Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Una thamani gani?

Kazi au shughuli unayoifanya ina thamani gani kwa wengine?unawasaidia au unawaumiza??
Biashara unayoifanya ina thamani gani kwa wengine?ni lazima uwaumize ndipo ufaidike au uwasaidie ili nawe upate faida?

Elimu yako uliyo nayo ina faida au thamani gani kwako na kwa wengine?unawadharau na kujiona wewe ndiye msomi pekee au unawasaidia?

Una thamani gani kwa ndugu,jamaa,marafiki na majirani zako?unasaidiana nao katika kila kitu au unajiona wewe ndiye matawi ya juu unyenyekewe?

Una faida au thamani gani kwa wasiojiweza??umewahi kuwasaidia chochote?kuwatembelea watu wenye Shida mbalimbali kama wagonjwa,wafungwa nk

Kila unachokifanya kina thamani yoyote kwa wanaokuzunguka??
Kumbuka mafanikio ni kugusa maisha ya watu wengi kwa kuwasaidia wao kwanza wafanikiwe ndipo Baraka za mafanikio zitamwagika kwako.
Mafanikio sio wengine waumie ndipo uyaone mafanikio.

Jifunze kuwasaidia wengine waweze kutimiza malengo na ndoto zao ndipo nawe Mungu atakubariki kufikia ndoto zako.

Kumbuka kuna watu wengi wapo nyuma yako wanakusubiri wewe ubadilike ndipo nao waweze kuungana na wewe muweze kufanya kitu cha maana na chenye thamani kwa wengine.

Jinsi ya kupika Visheti

Viamba upishi

Unga 2 Vikombe

Samli au shortening ya mboga 2 Vijiko vya supu

Maziwa ¾ Kikombe

Iliki Kiasi

Mafuta ya kukarangia Kiasi

Shira

Sukari 1 Kikombe

Maji ¾ Kikombe

Vanila ½ Kijiko cha chai

Zafarani (ukipenda) Kiasi

Jinsi ya kupika na kuandaa

Katika kisufuria pasha moto maziwa na wakati huo huo chemsha Samli katika kisufuria kengine.
Tia unga katika bakuli na iliki, kisha mimina samli iliyochemka na huku unachanganya, kisha tia maziwa na uwendele kuchanganya vizuri isiwe na madonge, ikiwa maziwa haitoshi ongeza maji kidogo.
Kisha uwache unga ukae mahali pa joto kwa muda wa dakika 10 hivi.
Halafu fanya viduara vidogo vidogo, kisha finyiza kwenye greta yenye vishimo vidogo ili upate umbo kama kwenye picha.
Kisha karanga kwenye mafuta yaliyopata moto hadi vibadilike rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta.
Chemsha shira, ikiwa tayari mimina visheti na upepete na kuzichanganya zipate shira kote.
Weka kwenye sahani na zitakuwa tayari kwa kuliwa na kahawa.

Ushauri wangu kwa leo: Zingatia hili, hamasika, badilika

Tupo kwenye dunia ambayo tulikuta watu na tutawaacha watu.
Vyote tulivyovikuta vilianzishwa na binadamu wengine wenye mawazo mema na wenye mawazo mabaya pia. Vitu vingi tunavyovifanya tunaendeleza tulivyovikuta ni mara chache kukuta kitu kipya ambacho hakitegemei mazingira na asili ya tulivyovikuta.

Hivyo basi kwa vyovyote vile unahitaji mtu wa kukuongoza au kuku Coach ili ufanikiwe katika pande zote za maisha.

Nitakwenda kuzungumzia sehemu kuu tatu za muhimu sana ambazo unatakiwa uwe na watu wa kukuongoza ili uweze kukua na kupanda viwango kila wakati.

Ni vitu vya kawaida sana lakini leo nitakwenda kuzungumzia uone ilivyo muhimu sana wewe kua na vitu hivi maana bila vitu hivi mafanikio yatakua magumu sana kufikia. Safari yako itakua ngumu zaidi kama utakosea sehemu hizi tatu.

Nitaomba tuelewane kwamba hapa huendi kuiga au kuwa hawa watu utakua wewe na utatimiza lile kusudi la Mungu ndani yako.

Kwanza kabisa uko hivyo ulivyo kwa sababu ya mazingira uliyokulia na watu ulioishi nao tangu ukiwa mtoto hadi hapo ulipo.

Kuna tabia nyingi sana unazo kutokana na mazingira uliyokulia.

(Hapa ndipo nakutana na kitu ambacho nakipenda sana kujifunza kwa wengine napenda kujifunza kwenye mazingira mapya na kwa watu wapya kwa kua wameishi maisha ambayo mimi siyajui na wanafahamu vitu vingi ambavyo mimi sifahamu. Watu wana utajiri mwingi sana ndani yao ukiweza kukaa na mtu ambaye humjui kabisa unaweza kujifunza mambo mengi ya ajabu kwake. )

Hawa ndio watu wa Muhimu sana kwenye safari yako usiwakose ili uweze kusonga mbele.

Sifa zao kabla hujawachagua ni za muhimu sana pia ili wasije wakakupoteza badala ya kukufikisha kule unakotaka kwenda.

(a)Awe na mafanikio (Amefika Mbali) kwenye hiyo sehemu.

(b)Awe na Tabia njema zinazokubalika na jamii yake na dini yake. (mfano hapa ukikutana na mtu ambaye anakuelekeza kuhusu biashara na ni mlevi na mzinzi hizi tabia lazima atakuambukiza kwasababu atakua mtu wako wa karibu sana)

(c)Awe amekuzidi sana kwenye kile unachotaka akulelee (akuongoze).

Hizo ni sifa za muhimu tu za kuangalia zipo nyingine nyingi sana utajifunza mwenyewe.

1. Mlezi wako wa Kiroho

Huyu ni mtu wa muhimu sana na nimemweka wa kwanza.

Bila roho hakuna mwili.

Bila roho mwili wako unakua umekufa.

Unahitaji ukue kiroho na upande viwango kila wakati ili uweze kuvutia mafanikio ya nje.

Ukishindwa hapa hata ukiwa bilionaire inaweza kuwa kazi bure.

Hutaweza kuzifurahia hizo pesa.

Tafuta mtu wa kukulelea kiroho.

Mtu wa kukufundisha kumcha Mungu.

Kama huna katafute mtu wa kukulea kiroho sifa nimezitaja hapo juu.

Mtu huyu anatakiwa akufahamu vizuri na wewe umfahamu vizuri.

Yaani muwe na mahusiano ya karibu sana.

Mtu huyu awe anafuatilia maendeleo yako ya kiroho kwa karibu sana.

Haijalishi uko Dini gani lazima umpate mlezi wa roho yako.

Dini ndio inahusika kulisha roho zetu.
Ndio maana hatufundishwi biashara kule.

2. Mlezi wa Mahusiano/Uchumba/Ndoa

Hapa ni kwa muhimu sana.

Ukiwa vizuri kiroho mahusiano yakawa na tatizo hutafika mbali.

Ukiwa vizuri kiroho ndoa ikasumbua nayo ni tatizo.

Tafuta mtu wa kukulea kwa upande huu pia mtu aliefika mbele zaidi yako.

Aliefanikiwa zaidi yako.

Kama unatafuta mchumba tafuta mtu aliye kwenye ndoa na amefanikiwa.

Ukimtafuta single mwenzako atakupoteza😀.

Mtu huyu awe karibu yenu kabisa kulea mahusiano/ uchumba au ndoa yenu.

Hakuna aliyezaliwa anajua kila kitu tunajifunza hapa duniani kwa waliotutangulia na waliopo pia.

3. Mlezi wa Maono yako/Ndoto zako/Malengo yako/Biashara Yako/Pesa. (Coacher).

Mtu huyu ni wa muhimu pia katika maisha yako.

Unataka kumiliki utajiri wa dollar billion moja lazima utafute mtu wa kukulelea na kukuwezesha ufikie huko.

Huwezi kwenda mwenyewe.

Unahitaji mtu wa kukuongoza kwenye kila unachotaka kukifanya.

Wengi wanakata tamaa kwa kua hawana watu hawa wa kuwalelea.

Mtu huyu anatakiwa awe anakufuatilia hatua kwa hatua kwenye kile unachokifanya.

Awe anapata taarifa za maendeleo yako kila wakati ikiwezekana hata kila week.

Ukipata mafanikio yeyote ajue pia ukipata changamoto ajue.

Mtu huyu anatakiwa awe amekupita kwenye kile unachokitaka na hapa huendi kuwa Follower,anakwenda kukutengeneza wewe uwe kiongozi.

Uweze kusimama mwenyewe na hatimae uongoze wengine.

Kwa Tanzania wapo watu wanaofanya kazi hizi kwa malipo pia.

Lakini hapa unaweza kuanza na mtu ambaye una mahusiano nae ya karibu awe anakulelea.

Siku hizi teknolojia imekua rahisi sana unaweza kuwa na mawasiliano na mtu yeyote unayemtaka popote alipo duniani.

Unaweza kujifunza pia vitu vingi sana kupitia mitandao hii kama hapa facebook.

Unaweza kusoma vitabu na vitu vingi sana vile unavyovitaka.

Naomba nimalizie kwa kusema kwamba.
Kwa hiki ulichokipata leo ukikifanyia kazi.

Utakua mshindi uliyezaliwa kuwa.

Utafikia Hatma yako kwa kufuata haya, namaanisha wewe uliyesoma hapa.

I will see you at the top!

Baadhi ya misemo mikali ya leo

1. Mwanaume hata awe bahili vipi, hawezi kumpa mwanamke mimba nusu.

2. Hata uwe na magari mangapi chooni utaenda kwa miguu.

3. Kama ubinadamu kazi mbona hatupewi mishahara?

4. Ukichanganya wali na choroko unapata mseto, lakini hautibu malaria.

5. Hata njiwa nae ana makinda, lakini hawezi kuwa spika wa Bunge.

6. Hata uwe na haraka vipi kwenda Zenj, huwezi kupanda Jahazi ya Yusuph Mzee.

7. Umeme hauna kiuno lakini unaongoza kwa kukatika.

8. Hata uwe kauzu vipi, huwezi kujamba wakati unatongoza.

9. Hata uwe na imani kali vipi, huwezi kusali wakati unafanya mapenzi.

10. Hata kizibo ni mfuniko lakini hauwezi kufunika sufuria.

Faida za kula Karoti kiafya

Asilimia kubwa tunapenda kutumia karoti katika kuunga katika mboga ya nyama na si kuila karoti kama karoti. wataalamu wanashauri ili uwe na afya bora unatakiwa ule karoti sita kwa wiki au moja kwa siku. Unaweza kula karoti ya kuchemshaa,juisi au mbichi.

Zifuatazo ndizo faida za kutumia karoti;

·Karoti ina element ijulikanayo kama beta-carotene ambayo husaidia kupambana na kansa.

·Pia ni chanzo kizuri cha vitamin na husaidia kuongeza kinga ya mwili,

·Karoti ina vitamin A ambayo ina patikana kwa wingi husaidia kuongeza uwezo wa kuona na mawasiliano ya seli.

· Pia ina madini kama sodiam,sulphur,chlorine na iodine.

·Juisi ya caroti husaidia sana katika kutibu ngozi iliyo kauka na ulaji wa mara kwa mara hupunguza uwezo wa kupata vidonda vya tumbo pamoja na madhara mengine kwenye mfumo wa chakula.

Soma huyu mtoto anachosema sasa, Ndoto za watoto bwana! Kazi ipo!

Mwalimu aliingia darasani na kuwauliza wanafunzi juu ya ndoto zao za baadae.
MWAL: John we unataka ukiwa mkubwa uwe nani?
JOHN: Nataka niwe daktari wa moyo niwasaidie watanzania wanaougua magonjwa ya moyo.
MWAL: vizuri. Na wewe Rose unataka kuwa nani?

ROSE: Nataka kuwa rubani, niweze kusaidia watu wanapenda kusafiri kw anga.
MWAL: Safi sana Rose. Utakua utakua mfano kwa wasichana wenzio kuwa na bidii kwenye masomo ya sayansi.
MWAL: Na wewe Nehemiah ??
Nehemiah : mimi nataka kuwa tajiri mkubwa sana. Niwe na nyumba Tanzania, S.Africa, Marekani na Dubai. Niwe na gari 7 za kutembelea. Kila siku nabadilisha. Leo nikipanda hii, siirudii hadi week iishe. Nataka niwe namiliki viwanda, Makampuni, ndege binafsi na mashamba makubwa. Nataka niwe na nguvu serikalini ya kuamua nani awe Rais na nani asiwe……”
Akameza mate kisha akaendelea….
“Nataka kuwa na walinzi 20 wenye silaha nzito wakinizunguka, na watumishi wakininyenyekea. Nataka kuwa bilionea ninayeogopwa. Lakini pia nataka kuwa na mke mzuuuri sana ambaye nitakuwa natembea nae kila mahali.”
MWAL: ndoto nzuri sn lakini unahitaji bidii sana kutimiza. Haya na wewe Jenny tueleze unataka kuwa nani??
JENNY: Nataka kuwa mke wa Nehemiah .!!

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia asali

Asali hasa asali mbichi ya asili ni dawa nzuri sana ya kutibu chunusi. Asali ni antibiotiki ya asili ambayo husaidia kupunguza ukubwa wa chunusi na maumivu ya chunusi.

Asali inaweza pia kuzuia ngozi yako isipatwe na maambukizi mengine ambayo yangeweza kusababisha matatizo kwenye ngozi au makovu.

Hivyo asali inachukuliwa kama moja ya dawa za asili nzuri za kutibu chunusi unazotakiwa kuzijaribu.

Kwanza safisha ngozi yako vizuri na maji ya uvuguvugu kasha jipake asali moja kwa moja sehemu yenye chunusi. Iache kwenye ngozi kwa dakika 30 kisha jisafishe na maji safi ya uvuguvugu.

Hizi hapa, Aina 10 za ndoa usizozijua

Karibuni tuangalie aina hizi 10 za ndoa.

1. NDOA YA MKEKA

Inatokana na kufumaniwa na Binti wa watu.
Ndoa hii huwa Haina mahari. Hii huvunjika
mwaka mmoja tu,baada ya wanandoa kugundua
hawakuwa wakipendana!

2. NDOA YA MIHEMKO (NYEGE)

Hufungwa na vijana wenye umri wa miaka kati
mume18 mke 16.Huvunjika baada ya miaka 3 au
4 ya ndoa.

4. NDOA YA MAONYESHO

Wenye ndoa Hii hupenda kujionyesha
barabarani.Ila ndani hazina utii.Hupigana kila
wanaporudi kutoka kwenye mizunguko. Cha
kushangaza huwa hazivunjiki lakini ndiyo ndoa
zinazoongoza kwa kuchepuka!

5. NDOA YA UHAMISHO.

Hufungwa na watumishi wa vijijini na mjini. Ili wa
kijijini ahamie mjini.Mahari utoa anaetaka
kuhamia mjini. Hata kama mahari atatoa mume
lakini hii ndiyo ndoa yenye ukakasi
zaidi.Huvunjika mara tu wanapoanza kuishi wote
mjini. Salama ya hii ndoa ni kuhama kutoka mjini
kwenda kijijini.

6. NDOA YA MIMBA.

Hufungwa kwa sababu wanaoowana hawataki
kuonekana makwao kuwa wamezaa nje. Au
muolewaji alikuwa hampendi muoaji kwa
dhati.Muoaji hutumia mimba kama mtego wa
kuingia ndoani. Hii huvunjika mtoto akizaliwa na
kufikisha mwaka 1.

7. NDOA YA MALI (UTAJIRI)

Muolewaji miaka 18 au 28 Muoaji 65 au 70.Ndoa
hii pia huitwa ndoa ya babu na mjuukuu. Ndoa ya
aina hii hudumu, kwasababu mwenye kauli ni
mwenye mali. Asilimia kubwa ya waume wa ndoa
hizi hulea watoto wasio wao.

8. NDOA YA KWASABABU.

Hufungwa ili mradi muoaji au muolewaji
aonekane tu kwa jamii kuwa naye kaoa au
kaolewa.Huwa hazina utii wala upendo dhati.
Ndoa ya aina hii ikifikisha miaka 4 huwa
hazivunjiki wahusika huishi kwa mazoea.

9. NDOA YA UPENDO.

Ndoa hizi ziliishia mwaka 1978 kabla ya vita vya
kagera.Muoaji na muolewaji hawakuangalia vitu
ila utu tu ambao uliwaunganisha na kutengeneza
upendo wa kudumu. Hii ilidumu miaka yote.

10. NDOA KUCHUMA

Ndoa hii ufungwa ili mradi muoaji au muolewaji
akapate kitu au vitu fulani kutoka kwa upande
mmoja wapo. Hii hudumu miaka kadhaa
kutegemea na malengo ya mhusika. Wengine
husubiri mpaka mhusika afe,lkn hujikuta
wanakufa wao kwanza.
Kuwa mwangalifu!

Kwa nini Bikira Maria hakuwa anaombwa akiwa hai? Watu na mitume hawakuwa wanasali kumuomba yeye

Kwa hiyo Mitume na wakristu wa mwanzoni hawakuwa kumuomba wakati akiwa hai. Ila Baada ya Kifo chake na kupalizwa kwake Mbinguni walianza ibada kwake.

Kumbuka, Kifo cha Bikira Maria hakijaandikwa kwenye biblia kwa kua wakati anakufa vitabu vya biblia vilikua vimekwishaandikwa

Ndio maana anaitwa Mama wa Wakristu. Mama mbarikiwa

Rejea Ufunuo 12:1-17

Visababishi, dalili, matibabu na kinga ya presha ya kushuka

Hypotension ndio jina linalotumika kuelezea presha ya kushuka ambayo mpaka sasa chanzo chake hakijawa wazi. Kipimo cha presha huwa na namba mbili. Namba moja huwa juu na nyengine huwa chini. Hivyo basi namba ya juu kikawaida kwa mtu mzima inapaswa kuwa 100 hadi 139 na ya chini inapaswa kuwa 60 hadi 90. Hivyo basi pressure yako ikiwa chini ya 100/60 Ndio inajulikana kama Hyptension yaani pressure iko chini.

Hypotension (haipo juu). Kwa watu wengi presha hii huwatia kizunguzungu na kuwaangusha. Presha hii ikiwa ya muda mrefu husababisha mtu kupata maradhi ya mshtuko.Watu wenye afya nzuri, hasa wakimbiaji, presha ya kushuka huwa ni dalili ya uzima kwao.

Si rahisi kuziona dalili kwa mtu mwenye presha ya kushuka hata kama imedumu kwa muda mrefu. Mara nyingi matatizo ya kiafya huonekana pale mtu presha yake inaposhuka ghafla. Wakati huo wa matatizo ya kiafya, damu kidogo hufika katika ubongo. Hali hii humfanya mtu awe na kizunguzungu au kuumwa na kichwa.

Kushuka ghafla kwa presha mara nyingi humtokezea mtu pale anapofanya jambo la haraka kama mtu aliyekaa na kutaka kusimama mara moja. Kitaalamu presha hii inajulikana kama postural hypotension, orthostatic hypotension, au neurally mediated orthostatic hypotension.

Postural hypotension inachukuliwa ni hali ile ya kushindwa kwa mfumo wa mawasilianao unaojiendesha wenyewe mwilini kufanya kazi yake kikamilifu (autonomic nervous system). Mfumo huu huendesha na kuongoza vitendo visivyo vya hiari (involuntary vital actions), kama vile mapigo ya moyo kubadilika kutokana na jambo lililotokea kwa wakati uleopo.

Kwa kawaida unapoinuka, kiwango fulani cha damu yako kinakuwa kimebaki sehemu ya chini (miguuni). Kukiwa hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa na mwili wako, hali hii itasababisha presha yako kushuka. Katika hali hii mwili wako unafanya nini ?

Mwili wako unapeleka taarifa kwenye moyo na kuamuru uongeze usukumaji wa damu ambao utaizidi mishipa yako na kuifanya kuwa membamba hali itakayopelekea kuifanya presha yako kubakia ileile. Ikiwa jambo hili halikufanyika au limaefanyika polepole sana, presha yako itashuka ghafla. Hapa ndipo mtu unapomuona anaguka ghafla.

Kwa ufupi athari ya maradhi ya presha ya kushuka na ya juu huongezeka kadri mtu anapokuwa na umri mkubwa na pia kubadilikabadilika kadri umri unavyoongezeka. Jambo jingine la kufahamu ni kuwa, ufikaji wa damu kikawaida kwenye ubungo unapungua kadri umri unavyoongezeka. Inakisiwa kiasi cha asilimia 10 mpaka 20 ya watu wenye umri unaozidi miaka 65, wanapata tatizo la presha yao kushuka.

Ni kiwango gani cha presha kinapofika ndio huwa maradhi ?

Hakuna kiwango maalum kinachojulikana ambacho ni sawasawa kwa watu wote kikifika ndio kinaitwa maradhi. Kiwango ambacho kwako ndio uzima, basi huenda kwa mwenzako ikawa ni maradhi. Katika presha ya kushuka, madaktari wengi huchukulia kuwa tayari mtu ana maradhi pale aambapo kiwango chake cha presha kinafuatana na dali za maradhi yenyewe.

Hata hivyo, baadhi ya wataalamu wanachukulia tayari mtu ana maradhi ya presha ya kushika pale vipimo vinapoonyesha kiwango hichi 90/60 mm Hg. Tufahamu kuwa kiwango cha namba inayosomwa chini katika kipimo cha presha (… /60 mm Hg ), hichi huonyesha tayari mtu huyu anapresha ya chini hata kama kile cha juu ( 90/…mm Hg) kina namba iliyozidi 100.

Mfano ikiwa umepimwa presha na ukapata kipimo hichi 115/60 mm Hg, presha yako itakuwa ipo chini. Na kama umepata kipimo hichi 115/50 mm Hg, sio kwamba presha yako itakuwa ipo chini tu, bali presha hii itakuwa si ya kawaida.

Dalili za maradhi

Kama nilivyokwisha tangulia kusema, presha inaweza kuwa sawa kati ya watu wawili lakini ikawa na matokeo tofauti. Presha hiyo inayoweza kuwa sawa na ikawa na matokeo tofauti si yenye kipimo hichi 120/80 mm Hg. Presha yenye kipimo hichi 120/80 mm Hg, ndiyo nzuri na watu wenye presha hii wanakuwa na afya nzuri. Kitu muhimu ni kujua, mabadiliko gani yanaleta tatizo katika presha hata inapelekea kuwa si ya kawaida.

Presha nyingi za watu wanapopimwa huwa zinakuwa kati ya 90/60 mm Hg (presha iliyo chini) mpaka 130/80 mm Hg (presha iliyo juu). Mabadiliko ya kushuka presha upande wa chini, hata kama kidogo kiasi cha 20 mm Hg, hupelekea matatizo kwa baadhi ya watu ( hasa watu wasiofanya mazoezi kila siku).

Mtu mwenye mazoezi ambaye presha yake nzuri (120/80 mm Hg) akapimwa presha na kupata kipimo hichi, 110/60 mm au 120/70 mm Hg, mtu huyu hatakuwa na tatizo lolote la presha
Kuna aina tatu za presha ya kushuka :

Orthostatic sambamba na postprandial orthostatic (Orthostatic hypotension, including postprandial orthostatic hypotension)

Orthostatic, hii ni aina ya kwanza ya presha inayosababishwa na kubadili mazingira uliyonayo kwa ghafla, maranyingi hutokea kwa mtu anayesimama kutoka alipolala. Presha hii haidumu muda mrefu, kiasi cha sekunde chache mpaka dakika moja. Ikiwa presha hii itatokeze. baada ya kula, basi itakuwa ni hatua ya pili (postprandial orthostatic) .

Hatua hii ya pili huwapata zaidi wazee na wenye presha ya juu.

Neurally mediated hypotension (NMH)

NMH kama ilivyo kifupisho cha presha aina ya pili, huwapata zaidi vijana na watoto. Presha hii hutokea pale mtu anaposimama kwa muda mrefu. Maranyingi huwapata sana watoto.

Aina hii ya pili ya presha ya kushuka maranyingi husababishwa na hali zifuatazo :

  1. Utumiaji wa pombe
  2. Utumiaji wa dawa za kutibu presha ya juu.
  3. Utumiaji wa dawa za kumtoa fahamu mtu wakati wa kufanyiwa upasuaji

Mambo mengine yanayosababisha presha kushuka ni pamoja na :

  1. Ugonjwa wa Kusukari
  2. Mtu kula kitu kinachomdhuru
  3. Mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida
  4. Maradhi ya kuharisha
  5. Kuzimia
  6. Maradhi ya moyo
  7. Maradhi ya kustuka

Severe hypotension hii ni aina ya tatu ya presha ya kushuka ambayo hutokana na kupoteza damu
Kwa muhtasari, dalili za presha ya kushuka ni pamoja na :

  1. Kuona kizunguzungu/kuumwa na kichwa kusiko kuwa kukubwa
  2. Kuzimia
  3. Kushindwa kuzingatia
  4. Kushindwa kuona vizuri ghafla
  5. Kuona baridi,
  6. Kujihisi kuchoka sana
  7. Kuvuta pumzi kwa tabu
  8. Kutapika
  9. Kuhisi kiu

Hali zinazosababisha kupata presha ya kushuka.

Kinachosababisha presha ya chini bado hakijatambulika hasa. Chanzo chake hakiko wazi. Hata hivyo mambo yafuatayo yanaweza kuhusiswa nayo :

  1. Kuwa na mimba
  2. Matatizo ya homoni mwilini, maradhi ya kisukari, au upungufu wa sukari mwilini
  3. Utumiaji mkubwa wa dawa
  4. Ulaji wa dawa za presha unaopindukia kiwango (Overdose) kwa mtu mwenye presha ya juu.
  5. Maradhi ya moyo
  6. Maradhi ya figo

Nani anapata presha ya kushuka ghafla ?

Presha ya kushuka ghafla inayompata mtu anapoinuka ghafla, inaweza kumpata mtu yeyote kwa sababu tofauti zikiwemo,

  1. kuharisha sana,
  2. kukosa chakula ( njaa kali) kwa muda mrefu,
  3. kusimama kwa mapigo ya moyo, au
  4. kuchoka kupita kiasi.
  5. Pia inawezekana ikawa ni urithi wa maradhi,
  6. Umri mkubwa,
  7. Matumizi ya dawa,
  8. Utapiamlo na mambo mengine kama kupatwa na madhara ya jambo fulani.

Nini kinaifanya presha inayoshuka iendelee ?

Pia Presha ya kushuka mara nyingi huwapata watu wanaotumia dawa kwa kutibu presha ya juu (hypertension). Pia huwapata wajawazito au wagonjwa wa kisukari. Mara nyingi wazee nao hupata maradhi haya hasa wale walio na presha ya juu wakiwa wanaendelea kutumia dawa zao za presha.

Baadhi ya maradhi ambayo yanasababisha presha kushuka kuendelea ni pamoja na;

  1. Ukosefu wa vitamin mwilini,
  2. Madhara kwenye uti wa mgongo, na
  3. Kansa hasa kansa ya mapafu.

Wakati gani wa kuchukua hatua za matibabu

Matibabu huanza na hatua zako wewe mwenyewe. Wakati utakapojiona presha yako inashuka, kaa chini au lala chali na unyanyue miguu yako juu. Wakati yanafanyika haya, ufanyike utaratibu wa kuonana na daktari haraka.

Pia ufanyike utaratibu wa kuonana na daktari yanapoonekana mambo yafuatayo yamemkuta mtu :

  1. Maumivu ya kifua
  2. Kizunguzungu
  3. Kuzimia
  4. Homa kali sana
  5. Mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida
  6. Kupumua kwa tabu

Pia afuatwe daktari haraka ikiwa baada ya hayo yaliyotokea, kuongezeka na haya yafuatayo :

  1. Mtu anapata matatizo makubwa ya mkojo
  2. Kushinwa kula au kunywa chochote
  3. Kuendelea kuharisha au kutapika kwa muda mrefu

Matibabu na Dawa

Presha ya kushuka ambayo haijulikani chanzo chake wala haileti dalili au inampa mtu kizunguzungu anaposimama, mara chache inaweza kutafutiwa matibabu. Ikiwa zipo dalili, matibabu yataendana na chanzo chenyewe na daktari atashughulikia hicho chanzo. ( kuharisha,maradhi ya moyo, kisukari). Ikiwa presha ya chini imesababishwa na matumizi ya dawa kwa matibabu, basi matibabu yake huwa kubadili dawa nyingine ua kuacha kutumia dawa kabisa.

Ikiwa hakuna uhakika wa sababu za presha ya kushuka au hayapatikani matibabu yaliyo sahihi, matibabu sahihi yatakuwa ni kuifanya presha yako ipande na kuondoa zile dalili zanazokupata inapokujia.

Kwa kutegemea umri wako, hali yako ya kiafya na aina ya presha uliyonayo, mambo haya yanaweza kukusaidia :

Kuongeza matumizi ya chumvi. Matumizi ya chumvi lazima yawe kwa kipimo, kwani chumvi nyingi hupandisha presha. Kabla hujaanza kuongeza matumizi ya chumvi, ni vizuri uwasiliane na daktari ili akupe kiwango cha matumizi.

Kunywa maji mengi. Kunywa maji mengi kunamsaidia kila mtu sio mtu mwenye presha ya chini tu. Tunapozungumzia maji tunalenga zaidi vinywaji na sio maji peke yake, lakini vinywaji vyenyewe viwe ni maji, maji ya matunda maziwa na hata kahawa au chai. Tahadhari ichukuliwe kwa vinywaji vya viwandani kwani huwaletea matatizo baadhi ya watu.

Kuvaa mavazi yenye kubana. Haya ni mavazi ya mpira ambayo yanavaliwa sehemu za miguuni. Mavazi haya yanasaidia kufanya damu yako isikae miguuni na iendelee kwenye mzonguko wake kikawaida.

Matumizi ya dawa. Zipo dawa mbalimbali ambazo zinatumika kufuatana na hali ya presha uliyonayo.

Matibabu hospitalini.

Presha ya kushuka inayomtokezea mtu mwenye afya nzuri ambayo haina dalili zozote na haimletei matatizo yeyote, hatahitajika kutumia dawa. Ikiwa zipo dalili, atahitaji matibabu kutokana na hizo dalili zilizoonekana. Ikiwa presha ulokuwa nayo inatokana na matumizi ya dawa, daktari atakubadilishia dawa nyengine au utaacha matumizi ya dawa. Wale wenye NMH pamoja na matumizi ya dawa, inabidi waache tabia ya kusimama muda mrefu. Kimtazamo presha ya chini inatibika hata kufikia mtu kuwa na presha ya kawaida.

Napenda nichukue nafasi hii kuwafahamisha kuwa, bila kubadili mfumo wa maisha ulionao, hata ukikusanyiwa dawa nzuri za dunia nzima kwa kutibu maradhi yako hutopata uzima wowote. Kubadili mfumo wa maisha si katika kuishughulikia presha tu, bali kwa maradhi yote ndio

Tiba sahihi. Nini dawa zinafanya?. Dawa zinalazimisha kuurudisha mfumo katika hali yake ya kawaida tu. Baada ya dawa kutoa msaada wake huu, kinachotakiwa kwako wewe kuendeleza mfumo huo unaofaa ambao dawa zimekurudishia tena.
Kwa kutegemea sababu za kupata presha uliyonayo, unaweza kuchukua hatua zifuatazo :

Kunywa maji mengi, kuacha kunywa pombe, Kula vyakula kiafya (kula nafaka, matunda, mbogamboga, kula mifupa ya samaki na hata ya ndege[kuku,njiwa nk]) Tupendelee kuku wa kienyeji zaidi. Ikiwa kuongeza chumvi katika chakula, basi usizidishe vijiko viwili vya chai kwa siku na ni vizuri sana upate ushauri kwa daktari.

Kujenga utamaduni wa kuinuka taratibu ulipo kaa ua kulala. kulalia mto, ikiwa unapenda kunalalia ubavu, pendelea kulalia upande wa kulia (kila unapozungumzia presha, basi jambo la kwanza la kukumbuka ni moyo, moyo wako uko upande wa kushoto, kitendo cha kulalia upande wa kushoto kinaweza kuupa tabu moyo katika utendaji wake wa kazi).

Kuwa na tabia ya kula chakula kidogo katika mlo wako. Kufanya hivyo kunasaidia presha yako kutoshuka baada ya kumaliza kula. Jipangie utaratibu wa kula mara kwa mara ili uweze kula chakula cha kutosha. Punguza kula vyakula vyenye uwanga kwa wingi kama vile, mbatata, wali na mikate. Kula chakula pamoja na chai au kahawa. Ni vizuri haya yote utakayoyafanya ukawasiliana na daktari kabla.

Kinga ya presha ya kushuka.

Ikiwa wewe ni mzima au tayari una presha ya kushuka, Daktari atakushauri hatua za kuzuia isitokee au isiendelee au kuipunguza. Hatua hizo ni pamoja na :
1. Kuacha unywaji wa pombe.
2. Kuepuka kusimama muda mrefu ( hasa ikiwa tayari una NMH)
3. Kunywa maji kwa wingi
4. Kuinuka taratibu kutoka ulipokaa ua kulala
5. Kuvaa mavazi ya kubana miguuni (ikiwa tayari unayo)

Jinsi ya kuandaa Pilau ya sosi ya soya, nyama na mboga

Mahitaji

Nyama isiyokuwa na mifupa – 1 ½ Lb(ratili)
Mchele wa Basmati (rowanisha) – 3 Magi
Vitunguu maji – 2
Mchanganyiko wa mboga za barafu – 1 Magi
(karoti, mahindi, njegere)
Pilipili Mbichi – 3
Pilipili mboga kijani na nyekundu – 1
Pilipili manga – ½ kijiko cha chai
Chumvi – Kiasi
Sosi ya soya (soy sauce) – 5 Vijiko vya supu
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa – 1 Kijiko cha supu
Mchanganyiko wa bizari (garam masala) – 1 Kijiko cha supu
Kotmiri iliyokatwa – ½ Kikombe
Mafuta ya kukaangia – Kiasi

Namna Ya Kutaarisha

Ndani ya sufuria, tia mafuta yakipata moto kaanga vitunguu mpaka ziwe rangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama iliyokatwa vipande vidogo vidogo pamoja na maji ya kiasi na viungo vyote isipokuwa mchele, mboga zote na kotmiri. chemsha mpaka nyama iwive na maji yakauke.
Halafu changanya na mboga na iwache kwa muda wa dakika kumi kisha tia kotmiri na umimine kwenye bakuli au treya ya oveni na uweke kando.
Chemsha mchele na chumvi uwive kama kawaida ya kupika wali wa kuchuja, kisha umwagie juu ya ile treya ya nyama.
Nyunyizia mafuta na sosi ya soya na ipike katika oveni moto wa 350° kwa muda wa dakika 20 hivi.
Ukishawiva, uchanganye ukiwa tayari kwa kuliwa

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Ya Keki Kavu (Shortcake)

VIAMBAUPISHI

Unga – 2 Magi (vikombe vya chai)

Sukari iliyosagwa – 2/3 Magi (kikombe cha chai)

Siagi – 220 g

Unga wa mchele – ½ Magi

Yai -1

Vanilla – 1 kijiko cha chai

MAANDALIZI

Changanya vitu vyote hivyo kwenye bakuli mpaka unga ushikamane.
Paka mafuta treya ya kuchomea kisha utandaze kwenye treya ya 20cm kwa 30 cm au (8 in kwa 12 in)
Choma kwenye moto 325˚C kwa muda wa saa nzima au mpaka ibadilike kuwa rangi ya dhahabu.
Epua acha ipoe kisha kata vipande kama mstatili, weak kwenye sahani tayari kunywewa na chai.

NYONGEZA

Kwa unga huo huo unaweza kutengeneza vibiskuti vya duara duara.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About