Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Siri ya kamba nyekundu

Miaka zaidi ya 3000 iliyopita katika mji wa Yeriko alikuwepo mwanamke mmoja kahaba, jina lake Rahabu. Huyu mwanamke aliwaokoa wapelelezi wa Israel waliotumwa kwenda kufanya uchunguzi ktk nchi yao.

Wakati wana wa Israel wanatoka Misri kuelekea nchi ya Kaanani, Mungu aliwaahidi kuwapa mji wa Yeriko. Kwahiyo walipofika ng’ambo ya mto Yordani, Yoshua akatuma wapelezi wawili kwenda kuipeleleza Yeriko kabla wana wa Israel kuivamia na kuitwaa. Wale wapelelezi walipofika mji wa Yeriko mfalme akapelekewa taarifa kuwa kuna watu wawili wameingia kuipeleleza nchi.

Kwahiyo mfalme akaagiza wakamatwe na wauawe. Wale wapelelezi wakaingia ktk nyumba ya mwanamke kahaba aitwaye Rahabu akawaficha darini. Akawafunika kwa mabua ya kitani. Wale askari walipofika na kumuuliza Rahabu kwamba wako wapi waisrael wawili walioingia humu ndani, Rahabu akajibu kuwa wameondoka.

Akasema ni kweli waliingia ktk nyumba yangu lakini walitoka kabla lango la mji halijafungwa. Akawaambia wafuateni haraka kabla hawajafika mbali. Wale askari wakatoka kuwafuata wale wapelelezi hadi katika vilima vya nje ya mji lakini wasiwaone. Ilipofika usiku Rahabu akawashusha darini wale wapelelezi na kuwaelekeza namna ya kutoroka mji wa Yeriko. Akawaelekeza wapite njia nyingine tofauti na ile waliyoiendea wale askari. Akawashusha kupitia dirishani ili watu wa mji ule wasiwaone.

Kwa ukarimu aliowatendea wale wapelelezi wakaweka agano nae kwamba siku wana wa Israel wakija kuiangamiza Yeriko, BWANA ataiponya nyumba ya Rahabu na ndugu zake wote. Ili kutimiza agano hilo wale wapelezi wakamwambia Rahabu weka kamba nyekundu katika dirisha lako kama alama, ili jeshi la Israel liltakapouteketeza mji nyumba yako isiangamizwe.

Yoshua 2:17 &18 “Wale wapelelezi wakamwambia Rahabu, Sisi tunataka tusiwe na hatia kwa ajili ya kiapo hiki ulichotuapisha. Angalia, tutakapoingia katika nchi hii, funga kamba hii nyekundu katika dirisha hili ulilotuteremshia; nawe uwakusanye nyumbani mwako, baba yako, mama yako, na ndugu zako, na watu wote wa nyumba ya baba yako.”

Rahabu akafanya hivyo, na siku Jeshi la Israel lilipovamia Mji wa Yeriko ili kuuteketeza, Rahabu na ndugu zake walipona.

Yoshua 6:23 &24 “Basi wale vijana wapelelezi wakaingia, wakamtoa Rahabu, na baba yake, na mama yake, na ndugu zake, na vitu vyote walivyokuwa navyo, wakawatoa na jamaa zake wote pia; wakawaweka nje ya matuo ya Israeli. Kisha wakauteketeza mji kwa moto, na vitu vyote vilivyokuwa ndani yakeโ€ฆ”

MORAL OF THE STORY.!
Habari hii ina mengi ya kutufundisha lakini leo nataka nikufundishe kuhusiana na siri ya kamba nyekundu ambayo Rahabu aliiweka katika dirisha lake na jinsi ilivyomuokoa.

Rahabu hakua mtakatifu, hakuwa mteule wa Mungu wala hakuwa kizazi cha Israel. Alikua mwanamke wa mataifa, tena kahaba. Hakuwa mwema sana machoni pa Mungu. Lakini aliokoka kwa sababu ya “kamba nyekundu” dirishani mwake. Pengine wapo maaskofu, wachungaji, mitume au manabii walioangamizwa, lakini kahaba Rahabu akaokolewa yeye na ndugu zake licha ya kwamba alikua kahaba. Siri ni “kamba nyekundu” dirishani mwake.

Jiulize je wewe unayo kamba nyekundu? Kuna watu katika maisha wanaonekana wenye dhambi, wachafu, dhaifu au wasiofaa, lakini Mungu huwanyanyua na kuwabariki na kuwaacha wale tunaodhani ni watakatifu au wenye haki. Mungu anaangalia “kamba nyekundu”. Unaweza kuwa mtakatifu lakini huna “kamba nyekundu” itakayomfanya Mungu akurehemu.

Unaweza kuwa umemaliza masomo yako na umefaulu vizuri, lakini kila unapoomba kazi huitwi hata kwenye usaili, na ukiitwa hupati kazi, miaka inazidi kwenda. Unaamua kwenda kwenye maombi. Kila siku unafanya maombi lakini bado hufanikiwi. Unajiuliza tatizo liko wapi. Unaji-asses na kuona hakuna tatizo mahali. Kumbe huna “kamba nyekundu”

Au unaweza kuwa una biashara yako lakini haifanikiwi. Hupati wateja. Umehitahidi kwa kila hali lakini bado huoni faida. Unadhani tatizo labda Mungu amekuacha. Unaamua kuwa mtu wa maombi. Unazunguka makanisa mbalimbali kuonbewa lakini bado haufanikiwi. Kumbe huna “kamba nyekundu”.

“Kamba nyekundu” imekuwa siri ya mafanikio ya watu wengi bila kujalisha mahusiano yao kiroho na Mungu. Bila kujalisha kama ni wakristo au si wakristo. Kamba nyekundu imewasaidia hata wenye dhambi kubarikiwa. Rahabu alikua kahaba lakini yeye na ndugu zake waliokolewa kwa sababu ya “kamba nyekundu”.

Je kamba nyekundu ni nini? Kamba nyekundu ni mfumo wako wa maisha; jinsi unavyoishi na unayowatendea watu wengine, hasa “wateule” wa Mungu.

Kuna wakati Mungu huamua kukubariki si kwa sababu wewe ni mwema sana, bali kwa sababu kuna watu wema wanaoomba kwa ajili yako. Inawezekana tangu uanze kuomba, maombi yako hayajawahi kufika kwa Mungu lakini unabarikiwa, kwa sababu ya kamba nyekundu.

Kuna watu ambao ni “wateule” wa Mungu, kwahiyo kadri unavyowatendea mema hao watu baraka zinakuja kwako “automatically” hata kama wewe si mkristo. Rahabu aliwatendendea mema wapelelezi wa Israel baraka zikaenda kwake “automatically” bila kujalisha kwamba alikua kahaba.

Yatima, wajane, maskini, wazee, wagonjwa na wengine wenye uhitaji ni wateule wa Mungu. Kwahiyo ukiwatendea mema watu hawa baraka zinakuja kwako hata kama wewe ni mwenye dhambi.

Kwa mfano kama kuna watoto yatima unawasomesha, au kuna wajane unawasaidia mahitaji yao, au wagonjwa unawasaidia matibabu, si rahisi Mungu kuondoa mkono wake wa baraka kwako hata kama wewe ni mwenye dhambi. Mungu akiondoa baraka kwako watu wake watateseka.

Wale yatima, wajane, wagonjwa ambao wewe ni msaada kwao kila wakiomba Mungu huongeza baraka kwako ili uzidi kuwahudumia. Inawezekana maombi yako hayafikagi kwa Mungu lakini unabarikiwa kwa sababu ya maombi ya hao unawaosaidia.

Kuna wakati Mungu anaweza kuamua kuzipiga dhoruba biashara za wenzako, lakini ya kwako ikasimama imara. Si kwa sababu wewe ni mwema sana, bali kwa sababu kuna watu wanamlilia Mungu kwa ajili yako. Kuna wanategemea ada za shule kwenye hiyo biashara yako. Kuna watu wanategemea pesa za matibabu kwenye biashara yako. Kwa hiyo Mungu akiyumbisha biashara yako atakua anawaumiza watu hao. So ili asiwaumize anaamua kukuaacha. Hiyo ni kamba nyekundu.!

Kuna wakati wenzio wakifanya makosa madogo kazini wanafukuzwa kazi, lakini unajishangaa wewe umefanya makosa makubwa na hufukuzwi. Si kwa sababu una bahati sana. Ni kamba nyekundu. Kuna watu walioko nyuma yako ambao ni wateule wa Mungu. Kuna yatima wanategemea kulipiwa ada kwa mshahara wako, kuna wagonjwa wanategemea kusaidiwa hela za matibabu kwenye mshahara wako, kuna wajane wanategemea hela ya kuishi kutoka kwako. Kwahiyo Mungu akikuadhibu anakua amewaadhibu na wao. Kwahiyo ili wapone inabidi akulinde hata kama umefanya kosa kazini. Unashangaa tu kesi imeisha hata kwa namna ambayo hujui. Hiyo ni kamba nyekundu.!

Kuna mtu ambaye ni maskini wa kutupwa hana hata uwezo wa kununua sukari. Lakini anamuomba Mungu kwa imani kuwa ampe sukari aweze kunywa chai kila siku. Kwa kuwa huyo maskini huwa anapata sukari kutoka kwako, Mungu atazidi kukubariki ili uendelee kumhudumia huyo maskini. Hiyo ni Kamba nyekundu.!

Kamba nyekundu ilimuokoa Rahabu na ndugu zake licha ya kwamba alikua kahaba. Jiulize wewe una kamba nyekundu? Je kuna watu wako nyuma yako ambao Mungu akiwaangalia anakubariki, anakuokoa hata kama upo kwenye hatari?

Kama unamsomesha mwanao shule ya “mamilioni” kwa mwaka wakati mtoto wa jirani yako hana hata uniform za kuendea shule, au unatumia “mamilioni” kwa pombe na starehe wakati kuna wagonjwa wanaokufa kwa kukosa panadol, siku Mungu akitaka kukuadhibu hajiulizi mara mbili maana huna “kamba nyekundu” nyuma yako.

Lakini yule anayesaidia wenye uhitaji, kama yatima, wagonjwa, wazee, wajane,walemavu, au maskini atazidi kubarikiwa tu hata kama ni mwenye dhambi, maana anayo kamba nyekundu.

Hii ni kwa sababu Mungu akitaka kumuadhibu, kabla hajamtizama yeye anatizama kwanza yatima walioko nyuma yake anaowasaidia, anatizama wagonjwa wanaomtegemea kwa matibabu, anatizama wajane. Anaona akimuadhibu, atakuwa ameadhibu na hao wanaomtegemea. Kwa hiyo anaamua kumuacha.

Hii ina maana kuwa baraka na utakatifu ni vitu viwili tofauti. Unaweza usiwe mtakatifu lakini Mungu akakubariki na akakulinda. Unaweza kubarikiwa si kwa sababu unastahili, bali kwa sababu kuna “wanaostahili” wapo nyuma yako wakikupigania kwa baba yao (Yehova). Ndio maana kuna watu wengi wasio Wakristo wanabarikiwa kila siku hata kama hawamjui Mungu. Ni kwa sababu wana “kamba nyekundu”.

Malisa G.J

Jinsi ya kupika Pilau Ya Nafaka Na Nyama Ya Kusaga

Viambaupishi

Mchele 3 vikombe

Nyama ya kusaga 1 LB

Mchanganyiko wa Nafaka (upendavyo) 1 kikopo

(maharagwe, njegere, mbaazi, na kadhalika)

Vitunguu maji kata vipande vipande 3 vya kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi 2 vijiko vya supu

Mafuta ยฝ Kikombe

Mchanganyiko wa bizari (Garam Masala) 2 vijiko vya chai

Vipande vya supu (Maggi cubes) 3

Maji (inategemea mchele) 5

Chumvi Kiasi

Jinsi ya kuandaa na kupika

1) Osha mchele na roweka.

2) Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitunguu mpaka viwe brown.

3) Tia Thomu na tangawizi, kaanga kidogo.

4) Weka nyama ya kusaga, chumvi na garam masala, endelea kukaanga mpaka nyama iwive.

5) Mwaga maji yaliomo katika kopo la nafaka na utie nafaka pekee humo.

6) Tia maji na vipande vya supu (Maggi cubes) huku unavivuruga, koroga kidogo.

7) Tia mchele, koroga kidogo.

8) Funika na pika kwa moto mdogo mpaka karibu na kukauka ukikorogoka kidogo. (kama unavyopika pilau ya kawaida)

9) *Epua uipike katika moto wa oven 350-400 Deg kwa muda wa dakika 15.

*Kama sufuria uliyotumia sio ya kupikia katika oven, mimina katika chombo chochote kinachotumika kwa oven kama bakuli la pyrex au treya za foil.

10) Pakua katika sahani na iko tayari kuliwa.

Jambo usilolijua kuhusu mwili wako

JE WAJUA!โ€ฆ..

Msuli mrefu kuliko yote kwenye mwili wa binadamu unaunganisha kope za macho na sehemu ya kutolea haja kubwa ndo mana kila ukijaribu kubana jicho moja sehemu ya haja kubwa hufunguka bila kutarajia?

.

.

.

.

.
.

.

.

.

.

.

.

.

.

Nakuona unavojaribu kubana jicho โ€ฆ..

UTAKUJA KUNYA BUREEEE, hutaniwiii?!

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Jinsi ya Kujitibu kwa njia ya matunda

Yafuatayo ni magonjwa na njia za kujitibu kwa kutumia matunda

KUTUBU KIUNGULIA

Aliyepatwa na kiungulia ale nyanya 1 asubuhi na jioni1 kitaondoka

JINSI YA KUZUIA KUHARISHA

Kamua maji ya chungwa lita1
Kunywa glass1 kutwa mara 3
Kuharisha kutakata

JINSI YA KUPATA HAMU YA KULA

Andaa juice ya machungwa usichanganye na chochte
Kunywa glass moja siku mara3 mpk iishe Hamu ya kula itakuja

KUTIBU KIDONDA SUGU(kisichosikia dawa)

Yaponde maua ya mchungwa mpaka yawe laini kisha weka kwenye kidonda baada ya kukiosha kitapona

KUTIBU MAGONJWA YA NGOZI

Osha sehemu iliyoathirika ponda maua ya mchungwa na pakaa sehemu iliyoathirka kutwa mara 2 patapona

KUTIBU MAPUNYE NA FANGASI

Chukua majani laiini ya mchungwa yaponde mpk yalainike kisha pakaa palipoathirika

KUTIBU VIDONDA VYA TUMBO

Anika maganda ya parachichi mpaka yakauke vizuri
Yatwange upate unga
Chota unga huo vijiko viwili changanya na asali safi vijiko viwili kula asubuhi na jioni kwa wiki1

JINSI YA KUONGEZA NGUVU ZA KIUMENI

vijiko3 vya unga wa parachichi
Vijiko2vya unga wa hiriki
vijiko3vya asali safi
Changanya kwenye glass1 ya maziwa kunywa asubuhi na jioni

KUTIBU TUMBO LA HEDHI

Chemsha majani ya mparachichi
Kunywa glass1 asubuhi na jioni siku7 litapona

DAWA YA ANAYEKOJOA KITANDANI

Chemsha ndevu za mahindi anywe kikombe cha chai asubuhi na jioni siku3-7

KUTIBU MATATIZO YA FIGO

Chemsha ndevu za mahindi chuja kunywa kikombe cha chai kutwa mara 3 siku 11-21

DAWA YA ASIYEONA VIZURI

Achemshe mizizi ya mahindi chuja kunywa glass1 Kutwa mara 2 kwa siku3

KUTIBU MALARIA

Chukua ndimu7,zikamue kwenye glass
Andaa glass1 ya maji ya dafu
Changanya kunywa kutwa mara2 mpk uponeย (Muone Daktari kwa ushauri kwanza)

JINSI YA KUTOA SUMU MWILINI

Kunywa nusu glass ya maji ya.ndimu kila mwezi kwa muda wa miezi 2 sumu itaondoka mwlini

Alichojibu dalali baada ya kufumwa na mke wa mtu ndani ya nyumba ya kupanga

Dalali aliwatafutia jamaa chumba Buguruni karibu na reli, nyumba nzuri sana. Jamaa na mkewe wakahamia kwa furaha, lakini furaha yao iliisha walipokuja gudundua nyumba ile iko karibu mno na reli treni ikipita mpaka kitanda kinacheza.

Siku hiyo dalali akapita mke akamwita na kumwambia tatizo wakati treni inapita, wakaanza kubishana, yule mama akamwambia dalali kwa kuwa kuna treni itapita sasa hiviโ€ฆ njoo ndani uone mwenyewe.

Bahati mbaya wakiwa wamejilaza kitandani ili dalali aone adhabu wanayopata, Mzee mwenye mali alirudi ghafla, akauliza,

‘Nyie mnafanya nini hapa?’

Masikini dalali kwa woga mkubwa akajibu’ Tunangoja treni’

Huyu mwanamke ni noma cheki alichomwambia mme wake baada ya kumnunulia nguo za ndani

Mume kaingia duka la nguo na kamnunulia mke wake chupi dazeni moja zote za rangi nyeusi, akaenda kumzawadia. Mpenzi akashukuru lakini alipogundua kuwa zote ni nyeusi si akaropoka.
MY HONEY: Sasa umeninunulia chupi zote nyeusi, sasa watu si watadhani nina chupi moja tu sibadili,

Jamaa alifura akawa kama mbogo na hapo ndipo zogo kuu lilipoanza

MUME:Watu gani hao watakaokuambia unachupi moje, inamaana unawaonyesha kitumbua changu? Leo utanambia’
Ungekuwa wewe ungefanya nini?

Angalia huyu msichana alichonifanyia

Kuna siku nilichalala kipesa nikaamua kuomba dem wangu aniazime 10,000/= akanipa.
Baada ya siku mbili nikapata pesa zaidi ya laki nne hivi, nikaamua kumpa 100,000/= mpenzi wangu bila yeye kuniomba.
Baada ya siku 3 akaja kuniambia:- “Bae, ile 10,000/- niliyokuazima mwenyewe amekuja kunidai, so kama unayo naomba unipe nimrudishie maana ananisumbua leo siku ya 3.”
SAA HIZI NIPO ZANGU SINGLE NATAFUTA DEM MWINGINE

Mipango ya Mungu kwetu sisi wanadamu

Utangulizi

Mipango ya Mungu daima ni myema, Mungu anapanga Mema katika maisha ya mtu kama akifuata mapenzi yake. Tatizo ni kwamba watu wanafuata mapenzi yao wenyewe na kisha kukosa yale mema Mungu aliyopanga kwao.

Sio kila jambo jema unalofikiri kulifanya ni jema, kama halipo katika mipango ya Mungu halifai na linaweza kuzuia yale mema Mungu aliyopanga kwako.

Kwa hiyo, jitahidi kufahamu mapenzi ya Mungu na kuyafanya ili uwe katika mipango yake.

Mipango ya Mungu Daima ni Myema

Mipango ya Mungu ni kamilifu na inatufanyia mema ikiwa tutaifuata. Mungu anapanga mema kwa ajili ya maisha yetu, lakini mara nyingi tunashindwa kuona mema hayo kwa sababu tunafuata mapenzi yetu wenyewe badala ya mapenzi ya Mungu. Katika kila jambo tunalofanya, ni muhimu kutafuta kujua mapenzi ya Mungu na kuyatekeleza ili tuweze kuwa katika baraka na neema zake.

Mipango ya Mungu ni Kamilifu

Jeremia 29:11 inasema:
“Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.” (Jeremia 29:11)

Mungu anatuwazia mema na anatupangia maisha yaliyojaa amani na mafanikio. Hata hivyo, ili tuweze kuona mipango ya Mungu ikitimia katika maisha yetu, tunahitaji kumfuata na kutii mapenzi yake.

Tatizo la Kufuata Mapenzi Yetu Wenyewe

Mara nyingi, tunachagua njia zetu wenyewe na kutozingatia mapenzi ya Mungu. Hii inatufanya tukose yale mema ambayo Mungu ameyapanga kwa ajili yetu. Mithali 14:12 inasema:
“Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti.” (Mithali 14:12)

Hii inatukumbusha kwamba si kila jambo tunalofikiri ni jema linakubalika mbele za Mungu. Ni muhimu kujua mapenzi ya Mungu na kuyafuata.

Jitahidi Kufahamu Mapenzi ya Mungu

Warumi 12:2 inasema:
“Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” (Warumi 12:2)

Tunapaswa kubadili mawazo yetu na kujua mapenzi ya Mungu kwa kusoma Neno lake na kuomba mwongozo wake. Kwa njia hii, tutaweza kutambua yale yaliyo mema na kukubalika kwake.

Mifano 10 ya Watu Waliopokea Mema kwa Kufuata Mapenzi ya Mungu

  1. Noa:
    Noa alifuata mapenzi ya Mungu kwa kujenga safina kama alivyoagizwa, na akawaokoa familia yake na wanyama wakati wa gharika. (Mwanzo 6:13-22)
  2. Ibrahimu:
    Ibrahimu alitii mapenzi ya Mungu alipomtoa mwanawe Isaka kama sadaka. Kwa imani yake, alibarikiwa na kuwa baba wa mataifa mengi. (Mwanzo 22:1-18)
  3. Yusufu:
    Yusufu alitii mapenzi ya Mungu hata alipouzwa utumwani na ndugu zake. Mwisho wa yote, Mungu alimtumia kuokoa Misri na familia yake kutokana na njaa. (Mwanzo 37-50)
  4. Musa:
    Musa alifuata mapenzi ya Mungu kwa kuwaongoza Waisraeli kutoka utumwani Misri kwenda kwenye nchi ya ahadi. (Kutoka 3:1-22)
  5. Yoshua:
    Yoshua alitii mapenzi ya Mungu alipowaongoza Waisraeli kuvuka mto Yordani na kushinda mji wa Yeriko kwa kuzunguka ukuta wake kama alivyoagizwa. (Yoshua 6:1-20)
  6. Gideoni:
    Gideoni alifuata mapenzi ya Mungu alipowachagua wanaume 300 kupigana dhidi ya jeshi kubwa la Wamidiani. Kwa imani yake, walipata ushindi mkubwa. (Waamuzi 7:1-25)
  7. Samueli:
    Samueli alitii mapenzi ya Mungu alipomteua Daudi kuwa mfalme wa Israeli, ingawa Sauli alikuwa bado anatawala. (1 Samweli 16:1-13)
  8. Daudi:
    Daudi alitii mapenzi ya Mungu alipompiga na kumuua Goliathi kwa jina la Bwana, na kuokoa Israeli kutoka kwa Wafilisti. (1 Samweli 17:45-50)
  9. Elia:
    Elia alifuata mapenzi ya Mungu alipotangaza njaa na mvua katika Israeli kulingana na amri ya Mungu. (1 Wafalme 17-18)
  10. Maria:
    Maria, mama wa Yesu, alitii mapenzi ya Mungu alipokubali kuwa mama wa Masiya, licha ya changamoto na aibu ambayo ingemkabili. (Luka 1:26-38)

Hitimisho

Mipango ya Mungu daima ni myema. Mungu anapanga mema katika maisha ya mtu kama akifuata mapenzi yake. Tatizo ni kwamba watu wanafuata mapenzi yao wenyewe na kisha kukosa yale mema Mungu aliyopanga kwao. Si kila jambo jema tunalofikiri kulifanya ni jema mbele za Mungu. Kwa hiyo, jitahidi kufahamu mapenzi ya Mungu na kuyafanya ili uwe katika mipango yake. Kwa kufuata mapenzi ya Mungu, tutapata mema yote aliyoyapanga kwa ajili yetu na kuishi maisha yenye baraka na amani.

Ilinde ndoto yako

Ndoto ni nini?

Ndoto ni zile ndoto za kiuhalisia ambazo mtu anaweza kuwa nazo akiwa macho na anatumia mawazo yake kutengeneza au kuunda picha ya maisha anayotamani kuishi siku zijazo. Hizi si ndoto ambazo mtu anaota usiku akiwa usingizini, bali ni matakwa ya dhati ambayo yanamfanya mtu ajizatiti na kutia bidii katika mambo anayofanya ili kuyafikia malengo yake.

Kila mtu ana ndoto tofauti ambazo anatamani kuzifikia, na mara nyingi ndoto hizi huwa zinaongoza maisha yake na kumpa dira na mtazamo wa maisha yake ya baadaye. Ndoto hizi zinaweza kuwa kubwa au ndogo, na zinaathiri jinsi mtu anavyochagua kuishi maisha yake ya kila siku, jinsi anavyofanya maamuzi, na hata jinsi anavyoingiliana na watu wengine.

Kwa mfano, mtu mwenye ndoto ya kuwa Rais atajituma katika masuala ya uongozi, atajifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na siasa na uongozi wa jamii au nchi. Ataweza pia kujihusisha na harakati mbalimbali za kijamii au kisiasa ili kujenga umaarufu na kuwa na uwezo wa kufikia ndoto yake.

Kwa upande mwingine, mtu anayetamani kuwa mwimbaji bora atajikita katika kuendeleza kipaji chake cha uimbaji, kuhudhuria mashindano ya muziki, na pengine atajitahidi kuwa karibu na watu wengine waliofanikiwa katika tasnia hiyo ili ajifunze mbinu za kufanikiwa.

Wale wenye ndoto za kumiliki vitu kama nyumba za kifahari, magari, au kuwa bilionea, mara nyingi wanajikuta wakihusika katika kufanya kazi kwa juhudi zaidi, kujifunza na kutafuta taarifa juu ya uwekezaji, na kutafuta njia bora za kukuza uchumi wao binafsi.

Ndoto za kutembelea nchi fulani zinaweza kumfanya mtu aweke akiba ya pesa, ajifunze kuhusu tamaduni mbalimbali, na hata kujifunza lugha tofauti ili kujiandaa kwa safari yake. Kwa kufanya hivi, mtu huyo anajiweka katika nafasi nzuri ya kufikia ndoto yake na kuifanya iwe halisi.

Kwa ujumla, ndoto za mchana ni muhimu sana katika kuhamasisha na kutoa motisha kwa mtu kufikia mafanikio makubwa maishani. Zinamfanya mtu kuwa na malengo, azimio la dhati, na muelekeo wa wapi anapenda maisha yake yawe siku za usoni. Ndoto hizi zinapoambatana na mipango mizuri na jitihada za makusudi, mara nyingi huwa na matokeo chanya na kutimia kwa matarajio ya mtu.

Zote hizo ni ndoto ambazo kila mmoja alikua nazo huenda ni kipindi anakua au hata sasa bado anayo.
Kwa bahati mbaya sana watu wengi wamekuwa na ndoto kubwa sana wakiwa wadogo na kuzipoteza walipoanza kuingia kwenye uhalisia wa maisha.

VITU VINAVYOWEZA KUIPOTEZA NDOTO YAKO.

Ugumu wa Maisha.

Maisha yanavyozidi kubadilika na kuwa magumu ndipo baadhi ya watu huanza kuasahu vile vitu ambavyo walikua wanatamani waje kuwa navyo. Maisha yanapokuwa magumu sana wengi huona haiwezekani tena wao kufikia ndoto zao hivyo kukata tamaa kabisa na kuamua kuwa na maisha ya kawaida.
Mtu anaweza kujitazama vile alivyo na kuona yeye hafananii kabisa kuja kuwa Rais wa nchi hii labda kutokana na familia aliyotokea au maisha yanayoendelea sasa hivi.
Nakuomba kama unapitia hali hiyo anza kuikataa kabisa ili usije kupotea.

Marafiki wabaya.

Marafiki na watu unaokuwa nao mara kwa mara wanaweza kuwa sababu kubwa sana kukupoteza kabisa na kukufanya wewe uache kupigania ndoto yako.
Ndoto yako ni ya thamani sana ndio maana inapata upinzani.
Ndio maana utaambiwa haiwezekani. Ndio maana watakucheka ukiwaambia wewe unataka kuwa Rais wa nchi hii au unataka kua Bilionea.
Mara zote watu wanakuhukumu kutokana na hali uliyonayo sasa hivi.
Unaweza kuachwa na Mpenzi wako umpendaye kwa sababu tu yeye anaangalia maisha uliyonayo sasa hivi na hata ukimueleza ndoto zako haamini kutokana na hali yako ya maisha uliyonayo sasa.

Ufanyeje?

Kaa nao mbali wale watu ambao hawana ndoto kama za kwako. Kaa mbali na watu ambao wanafikiri kama kuku. Yaani wao wamejiona kwamba ni maskini na haiwezekani kuwa tajiri labda kuiba tu. Inawezekana ni watu wako wa karibu sana labda kaka, dada, wazazi.
Ufanyeje?
Usikubali kuwasikiliza weka pamba sikioni. Mimi kuna mtu aliniambiaga hizo ni ndoto za mchana haziwezi kutokea kamwe lakini sijakata tamaa naendelea kufanyia kazi ndoto zangu.

UNALINDAJE NDOTO YAKO?

Iandike.

Kama unasema una ndoto lakini bado ipo kichwani bado hujaelewa maana yake. Katafute Notebook nzuri sana ya gharama Huwezi kuandika ndoto ya kuwa Bilionae kwenye note book ya elfu mbili aisee.
Tafuta notebook ya Gharama hata ya 20,000 ili uweze kuitunza vizuri. Andika kila kitu unachokitaka kwenye dunia hii. Hakikisha umeandika kila Kitu na usiache hata kimoja.
Hii ni njia ya kwanza ya kuilinda ndoto yako. Nikikutana na wewe sehemu Uniambie au unionyeshe kilipo kitabu chako cha ndoto. Andika ni Jinsi gani unaweza kupata vile vitu. Ni ujuzi wa namna gani unahitaji ili uweze kufikia ndoto zako. Ni watu wa namna gani unahitaji kuambatana nao ili ufanikiwe kwenye doto zako. Andika ni Baada ya Muda gani utakua umefikia Ndoto zako. Sasa hapa Ni somo jingine kabisa jinsi ya kuandika malengo. Malengo ya muda mfupi na Muda mrefu.

Soma ndoto zako kila siku Asubuhi na kabla ya Kulala.

Soma kila siku namaanisha kila siku asubuhi na jioni. Kwanini usome kila siku ? Unaichora au unaiingiza picha ya ndoto zako ndani ya ubongo wako hii itakufanya chochote utakachokutana nacho kama hakiendani na ndoto yako uweze kukiepuka na kama kinaendana basi uweze kukivuta. Unaposoma inajijenga kwenye akili yako na kutengeneza ukaribu wa wewe kuifikia zaidi.
Soma na tafakari.

Tenga Muda peke yako.

Hakikisha unatenga Muda wa peke yako angalau kila wiki ukiwa peke yako sehemu ambayo haina usumbufu wowote. Sehemu hiyo utakua unaipa akili yako nafasi ya kutafakari juu yako wewe. Jitazame ulivyo sasa halafu jitazame wewe ukiwa umefikia kwenye ile ndoto yako. Kama ni gari basi anza kujiona jinsi unavyoliendesha lile gari la ndoto yako. Kama ni Rais ebu jione ukiwa Ikulu basi Jione ukiongoza majeshi. Kama ni Bilionea anza kuona ukiwa Bilionea utakavyokua. Utakavyoweza kubadilisha maisha ya watu wengi sana Duniani. Ona jinsi dunia inavyofurahia Mungu Kukuumba wewe kwasababu maisha yao yamebadilika. Nashauri hili ufanye angalau lisaa limoja ukiwa peke yako bila simu wala kifaa chochote cha mawasiliano.

Soma Vitabu na Fanyia Kazi ndoto yako Kila siku.

Soma vitabu ambavyo vitakuza ufahamu wako ili wewe uweze kuifkia ndoto yako.
Kama unataka kuwa Rais wa Nchi lazima ujue kua unakwenda kuongoza watu hivyo vitabu gani usome ili ukuze ufahamu wako.
Unataka kuwa Bilionea hutaweza kuwa bilionea na ufahamu ulionao sasa hivi mali zote zinatakiwa ziongozwe na wewe hivyo jijengee tabia ya kujisomea vitu mbalimbali juu ya ile ndoto yako.
Ili ufikie Ubilionea unaanza na hatua moja anza leo kupiga hatua moja moja hadi ufikie kule unakotaka. Usikubali kabisa siku ipite ujafanya chochote juu ya Ndoto yako ni kupoteza fursa.

Kama tunavyojua fursa ya kwanza ni uhai tulionao leo hivyo usitumie vibaya leo siku zote unakuwaga na leo tu. Ukiweza kuipangilia leo vizuri itakufikisha kwenye ndoto yako.

Jipongeze

Kwenye kila hatua unayopiga jipongeze ili kujiongezea hamasa na wewe uweze kusonga mbele. Unaweza kujipa zawadi ndogo ndogo ambazo huwa unazipenda kila unapopiga hatua kuelekea kule unapotaka.

Iseme ndoto yako sehemu yeyote unapokuwa.

Kwanini uiseme kwa sababu una Imani na Imani ni kua na hakika juu ya mambo yasiyoonekana.
Hata Yusuf alianza kuwaambia ndugu zake kwamba anaona ndoto anaona akiwaongoza. Walimkemea lakini hakusita kuendelea kuwaambia.
Hii itakusaidia unapokamilisha iwe ushuhuuda kwamba huyu jamaa alituambiaga anakuja kuwa Rais, Bilionea, Mtu mkuu sana.

Kuwa na ndoto kubwa ni jambo la muhimu sana katika maisha. Mara nyingi, inasemekana kwamba ikiwa una ndoto ambazo hazikutoi usingizi, basi unaelekea katika mwelekeo sahihi. Mara nyingine, watu watakuita mchawi au Freemason wanapoona unafanikiwa. Lakini, kumbuka, maneno hayo hayana msingi kama yanasemwa wakati unapoanza tu kuota ndoto zako kubwa, kama vile kujenga ghorofa au kumiliki gari la kifahari kama BMW, wakati huna chochote.

Watu wanaokatisha tamaa mara nyingi ni wale wale ambao hawawezi kuona mbali kuliko hali yako ya sasa. Hawaelewi kwamba ndoto huenda zaidi ya hali ya sasa. Kama mtoa hamasa Norman Vincent Peale alivyosema, “Panda picha ya mafanikio ya kustaajabisha katika akili yako. Fikiria hili kwa nguvu. Kisha, fanya kazi kwa ujasiri kila siku kufanya picha hiyo kuwa uhalisia.”

Ni muhimu pia kutambua kwamba kuisema ndoto yako, kuiweka wazi mbele ya wengine na kujiamini, kunaweza kukujengea ujasiri. Hiyo ina maana ya kuendelea kutafakari kwa bidii jinsi ya kuifanya ndoto yako iwe kweli. Usemi unasema, “Ujumbe mzito huvunjika moyo pale unapotamkwa.” Hivyo, endelea kuongea kuhusu matarajio yako, mipango yako, na ndoto zako. Hii itakupa nguvu ya kuvumilia nyakati ngumu na kukusaidia kubaki thabiti katika njia yako.

Naamini una kila kitu kinachohitajika kuilinda ndoto yako. Itapasa uwe na nidhamu, uvumilivu, na azma thabiti. Kikubwa zaidi, uwe tayari kujifunza na kukua. Kila hatua unayopiga kuelekea katika ndoto yako, hata ikiwa ni ndogo, ni hatua muhimu.

Kumbuka kwamba hakuna jambo la maana ambalo hutokea usiku mmoja. Mafanikio ya kweli hujengwa kidogokidogo. Kwa hiyo, hata kama unakabiliwa na kejeli au shutuma, usiruhusu hiyo ikuvunje moyo. Kama alivyosema mwanasiasa na mwandishi wa Marekani Adlai Stevenson, “Ni jambo kubwa kuweza kukumbuka wakati umefanikiwa, kwamba kuna wakati pia uliwahi kushindwa, na kwa vipimo vilevile, ukatumia fursa hiyo kukua na kuboresha.”

Hivyo basi, lipokee wazo la mafanikio moyoni mwako, liweke hai katika mazungumzo yako na hatua zako, na kisha, lifanyie kazi kwa ajili ya kesho yenye matumaini. Jitahidi kwa kila njia kuona ndoto yako ikitimia. Jipe moyo na usisahau kusherehekea kila hatua unayopiga kwa mwelekeo chanya.

Mapishi ya Maini ya kuku

Mahitaji

Maini ya kuku 1/2 kilo
Vitunguu vikubwa 2
Hoho 1
Pilipil 1
Limao 1/2
Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chai
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Mafuta ya kupikia

Matayarisho

Safisha maini weka pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu,swaum na tangawizi pamoja (hakikisha vitunguu visiwe vya brown), kisha tia maini, curry powder, pilipili, chumvi ,hoho na limao kisha changanya vizuri na ufunike. Pika mpaka maini yaive na hakikisha yanakuwa na rojo kidogo. Baada ya hapo ipua na yatakuwa tayari kwa kuliwa na chochote upendacho kama vile chapati, chips, ugali, wali.

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Viambaupishi: Wali

Mchele 3 Magi

Mafuta 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu 3

Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa 1 kikubwa

Pilipli manga 1/2 kijicho chai

Hiliki 1/2 kijiko chai

Karafuu ya unga 1/4 kijiko cha chai

Mdalasini wa unga 1/2 kijiko cha chai

Zaafarani (ukipenda) roweka katika maji 1 kijiko cha chai

Zabibu kavu (ukipenda) 1/4 kikombe

Chumvi kiasi

Jinsi ya kuandaa na kupika

1. Kwenye sufuria tia mafuta na kaanga karoti kidogo.

2. Tia vitunguu kisha tia bizari zote.

3. Tia maji kiasi (kutegemea aina ya mchele) na chumvi

4. Tia mchele upike uwive.

5. Karibu na kuwvia tia zabibu ukipenda.

6. Funika endelea kuupika hadi uwive.

Viambaupishi kwa Nyama

Nyama 2 Ratili (LB)

Chumvi Kiasi

Mafuta 1/4 kikombe

Kitunguu (kata virefu virefu) 1 Kikubwa

Pilipili mboga kubwa 2

(ukipenda moja nyekundu moja kijani)

unazikata vipande virefu virefu.

Figili mwitu (celery) kata vipande Miche miwili

virefu virefu

Jinsi ya kuandaa na kupika

1. Chemsha nyama hadi iwive

2. Ikaange kwa mafuta hadi iwe nyekundu

3. Weka vitunguu, pilipili mboga na figili mwitu

4. Kaanga kidogo tu kama dakika moja.

Hofu inavyo tugharimu katika safari ya ujasiriamali na Jinsi ya kuiepuka

Wengi wetu tunapenda Mafanikio, tunapenda kufika mbali tunapeda kuwa kama Mengi siku moja.

Tunavyo kuwa tunaendelea kutamani kiwa kama wakina Azam au Mengi nyuma ya pazia tuna matatizo nayo ni hofu kuu,

1. Hofu ya kuchekwa
Wengine tuna hofu ya kuchekwa kwamba tunafanya biashara gani hizi? Tuna lima kilimo gani hiki au tunafuga nini? Kuna watu hofu ya kuchekwa tu inatosha kumtoa Barabarani mazima.
Mtua leo hii anashindwa Kuanzisha project anayo peda kwa sababu tu anaogopa kuchekwa

2. Hofu ya kushindwa kabla ya kuanza
Tuna hofu za kushindwa, naona nikifuga kuku nitashindwa, naona nikilima nitashindwa tu, hofu hii inatufanya tuone bora kusubilia kwanza
Fear of Unknown inatusumbua.
Watu tunashindwa kuanzisha miradi kisa tu mtu anaogopa kushindwa.

3.Hofu baada ya kuona walioa anza wakashindwa
Hii ni kubwa sana, mtu anakuambia fulani alifuga Broiler wakafa wote, fulani alifuga layers wakamshinda, Fulani alilima nyanya kavuna debe moja tu, fulani.
Watu wengi tunashindwa kuanza kwa sababu fulani alishindwa. Sikiliza fulani sio wewe, fulani ana akili yake na wewe una akili na nguvu zako.

4. Hofu ya Elimu zetu.
Kuna walio bahatika kusoma hadi Univesity na wana Degree na Wengine Masters. Sasa elimu zetu nazo zimekuwa.kikwazo, mtu anaona kwa elimi yake hapaswi kufanya aina fulani ya biashara, hapaswi kufuga au kulima anapaswa kufungua Yard ya kuuza Magari
Elimu zetu ni.kama tulienda kusomea uoga vile.

5. Hofu ya Ndugu,jamaa, Marafiki na kadhika.
Kuna mtu mpaka sasa hawezi fuga au anzisha mradi kwa sababu tu ndugu jamaa na marafiki hawatamuelewa. Mama hatanielewa kwamba nalima na nimesoma, Mama mkwe na Baba mkwe watanishangaa sana kwamba nafuga Bata,
Mchumba hatanielewa kabisa na anaweza nikimbia mazima kwa sababu nalima Nyanya na nina Degree,

6. Hofu ya kukosa baadhi ya vitu.
Mtu anaona kuliko akose kwenda kutazama mpira na washikaji bora huo mradi usianze tu, kuliko nishindwe kwenda viwanja bora nisianze ,siwezi enda kulala shambani nikashindwa kwenda kuona npira au kucheki move.

Kwa Kifupi tuna hofu nyingi sana zinazo tugharimu.

SASA BASI

Kama unaishi kwenye hofu za aina hizo kamwe sahai kufanikiwa labda tu ukomae na ajira,

Nilazima utambue kwamba uko wewe na honor uwezo wako, ipe heshima Uwezo wako.
Ukiona hofu hizo ni kikwazo kwako na huwezi ziacha kama una mtaji basi kanunue vipande ya hata UTT na usubilia gawio, au nunua hisa za kampuni na subiliaga gawio kulingana na faida.

Kwenye ulimwengu wa Ujasiriamali lazima kwanza Uonekane mwehu, lazima second person akuone kichaa, lazima watu wakushangae ,
Ujue hata kichaa yeye huwa hajui kama ni kichaa ila second person na third ndo tunaona na tunajua kwamba fulani ni kichaa, the same na wewe kwamba lazima ifikie mahali watu washindwe kukuelewa kati ya haya yaani wajiulize maswal mengi bila majibu.
– Fulani hivi kafukuzwa kazi?
– Fulani hivi kweli alimaliza chuo? Au alidisco?
– Fulani anaongea mwenyewe barabarani
-Fulani maisha ni kama yamemkamata, hapa kisa tu huonekani viwanja.
-Fulani haonekani viwanja kabisa.
– Fulani anacheza na ujasiriamali hiyo awaachie wakina Mangi

Watu wakianza story za aina hizi basi jua uko kwenye track nzuri.

UJASIRIAMALI SIO ISHU YA KITOTO, LAIZMA UWE KAMA UKO ULIMWENGU MWINGINE KABISA

Shopping Cart
15
    15
    Your Cart
    ๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About