Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Mapishi ya Wali Wa Tambi Na Kuku Wa Sosi Ya Mtindi

Vipimo Vya Wali

Mchele – 3 vikombe

Tambi – 2 vikombe

Mafuta – ยผ kikombe

Chumvi

Vipimo Vya Kuku

Kuku kidari (boneless) aliyekatwa katwa vipande – 1 Kilo

Kitunguu maji kilichokatwa katwa – 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa – 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa – 1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Paprika – 1 kijiko cha supu

Masala ya kuku (tanduri au yoyote) – 1 kijiko cha supu

Ndimu – 2 vijiko vya supu

Mtindi (yoghurt) au malai (cream) – 1 kikombe

Mafuta – ยผ kikombe

Majani ya kotmiri (coriander) – ยฝ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali:

Osha Mchele, uroweke.
Tia mafuta katika sufuria, kaanga tambi zilizokatwakatwa hadi zigeuke rangi kuwa nyekundu.
Tia mchele endelea kukaanga kidogo.
Tia maji kiasi cha wali kupikika kama unavyopika pilau. Kiasi cha maji kinategemea aina ya mchele
Funika katika moto mdogo mdogo hadi uive ukiwa tayari.

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku

Katika bakuli, changanya vitu vyote isipokuwa mtindi na kitunguu.
Tia mafuta katika karai, kisha tia kitunguu ukaange muda mdogo tu, usikiache kugeuka rangi.
Tia kuku na masala yake, endelea kukaanga, kisha tia mtindi au malai ufunike apikike na kuiva vizuri.
Nyunyuzia kotmiri iliyokatwakatwa ikiwa tayari kuliwa na wali wa tambi.

Mapishi ya Mlenda wa bamia na nyanya chungu

Mahitaji

Bamia (okra) 20
Nyanya chungu (garden eggs) 5
Magadi soda (Bicabonate soda) 1/4 ya kijiko cha chai
Nyanya (fresh tomato) 1
Chumvi (salt) kidogo
Pilipili 1/4

Matayarisho

Osha bamia, nyanya chungu na nyanya kisha vikatekate katika vipande vidogovidogo. Baada ya hapo vitie kwenye sufuria na vitu vyote vilivyobakia na kisha tia maji kidogo.Chemsha mpaka bamia na nyanya chungu ziive na vimaji vibakie kidogo sana. Baada ya hapo ziponde na mwiko kidogo kisha zikoroge na uipue na mlenda utakuwa tayari kwa kuliwa na ugali.

Cha kufanya msichana akikukimbia halafu atake kukurudia

โ€ฆโ€ฆโ€ฆ Kama msichana atakutupa kwa sababu huna pesa, na baadaye unapopata pesa akarudi tena kuomba msamahaโ€ฆ Ndugu yanguโ€ฆ.. Msameheโ€ฆ. Mpe ahadi ya ndoa, mwambie utamuoaโ€ฆ. iambie familia yake unataka kufanya ukarabati wa nyumba yaoโ€ฆโ€ฆ Ondoa paa lote la nyumba yao halafu TOWEKAโ€ฆ..

๐Ÿ˜‚โ€ฆโ€ฆโ€ฆ ๐Ÿ˜‚โ€ฆโ€ฆ.. ๐Ÿ˜‚

Mapishi ya Samaki wa kuokwa

Mahitaji

Mackerel 2
Kitunguu swaum na tangawizi (ginger and garlic paste) 1 kijiko cha cha kula
Pilipili iliyo katwakatwa (chopped scotch bonnet ) 1/2
Limao (lemon) 1/2
Chumvi (salt) kiasi
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Coriander powder 1/2 kijiko cha chai
Mafuta 1 kijiko cha chai

Matayarisho

Safisha samaki kisha wakaushe maji ( ukipenda unaweza kuwakata kati au ukawapika wazima) Baada ya hapo wakate mistari kila upande ( ili spaces ziweze kuingia ndani) kisha waweke kwenye bakuli na utie spice zote. Wachanganye vizuri kisha waweke frijini na uwaache wamarinate kwa muda wa masaa 3. Baada ya hapo washa oven kisha wapakaze mafuta na uwafunge kwenye foil na uwatie kwenye oven kwa muda wa dakika 20. Baada ya hapo fungua foil na uwaache kwenye oven kwa muda wa dakika 10 ili wapate kukauka kidogo. Na hapo watakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuwala kwa kitu chochote upendacho.

Mafundisho kuhusu Binadamu, Mtu na Utu

Mungu alisema nini alipotaka kumuumba mtu?

Mungu alipotaka kumwumba mtu alisema;
“Tumfanye mtu kwa mfano wetu na kwa sura yetu” (Mwa 1:26-27)


Mtu ni nani?

Mtu ni kiumbe chenye mwili na roho kilichoumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. (Mwa 1:26)


Tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu maana yake ni nini?

Tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu maana yake tuna roho zenye akili na utashi yaani uwezo wa kutofautisha mema namabaya, na zitakazoishi milele.


Watu wa kwanza kuumbwa na Mungu ni akina nani?

Watu wa kwanza kuumbwa na Mungu ni Adamu na Hawa (Eva). (Mwa 1:27)


Mungu alimwumbaje Adamu?

Mungu aliufanya mwili wa Adamu kwa udongo, akaupulizia roho yenye uhai. (Mwa 2:7)


Mungu alimwumbaje Eva (Hawa)?

Mungu alimwumba Eva kwa mfupa wa ubavu kutoka kwa Adamu, akamtia roho. (Mwa 2:21-24)


Kwa nini Mungu alituumba? Kwa nini Mungu aliumba mtu?

Mungu ametuumba tumjue, tumpende, tumtumikie tulipo wazima hapa duniani, hata mwisho tukisha kufa tuende kwake Mbinguni katika katika makao ya raha milele. (Mwa 2:7; Mt. 19:17; Yoh 14:1-3 na Yoh 17:24)


Ni kipi cha kutunza kwa makini zaidi kati ya mwili na roho yako?

Yatupasa kutunza roho zetu zaidi kwni Yesu mwenyewe alisema:
“Itamfaa nini mtu ikiwa ataupata ulimwengu wote na kuupoteza ufalme wa Mungu.” (Mk 8:38)


Mungu aliwapa watu wa kwanza mapaji gani?

Mungu aliwapa watu wa kwanza neema ya utakaso na neema nyingine nyingi, na kukaa paradisini wenye heri bila kufa. (Mwa 28-30; 3:7)


Mungu aliwaamuru nini watu wa kwanza?

Mungu aliwaamuru watu wa kwanza wasile matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya wasije wakafa. (Mw 2:16-17)


Je, Adamu na Eva walimtii Mungu?

Hapana, Adamu na Eva walitenda dhambi ya kutotii, wakataka kuwa kama Mungu lakini bila Mungu na pasipo kufuata maagizo ya Mungu. (Mwa 3:1-16)


Dhambi ya asili ndio nini?

Dhambi ya asili ambayo binadamu wote wanazaliwa nayo, ni hali ya kukosa utakatifu na hali ya asili ya urafiki na Mungu


Adhabu gani walipewa Adamu na Eva?

Adamu na Eva kwa ukubwa wa dhambi yao ya kiburi na ya uasi:
1. Walipoteza neema ya utakaso
2. Walifukuzwa paradisini
3. Walipungukiwa akili na kushikwa na tamaa ya kutenda dhambi
4. Walipitia mahangaiko na taabu nyingi
5. Kupaswa kufa. (Mwa 3:16-20: 5:5)


Kisha kosa la Adamu na Eva Mungu aliahidi nini?

Kisha kosa la Adamu na Eva Mungu aliahidi kuwaletea Mkombozi. (Mwa 3:15)


Alipokwisha umba watu Mungu aliwafundisha nini?

Alipokwisha umba watu Mungu aliwafundisha Dini (Mwa 2:15-17)


Dini ni nini?

Dini ndio mambo yatupasayo kwa Mungu Bwana wetu na Baba yetu. (Mk 16:15-16)


Mungu alinena na nani?

Alinena na;
1. Adamu na Mababu
2. Musa na Manabii
3. Mwishowe Mungu alimleta mwanawe atufumbulie kabisa dini. (Waebr 1:14-45)


Baada ya kifo cha mtu nini hutokea?

Baada ya kifo roho yake inafika mbele ya Mungu kwa hukumu ya mtu binafsi.


Matokeo ya hukumu hiyo ni nini?

Matokeo ya Hukumu hiyo ni roho kwenda Mbinguni, Toharani au Motoni. (Mt 25:34-46)


Ikiwa Mungu anatushughulikia, tunapaswa kufanya nini?

Ikiwa Mungu anatushughulikia, tunapaswa kujiachilia mikononi mwake kwa moyo wa kitoto, tukiwajibika bila ya mahangaiko yanayowapata watu wasiomjua.
โ€œWaangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je, si bora kupita hao?โ€ (Math 6:26).
โ€œNawe una nini usichokipokea?โ€ (1Kor 4:7).
โ€œNimrudishie Bwana nini kwa ukarimu wake wote alionitendea?โ€ (Zab 116:12).


Kwa kuwa tumetoka kwa Mungu na tutarudi kwake, tunapaswa kuishi vipi?

Kwa kuwa tumetoka kwa Mungu na tutarudi kwake, tunapaswa kuishi kulingana na hakika hiyo, kwa kumpa daima nafasi ya kwanza katika mawazo na mapendo yetu, tusijali kiumbe chochote kuliko yeye wala badala yake.
โ€œBwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zoteโ€ (Kumb 6:4-5).
Tusipoitikia upendo wake na kuambatana naye, basi, tumeshindikana kabisa.


Tunaanzaje kumjua Mungu?

Tunaanza kumjua Mungu kwa kuzingatia viumbe vyake, hasa dhamiri yetu.
โ€œKwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wakeโ€ (Rom 1:20).


Je, Mungu amewasiliana nasi?

Ndiyo, Mungu amewasiliana nasi, akijitambulisha na kujitoa kwetu, tuweze kuishi katika urafiki naye na hatimaye tushiriki heri yake.
โ€œNikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizoziratibisha; mtu ni kitu gani hata umkumbuke, na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; umemvika taji ya utukufu na heshimaโ€ (Zab 8:3-5).
โ€œSiwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifuโ€ (Yoh 15:15).


Mungu ametufunulia nini?

Mungu ametufunulia pia ukweli juu yetu wenyewe akijibu kabisa maswali yanayotusumbua kuhusu maana na lengo la maisha yetu.
Amefanya hivyo kwa maneno na matendo yanayoshikamana sana kwa kuwa maneno yanafafanua matendo, nayo matendo yanathibitisha maneno.
โ€œMungu hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweliโ€ (1Tim 2:4).
โ€œMungu si mtu, aseme uongoโ€ (Hes 23:19).
Yeye hadanganyiki wala hadanganyi.


Mungu akiwa wema mkuu na mwenye uwezo wote, mbona katika viumbe vyake kuna ubaya? Kwa nini Mungu anaruhusu mabaya na maovu?

Kwa nini dhambi zipo?

Mungu akiwa wema mkuu na mwenye uwezo wote, hakuumba ubaya wowote. Tena kila anapovumilia ule uliosababishwa na viumbe vyenye hiari anaufanya uzae mema makubwa zaidi kwa njia tusizoweza kuzifahamu vizuri hapa duniani.
โ€œMimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri. Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi zenu, kwa kuniuza huku; maana Mungu alinipeleka mbele yenu kuhifadhi maisha ya watuโ€ฆ Nanyi kweli mlinikusudia mabaya, bali Mungu aliyakusudia kuwa mema, ili itokee kuokoa taifa kubwa, kama ilivyo leoโ€ (Mwa 45:4-5; 50:20).


Viumbe vyenye hiari ni vipi?

Malaika na watu ndio viumbe pekee vyenye hiari ya kuchagua wenyewe wachangie mpango wa Mungu au la.
โ€œNazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi, chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda Bwana, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wakoโ€ (Kumb 30:19-20).


Malaika na watu wanaweza kuchagua hata nini?

Malaika na watu wanaweza kuchagua hata wawe wema au wabaya milele.
โ€œKulikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguniโ€ (Ufu 12:7-8).
Chaguo letu binadamu linafanyika siku kwa siku kwa kuchukua misimamo mizuri au mipotovu kuhusu dini na maadili.
โ€œMwayachunguza Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzimaโ€ (Yoh 5:39-40).


Sisi binadamu tukoje?

Sisi binadamu ni umoja wa mambo mawili: roho iliyoumbwa na Mungu moja kwa moja, na mwili ulioumbwa naye kwa njia ya wazazi.
Maumbile hayo yanatakiwa kukamilika kwa kupokea na kutimiza upendo wa Mungu aliyesema,
โ€œโ€™Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchiโ€™. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumbaโ€ (Mwa 1:26-27).


Je, mwili wetu ni muhimu?

Ndiyo, mwili wetu ni muhimu, kwa sababu umeumbwa na Mungu, umetwaliwa na Mwanae ili atuokoe, umehuishwa na Roho Mtakatifu atakayeutukuza siku ya ufufuo kwa mfano wa Yesu.
โ€œMwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa uweza wake. Je, hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha! Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye?โ€ฆ Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu?โ€ (1Kor 6:13-16,19).


Mungu aliwahi kujifunua kwa watu gani?

Mungu aliwahi kujifunua kwa wazazi wetu wa kwanza, akaendelea hasa kwa taifa la Israeli, hadi alipomtuma Mwanae ajifanye mtu wa taifa hilo teule.
โ€œMungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwanaโ€ (Eb 1:1-2).


Je, Mungu aliumba watu wa kwanza katika hali ya mateso na mauti tuliyonayo sasa?

Hapana, Mungu aliumba watu wa kwanza katika hali ya heri, wakiwa na upendo wake, utakatifu na uadilifu.
Mateso na mauti yametokana na uasi wetu ambao tangu mzazi wetu wa kwanza tunajaribu kuboresha maisha yetu mbali na Mungu.
โ€œMungu hakuifanyiza mauti, wala haimpendezi walio hai wakipoteaโ€ฆ Ila ulimwengu uliingiwa na mauti kwa husuda yake Shetaniโ€ (Hek 1:13; 2:24).
โ€œDhambi iliingia ulimwenguni kwa mtu mmoja, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambiโ€ (Rom 5:12).


Mungu angeweza kuzuia watu wasitende dhambi?

Ndiyo, Mungu angeweza kuzuia watu wasitende dhambi, lakini aliwaacha watende kwa hiari yao awaonyeshe ukuu wa huruma yake.
โ€œMaana Mungu amewafunga wote pamoja katika kuasi ili awarehemu woteโ€ (Rom 11:32).


Je, toka mwanzo sisi watu tunaasi mpango wa Mungu peke yetu?

Hapana, toka mwanzo sisi watu tunaasi mpango wa Mungu kwa kuvutwa na mashetani, yaani malaika waliokataa moja kwa moja kumtumikia; baada ya dhambi ya asili hao wanatutumia sisi pia tuangushane na wenzetu.
Lakini Mungu aliwahi kumuambia Shetani:
โ€œNitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako, na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisiginoโ€ (Mwa 3:15).
โ€œHata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamkeโ€ (Gal 4:4).


Dhambi zimetuathiri vipi tena?

Dhambi zimetuathiri kwa ndani zaidi, zikitutia udhaifu katika mwili, ujinga katika akili na uovu katika utashi; madonda hayo yanatufanya tuzidi kushindwa.
โ€œKwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitiiโ€ (Rom 8:7).


Katika unyonge wetu tutumainie nini?

Katika unyonge wetu tutumainie huruma ya Mungu aliyetutumia Mkombozi hata โ€œdhambi ilipozidi, neema ikawa kubwa zaidiโ€ (Rom 5:20).
Ushindi wake juu ya dhambi umetupatia mema makubwa kuliko tuliyoyapoteza kwa dhambi.
โ€œMungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa ajili ya makosa yetu; alituuhisha pamoja na Kristo; yaani, mmeokolewa kwa neemaโ€ (Ef 2:4-5).


Yesu ni Mungu au mtu?

Yesu ni Mungu na mtu kwa pamoja, ndiyo sababu ni mshenga pekee kati ya Mungu na watu. โ€œKwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, mwanadamu Kristo Yesuโ€ (1Tim 2:5). โ€œKatika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwiliโ€ (Kol 2:9). Hivyo ni Mungu kweli na mtu kweli.

1 Hapo mwanzo, kabla ya kuwapo kitu kingine cho chote, aliku wapo Neno. Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye alikuwa Mungu. 2 Tangu mwanzo Neno amekuwa na Mungu. 3 Vitu vyote viliumbwa na yeye, wala hakuna cho chote kilichoumbwa ambacho hakukiumba. 4 Uzima ulikuwa ndani yake na uzima huo ndio ulikuwa nuru ya watu. 5 Nuru hiyo huangaza gizani na giza haliwezi kamwe kuizima.
6 Mtu mmoja aitwaye Yohana alitumwa na Mungu 7 awaambie watu kuhusu hiyo nuru, ili kwa ushuhuda wake wapate kuamini. 8 Yohana mwenyewe hakuwa ile nuru. Yeye alitumwa kuishuhudia hiyo nuru. 9 Nuru halisi ambayo inawaangazia watu wote ilikuwa inakuja ulim wenguni. 10 Neno alikuwepo ulimwenguni, lakini japokuwa aliumba ulimwengu, watu wa ulimwengu hawakumtambua! 11 Alikuja nyumbani kwake, lakini watu wake hawakumpokea! 12 Bali wote waliompokea na kumwamini aliwapa haki ya kufanywa watoto wa Mungu. 13 Hawa hawakuwa watoto wa Mungu kwa kuzaliwa kwa njia ya asili, wala kwa mapenzi au mipango ya watu bali wamezaliwa na Mungu mwenyewe.
14 Neno akawa mwanadamu akaishi kati yetu akiwa amejaa utu kufu na kweli. Tuliona utukufu wake, utukufu wa Mwana pekee wa Baba. 15 Yohana alishuhudia habari zake, akatangaza: โ€œHuyu ndiye yule niliyewaambia kuwa, โ€˜Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi kwa kuwa alikuwapo kabla sijazaliwa.โ€โ€™ 16 Na kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema tele. 17 Musa alitule tea sheria kutoka kwa Mungu, lakini Yesu Kristo ametuletea neema na kweli. 18 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Lakini Mwanae pekee, ambaye ana uhusiano wa karibu sana na Baba yake, amemdhihirisha Mungu kwetu. Yohana 1:1-6:37


5 Tomaso akamwuliza, โ€œBwana, hatujui unakokwenda; tutaijuaje njia?โ€ 6 Yesu akawaam bia, โ€œMimi ndiye Njia na Kweli na Uzima; mtu hawezi kufika kwa Baba bila kupitia kwangu. 7 Kama mngekuwa mnajua mimi ni nani, mngemfahamu na Baba yangu. Tangu sasa mnamfahamu Baba yangu na mmemwona.โ€
8 Filipo akamwambia Yesu, โ€œBwana, tuonyeshe Baba yako nasi tutaridhika.โ€ 9 Yesu akamjibu, โ€œFilipo, imekuwaje hunifahamu baada ya mimi kuwa pamoja nanyi muda wote huu? Mtu ye yote ambaye ameniona mimi, amemwona Baba. Sasa inakuwaje unasema, โ€˜Tuonyeshe Babaโ€™? 10 Je, huamini ya kuwa mimi niko ndani ya Baba yangu, na Baba yangu yuko ndani yangu? Mambo ninayowaambia siyasemi kwa mamlaka yangu mwenyewe, bali yanatoka kwa Baba yangu ambaye anaishi ndani yangu, na ndiye anayetenda haya yote. Yohane 14:5-10


29 Baba yangu ambaye amenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwatoa hawa kutoka katika mikono yake. 30 Mimi na Baba yangu tu mmoja.โ€
31 Kwa mara nyingine wale Wayahudi wakainua mawe ili wampige nayo. 32 Yesu akawauliza, โ€œNimewaonyesha mambo mengi mazuri kutoka kwa Baba yangu. Kati ya hayo ni lipi linalosababisha mtake kunipiga mawe?โ€ 33 Wao wakamjibu, โ€œTunataka kukupiga mawe si kwa sababu ya mambo mema uliyotenda bali ni kwa kuwa umekufuru. Wewe ni mtu tu lakini unajiita Mungu.โ€ Yohane 10: 29-33


Yesu anapatikana wapi? Yesu anakaa wapi? Yesu Yupo wapi kwa sasa?

Yesu kama Mungu yupo kila mahali, hakuna mahali asipokuwepo. Yesu kama mwanadamu yupo Mbinguni kwa Baba na anakaa nasi duniani katika Maumbo ya Mkate na Divai Katika Ekaristi.


Je, Umungu na utu wa Yesu vinachanganyikana?

Hapana, Umungu na utu wa Yesu vimeunganika katika nafsi moja visichanganyikane, kwa kuwa ndani yake hali hizo mbili zinatenda kila moja ya kwake.
โ€œBasi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, โ€˜Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Munguโ€™โ€ (Mk 15:39).


Je, Mwana wa Mungu tangu atwae mwili ni mtu kamili mwenye akili na utashi wa kibinadamu?

Ndiyo, Mwana wa Mungu tangu atwae mwili ni mtu kamili mwenye akili na utashi wa kibinadamu. Katika umoja wa nafsi yake vipawa hivyo vinatenda kulingana na Umungu anaouchanga na Baba na Roho Mtakatifu milele.
โ€œHayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zakeโ€ (Yoh 14:10).


Kwa nini Yesu alishawishiwa/alijaribiwa na Shetani?

Yesu alishawishiwa na Shetani kwa kuwa ni mtu kweli, akamshinda kwa niaba ya watu wote, akituonyesha namna ya kumtii Mungu moja kwa moja, โ€œhata mauti, naam, mauti ya msalabaโ€ (Fil 2:8).
โ€œKwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye hakiโ€ (Rom 5:19).


Tutakapofariki dunia itatutokea nini?

Tutakapofariki dunia roho yetu isiyokufa, mbali na mwili unaooza, itapewa tuzo au adhabu tuliyostahili kwa maisha yetu. โ€œIkawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwakeโ€ (Lk 16:22-23). โ€œKwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faidaโ€ฆ ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo, maana ni vizuri zaidi sanaโ€ (Fil 1:21,23). โ€œNasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwanaโ€ (2Kor 5:8). Kwa kuwa kifo ni โ€œmavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoaโ€ (Mhu 12:7). Siku ya ufufuo roho na mwili vitaungana tena kwa ajili ya uzima au moto wa milele. โ€œPumzi iliwaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mnoโ€ (Ez 37:10).

Je baada ya kufa ni hapo hapo roho inaenda motoni au mbinguni, Au ni mpaka Siku ya hukumu Yesu Atakaporudi?

Ni siku ile ile Roho ya mtu aliyekufa inaenda Mbinguni, toharani au Motoni. Yesu alimwahidi yule mtu waliyesulubiwa pamoja kuwa watakuwa peponi pamoja siku hiyo hiyo na sio siku ya hukumu.
“Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.” 43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.” (Luka 23:42-43)
Sauli aliweza kuongea na Samweli hata baada ya kufa na Samweli alimbashiria mambo yatakayotokea kwa Sauli maanake ni kwamba Japokuwa alikuwa amekufa bado anayomuungano na Mungu ndio maana aliweza kumwambia Sauli mambo yatakayompata,
“7Basi Sauli akawaambia watumishi wake, โ€œNitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi ili nimwendee nipate kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, โ€œYuko mwanamke mmoja huko Endori.โ€ 8Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, โ€œNibashirie na unipandishie huyo nitakayekutajia,โ€ 9Huyo mwanamke akamwambia, โ€œWewe unajua lile alilofanya mfalme Sauli. Amewakatilia mbali wapunga pepo, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?โ€ 10Sauli akamwapia huyo mwananmke kwa Jina la BWANA, akasema, โ€œKwa hakika kama BWANA aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.โ€ 11Ndipo yule mwanamke akauliza, โ€œJe unataka nikupandishie nani? Sauli akasema, โ€œNipandishie Samweli.โ€ 12Yule mwanamke alipomwona Samweli alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamwuliza Sauli, โ€œMbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.โ€ 13Mfalme akamwambia, โ€œUsiogope. Unaona nini? Yule mwanamke akasema, โ€œNaona Mungu anapanda kutoka ardhini.โ€ 14Sauli akamwuliza, โ€œNi mfano wa nini?โ€ Yule mwanamke akasema, โ€œNi mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.โ€ Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi uso wake hadi ardhini. 15Samweli akamwuliza Sauli, Kwa nini unanitaabisha, kunipandisha juu?โ€ Sauli akasema, โ€œMimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe lakufanya.โ€ 16Samweli akamwuliza, โ€œKwa nini uniulize mimi, maadam BWANA amekuacha na kuwa adui yako? 17BWANA ametenda lile alilotangulia kusema kwa kupitia kwangu. BWANA ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani, Daudi. 18Kwa sababu wewe hukumtii BWANA, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, BWANA amekutendea mambo haya leo. 19Zaidi ya hayo, BWANA atawatia Israeli pamoja na wewe mkononi mwa Wafilisti na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. BWANA pia atalitia jeshi la Israeli mkononi mwa Wafilisti.
Mfano Wa Tajiri Na Maskini Lazaro Yesu alisimulia hivi
19 Akasema, โ€œPalikuwa na tajiri mmoja aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, nguo za gharama kubwa, kila siku. 20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima, alikuwa akiletwa mlangoni kwa huyo tajiri kila siku. 21 Lazaro alikuwa akitamani kula makombo yaliyodondoka mezani kwa tajiri. Hata mbwa walikuwa wakiramba vidonda vyake. 22 โ€œHatimaye, yule maskini alikufa. Malaika wakamchukua akakae pamoja na Ibrahimu mbinguni. Yule tajiri naye pia akafa, akazikwa. 23 Alipokuwa kuzimuni ambapo alikuwa akiteseka, alita zama juu, akamwona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro karibu yake. 24 Akaita, โ€˜Baba Ibrahimu, nionee huruma umtume Lazaro achovye japo ncha ya kidole chake katika maji aupoze ulimi wangu maana ninateseka kwenye moto huu.โ€™ 25 Lakini Ibrahimu akamjibu, โ€˜Mwa nangu, kumbuka kwamba ulipokuwa hai ulipata kila kitu kizuri uli chotaka, ambapo Lazaro alipokea mabaya. Lakini sasa anafarijika hapa na wewe unateseka. 26 Isitoshe, kati yetu na ninyi huko, kumewekwa bonde kubwa lisilopitika ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko au kutoka huko kuja huku wasiweze.โ€™ 27 Akasema, โ€˜Basi, baba, tafadhali umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu, 28 awaonye ndugu zangu, wasije wao pia wakaletwa mahali hapa pa mateso watakapokufa.โ€™ 29 Ibrahimu akamjibu, โ€˜Ndugu zako wanazo sheria za Musa na maandiko ya Manabii. Itawapasa watii hayo.โ€™ Lakini yule tajiri akazidi kumsihi, 30 โ€˜Hapana baba Ibrahimu, ndugu zangu hawatashawishiwa na hayo. Lakini mtu kutoka kuzimu akitumwa kwao watatubu na kuziacha dhambi zao.โ€™ 31 โ€œIbrahimu akamwambia, โ€˜Wasiposikiliza na kutii sheria za Musa na Maandiko ya manabii, hawatashawishika kutubu hata kama mtu akifufuka kutoka kuzimu.โ€โ€™ (Luka 16:19-31)
Wakati Yesu anabadilika Sura walitokea Musa na Eliya.
“Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu. 2 Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang’aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru. 3 Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye. 4 Hapo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya.” (Mathayo 17:1-5)
Yesu alituambia kuwa Mungu sio wa wafu bali wa walio hai ndio maana akaitwa Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo kwa kuwa Wote wako hai kwake.
37Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila keteketea, alipomwita Bwana โ€˜Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki na Mungu wa Yakobo.โ€™ 38Yeye Mungu si Mungu wa wafu bali wa walio hai, kwa kuwa Kwake wote ni hai.โ€ (Luka 20:37-38)
Yesu alimwahidi yule mtu waliyesulubiwa pamoja kuwa watakuwa peponi pamoja siku hiyo hiyo na sio siku ya hukumu.
“Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.” 43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.” (Luka 23:42-43)
Angalia pia wakati Stefano akipigwa Mawe aliikabidhi roho yake kwa Mungu baada ya kuona mbingu zimefunguka hii ni kama Yesu alivyokuwa pale msalabani aliikabidhi Roho yake kwa Baba yake.
55Lakini yeye Stefano akiwa amejazwa Roho Mtakatifu, alikaza macho mbinguni, akaona utukufu wa Mungu, naye Yesu akiwa amesimama mkono wa kuume wa Mungu. 56Akasema, โ€œTazameni! Naona mbingu zimefunguka na Mwana wa Adamu amesimama upande wa kuume wa Mungu.โ€™โ€™ 57Lakini wao wakapiga kelele kwa sauti kubwa, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja. 58Wakamtupa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka nguo zao miguuni mwa kijana mmoja aitwae Sauli. 59Walipokuwa wakimpiga mawe, Stefano aliomba, โ€œBwana Yesu, pokea roho yanguโ€ 60Kisha akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa akasema, โ€œBwana usiwahesabie dhambi hii.โ€™โ€™ Baada ya kusema haya, akalala. (Mdo 7:55-60)
Kwenye Ufunuo tunasoma (Ufunuo 6:9-10) โ€œNa alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi? Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao.โ€
Kwa hiyo mtu akifa anaenda mbinguni au motoni kulingana na alivyoishi.
โ€œNasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwanaโ€ (2Kor 5:8). Kwa kuwa kifo ni โ€œmavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoaโ€ (Mhu 12:7).
Siku ya ufufuo roho na mwili vitaungana tena kwa ajili ya uzima au moto wa milele.
โ€œKwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faidaโ€ฆ ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo, maana ni vizuri zaidi sanaโ€ (Fil 1:21,23).
Mtume Petro ameandika hiviโ€ฆ
“18 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri; 20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji.” (1Petro 3:18-20)


Je, mwili utakaofufuliwa ni huuhuu tulionao sasa?

Ndiyo, mwili utakaofufuliwa ni huuhuu tulionao sasa, lakini katika hali tofauti: > โ€œhupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibikaโ€ (1Kor 15:42).
Siku ya ufufuo โ€œndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingiโ€ (Lk 21:27).
โ€œSaa yaja ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuko wa uzima, na waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumuโ€ (Yoh 5:28-29).
โ€œNa hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa mileleโ€ (Math 25:46).


Haki gani ya Binadamu ni ya msingi kupita zote?

Haki ya binadamu iliyo ya msingi kupita zote ni uhai wake ambao ni lazima uheshimiwe na kulindwa tangu siku ya kutungwa mimba


Hamu kuu ya binadamu ni ipi?

Hamu kuu ya binadamu ni kumwona Mungu

Angalia huyu secretary anavyomjibu bosi wake

Boss mmoja aliingia kazini kwake kasahau kufunga zipu ya suruali yake sasa secretary wake akamfuata na mazungumzo yakawa hivi:

SECRETARY: Boss leo umesahau kufunga geti nyumbani kwakoโ€ฆ

Boss akabaki anashangaaโ€ฆ Baadae wakati anakwenda chooni kujisaidia ile anataka kufungua zipu akaikuta iko wazi ndio akajua alichokuwa ameambiwa na Secretary wake.

Akarudi mpaka kwa secretary na mazungumzo yakaendelea:

BOSS: Bibie ulivyoona geti wazi je uliona benz langu lime paki auโ€ฆ?

SECRETARY: Hapana Boss niliona kitoroli kidogo kimepaki kina matairi mawili

Mambo makubwa yanayosababisha kulazimika kulima au kutifua udongo

Kutifua udongo ni jambo la muhimu sana ili kuufanya udongo kuwa bora.

Umuhimu wa kutifua udongo ni kama ifuatavyo
1. Hulainisha udongo ili kuruhusu mizizi ya mimea kupenya kwa urahisi.
2. Kutifua kunaboresha uwezekano wa kupenya kwa nitrogen na oxygen kutoka kwenye hewa.
3. Kunawawezesha viumbe hai waliopo kwenye udongo kufanya kazi zao ipasavyo.
4. Kunasaidia Kuandaa sehemu ya kuwekea mbegu.
5. Kutifua kunauongeza uwezekano wa maji kupenya kwenye udongo na kupunguza uyeyukaji wa maji.
6. Kuchanganya mabaki ya mimea na samadi kwenye udongo

Siri ya mafanikio katika maisha Ni Kutoangalia Watu

Baada ya kusoma makala kuhusu hofu zinazotugharimu katika safari ya mafanikio, Leo nimekuandalia Makala hii ya Siri ya mafanikio.

Katika safari ya mafanikio, watu wanaweza kuwa kikwazo kikubwa kinachosababisha ugumu wa kuendelea mbele. Wanaweza kuleta upinzani, kukosa imani, au hata kuzua vikwazo visivyo na msingi. Hata hivyo, ni muhimu kuelewa kuwa changamoto hizi zilizoletwa na watu ni sehemu ya mchakato wa kufikia mafanikio. Ingawa inaweza kuwa ngumu kukabiliana na watu wenye upinzani au wasioamini katika safari yetu ya kufikia malengo yetu, tunapaswa kuzingatia kuwa hakuna mafanikio ya kweli ambayo hayakuja na changamoto. Naam, inaweza kuwa rahisi kufanya kazi peke yetu na kuepuka kukabiliana na watu wasioamini au wenye upinzani, lakini hiyo haitatupeleka mbali sana.

Tunahitaji kushughulikia changamoto hizi na kuona jinsi tunaweza kuzishinda. Kukutana na watu ambao hawana imani na malengo yetu inaweza kuwa kama mtihani mkubwa kwetu. Wanaweza kutushawishi kuacha au kuanza kutilia shaka uwezo wetu. Lakini ni muhimu kukumbuka kuwa imani yetu ndio itakayotuendesha mbele. Tunapaswa kujikumbusha kuwa mafanikio hayangeweza kupatikana ikiwa tungekuwa na imani ndogo ndani yetu wenyewe. Mbali na hilo, tunapaswa pia kutambua kuwa vikwazo visivyo na msingi vinaweza kuwepo katika safari yetu ya mafanikio. Watu wanaweza kuzua vikwazo hivi kwa sababu ya wivu, woga, au tu kutokuelewa malengo yetu. Ni muhimu kutambua kuwa hatuwezi kudhibiti tabia au mitazamo ya watu wengine, lakini tunaweza kujifunza kuweka mipaka na kuendelea kufuata malengo yetu licha ya vikwazo hivyo. Katika safari yetu ya mafanikio, tunapaswa kuwa na uvumilivu na subira.

Tunapaswa kutambua kuwa kila changamoto tunayokutana nayo inatupa fursa ya kukua na kujifunza. Tunapaswa kutumia changamoto hizi kama nguvu ya kuendelea mbele badala ya kutuacha tukata tamaa. Kwa kumalizia, ingawa watu wanaweza kuwa kikwazo katika safari yetu ya mafanikio, tunapaswa kuona changamoto hizi kama sehemu ya mchakato wa kufikia malengo yetu. Tunapaswa kuwa na imani thabiti ndani yetu wenyewe, kuweka mipaka na kuendelea kusonga mbele licha ya vikwazo vinavyoweza kuzuka. Kwa kufanya hivyo, tutapata mafanikio kamili na kuwa bora zaidi katika safari yetu ya kuelekea mafanikio.

Wakati mwingine, tunaweza kukutana na watu ambao hawana imani na uwezo wetu au wanajaribu kutuweka chini kwa sababu ya wivu au tamaa. Ni muhimu kujifunza kuweka mipaka na kuendelea kusonga mbele, kujiamini katika uwezo wetu na kuendelea kufanya kazi kwa bidii kuelekea malengo yetu.

Watu wanaweza pia kuwa vikwazo kwa kuwa na maoni tofauti au kutokuwa na uelewa kamili wa malengo yetu. Katika hali hizi, ni muhimu kuwa na uvumilivu na kuwasiliana kwa wazi ili kuelezea malengo yetu na kutafuta njia za kuwashawishi au kuwashirikisha katika safari yetu ya mafanikio.

Hakikisha pia kuwa unazungukwa na watu wenye mawazo chanya ambao wanakuunga mkono na kukusaidia kufikia malengo yako. Kuwa na timu ambayo inakusaidia na kukutia moyo ni muhimu sana katika safari ya mafanikio.

Kwa hiyo, tunapokabiliana na vikwazo kutoka kwa watu katika safari yetu ya mafanikio, ni muhimu kujifunza kutokana na hilo, kuweka mipaka, kuwasiliana kwa wazi, na kuwa na timu yenye msaada karibu nasi. Hatimaye, tunapaswa kuendelea kuamini katika uwezo wetu wenyewe na kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yetu.

Waziri mkuu wa zamani wa uingereza Sir Wiston Churchill aliwahi kusema;

“huwezi kufika mwisho wa safari yako kama utakuwa unasimama kila mahali kumtupia jiwe kila mbwa anaye kubwekea”

Sir Wiston Churchill

Kauli hii ina maana kwamba kama una picha kichwani ya kule unakokwenda au umekusudia kufikia na kutimiza lengo fulani katika maisha hupaswi kusikiliza, kupambana au kushindana nakila mtu.

Unapokuwa njiani kutimiza lengo lako lazima utakutana na watu wa aina hizi;

  1. Watakaokurudisha nyuma kwa kukuharibia mipango na juhudi zako
  2. Watakaokuvunja moyo na kukukatisha tamaa
  3. Watakaokusema vibaya hata kwa mazuri yako na kukuzushia uongo
  4. Watakaokuchukia kwa sababu ya bidii yako

Unaweza kushawishika kutaka kumjibu kila mtu anayekusema vibaya, kukuchukia au kukukatisha tamaa (hapo ndo unakuwa sawa na yule anayesimama kumtupia jiwe kila mbwa anayebweka).

Unaweza ashawishika kutaka kuona kila mtu anakukubali na kukuunga mkono, kitu ambacho hakiwezekani.
Kuna Msemo usemao “siri kubwa ya kufeli katika maisha ni kujaribu kumpendeza kila mtu”.

Hapa duniani huwezi kumpendeza kila mtu hata ufanye jambo zuri kiasi gani “hata ukichezea maji utaambiwa unatimua vumbi”. Mara nyingi tunajitahidi kufanya mambo mema na kuwa na nia njema, lakini bado kuna watu ambao hawatafurahia jitihada zetu na watatupinga tu. Hii inaweza kuwa changamoto kubwa kwetu kihisia na kijamii, kwani tunatamani kukubalika na kupendwa na kila mtu.

Lakini kumbuka, haifai kuchukulia kila upinzani kibinafsi au kuathiri thamani yako. Watu wana mitazamo tofauti na uzoefu wao binafsi, na huenda hawana ufahamu kamili wa hali yako au malengo yako. Badala yake, ni muhimu kuwa na imani katika nia zako na kuendelea kufanya mambo mema bila kujali jinsi watu wengine watakavyokuona au kukupinga.

Njia bora ya kushughulikia upinzani ni kujielewa na kuweka mipaka. Jifunze kuamini kwamba wewe ni wa thamani na una uwezo mkubwa wa kuathiri mazingira yako. Wacha maadili yako yaongoze vitendo vyako na usiruhusu maneno au maoni ya wengine kukufanya ujisikie vibaya au kupoteza lengo lako.

Kumbuka pia kuwa hakuna mtu aliyeweza kufanya kila mtu awe radhi. Hata watu mashuhuri na viongozi wa kiroho hawakuepuka upinzani. Kina Mandela, Mahatma Gandhi, au Martin Luther King Jr., walikabiliana na upinzani mkubwa, lakini waliendelea kusimama imara kwa imani zao na kufanikisha mabadiliko makubwa.

Ili kufanya mabadiliko katika jamii au ulimwengu, ni muhimu kuwa tayari kukabiliana na upinzani. Upinzani unaweza kukusaidia kukua kibinafsi na kitaaluma, kurekebisha njia zako, na kukuza uvumilivu wako. Ni nafasi ya kujifunza na kujenga hoja zako kwa msingi thabiti.

Hivyo, jinsi unavyokabili upinzani ina athari kubwa kwa maendeleo yako na mtazamo wako kwa maisha. Usikate tamaa na usiruhusu upinzani ukuzuie kufuata ndoto zako na kufanya mambo makubwa. Jiamini, thamini uwezo wako, na endelea kusonga mbele bila kujali kile ambacho wengine wanaweza kusema au kufikiria. Hakuna kitu kikubwa kilichofanyika bila ya upinzani, kwa hiyo endelea na safari yako na uhakikishe kuwa unaamini kwamba una nguvu ya kufanya tofauti.

Wewe fwatilia Mipango yako huku ukitazame hatima yako. Soma hapa mbinu hizi za kukunufaisha maishani.

Lakini haimaanishi uwachukie watu na kuwatendea mabaya ili ufanikiwe mwenyewe. Chuki na Mapambano hayanufaishi bali yanakufanya kuwa dhaifu.

Vivyo hivyo, Sio watu wote ni kikwazo. Kuna watu wa aina nyingine ambao wanaweza kukusaidia kufanikiwa. Unapaswa kuwa makini na kutumia Busara yako kuweza kuwatambua watu unaokuwa nao katika safari ya Mafanikio.

Umasikini isiwe sababu wala utajiri isiwe sababu ya kuwa mchafu au kutokuwa na usafi

Katika maisha, umasikini siyo sababu ya mtu kuwa mchafu au kutokuwa na usafi. Hali ya umasikini inaweza kuathiri uwezo wa mtu kumudu bidhaa za usafi au kuishi katika mazingira safi, lakini hii haimaanishi kuwa mtu mwenye utajiri automatically ni mtu mwenye usafi.

Kinyume chake, utajiri haujazi hakika mtu kuwa na kila kitu ambacho hahitaji. Utajiri ni kuwa na uwezo wa kununua au kumiliki vitu vingi, lakini ukweli ni kwamba tunahitaji tu vitu vichache sana katika maisha yetu. Tunapojikuta tukiwa na wingi wa vitu visivyotumiwa, tunaweza kujikuta tukichafua mazingira yetu na kutopenda kila kitu tunachomiliki.

Sasa angalia nyumbani kwako! Je, kuna vitu ambavyo haujahitaji kwa muda mrefu au vinachafua tu nafasi yako? Kufanya maamuzi ya busara na kujiondoa na vitu visivyohitajika, vitakuwezesha kuishi katika mazingira safi na yenye upangaji mzuri. Usafi sio lazima uendane na utajiri, bali ni suala la utaratibu na umakini katika kusimamia mazingira yetu.

Umasikini sio sababu ya kuwa mchafu wala utajiri Sio kuwa na kila kitu hata kama hukihitaji. Hebu angalia hapo nyumbani kwako!

Vitu msivyovihitaji Leo wala kesho mmeweka vya nini? Umenunua makochi mapya Yale ya zamani mmegawana vyumbani mnaishia kurundika minguo hapo na kufuga mipanya.

Godoro umenunua jipya la zamani umeviringisha juu ya kabati. Kabatini kwako kuna nguo ulivaa ukiwa secondary mpaka Leo unazo eti ukumbusho au utazivaa ukipungua.

Jikoni ndo shida iliposhika hatamu! Mivyombo ya plastiki imepaukiana imeyayuka na moto ipo tu eti vyombo vya watoto. Mahotpot yamekata roho imebaki kuwa sufuria we unalo tuu. Mxiuuu

Ndoo hata hazitumiki zipozipo tu, hata maua hazifai kupandia we unazogo tu huchomi, hutupi wala huzihitaji.. Sa zanini hapo?? ๐Ÿ˜ก๐Ÿ˜ก

Vyombo vya udongo vina mapengo na magego kama vinang’atwaga au vinapiganaga vyenyewe. ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚. Isitoshe kila kimoja na dizaini yake havifanani coz seti imeshavunjikavunjika hivo ndo vimebaki. Unaboaโ€ฆ ๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜

Dressing table imejaa mikopo na mibox haina Kazi, perfume ya mwaka 2000 unayo hapo kisa ukumbusho wa zawadi. Ushamba huoooโ€ฆ ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ

Stoo yako mwenyewe ila unaiogopa kuingia coz imejaa vitu visivyohitajika imekuwa ghetto la panya na nyoka kama sio nge badala Ukiweka mnavyohitaji. Ipo siku mtakuta mamba humo.. ๐Ÿฒ๐Ÿฒ๐Ÿฒ

Nje ya nyumba kuna gari la urithi la babu lipogo tu hapo linafuga ndege na vibakaโ€ฆ Aaalaaaa ๐Ÿ˜ก๐Ÿ˜ก๐Ÿ˜ก

Kutupa vitu visivyohitajika hamtupi eti Dhambi na kugawa hamgawi coz mmeviharibu hadi mwisho mtampa nani? Kutwa mnapishana mahospitalini mnaumwa mafua na vifua kila siku.

Kwann msiumwe na mnakaa dampo ? Hivi mnajua km huu ni ugonjwa? Unaitwa hoarder disorder. Tena mnawaambukiza watoto wenu kwani wanajua kwao hata kikopo cha icecream hakitupwagi kinaoshwa kinawekwa hapo.

Halafu bado unaendelea kumuomba Mungu akupe, akupe uweke wapi na kwako pameshajaa?

Kwa kweli, mtazamo wa kuridhika na hali ilivyo sio tu hatari kwa maendeleo binafsi, lakini pia kwa jamii kwa ujumla. Mazingira tunayoishi yanahitaji uangalizi na uhusiano wa moja kwa moja na afya zetu, usalama, na hata uchumi wetu. Kama ilivyosemwa awali, kila mmoja wetu โ€“ bila kujali hadhi yetu kifedha โ€“ ana wajibu wa kuchukua hatua za makusudi katika kudumisha usafi wa mazingira yetu.

Tunapaswa kuzingatia kuwa usafi na umakini wa mazingira yanatuhusu sote na yana faida zinazoonekana na zisizoonekana. Uchafuzi wa mazingira, kwa mfano, unaweza kuathiri ubora wa hewa tunayopumua na maji tunayotumia, na hivyo kusababisha matatizo ya kiafya. Kwa upande mwingine, mazingira safi na yenye kuendelezwa vizuri yana uwezo wa kuongeza thamani za mali, kuboresha uzuri wa jamii, na kuvutia uwekezaji na utalii ambao unaweza kukuza uchumi wa eneo husika.

Kila mtu anapaswa kuchukua hatua, iwe ni katika kutupa takataka mahali pake, kushiriki katika shughuli za kusafisha mazingira, kupanda miti, au kufunza wengine umuhimu wa uhifadhi wa mazingira. Serikali na asasi zisizo za kiserikali zinaweza kusaidia kwa kutoa elimu, rasilimali na sera zinazosaidia usafi na utunzaji wa mazingira.

Ni muhimu kutambua kwamba uamuzi wa kutunza mazingira unapaswa kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku na sio tu wakati wa maadhimisho au mikakati ya muda mfupi. Uendelezaji wa mazingira safi na salama ni jukumu letu la kudumu, linalohitaji kujitolea na ushirikiano kutoka kwa watu wote katika jamii.

Mambo madogo hayapaswi kupuuzwa โ€“ matumizi ya mifuko inayoweza kutumika tena badala ya plastiki zinazotupa sana, kutumia njia mbadala za nishati zinazoweza kujazwa upya ili kupunguza uchafu, na hata kusimamia taka za kielektroniki โ€“ yote haya ni sehemu muhimu ya kujenga mazingira endelevu. Hivyo basi, hebu tuchukue hatua, kila mmoja wetu, kwa mustakabali mzuri zaidi. Tunalo jukumu hilo, kwa ajili ya kizazi chetu na vizazi vijavyo.

Huyu mchaga kazidi sasa, angalia anavyomfanya huyu mbuzi

Mchaga alinunua mbuzi akamwambia mpishi Nyama nusu ipike pilau na ingine itie kwenye friza. Kichwa fanya supu, miguu fanya mchuzi chukuchuku. Ngozi usitupe tutafanya mswala, utumbo pikia ndizi na mifupa tutawauzia wenye mbwa. Kinyesi kihifadhi kwa mbolea ya bustani.

Mpishi akamuuliza Hutaki na sauti ya mbuzi tufanye ring tone kwenye simu yako? Mchaga akajibu Yesuu! hivi inawezekana? bac fanya hivyo tuwauzie na wengine hiyo ringtone. Chezeya mchaga!

JITAMBUE: Kipi hauna kati ya pesa na muda?

Soma kidogo hapa.. Kuna watu wa aina NNE tunapoongelea pesa na muda.

1. WANA MUDA MWINGI ILA HAWANA PESA

Watu ambao hawana pesa ila wana muda wa bwerere. Hawajui thamani ya muda. Hawa ndo wale ambao hawajui cha kufanya. Anaamka mpaka analala usiku hana specific timetable. Unaweza kumkuta anaenda dukani ukamwambia nisindikize saluni na akakubali. Yupo yupo tu. Unaweza kuta ameingia Facebook hajui hata kwa mini. Basi tu kwa sababu ana bando. Akiperuzi akaona mahali wanaongelea mpira yumo. Akiscroll post za chini akakuta kuna mtu kapost kuhusu UKAWA yumo. Akikuta kuna mtu kapost mtu ana uvimbe mkuuubwa watu wameambiwa wacomment AMEN na yeye huyo anacomment AMEN. Akikuta watu wanaongelea TRUMP na yeye anaingia kucomment. Kundi hili ni kundi lenye watu wengi mno. Watu wa aina hii kufanikiwa ni bahati nasibu. Labda kwa bahati tu akutane na post nzuri kama hii na post zingine nzuri huenda ikamsaidia. Otherwise hawa ndo hawaelewi maisha yanaenda wapi maana hawana kitu fulani specific wanachofanya. Wakisikia tu kuna kitu kiko kama dili hivi wanaenda. Wakikuta kumbe kinahitaji bidii na kujituma wanaondoka. Wanataka maisha mazuri yaje tu yenyewe.

2. WANA PESA ILA HAWANA MUDA

Hili ni kundi la watu wenye shughuli fulani ya kiuchumi. Labda ameajiriwa au amejiajiri. Wako busy kweli kweli. Na ukweli pesa inaonekana. Hawa huwezi kumwambia njoo tuonane akaja hapo hapo. Huyu lazima apange kwanza ratiba zake. Maana yupo busy. Au lazima aombe ruhusa kazini maana hana uhuru na muda wake. Muda wake kamuuzia mtu (mwajiri). Au labda atoroke ndo anaweza kupata muda wa kufanya mambo yake binafsi. Au asubiri weekend ambapo kila ratiba itategemea siku hizo mbili, kama ni ibada, usafi, kutembelea wagonjwa au ndugu kwenda mahali kuona labda kiwanja kinauzwa au kuona ujenzi au mradi wake unaendeleaje nk. Mara nyingi watu wa kundi hili hushindwa kufanya vitu vingi vinavyohusu maendeleo yako binafsi mfano kujisomea, kuhudhuria semina zinazofundisha mambo yanayoweza kuwa na manufaa kwake nk. Sababu ana ratiba iliyobana. Ukiwa na sherehe ukamwomba mchango hashindwi kukuchangia angalau chochote kile lakini muda wa kuja kujumuika na wewe ni vigumu akaupata.
Hili ni kundi ambalo kuna watu wanaitwa MIDDLE CLASS people. Watu wa maisha ya kati. Mambo yako si mabaya sana lakini si kwamba ni mazuri. Wasomi wengi na watafutaji wengi wapo hapa. Afu ndo wanahisi wanajua kila kitu. Na wengi wao huishia kupata changamoto za kifedha na kiafya ukubwani au uzeeni kama stress na maradhi mbali mbali nk. Sababu ya kutokuwa na muda hata wa kuangalia wa kuinvest na kujifunza biashara au ujasiriamali mapema wala kujishughulisha na afya zao, mazoezi, kupumzika vizuri nk kwa kuwa walikuwa busy siku zote. Maisha ya watu hawa middle class mwishoni huja kuwa magumu kwa kuwa hata kuwa na muda na majirani tu ilikuwa ishu. Kwa kuwa wengi wana magari (mengi ni mkopo. Wengine gari la kazini) na kwa kuwa wanaweza kulipa kodi ya nyumba au hata kupata kakiwanja na kuanza kujenga huko Malamba Mawili basi wanaridhika. Hawawezi kuota kumiliki nyumba Masaki au kununua kiwanja Upanga. Kama upo kundi hili lazima uanze kutafuta mbinu mbali mbali za kuyakabili maisha vizuri siku za usoni. Waangalie wastaafu ambao walikuwa busy zamani. Saivi utasikia mgongo, miguu, macho nk vinasumbua. Hawa middle class people ndo ukimkuta social media wengi wao wako critical kwa kila kitu. Maana haoni kama ana shida yoyote.

3. HAWANA MUDA WALA HAWANA PESA

Ulishasikia mtu anaambiwa “busy for nothing”? Ni kitu kama hicho. Yani mtu unakuta labda ni kibarua tu mahali anatumwa kazi asubuhi mpaka jioni. Labda ameajiriwa kazi ya ulinzi, au gereji, au kwenye mradi wa ujenzi anabeba zege au kupaka rangi. Hashindi njaa ni kweli lakini ukweli hana hela. Wala hatamani kuendelea kuwa hivyo. Kuamka alfajiri kulala saa tano usiku. Hela anayopata inatosha kula kwa mama ntilie tu na nauli. Basi. Hawezi kuota hata gari. Hata ya mkopo. Maana hata hakopesheki. Huyu hata muda wa Facebook ni nadra akiingia ni kupitisha macho afu anatoka. Au hata simu ya Facebook hana.

4. WANA MUDA NA WANA PESA

Hapa ndo utakuta wale ambao hana tena shida ya pesa. Pesa iko. Hana tena shida ya muda. Akihitaji kwenda mahali haombi ruhusa wala kuaga mtu labda kumuaga mwenza wake tu. Anaweza kusikia kuna shamba linauzwa mahali na hahitaji kutafuta hela tena ili akalinunue bali anaanza michakato ya kisheria pale pale kununua kama amelipenda. Kuna siku nilienda Morocco Square hapo Kinondoni jirani na Airtel kuna Apartments zinajengwa nikaonana na watu wa NHC waliokuwa wanakagua ujenzi unaendeleaje. Nikawauliza hizo apartments zinauzwaje wakasema kuna za milioni 600 na za milioni 800. Na unatakiwa kulipa cash 10% (yaani aidha milioni 60 au 80 cash) halafu inayobakia unaweza kuimalizia ndani ya miezi 12. Na kuna watanzania kadhaa wamenunua tena kwa hela halali. Hawa wako kundi hili hapa. Hela ipo. Muda upo. Kuna watu walienda kutembea Marekani kibiashara walipokuwa njiani kurudi wakapita mahalinchi nyingine wakakuta kuna mnada wa nyumba kwenye nchi hiyo. Hawakujiuliza mara mbili wakanunua. Kuna wazee fulani wana mtoto wao alikuwa akisoma Canada. Alipograduate wakamuuliza unataka kuishi wapi akasema huku huku Canada wakamnunulia nyumba Canada. Ukisikia hivyo unaanza kuwaza ni mafisadi. Mawazo yako ninkuwa bila ufisadi watu hawanunui nyumba Canada. Kwa taarifa yako Hawa siyo waajiriwa serikalini wala popote ni wafanya biashara.. Kundi la watu kwenye pesa. Na muda. Wanaweza kuamua kesho wakaenda kutembea visiwa vya Comoros. Watu wanaoishi kundi hili wana discipline kubwa ya maisha. Na watu wengi wanatamani kufika kundi hili. Lakini HAWANA discipline ya kujifunza tabia zinazoweza kukufikisha huko.

Swali muhimu tu la kujiuliza tu ni kuwa je, wewe upo kundi lipi.

Una muda mwingi lakini huna hela? = FUKARA

Una hela nyingi lakini huna muda? = MIDDLE CLASS

Huna muda wala huna hela.. Vijisenti unavyopata vinaishia nauli kula kodi ya nyumba nk? = MASKINI

Au una muda mwingi na hela siyo shida tena? = TAJIRI

Utani wa wahindi, cheka kidogo

Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili

(1) Mfa maji ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?โ€ฆโ€ฆ. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?โ€ฆโ€ฆ.. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?โ€ฆโ€ฆ Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ Takosa guo ya sikukuuโ€ฆ
(10) Kila ndege ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. โ€ฆHutua Airport
(11) Bandu bandu ?โ€ฆ.. โ€ฆโ€ฆ.Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?โ€ฆ Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?โ€ฆ.Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?โ€ฆโ€ฆ.. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?โ€ฆ. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? โ€ฆโ€ฆ.. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?โ€ฆโ€ฆ.. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?โ€ฆ.Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?โ€ฆโ€ฆ.. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? โ€ฆโ€ฆโ€ฆ.Taenda Chadema
(23) Bendera ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?โ€ฆโ€ฆ. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? โ€ฆโ€ฆ.. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.

Tafakari Upendo Mkuu wa Mungu kwa Mwanadamu

Utangulizi

Mungu alimpenda sana binadamu hata akauvaa Mwili wa Binadamu akashuka duniani na kuishi kama Binadamu ili amkomboe Mwanadamu na hata akaamua kufa kwa ajili ya Binadamu kwa malipizi ya dhambi za Binadamu na kwa maondoleo ya dhambi.

Je, ni Kitu gani ambacho Mungu angemfanyia mtu ambacho hajakifanya?

Kweli nakwambia hata kama Yesu angebaki duniani na kuwa hai mpaka leo bado watu wasinge mwamini na wapo ambao wangemchukia na kumfanya adui yao hata kumuwinda.

Ni watu wachache sana duniani wanaouona upendo huu mkuu wa Mungu, wengi hawaoni wala hawataki kuona. Wapo hata wacha Mungu lakini hawaelewi upendo huu.

Upendo Mkuu wa Mungu kwa Mwanadamu: Kwa Nini Yesu Alikuja Duniani?

Mungu alimpenda sana binadamu hata akaamua kuuvaa mwili wa binadamu na kushuka duniani ili amkomboe mwanadamu. Alishuka na kuishi kama binadamu, akakubali kuteseka na kufa kwa ajili ya malipizi ya dhambi za wanadamu. Huu ni upendo mkuu ambao Mungu ametufanyia, na ni muhimu kuelewa kwa kina ukubwa wa tendo hili la ajabu.

Mungu Alishuka na Kuishi Kama Binadamu

Mungu, kwa upendo wake usio na kifani, aliona mateso na maumivu ya wanadamu na akaamua kushuka duniani kama binadamu kupitia Yesu Kristo. Aliacha utukufu wake wa mbinguni na kuja kuishi kati yetu. Yohana 1:14 inasema:

“Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.” (Yohana 1:14)

Yesu alikuja na kuishi kama binadamu, akakutana na changamoto zote tunazokutana nazo, ili aweze kutuelewa na kutukomboa kikamilifu.

Alikufa kwa Ajili ya Dhambi Zetu

Upendo wa Mungu ulionyeshwa kwa namna ya ajabu pale Yesu alipokubali kuteseka na kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu. Alibeba mzigo wa dhambi za ulimwengu mzima na kutoa maisha yake kama sadaka takatifu. Warumi 5:8 inasema:

“Lakini Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.” (Warumi 5:8)

Yesu hakufa kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wenye dhambi, ili kutupa nafasi ya kupokea msamaha na uzima wa milele.

Je, Ni Kitu Gani Ambacho Mungu Angemfanyia Mtu Ambacho Hajakifanya?

Mungu ametufanyia kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya wokovu wetu. Alitoa mwanawe wa pekee, Yesu Kristo, ili afe kwa ajili yetu na kutuondolea dhambi zetu. Ni nini zaidi tunachoweza kumwomba Mungu ambacho hajakifanya? Hakuna upendo mkuu zaidi ya huu ambao Mungu ametufanyia. Kama ilivyoandikwa katika Yohana 15:13:

“Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.” (Yohana 15:13)

Yesu Angekuwa Hai Mpaka Leo, Bado Watu Wasingemwamini

Hata kama Yesu angeendelea kuishi duniani mpaka leo, bado kungekuwa na watu wasiomwamini na kumchukia. Hii ni kwa sababu mioyo ya watu wengi imejaa ugumu na kutokuamini. Yesu mwenyewe alisema katika Yohana 15:18:

“Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni ya kwamba ulinichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.” (Yohana 15:18)

Hii inaonyesha kwamba kuna watu ambao hata wakiweka wazi upendo wa Mungu, bado watakataa na kumwona Yesu kama adui.

Wengi Hawaoni Upendo Huu Mkuu wa Mungu

Ni watu wachache sana wanaoona na kuthamini upendo huu mkuu wa Mungu. Wengi hawaoni wala hawataki kuona. Wengine ni wacha Mungu lakini hawaelewi kabisa kina cha upendo huu. Hata hivyo, wale wanaoona upendo huu na kuukubali wanapata uzima wa milele na uhusiano wa karibu na Mungu. Yesu alisema katika Yohana 3:16:

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16)

Hitimisho

Upendo wa Mungu kwa mwanadamu ni mkubwa sana na umedhihirishwa kwa Yesu Kristo kushuka duniani, kuishi kama binadamu na kufa kwa ajili ya dhambi zetu. Mungu ametufanyia kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya wokovu wetu. Ni jukumu letu kutambua na kuthamini upendo huu, na kuishi maisha yanayodhihirisha imani na shukrani zetu kwake. Tunapoona upendo huu wa ajabu, mioyo yetu inapaswa kujazwa na furaha na amani, tukijua kwamba Mungu ametupenda sana na anataka tuwe na uzima wa milele.

Cheki huyu jamaa anavyoungama kwa padri sasa

JAMAA: Baba Padri nimekuja kuungama
PADRI: Haya
JAMAA: Niliiba kamba
PADRI: Kamba?
JAMAA: Ndio, kamba lakini kule mwisho kulikuwa kumefungwa ng’ombe
PADRI: Kwa hiyo uliiba ng’ombe?
JAMAA: Kiukweli nilikuwa nina lengo la kuiba kamba, kwa bahati mbaya mwisho kulikuwa na ng’ombe
PADRI: Mi naona mueleze Mungu direct, mi sikuelewi kabisaaa

๐Ÿ™ˆ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜‚๐Ÿ™Š

Kilichotokea kwa binti na mvulana wake walipotaitishwa na baba yake msichana

Msichana alikuwa amekaa na baba yake kibarazani, mara akamuona MVULANAfriend wake akija, yule mvulana alipokaribia tu, yule msichana akamwambaia:

MSICHANA: Umekuja kuchukua kile kitabu chako, kinachoitwa “DADDY IS AT HOME?” by Ngozi Okafor
MVULANA: Hapana!, Nimekuja kuazima kitabu cha Maombi kama kinaitwa “WHERE SHOULD I WAIT FOR YOU?” by Ngลฉgฤฉ wa Thiong’o
MSICHANA: Aaah! Icho sina ila ninacho kimoja kinaitwa “UNDER THE MANGO TREE” by Chimamanda Adichie
MVULANA: Ooh! Vizuri, Basi usisahau kuja nacho kesho kitabu cha Okot p’Bitek kile kinachoitwa “CALL ME IN 5 MINUTES BEFORE” Utakapokuja shule.
MSICHANA: Usijali, tena nina kitabu kipya kinaitwa “I WON’T LET YOU DOWN” by Chinua Achebe
Baba mtu akawatazamaaaa kisha akasema
BABA: Vitabu vyote hivyo, mbona vingi sana, atavisoma vyote kweli
MSICHANA: Ndio Daddy, huyu mvulana hupo smart sana na ana akili atavisoma vyote hivyo!
BABA: Sawa! Usisahau kumpatie na kile ambacho nimekiweka pale juu ya meza, kinaitwa “I AM NOT STUPID, I UNDERSTOOD EVERYTHING YOU’VE BEEN SAYING” by Shakespeare!
Na kuna kingine nimekiweka juu ya kabati la vyombo, kinaitwa “IF YOU GOT PREGNANT PREPARE TO GET MARRIED”

Kwa nini tarehe ya Pasaka hubadilika

KALENDA za mwanzo ziliutumia mwezi wa
angani kama kipimo cha muda. Ziliitwa
โ€œLunar calenderโ€ au Kalenda-Mwezi. Tarehe 1
ya Mwezi ilikuwa ni siku ulipoandama yaani
Mwezi-Mdogo (Crescent Moon).
Mwezi unapofika siku ya 15 unakuwa
umefikia ukubwa wa juu na huitwa Mwezi-
Mkubwa (Full Moon). Hivyo kwa kalenda ile
tarehe 15 ilikuwa ni siku ya Mwezi-Mkubwa.
Mwaka 45KK, Julius Caesar alitangaza
kalenda mpya ikaitwa โ€œJulian Calenderโ€ iwe
na siku 365. Wakati huo ikijulikana kwamba
jua huzunguka kwa siku 365.25. Hivyo pengo
la kalenda na mzunguko likabaki robo siku.

Robo hiyo ifidiwe kila baada ya miaka minne
mwishoni mwa mwezi Februari ambayo sasa
ulifanywa kuwa wa pili baada ya January.
Inapofanyika hivyo, huo ukaitwa mwaka-
mrefu (Leap year).
Mwaka mrefu ukachaguliwa kuwa ni ule tu
unaogawanywa kwa nne mfano miaka
ifuatayo 1700, 1800, 1900, 2100, 2200, 2300.
Baadaye iligundulika kuwa jua huzunguka
kwa siku 365.24218967 ziitwazo โ€œTropical
yearโ€. Hizi ni chache kuliko siku 365.25
zilizokadiriwa mwanzoni. Uchache huu
husababisha kuwe na pengo la dakika 11 na
sekunde 14.812512 kwa mwaka.
Pengo hili ni dogo, lakini hupanuka hadi kuwa
siku nzima kila baada ya miaka 128.0355.
Mwaka 1545 lilivuka siku 9.25.
Kuondoa tatizo hili, Papa Gregory XIII
aliamuru iundwe kalenda mpya na akachagua
Oktoba 04, 1582 iwe siku ya mwisho
kutumika โ€œJulian Calenderโ€. Kesho yake,
kalenda mpya ikaanza kutumika.
Ungetegemea hiyo kesho iwe ni Oktoba 05,
1582. Lakini ili uzibe pengo lile lililofikia siku
kumi, ilibidi kalenda mpya kuziruka siku hizo
siku kumi. Hivyo hii mpya iliyoitwa
โ€œGregorean Calenderโ€ ikaanza kama Oktoba
15 badala ya Oktoba 05.
Ndiyo sababu katika historia ya nchi nyingi
Ulaya, hakuna tarehe za Oktoba 05, 1582
hadi Oktoba 14, 1582. Watu walilala Oktoba
04, 1582 kesho yake wakaamka ikiwa ni
Oktoba 15, 1582.
Teresa Alonso huandikwa kwamba alifariki
Oktoba 1582, kwenye usiku wa tarehe NNE
kuamkia tarehe KUMI NA TANO!
Alipotangazwa kuwa Mtakatifu, Kanisa
Katoliki likaifanya Oktoba 15 kuwa siku ya
kumkumbuka, yaani siku ya Mtakatifu Teresa
wa Avila.
Usipofahamu kwamba Mtakatifu Teresa
alifariki siku kalenda zinabadilishwa, utadhani
aliyeandika vile tarehe za kifo chake
amekosea!
Waandishi, William Shakespeare wa
Uingereza na Miguel de Cervantes wa Spain
huandikwa kwamba wote walifariki Aprili 23,
1616. Lakini ukweli ni kwamba hawakufa siku
moja bali walipishana siku kumi kwani
England ilichelewa kwa karibu miaka 200
kuikubali โ€œGregorean Calenderโ€!
โ€œGregorean Calenderโ€ haikuundwa ili kuishia
kuliziba lile pengo. Bali pia, kuhakikisha
halitokei tena. Tumeshaona kuwa lile pengo
ni dakika 11 na sekunde 14.812512. Hivyo,
linapanuka na kuwa siku tatu ndani ya miaka
400.
Hivyo kuliziba inatakiwa kupunguza siku tatu
kila baada ya miaka 400.

Je, zipunguzweje?

Kipande cha miaka 400 kina miaka mitatu ya
karne inayogawanyika kwa 4 lakini
haigawanyiki kwa 400.
Ikakubalika kwamba unaogawanyika kwa 4,
lakini haugawanyaiki kwa 400, usiendelee
kuwa mrefu. Humo siku moja ichomolewe na
uwe mfupi.
Ndipo miaka 1700, 1800, 1900 haikuwa tena
mirefu. Ndivyo pia miaka 2100, 2200, 2300
nayo haitakuwa mirefu. Kwa sababu ni miaka
ambayo โ€œGregorean Calenderโ€ inachomoa
siku moja ili kutosababisha pengo tena.
Kipande hiki cha miaka 400 kikaleta wastani
mpya wa siku 365.2425 kwa mwaka. Sasa
lile pengo lile la siku moja si rahisi kufikiwa.
Kwenye โ€œJulian Calenderโ€ tumeona lilikuwa
miaka 128.0355 lakini sasa limekuwa miaka
3,222.
Sasa tuijadili tarehe ya siku ya Pasaka
tukiwa na ufahamu wa kalenda zile. +++ Je, tarehe ya Pasaka imetajwa ndani ya Biblia?

Kuna kifungu kinasema hivi:
โ€œ..Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya
mwezi, wakati wa jioni, ni Pasaka ya BWANA.
Na siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni
sikukuu ya BWANA, ndiyo siku ya mikate
isiyotiwa chachu. (Walawi 23:5)..โ€. Hivyo
Pasaka ni tarehe 15 ya mwezi wa Kwanza.
Lakini Biblia pia inautaja mwezi wa kwanza
kwa jina la Nisan (Esta 3:7, Nehemia 2:1).
Yesu alisulubiwa mwaka ambao Ijumaa
iliitangulia sikukuu ya Pasaka kwa siku moja
(Yohana 18: 28, Marko 15:42-43). Hivyo
tarehe ya Yesu kusulubiwa ni Ijumaa, Nisan
14. Siku moja kabla ya Nisan 15. Siku moja
kabla ya Mwezi-Mkubwa.
Baada ya Yesu, Wakristo wengi Pasaka
waliiadhimisha Jumapili, lakini utata
ulijitokeza kuhusu tarehe ya kuiweka hiyo
Jumapili ya Pasaka. Ilifika wakati jimbo moja
la Wakristo linaadhimisha siku tofauti na
jingine na kwa njia wanayoijua wao.
Utata huu uliondolewa kule Nicaea mwaka
325 ambapo Kanisa Katoliki lilipoamua kuwa,
tarehe ya Pasaka iwe moja tu duniani kote,
yaani iwe ni Jumapili inayokuja baada ya
Mwezi-Mkubwa (Full Moon) unaotokea baada
ya siku ya Ikweta, yaani baada ya Machi 21
(Equinox).
Baada ya uamuzi huu, wataalamu walipania
kuunda chati maalum zenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa zitazokasaidia kuitambua tarehe ya
Pasaka kwa mwaka wowote.
Mwezi huizunguka dunia kwa siku
29.5305891203704 (Synodic Month), wakati
dunia hulizunguka jua kwa siku
365.24218967 (Tropical year).
Mizunguko hii miwili ikianza safari siku moja,
itapishana kila mwaka, lakini itakutana tena
mwezi unapokamilisha mizunguko 235. Dunia
nayo inakuwa imekamilisha mizunguko 19,
yaani miaka 19.
Wataalamu wakaitumia hii miaka 19
kutengeneza chati yenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa unaotokea March 22 hadi April 18.
Tarehe zile zikaitwa tarehe za Mwezi-
Mkubwa Wa Pasaka au Ecclesiastical Full
Moon (EFM).
Ndani ya ile miaka 19, kila mwaka ukapewa
tarakimu iitwayo Golden Number
inayosimama badala ya mwaka ikiwa na
tarehe zile ziliorekodiwa za Mwezi Mkubwa
wa Pasaka. Chati yenyewe ya Golden
Number na tarehe zake (siku/Mwezi) ni hii
ifuatayo: {1=5/4, 2=25/3, 3=13/4, 4=2/4,
5=22/3, 6=10/4, 7=30/3, 8=18/4, 9=7/4,
10=27/3, 11=15/4, 12=4/4, 13=24/3, 14=12/4,
15=1/4, 16=21/3, 17=9/4, 18=29/3, 19=17/4}
Golden Number ya mwaka inapatikana
kuanza kuugawa mwaka kwa 19.
Tulifundishwa mashuleni kuwa namba
inayosalia baada ya kugawa huitwa โ€œBakiโ€ .
Hii โ€œBakiโ€ ukiijumlisha na 1 unapata Golden
Number (GN).
Mfano unatafuta GN ya 27. Hatua ya kwanza
ni kutafuta โ€œBakiโ€ baada ya kugawa 27 kwa
19. Hizi ni hesabu za โ€œmoduloโ€ , yaani
zinahitaji tu namba inayobaki baada ya
kugawa.
Ikiandikwa hivi: (27 mod 19) inatakiwa
namba inayobaki baada ya kuigawa 27 kwa
19. Jibu ni 8. Hivyo tulipaswa tuandike hivi:
(27 mod 19=8). โ€œBakiโ€ 8 tuliyoipata, ndiyo
tunaihitaji ili tuijumlishe na 1 ili tupate GN
ambayo hapa ni 9 kwani (8+1=9).
Tungeweza pia kuandika hivi : 27 mod 19 +
1=9. Hivyo kanuni ya kupata GN kwa mwaka
wowote ni hii:
(MWAKA mod 19 + 1). Yaani, ugawe huo
mwaka kwa 19, kisha namba itakayobaki
ijumlishe na moja.
Ukishaipata GN, itafute kwenye ile chati
ambapo utaiona ikiwa na mwezi na tarehe.
Jumapili inayofuata baada ya tarehe hii ndiyo
tarehe ya Pasaka ya mwaka huo.
Tutumie chati ile na kanuni hii kujua tarehe
ya Pasaka ya mwaka 1474. GN ni (1474 mod
19 + 1=12). Hivyo GN ni 12.
Kwenye chati, 12 inaonyesha ni tarehe 4/4.
Hivyo, mwaka 1474 Mwezi-Mkubwa wa
Pasaka ulikuwa tarehe 4/4/1474. Hiyo ilikuwa
ni Jumatatu. Hivyo Pasaka ilikuwa ni
Jumapili iliyofuata yaani tarehe 10/4/1474.
Lakini, Kanisa Katoliki liliikubali kanuni hii
karne ya sita. Hii ndiyo sababu, tarehe za
Pasaka zinazojulikana ni zile tu zinazoanza
mwaka 533.
Ndivyo Pasaka ilivyotafutwa miaka ile. Sasa
tuone Pasaka ya kizazi chetu. Kizazi cha
โ€œGregorean Calenderโ€ iliyoanza mwaka 1582.
Tumelijadili lile pengo la siku lililofikia ambalo
mwaka 1582 lilishafika siku 10. Ukweli ni
kwamba kabla halijazibwa, Pasaka ilikuwa
inawadia lakini uhalisi ni kwamba inakuwa
tayari imepitwa siku 10. Kinyume kabisa na
maamuzi ya Kanisa kule Nicaea!
Ili kulizuia lisitokee tena, tumeona uchomoaji
wa siku moja toka kwenye miaka inayofunga
karne, isiyogawanyika kwa 400. Uchomoaji
huu umewekwa kwenye kanuni (formula)
iitwayo โ€œSolar Equationโ€.
Kama mwendo wa kuzunguka jua
umezingatiwa na โ€œGregorean Calenderโ€, vipi
kuhusu mwendo wa mwezi?
Tumeuona kwamba mizunguko ya mwezi na
dunia hukutana kila baada ya miaka 19.
Kadirio la dunia kuzunguka kwa siku 365.25

linafanya ikizunguka kwa miaka 19 zinakuwa
siku 6,939.75. Mwezi utakuwa nao
umezunguka mara 235, huku kila mzunguko
ukitumia siku 29.5305891203704.
Hivyo, kukutana kule ndani ya kila miaka 19,
huleta pengo dogo la saa 1, dakika 28,
sekunde 38.5.
Mapengo madogo haya tunayoyapuuza
mwanzoni, yameshatugharimu vya kutosha.
Pengo hili kwa mwaka ni dogo lakini kwa
miaka 2500 linakuwa hadi kufika siku nane.
Kwenye hesabu za kutafuta Pasaka
urekebishaji wa hili pengo hutokea kwenye
kanuni iitwayo โ€œLunar Equationโ€. Lakini kwa
sababu ya tofauti ya uelekeo wa mzunguko
wa mwezi na dunia, โ€œLunar Equationโ€
hujumlisha mara nane kila baada ya miaka
2500.
Hivyo, mahesabu yoyote ya kuitafuta tarehe
ya Pasaka hayakosi kanuni hizi mbili โ€œSolar
Equationโ€ na โ€œLunar Equationโ€ .
Tumeona kwamba kalenda ilianza mwaka
1582. โ€œSolar Equationโ€ inaondoa siku moja
toka kwenye miaka 1700, 1800, 1900. Hivyo,
ni kujidanganya kusema kwamba miaka yote
inayogawanyika kwa nne ni mirefu, jambo
ambalo hata mimi nilifundishwa shuleni.
Hapa tumeona kwamba โ€œSolar Equationโ€
imeondoa siku moja kwenye mwaka 1900 na
hivyo haukuwa mwaka mrefu ingawa
unagawanyika kwa nne.
โ€œLunar Equationโ€ huongeza siku moja kwenye
miaka 1800, 2100, 2400. Mwaka 1800
unaguswa na vyote โ€œSolar Equationโ€ na
โ€œLunar Equationโ€. Hivyo hauathiriki.
Kanuni zote za kuitafuta Pasaka huzingatia
zaidi ya niliyoyaeleza, lakini cha muhimu
zaidi ni hizi mbili yaani โ€œSolar Equationโ€ na
โ€œLunar Equationโ€ ambazo sijawahi kuzisikia
kwa kiswahili.
Ni vigumu kuepuka hesabu za โ€œmoduloโ€ au
โ€œmodโ€ unapotafuta tarehe ya Pasaka. Lakini
ukiwauliza wanafunzi wa darasa la nne
kwamba machungwa 2011 yakipangwa
kwenye mafungu 19, ni mangapi yatakosa
fungu?

Wapo watakaopata jibu sahihi kwamba ni
machungwa 16. Kimahesabu swali hilo
linaandikwa hivi: (2011 mod 19) na jibu lake
ni 16, yaani (2011 mod 19=16).
Ifuatayo ni moja ya kanuni zinazotumika
kuipata tarehe za Pasaka ya mwaka wowote
kuanzia 1700 hadi 2099:
(1) : a=MWAKA mod 19;
(2) : b=MWAKA \ 100;
(3) : c=MWAKA mod 100;
(4) : d=b \ 4;
(5) : e=b mod 4;
(6) : f=c \ 4;
(7) : g=c mod 4;
(8) : h=(b + 8)\25;
(9) : i=(b โ€“ h + 1)\3;
(10) : j=(19xa + b โ€“ d โ€“ i + 15) mod 30;
(11) : k=(32 + 2xe + 2xf โ€“ j โ€“ g) mod 7;
(12) : m=(a + 11xj + 22xk) \ 451;
(13) : n=j + k โ€“ 7xm + 114;
(14) : Tarehe=(n mod 31) + 1
(15) : Mwezi =n\31;
Penye neno MWAKA, andika mwaka
unaotafuta kujua tarehe yake ya Pasaka.
Panapotokea alama (\) ni kugawanya
ambako hata kama jibu litaleta desimali, basi
hiyo desimali unatakiwa kuachana nayo ili
jibu libaki namba nzima. Penye alama (x)
hiyo ni ya kuzidisha.
Yafuatayo ni majibu niliyopata kwa hatua
zote baada ya kuuingiza mwaka 2015 ili
kujua siku ya Pasaka ya mwaka huu: (1): 1,
(2): 20, (3): 15, (4): 5, (5): 0, (6): 3, (7): 3,
(8): 1, (9): 6, (10): 13, (11): 1, (12): 0, (13):
128, (14): 5, (15): 4.
Tarehe imepatikana kwenye hatua ya 14
ambako jibu ni โ€œ5โ€. Mwezi umepatikana
kwenye hatua ya 15 ambako jibu ni โ€œ4โ€. Hivyo
Pasaka ya mwaka (2015) huu ni Tarehe 5,
mwezi wa 4.
Hivyo, kwa njia hii, unaweza kujua tarehe za
Pasaka kwa miaka ijayo kama unavyoijua
tarehe ya Krismas. Kama kuna tukio
lilifanyika siku ya Pasaka miaka iliyopita na
hukumbuki tarehe, basi tumia kanuni hii.
Zifuatazo ni siku zinazoitangulia Pasaka kwa
idadi ya siku zilizoandikwa kwenye mabano:
Jumatano Ya Majivu (46), Jumapili ya
Matawi (7), Ijumaa Kuu (2).
Zinazotanguliwa na Pasaka ni hizi zifuatazo:
Kupaa (42), Pentekoste (49), Utatu Mtakatifu
(56), Ekaristi (63).
Mwanzo tuliona kwamba Mwezi-Mkubwa wa

Pasaka au โ€œEcclesiastical full Moonโ€ ni ule wa
March 22 hadi April 18. Ukitokea March 22
basi kuna uwezekano siku hiyohiyo ikawa
Pasaka na ikawa imevunja rekodi ya kuwahi
mapema.
Ukitokea April 18, kuna uwezekano wa
Pasaka kuwa siku saba zaidi ya hapa yaani
April 25, na hiyo ikawa ni tarehe ya juu mno
ya Pasaka. Hivyo, Pasaka yoyote haiwezi
kuwa chini ya Machi 22, wala haiwezi
kuwazaidi ya April 25.
Pasaka tuliyoiona mwaka 2008 ndiyo ya
mwisho kwa kizazi chetu kuiona ikiwahi
mapema kiasi kile, kwani ilitokea Machi 23 na
itairudia tena tarehe hiyo mwaka 2160!

by JOSEPH MAGATA

Jinsi ya kupika Wali Wa Sosi Ya Tuna

Viambaupishi

Sosi Ya tuna

Tuna (samaki/jodari) 2 Vikopo

Vitunguu (kata kata) 4

Nyanya zilizosagwa 5

Nyanya kopo 3 Vijiko vya supu

Viazi (vilivyokatwa vipande vidogo – cubes) 4

Dengu (chick peas) 1 kikombe

Kitunguu saumu(thomu/galic)&Tangawizi iliyosagwa 1 Kijiko cha supu

Hiliki 1/4 kijiko cha chai

Mchanganyiko wa bizari 1 kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Pilipili manga 1 Kijiko cha chai

Vipande cha Maggi (Cube) 2

Wali

Mchele 3 Vikombe vikubwa (Mugs)

Mdalasini 2 Vijiti

Karafuu chembe 5

Zaafarani kiasi

*Jirsh (Komamanga kavu au zabibu kavu -raisins) 1/2 Kikombe

Jinsi ya kuandaa na kupika

1. Kosha Mchele na roweka.

2. Kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi (brown) chuja mafuta uweke kando.

3. Kaanga viazi, epua

4. Punguza mafuta, kaanga nyanya.

5. Tia thomu/tangawizi, bizari zote, vipande vya Maggi, nyanya kopo, chumvi.

6. Mwaga maji ya tuna iwe kavu, changanyisha kwenye sosi.

7. Tia zaafarani kidogo katika sosi na bakisha ya wali.

8. Chemsha mchele pamoja na mdalasini na karafuu.

9. Karibu na kuwiva, chuja maji utie katika chombo cha kupikia katika jiko (oven)

10. Nyunyizia zaafarani, mwagia vitunguu, viazi, na dengu juu ya wali.

11. Mwagia sosi ya tuna na pambia jirshi (au zabibu).

12. Funika wali na upike katika jiko moto wa 450ยบ kwa muda wa kupikika wali.

* Jirsh (komamanga) kavu zioshwe vizuri kutoa vumbi au tumia zabibu kavu (raisins)

Kushindwa au vikwazo sio sababu ya kutofanikiwa

“Nilibakwa nikiwa na miaka 9 lakini leo mimi ni mmoja wa wanawake wenye ushawishi mkubwa duniani”- OPRAH WINFREY!

“Sikumaliza elimu yangu ya Chuo Kikuu lakini mimi ndiye binadamu tajiri kuliko wote duniani” – BILL GATES!

“Nilikuwa napata matokeo mabaya sana darasani wakati nilipokuwa shule ya msingi lakini bado mimi ni Daktari Bingwa wa Upasuaji duniani” – DR. BEN CARSON!

“Nilimwambia baba yangu tutakuwa na mali na utajiri mkubwa lakini hakuamini, leo hiyo ndiyo hali halisi”
– CHRISTIANO RONALDO!

“Nilikuwa mhudumu kwenye mgawahawa wa chai ili kulipia ada za mafunzo yangu ya mpira lakini leo mimi ni mchezaji bora wa dunia” – LIONEL MESSI!

“Nilikuwa nalala chini kwenye vyumba vya marafiki zangu, natafuta chupa tupu za soda nipate chakula, pesa na mlo wa bure wa kila wiki lakini bado mimi ndiye mwanzilishi wa APPLE” – STEVE JOBS!

“Walimu wangu waliniita mwanafunzi mjinga na asiyejiweza lakini bado nimekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza” – TONY BLAIR!

“Niliendesha TAKSI ili kulipia ada yangu Chuo Kikuu lakini leo mimi ni Bilionea” – MIKE ADENUGA!

#NOTE: Kushindwa au Vikwazo vya nyuma ni mambo yasiyo na nafasi kwa UWEZO mkubwa uliomo ndani yako. Kwa mtu anayeamini, kila kitu kinawezekana. Ni tunu ulizonazo na talent ulizopewa ndizo ufunguo wa maisha yako. Usiende kukopa shaba kwa jirani wakati umeacha dhahabu nyumbani kwako, tumia dhahabu zako

Siri ya kamba nyekundu

Miaka zaidi ya 3000 iliyopita katika mji wa Yeriko alikuwepo mwanamke mmoja kahaba, jina lake Rahabu. Huyu mwanamke aliwaokoa wapelelezi wa Israel waliotumwa kwenda kufanya uchunguzi ktk nchi yao.

Wakati wana wa Israel wanatoka Misri kuelekea nchi ya Kaanani, Mungu aliwaahidi kuwapa mji wa Yeriko. Kwahiyo walipofika ng’ambo ya mto Yordani, Yoshua akatuma wapelezi wawili kwenda kuipeleleza Yeriko kabla wana wa Israel kuivamia na kuitwaa. Wale wapelelezi walipofika mji wa Yeriko mfalme akapelekewa taarifa kuwa kuna watu wawili wameingia kuipeleleza nchi.

Kwahiyo mfalme akaagiza wakamatwe na wauawe. Wale wapelelezi wakaingia ktk nyumba ya mwanamke kahaba aitwaye Rahabu akawaficha darini. Akawafunika kwa mabua ya kitani. Wale askari walipofika na kumuuliza Rahabu kwamba wako wapi waisrael wawili walioingia humu ndani, Rahabu akajibu kuwa wameondoka.

Akasema ni kweli waliingia ktk nyumba yangu lakini walitoka kabla lango la mji halijafungwa. Akawaambia wafuateni haraka kabla hawajafika mbali. Wale askari wakatoka kuwafuata wale wapelelezi hadi katika vilima vya nje ya mji lakini wasiwaone. Ilipofika usiku Rahabu akawashusha darini wale wapelelezi na kuwaelekeza namna ya kutoroka mji wa Yeriko. Akawaelekeza wapite njia nyingine tofauti na ile waliyoiendea wale askari. Akawashusha kupitia dirishani ili watu wa mji ule wasiwaone.

Kwa ukarimu aliowatendea wale wapelelezi wakaweka agano nae kwamba siku wana wa Israel wakija kuiangamiza Yeriko, BWANA ataiponya nyumba ya Rahabu na ndugu zake wote. Ili kutimiza agano hilo wale wapelezi wakamwambia Rahabu weka kamba nyekundu katika dirisha lako kama alama, ili jeshi la Israel liltakapouteketeza mji nyumba yako isiangamizwe.

Yoshua 2:17 &18 “Wale wapelelezi wakamwambia Rahabu, Sisi tunataka tusiwe na hatia kwa ajili ya kiapo hiki ulichotuapisha. Angalia, tutakapoingia katika nchi hii, funga kamba hii nyekundu katika dirisha hili ulilotuteremshia; nawe uwakusanye nyumbani mwako, baba yako, mama yako, na ndugu zako, na watu wote wa nyumba ya baba yako.”

Rahabu akafanya hivyo, na siku Jeshi la Israel lilipovamia Mji wa Yeriko ili kuuteketeza, Rahabu na ndugu zake walipona.

Yoshua 6:23 &24 “Basi wale vijana wapelelezi wakaingia, wakamtoa Rahabu, na baba yake, na mama yake, na ndugu zake, na vitu vyote walivyokuwa navyo, wakawatoa na jamaa zake wote pia; wakawaweka nje ya matuo ya Israeli. Kisha wakauteketeza mji kwa moto, na vitu vyote vilivyokuwa ndani yakeโ€ฆ”

MORAL OF THE STORY.!
Habari hii ina mengi ya kutufundisha lakini leo nataka nikufundishe kuhusiana na siri ya kamba nyekundu ambayo Rahabu aliiweka katika dirisha lake na jinsi ilivyomuokoa.

Rahabu hakua mtakatifu, hakuwa mteule wa Mungu wala hakuwa kizazi cha Israel. Alikua mwanamke wa mataifa, tena kahaba. Hakuwa mwema sana machoni pa Mungu. Lakini aliokoka kwa sababu ya “kamba nyekundu” dirishani mwake. Pengine wapo maaskofu, wachungaji, mitume au manabii walioangamizwa, lakini kahaba Rahabu akaokolewa yeye na ndugu zake licha ya kwamba alikua kahaba. Siri ni “kamba nyekundu” dirishani mwake.

Jiulize je wewe unayo kamba nyekundu? Kuna watu katika maisha wanaonekana wenye dhambi, wachafu, dhaifu au wasiofaa, lakini Mungu huwanyanyua na kuwabariki na kuwaacha wale tunaodhani ni watakatifu au wenye haki. Mungu anaangalia “kamba nyekundu”. Unaweza kuwa mtakatifu lakini huna “kamba nyekundu” itakayomfanya Mungu akurehemu.

Unaweza kuwa umemaliza masomo yako na umefaulu vizuri, lakini kila unapoomba kazi huitwi hata kwenye usaili, na ukiitwa hupati kazi, miaka inazidi kwenda. Unaamua kwenda kwenye maombi. Kila siku unafanya maombi lakini bado hufanikiwi. Unajiuliza tatizo liko wapi. Unaji-asses na kuona hakuna tatizo mahali. Kumbe huna “kamba nyekundu”

Au unaweza kuwa una biashara yako lakini haifanikiwi. Hupati wateja. Umehitahidi kwa kila hali lakini bado huoni faida. Unadhani tatizo labda Mungu amekuacha. Unaamua kuwa mtu wa maombi. Unazunguka makanisa mbalimbali kuonbewa lakini bado haufanikiwi. Kumbe huna “kamba nyekundu”.

“Kamba nyekundu” imekuwa siri ya mafanikio ya watu wengi bila kujalisha mahusiano yao kiroho na Mungu. Bila kujalisha kama ni wakristo au si wakristo. Kamba nyekundu imewasaidia hata wenye dhambi kubarikiwa. Rahabu alikua kahaba lakini yeye na ndugu zake waliokolewa kwa sababu ya “kamba nyekundu”.

Je kamba nyekundu ni nini? Kamba nyekundu ni mfumo wako wa maisha; jinsi unavyoishi na unayowatendea watu wengine, hasa “wateule” wa Mungu.

Kuna wakati Mungu huamua kukubariki si kwa sababu wewe ni mwema sana, bali kwa sababu kuna watu wema wanaoomba kwa ajili yako. Inawezekana tangu uanze kuomba, maombi yako hayajawahi kufika kwa Mungu lakini unabarikiwa, kwa sababu ya kamba nyekundu.

Kuna watu ambao ni “wateule” wa Mungu, kwahiyo kadri unavyowatendea mema hao watu baraka zinakuja kwako “automatically” hata kama wewe si mkristo. Rahabu aliwatendendea mema wapelelezi wa Israel baraka zikaenda kwake “automatically” bila kujalisha kwamba alikua kahaba.

Yatima, wajane, maskini, wazee, wagonjwa na wengine wenye uhitaji ni wateule wa Mungu. Kwahiyo ukiwatendea mema watu hawa baraka zinakuja kwako hata kama wewe ni mwenye dhambi.

Kwa mfano kama kuna watoto yatima unawasomesha, au kuna wajane unawasaidia mahitaji yao, au wagonjwa unawasaidia matibabu, si rahisi Mungu kuondoa mkono wake wa baraka kwako hata kama wewe ni mwenye dhambi. Mungu akiondoa baraka kwako watu wake watateseka.

Wale yatima, wajane, wagonjwa ambao wewe ni msaada kwao kila wakiomba Mungu huongeza baraka kwako ili uzidi kuwahudumia. Inawezekana maombi yako hayafikagi kwa Mungu lakini unabarikiwa kwa sababu ya maombi ya hao unawaosaidia.

Kuna wakati Mungu anaweza kuamua kuzipiga dhoruba biashara za wenzako, lakini ya kwako ikasimama imara. Si kwa sababu wewe ni mwema sana, bali kwa sababu kuna watu wanamlilia Mungu kwa ajili yako. Kuna wanategemea ada za shule kwenye hiyo biashara yako. Kuna watu wanategemea pesa za matibabu kwenye biashara yako. Kwa hiyo Mungu akiyumbisha biashara yako atakua anawaumiza watu hao. So ili asiwaumize anaamua kukuaacha. Hiyo ni kamba nyekundu.!

Kuna wakati wenzio wakifanya makosa madogo kazini wanafukuzwa kazi, lakini unajishangaa wewe umefanya makosa makubwa na hufukuzwi. Si kwa sababu una bahati sana. Ni kamba nyekundu. Kuna watu walioko nyuma yako ambao ni wateule wa Mungu. Kuna yatima wanategemea kulipiwa ada kwa mshahara wako, kuna wagonjwa wanategemea kusaidiwa hela za matibabu kwenye mshahara wako, kuna wajane wanategemea hela ya kuishi kutoka kwako. Kwahiyo Mungu akikuadhibu anakua amewaadhibu na wao. Kwahiyo ili wapone inabidi akulinde hata kama umefanya kosa kazini. Unashangaa tu kesi imeisha hata kwa namna ambayo hujui. Hiyo ni kamba nyekundu.!

Kuna mtu ambaye ni maskini wa kutupwa hana hata uwezo wa kununua sukari. Lakini anamuomba Mungu kwa imani kuwa ampe sukari aweze kunywa chai kila siku. Kwa kuwa huyo maskini huwa anapata sukari kutoka kwako, Mungu atazidi kukubariki ili uendelee kumhudumia huyo maskini. Hiyo ni Kamba nyekundu.!

Kamba nyekundu ilimuokoa Rahabu na ndugu zake licha ya kwamba alikua kahaba. Jiulize wewe una kamba nyekundu? Je kuna watu wako nyuma yako ambao Mungu akiwaangalia anakubariki, anakuokoa hata kama upo kwenye hatari?

Kama unamsomesha mwanao shule ya “mamilioni” kwa mwaka wakati mtoto wa jirani yako hana hata uniform za kuendea shule, au unatumia “mamilioni” kwa pombe na starehe wakati kuna wagonjwa wanaokufa kwa kukosa panadol, siku Mungu akitaka kukuadhibu hajiulizi mara mbili maana huna “kamba nyekundu” nyuma yako.

Lakini yule anayesaidia wenye uhitaji, kama yatima, wagonjwa, wazee, wajane,walemavu, au maskini atazidi kubarikiwa tu hata kama ni mwenye dhambi, maana anayo kamba nyekundu.

Hii ni kwa sababu Mungu akitaka kumuadhibu, kabla hajamtizama yeye anatizama kwanza yatima walioko nyuma yake anaowasaidia, anatizama wagonjwa wanaomtegemea kwa matibabu, anatizama wajane. Anaona akimuadhibu, atakuwa ameadhibu na hao wanaomtegemea. Kwa hiyo anaamua kumuacha.

Hii ina maana kuwa baraka na utakatifu ni vitu viwili tofauti. Unaweza usiwe mtakatifu lakini Mungu akakubariki na akakulinda. Unaweza kubarikiwa si kwa sababu unastahili, bali kwa sababu kuna “wanaostahili” wapo nyuma yako wakikupigania kwa baba yao (Yehova). Ndio maana kuna watu wengi wasio Wakristo wanabarikiwa kila siku hata kama hawamjui Mungu. Ni kwa sababu wana “kamba nyekundu”.

Malisa G.J

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About