Sala ni chimbuko la Fadhila
Sala ndiyo chimbuko la fadhila. Kwa njia ya sala tunapata fadhila za Kimungu na Neema za Mungu. Asaliye daima hujazwa neema na fadhila.
Sala ndiyo chimbuko la fadhila. Kwa njia ya sala tunapata fadhila za Kimungu na Neema za Mungu. Asaliye daima hujazwa neema na fadhila.
Usikimbie nyuki ukakosa asali, utamu wa samaki ni kula na wali, usizidishe siki akawa mkali. Ni mimi niliye na dhiki nakujulia tu hali.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Ngโombe wa maziwa wanahitaji virutubisho zaidi ili kuweza kuzalisha maziwa kwa wingi hasa katika kipindi cha miezi 3-4 ya mwanzo baada ya kuzaa, wakati ambao uzalishaji wa maziwa unakuwa juu.
Malisho ya ng’ombe wa maziwa ni lazima yawe na uwiano sahihi wa viungo. Mifugo inahitaji chakula kitakachowapa nguvu, protini, madini, na vitamin ili kujenga miili yao, kuzalisha maziwa, na kuzaliana.
Kulisha ngโombe wa maziwa kwa kutumia aina yoyote ya malisho haitoshi kukuhakikishia ngโombe anakuwa na afya nzuri na kutoa maziwa ya kutosha. Kama ilivyo kwa mifugo mingine kama kuku na hata binadamu, ngโombe anahitaji
mlo bora yaani kamili.
Huu ni mlo mkuu kwa ng’ombe wa maziwa. Mlo ni muhimu na wenye virutubisho. Lakini malisho bora ya kijani ni yale yanayoweza kumpatia ngโombe wa maziwa virutubisho muhimu vinavyohitajika.
Malisho ya kijani yanatakiwa yawe ya kijani kibichi na machanga, hii ina maana kuwa, majani ya malisho ni lazima yakatwe na kuhifadhiwa yakiwa bado machanga na kabla ya kuchanua. Hii ina maana kuwa mimea ambayo imepoteza rangi yake halisi ya kijani inaweza tu kuwasaidia mifugo kuishi lakini haina virutubisho muhimu vya kuwapa mifugo nguvu, madini, protini na haiwezi kusaidia katika uzalishaji wa maziwa.
Malisho yenye viwango vya chini vya virutubisho yanatakiwa yaongezewe kwa chakula cha ziada chenye virutubisho vya kutosha kitakachoziba pengo la virutubisho vilivyokosekana.
Kwa kawaida aina zote za majani ni chanzo kizuri cha vyakula vya kutia nguvu kwa mifugo, kama tuu tu yatalishwa yakiwa bado machanga.
Mfano wa Majani yaliyo maarufu kwa malisho ni matete, ukoka, majani ya tembo, seteria na Guatemala. Majani ya mahindi au mtama ni chakula kizuri sana kwa kuwapa nguvu mifugo.
Vyakula vingine vinaweza kutokana na aina zote za nafaka, punje za ngano, au molasesi.
Vyakula hivi vya kutia nguvu vinatakiwa vilishwe kwa kiasi kidogo.
Mimea michanga ina kiasi kikubwa cha protini kuliko mimea iliyokomaa. Mahindi machanga pamoja na majani ya viazi vitamu ni mahususi kwa protini.
Mikunde ina protini nyingi zaidi kuliko nyasi. Mfano, mabaki ya majani ya maharage, njegere, desmodium na lusina. Majani yanayotokana na mimea kama lusina, calliandra au sesbania ina kiwango kikubwa cha protini pia.
Aina nyingine ya vyakula vyenye protini ni mashudu ya pamba, mashudu yaalizeti na soya.
Ngโombe wa maziwa wasilishwe kwa kutumia aina zote za jamii ya mikunde kwa zaidi ya asilimia 30 ya uwiano wa mchanganyiko wa malisho ili kuepuka matatizo ya kiafya.
Ng’ombe wa maziwa wanahitaji madini ya ziada. Madini Ni lazima yapatikane muda wote, mfano kama jiwe la chumvi au kama chumvi ya unga ya kuweka kwenye (chakula) pumba.
Wanyama wanaokuwa, wenye mimba, na ngโombe anaenyonyesha wanahitaji kiasi kikubwa cha madini, mfano calcium na phosphorous kwa kuwa madini mengi yanatoka kwenye maziwa.
Madini yanaweza kupatikana katika Mimea ya jamii ya mikunde na mengineyo isipokuwa nyasi. Mimea hii inatoa kiasi kikubwa cha calcium na madini mengineyo.
Ng’ombe wa maziwa anapewa cha kula cha ziada mfano pumba. Pumba inahitajika kwa ng’ombe lakini kwa kiasi kidogo. Pumba aina ya Dairy meal ina kiwango kikubwa sana cha madini. Lakini ina madhara kwa mifugo endapo wanyama watalishwa kwa kiwango kikubwa.
Malisho yanayotokana na majani au nyasi kavu ni lazima yabakie kuwa chakula kikuu kwa mifugo. Haishauriwi kulisha zaidi ya kilo 6 za pumba kwa siku kwa ngโombe mwenye kilo 450.
Ni lazima wapewe kwa kiwango kidogo sana, ambacho si zaidi ya Kilo 2 kwa mara moja na kichanganywe na majani. Kuongeza kiwango cha pumba kabla na wakati wa kunyonyesha/kukamuliwa, kisizidi kiasi cha kilo 2 kwa wiki ili tumbo la mnyama lizoee.
Watu wengi hulitumia tunda la papai kwa sababu ya utamu wake. Hata hivyo mbali na kuwa na ladha nzuri, tunda la papai lina faida lukuki kwa afya ya mwanadamu.
Tunda la papai lina vitamini A,B,C,D, na E jambo linalo liweka tunda hili katika kundi la matunda na vyakula vyenye utajiri mkubwa wa vitamin.
Tunda la papai lina faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Miongoni mwa faida hizo ni pamoja na kuwa na uwezo wa :
1. Kutibu tatizo la Shida ya kusaga chakula tumboni.
2. Kutibu Udhaifu wa tumbo.
3. Kutibu Kisukari na asthma au pumu.
4. Kutibu Kikohozi kitokacho mapafuni.
ยท Kutibu Kifua kikuu
ยท Tunda hili huleta afya nzuri ukitumia kila siku
ยท Maziwa yanayotoka katika jani lake huponya vidonda
ยท Vilevile yanasaidia kutibu sehemu palipoungua moto
ยท Kama hiyo haitoshi, maziwa yanayotoka katika jani la mpapai yanatibu kiungulia na Ugonjwa wa colon (njia ya haja kubwa ndani)
ยท Pia yanasaidia kutofunga choo
ยท Maganda ya tunda la papai yanasaidia kutibu tatizo la kuungua, vipele na saratani ya ngozi.
ยท Mbegu zake zinatibu ini zikitafunwa 10 โ 12 kwa siku 5.
ยท Majani yake yakaushie ndani, yanatibu pumu. Inapoanza kubana yachome majani yaliyokaushwa kisha jifukize, kule kubanwa kutakisha.
ยท Majani yake yanasaidia katika kutibu shinikizo la damu.
ยท Papai likimenywa na kupondwa linafaa Sana katika masuala ya urembo kwani linaweza kutumika Kama vile unavyotumia lotion kulainisha uso.
ยท Mbegu za papai zina uwezo wa kutibu homa. Meza mbegu za papai kiasi cha kijiko cha chakula mara 3 kwa ajili ya kutibu homa.
ยท Mbegu za papai zilizokaushwa ndani kisha zikasagwa kuwa unga zinatibu malaria, tumia kijiko 1 cha chai changanya na uji, kunywa mara 3 kwa siku 5 Mgonjwa wa kifua kikuu akila matunda haya kwa muda mrefu atapona bila dawa nyingine.
ยท Mizizi yake ikipondwa na kulowekwa katika maji yaliyochemshwa, lita 2 na nusu kwa dakika 15, yanatibu figo, bladder, yanazuia kutapika.
Wapo baadhi ya watu wanashindwa hata kuachia kicheko chenye bashasha hii ni kwa sababu meno yao yamekuwa na rangi, hivyo kuwafanya watu hao kuona aiabu. Pia watu wengi wakiona meno yana rangi ya njano hudhani ni machafu, meusi yanahitaji kusafishwa ili yawe meupe.
Meno kubadilika rangi huweza kuwa ni sababu moja au muunganiko wa sababu mbalimbali kama ifuatavyo;
Matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye kaboni, sigara na mvinyo (wine) kwa muda mrefu husababisha kubadilika kwa rangi ya meno kwa juu (extrinsic staining).
Utumiaji wa maji yenye madini mengi ya fluoride katika kipindi cha utoto (dental fluorosis).
Matumizi ya dawa aina ya tetracycline kwa mama mjamzito ambaye tayari meno ya mtoto aliye tumboni yameanza kuumbwa lakini hayapata madini ya kutosha.
Maumbile yasiyo sahihi ya sehemu ya juu ya jino (amelogenesis imperfecta). Iwapo sehemu hii imeumbwa ikiwa laini kuliko inavyotakiwa huwa rahisi kufyonza rangi na jino huota likiwa limebadilika rangi au hubadilika baada ya muda.
Kufa kwa sehemu hai ya jino hasa kutokana na kuumia kwa jino au ajali (pulp necrosis), hali hii huweza huchukua miaka mingi mpaka kutokea kubalika rangi ya jino..
Jino liliozibwa kwa kutumia material aina ya amalgam huweza kubadilika rangi na kuwa nyeusi.
Mara nyingne jino lililotibiwa kwenye mzizi wa jino (root canal treatment ) huweza kubadilika rangi baada ya miaka mingi.
Kuna njia mbalimbali ambazo hutumika kuyafanya meno yaliyo na rangi isiyo ya kawaida kuwa meupe.
Njia hizi hutofautiana kati ya mtu na mtu kutokana na jinsi alivyoathirika. Kuna njia nyingi ambazo huweza kuyangโarisha kwa ndani (internal bleaching) au kuyangarisha kwa nje (external bleaching).
Endapo una tatizo la meno yaliyobadilika rangi, muone daktari wa kinywa na meno kwaajili ya ushauri na matibabu kwani kinywa kizuri na chenye afya huongeza kujiamini.
BareFoot Sprayer ni Pump Imara na yenye Nguvu Maalumu kwa ajili ya kunyunyiza/kupuliza dawa mashambani, kwenye mifugo nakadhalika.
BareFoot Sprayer imetengenezwa kwa Muundo mzuri kwa kurahisisha ubebaji na upigaji wadawa.
BareFoot Sprayer ina dumu imara lisilopasuka kirahisi na linaloweza kudumu kwa muda mrefu.
โ
โ
โ
Wakati mtu anapoanguka dhambini ndio wakati ambao Yesu anakua karibu na mtu sana hata kuzidi wakati mwingine wowote.
Wakati mtu anapoanguka dhambini ndio Yesu anakua karibu zaidi, lakini tatizo ni kwamba huo ni wakati ambao mtu hawezi kutambua uwepo wa Yesu. Neno moja tuu la Matumaini na Upendo wakati huo linaweza kumfungua mtu na kumbadilisha.
Ni hivi, Yesu anataka na anapenda kumuokoa kila mtu, kumsamehe, na kumuonyesha HURUMA na UPENDO wake na hivi anavifanya hasa mtu anapokua ameanguka dhambini.
Tatizo ni kwamba watu wengi wanazani wanapoanguka dhambini Mungu yupo pale kwa ajili ya kuwaadhibu na kuwahukumu! Ukweli ni kwamba hofu ya adhabu na hukumu inatoka kwa shetani, unapoanguka dhambini unakua katika vita nafsini mwako kati ya Uovu na Mema kwa hiyo neno moja tuu linaweza likakufungua au likakufunga , ukinena neno jema litakufungua na ukinena neno baya mfano la kukata tamaa utafungwa zaidi katika dhambi.
Ukiwa umetenda dhambi hata mbaya kiasi gani, Kwanza kiri na kubali mbele ya Mungu kuwa umetenda dhambi kisha Mwambie Mungu wazi kuhusu dhambi yako kwa majuto. Kisha fuata taratibu za maondoleo ya dhambi.
Ni muhimu sana wakati umeanguka dhambini kuongea na Mungu au kumwambia Mungu kwa Mdomo wako kuhusu dhambi yako wazi huku ukimaanisha kile unachokisema. Ongea na Mungu kama unavyoongea na rafiki yako wa karibu kama umemkosea na sio uongee kama unaongea na hakimu akiwa anakuhukumu. Ukitaka kujua na kuonja Upendo na Huruma ya Mungu hasa unapokua dhambini, Ongea naye kwa Majuto katika upendo na matumaini
Ukweli ambao shetani anaupotosha wakati unapokua dhambini ni kwamba Yesu anasimama kama Bwana wa Huruma, msamaha na Rehema na sio hakimu.
Uwe na Matumaini rafiki yangu Yesu ni Bwana wa Huruma na Mwokozi wako na sio hakimu wako. Hayupo kwa ajili ya kukuadhibu bali kukuponya.
Mungu haangalii Uovu wako bali IMANI na UPENDO wako kwake na anakutendea yote kulingana na kiasi cha Imani na Upendo anachokipata kutoka kwako.
Wakati mtu anapoanguka dhambini, huo ndio wakati ambao Yesu anakua karibu sana na mtu huyo, hata kuzidi wakati mwingine wowote. Hii ni kutokana na upendo wake mkuu na huruma isiyo na kikomo. Yesu anatufuatilia kwa upendo wa kweli, na anataka tuwe na matumaini hata tunapojikuta katika hali ya dhambi. Tatizo ni kwamba huo ni wakati ambao mtu hawezi kutambua uwepo wa Yesu. Hata hivyo, neno moja tu la matumaini na upendo wakati huo linaweza kumfungua mtu na kumbadilisha.
“Hakika, mkono wa Bwana haukupungukiwa, hata usiweze kuokoa, wala sikio lake kuzibwa, hata lisiweze kusikia.” (Isaya 59:1)
“Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, na kuwaokoa wale waliopondeka roho.” (Zaburi 34:18)
“Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.” (Luka 19:10)
Yesu anataka na anapenda kumuokoa kila mtu, kumsamehe, na kumuonyesha huruma na upendo wake, hasa mtu anapokuwa ameanguka dhambini. Huruma na upendo wa Yesu hauna mipaka, na anafurahia kumrudisha mtu kwenye njia sahihi ya wokovu.
“Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.” (Yohana 3:17)
“Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi, wapate kutubu.” (Luka 5:32)
“Kwa maana mimi najua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa tumaini katika siku zenu za mwisho.” (Yeremia 29:11)
Tatizo ni kwamba watu wengi wanadhani wanapoanguka dhambini Mungu yupo pale kwa ajili ya kuwaadhibu na kuwahukumu! Ukweli ni kwamba hofu ya adhabu na hukumu inatoka kwa shetani. Unapoanguka dhambini, unakua katika vita nafsini mwako kati ya uovu na mema. Hivyo, neno moja tu linaweza kukufungua au kukufunga. Ukinena neno jema litakufungua na ukinena neno baya, kama la kukata tamaa, utafungwa zaidi katika dhambi.
“Kwa maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.” (2 Timotheo 1:7)
“Wala msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.” (Luka 12:32)
“Acheni moyo wenu usifadhaike; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.” (Yohana 14:1)
Ukiwa umetenda dhambi hata mbaya kiasi gani, kwanza kiri na kubali mbele ya Mungu kuwa umetenda dhambi kisha mwambie Mungu wazi kuhusu dhambi yako kwa majuto. Kisha fuata taratibu za maondoleo ya dhambi. Ni muhimu sana wakati umeanguka dhambini kuongea na Mungu au kumwambia Mungu kwa mdomo wako kuhusu dhambi yako wazi huku ukimaanisha kile unachokisema. Ongea na Mungu kama unavyoongea na rafiki yako wa karibu kama umemkosea na sio kama unaongea na hakimu akiwa anakuhukumu.
“Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na mwenye haki, atasamehe dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote.” (1 Yohana 1:9)
“Kwa maana nitawasamehe maovu yao, dhambi zao sitazikumbuka tena.” (Yeremia 31:34)
“Sasa, enyi ndugu, nataka mjue kwamba, kupitia kwake huyu Yesu, msamaha wa dhambi unatangazwa kwenu.” (Matendo 13:38)
Ukitaka kujua na kuonja upendo na huruma ya Mungu hasa unapokuwa dhambini, ongea naye kwa majuto katika upendo na matumaini. Yesu anasimama kama Bwana wa huruma, msamaha na rehema na sio hakimu. Uwe na matumaini, rafiki yangu, Yesu ni Bwana wa huruma na mwokozi wako na sio hakimu wako. Hayupo kwa ajili ya kukuadhibu bali kukuponya.
“Kwa maana mimi najua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa tumaini katika siku zenu za mwisho.” (Yeremia 29:11)
“Jitieni moyo na msiogope; maana Bwana Mungu wenu yu pamoja nanyi kila mahali mwendapo.” (Yoshua 1:9)
“Na Mungu wa matumaini awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana katika matumaini, kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.” (Warumi 15:13)
Mungu haangalii uovu wako bali imani na upendo wako kwake, na anakutendea yote kulingana na kiasi cha imani na upendo anachokipata kutoka kwako. Vile unavyomuonyesha Mungu upendo na imani, ndivyo na yeye anavyokutendea kwa upendo na nguvu. Huu ndio ukweli ambao shetani anaupotosha wakati unapokuwa dhambini.
“Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” (Waebrania 11:1)
“Basi, utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake, na hayo yote mtazidishiwa.” (Mathayo 6:33)
“Nanyi msichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.” (Wagalatia 6:9)
Wakati unapoanguka dhambini, kumbuka kuwa Yesu yupo karibu na wewe zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Uwe na matumaini na ujue kwamba Yesu ni Bwana wa huruma na mwokozi wako. Mungu haangalii uovu wako bali imani na upendo wako kwake. Ongea na Mungu kwa majuto na matumaini, na utaonja upendo na huruma yake isiyo na kikomo. Kumbuka, Yesu hayupo kwa ajili ya kukuadhibu bali kukuponya na kukuokoa.
Yesu Kristo aliwakabidhi mitume kumi na wawili uongozi wa Kanisa wakiwa kundi moja lenye mkuu wake, yaani Petro. Vilevile waandamizi wao, yaani maaskofu wote, ni kundi moja na Papa wa Roma ndiye mkuu wao. Huyo peke yake, na kundi la maaskofu likiwa pamoja naye na chini yake, ndio wenye mamlaka ya juu katika Kanisa lote. Mamlaka hiyo inatumika kwa namna ya pekee unapofanyika mtaguso mkuu, yaani mkutano maalumu wa maaskofu uliokubaliwa na Papa kuwa unawakilisha kundi hilo lote. Hakuna uamuzi wa kudumu kuhusu ipi ni mikuu kati ya mitaguso yote iliyofanyika katika historia ya Kanisa. Tangu karne XVI Wakatoliki wataalamu wa sheria za Kanisa wanatoa orodha yao, ambayo kwa sasa ni kama ifuatavyo.
ORODHA YA MITAGUSO MIKUU
โข Katika milenia ya kwanza ilifanyika mashariki (Uturuki wa leo):
1. Nisea I (mwaka 325)
2. Kostantinopoli I (381)
3. Efeso (431)
4. Kalsedonia (451)
5. Kostantinopoli II (553)
6. Kostantinopoli III (680-681)
7. Nisea II (787)
8. Kostantinopoli IV (869-870)โข Katika milenia ya pili ilifanyika magharibi (Italia, Ufaransa, Ujerumani, Uswisi na Vatikano ya leo):
9. Laterano I (1123)
10. Laterano II (1139)
11. Laterano III (1179)
12. Laterano IV (1215)
13. Lyon I (1245)
14. Lyon II (1274)
15. Vienne (1311-1312)
16. Konstanz (1414-1418)
17. Firenze (1431-1445)
18. Laterano V (1512-1517)
19. Trento (1545-1563)
20. Vatikano I (1869-1870)
21. Vatikano II (1962-1965)
Mchele (Basmati) 3 vikombe
Nyama ya ngoโmbe 1 kg
Pilipili boga 1 kubwa
Nyanya 2 kubwa
Vitunguu maji 2 vikubwa
Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa 1 kijiko cha supu
Tangawizi 1 kijiko cha chai
Ndimu 1
Mafuta ya kupikia ยฝ kikombe
Mdalasini ยฝ kijiko cha chai
Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai
Pilipili manga ยฝ Kijiko cha chai
Hiliki ยฝ Kijiko cha chai
Loweka mchele wako katika chombo
Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie thomu, tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi
Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi
katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni
Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia
Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto
Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya
Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi
Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke
Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza
Funika na punguza moto na uache uive taratibu
Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.
Pale unapo gundua kuwa yule ulie mtukana kwenye bajaji ndio boss anaeenda kukufanyia interview๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐ญ
My freand apo ndo utagundua kwaanini wimbo wa Taifa tokea 1961 ni audio aujatolewa video
๐๐๐๐๐๐๐๐
Kilishe mayai yote ni sawa. Virutubishi vinavyopatikana kwenye yai la kuku wa kienyeji kama protini, vitamini A, madini ya chuma na virutubishi vya aina nyingine, ndivyo hivyo vinavyopatikana pia kwenye yai la kuku wa kisasa.
Tatizo linaweza kutokea pale ambapo wafugaji wa kuku wa kisasa hawafuati taratibu za ufugaji na pengine hawawapi kuku vyakula muhimu wanavyohitaji au wanawapa dawa na vyakula visivyo bora kiafya, hivyo wakati mwingine kiini cha yai la kuku wa kisasa huonekana kupungua rangi ya njano kuliko kiini cha yai la kuku wa kienyeji.
Mtu anashauriwa kula yai bila kujali ni la kuku gani, kwa kutegemea ni yai lipi linapatikana kwa urahisi. Lakini nivizuri kula mayai ambayo yapo salama.
Tafakari na ujumbe huuuu!!!โฆ
DAKTARI :- Unajisikiaje?
CHIZI:-Kila siku naota nyani wanacheza mpira wa miguu.
DAKTARI :- Nitakupa dawa leo hautaota tena.
CHIZI:-hiyo dawa nipe kesho sababu leo wanacheza fainali. na nilibet
๐๐๐๐
Kuna mchepuko nilimtumia nauli jana ili aje,.kwang sasa leo kaniambia eti ” nimesahau ile line yenye M-pesa home plz nitumie tena kwa tigo mpenz””!! Me nikajifanya chizi nikatuma Kule kule kwenye voda (aliosema kaacha home) Nikatuma huko message ivi “nikuongezee Sh. Ngapi tena mpenz..!!” Akanjbu “elfu 20,000 tu mpenzi” Mtuhurumie jamani ๐๐๐
Viazi utamu 3
Nyanya 2 kubwa
Kitunguu
Tango
Limao
Chumvi
Pilipili
Mafuta (vegetable oil)
Menya viazi na kisha vikate katika vipande. Tia mafuta kwenye chuma cha kukaangia, yakisha pata moto tia viazi nauviache vikaangike mpaka upande mmoja uwe wa brown na kisha geuza upande wa pili na upike mpaka uwe wa brown. Vikisha iva ipua na uweke kwenye kitchen towel ili vikauke mafuta.
Kachumbali: Katakata vitunguu katika bakuli na kisha tia chumvi kwa ajili ya kuondoa ukali wa vitunguu. Baada ya hapo vioshe mpaka chumvi yote iishe. osha nyanya, Pilipili tango na kisha katakata slice nyembamba na uchanganye na vitunguu. Baada ya hapo tia chumvi, kamulia limao na uchanganye zote pamoja .Baada ya hapo viazi na kachumbali vitakuwa tayari kwa kuliwa.
Kuwa na nywele zenye afya nzuri ni muhimu kwa wote bila kujali jinsi, hali hii husababisha wengi kutumia madawa ya aina mbalimbali ya kuhakikisha nywele zao zinastawi na kuwa na muonekano mzuri.
Kwa bahati mbaya, wengi waliotumia madawa yanayotengenezwa kwa kemikali hujikuta katika wakati mgumu siku za usoni wakikabiliwa na matatizo ya nywele kukatika na hata kupata madhara katika ngozi ya kichwa.
Njia bora na salama zaidi ya kustawisha nywele, kuzifanya ziwe na mvuto wa aina yake bila kujali wewe ni mtu wa asili ya bara Asia, Afrika au Marekani, ni kula vyakula vyenye virutubisho muhimu kwa afya ya nywele.
Vifuatavyo ni sehemu ya vyakula ambavyo hupatikana kirahisi barani Afrika na kwa bei nafuu, ambavyo vitakupa afya bora zaidi ya nywele zako.
Nywele za binadamu zina protini ambayo zimeumbiwa. Hivyo ni muhimu kuhakikisha kuwa zina protini ya kutosha, na hilo hufanyika kupitia vyakula. Protini ni nguzo kuu ya nywele za binadamu, na yai ni moja kati ya vyakula vyenye utajiri mkubwa wa protini. Hakikisha unakula yai angalau mara tatu kwa wiki.
Nywele zinahitaji madini ya chuma ili ziweze kuwa katika hali nzuri ya afya. Kukosekana kwa madini ya chuma husababisha nywele kunyonyoka. Mwili unapokosa madini ya chuma, hewa ya oxygen na virutubisho hushindwa kufika vizuri kwenye mizizi ya nywele hivyo hufanya nywele kuwa dhaifu na zisizo na muonekano mzuri.
Mboga za majani aina ya spinachi ni suluhisho, kwakuwa zina madini ya chuma kwa wingi ambayo seli za nywele huhitaji.
Mwili wa binadamu huhitaji vitamini C ambayo husaidia kuhuisha utendaji wa madini ya chuma. Hivyo, unapaswa kuongeza matunda ya jamii ya โcitrusโ, kama vile machungwa, chenza, balungi na limao. Pia, unaweza kutumia na asali pamoja.
Vitamini C husaidia katika ukuaji wa nywele kusaidia usambaaji wa virutubisho na ukuaji wa haraka wa nywele.
Ni muhimu sana kuhakikisha unakunywa juice ya karoti kila siku, kama unataka nywele zako zikue haraka zikiwa na mwonekano mzuri wenye afya. Vitamini A inayopatikana kwenye karoti ni muhimu sana kwa ukuaji wa seli za nywele. Kumbuka nywele zina tishu ambazo hukua haraka zaidi katika mwili.
Karoti ina mafuta asili yanayofahamika kama โsebumโ na mizizi ambayo husaidia kukuza nywele kwa haraka.
Tunda aina ya parachichi lina kazi nyingi sana mwilini kama matunda mengine, lakini hili ni tunda la kipekee amnbalo lina utajiri wa vitamini E ambayo husaidia mzunguko wa damu na katika hilo husaidia mfumo wa ukuaji wa nywele kwa haraka.
Tunda hili husaidia kuhuisha na kurekebisha mafuta na kiwango cha PH (inayosafisha kemikalii mwilini) ambavyo kama vitazidi kwenye mwili vinaweza kusababisha kusimama kwa ukuaji wa nywele, yaani nywele hudumaa.
Kwa faida zaidi, vitamin E inayopatikana kwenye parachichi kwa wingi husaidia zaidi afya ya moyo wa binadamu na zaidi ngozi. Hakikisha unapata tunda hili kadiri iwezekanavyo.
Hivi ni baadhi tu ya vyakula na matunda kwa ukuaji mzuri wa nywele zako. Kama unatumia vizuri mlo wako, utakuwa adimu sana kutumia mafuta yenye kemikali ambayo yanaweza kukuletea madhara mabaya.
Baada ya kumaliza Degree yake ya sheria Bwana Rwegashora aliamua kurudi nyumbani Bukoba mjini na kufungua ofisi yake kwa ajili ya huduma kwa wateja.
Siku moja akiwa ndani ya ofisi yake alimuona mtanashati na mdada mmoja mrembo anakuja ofisini kwake akajua ni mteja anamletea kesi.
Ndipo akanyanyua mkoni wa wa simu ya TTCL na kuanza kuongea huku anajizunguusha kwenye kiti cha kuzunguuka.
Wakati mdada alipokaribia Rwegashora alimkaribisha kwa ishara maana alijifanya yupo busy na kuongea na simu ya umuhimu.
Wakati anaongea na simu akisikika akisema No, No, Noโฆ.. Absolutely No. Wajuulishe hao lay person wa New York kua siwezi kushuhulika na kesi ambayo itanilipa chini ya 50 million. Mimi ni profesional lawyer and im crossing the border to sarve international community.
Aka pose kidogo na akanywa maji kisha akaendeleaโฆ..
Naweza kuanza kukusanya primary evidence next weak but tell them watume kwanza ten million kwa kuanzaโฆ
Hahahahaha you dont know my Account
Mr Roger. Ok waambie watume kwenye Account ileile walionitumia million 100 last monthโฆ
Aka pose tena akameza fundo la maji na kurekebisha tai yake kisha akaendeleaโฆ Ok usisahau kumueleza muendesha mashtaka mkuu wa marekani kua nitakuja New York mwezi ujao maana nitapita kwanza Amsterdam kuwasilisha utetezi wa yule mteja wangu mholanzi kisha nitaenda Tokyo kulipia ile gari yangu niloagiza.
Wakati anaongea hayo yote yule mdada alikua ametulia na anamuangalia Bwana Rwegashora anavyojizunguusha kwenye
kiti chake huku akiongea kwa tambo kwenye ile simu ya TTCL.
Baada ya kumaliza kuongea na simu Bwana Rwegashora aliweka mkono wa simu yake ya TTCL chini kisha akamgeukia mdada mrembo.
Samahan sana kwa kukupotezea muda wako unajua tena kazi zetu zinaumiza kichwa sana kama unavyoona mwenyewe yaani niko busy sana ninapokea simu sana mpaka nimechoka na simu nyingi ni za wateja wa njee ya nchi.
Anyway nikusaidie nn? Mdada akajibu mimi ni mfanyakazi wa kampuni ya TTCL nimekuja kuunganisha line yako ya simu kwani haipo hewani tangu wiki iliyopitaโฆ!!!
Unadhani Bwana Rwegashora alifanyajeโฆ???
Mchele wa basmati – 3 vikombe
Kuku – ยฝ
Viazi – 4
Vitunguu – 2
Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa – 2 vijiko vya supu
Binzari ya pilau nzima – 1 Kijiko cha chakula
Binzari ya pilau – ยฝ kijiko cha chai
Pilipili manga nzima – ยฝ kijiko cha chai
Karafuu nzima – 8
Iliki nzima – 6
Mdalasini nzima – 5 vijiti
Pilipili mbichi iliyosagwa – 2
Chumvi – kiasi
Mafuta ya kupikia – ยผ kikombe
Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele.
Kata kuku vipande upendavyo, safisha kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu na tangawizi.
Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria.
Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi.
Tia thomu na tangawizi na binzari zote kaanga kidogo
Kisha tia viazi kanga kidogo kisha tia kisha tia vipande vyako vya kuku na supu acha ichemke kidogo kisha tia maji ukisie kutokana na mchele unaotumia.
Mwisho tia mchele koroga uchanganye na vitu vyote acha ichemke kiasi kisha funika na punguza moto mpaka uive (huku ukiugeuzageuza)
Ukishakuwa tayari pakua kwenye sahani tayari kwa kula na salad na pilipili.
Asthma /pumu ni ugonjwa sugu ambao huathiri njia ya hewa ambazo huingiza na kutoa hewa katika mapafu, pia hufanya kuta za ndani ya njia ya hewa kuvimba na hivyo hupunguza kiasi cha hewa kinachoingia na kutoka ktk mapafu, Hali hii husababisha mgonjwa kutoa mlio kama wa filimbi/mluzi wakati wa kupumua, kifua kubana, kushindwa kupumua vizuri na kukohoa sana, watu wa pumu huwa na dalil hizo nyakat za usiku na asubuhi sana pia ugonjwa huu huwaathiri watu wa Rika zote ingawaje Mara nying huwaathiri watoto kwa sababu huanza utoton na hivyo takriban MILION 6 ya watoto wanaumwa pumu na watu takriban 255,000 hufa kila mwaka kwa ugonjwa huu.
Hii ni aina ya pumu inayotokea baada ya mtoto kuzaliwa na kupata mzio (aleji) ambayo hupatkana katika vumbi la wadudu kama mende, pia manyoya ya wanyama kama paka, mbwa pia kutumia baby wipe zenye harufu na sabun zenye harufu kwa watoto huwa ni hatari.
Pumu hii hutokea kwa kuwa mwil wa mtoto hutengeneza Kinga ya mwil (ANTIBODIES) za IgE zinazosababisha pumu.
Ugonjwa wa pumu ni sugu sana kwa watoto wanaozaliwa na uzito mdogo wenye asili ya kiafrka pia pumu ya utotoni huwaathiri Zaidi watoto wa kiume.
Pumu hii huanza baada ya kufika miaka 20, PUMU hii huathiri Zaid wanawake kuliko wanaume na pia haitokei sana kama pumu ya utotoni, Vizio pia husababisha aina hii ya pumu kwa asilmia kubwa sana
Ikiwa utatokewa na Hali ya kukosa pumzi wakati wa mazoez au baada ya mazoezi inawezekana una pumu inayosababishwa na mazoezi pia hata kama sio mwanamichezo kukimbia kwa Kasi angalau dk 10 kunaweza kusababisha kukosa pumzi kwa muda mrefu.
Hii ni aina ya pumu iliyo ngumu kwa baadhi ya madaktari kuigundua kwa sababu katika pumu hii inawezekana isitokee hata dalil zingine Zaidi ya kukohoa tu hvyo madaktari wanalazimka kuchunguza Zaidi sababu zingne za kukohoa sana na kuhakiksha sio zinazosababishwa na kukohoa huko.
Aina hii ya pumu humtokea mtu akiwa mahali anapofanya Kazi pia huwatokea sana watumish wa viwandani ambapo kuna Moshi na gesi ya nitrogen oxide.
Pumu hii hutokea Kati ya saa sita usiku na saa 2 asubuhi, pumu hii huamshwa na vumbi, harufu za pafyum, harufu za rangi za nyumba na vinyes vya wanyama pia Mara nying wagonjwa wa pumu hii hushtuka usingizini wakat wa usiku wa manane baada ya kukosa pumzi.
Wakat wagonjwa wengi wakipata nafuu baada ya kupata steroid wachache hawapati unafuu na hvyo kuhitaj matibabu makubwa Zaidi.
Visababishi vya pumu havijulikani waziwazi ila vitu vinavyochangia pumu ni VIZIO mfano MOSHI WA SIGARA, BANGI, GESI, GARI NA KEMIKALI pia kila mgonjwa wa pumu ana mzio, Zaid ya 25%hupatwa na mafua yanayosababishwa na mzio (HIGH FEVER /ALLERGIC RHINITIS) na kuwashwa macho (ALLERGIC CONJUCTIVITY) pia wanaweza kupata pumu.
Pia mzio unaweza kusababishwa na antibodies zilizo ndani ya damu zinazopelekea njia ya hewa kuvimba na kusababisha pumu, pia Moshi wa SIGARA, MARASHI, NK husababisha pumu pia watu wazima wenye uzito unaozid vimo vyao yaani BMI Kat ya 25 na 30 na wanaopata pumu ukilinganisha na wenye mwili mkubwa pia watoto waliozaliwa kwa njia ya upasuaj na Zaidi watu walio katika stress na pia tatizo la ngozi linalosababishwa na mzio /allergc (ECZEMA /ATOPIC DERMATITIS au pumu ya ngozi ni hatar ktk jamii yetu.
Sio watu wote wenye pumu Wana Dalili HIZI na pia sio watu wote wenye Dalili hizi wana pumu.
~KUKOHOA SANA
~KUTOA SAUTI KAMA YA MLUZI /FILIMBI WAKAT WA KUPUMUA
~KUBANWA NA KIFUA
~KUPUNGUKIWA PUMZI
~kuna aina mbil za matibabu ya pumu moja ni ya dawa ambayo husaidia kutanua njia za hewa ambazo zimesinyaa (BRONCHOPDILATORS) pia na matibabu mengine ni kutumia dawa za kotikosteroid za kuvuta (INHALED CORTICOSTEROIDS) ila kwa kawaida matibabu haya huwa chanzo cha magonjwa mbalmbal kutokana na dawa za kemikal hivyo si nzur sana.
NI KUJIKINGA NA Vitu vyenye mzio Kama vile PERFUME, DAWA ZA KEMIKAL, RANGI ZA NYUMBA, KUVUTA SIGARA, PIA EPUKA KUNYWA POMBE NA KUCHEZA NA WANYAMA KAMA PAKA NA MBWA PIA WAZAZI MUACHE KUTUMIA BABY WIPES ZENYE HARUFU KWA WATOTO WENU.
Recent Comments