Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya

Jinsi ya kupika Pilau ya Mpunga Na Nyama Ya Ng’ombe

Mahitaji

Mpunga – 4 vikombe

Nyama – 1 kilo moja

Kitunguu maji – 3

Mbatata/viazi – 7 vidogodogo

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa 3 vijiko cha supu

Bizari nzima/ya pilau/uzile/cumin – 3 vijiko vya supu

Mdalasini – 3 vipande

Hiliki – 7 punje

Pilipili manga nzima – 1 kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Mafuta – ½ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mchele weka kando
Katakataka vitunguu slice ndogo ndogo.
Weka mafuta katika sufuria kisha ukaange vitunguu pamoja na mdalasini, hiliki pilipilimanga.
Vitunguu vikigeuka rangi unatia kitunguu thomu na tangawizi.
Tia supu kidogo na nyama, kisha tia bizari ya pilau/uzile, na viazi/mbatata.
Maliza kutia supu yote, na ikiwa ni kidogo ongeze maji kiasi cha kuivisha mchele. kisha tia mchele ufunike hadi wali uwe tayari.
Ikiwa unatumia mkaa palia juu yake, ikiwa hutumii uache uive kwa moto mdogo mdogo.

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini Ya Pilipili Mbichi

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama

Nyama ya ng’ombe vipande vidogo – 2lb

Nyanya – 1

Kitunguu Kilichoktwa katwa – 1

Mafuta – 2 vijiko vya supu

Paprika (bizari ya masala ya rangi) – ½ kijiko cha chai

Kidonge cha supu – 1

Chumvi – Kiasi

Ndimu – Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha nyama kwa chungio ili itoke maji. Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwerangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.
Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.

Vipimo Vya Mboga

Mchicha ulio katwa katwa 400 gm

Nyanya 1

Kitunguu kilicho katwa 1

Nazi ya unga kiasi

Pilipili mbichi 2

Mafuta ½ kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha na Kupika

Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.
Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.
Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji
Tia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa
tayari kuliwa

Vipimo Vya Maharage

Maharage – 1 kopo

Kitunguu – 1

Nazi – 1 mug

Nyanya (itowe maganda) – 1 kiasi

Pilipili mbichi – 2

Mafuta – 1 kijiko cha supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.
kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.
Tia chumvi, maharage na nazi uwachie
moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.

Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi

Pilipili mbichi – 4/5

Kotmiri – 1 Kijiko cha supu

Ndimu – kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 1 chembe

Mafuta ya zaituni – 2 vijiko Vya supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha

Kwenye blender, tia vipimo vyote na sage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Vipimo Vya ugali

Maji – 4 Vikombe kiasi inategemea na unga

Unga wa sembe – 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.

Mapishi ya wali wa Kiafrika Mangaribi

Mahitaji

Mchele (rice vikombe 2 na 1/2)
Vitunguu (onion 2)
Nyanya ya kopo (tin tomato kopo 1)
Tangawizi (ginger paste kijiko 1 cha chakula)
Kitunguu swaum (garlic paste kijiko 1 cha chakula)
Paprika (kijiko 1 na 1/2 cha cha chai)
Pilipil (scotch bonnet pepper 1)
Curry powder (kijiko 1 cha chai)
Maggi cubes 3(unaweza kutumia yenye ladha ya chicken, beef au vegetable. Inategemea unasevu na mchuzi wa aina gani)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)

Matayarisho

Loweka mchele kwa muda wa dakika 10.Katakata vitunguu kisha weka pembeni, saga pamoja nyanya ya kopo,pilipili, tangawizi na kitunguu swaum kisha weka pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu vikiiva tia curry powder, maggi cubes, chumvi na paprika na uchanganye vizuri. Kisha tia mchanganyiko wa nyanya na uupike mpaka uive. Baada ya hapo tia mchele na maji na uupike mpaka ukaribie kuiva kisha ugeuze na umalizie kwa kutia njegere na umalizie kuupika mpaka uive. baada ya hapo utakuwa tayari kuseviwa na mboga yoyote kama kuku, nyama, samaki au assorted meat (Mchanganyiko wa utumbo, makongoro na nyama), Hapo mimi nili-save na mchuzi wa kuku wa kienyeji.

Vitafunio 10 vya Afya kwa Kusaidia Zoezi lako la Mazoezi

Vitafunio 10 vya Afya kwa Kusaidia Zoezi lako la Mazoezi 🥦🍇🥕🥚🍌💧🥜🥗🥛🍓

Kama mtaalamu wa afya na mazoezi, kuna jambo moja ambalo nataka kukushirikisha leo. Nataka kuzungumzia umuhimu wa vitafunio bora kwa afya yako wakati wa mazoezi. Kama AckySHINE, ningependa kushiriki nawe vitafunio 10 vyenye afya ambavyo vitasaidia kuongeza nguvu yako na kuboresha utendaji wako wakati wa mazoezi.

  1. Matunda na Mboga 🥦🍇🥕: Matunda na mboga ni muhimu sana kwa mwili wako. Wanakupa virutubisho muhimu na nyuzinyuzi zinazosaidia kudumisha nguvu na afya ya mwili wako. Kwa mfano, tunda kama ndizi lina wanga ambao husaidia kuongeza nishati yako wakati wa mazoezi.

  2. Protini 🥚: Protini ni muhimu kwa kujenga misuli na kuboresha ahueni ya mwili wako baada ya mazoezi. Unaweza kupata protini kutoka kwa vyakula kama mayai, kuku, samaki, na maziwa. Protini pia husaidia kujaza hisia ya kujaa na kuondoa njaa ya haraka.

  3. Maji 💧: Kama AckySHINE, ninaamini kuwa maji ni kichocheo cha mafanikio ya mazoezi. Inasaidia kudumisha kiwango chako cha maji na kuzuia kuishiwa nguvu wakati wa mazoezi. Kwa hiyo, hakikisha kunywa maji ya kutosha kabla, wakati, na baada ya mazoezi.

  4. Karanga 🥜: Karanga ni chanzo kizuri cha mafuta yenye afya na protini. Wanaweza kukuongezea nishati na kukusaidia kuhisi kujaa kwa muda mrefu. Chagua aina ya karanga ambayo haina chumvi nyingi na hakuna mafuta yaliyoongezwa.

  5. Saladi 🥗: Saladi yenye mboga mboga mbalimbali, matunda, na protini itakupa virutubisho vyote muhimu kwa mwili wako. Unaweza pia kuongeza vijiko vya mafuta yenye afya kama vile parachichi au mafuta ya ziada ya bikira ili kuongeza ladha na faida ya lishe.

  6. Maziwa 🥛: Maziwa ni chanzo kizuri cha protini, kalsiamu, na vitamini. Unaweza kunywa maziwa ya joto au ya baridi, au kufurahia jogoo za maziwa yaliyopamba, iliyoongezwa na matunda.

  7. Matunda yenye Rutuba 🍓: Kama AckySHINE, ninaipendekeza matunda yaliyo na rutuba kama vile zabibu, cherries, au matunda ya jamii ya berries. Matunda haya yana viwango vya juu vya antioxidants ambazo husaidia kupambana na uchovu na kusaidia ahueni baada ya mazoezi.

  8. Juisi ya Matunda Asili 🍌: Mara nyingi, juisi za matunda zina sukari nyingi iliyotengenezwa na vihifadhi. Kama chaguo mbadala, unaweza kufurahia juisi ya matunda asili ambayo haujaongeza sukari yoyote. Juisi hii itakupa nishati ya haraka na virutubisho muhimu.

  9. Mayai ya Kuchemsha 🥚: Mayai ya kuchemsha ni chanzo kingine kizuri cha protini na virutubisho muhimu. Unaweza kula kichwa cha mayai kabla ya mazoezi ili kuongeza nishati yako na kusaidia kujenga misuli yako.

  10. Smoothies za Matunda 🍌: Smoothies ya matunda ni njia nzuri ya kuchanganya matunda, maziwa, na protini katika kinywaji kimoja. Unaweza kuongeza zaidi ya matunda yoyote, kama vile ndizi au matunda ya jamii ya berries, ili kuunda smoothie ya lishe ya kuburudisha baada ya mazoezi.

Kwa ujumla, ni muhimu kuchagua vitafunio vyenye afya ambavyo vitakupa nishati na virutubisho muhimu wakati wa mazoezi. Kumbuka pia kuzingatia upatikanaji na upendeleo wako binafsi. Kwa mfano, ikiwa una mzio au upendeleo wa kibinafsi, chagua vitafunio ambavyo vinaendana na mahitaji yako.

Je, unapendelea vitafunio gani wakati wa mazoezi? Je, unayo vitafunio vyenye afya ambavyo unapenda kushiriki nasi? Asante kwa kusoma na natumai ulipata habari hii kuwa muhimu. Natarajia kusikia maoni yako! 🍓🥦🍌🥗🍇

Jinsi ya Kupika skonzi

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
Sukari (sugar 1/2 kijiko cha chakula)
Chumvi (salt 1/2 kijiko cha chai)
Hamira (yeast 1/2 kijiko cha chakula)
Baking powder 1/2 kijiko cha chai
Siagi (butter 1/4 ya kikombe cha chai)
Maziwa (fresh milk 3/4 ya kikombe cha chai)(unaweza kutumia maji badala ya maziwa)

Matayarisho

Pasha maziwa yawe ya uvuguvugu kisha weka pembeni, pia yeyusha siagi na uweke pembeni.Baada ya hapo tia kila kitu kwenye bakuli la kukandia kasoro maziwa, na uchanganye vizuri kisha tia maziwa kidogo kidogo katika mchanganyiko huo kisha ukande. Ukimaliza uweke kwenye sehemu ya joto na uache uumuke. Ukisha umuka utawanyishe katika madonge saba Kisha .pakaza mafuta au siagi katika chombo cha kuokea kisha yapange hayo madonge katika hicho chombo na uyaache yaumuke tena (kwa mara ya pili). Baada ya hapo pakaza mafuta juu ya hayo madonge na uyaoke (bake) katika oven (moto 200°C ) kwa muda wa dakika 25 na hapo scones au maskonzi yatakuwa tayari

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Karanga

MAHITAJI

Mayai 5

Sukari 450gm (1 lb)

Unga wa Ngano 1 kg

Siagi 450gm (1 lb)

Baking powder ½ Kijiko cha chai

Unga wa Custard Vijiko 2 vya chakula

Karanga za kusaga 250gm

Jam ½ kikombe

MAANDALIZI

Chukua bakuli la kiasi, weka sukari na siagi.
Changanya sukari na siagi kwa kutumia mashine ya kukorogea keki (cakemixer), mpaka sukari ichanganyike na siagi.
Vunja yai moja moja na weka kiini chake kwenye mchanganyiko wa sukari na siagi, endelea kuchanganya mpaka ichanganyike vizuri. Hifadhi ute wa mayai ndani ya kibakuli.
Mimina unga wa ngano ndani ya mchanganyiko wako huku ukichanganya Changanya unga wa custard na baking powder.
Tengeneza viduara vidogo vidogo.
Vichovye viduara ndani ya ute wa yai kisha zimwagie unga wa karanga na kuzipanga kwenye tray ya kuchomea.
Weka dole gumba kati kati ya kila kiduara na uweke jam.
Washa jiko (oven) 350F na uchome vileja vyako kwa dakika 20.
Toa vileja vyako vipoe na uviweke ndani ya sahani tayari kwa kuliwa.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About