Karibu AckySHINE
Karibu AckySHINE
Chagua Unachotaka Kusoma Hapa
Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.
Amini unashinda
Amini kuwa unashinda na wewe utashinda. Hata vita wanashinda wale wanaoamini katika ushindi. Kutokujiamini ni sawa na kushindwa tayari.
Jinsi ya kutengeneza mishumaa
MALIGHAFI ZINAZO HITAJIKA WAKATI WA UTENGENEZAJI WA MISHUMAA.
1. Paraffin Wax
2. Utambi
3. Mould ( Umbo )
4. Stearine au mixture
5. Rangi
6. Jiko la mafuta ya taa au mkaa.
7. Sufuria.
8. Boric acid.
VIDOKEZO MUHIMU :
1. Paraffin Wax :
Hii inatokana na nta na sega ya nyuki iliyo changanywa na mafuta ya taa. Ina rangi nyeupe na katika utengenezaji wa mishumaa ina ubora kuliko bee wax.
* Bee Wax : Inatokana na masega ya nyuki yaliyo changanywa na mafuta ya petroli na diesel na rangi yake ni ya njano.
2. STEARINE
Hii dawa maalumu inayo fanya mishumaa iungane ama ishikamane.
3. BORIC ACID :
Hii ni maalumu kwa ajili ya kuufanya utambi usiishe mapema na uwake bila kutoa moshi.
4. RANGI :
Rangi nzuri zinazo tumika katika utengenezaji mishumaa ni rangi za chakula na nyingi huwa ni za maji.
JINSI YA KUTENGENEZA
Andaa mould ( umbo lako ) utakalo litumia baada ya kuyeyusha ( paraffin wax ) na kuchanganya na michanganyo yote.
Kwa Mfano : ( Kipimo cha stearine )
1. Wax kilo moja – Stearine vijiko vinne vya chakula.
2. Wax nusu kilo – Stearine vijiko vinne vya chakula
3. Wax robo kilo – Stearine kijiko cha chakula.
Baada ya mould ( umbo ) kuwa tayari , chemsha wax mpaka iyeyuke na itoe kwenye vyombo ambavyo umetayarisha na usubiri ikauke ili uanze kutoa mishumaa.
Sasa Hawa wadada Wapo in Relationship Na Nan!!??
Asilimia 76% Ya Wasichana Kila Ukiwatongoza Wanakwambia Wapo In relationship SAWA ATUKATAI…
Asilimia 98% Ya Mamen Wapo SINGLE… HAPA NDIPO HESABU ZANGU ZINAFELI..
Sasa Hawa wadada Wapo in Relationship Na Nan!?.
Hawa wanaume wanaopenda wanawake hovyo barabarani wamepatikana, hawatarudia 😂😂😂
Marafiki wawili (Jose na Ben) walikuwa wanatembea mtaani akatokea mwanamke akarusha busu kwa mmojawapo kupitia dirishani katika jengo la ghorofa tatu.
Wakaanza kujadiliana kama ifuatavyo:
Ben: Muone yule mrembo amenirushia busu
Jose: tafadhali achana na huyo mwanamke, usimjali..
(baadae yule mwanamke akamuashiria aende)
Ben: yule mwanamke ameniita!
Jose: Rafiki yangu, usiende. Nakutafadhalisha.
Ben: Kwa nini unaniambia nisiende Wakati mrembo kama yule ananiita? Huo ni wivu
Jose: Ben, Ninakutafadhalisha tena, usiende, tafadhali usiende kule (akihisi kutotiliwa maanani)
(Rafiki yake alimpuuza na alienda kwa yule mwanamke, mwanamke alishuka kukutana naye na wakapanda juu. Ghafla wakiwa wanataka kuanza taratibu za kula uroda, wakasikia mlio WA gari getini).. 🔊🔊
Lady: _(akiangalia kupitia dirishani)_
Oooh! Yule ni mume wangu!!
Ben: Mama yangu !
Nipo matatani, kweli ? ..!!
Lady: Usiwe na khofu, jifanye kuwa Dobi na anza kupiga pasi hizo nguo
(akimuonyesha lundo la nguo)
(Ben alitumia masaa matano kukamilisha kunyoosha zile nguo kwa sababu yule mume hakutoka tena siku ile)
(Siku iliyofuatia Ben alikwenda kwa Rafiki yake)
Ben: Kaka, unaweza kuamini Jana nimepiga pasi nguo kwa masaa matano???
Jose: Lakini nilikwambia usiende. Nguo zote hizo ulizonyoosha, Nilizifua Mimi Juzi!!
😂😂😂😂😂😂😂😂😂
When an experienced person speaks … 👂you must listen..!
Vyakula vinavyofaa kutumiwa kwa mtu mwenye kisukari aina ya kwanza
Vyakula hivyo ni;
- Maharage
- Nyanya
- Samaki
- Mboga za majani zenye rangi ya kijani
- Matunda jamii ya machungwa
- Mafuta ya nazi
- Viazi vitamu
- Vyakula ambavyo havijakobolewa
- Maziwa yasiyo na mafuta ndani yake
- Mbegu za maboga
- Mtindi usio na mafuta ndani yake
Ni vizuri kujua haya
👉🏿Degree au vyeti ulivyo navyo haviwezi kukupa mafanikio.
👉🏿Uzuri ulio nao hauwezi kukupeleka kwenye ndoto zako.
👉🏿Usipobadilisha hao marafiki ulio nao hutofika mahali popote.
👉🏿Usipobadilisha vitendo unavyovifanya kila siku hivyo hivyo mafanikio utayasikia kwa wengine.
👉🏿Kazi au ajira unayoifanya usipojiongeza haiwezi kukupeleka kwenye maisha unayoyataka.
👉🏿Huo mshahara unaolipwa usipoutumia vizuri na kujiwekea akiba au kuwekeza kidogokidogo hutoacha kulalamika kila siku mshahara mdogo au hautoshi.
👉🏿Usipoacha kukopa bila malengo mafanikio ni ngumu kuyapata.
👉🏿Usipowekeza muda kwa ajili ya kujifunza na kuelewa mambo mengi ya biashara na ujasiriamali kwa ujumla na kufahamu dunia imetoka wapi,iko wapi na inaelekea wapi huytoacha kulalamika.
👉🏿Usipolipia gharama za kujifunza na ukajifunza kweli kile unachoelekezwa ikiwa ni pamoja na Pesa na muda haya mambo waachie wengine.
👉🏿Usipobadili fikra na mtazamo wako huwezi kubadilisha chochote katika maisha yako.
👉🏿Ukiacha kusikiliza kila aina ya ushauri unaopewa na ndugu zako,jamaa zako,marafiki zako,familia yako,majirani zako na kujisikiliza wewe mwenyewe utahangaika sana.
👉🏿Usipofanya bidii na juhudi na ukakubaliana na changamoto zozote utakazokutana nazo maisha yatakuwa magumu sana kwako.
Kumbuka mtu pekee Wa kuyabadilisha maisha yako na kukusaidia kufikia malengo na ndoto zako wala sio mwingine ni mmoja tu nae ni WEWE.
Badilisha fikra zako,badilisha mtizamo wako,badilisha maisha yako.
Jinsi ya kumjua mwanamke ambaye hajatulia a.k.a kicheche
Kumjua mwanamke ambaye hajatulia unaangalia mambo haya yafuatayo
Siyo rahisi kupenda
Dalili ya kwanza ya mwanamke kicheche mi kwamba huwa huwa mara nyingi hawataki mambo ya mahusiano na mambo ya kupendana, wanataka siku zote wawe huru hata mtu yeyote mwenye uwezo zaidi ya aliyenaye akitokea, iwe rahisi kwake kujihusisha naye. Utasikia akisema tuwe Marafiki tuu.
Anachukulia mahusiano kama njia ya kujinufaisha
Wanawake vicheche huwa hawaingii katika mahusiano kwa sababu wamependa, siku zote wanakuwa na agenda ya siri nyuma yake, unaweza kuita faida, kiujumla kwa kitu chochote atakachokupa katika mahusiano, ujue hapo anatarajia faida yake, utakuta anakuchangamkia na kukufanyia vitu ambavyo hukutarajia, ila lengo lake mwisho wa siku utakuta anaishia kukuomba kitu Fulani kutoka kwako. Yupo tayari kufanya chochote hata kama kinamgarimu ilimradi apate kile anachokitaka.
Anategeka kirahisi kwa vitu vidogo na kwa mtu yoyote
Kwa kawaida mwanamke kicheche, pale tu utapomfurahisha na kumpa zawadi, au hela kila akuombapo unamsaidia, ni rahisi sana kukubali chochote utakacho mwambia afanye, haijalishi kuwa unamalengo gani nae ya baadae au la, ilimradi tu unampa anachotaka. Na hii hutokea kwa kila mwanaume anayemkuta ambaye anaweza kumpa kile anachotaka basi atamfanyia chochote huyo mwanaume anachotaka.
Anamarafiki wakiume kwa manufaa
Mwanamke kicheche huwa na Marafiki wengi wa kiume kila mmoja kwa ajili ya faida. Mwanamke kuwa na marafiki wa kiume siyo tatizo, ila tatizo linakuja pale ukute mwanamke ana marafiki wa kiume ambao kila rafiki yake huyo anajukumu lake katika maisha yake, kifaida zaidi na siyo tu rafiki wa story za hapa na pale. Unakuta Marafiki hao wote kila mtu anahudumia na wote unaambiwa ni marafiki tu, unaweza kusikia huyu wa kulipia saloon, mwingine wa vocha n.k, basi ujue huyo ni kicheche.
Ni rahisi kuvunja mahusiano usipompa anachotaka
Mwanamke kicheche anakasirika haraka usipompa kile anachokitaka. Wanawake kama hawa wamezoea kupata kitu chochote watakacho kutoka kwa mwanamme, na ukibahatika kupendwa na mtu kama huyu ujue si bure, ameona kuna kitu utakachoweza kumsaidia, wengine utakuta wanapohitaji kitu wanazunguka na story nyingi ila mwisho wa siku kama mtu muelewa utajua tu anataka nini, tena hata kubembelezwa hashindwi, ila usimpe sasa anachohitaji, unaweza usiongeleshwe wiki nzima hadi pale utapokamilisha hitaji lake. Ukishindwa kabisa kumpa anachokitaka basi anavunja uhusiano na wewe na kutafuta mtu mwingine anayeweza kumpa anachokitaka.
Unaweza kuwafahamu wanawake zaidi kupitia Kitabu hiki cha SIRI ZA WANAWAKE. Unaweza kudownload kitabu hiki moja kwa moja hapa
-
Familia, Mapenzi na Mahusiano
📕Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE👧👗👠
Original price was: Sh7,500.Sh3,000Current price is: Sh3,000. Download Now
LISHE BORA KWA WATU WENYE AFYA NZURI
• Kula chakula bora kunamaanisha kula vyakula aina tofauti ya vyakula kila siku kama vile matunda, mboga, maziwa na aina ya vyakula vyenye asili ya nyama wa kufuga kama kuku, mbuzi, ngombe, samaki na na vyakula vya nafaka.
• Lishe bora linamaanisha pia kula chakula ambacho hakina mafuta mengi, sukari au chumvi nyingi
• Zingatia angalau vyakula vya nafaka kama vile mtama, mahindi, mchele, ngano, wimbi, ndegu, njegere. n.k
• Ni bora kula matunda mengi kama ‘maembe, ndizimbivu, papai, pera, chungwa, ubuyu, nanasi, pesheni, zambarau” na mbogamboga kama vile “mchicha, majani ya mboga, karoti, nyanya chungu, nyanya, mkunde, biringanya” mara tano kwa siku.
• Kama mboga na matunda hazipatikani ni bora kununua zile ambazo zimehifadhiwa tayari kwenye mikebe au zile ziko kwenye jokofu (friji).
• Punguza kula vyakula ambavyo vinapikwa kwa mafuta mengi na chumvi nyingi
• Lishe bora hukusaidia wewe na jamii yako kuishi vyema, kuwa na afya bora, kufanya kazi vizuri na kwa bidii, shuleni na hata kucheza.
Jinsi ya kutengeneza Rock-cakes Za Njugu Na Matunda Makavu
Mahitaji
Unga – 4 Vikombe
Sukari -10 Ounce
Siagi – 10 Ounce
Mdalasini ya unga – 2 vijiko vya chai
Matunda makavu/njugu (kama lozi, Zabibu, maganda ya chungwa, Cherries na kadhalika – 4 ounce
Maziwa ya maji – 4 Vijiko vya supu
Maandalizi
Chukua siagi na sukari koroga na mixer mpaka iwe kama cream.
Tia vanilla mdalasini, tia yai moja mix tena endelea kuongeza yai lingine mpaka umalize yote, changanya mpaka iwe laini kama sufi (fluffy)
Tia unga na baking powder na dried fruits, changanya na mwiko.
Chota mchanganyiko na kijiko cha soup weka kwenye treya ya kupikia tandaza na uma ili upate matundu juu ya biskuti.
Pika (bake) kwenye oven lenye moto wa 375 F. kwa muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama.
Uvaaji wa Tai kulingana na Umbo lako
Kuna mambo mengi ya kufanya ili tuwe watu wa kuvutia kila wakati.Mpangilio wa mavazi hufanya mtu kuonekana maridadi. Kama wewe ni mvaaji wa tai unapovaa unazingatia mambo yapi? Na je unafunga tai yako kwa namna inayokubalika?
Wengine huwa hawafahamu jinsi ya kufunga tai na hivyo kuleta mushkeri wakati wa kuvaa tai na kusababisha tai kukaa upande. Unapoamua kuvaa tai na shati ambalo halijanyooshwa ambalo linakuwa kwenye mikunjo au kuvaa tai na ndala unakuwa umeua maananzima na kulivunjia heshima vazi hili.
Tai ni vazi lawatu walio maridadi kama huwezi kuwa maridadi basi vazi hili halikufai kabisa.
Unapovaa taa unatakiwa kuzingatia aina ya umbo lako kama wewe ni mnene vaa tai inayoendana na mtu mnene na kama wewe ni mwembamba basi vaa tai inayoendana na mtu mwembamba.
Kuna wengine huvaa tai zinazofika magotini na kuwa kichekesho anapopita mtaani
Tai ni vazi ambalo huongeza heshima na hadhi ya mvaaji cha muhimu ni jinsi gani unavaa tai yako na ikiwezekana jaribu kumechisha tai na suruali kwa vile ili tai upendeze ni laima iendane na nguo unayovaa.
Ni vyema ukahakikisha kuwa unakuwa na tai zenye rangi tofauti ambazo zitaendana na nguo unazovaa.
Duh. mjamzito ana kazi
😂😂😂😂ukimuona mjamzito katema mate ujue mtoto kajamba
Aina mojawapo ya watoto ambao ni hasara kuwa nao
Alipelekwa Hospitali na baba yake, baada ya vipimo Doctor akawa anamuandikia dawa, baba yake akatoka nje kuongea na cm.
Mtoto akamwinamia Doctor na kusema kwa sauti ya chini:- “Doctor Kwenye dozi ya dawa niandikie na FANTA BARIDII, CHIPS na MISHIKAKI kutwa mara 2 kwa siku 30.
Faida za ulaji wa Peasi
Peasi ni tunda ambalo limekuwa halithaminiwi licha ya kuwa na faida lukuki katika mwili wa binadamu. Tunda hilo ambalo kwa umbo linafanana na tufaa (apple), lina faida nyingi kwa binadamu iwapo atalitumia mara kwa mara.
Tunda hili limekuwa adimu kutokana na kutostawi katika maeneo mengi hivyo watu wengi hawalifahamu na hata walionapo hawalitilii maanani kama ilivyo kwa matunda mengine kama vile ndizi, embe, papai na mengine.
Tunda hili lina faida mbalimbali katika mwili wa binadamu kama vile kukausha jasho la kwapa kwa wale wenye kutokwa na jasho jingi endapo litaliwa mara kwa mara.
Pia tunda hilo ambalo hulimwa sana katika Mkoa wa Tanga husaidia kupunguza mwasho wa koo na juisi yake ni nzuri skwa kuua mba, hutibu kibofu cha mkojo na uti wa mgongo.
Vilevile tunda hili lina Vitamin A na B ambazo husaidia kuepukana na upofu, pia husaidia kuongeza hamu ya kula na kuboresha mfumo wa fahamu.
Wakati mwingine tunda la peasi husafisha mishipa ya moyo na kutibu mafua ya ndege na husaidia mmeng’enyo wa chakula ufanyike vizuri.
Tunda la Peasi husaidia kuongeza kinga za mwili, kuupa mwili nguvu, hupunguza shinikizo la damu, kuzuia mafuta kuganda mwilini (cholestrol), huzuia magonjwa ya saratani, kiungulia pamoja kupunguza homa.
Pia tunda hili likitumika baada ya chakula cha usiku au baada ya kupata kifungua kinywa huweza kuleta matokeo mazuri.
Angalia alichojibu huyu mwanafunzi, Ungekua wewe ni mwalimu wake ungemfanyaje?
Mwanafunz alikuwa kila siku anachelewa shule, na kila siku alikuwa anachapwa, basi siku moja mwalimu akaona ngoja amuulize.
Mwalimu: Mbona unachelewa kila siku?
Mwanafunzi: Nakaa mbali mwalimu
Mwalimu: (huku ana hasira akauliza)Mbali mbinguni?
Mwanafunzi: Mbinguni kwa mbele😂😂😂😂😂
Namna ya kutengeneza Visheti Vya Nazi Na Njugu (Sudani)
VIAMBAUPISHI
Unga – 3 mug za chai
Samli – ½ mug ya chai
Maziwa – 1¼ mug ya chai
Baking powder – 2 vijiko vya chai
VIAMBAUPISHI VYA MJAZO
Njugu zilizomenywa vipande vipande – 2 vikombe cha chai
Sukari – ½ kikombe cha chai
Iliki – 1 kijiko cha chai
Nazi iliyokunwa – 2 vikombe vya chai
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari – 2 vikombe vya chai
Maji – 1 kikombe cha chai
Ndimu – 1
JINSI YA KUVIANDAA
1-Changanya unga na samli kisha tia baking powder na maziwa. Ukande ulainike kisha
uwache kama dakika 5 uumuke.
2-Kwenye bakuli nyingine changanya njugu, sukari na iliki.
3-Kata madonge madogo dogo sukuma kila donge duara jembamba, kisha tia kijiko cha mchanganyiko wa njugu juu yake ifunikie juu yake na ibane pembeni.
4-Panga kwenye treya isiyoganda (non stick) kisha choma kwenye oven kwa moto wa chini
(bake) 350° C kwa dakika kama 15-20.
5-Chemsha maji na sukari katika sufuria ndogo kisha tia ndimu acha ichemke mpaka inatenate unapoigusa.
6-Kwenye sahani ya chali mimina nazi iliyokunwa.
7-Vibiskuti vikiwa tayari vya motomoto chovea kwenye shira kisha zungushia katika nazi iliyokunwa,
panga kwenye sahani tayari kwa kuliwa.
Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ya Ng’ombe Na Nyanya
Vipimo
Mchele (Basmati) – 3 vikombe
Nyama ya ngo’mbe – 1 kg
Pilipili boga – 1 kubwa
Nyanya – 2 kubwa
Vitunguu maji – 2 vikubwa
Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa – 1 kijiko cha supu
Tangawizi – 1 kijiko cha chai
Ndimu – 1
Mafuta ya kupikia – ½ kikombe
Mdalasini – ½ kijiko cha chai
Binzari nyembamba – 1 kijiko cha chai
Pilipili manga – ½ Kijiko cha chai
Hiliki – ½ Kijiko cha chai
Namna ya kutayarisha na Kupika
Roweka mchele wako katika chombo
Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie thomu, tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi
Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi
Katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni
Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia
Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto
Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya
Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi
Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke
Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza
Funika na punguza moto na uache uive taratibu
Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.
Angalia huyu dada alivyoumbuka, Duh! Alijua haoni!!!
Dem anatoka kuoga akiwa na kanga moja tu anaskia hodi,kufungua mlango akakuta ni jirani yake frank ambaye ni kipofu, akamkaribisha ndani akakaa, dem kavua ile kanga akabaki uchi akainama akaanza kujipaka mafuta akijua frank hamuoni na mazungumzo yakawa ni Haya..
DEM: VIPI FRANK MBONA UMEPOTEA YAANI HUONEKANI SIKU HIZI..?
FRANK: AH NILIENDA INDIA KUFANYIWA OPERESHENI YA MACHO SASA HIVI NAONA VIZURI KABISA!…
😂😂😂
🏃🏻🏃🏻🏃🏻🏃🏻🏃🏻
Hii ndio ngoma droo kwa wanaume kati ya wanawake
{ NGOMA DROO}
Sikuizi utawasikia wadada wakisema kuachwa na mwanaume asie na pesa nisawa na kuluhusiwa hospital
{Sasa na sisi} wanaume tunasema
Kuachwa na demu mpenda pesa nisawa na kumaliza mkopo benk 😂😂😂😂😂😂
Wanaume atutakagi ujinga!!!! Wanaume heeeeee🏃🏾♂🏃🏾♂🏃🏾♂🏃🏾♂
Fahamu kuhusu kitambi na uzito uliopitiliza
Mwili wa binadamu umeundwa kwa organs na mifumo mbalimbali ili kuuwezesha kufanya kazi sawia. Mfano,
Moyo
Ini
Figo
Mapafu
Mfumo wa fahamu
Mfumo wa uzazi
Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula.
Vyote hivi hufanya kazi kwa usahihi ikiwa mwili una balance ya
Mafuta
Sukari
Nishati
Protein
Vitamins
Lakini kutokana na mfumo wa maisha kubadilika kwa kiasi kikubwa, watu wengi inasemekana wankumbwa na tatizo la OVERWEIGHT (Uzito uliopitiliza) na OBESITY (Kitambi).
Kwa nini tatizo ni kubwa katika rika zote..!?
1.°° Ulaji wa vyakula vya wanga, kama ugali wa sembe , chapati.
2.°° Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi.
3.°° Ulaji wa nyama nyekundu, kuku wa kisasa na mayai.
4.°° Utumiaji wa beer na soda kwa wingi.
5.°° Mfumo mbaya wa ulaji kwa ujumla.
Madhara yake.
- Shinikizo la damu (Pressure).
- Kisukari (Diabetes)
- Maradhi ya moyo (Heart attack).
- Maumivu ya mgongo na joints.
- Kiharusi
- Maradhi ya mifupa (Osteoporosis)
Nini cha kufanya
- Mazoezi ya viungo ni muhimu sana.
- Kuepuka ulaji wa mafuta mengi.
Recent Comments