Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuheshimu Damu Takatifu ya Mkombozi wetu.
Yesu alimwahidi Mt. Brigita wa Sweden kwamba wale watakaosali Baba Yetu 7 na Salamu Maria 7 kwa miaka 12 kwa kuheshimu damu yake takatifu na kutafakari juu ya Kutahiriwa kwake, jasho lake la damu, kupigwa kwake mijeledi, kuvikwa taji la miiba, kuchukua kwake Msalaba, kusuliwa kwake na kuchomwa ubavuni; watapata neema 5 zifuatazo: (1) Hawataingia toharani, (2) Yesu atawapa cheo cha mashahidi waliomwaga damu yao kwa ajili ya imani, (3) Yesu atawadumisha jamaa zake watatu katika hali ya neema, (4) Roho za jamaa zake zitakingwa na Jehanam mpaka kizazi cha nne, (5) Mwezi kabla ya kufa, Yesu atawajulisha. Wakifa kabla ya kutimiza miaka ile, watahesabiwa wamemaliza.
Ee Yesu, sasa ninataka kusali Baba yetu mara saba nikiungana na ule upendo ambao kwao uliitakasa sala hii katika Moyo wako. Uichukue kutoka mdomoni mwangu hadi moyoni mwako. Uiboreshe na kuikamilisha hivyo kwamba iupatie heshima na furaha kwa Utatu Mtakatifu kama vile Wewe ulivyoupatia kupitia sala hii wakati ulipokuwa bado hapa duniani. Utukuzwe ee Yesu, itukuzwe Damu Yako Takatifu sana uliyoimwaga kutoka katika Majeraha Yako Matakatifu.
1. Yesu anatahiriwa.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Majeraha ya kwanza, maumivu ya kwanza na Damu ya kwanza aliyomwaga Mwanao mpenzi, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu na dhambi za dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi ya kwanza ya mauti, hasa kati ya ndugu zangu.
2. Yesu anatokwa Jasho la Damu bustanini Gethsemane.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso na mahangaiko makali sana ya moyoni, ya Bwana wetu Yesu Kristu katika mlima wa mizeituni na kila tone la jasho lake la damu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za kimoyomoyo, na dhambi za namna hiyo zinazotendwa na dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za moyoni na kwa ajili ya kueneza upendo wa kiMungu na wa kindugu.
3. Yesu anapigwa mijeledi.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha elfu elfu aliyopata, maumivu makali sana na Damu Takatifu sana aliyomwaga, alipopigwa mijeledi, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za tamaa ya mwili, kwa malipizi ya dhambi za tamaa ya mwili za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za tamaa ya mwili, na kwa kulinda usafi wa moyo, hasa kati ya ndugu zangu.
4. Yesu anavikwa taji la miiba.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha, maumivu na Damu Takatifu kutoka katika Kichwa Kitakatifu cha Yesu wakati alipovikwa taji la miiba, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za rohoni, kwa malipizi ya dhambi za rohoni za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za rohoni, na kwa ajili ya kueneza Ufalme wa Kristu hapa duniani.
5. Yesu anachukua Msalaba.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso ya njia ya Msalaba, hasa donda lake la begani na Damu Takatifu iliyomwagika, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za ukaidi dhidi ya msalaba, na dhambi za ukaidi dhidi ya msalaba za wanadamu wote, malalamiko yote dhidi ya mipango yako mitakatifu na dhambi zote za ulimi, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za ulimi na kwa ajili ya upendo wa kweli kwa Msalaba.
6. Yesu anasulibiwa.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Mwanao Msalabani, kupigwa kwake misumari na kuinuliwa kwake, madonda yake mikononi na miguuni na mifereji mitatu ya Damu yake Takatifu iliyomwagika kutoka katika majeraha haya, mateso yake makali sana ya mwili na roho, kifo chake kitakatifu, ukumbusho usio wa kumwaga wa damu wa kifo hiki katika Misa zote Takatifu ulimwenguni, kwa ajili ya majeraha yote yanayosababishwa na ukaidi wa nadhiri na kanuni katika madaraja matakatifu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu zote na za ulimwenguni mzima, kwa ajili ya wagonjwa na wanaokufa, kwa ajili ya mapadre watakatifu na walei, kwa ajili ya nia za Baba Mtakatifu za kukarabati familia za kikristu, kwa ajili ya kuimarika kwa imani ya kikristu ulimwenguni, kwa ajili ya nchi yetu na muungano kati ya mataifa ndani ya Kristu na Kanisa lake, na kwa ajili ya wokovu wa dunia nzima.
7. Yesu anachomwa kwa mkuki moyoni.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, ukubali kupokea, kwa ajili ya mahitaji ya Kanisa Takatifu na kwa ajili ya malipizi ya dhambi za wanadamu wote, Damu na Maji Takatifu vilivyomwagika kutoka jeraha la Moyo Mtakatifu wa Yesu. Utuhurumie. Damu Takatifu ya Yesu, tone lile la mwisho lililomwagika kutoka katika Moyo wake Mtakatifu, unioshe mimi na wengine wote dhambi zetu zote! Ee Maji kutoka katika Moyo Mtakatifu wa Yesu, unioshe na adhabu zote za dhambi zangu na uizime miale ya moto wa toharani kwa ajili yangu na kwa ajili ya roho zote zilizomo toharani. Amina.
Katika mwaka wa Kanisa wa kiliturjia, mwezi Julai ni wa kuiheshimu Damu Takatifu ya Yesu.
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
Nakuombea 🙏
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
🙏🌟 Mungu akujalie amani
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mungu akubariki!
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
🙏🌟 Mungu alete amani
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
🙏💖 Nakusihi Mungu
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
🙏🌟 Mbarikiwe sana
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
🙏🙏🙏
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
Dumu katika Bwana.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mwamini katika mpango wake.
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Amina
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
Sifa kwa Bwana!
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Neema na amani iwe nawe.
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
🙏❤️ Mungu akubariki
Endelea kuwa na imani!
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
🙏💖💫 Mungu ni mwema
Tumaini ni nanga ya roho
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu ni mwema, wakati wote!
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe
🙏💖 Nakushukuru Mungu
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie
Rehema zake hudumu milele
🙏✨ Mungu atakuinua
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
Nguvu hutoka kwa Bwana
Neema ya Mungu inatosha kwako
🙏🙏🙏
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
Baraka kwako na familia yako.
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mwamini Bwana; anajua njia
Katika imani, yote yanawezekana
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Imani inaweza kusogeza milima
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
🙏✨ Mungu atupe nguvu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rehema hushinda hukumu
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu