Mama Bikira Maria alitoa ahadi 15 kwa yule au wale watakaosali Rozari takatifu kila siku. Ahadi hizi aliwapa Mtakatifu Dominic na mwenye heri Alan de la Roche.
1. Yeyote yule atakayesali kwa imani rozari hii takatifu atapokea neema kuu zenye nguvu
2. Naahidi ulinzi wa kipekee na neema za kipekee kwa yule atakayesali rozari hii
3. Rozari itakuwa silaha kubwa dhidi ya nguvu za kuzimu, itaharibu maovu, itapunguza dhambi na kushinda kutofautiana
4. Itafanya fadhila kukua, kazi nzuri kuongezeka, itapatia roho huruma tele toka kwa MUNGU, itaondoa hamu ya wanadamu kupenda mambo ya dunia na majivuno yake na kufanya wapende zaidi mambo ya mbinguni. Ooh, ni kwa namna gani roho hizo zitajifurahisha na kubarikiwa kwa namna hii.
5. Roho zitakazojikabidhi kwangu kwa njia ya kusali rozari, kamwe hazitapotea.
6. Yeyote atakayesali rozari kwa uaminifu huku akiyatafakari matendo makuu ya rozari, kamwe hatashindwa na ubaya. MUNGU hatamwadhibu katika hukumu yake, hatapotea katika kifo asichopangiwa na atabaki katika neema za MUNGU na kustahili kupata uzima wa milele.
7. Yeyote atakayekuwa mwaminifu katika kusali rozari, kamwe hatakufa bila ya kupokea Sakramenti takatifu za Kanisa.
8. Wote watakaokuwa waaminifu katika kusali rozari watadumu katika mwanga wa MUNGU katika maisha yao na saa yao ya kufa na kupata neema zake tele; katika saa yao ya kufa watashiriki fadhila za watakatifu waliopo peponi
9. Nitawatoa toharani wale wote waliokuwa waaminifu katika kusali rozari
10. Watoto wangu waaminifu katika kusali rozari watapata fadhila kuu ya utukufu Mbinguni.
11. Utapata yale yote unayoniomba kwa kusali rozari
12. Wote wale wanaoeneza rozari hii takatifu nitawasaidia katika mahitaji yao
13. Nimepata toka kwa mwanangu Mtukufu kuwa mawakili wote wa rozari takatifu watapata
waombezi toka baraza lote kuu la Mbinguni wakati wa maisha yao na wakati wa saa yao ya kufa.
waombezi toka baraza lote kuu la Mbinguni wakati wa maisha yao na wakati wa saa yao ya kufa.
14. Wote wanaosali rozari hii takatifu ni wanangu, na kaka na dada wa mwanangu wa pekee YESU KRISTO
15. Ibada kwa rozari takatifu ni ishara kuu ya kuelekea ukombozi
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mungu akubariki!
Imani inaweza kusogeza milima
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Endelea kuwa na imani!
Mwamini Bwana; anajua njia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema zake hudumu milele
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Katika imani, yote yanawezekana
Nakuombea 🙏
Rehema hushinda hukumu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Neema na amani iwe nawe.
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ni mwema, wakati wote!
Dumu katika Bwana.
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Tumaini ni nanga ya roho
Sifa kwa Bwana!
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Baraka kwako na familia yako.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi