VIAMBAUPISHI
Unga – 4 Vikombe vya chai
Siagi – 1 Kikombe cha chai
Hiliki ½ Kijiko cha chai
VIAMBAUPISHI:SHIRA
Sukari – 2 Vikombe vya chai
Maji – 1 Kikombe cha chai
Vanilla ½ Kijiko cha chai
(cocoa ukipenda kugawa visheti aina mbili) 2 Vijiko vya chai.
JINSI YA KUTENGENEZA
Tia unga kwenye bakuli pamoja na siagi na hiliki.
Changanya vizuri isiwe na madonge.
Tia maji baridi vikombe viwili kasoro vya chai changanya ukiona bado ongeza maji kidogo, iwe kama chapati usikande uchanganye tu.
Halafu utakata sampuli unayopenda mwenyewe.
Unaweka karai ya mafuta yakisha kupata moto unaanza kuchoma moto usiwe mkali sana, kiasi, baadae unaweza kuongeza moto na vikaange hadi viwe rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta. .
Ukipenda gawa visheti sehemu mbili, na shira pia igawe sehemu mbili
Changanya nusu ya visheti kwa shira nyeupe.
Nusu ya shira nyingine ibandike tena motoni na tia cocoa vijiko viwili vidogo vya chai.
Inapochanganyika cocoa vizuri changanya nusu ya visheti ulivyogawa kupata visheti vya shira ya cocoa.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Mapishi ya Kidheri – Makande
Mapishi ya Ndizi Za Supu Ya Nyama Ya Ng’ombe
Jinsi ya kupika Biskuti Za Tende
Mambo ya msingi kufahamu kuhusu Lishe
Mapishi ya Biriani Nyepesi Kupika Ya Samaki
Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nazi Wa Nyanya Chungu/Mshumaa/Ngogwe Na Bamia, Mboga Ya Matembele Na Samaki Wa Kukaanga
Upishi na Majani ya kijani: Vyakula Vyenye Virutubisho na Ladha Nzuri
Madhara ya kula yai bichi