VIAMBAUPISHI
Unga – 3 mug za chai
Samli – ½ mug ya chai
Maziwa – 1¼ mug ya chai
Baking powder – 2 vijiko vya chai
VIAMBAUPISHI VYA MJAZO
Njugu zilizomenywa vipande vipande – 2 vikombe cha chai
Sukari – ½ kikombe cha chai
Iliki – 1 kijiko cha chai
Nazi iliyokunwa – 2 vikombe vya chai
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari – 2 vikombe vya chai
Maji – 1 kikombe cha chai
Ndimu – 1
JINSI YA KUVIANDAA
1-Changanya unga na samli kisha tia baking powder na maziwa. Ukande ulainike kisha
uwache kama dakika 5 uumuke.
2-Kwenye bakuli nyingine changanya njugu, sukari na iliki.
3-Kata madonge madogo dogo sukuma kila donge duara jembamba, kisha tia kijiko cha mchanganyiko wa njugu juu yake ifunikie juu yake na ibane pembeni.
4-Panga kwenye treya isiyoganda (non stick) kisha choma kwenye oven kwa moto wa chini
(bake) 350° C kwa dakika kama 15-20.
5-Chemsha maji na sukari katika sufuria ndogo kisha tia ndimu acha ichemke mpaka inatenate unapoigusa.
6-Kwenye sahani ya chali mimina nazi iliyokunwa.
7-Vibiskuti vikiwa tayari vya motomoto chovea kwenye shira kisha zungushia katika nazi iliyokunwa,
panga kwenye sahani tayari kwa kuliwa.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Mapishi ya Sponge keki
Jinsi ya kutengeneza Bisikuti Za Kaukau Na Kahawa (Cocoa Coffee Biscuits)
Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Tambi
Mapishi – Kisamvu cha Karanga
Jinsi ya kupika pizza ya mboga mboga na cheese
Jinsi ya kupika Keki Ya Maboga
Mapishi ya tambi za kukaanga
Jinsi ya kupika Mkate wa sinia