitaji yao
13. Nimepata toka kwa mwanangu Mtukufu kuwa mawakili wote wa rozari takatifu watapata
waombezi toka baraza lote kuu la Mbinguni wakati wa maisha yao na wakati wa saa yao ya kufa.
14. Wote wanaosali rozari hii takatifu ni wanangu, na kaka na dada wa mwanangu wa pekee YESU KRISTO
15. Ibada kwa rozari takatifu ni ishara kuu ya kuelekea ukombozi

Ishi kama Penseli ili uwe mtu bora

Muumbaji wa penseli alipomaliza kuiumba penseli yake aliiambia mambo muhimu ya kuzingatia ili iweze kuwa penseli bora kabla hajaituma kuingia kazini kwa matumizi.

โ€œKuna vitu sita unatakiwa uvitambue, โ€œ Aliiambia penseli,

โ€œKabla sijakutuma kwenda kutumika, unatakiwa uviweke akilini vitu hivyo na usivisahau kamwe. Vitakusaidia siku zote na utakuwa penseli bora maisha yako yote.โ€

Alisema muumbaji wa penseli.

โ€œMoja,โ€ alianza kuvitaja,โ€utakuwa na uwezo wa kufanya vitu vingi, lakini kama utakubali na utaruhusu kuongozwa na mkono wa mtumiaji wakoโ€

โ€œMbiliโ€ aliendelea kutoa nasaha, โ€œutapata maumivu makali kutokana na kuchongwa mara kwa mara. Lakini vumilia kwani itakusaidia kuwa penseli bora na kuandika vizuri.โ€

โ€œTatu, utakuwa na uwezo wa kusahihisha makosa utakayo yafanya.โ€

โ€œNne, kitu pekee cha muhimu katika maisha yako ni kile kilicho ndani yako kwa sababu ndicho chenye uwezo wa kuandika.โ€

โ€œTanoโ€ alisisitiza mtengenezaji penseli, โ€œkwenye kila sehemu utakayotumika, utaacha alama yako. Hata ikiwa ni kwenye sehemu ngumu au mbaya kiasi gani, ni lazima alama yako ibaki.

โ€œNa sitaโ€, alimalizia muumbaji yule wa penseli, โ€œipo siku utaisha na kupotea. Hivyo usiwe na hofu wala woga wala hudhuni uikaribiapo siku hiyo na ukaogopa kutimiza wajibu wako kwa kuhofia kuisha. Ukiogopa kuisha hautotumika na umuhimu wako hautonekana kwani hautatimiza wajibu uliombiwa kuufanyaโ€

Penseli ilielewa na kuahidi kukumbuka na ikaingia sokoni ikiwa na dhamira yake moyoni.

Sasa tutumie mfano huo wa penseli katika maisha yetu halisi. Ukivikumbuka vitu hivyo sita ilivyopewa penseli, utaweza kuwa mtu bora kabisa kwenye maisha yako yote.

Moja, una uwezo wa kufanya mambo mengi na makubwa, kama utajiweka kwenye mikono ya Mungu.

Mbili, utakutana na magumu mengi ya kuumiza, lakini hayo ndiyo yatakufanya uwe mtu imara na bora, usiyakimbie.

Tatu, una uwezo wa kurekebisha makosa yote uliyoyafanya. Usijilaumu.

Nne, sehemu yako ya muhimu ni ile iliyo ndani yako kwani ndiyo inayoandika maisha yako. Ilinde.

Tano, kila sehemu utakayopita, acha alama yako kwa kufanya mazuri yatakayokufanya ukumbukwe daima, bila kujali mazingira. Timiza wajibu wako kwa kiwango cha juu.

Sita, tambua kuwa ipo siku utakufa. Usiwe na hofu yoyote juu ya kifo kwani ukiogopa kifo hutafanya lolote hapa duniani.

Tumia mfano huu wa penseli upate ujasiri wa kutambua kuwa wewe ni mtu muhimu hapa duniani na umeumbwa kwa madhumuni maalumu na umepewa uwezo mkubwa sana na Muumba wako! Ni wewe pekee mwenye uwezo wa kutimiza dhamira uliyotumwa na Muumba.

UBARIKIWE SANA.

BADILIKA: Anza kupiga hatua ya maendeleo sasa

Ili kutoka hapo ULIPO uweze kwenda HATUA inayofuata kuna SWALI muhimu sana unahitaji kujiuliza.
Watu ambao huwa wanashindwa kupiga hatua katika maisha yao ni kwa sababu huwa wanajiuliza kinyume cha swali hili.
Swali hili ndilo wanalojiuliza watu wote waliofanikiwa:

Swali: “Hivi kwa sasa nina nini ambacho naweza kuanza kukitumia kama mtaji wa kwanza kuanza kufanya ninachotaka”?

Siku moja wakati nasoma biblia niliona Mungu alipotaka kumtumia Mussa kuokoa wana wa Israel akamuuliza-

โ€œUna nini mkononi mwakoโ€-

Mussa akajibu
kwa kudharau alichonacho kuwa โ€œNina fimbo kavu tu ya kuchungia mifugoโ€.

Ndipo Mungu alianza kumuonyesha miujiza kutumia fimbo ambayo siku zote
alikuwa nayo na kujidharau ndiyo ambayo ikatumika kwenda kuokoa wana wa Israel.

Watu wengi sana wanashindwa kuanza kwa sababu huwa wanajiuliza-

“Hivi ninakosa nini ili niweze kuanza”
badala ya ‘Hivi nina nini cha kuanzia’.

Cha kuanzia sio lazima iwe pesa-Inawezekana ni uwezo wa kufanya jambo fulani la kipekee,inawezekana ni
mahusiano mazuri uliyonayo na watu fulani(mtandao wako),inawezekana ni uzoefu ulionao,inawezekana ni kipaji n.k
Leo unapoanza siku yako naomba ijiulize-

โ€œNina nini mkononi mwangu ambacho naweza kutumia katika
hatua ya kwanzaโ€?.

Kumbuka hakuna mtu ambaye hana
kitu kabisa-KITAFUTE HADI UKIPATE NA ANZA KUKITUMIA KUCHUKUA HATUA.

Share ili wengine wajifunzeโ€ฆ..uwe na Jumatatu njemaโ€ฆโ€ฆ..

Matumizi ya mihogo kama dawa ya kuzuia wadudu kwenye mimea

Muhogo Inazuia Minyoo na vidukari.

Hatua za Kutayarisha dawa

  • Toa maji ya matunda kwa kuponda mizizi;
  • Pima k i w a n g o kimoja cha maji ya m a t u n d a sawa na maji ya kawaida (1:1).
  • Nyunyiza haraka ukitumia lita nne kwa mita moja za mraba, inasemekana kuwa na athari kubwa.
  • Subiri kwa siku ishirini kabla ya kupanda.

Angalizo:ย Tafuta ushauri wa mtaalamu wa kilimo kabla ya kutumia dawa yoyote ya asili

Cheki nilichomfanyia boss wangu

Bosi wangu karudi safari yake kutoka serengeti..! Si akanitumia picha, lakini ilikuwa network yenyewe tabu.. kwahio picha haikufunguka na kwa vile niliona itachelewa kufunguka na ataona sikumjibu basi nami..

Nikampelekea msg nikamuandikia umependeza saana bosi mashaallahโ€ฆ!!
sasa baada tu ya kumfika msg.. na huku picha ikafunguka kumbe picha ya Sokwe..!!
Basi Kaniambia kesho niende ofsini kwake kuna barua yangu..
Nahisi hyo barua ina pesa, hapa cjalala, nmekosa usingizi kabisa,nawaza ninunulie nn hyo pesa.Na kesho asubuhi sa 12 asubuhi atanikuta ofisini kwake naisubiri barua, sipendagi ujinga mimi.

BREAKING NEWS!!! Nyoka wa ajabu agundulika

HABARI MPASUKO..

jana katika taasisi ya wanyama pori ya Nat Geo ilitangazwa kuwa ametokea Nyoka hatar san Ambaye hajawah kutokea duniania.. wanadai kwamba nyoka huyo anaongezeka ulrefu wa 0.5sm kila akila chakula na huwa anakula chakula kuanzia sekunde 30 kurudi nyuma.. mpaka sasa hakuna siraha ya kuweza kumuua nyoka huyo isipokuwa akiji uma mwenye ndo anaweza kufa, wanasayansi hao walieleza japo uchunguz zaid bado unaendeleaโ€ฆ huyu ni nyoka anayeua kuliko nyoka wote waliowah kutokea katika historia ya maisha ya mwanadam..

nyoka huyu hupatikana katika simu pekee za nokia toch katika sehem ya game inaitwa snake xenzia..

asanteni kwa kufurah na umakin mkubwa katika usomaji wa matini hiiโ€ฆ

haya ni mambo ya wikiend jaman na iwe njema kwenu wote

Kuwa na mahusiano na msichana kama huyu ni changamoto, Mabinti bwana!

Binti: Hallow mpenzi, Mambo

Jamaa: Poa baby

Binti:Uko wapi?

Jamaa: Niko town napata lunch

Binti: Wow unarudi saa ngap? Nina njaa dear naomba uniletee msosi

Jamaa: Narudi baada ya nusu saa nikuletee nini?

Binti: Niletee chipsi kuku, soseji, mayai manne ya kukaangwa pembeni, baga, piza, coke take away baridi, mkate wa moto kwenye ile bekari ya wapemba na maji ya kunywa ya kiimanjaro.

Jamaa:Umesahau viti, meza, masufuria, sahani na beseni na vijiko.

Binti: Kwanini dear?

Jamaa: Naona hutaki kula unataka kufungua hoteli!

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About