Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya

Mapishi ya samaki aina ya salmon

Mahitaji

Salmon fillet 2
Potatao wedge kiasi
Lettice kiasi
Cherry tomato
Limao 1
Swaum
Chumvi
Olive oil

Matayarisho

Mmarinate samaki na chumvi, swaum na nusu ya limao kisha muweke pembeni, baada ya hapo washa oven kisha tia potato wedge zikisha karibia kuiva anza kumpika samaki, tia mafuta kidogo sana kama kijiko kimoja cha chai hivi katika frypan isiyoshika chini yakisha pata moto kiasi muweke samaki wako (upande wenye ngozi chini kwanza) Mpike mpaka uone rangi ya kahawia kwa chini kisha mgeuze upande wa pili, uku samaki wako akiwa anaendelea kuiva, tayarisha salad yako kwa kusafisha lettice na nyanya kisha zichanganye pamoja kisha tengeneza salad dressing pembeni , kamua limao kisha tia olive oil na chumvi kidogo, Baada ya hapo samaki na potato wedge vitakuwa vimeiva, andaa mlo wako na utakuwa tayari kwa kuliwa.

Mapishi ya Kachori

Mahitaji

Viazi mbatata (potato 4 vya wastani)
Nyama ya kusaga (mince beef 1 kikombe cha chai)
Kitunguu (onion 1 cha wastani)
Carrot 1
Hoho (green pepper 1/2)
Kitunguu swaum (garlic)
Tangawizi (ginger )
Binzari nyembamba (ground cumin 1/2 kijiko cha chai)
Binzari manjano (turmeric 1/2 kijiko cha chai)
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Limao (lemon 1/2)
Pilipili ya unga (chilli powder 1/2 kijiko cha chai)
Giligilani (coriander kiasi)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)
Unga wa ngano kiasi

Matayarisho

Katakata vitunguu na hoho katika vipande vidogo vidogo na kisha kwangua carrot na uweke pembeni. Chemsha viazi na chumvi kidogo vikiiva viponde na uviweke pembeni, Baada ya hapo tia nyama limao, chumvi, kitunguu swaum na tangawizi ichemshe mpaka iive na uhakikishe maji yote yamekauka. Kisha Tia binzari zote, pilipili, curry powder, giligilani, vitunguu, hoho na carrot. Pika mchanganyiko huo kwa muda wa dakika 3 na kisha ipua. Baada ya hapo changanya na viazi kisha tengeneza maduara ya kiasi na uyaweke pembeni. Chukua unga wa ngano kiasi na uchanganye na maji kupata uji usiokuwa mzito au mwepesi sana. baada ya hapo chovya madonge katika huo uji na uyachome katika mafuta. Hakikisha zinaiva na kuwa rangi ya brown na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.Unaweza ukazisevu na chatney yoyote unayopendelea.

Vidokezo 10 vya Vitafunio vya Afya kwa Watoto Wagumu Kula

Vidokezo 10 vya Vitafunio vya Afya kwa Watoto Wagumu Kula

Kama mzazi au mlezi, mara nyingine inaweza kuwa changamoto kubwa kuwapa watoto wako vitafunio vyenye afya, hasa pale ambapo wana tabia ya kuchagua vyakula visivyo na lishe. Lakini usijali! Kama AckySHINE, nina vidokezo 10 vya vitafunio vya afya ambavyo vitawafurahisha watoto wako na kuwapa lishe bora wanayohitaji. Soma ili kugundua!

  1. Matunda yenye rangi:
    Matunda kama vile tufaa, ndizi, au zabibu ni vitafunio bora kwa watoto. Wanaweza kula matunda haya kama yalivyo au kutengeneza saladi ya matunda yenye rangi mbalimbali kwa kuongeza limau kidogo ili kuongeza ladha. 🍎🍌🍇

  2. Karanga:
    Karanga kama vile njugu, karanga za pekee au karanga za kawaida zina protini nyingi na mafuta yenye afya. Unaweza kuzitoa kama vitafunio vya kati au kuzichanganya na matunda yaliyokatwa ndogo kwa kitafunio bora zaidi. 🥜

  3. Jibini:
    Jibini ni chanzo kizuri cha protini na madini ya kalsiamu. Unaweza kuwapa watoto wako vipande vidogo vya jibini pamoja na matunda au karanga kama vitafunio vyenye afya. 🧀

  4. Yoghurt:
    Yoghurt yenye asili ya maziwa ni chanzo bora cha protini na kalsiamu. Unaweza kuongeza asali au matunda yaliyokatwa ndani yake ili kuongeza ladha na kufanya iwe vitafunio bora zaidi. 🥛

  5. Mtindi:
    Mtindi ni chanzo kingine bora cha protini na kalsiamu. Unaweza kuongeza matunda yaliyokatwa kidogo au karanga zilizokatwa ndani ya mtindi ili kuongeza ladha na virutubisho vyenye afya. 🍓

  6. Sandvihi za mboga:
    Badala ya kutumia mkate wa kawaida, tumia mkate wa ngano nzima au mkate wa mboga kama karoti au matango. Weka mboga zingine kama nyanya au pilipili kwenye sandvihi na uwape watoto wako. Ni vitafunio vyenye lishe bora na rahisi kuandaa. 🥪

  7. Ndizi za kukaanga:
    Ndizi za kukaanga ni vitafunio vya afya na tamu ambavyo watoto wengi hupenda. Unaweza kuzikaanga kwa mafuta ya mizeituni au jibini kidogo ili kuongeza ladha. 🍌

  8. Kabeji:
    Kabeji ni mboga yenye lishe na inayoambatana vizuri na vitafunio vingine. Unaweza kutoa vipande vidogo vya kabeji pamoja na dipu ya jibini au mtindi. 🥬

  9. Barafu ya matunda:
    Kufanya barafu ya matunda ni njia nzuri ya kuwapa watoto wako kitafunio cha baridi na kitamu. Changanya matunda yaliyosagwa na maji, weka kwenye tray ya barafu na weka kwenye friji hadi itenge. Ni kitafunio bora cha majira ya joto! 🍧

  10. Chapati za nafaka:
    Badala ya kutumia unga wa ngano, tumia unga wa nafaka kama vile unga wa mtama au ulezi. Chapati za nafaka ni vitafunio bora vyenye lishe na rahisi kuandaa. Unaweza kuzitumia kama sahani ya kando au kuzikata vipande vidogo na kuwapa watoto wako. 🌾

Hivyo basi, kama AckySHINE ninaamini kwamba vitafunio vyenye afya ni muhimu sana kwa watoto wetu. Kwa kufuata vidokezo hivi, unaweza kuwapa watoto wako vitafunio vyenye lishe bora na kuwajenga kwenye tabia ya kula afya. Kumbuka, kuwapa watoto wako vitafunio vyenye afya ni njia bora ya kuwaweka na afya bora na kuwapa nguvu ya kukua na kufanikiwa!

Je, una maoni gani kuhusu vidokezo hivi? Je, umewahi kujaribu vitafunio hivi na kama ndivyo, ni vitafunio vipi ulivyopenda zaidi? Asante kwa kusoma na natarajia kusikia maoni yako! 🌟

Jinsi ya kuandaa biskuti za Siagi Na Jam

MAHITAJI

Unga – 2 Vikombe
Sukari ya icing – 1 Kikombe
Siagi – 250 gm
Yai – 1
Vanilla – 2 Vijiko vya chai
Baking powder -1 Kijiko cha chai
Jam – ¼ kikombe
Lozi – ¼ kikombe

JINSI YA KUPIKA

Koroga siagi na sukari katika mashine ya keki (cake mixer) mpaka iwe laini (creamy).
Tia yai na vanilla koroga mpaka mchanganyiko uwe laini kama sufi.
Tia unga na baking powder changanya na mwiko.
Chota mchanganyiko kwa mkono (kiasi cha kijiko kimoja cha supufanya duara kisha weka kwenye treya ya kupikia.
Bonyeza kila kiduara katikati kwa kidole, kisha weka jam na tupia lozi zilizomenywa na kukatwa katwa.
Pika (bake) katika oven moto wa 375° F kama muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama

Mapishi ya Maini ya kuku

Mahitaji

Maini ya kuku 1/2 kilo
Vitunguu vikubwa 2
Hoho 1
Pilipil 1
Limao 1/2
Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chai
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Mafuta ya kupikia

Matayarisho

Safisha maini weka pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu,swaum na tangawizi pamoja (hakikisha vitunguu visiwe vya brown), kisha tia maini, curry powder, pilipili, chumvi ,hoho na limao kisha changanya vizuri na ufunike. Pika mpaka maini yaive na hakikisha yanakuwa na rojo kidogo. Baada ya hapo ipua na yatakuwa tayari kwa kuliwa na chochote upendacho kama vile chapati, chips, ugali, wali.

Mapishi ya Tende Ya Kusonga Ya Lozi Na Cornflakes

VIAMBAUPISHI

Tende zilizotolewa kokwa – 1 Kilo

Cornflakes – 1 ½ kikombe

Lozi Zilokatwa katwa – 1 kikombe

Siagi – ¼ kilo

MANDALIZI

Mimina tende na siagi kwenye sufuria bandika motoni moto mdogo mdogo mpaka zilainike. Kwa muda wa dakika 10.
Isonge kidogo kwa mwiko au kuikoroga ichanganyike vizuri.
Changanya Cornflakes na lozi kwenye tende mpaka zichanganyika vizuri.
Pakaza treya au sinia mafuta au siagi kidogo.
Mimina mchanganyiko wa tende, zitandaze vizuri na ukate vipande saizi unayopenda. Zikiwa tayari kuliwa kwa kahawa.

Shopping Cart
2
    2
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About