Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Cheki huyu jamaa alivyoumbuka kwenye harusi

Jamaa mmoja alialikwa ktk harusi. Akafika mlango Wa 1 umeandikwa kulia ni ndugu Wa maharusi, kushoto ni wageni waalikwa, akaenda kushoto maana yy alialikwa. Akakuta mlango wa2 umeandikwa kulia wenye zawadi kushoto wasionazawadi yy hakuwa na zawadi. Mlango Wa 3 umeandikwa kulia wanawake kushoto waume akapita kushoto akajikuta ametokea mtaani

๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„. Tujifunze kutoa wandugu

*hatupendagi ujinga sisi*
๐Ÿšถ๐Ÿฟ๐Ÿšถ๐Ÿฟ๐Ÿšถ๐Ÿฟ๐Ÿšถ๐Ÿฟ๐Ÿšถ๐Ÿฟ๐Ÿšถ๐Ÿฟ๐Ÿšถ๐Ÿฟ

Karibu Ujitafakari: Kwa nini Unasali na Kumuabudu Mungu? Jifunze Kitu Hapa

Utangulizi

Embu tafakari kwa nini unasali na Kumuabudu Mungu!

Je unasali kwa hofu ya kutokua na uhakika na maisha?

Je unasali kwa sababu ya shida na matatizo katika maisha?

Je unasali kwa kuwa unaona wengine wanasali kwa hiyo unafikiri na wewe lazima usali?

Je unasali kwa kuwa unamwogopa Mungu?

Je unasali na kuabudu kama kutimiza wajibu katika dini au kanisa lako?

Je Unasali kutimiza wajibu kama kiumbe kwa Mungu?

Je unasali kwa kuwa unapenda Kusali?

Je unasali kwa kuwa Unampenda Mungu?

Je unasali kwa kuwa Unampenda Mungu na unaona ni wajibu wako Kusali?

Je unasali kwa kuwa Unampenda Mungu na unaona ni njia ya kujenga mahusiano na Mungu?

Je unasali na Kumuabudu Mungu kwa kuwa unajisikia vibaya kwa kuwa unaona wengine hawasali kwa hiyo unataka kumfariji Mungu kwa sala zako?

Tafakari uko wapi wewe?

Tafakari Maisha Yako ya Sala: Jiulize Maswali Haya

Katika maisha yetu ya kiroho, sala na ibada ni sehemu muhimu. Lakini je, umewahi kutafakari kwa nini unasali na kumwabudu Mungu? Hebu tuingie ndani ya mioyo yetu na kujitafakari kwa undani. Jiulize maswali haya ili kujielewa vizuri na kuboresha uhusiano wako na Mungu.

Je, Unasali kwa Hofu ya Kutokuwa na Uhakika na Maisha?

Wakati mwingine, tunaweza kujikuta tunasali kwa sababu ya hofu โ€“ hofu ya kesho, hofu ya hali ya kifedha, hofu ya magonjwa. Je, sala yako inachochewa na hofu hii? Ni muhimu kutambua kuwa Mungu anatuita tuje kwake si kwa sababu ya hofu, bali kwa sababu ya upendo na imani. Tafakari, je, sala zako zinakutoka kwa moyo wa hofu au moyo wa imani?

Je, Unasali kwa Sababu ya Shida na Matatizo Katika Maisha?

Mara nyingi, matatizo na changamoto za maisha zinatusukuma kuingia kwenye sala. Ni kawaida na ni sahihi kutafuta msaada wa Mungu wakati wa dhiki. Lakini je, sala zako ni za kudumu hata wakati mambo yakiwa mazuri? Mungu anataka uhusiano wa kudumu na wewe, si wakati wa matatizo tu bali pia wakati wa furaha. Tafakari, je, unasali tu unapokuwa na matatizo?

Je, Unasali kwa Kuwa Unaona Wengine Wanasali?

Katika jamii zetu, tunaweza kushawishika kufuata mkumbo. Unapoona wengine wakisali, je, unajikuta unasali kwa sababu tu na wewe unataka kuwa kama wao? Ni muhimu kujua kwamba sala ni uhusiano binafsi kati yako na Mungu. Sali kwa sababu unataka kuzungumza na Mungu, sio kwa sababu wengine wanasali. Tafakari, je, sala yako inatokana na msukumo wa ndani au ni kwa sababu ya wengine?

Je, Unasali kwa Kuwa Unamwogopa Mungu?

Hofu ya Mungu ni kitu cha kawaida, lakini Mungu hataki tuwe na hofu inayotutenga naye. Badala yake, anataka tuwe na hofu ya heshima inayotufanya tumkaribie zaidi. Je, unasali kwa kuwa unamwogopa Mungu au unamsali kwa sababu unampenda? Tafakari, je, hofu yako inakupeleka mbali na Mungu au inakukaribisha karibu naye?

Je, Unasali na Kuabudu Kama Kutimiza Wajibu Katika Dini au Kanisa Lako?

Wakati mwingine, tunaweza kujikuta tunatimiza wajibu wa kidini kama sehemu ya ibada zetu. Ni muhimu kutambua kuwa ibada na sala si tu wajibu, bali ni njia ya kuimarisha uhusiano wetu na Mungu. Je, unasali kwa sababu ni wajibu wa kidini au ni kwa sababu ya upendo wako kwa Mungu? Tafakari, je, sala zako ni sehemu ya utaratibu tu au zinatokana na moyo wako?

Je, Unasali kwa Kuwa Unapenda Kusali?

Sala inapaswa kuwa ni tendo la upendo na shauku. Unapenda kusali kwa sababu unapenda kuzungumza na Mungu. Kama unasali kwa sababu unapenda kusali, basi unafanya jambo sahihi. Tafakari, je, unasali kwa shauku na upendo au kwa sababu ya kawaida?

Je, Unasali kwa Kuwa Unampenda Mungu?

Upendo ni msingi wa imani yetu. Je, sala zako zinatokana na upendo wako kwa Mungu? Kama unampenda Mungu, basi sala zako zitakuwa na nguvu na maana zaidi. Tafakari, je, unasali kwa upendo wa dhati kwa Mungu?

Je, Unasali kwa Kuwa Unaona Ni Wajibu Wako Kusali?

Kama kiumbe cha Mungu, ni wajibu wetu kusali na kumwabudu. Lakini wajibu huu unapaswa kutoka moyoni, si kwa kulazimishwa. Je, unahisi ni wajibu wako kusali kwa sababu unampenda Mungu? Tafakari, je, wajibu wako unakufanya usali kwa moyo mkunjufu?

Je, Unasali kwa Kuwa Unaona Ni Njia ya Kujenga Mahusiano na Mungu?

Sala ni njia bora ya kujenga na kuimarisha uhusiano wetu na Mungu. Unapozungumza na Mungu kupitia sala, unajenga daraja la upendo na imani. Tafakari, je, unasali kwa lengo la kujenga mahusiano ya karibu na Mungu?

Je, Unasali kwa Kuwa Unajisikia Vibaya kwa Kuona Wengine Hawasali?

Wakati mwingine, tunaweza kujisikia vibaya kuona wengine hawasali. Unaweza kujikuta unasali kwa bidii zaidi ili kumfariji Mungu kwa niaba ya wale ambao hawasali. Hii ni ishara ya upendo na kujali, lakini ni muhimu kuhakikisha kwamba sala zako zinatoka moyoni. Tafakari, je, unasali kwa bidii ili kumfariji Mungu au kwa sababu ya upendo wako binafsi?

Tafakari Uko Wapi Wewe

Tafakari maisha yako ya sala. Jiulize maswali haya kwa dhati na uone ni wapi ulipo katika uhusiano wako na Mungu. Sala ni uhusiano binafsi na Mungu. Ni njia ya kuzungumza na Yeye, kumshukuru, kumuomba msaada na kuelezea upendo wetu kwake. Jitafakari, jichunguze, na ujitahidi kuboresha maisha yako ya sala ili yawe na maana na nguvu zaidi. Mungu anakuita katika uhusiano wa dhati na wa kweli. Tafakari, uko wapi wewe?

Maujanja ya kumkalisha mwanamme wako nyumbani weekend haya hapa

Siku hizi wa naume licha ya kukimbia nyumba zao kwa kisingizio cha kazi maajabu weekend hasa Jumamosi utasikia wanaaga nafika hapo njiani naja naenda kununua gazeti.

Kumbe wanaenda kunywa supu unasubiri wee mpaka alasiri au jioni

Hivyo wanandoa wengi hili limekuwa tatizo mwanaume kiguu na njia asb mchana na njia kumuacha mama na watoto.

Nini kifanyike hasa weekenda Mwanaume ashinde NYUMBANI akikupumzikia??

Zipo njia nyingi mojawapo SUPU YA WEEKEND NA MAZUNGUMZO NA MKAO

Ni kweli wanawake wengi hamjuagi kuwakalisha waume home.

Anza hivi
Siku uko home wewe amka mapema kabla yake anza makeke jikoniโ€ฆ

Mara blenda priiiiiโ€ฆ juiceโ€ฆ ama milk shakeโ€ฆ. hahahaha..Utaona anasogea jikoni..

Wakati anakunywa juice ama milk shakeโ€ฆAnza kukuna naziโ€ฆ

Chambua mnafuโ€ฆ

Hapo jikoni kuna kanyama kanachemkaโ€ฆ katia kitunguu tupia viazi 2 na ndizi.Hahaha..

ile harufu ikianza kutoka utasikia anafuata maji jikoniโ€ฆ hahahaha kwenye frijiโ€ฆ wala hatumi..

Hahaahhaโ€ฆ utasikia nini kiko jikoni?Hahahaa.

Mmiminie supuโ€ฆ

Na ndizi mbili na kiazi kimoja kapilipili mbuzi pembeni..

Muulize kuna chapatiโ€ฆMpe.. hahahahaha..Akimaliza supu nakuapia atasinzia..

.Akishtuka ugali na mnafu na nyama umeivaโ€ฆMpe ale..Mshushie na glass ya mtindiโ€ฆHahahaha..

analewa full Hata kama kuna mama junior anaambiwa usipigeโ€ฆ

Hahahahahahaโ€ฆ.Baada ya hapo acha apumzikeโ€ฆ aogeโ€ฆ

Kisha funga ka khanga kako kepesi jilaze pembeni.. woiiiiiiiii..

Mkimaliza muombe pesa ya sokoniโ€ฆ

NAKUAPIA HATA KAMA JANA YAKE ALIKUPA ATAKUPA TENA.

Hahahahaha.. jamaniโ€ฆ

Hahahahahaโ€ฆ yani kwa raha ya supuโ€ฆ nakuapia utaambiwa hata mama alipiga simu janaโ€ฆ hahahaha.. ama utasikia mamii.. njoo uone njooโ€ฆ unaitiwa kitu cha kwenye tv.. hahaha.

Hata hujaona mwanzo ila kwa raha yakasupu utaitwaโ€ฆ

Hata kama huna kalio nakuambia utapigwa kibao hata cha mgongoโ€ฆ. hahahahahahahahahaha.

Sasa wewe unaamka chai na mkate kama chuo cha uhaziliโ€ฆ
Wali maharage kama jeshi la j

Jinsi ya kupika Biskuti Za Njugu/Matunda Makavu (Rock Cakes)

Viambaupishi

Unga 4 Vikombe

Sukari 10 Ounce

Siagi 10 Ounce

Mdalasini ya unga 2 vijiko vya chai

Matunda makavu/njugu (kama lozi,
Zabibu, maganda ya chungwa,
Cherries na kadhalika 4 ounce

Maziwa ya maji 4 Vijiko vya supu

Jinsi ya kuandaa na kupika

1) Chukua siagi na sukari koroga na mixer mpaka iwe kama cream.

2) Tia vanilla mdalasini, tia yai moja mix tena endelea kuongeza yai lingine mpaka umalize yote, changanya mpaka iwe laini kama sufi (fluffy)

3) Tia unga na baking powder na dried fruits, changanya na mwiko.

4) Chota mchanganyiko na kijiko cha soup weka kwenye treya ya kupikia tandaza na uma ili upate matundu juu ya biskuti.

5) Pika (bake) kwenye oven lenye moto wa 375ย F. kwa muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama.

Mambo ya Kuzingatia ili uwe na ngozi laini

Takribani kila mtu angependa kuwa na ngozi laini, au hata laini zaidi. Watu wengi wamekuwa wakiitafuta ngozi nzuri au kujitahidi kuitunza ili isiharibike. Lakini je, wamefanikiwa?
Wachache hufanikiwa na wengi hushindwa. Na hata hao waliofanikiwa wengi wao hutumia vipodozi vikali ambavyo vingi huchubua na kuharibu ngozi zao na kuwaletea madhara makubwa sana baadae.

Vipi wewe, ungependa kuwa na ngozi nzuri bila kuidhuru afya yako? Karibu somo la leo ili uweze kuwa na ngozi nzuri bila kuidhuru afya yako.

Ngozi laini ni nzuri na inaongeza mvuto wa mwili. Ulaini wa ngozi hupotezwa na mambo mbalimbali kama vile seli za ngozi kupungukiwa na maji na kuanza kusinyaa na kunyauka, seli za ngozi kujeruhiwa, na seli za ngozi kufa. Matokeo yake ni michirizi, makunyanzi, makovu, chunusi, madoa, ngozi kufubaa na kuzeeka.

Kuifanya ngozi kuwa laini unahitaji kuupatia mwili virutubisho vyote vya kujenga mwili vizuri na kunywa maji ya kutosha ili seli zisikauke, kusinyaa wala kunyauka. Kula mlo kamili, matunda mengi na kunywa maji ya kutosha.

Pia unahitaji kuepuka jua kali ambalo litaunguza ngozi, kuikausha na kuifanya iwe na makunyanzi na vitu vingine vinavyoota kwenye ngozi kutokana na jua.

Tumia vipodozi vizuri vinavyosaidia ngozi kuwa laini bila kuidhuru. Hapa kuna vipodozi vya aina mbali mbali na vinavyofanya kazi kwa njia mbali mbali. Vipodozi vya muhimu ni

  1. Vipodozi vya kuongeza unyevu au maji kwenye (seli za) ngozi
  2. Kwa kiingereza vinaitwa โ€œMoisturizersโ€. Hivi hufanya kazi ya kufunika ngozi na kuzuia maji yasipotee kutoka kwenye ngozi, na pia husaidia kuongea maji kuingia kwenye seli za ngozi. Vipo katika mtindo wa sabuni, mafuta na losheni.
  3. Vipodozi vya kusaidia kuongeza kasi ya kuzalishwa kwa seli mpya za ngozi
  4. Hivi husaidia kuzalisha seli mpya za ngozi ambazo zitaleta ngozi mpya na nzuri na kuondoa ile ya zamani iliyochoka na kuzeeka. Mifano ni losheni na krimu zenye Vitamini A na Vitamini E.
  5. Vipodozi vya kusaidia kuondoa uchafu na seli (ngozi) zilizozeeka au kufa

Tumia sabuni zenye uwezo mkubwa wa kuondoa uchafu kutoka kwenye ngozi, na ukiweza tumia โ€œface washโ€ au โ€œfacial cleansersโ€. Hivi husaidia kusafisha kabisa ngozi na kuondoa uchafu.

Kwa upande wa seli zilizokufa na kubaki juu ya ngozi tumia โ€œscrubโ€. Scrub hufanya kazi kwa kuondoa seli zilizoharibika na zilizokufa na kuacha seli changa na ngozi nzuri.

USHAURI:

  1. Pata ushauri wa kulainisha na kupendezesha ngozi yako kutoka kwa wataalam wanaojua vizuri afya, urembo na vipodozi. Utashauriwa vizuri jinsi ya kufanya, vipodozi vya kutumia na jinsi ya kuvitumia vizuri kwa matokeo mazuri zaidi. Epuka wauza vipodozi wasio waaminifu au wasiovijua vizuri vipodozi, maana wanaweza kukupa vipodozi vya tofauti na mahitaji yako au vipodozi vinavyodhuru afya yako.
  2. Safisha ngozi yako vizuri, kila siku. Hakikisha unaondoa uchafu na vijidudu vyote vinavyotua na kukaa juu ya ngozi yako. Ondoa vumbi, seli zilizokufa, mafuta ya ziada, jasho nk Lala na pumzisha ngozi yako kiasi cha kutosha ili iweze kujitengeneza na kuwa nzuri. Ipumzishe kila siku kwa matokeo mazuri zaidi. Pata usingizi wa kutosha na ulio bora
  3. Tumia vipodozi vizuri vyenye uwezo wa kukupa matokeo mazuri unayoyataka na visivyodhuru afya yako. Pata ushauri mzuri kutoka kwa wataalam ili uweze kufanikisha hili vizuri. Tumia vipodozi vinavyoendana na ngozi yako. Kama ngozi yako ni kavu tumia vipodozi ambavyo ni maalum kwa ajili ya ngozi kavu, na kama ngozi yako ni ya mafuta basi tumia vipodozi ambavyo ni mahususi kwa ajili ya ngozi ya mafuta.
  4. Usitumie vipodozi vinavyoharibu ngozi na kuihatarisha ngozi yako. Epuka vipodozi vyote visivyo salama na vile visivyoendana na ngozi yako.
  5. Jihadhari na michubuko au majeraha mengine yoyote yatakayoweza kuharibu ngozi yako. Hii ni kwa sababu michubuko na majeraha hayo yatakuharibia uzuri wa ngozi yako na pia yatakuachia makovu baada ya kupona
  6. Kuwa na furaha, amani na tabasamu itakusaidia pia kuwa na ngozi nzuri, hususan ngozi ya usoni.

Hii mitoto mingine mijinga, cheki alichokifanya huyu

Nimeamka asubuhi nikiwa na elfu 1 tu mfukoni, nikamtuma mtoto wa jirani akaninunulie maandazi nipate kunywa chai. Baada ya muda namuona anarudi huku analamba askrimu ya AZAM kama Simba vile. Nikamuuliza maandazi yako wapi? Akanijibu eti wakati anafika yanapouzwa maandazi akagundua kuwa kapoteza hela yangu, hivyo akaanza kurudi, ila bahati nzuri wakati anarudi ili kuja kunitaarifu kuhusu kupotea kwa hela yangu, njiani akaokota elfu 1 ambayo kuna mtu alipoteza ndio akaamua kununua askrimuโ€ฆ.kwa sasa niko polisi na mtoto yuko dispensari na mamake๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€

Mambo ya Msingi kuyajua Ili uishi na watu vizuri

Nimezipenda hizi nasaha. Naamini na nyinyi wenzangu hamtakosa japo machache ya kujifunza:-
1. Epuka hasira za ovyo na kila mtu, kuwa msikivu kabla ya kukimbilia maamuzi (elewa kuwa ukiwa na hasira huwezi kupata suluhu ya jambo)
2. Usiwatendee wengine ubaya ukadhani kuwa utakuwa salama (ubaya hulipwa kwa ubaya, ipo siku ubaya wako kwa wengine utakurejea kama sio kuwarejea watu wa kizazi chako)

3. Usichukue maamuzi kabla ya kutafiti ukweli (pengine wapo wanadamu wanaopenda kuonekana wao wema kwa kuumiza wengine). Mtuhumu mtu lakini mpe muda wa kumsikiliza, usimshambulie mtu kwa maneno makali bila kuujua ukweli, ukijua ukweli nafsi inaweza kukusuta.

4. Mchukulie kila mwanadamu ni mkosaji (tambua kuwa hata wewe unawakosea sana wengine na wanakuvumilia. Hivyo usiwe mwepesi wa kuwaadhibu wenzio kwa ubaya).

5. Usipande mbegu ya chuki na ubaya katika jamii unayoishi ukadhani itakuacha salama (chuki hukua kama mti utambaao, ukiipanda ndani ya jamii yako, haitatoka kwako na inaweza kutafuna kizazi chako ukajutia.

6. Tambua kuwa yule unayeishi nae ni mwanadamu kama wewe, mpe heshima na mwonyeshee upendo hata kama huoni anafanana nawe. Maisha ni duara huenda ulikuwa kama yeye au atakuja kuwa kama wewe baadae.

6. Usiwe muongeaji ovyo ovyo na usiye na subira. Kuongea sana kunapoteza busara.

7. Jiepushe na maisha ya kusukumwa na wengine kufanya jambo usilojua manufaa yake. Jifunze kujitegemea kiakili. Sio kila unayemdhania rafiki moyoni mwake yupo pamoja nawe, na ukashirikiana nae, wengi wa marafiki zetu hututumia sana kuliko tunavyoweza kuwatumia wao.

8. Usipende sana kugombana na watu kwa njia ya maongezi yanayodumu kama vile, ujumbe wa maandishi, mawasiliano ya simu au ujumbe wa maneno (SMS). Kumbuka kuwa maneno yanaishi kuliko ugomvi au uadui, ipo siku yatakurudi na utajiona mpumbavu na kukosa pa kujificha. Jifunze kusubiri.

9.Usifumbue mdomo wako kutamka ubaya au kunyanyua kidole chako kuandika ubaya juu ya mwenzio bila kujiuliza mara mbili moyoni mwako hatima ya unachokitoa kwa mwingine.

10. Jishushe na jifunze kusikiliza wengine wakati wa mazungumzo ili uweze kujifunza kabla ya kukurupuka kujibu, usikivu ni kipimo cha busara, mtu anayekurupuka kujibu jibu kila anachosikia hawezi kuwa kiongozi, Mume au Mke mwema kwani mara nyingi atapotoka tu.

10. Usitunze hasira nyingi moyoni kwani hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu. Jitahidi pia kuepuka kuwa na hasira mara kwa mara na zisizo na maana. Elewa kuwa hasira zisizo maana hukupunguzia maisha na kukupa maumivu wewe mwenyewe kuliko yule uliyemfanyia hasira, utakufa kwa magonjwa kabla ya wakati ufaao.

11. Thamani yako inategenezwa na watu wengine, wewe kama ni mtoto, mheshimu sana mzazi wako na kama umeoa au kuolewa, heshimu wazazi na familia ya mke au mumeo kwa kuwa bila wao, usingekuwa hivyo ulivyo leo unajivunia ndoa njema, kwa kuwa yupo mtu alimzaa huyo mwenzio. Mheshimu kwa lolote liwe jema au baya, utalipwa kwa wakati ufaao.

13. Usijibizane na mtu usiyemjua au ambaye hawezi kukupunguzia kitu katika maisha yako. Tambua kuwa unapunguza sehemu kubwa ya maisha yako kwa kutafuta magomvi na mtu wa mbali nawe.

14. Kumbuka asili yako, kumbuka upo hapo kwa kuwa kuna mahali ulitoka, maisha yanabadilika, usidharau pale ulipokuwa zamani kwa kuwa ndipo palipokufanya leo uwe hapo.

15. Subiri, sikiliza, elekeza, vumilia. Elewa sio kila mtu ana uelewa kama wako. Jitahidi kuwa mvumilivu katika kila jambo, usiinuke kuwafokea au kuwakaripia wengine kwa jambo ambalo pengine nao wanahitaji muda kueleweshwa ili walifanye vyema. Kumbuka sana, kuna wakati nawe ulikuwa huelewi kabisa lakini wapo wenzio walikuvumilia, wakakuelekeza njia njema, kufokea wengine mara kwa mara sio njia njema ya kuwafundisha bali ni kuwaweka mbali nawe.

Kumbuka: Ishi kwa kumpendeza Mungu.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Wale wa kupenda kupewa pewa namba za simu soma hii

Unaomba namba ya simu ya mdada af anakunyima ila unalazimisha akupe anaona kuliko muendelee kuongea bora tu akupe anakutajia 071112016 unafuraahi unaondoka unafika nyumbani unajaribu kuipiga but kabla hujapiga unagundua alikutajia tarehe ya leoย Wadada acheni hizoย ๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿƒ๏ฟฝ๐Ÿƒ๏ฟฝ๐Ÿƒ๏ฟฝ๐Ÿƒ

Tabia za Kimama kwa wanaume

1, mwanaume kuoga haraka haraka ili uwahi kuangalia igizo, huo ni UMAMA..๐Ÿ˜‚

2, mwanaume kupiga picha umeng’ata Lips na Unapiga na Camera Beauty Plus huo ni UMAMA..๐Ÿ˜‚

3, Mwanaume kuangalia tamthilia na Jamai Raja na Maigizo kwenye chanel ya sinema zetu wakati mechi za kombe la dunia zinaendelea, pia nawe ni MMAMAAโ€ฆ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

4, Mwanaume kuandika ‘Jomon’ badala ya Jamani, kuandika ‘Pw’ badala ya Poa, kuandika ‘Thatha’ badala ya Sasa, kumwandikia mwanaume mwenzio ‘Mambo my’ Huu ni UDADA, tena UDADA wa CHUO..๐Ÿ˜‚
.
5, Mwanaume kunywa soda au Juice na kubakisha, kununua chakula halafu unakibakisha, kubagua bagua chakula na kujamba hovyo hovyo baada ya kushiba, huo nao ni UMAMAA..๐Ÿ˜‚
.
6, Mwanaume kumuuliza mwanaume mwenzio anapata faida gani kuangalia Mpira, pia nawe ni MMAMAโ€ฆ
.
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Namna ya kulisha kuku ili wasipatwe na magonjwa

Safisha vyombo vya kulishia na kunyweshea kila siku. Osha, sugua vizuri, kisha suuza kuondoa utando unaobeba bakteria.

Kuku wanahitaji wapewe chakula cha kutosha na chenye virutubisho vyote. Unaweza kuwaongezea majani, makombo, nafaka, mchanga laini, au maganda ya mayai.

Wapatie kuku maji safi muda wote. Wafugaji wengi wameripoti kuwa na matokeo mazuri baada ya kuchanganya dawa ya kuua vimelea kwenye maji ya kunywa.

Nunua chakula kwa wauzaji wazuri na wanaoaminika ili kuepuka minyoo na sumu hatarishi. Usiwape kuku chakula chochote kinachoonekana kuoza au kunuka uvundo.

Hifadhi chakula cha kuku katika sehemu kavu isiyo na joto na isiwe kwa zaidi ya miezi mitatu ili kuepuka kuharibiwa na fangasi.

Jinsi ya Kubana matumizi X-mass

Badala yakupika PILAU tutapika TAMBI kwenye Xmas maana tutakua tumeokoa sh.15,000/= Vitunguu swaumu 2000, Vitunguu maji 1000, hiliki 1000, Magome 1000, Michele wa 2000, Soda 3000, Nyama 5000 . Fedha hizi zitatumika kununua mfuko wa cement ili tuanze kujaza kibubu cha ujenzi wa nyumba badala ya kupanga. Karibuni saana maji ya kunywa tumechemsha ndoo nzima.

๐ŸŽ€โœจMarry Xmas & Happy new year.โœจ๐ŸŽ€

Aina ya vyakula vinavyotakiwa kwa wajawazito

Kwa ajili afya ya mama na mtoto ni muhimu sana, mwanamke anatakiwa apate chakula bora kilicho na madini yote kama vitamini na protini. Mama mjamzito anatakiwa apate gramu 100 za protini kila siku. Ifuatayo ni mlo kamili anaotakiwa apate mama mjamzito kila siku ya ujauzito wake kwa afya bora.

Hivi ndivyo vyakula bora ambavyo mama mjamzito na mtoto wake wanastahili kula;

1. Jamii Kunde

Mbegu za kunde ni sehemu muhimu ya chakula kwa mama mjamzito kwa sababu huwa na kiwango kikubwa cha protini. Kwa watu wasiokula nyama au wana uwezo mdogo tu kujipatia nyama mbegu za jamii kunde zinatosheleza mahitaji ya protini. Hivi ni vyakula vya mimea kama Soya,Peas,Karanga, Alfa alfa,Mikunde, maharage.

2.Mayai

Mayai mawili kwa siku husaidia kuupa mwili protini, vitamini A na madini ambayo itasaidia kuzuia kupatwa na maradhi ya magonjwa mbali mbali.

3. Maziwa na vyakula vya jamii ya maziwa

Glasi nne au zaidi ya maziwa ya aina yoyote pamoja na/au vyakula vyenye jamii ya maziwa kama jibini, mtindi na siagi. Maziwa ni muhimu kwa protini, calcium, vitamini na virutubisho vingi. Vitasaidia ukuaji wa mifupa na misuli, Ni muhimu kwa damu yenye afya, kusaidia usingizi na kusawazisha mdundo wa moyo.

4. Viazi tamu

Viazi vitamu vina vitamini A ambayo husaidia ukuaji wa macho ya mtoto,ngozi na mifupa

5. Nyama

Nyama ya kuku au ngombe huwa na protini nyingi sana na husaidia katika ukuaji wa mwili wa mtoto hasa kwa mama mjamzito wa miezi minne

6. Nafaka na vyakula vya Wanga

Vyakula hivi huipa mwili nguvu ya kufanya kazi na pia ukuaji wa mtoto tumboni.Vyakula hivi ni kama mahindi,mtama ,mihogo,vyakula vya ngano kama mkate n.k.

7. Avocado

Ni matunda ambayo yana mafuta mengi maarufu kama fatty acid. Avocado inasaidia katika ukuaji wa ubongo,ngozi nyororo na ukuaji wa misuli ya mtoto tumboni.

8 .Mboga za majani

Mboga za majani kama spinach, kabeji, mchicha na matembele. Mboga hizi zinafaa ziwe zenye rangi ya kijani iliyokolea kwa sababu hizi ndizo zenye virutubisho vya kutosha. Mboga hizi zitampa mama na mtoto wake Vitamin A na B, pia virutubisho vitakavyosaidia mwili kupata protini ya kutosha, ukuaji wa mwili, na utengenezaji wa damu. Kutopata mboga za kutosha kunaweza sababisha mama kupata ugonjwa wa Anemia.

9. Mafuta ya samaki

Mafuta ya maini ya samaki huwa na Omega fatty acids ambayo inasaidia ukuaji wa ubongo na macho ya mtoto.

10.Maji

Maji ni muhimu kwa mwili kwa sababu inasaidia kwenye mmenyenyo na unyonywaji chakula na pia husaidia kuzia choo ngumu Maji pia huzuia uvimbe wa mwili na maambukizi ya mfumo wa mkojo(UTI)

Shopping Cart
22
    22
    Your Cart
    ๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About