Karibu AckySHINE
Karibu AckySHINE
Chagua Unachotaka Kusoma Hapa
Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.
Maisha ya kiroho yanahitaji Mipango (Strategy)
Kama yalivyo maisha ya kimwili, maisha ya kiroho pia yanahitaji mipango. Kila siku panga utafanya nini kiroho, mfano unaweza kupanga sala, kusaidia masikini, kuwa mpole au mwema. Vivyo hivyo kila wiki, kila mwezi na kila mwaka mpya panga cha kufanya kiroho naye Mungu atakubariki na kukupangia zaidi. Huwezi kufanikiwa kiroho kama hujui unafanya nini kiroho.
Mafundisho ya kumfundisha mtu mzima kabla ya ubatizo wa hatari
- Mungu yupo mmoja. Bwana wetu na Baba yetu, mwenye kuwatunza watu wema mbinguni na kuwaadhibu watu wabaya motoni milele (Mt. 15:41,46)
- Katika Mungu mmoja kuna nafsi tatu: Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (Yoh. 14:16, 17).
- Nafsi ya pili alishuka duniani akajifanya mtu, akatuokoa utumwani mwa shetani, akatufundisha mambo gani tusadiki, mambo gani tutende, akatupa alama ya ukombozi wetu ndio ubatizo.
- Ubatizo wafuta kabisa uovu wa mtu na kutakasa roho zetu.
- Mwenye kubatizwa atubu na kurudisha alichoiba na kupatana na maadui n.k
Walevi wana Mambo! Angalia wanachokisema
WALEVI WAWILI KATIKA MAZUNGUMZO YAO
MLEVI 1 hivi rafiki yangu china ni mbali kweli
MLEVI 2 sidhani mbona pale kazin kuna mchina anakuja na baiskeli
😆😆😆😆😆
Zawadi ya Kipekee kwa Mtu Ambayo Inadumu Milele
Kuna Zawadi moja ya Kipekee ya kumpa mtu ambayo ni Kusali na Kuomwombea Mtu aweze kuingia Mbinguni. Je, ulishawahi kutoa zawadi hii hasa kwa wale unaowapenda? Kila kitu kitabaki hapa duniani na kitapita na kusahauliwa lakini hili halina mwisho
Zawadi ya Kipekee: Kusali na Kuombea Wapendwa Wetu
Kuna zawadi moja ya kipekee ambayo unaweza kumpa mtu, nayo ni kusali na kumuombea ili aweze kuingia Mbinguni. Katika maisha haya ya kidunia, mara nyingi tunatafuta zawadi za kuwafurahisha wapendwa wetu, lakini zawadi ya sala ina thamani kubwa kuliko zawadi yoyote ya kidunia. Je, ulishawahi kutoa zawadi hii hasa kwa wale unaowapenda?
Thamani ya Zawadi ya Sala
Kusali na kumuombea mtu ni tendo la upendo wa kweli. Ni njia ya kuonyesha kwamba unajali sana kuhusu hali ya kiroho ya mtu huyo na unataka kumwona akifurahia maisha ya milele. Sala ni mazungumzo na Mungu, na kwa kuomba kwa ajili ya wengine, tunawaweka mikononi mwa Mungu mwenye uwezo wote. Biblia inatufundisha umuhimu wa kuombeana.
“Basi, aombeeni hivyo na kusema, Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe.” (Mathayo 6:9)
“Kwa sababu hii tena, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kuomba kwa ajili yenu, na kusiomba kwamba mjazwe na maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa kiroho.” (Wakolosai 1:9)
“Sasa basi, waombeeni kila siku ili wasimame imara katika imani yao.” (Waebrania 13:18)
Kila Kitu Kitabaki Hapa Duniani
Katika maisha haya, tunaweza kumiliki vitu vingi: nyumba, magari, fedha, na mali nyingine nyingi. Hata hivyo, kila kitu kitabaki hapa duniani na kitabakia kuwa mali isiyo na thamani tunapovuka kwenda kwenye maisha ya milele. Mali ya kidunia inapitiliza na kusahaulika, lakini zawadi ya sala inaendelea hata baada ya kifo.
“Hatujaingia na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu.” (1 Timotheo 6:7)
“Usiweke hazina zenu duniani, ambako nondo na kutu vinaharibu, na wevi huvunja na kuiba; bali wekeni hazina zenu mbinguni, ambako hakuna nondo wala kutu viiharibuyo, na wevi hawavunji wala kuiba.” (Mathayo 6:19-20)
“Mna haja moja, nayo ni hii; utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake, na hayo yote mtazidishiwa.” (Mathayo 6:33)
Zawadi ya Sala Haina Mwisho
Sala ni zawadi ya kudumu. Inapotolewa kwa nia safi, inaweza kubadilisha maisha ya mtu na kumwongoza kwenye njia ya wokovu. Kwa kumwombea mtu, tunasaidia roho yake kupata nafasi ya kumkaribia Mungu na kuishi maisha matakatifu. Hii ni zawadi ambayo haitaisha au kupotea, bali itaendelea kuwa na athari milele.
“Naomba kwa ajili yao. Siombi kwa ajili ya ulimwengu, bali kwa ajili ya wale ulionipa, kwa maana wao ni wako.” (Yohana 17:9)
“Kwa hiyo, ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, ili mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.” (Yakobo 5:16)
“Basi nakuomba, kama ambavyo hujaacha kumwombea Mtakatifu huyo; unapoomba usife moyo, bali uongeze juhudi.” (Wakolosai 4:12)
Hitimisho
Je, ulishawahi kutoa zawadi hii kwa wale unaowapenda? Kusali na kuwaombea wapendwa wako ni tendo la upendo na kujali ambalo lina thamani kubwa sana kuliko zawadi yoyote ya kidunia. Kila kitu kingine kitabaki hapa duniani na kitapita na kusahauliwa, lakini zawadi ya sala ina athari za milele. Kwa kumwombea mtu, unampa nafasi ya kuingia Mbinguni, na hiyo ni zawadi ya pekee zaidi unayoweza kumpa mtu yeyote.
Kila wakati unapomwomba Mungu kwa ajili ya wapendwa wako, kumbuka kwamba unawawekea hazina mbinguni, ambako hazina hizo hazitaharibika kamwe. Ni tendo lenye upendo na lenye kuleta baraka zisizo na mwisho.
“Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwana wake pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16)
“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.” (Mathayo 7:7)
“Na imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” (Waebrania 11:1)
Angalia huyu bibi alichotufanyia kwenye gari
tulikua kwenye gari kibao ad wengne mlangon likasmimama kituo kimoja kulikua kuna bibi anataka kupanda
Konda- bibi twende sit kibao ata utalala
Bibi – oooh sawa mjukuu
Konda – simama tu apo wanashuka mbele
Bibi – akacheka sana tu
Konda- mbona unacheka bibi
Bibi – mjukuu hawa wote hawashuki wanakufa apo mbele
Watu- simamisha gar
Saiv bibi kabaki mwenyewe amelala sit ya nyuma😆😆😅😂😂
Nifunge nini Kwaresma? Mambo ya kufunga kipindi cha Kwaresima
Funga huzuni upate furaha,
Funga ulabu upate siha,
Funga majivuno upata utukufu,
Funga uzinzi upate wongofu,
Funga kisirani upate utakatifu,
Funga wivu upata baraka,
Funga unafiki upate uchaji,
Funga kinyongo upate faraja,
Funga kwaresima wakati ni huu
Funga jeuri ujawe rehema,
Funga hofu ujazwe imani,
Funga kinywani ujazwe moyoni,
Funga kisirani ujazwe rohoni,
Funga dharau ujazwe heshima,
Funga majungu, ujazwe neema,
Funga usiri ujawe wafuasi,
Funga tamaa ujazwe kiasi,
Funga kwaresima wakati ni huu.
Faida na namna ya kutumia mafuta ya Zaituni Olive Oil kwenye nywele
Faida ya Mafuta Ya Zaituni Olive Oil kwenye nywele.
1. Yanasaidia kufanya mzunguko wa damu kufanya kazi vizuri kwenye ngozi ya kichwa na kupenyeza hadi kwenye shina ya nywele kisha kuifanya nywele inayoota kuwa imara
2. Yanasaidia kupambana na mba kwenye ngozi ya kichwa
3. Yanasaidia uzalishwaji wa mzizi au shina ya nywele
4. Yanasaidia uzalishwaji wa melanin ambayo inafanya kazi ya kutoa rangi ya nywele inayotakiwa.
5. Yanasaidia kuifanya nywele isiwe kavu sana.
NAMNA YA KUZIHUDUMIA NYWELE:
Unaweza kuchanganya na Mdalasini pamoja na Asali.
1. Olive oil vijiko 2 vya chakula
2. Asali kijiko 1 cha chakula
3. Mdalasini kijiko 1 cha chai
Pasha moto olive oil kisha changanya vyote kwa pamoja pakaa kwenye nywele acha kwa muda wa dakika 20 kisha osha nywele zako na upakae mafuta zikishakauka.
Ninashauri utumie mafuta haya kwenye nywele na ngozi ni mazuri sana. Ukiwa na mba pakaa kwenye ngozi mba itaisha na muwasho utaondoka.
Jinsi ya kumfanya mwanamke afurahi na akupende kwa kumfanyia mambo anayoyataka
Kuna mambo ya msingi ambayo mwanamke anahitaji kutoka kwa mwanamme ili kufurahi na kutulia katika mahusiano japokuwa sio rahisi kukwambia mojakwa moja.
Mambo hayo ni kama ifuatavyo;
Kupewa nafasi na kipaumbele.
Wanawake wanapenda kuwa namba moja au kupendwa kuliko yeyote. Kumpenda mwanamke haikuishii kwenye kumpata na kumliki, kisha kujisahau kwa kisingizio kuwa umemuoa au umemvisha pete ya uchumba, ni zaidi ya hapo. Wanawake wanapenda watangulizwe katika mapenzi na kusiwepo na mwingine wa kuchukua nafasi yao katika mazungumzo na mapenzi kwa ujumla na katika maisha yao.
Kuheshimiwa
Wanawake wanapenda kueshimiwa kwa maneno na matendo. Wanawake hawapendi kuitwa majina mabaya kwa mfano mjinga, Malaya au kulinganishwa na wanawake wenzao wabaya. Wanawake hawapendi kukosewa heshima hasa mbele za watu, hata kama ni kwa mambo madogo madogo.
Kuridhishwa Kwenye tendo la ndoa
Mwanamke anapenda aridhishwe Kwenye tendo la ndoa. Hata kama utakuwa na kiwango kikubwa cha mapenzi juu ya mpenzi wako kwa kiwango gani, ukiwa dhaifu katika tendo la ndoa utayumbisha penzi lako. Utundu na ufundi unahitajika ili kumkata kiu mpenzi wako. Mwanamme anatakiwa kuhakikisha kuwa anamtosheleza mpenzi wake katika tendo hilo.
Nafasi ya kuongea na kujieleza
Wanawake wanapenda wapewe nafasi ya kuongea na kujieleza vile watakavyo. Mpe uhuru mpenzi wako kuzungumza na kumsikiliza bila kumkatiza kwa ukali pale anapoongea sana. Kwa kawaida wanawake wanatajwa kuzungumza maneno 25,000 kwa siku, wakati wanaume wakibaki na kiwango cha maneno 5,000 kwa siku, wanawake hupenda zaidi kujieleza walivyo mbele ya wengine. Kwa hiyo wakizuiwa wasiongee hujiona kama wanakosa nafasi muhimu ya kueleza mawazo yao.
Kusaidiwa katika shida na matatizo yao
Wanawake wengi hutegemea kuwa wanapokuwa na wapenzi watasaidiwa katika matatizo ya kimaisha na migogoro ya kimawazo. Kwa mfano ushauri juu ya maisha yao, kulindwa na hatari za kimaisha, kusaidiwa katika shida na kuongozwa pale wanapohisi kushindwa kufanya jambo. Kama mwanaume hatamfanyia mpenzi wake hili atakuwa amekosa sifa za kuteka penzi la mwanamke.
Kubembelezwa
Wanawake hupenda kubembelezwa hasa pale wanapokuwa na huzuni. Wanawake wengi hupenda kuelimishwa zaidi kuliko kufokewa. Wanawake hawapendi kukaripiwa, mara nyingi hupenda kuungwa mkono wanapokuwa na misuguano na wengine. Ili mwanaume amteke kimapenzi mwanamke lazima awe nyuma yake hata kama atakuwa na kosa.
Mfahamu zaidi Mwanamke kwa Kupitia Kitabu hiki kizuri cha SIRI ZA MWANAMKE
-
Familia, Mapenzi na Mahusiano
📕Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE👧👗👠
Original price was: Sh7,500.Sh3,000Current price is: Sh3,000. Download Now
Jinsi ya kupika Biskuti Za Tende Na Ufuta
Viambaupishi
Unga 3 Vikombe vya chai
Baking powder 1 ½ Vijiko vya chai
Sukari 1 Kikombe cha chai
Siagi 1 Kikombe cha chai
Mayai 2
Maji kiasi ya kuchanganyia
Tende 1 Kikombe
ufuta ¼ kikombe
Jinsi ya kuandaa na kupika
1. Changanya unga, siagi, baking powder, na sukari katika bakuli
2. Tia mayai, na maji kidogo uchanganye vizuri.
3. Sukuma kiasi kama unavyosukuma chapati duara kubwa.
4. Tandaza tende juu yake halafu kunja hadi mwisho.
5. Paka mayai juu yake halafu mwagia ufuta kisha kata kata vipande kama katika picha.
6. Vipange kwenye treya ya oveni kisha choma(bake)moto wa 350°F kwa muda wa nusu saa takriban.
7. Ziepue katika moto naziache zipowe. Panga katika sahani.
Mapishi ya Kabichi
Mahitaji
Kabichi 1/2 kilo
Nyanya ya kopo 1/2
Kitunguu 1
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Chumvi
Olive oil
Matayarisho
Kwanza kabisa bandua magada ya juu ya kabichi, kisha ioshe na uikaushe maji baaba ya hapo katakata kabichi (inapendeza zaidi kama ikikatwa nyembamba) kisha saga pamoja nyanya na kitunguu. Baada yahapo tia katika sufuria ya kupikia, ipike mpaka maji yote yatakapokauka kisha tia chumvi, curry powder na mafuta pika kwa muda kiasi kisha tia kabichi na upunguze moto. Pika mpaka kabishi itakapoiva kisha ipua na itakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuila kwa wali au ugali.
Utayarishaji bora wa chakula
· Osha mikono yako kwa sabuni kabla na baada
ya kutayarisha chakula
· Tumia vyombo safi na sehemu safi kwa
kutayarisha na kula chakula
· Viporo vipashwe moto vizuri kabla ya kula
· Chemsha maji ya kunywa na kuyaacha jikoni
dakika kumi baada ya kuchemka
Meseji ya usiku mwema kwa umpendaye
Ckia ckupend, cktaki na wala ckhitji tena ww ni kikwzo
ktka maisha yangu ucnizoee! Mwmbie shtan maneno hya kabla
hjalala. g9t
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Ukata wa January
Boss;- kwa nini umechelewa kazini
Juma;- kuna mtu njiani alidondosha elfu1
Boss;- ohhoh kwa hiyo ulikuwaunamsaidia kuitafuta
Juma;- hapana nilikuwa nimeikanyaga
😃😃😃😃😃😃😃😂😂😂😂😂😂😂
Eti kwa nini Watu hawapostigi hii? Hata selfie sijaonaga
Vijana mkiwa mnaendesha magari mna post mukiwa mpo beach mna post mkiwa kwenye masherehe mna post Lakin mkiwa mmeenda kwa mganga siwaoni kupost mitunguli na vibuyu vya mganga unakuwa je wa zee tena. 😀😀😀😀
Tafakari Upendo Mkuu wa Mungu kwa Mwanadamu
Utangulizi
Mungu alimpenda sana binadamu hata akauvaa Mwili wa Binadamu akashuka duniani na kuishi kama Binadamu ili amkomboe Mwanadamu na hata akaamua kufa kwa ajili ya Binadamu kwa malipizi ya dhambi za Binadamu na kwa maondoleo ya dhambi.
Je, ni Kitu gani ambacho Mungu angemfanyia mtu ambacho hajakifanya?
Kweli nakwambia hata kama Yesu angebaki duniani na kuwa hai mpaka leo bado watu wasinge mwamini na wapo ambao wangemchukia na kumfanya adui yao hata kumuwinda.
Ni watu wachache sana duniani wanaouona upendo huu mkuu wa Mungu, wengi hawaoni wala hawataki kuona. Wapo hata wacha Mungu lakini hawaelewi upendo huu.
Upendo Mkuu wa Mungu kwa Mwanadamu: Kwa Nini Yesu Alikuja Duniani?
Mungu alimpenda sana binadamu hata akaamua kuuvaa mwili wa binadamu na kushuka duniani ili amkomboe mwanadamu. Alishuka na kuishi kama binadamu, akakubali kuteseka na kufa kwa ajili ya malipizi ya dhambi za wanadamu. Huu ni upendo mkuu ambao Mungu ametufanyia, na ni muhimu kuelewa kwa kina ukubwa wa tendo hili la ajabu.
Mungu Alishuka na Kuishi Kama Binadamu
Mungu, kwa upendo wake usio na kifani, aliona mateso na maumivu ya wanadamu na akaamua kushuka duniani kama binadamu kupitia Yesu Kristo. Aliacha utukufu wake wa mbinguni na kuja kuishi kati yetu. Yohana 1:14 inasema:
“Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.” (Yohana 1:14)
Yesu alikuja na kuishi kama binadamu, akakutana na changamoto zote tunazokutana nazo, ili aweze kutuelewa na kutukomboa kikamilifu.
Alikufa kwa Ajili ya Dhambi Zetu
Upendo wa Mungu ulionyeshwa kwa namna ya ajabu pale Yesu alipokubali kuteseka na kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu. Alibeba mzigo wa dhambi za ulimwengu mzima na kutoa maisha yake kama sadaka takatifu. Warumi 5:8 inasema:
“Lakini Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.” (Warumi 5:8)
Yesu hakufa kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wenye dhambi, ili kutupa nafasi ya kupokea msamaha na uzima wa milele.
Je, Ni Kitu Gani Ambacho Mungu Angemfanyia Mtu Ambacho Hajakifanya?
Mungu ametufanyia kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya wokovu wetu. Alitoa mwanawe wa pekee, Yesu Kristo, ili afe kwa ajili yetu na kutuondolea dhambi zetu. Ni nini zaidi tunachoweza kumwomba Mungu ambacho hajakifanya? Hakuna upendo mkuu zaidi ya huu ambao Mungu ametufanyia. Kama ilivyoandikwa katika Yohana 15:13:
“Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.” (Yohana 15:13)
Yesu Angekuwa Hai Mpaka Leo, Bado Watu Wasingemwamini
Hata kama Yesu angeendelea kuishi duniani mpaka leo, bado kungekuwa na watu wasiomwamini na kumchukia. Hii ni kwa sababu mioyo ya watu wengi imejaa ugumu na kutokuamini. Yesu mwenyewe alisema katika Yohana 15:18:
“Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni ya kwamba ulinichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.” (Yohana 15:18)
Hii inaonyesha kwamba kuna watu ambao hata wakiweka wazi upendo wa Mungu, bado watakataa na kumwona Yesu kama adui.
Wengi Hawaoni Upendo Huu Mkuu wa Mungu
Ni watu wachache sana wanaoona na kuthamini upendo huu mkuu wa Mungu. Wengi hawaoni wala hawataki kuona. Wengine ni wacha Mungu lakini hawaelewi kabisa kina cha upendo huu. Hata hivyo, wale wanaoona upendo huu na kuukubali wanapata uzima wa milele na uhusiano wa karibu na Mungu. Yesu alisema katika Yohana 3:16:
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16)
Hitimisho
Upendo wa Mungu kwa mwanadamu ni mkubwa sana na umedhihirishwa kwa Yesu Kristo kushuka duniani, kuishi kama binadamu na kufa kwa ajili ya dhambi zetu. Mungu ametufanyia kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya wokovu wetu. Ni jukumu letu kutambua na kuthamini upendo huu, na kuishi maisha yanayodhihirisha imani na shukrani zetu kwake. Tunapoona upendo huu wa ajabu, mioyo yetu inapaswa kujazwa na furaha na amani, tukijua kwamba Mungu ametupenda sana na anataka tuwe na uzima wa milele.
Aina kuu ya mizinga bora ya nyuki kwa ajili ya kupata asali nyingi
Mizinga ya Kifuniko juu (Top bar)
Hii ni aina ya mizinga inayotumika sana na wengi. Gharama yake ni ndogo kiasi kulinganisha na mingine. Ni aina nzuri sana kwa mtu anaeanza ufugaji wa nyuki kwa kuwa ni wa gharama nafuu. Mfugaji wa nyuki anaweza kutengeneza mzinga Yya aina hii mwenyewe kama ana utaalamu wa useremala.
Faida ya Mizinga ya Kifuniko juu (Top bar)
• Ni rahisi kukagua asali iliyo tayari.
• Ni rahisi kuvuna asali kuliko kuvuna toka kwenye mzinga wa kienyeji.
• Ni rahisi kuwatunza nyuki wakati wa kiangazi na inapokuwa hakuna maua. Kwa mfano unaweza kuwapatia nyuki chakula ili kuongeza uzalishaji wa asali.
• Ni rahisi kurina asali ukilinganisha na mizinga ya magogo inayotundikwa juu ya mti, kwa kuwa haihitaji vifaa maalumu.
• Aina hii ya mizinga huwekwa kwa kuninginia jambo ambalo siyo rahisi kushambuliwa na wadudu/wanyama wanaokula asali kwa kuwa Inajaa haraka sana wakati ambao ni msimu wa asali kutengenezwa kwa wingi.
Hasara ya Mizinga ya Kifuniko juu (Top bar)
• Kichane kwenye mzinga wa boksi hakina kishikizo hivyo huvunjika kwa urahisi sana kama hakitashikwa kwa uangalifu.
• Masega huvunwa pamoja na asali, kwa hiyo nyuki wanalazimika kutengeneza tena masega mengine ambapo husababisha kupungua kwa uzalishaji wa asali.
Mzinga wa Langstroth
Mzinga wa Langstroth unaweza kukupatia asali zaidi kulinganishwa na mizinga mingine Hii ni aina nzuri na rahisa sana ya mzinga. Mizinga hii hufahamika kama mzinga wa fremu, kwa kuwa ina fremu ambazo vichane vya masega hujishikiza. Chumba kikubwa ambacho malkia hutagia mayai. Malkia anazuiliwa kuhama kwenda chumba kingine kwa kutumia waya. Kwenye chemba maalumu ya kutagia juu yake pana chemba ya kuhifadhia asali.
Vichane vya masega vinatengezwa kwenye fremu na si kwenye nguzo kama ilivyo kwenye Top bar. Ili kuvuna asali, mfugaji akiwa na masega yaliyojaa asali, hutumia vifaa maalum kwa ajili ya urinaji na kuhifadhi asali bila kupata tabu.
Mzinga wa Langstroth ni gharama kiasi kulinganisha na mizinga mingine.Unaweza kuipata kutoka katika taasisi zinazojiusisha na uuzaji wa mizinga, taasisi na karakana binafsi, au wakala wa Serikali.
Cheki huyu jamaa alivyoumbuka kwenye harusi
Jamaa mmoja alialikwa ktk harusi. Akafika mlango Wa 1 umeandikwa kulia ni ndugu Wa maharusi, kushoto ni wageni waalikwa, akaenda kushoto maana yy alialikwa. Akakuta mlango wa2 umeandikwa kulia wenye zawadi kushoto wasionazawadi yy hakuwa na zawadi. Mlango Wa 3 umeandikwa kulia wanawake kushoto waume akapita kushoto akajikuta ametokea mtaani
😄😄😄😄😄😄😄😄. Tujifunze kutoa wandugu
*hatupendagi ujinga sisi*
🚶🏿🚶🏿🚶🏿🚶🏿🚶🏿🚶🏿🚶🏿
Mapishi ya Pilau Ya Nyama Na Mtindi
MAHITAJI
Nyama iliyokatwa vipande – 1 Ratili(LB)
Mchele Basmati – 2 Magi
Chumvi ya wali – kiasi
Kitungu kilichokatwa katwa – 1 kikubwa
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi – 1 kijiko cha supu
Mtindi (yogurt) – ½ kikombe
Mchanganyiko wa bizari ya pilau ya tayari – 2 vijiko vya supu
Mafuta kidogo yakukaangia
Rangi ya manjano (ukipenda)
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
Osha mchele na roweka nusu saa .
Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitungu mpaka viwe rangi ya hudhurungi (brown).
Tia thomu na tangawizi na ukaange kidogo.
Kisha weka bizari ya pilau halafu nyama huku unakaanga hadi nyama isiwe nyekundu tena.
Tia maji gilasi 1½- 2 ichemke mpaka nyama iwive na karibu kukauka.
Mimina mtindi na iachie moto mdogo ikauke kidogo.
Kwenye sufuria nyingine chemsha mchele pamoja na chumvi na mafuta kidogo mpaka uive.
Mimina wali juu ya nyama, kisha nyunyiza rangi (ukipenda) kama vile wali wa biriani na ufunike kwa dakika kumi hivi.
Changanya wali na nyama pamoja ikiwa tayari kuliwa.
Jinsi ya kupika Donati
Viamba upishi
Unga
2 Magi (kikombe kibuwa cha chai)
Sukari
1/3 Kikombe cha chai
Mayai 5
Siagi 4 Vijiko vya chakula
Hamira 1 Kijiko cha chakula
Baking Powder 1 Kijiko cha chai
Vanilla 1 Kijiko cha chai
Hiliki zilizosagwa 1 Kijiko cha chai
Sukari ya laini ya unga
(icing sugar) 1 Magi
Jinsi ya kuandaa na kupika
Unavunja mayai, unatia sukari, hamira, baking powder, vanilla na hiliki ikisha unapiga kwa kutumia mchapo wa kupigia keki. Unapiga mchanganyiko kwa muda wa dakika tano.
Unatia siagi kwenye sufuria na unaiyayusha na kuipasha moto mpaka iwe moto ikisha unaimimina kwenye mchanganyiko na unapiga tena kwa dakika mbili tu.
Unatia unga kwenye sinia au bakuli kubwa ikisha unamimina ule mchanganyiko kwenye unga na unaukanda kutumia mkono, mpaka ulainike.
Ukiona unga mwingi basi ongeza maziwa kidogo mpaka uwe sawa, na ukiona unga mwepesi sana basi unaweza kuongeza unga kidogo pia mpaka ukae sawa mfano wa unga wa maandazi.
Sukuma na ukate madonge kama unavyoyaona hapo juu. Tumia kifuniko cha chupa kwa kukatia kiduara kidogo katikakti ya madonge.
Ukimaliza kukata madonge yote, yaweke kidogo yavimbe halafu teleka mafuta na uyachome.
Ukitoa kwenye mafuta yachuje moto na kabla ya kupoa yawe moto moto yarovye kwenye icing sugar na uhakikishe yote yameenea sukari juu.
Ukimaliza tia kwenye sahani acha zipowe na zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Recent Comments