Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Faida za kula ukwaju

Ukwaju ni tunda maarufu sana ambalo hupatikana katika maeneo yenye uoto wa kitropiki. Kwa kingereza hujulikana kama tamarind, na kwa kitaalamu (botanical name) huitwa tamarindus indica, waarabu huita tamru alhind. Katika baadhi ya maeneo hutumiwa kama kiungo katika mboga.

Ukwaju umetunukiwa viambata muhimu na madini ambayo ni muhimu sana kwa mustakabali wa afya zetu. Una viambata kama calcium, vitamin C, copper, phosphorus, madini ya chuma, magniziam, na pyridoxine. Wataalamu wa afya wanasema kila gramu 100 za ukwaju kuna 36%za thiamin, 35% Iron, 23% magnesium ,na 16%phosphoras.
Pia ukwaju una kiwango kikubwa cha tartic acid Ma citric acid

Namna ya kuutumia ukwaju, tengeza juisi nzuri ya ukwaju, tumia kama kiungo katika chakula, unaweza kutafuna majani yake yenye ladha ya chumvichumvu, au kuyakausha majani ya mkwaju kivulini na kuweka katika uji, au supu au juisi ya matunda.

Zifuatazo ni faida zitokanazo na matumizi sahihi ya ukwaju;

Husaidia kuongeza uwezo wa macho kuona (improving eyesight). Matumizi ya ukwaju kwa kula au kutumia kama juisi huondoa matatizo ya macho na kukufanya uwe na macho yenye afya.

Husaidia kwa wenye kisukari, kwa sababu ukwaju unaviambata muhimu kama polyphenols na flavonoids ambavyo ni madhubuti katika kurekebisha sukari mwilini na kupunguza vitambi.

Husaidia kwa wenye shinikizo la damu .unashauriwa kunywa juisi ya ukwaju Mara kwa mara. Kwasababu ukwaju hupunguza kiwango kikubwa cha lehemu mwilini (cholesterol). Pia unakiwango kikubwa cha madini ya potasiam .licha ya hayo ukwaju unafaida ya kusafisha damu.

Huondoa tatizo la nywele kukatika, na kuzipa mng’aro halisi, chemsha ukwaju, kisha tumia maji yake, changanya na vijiko viwili vya bizari, oshea nywele zako. Kisha ziache nusu saa na uzioshe kwa maji ya vuguvugu.

kuboresha mfumo wa mmeng ‘enyo na kuondoa gesi, tumia juisi ya ukwaju.

Mengineyo ni kupunguza uzito

Kuboresha ngozi yako

Jinsi ya kutengeneza Mkate wa mayai

Mahitaji

Slice za mkate 6
Mayai 3
Chumvi
Olive oil

Matayarisho

Vunja mayai yote katika sahani kisha tia chumvi kidogo sana na uyapige mpaka chumvi ichanganyike. Kisha chukua frying pan na utie vimafuta kidogo na uweke jikoni. Mafuta yakishapata moto kiasi,chovya slice za mkate katika hayo mayai na uzipike pande zote zikishaiva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili kukausha mafuta.Na baada ya hapo mikate yako itakuwa tayari kwa kuliwa na chai.

JE IMANI AU MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI YANAPATIKANA KATIKA BIBLIA?

Wakatoliki wengi huyumbishwa kwa kuambiwa huamini mambo ambayo hayako au ni kinyume na Biblia. Aya zifuatazo zitakusaidia wewe mkatoliki kuelewa au kujua mistari ya Biblia inayofafanua imani katoliki.
1) KUOMBEA MAREHEMU:
2 Mak. 12:38-46
Hek. 3:1
Tob 4:17
2) MATUMIZI YA SANAMU NA VISAKRAMENTI
2Fal 3:20-21
Hes. 21:8-9
Kut. 25:17-22
Kol. 1:20, 2:14
Yn. 12:32
Mt. 19:11-12
3) USAHIHI WA MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI KAMA CHANZO CHA IMANI
2 The 2:15
2 Kor. 10:10-11
Yn 21-25
2 Yoh. 1:12
3 Yoh. 1:13
4) KUABUDU JUMAPILI BADALA YA JUMAMOSI(SABATO)…. Hasa ni kwa sababu Yesu aliitukuza siku ya kwanza ya juma kwa ufufuko wake na kwa kuwatokea wanafunzi wake siku hiyo.
Ufu 1:10
Mdo 20:7
Mt 28:1-8
Lk. 24:1-7
Lk. 24:13ff
1 Kor. 16:1-2
Yn. 20:1-22
5) MAMLAKA YA PAPA KAMA MFUASI AU MRITHI WA MT. PETRO
Yn. 21:15-17
Mt 16:18-19
W 2:1-14
6) MAPADRI KUITWA BABA WAKATI BABA NI MMOJA ALIYEKO MBINGUNI
Mwa 17:4
Yer. 7:7
Hes. 12:14
Yn. 6:49
Mt 23:30
Lk. 1:73
7) JE BIBLIA INATAMBUA MUUNDO WA UONGOZI WA KANISA?
Efe. 4:11-13
1Tim 5:17-25
1Tim 3:1-7,8-18
8) JE BIBLIA INASEMAJE KUHUSU TOHARANI.
Isa 35:8, 52:1
Zek 13:1-2
1Kor 3:15
Lk 12:47-48, 58-59
Ufu 21:27
Ebr 12:22-23
Ayu 14:13-17
9) KUHUSU MATUMIZI YA UBANI
Kut 30:34-37
Hes 16:6-7
Law 16:12-13
Lk 1:10
Ufu 8:32
10) ROZARI IKO KATIKA BIBLIA?
Lk 1:28
Lk 1:42
11) JE KUTUMIA MAJI YA BARAKA NI MAPENZI YA MUNGU?
2Fal 2:19-22
Yn 5:1-18
Yn 7:37
Hes 19:1-22
12) KWANINI TUNAOMBA WATAKATIFU WATUOMBEE?
Mit 15:8, 15:29
Ayu 42:8
Yak 5:16
Mt 16:19
13)KWANINI TUNATUMIA MEDALI, MISALABA, SCAPURALI NA MIFUPA YA WATAKATIFU?
2Fal 13:20-21
14) KWANINI TUNAUNGAMA DHAMBI ZETU KWA PADRI
Mt 16:19,1-20
Yak 5:15-16
15) UBATIZO WA WATOTO WACHANGA UKO KATIKA BIBLIA
Mdo 16:15-33
Mdo 18:8
Mt 28:19
Mdo 10:47-48
16) KUSIMIKWA KWA UTUME
Kut 28:4-43
17) RANGI ZA KANISA
Kut 27:9-29
18) MATUMIZI YA MISHUMAA
Kut 25:31-40; 27:20-21
Hes 8:1-4
19) MPAKO WA MAFUTA YA KRISMA
Kut 30:22-32
20) MPAKO WA MAFUTA YA WAGONJWA
Yak 5:14-15

Huu ndio mlolongo wa michepuko kuwahi kutokea kati ya mke, mume mwanafunzi na boss

BOSS anamwambia sekretari wake: Wiki hii tutaenda wote Serena Hotel kwenye mkutano fanya mipango yote.
SEKRETARI (anamuaga mumewe): Tunaenda na bosi Serena hotel kwenye mkutano for 1 week.
MUME (anampigia mpango wa kando): Mambo safi, wife anaenda kikazi Serena, jitayarishe tujipe raha for 1 week
(Mpango wa kando) anamwambia mwanafunzi wake wa tution: wiki hii nina kazi fulani hakuna tution mpaka week ijayo.
MWANAFUNZI anampigia simu sugar daddy wake ambaye ndo (BOSS): Dear hakuna tution wiki hii nakuja kwako…..

BOSS anamwambia sekretari wake: Siendi Serena tena coz mjukuu wangu atanitembelea.
SEKRETARI: Mume wangu hatuendi Serena
MUME (anampigia Mpango): dah! mpenzi, huyu mke wangu haendi tena. Shit! So hadi next time plz
Mpango wa kando a.k.a teacher (anampigia mwanafunzi): Darasa kama kawaida sorry for the earlier message.
MWANAFUNZI: darling tution inaendelea kumbe, so nakuja wiki ijayo!!
BOSS: Sekretari sorry jitayarishe ile safari ya Serena iko palepale……

Mipango ya Mungu kwetu sisi wanadamu

Utangulizi

Mipango ya Mungu daima ni myema, Mungu anapanga Mema katika maisha ya mtu kama akifuata mapenzi yake. Tatizo ni kwamba watu wanafuata mapenzi yao wenyewe na kisha kukosa yale mema Mungu aliyopanga kwao.

Sio kila jambo jema unalofikiri kulifanya ni jema, kama halipo katika mipango ya Mungu halifai na linaweza kuzuia yale mema Mungu aliyopanga kwako.

Kwa hiyo, jitahidi kufahamu mapenzi ya Mungu na kuyafanya ili uwe katika mipango yake.

Mipango ya Mungu Daima ni Myema

Mipango ya Mungu ni kamilifu na inatufanyia mema ikiwa tutaifuata. Mungu anapanga mema kwa ajili ya maisha yetu, lakini mara nyingi tunashindwa kuona mema hayo kwa sababu tunafuata mapenzi yetu wenyewe badala ya mapenzi ya Mungu. Katika kila jambo tunalofanya, ni muhimu kutafuta kujua mapenzi ya Mungu na kuyatekeleza ili tuweze kuwa katika baraka na neema zake.

Mipango ya Mungu ni Kamilifu

Jeremia 29:11 inasema:
“Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.” (Jeremia 29:11)

Mungu anatuwazia mema na anatupangia maisha yaliyojaa amani na mafanikio. Hata hivyo, ili tuweze kuona mipango ya Mungu ikitimia katika maisha yetu, tunahitaji kumfuata na kutii mapenzi yake.

Tatizo la Kufuata Mapenzi Yetu Wenyewe

Mara nyingi, tunachagua njia zetu wenyewe na kutozingatia mapenzi ya Mungu. Hii inatufanya tukose yale mema ambayo Mungu ameyapanga kwa ajili yetu. Mithali 14:12 inasema:
“Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti.” (Mithali 14:12)

Hii inatukumbusha kwamba si kila jambo tunalofikiri ni jema linakubalika mbele za Mungu. Ni muhimu kujua mapenzi ya Mungu na kuyafuata.

Jitahidi Kufahamu Mapenzi ya Mungu

Warumi 12:2 inasema:
“Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” (Warumi 12:2)

Tunapaswa kubadili mawazo yetu na kujua mapenzi ya Mungu kwa kusoma Neno lake na kuomba mwongozo wake. Kwa njia hii, tutaweza kutambua yale yaliyo mema na kukubalika kwake.

Mifano 10 ya Watu Waliopokea Mema kwa Kufuata Mapenzi ya Mungu

  1. Noa:
    Noa alifuata mapenzi ya Mungu kwa kujenga safina kama alivyoagizwa, na akawaokoa familia yake na wanyama wakati wa gharika. (Mwanzo 6:13-22)
  2. Ibrahimu:
    Ibrahimu alitii mapenzi ya Mungu alipomtoa mwanawe Isaka kama sadaka. Kwa imani yake, alibarikiwa na kuwa baba wa mataifa mengi. (Mwanzo 22:1-18)
  3. Yusufu:
    Yusufu alitii mapenzi ya Mungu hata alipouzwa utumwani na ndugu zake. Mwisho wa yote, Mungu alimtumia kuokoa Misri na familia yake kutokana na njaa. (Mwanzo 37-50)
  4. Musa:
    Musa alifuata mapenzi ya Mungu kwa kuwaongoza Waisraeli kutoka utumwani Misri kwenda kwenye nchi ya ahadi. (Kutoka 3:1-22)
  5. Yoshua:
    Yoshua alitii mapenzi ya Mungu alipowaongoza Waisraeli kuvuka mto Yordani na kushinda mji wa Yeriko kwa kuzunguka ukuta wake kama alivyoagizwa. (Yoshua 6:1-20)
  6. Gideoni:
    Gideoni alifuata mapenzi ya Mungu alipowachagua wanaume 300 kupigana dhidi ya jeshi kubwa la Wamidiani. Kwa imani yake, walipata ushindi mkubwa. (Waamuzi 7:1-25)
  7. Samueli:
    Samueli alitii mapenzi ya Mungu alipomteua Daudi kuwa mfalme wa Israeli, ingawa Sauli alikuwa bado anatawala. (1 Samweli 16:1-13)
  8. Daudi:
    Daudi alitii mapenzi ya Mungu alipompiga na kumuua Goliathi kwa jina la Bwana, na kuokoa Israeli kutoka kwa Wafilisti. (1 Samweli 17:45-50)
  9. Elia:
    Elia alifuata mapenzi ya Mungu alipotangaza njaa na mvua katika Israeli kulingana na amri ya Mungu. (1 Wafalme 17-18)
  10. Maria:
    Maria, mama wa Yesu, alitii mapenzi ya Mungu alipokubali kuwa mama wa Masiya, licha ya changamoto na aibu ambayo ingemkabili. (Luka 1:26-38)

Hitimisho

Mipango ya Mungu daima ni myema. Mungu anapanga mema katika maisha ya mtu kama akifuata mapenzi yake. Tatizo ni kwamba watu wanafuata mapenzi yao wenyewe na kisha kukosa yale mema Mungu aliyopanga kwao. Si kila jambo jema tunalofikiri kulifanya ni jema mbele za Mungu. Kwa hiyo, jitahidi kufahamu mapenzi ya Mungu na kuyafanya ili uwe katika mipango yake. Kwa kufuata mapenzi ya Mungu, tutapata mema yote aliyoyapanga kwa ajili yetu na kuishi maisha yenye baraka na amani.

SMS nzuri sana ya kutakia usiku mwema

Dah! Safari yetu ilikuwa ngumu kweli ila hatimaye tumefika japo ni usiku sana hebu tupige hodi tusije kabwa na vibaka hapa nje. Hodiiiiii, Hodiiiii, Tunaomba tufungulie Mlango,, sisi tunaitwa FURAHA, AMANI na UPENDO. Tumebeba HEKIMA, BUSARA na MAFANIKIO. Tulikuwa wengi HURUMA na UPOLE wanakuja nyuma. CHUKI na WIVU hawana nauli. TABU ni mahututi. SHIDA yuko jela. MATATIZO amepigwa shoti ya umeme. MIKOSI amefariki njiani. LAANA ameliwa na mamba. UVIVU ameungua na maji ya moto hajiwezi. Tutakuwa nawe daima maana tumefika kwa NEEMA . Mungu akulinde na mabaya yote katika dunia hii. ucku mwema.

Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa

Mapishi ya Ndizi na samaki

Mahitaji

Ndizi laini (Matoke 6)
Viazi mbatata (potato 3)
Samaki wabichi wa wastani ( Fresh tilapia 2)
Kitunguu swaum (garlic 6 cloves)
Tangawizi (fresh ground ginger vijiko 2 vya chai)
Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2 kopo)
Vitunguu (onion 1)
Pilipili (chilli 1 nzima)
Chumvi (salt to your taste)
Mafuta (vegetable oil)
Limao (lemon 1/2)
Curry powder (1/2 kijiko cha chai)

Matayarisho

Safisha samaki kisha wakate vipande vitatu. Wakaushe maji kisha wamarinate na kitunguu swaum,tangawizi, chumvi, na limao kwa muda wa masaa 2. baada ya hapo waoke kwenye oven kwa muda wa dakika 30. baada ya hapo andaa ndizi na viazi kwa kuzimenya na kuziosha kisha ziweke pembeni. Kisha katakata vitunguu maji, Tangawizi, vitunguu swaum na nyanya kisha vitie kwenye blenda na usage mpaka mchanganyiko usagike vizuri. Baada ya hapo tia mchanganyiko katika sufuria na ubandike jikoni, acha uchemke mpaka maji yote yakauke. Maji yakisha kauka punguza moto na utie mafuta, curry powder, pilipili na chumvi. Kaangiza mpaka mchanganyiko uive na baada ya hapo tia viazi na maji kiasi na uache viazi vichemke mpaka vikaribie kuiva kisha tia ndizi na samaki na ufunike. Pika mpaka ndizi na viazi viive. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuseviwa.

Mapishi ya Mandazi Matamu

Mahitaji

Unga wa ngano (nusu kilo)
Sukari (Kikombe 1 cha chai)
Chumvi (nusu kijiko cha chai)
Hamira (kijiko kimoja cha chai)
Yai (1)
Maziwa ya unga (vijiko 2 vya chakula)
Butter (kijiko 1 cha chakula)
Hiliki (kijiko1 cha chai)
Maji ya uvuguvugu ya kukandia
Mafuta ya kuchomea

Matayarisho

Tia unga kwenye bakuli kisha tia sukari, chumvi, yai, maziwa ya unga, butter na hiliki kisha uchanganye pamoja mpaka mchanganyiko wote uchanganyike vizuri. Baada ya hapo tia maji ya uvuguvugu kiasi na uanze kuukanda. Ni vizuri ukaukanda kwa muda wa dakika 15 ili kuhakikisha donge lote la unga limelainika vizuri.
Baada ya hapo Tawanyishaa unga uliokwandwa katika madonge 4. Tia unga wa ngano kidogo katika kibao cha kusukumia na uanze kusukuma donge moja katika shape ya chapati na hakikisha haiwi nyembamba sana wala nene sana yani inatakiwa iwe ya wastani.Ukishamaliza kusukuma unatakiwa ukate shape uipendayo na uyatandaze katika kitu kilichopo flat na kiwe kimenyunyuziwa unga wa ngano ili kuyazuia yasigandie. Rudia hiyo process kwa madonge yote yaliyobakia. Baada ya hapo yaweke mandazi katika sehemu iliyokuwa na joto ili yaweze kuumuka (inaweza kuchukua masaa 3 kuumuka). Yakisha umuka unatakiwa uweke mafuta katika karai la kuchomea. Yakisha pata joto la kiasi unatakiwa utumbukize mandazi na unaze kuyachoma mpaka yawe ya brown. Yakisha iva yaipue na uyaweke kwenye kitchen towel iliyakauke mafuta. Yakisha poa yatakuwa tayari kwa kuliwa.

Angalia utofauti wa mawazo ya maskini na tajiri

MASKINI NA TAJIRI WANA MAWAZO TOFAUTI.
Maskini hudhani utajiri ni chanzo cha matatizo.
Tajiri hudhani umaskini ni chanzo cha matatizo.

Maskini hudhani ubinafsi ni kitu kibaya. Tajiri hudhani ubinafsi ni kitu kizuri.

Maskini ana mawazo ya kupata pesa bila kufanya kazi.
Tajiri ana mawazo ya kupata pesa kwa kufanya kazi.

Maskini hudhani tajiri ana tabia ya kuringa.
Tajiri hupenda kuzungukwa na watu sahihi wenye mawazo sawa na ya kwake.

Maskini hutengeneza pesa kwa kufanya kazi asizozipenda.
Tajiri hutengeneza pesa kwa kufanya kazi anazozipenda.

Maskini hudhani kuwa tajiri lazima usome sana.
Tajiri hudhani kuwa tajiri si lazima usome sana.

Maskini hutamani mambo mazuri ya wakati uliopita.
Tajiri hutamani mambo mazuri ya wakati unaokuja.

Maskini huamini ili uwe tajiri lazima ufanye kitu fulani.
Tajiri huamini ili uwe tajiri lazima uwe kitu fulani.

Maskini hupenda kuburudishwa kuliko kuelimishwa.
Tajiri hupenda kuelimishwa kuliko kuburudishwa.

Maskini ana woga.
Tajiri hana woga.

Maskini hufundisha watoto wake jinsi ya kupambana na maisha.
Tajiri hufundisha watoto wake jinsi ya kuwa matajiri.

Maskini hana nidhamu ya mapato na matumizi.
Tajiri ana nidhamu ya mapato na matumizi.

Maskini hufanya kazi kwa bidii kupata pesa.
Tajiri hutumia pesa kupata pesa.

Maskini ni mdogo kuliko matatizo yake. Tajiri ni mkubwa kuliko matatizo yake.

Maskini huamini unahitaji pesa kupata pesa. Tajiri huamini utapata pesa kwa kutumia pesa za wengine.

Maskini ana wivu wa chuki.
Tajiri ana wivu wa maendeleo.

Fikiri kama anavyofikiri tajiri.
Ukifikiri tofauti na anavyofikiri tajiri, utakufa maskini.

#Badilika#
#Shtuka#

Angalia huyu msichana alichonifanyia

Kuna siku nilichalala kipesa nikaamua kuomba dem wangu aniazime 10,000/= akanipa.
Baada ya siku mbili nikapata pesa zaidi ya laki nne hivi, nikaamua kumpa 100,000/= mpenzi wangu bila yeye kuniomba.
Baada ya siku 3 akaja kuniambia:- “Bae, ile 10,000/- niliyokuazima mwenyewe amekuja kunidai, so kama unayo naomba unipe nimrudishie maana ananisumbua leo siku ya 3.”
SAA HIZI NIPO ZANGU SINGLE NATAFUTA DEM MWINGINE

Angalia jinsi maamuzi yako ya jana na ya leo yanavyoweza kukuathiri

By Malisa GJ,
Nimeitoa kwa Comrade Markus Mpangala na kuitafsiri kwa Kiswahili (kisicho rasmi sana).
Mwaka 1998 “Google” walitaka kuiuza kampuni yao kwa “Yahoo” kwa dola Milioni 1 (sawa na Shilingi Bilioni 2) lakini Yahoo wakakataa. Yani Yahoo wakakataa kuinunua Google.

Mwaka 2002 Yahoo wakagundua kwamba walifanya makosa kuikataa Google kwahiyo wakarudi na kutaka kuinunua kwa dola Bilioni 3 (sawa na Trilioni 6). Lakini Google wakataka wapewe Dola Bilioni 5 (sawa na Trilioni 10). Yahoo wakagoma.

Mwaka 2008 kampuni ya Microsoft ikataka kuinunua Yahoo kwa Dola Bilioni 40 (sawa na Trilioni 80) lakini Yahoo wakakataa offer hiyo. Wakaona ni “ndogo”

Lakini Yahoo ikazidi kuporomoka kwenye soko na ilipofika mwaka 2016 hatimaye ikauzwa kwa dola Bilioni 4.6 (sawa na Trilioni 9) kwa kampuni ya Verizon.

#MyTake:

Unajifunza nini kupitia kisa hiki cha Yahoo? Binafsi nimejifunza mambo kadhaa:

#Mosi ni kuhusu fursa. Ukipata fursa leo itumie huwezi kujua kesho itakuaje. Yahoo wamechezea fursa nyingi sana. Kama wangekua makini huenda wao ndio wangekua wamiliki wa Google leo. Au wangeuzwa kwa bei kubwa (Trilioni 80) kwa Microsoft mwaka 2008. Lakini maringo yao yamewafanya kuja kuiishia kuuzwa bei ya “mbwa” (trilioni 9). Usifanye makosa ya Yahoo.!

#Pili ni kuhusu Thamani. Ukiwa kwenye nafasi leo usijione una thamani kuliko asiye na nafasi hiyo. Huwezi kujua kesho itakuaje. Maisha ni kupanda na kushuka. Unaweza kumnyanyasa mtu leo kwa sababu una nafasi fulani, kesho ukaenda kuomba kazi ukakuta ndio “boss” anayeajiri. Unayemuona leo yupo chini kesho aweza kuwa juu, na aliye juu akawa chini. Yahoo ilikua juu sana miaka ya 1990’s lakini kwa sasa imebaki “skrepa”. Hata sijui kama kuna watu wanaitumia siku hizi zaidi ya wale wabibi waliofungua email kipindi kile cha zama za kale za mawe.

Yahoo ilijiona juu kuliko wengine kwahiyo ikadharau kampuni zingine. Hata Google ilipotaka kuuzwa kwa Yahoo mwaka 1998, Yahoo iliona kama vile kuinunua Google ni kupoteza fedha. Leo inatamani kuwa hata “department” ya Google lakini haiwezekani. Usifanye makosa ya Yahoo.!

#Tatu nimejifunza majuto ni mjukuu. Wamiliki wa Yahoo huenda wanajuta sana kwa kupoteza fursa zote zilizokuja mbele yao. Vivyo hivyo katika maisha kuna maamuzi unaweza kufanya leo kesho ukayajutia. Mwanadada anaweza kukataa kuchumbiwa na kijana kwa sababu hana kazi, hana nyumba wala gari. Lakini baada ya miaka kadhaa anamuona yule kijana amefanikiwa kuliko alivyofikiri. Anatamani awe hata mchepuko wake lakini haiwezekani.
Usifanye makosa ya Yahoo.!

#Nne nimejifunza kuwa ukichagua sana nazi utapata koroma. Yahoo walijifanya kuchagua sana. Kila aliyekuja na “Offer” walikataa. Matokeo yake wakaja kuuzwa bei ya kuku za kienyeji kutoka Singida. Mwaka 2008 Microsoft walitaka kuinunua Yahoo kwa Dola bilioni 40 wakagoma. Lakini miaka 8 baadae (2016) wamekuja kuuzwa Dola bilioni 4.6 (yani 10% ya kile walichokua wapewe mwaka 2008).

Vivyo hivyo na binadamu ndivyo tulivyo. Ngoja nitumie mfano wa akina dada ili unielewe vzr. Kuna kina dada kuringa kwao ni fahari. Sisemi kina dada wasiringe. Ni vizuri kuringa lakini isiwe “too much”. Sasa wewe unaringa wanaume zaidi ya 10 waliokuja kukuposa, wote unawakataa unataka uolewe na nani?

Mwenye elimu umemkataa, mwenye gari umemkataa, mwenye nyumba umekataa, mwenye biashara umekataa. Umewakataa wote. Ukija kuhamaki umekuwa kama “Yahoo”… una miaka 35 na huna hata mchumba wa kusingiziwa. Unaanza kwenda kwenye mikesha ya maombi ili upate muujiza. Miaka mitatu inaisha hakuna muujiza wala mazingaombwe.

Unaamua kuweka tangazo gazetini “natafuta mchumba mwenye miaka 40 na kuendelea. Hata kama hana kazi mimi nina kazi tutasaidiana”. Miaka miwili inapita hupati. Unagundua ulikosea kama Yahoo. Hakuna mwanaumwe wa miaka 40 ambaye yupo single. Unarekebisha na kusema kuanzia miaka 25, wakati wewe una 40.

Unaamua kujilipua kama Jackline Wolper na Harmonizer. Au Zari na Diamond. Au Wema na Idris. Hujui wakati Wema anachukua taji la Miss Tanzania Idriss alikua form one?? Lakini leo wanamitana mababy?? Kwahiyo unaona miaka 25 kwa 40 sio issue. Na wewe unaamua kuingia kwenye kundi la “akina bibi wanaolea wajukuu zao”

Lakini hupati “husband material”. Unawapata “maplay boy” wa mjini. Wanakuja wanakuta ni bibi wa miaka 40 wanakuuliza “umemaliza eddah” wakidhani ni mjane umefiwa na mume unataka kuolewa tena. Kumbe hujawahi kutolewa mahari hata mara moja. Wanakuambia ngoja tufikirie, halafu haoooo wanapotea kama Microsoft ilivyopotea mbele ya uso wa Yahoo. Hawarudi ng’o.

Baadae baba yako anaamua kuondoa tangazo la “Jihadhari mbwa mkali” lililokuwa getini anaweka tangazo jipya “tunauza barafu” Na hapo ndipo utakapogundua kuwa vifusi vya mchanga wa mgodini vinaweza kutumika kupiga “plasta” nyumba yenu.

My dear Life is too short to be complicated. Live your life. Enjoy every moment of your life. Tumia fursa zote muhimu unazozipata. Usiringe. Usimdharau mtu. Heshimu kila mtu. Mche Mungu. Usifanye makosa ya “Yahoo”.!

Angalia ndoto nyingine zilivyo na Majanga

Ndoto zingine bwana usiombe zikupate

Mimi usiku wa kuamkia Leo nikiwa nimelala nimeota naendesha gari Yangu aina ya BMW mpya Mara gafla ikakwama kwenye tope .hivyo ikabidi nishuke ili kuisukuma loh! Yani kudadeki ile kuamka nikakuta nimesukuma kitanda hadi sebleni Daaa ilinisikitisha sana jiangalie sana sese hivi ndio narudisha kitanda chumbani .angalizo angalia ndoto unazo ota unaweza kuota upo baharini ukaamka unajikukuta unaogelea kwenye Jaba la Maji shauri yako.

Mvua zazua kasheshe! Soma hii..

Baba- : Halloo mke wangu.. yaani ni shida sitaweza kurudi nyumban, daraja limevunjika na kutoka morogoro kurudi dar haiwezekani
MAMA:- Mme wangu morogoro ulienda bila kuniaga! ?
BABA:- Ilikuwa ni ghafla sana mke wangu sikuweza kukwambia
MAMA:- kha! Sasa watoto nani atawaangalia
BABA:- Unasemaje! We uko wapi kwan
MAMA:- Niko bagamoyo na daraja limeondolewa na maji sitaweza kurudi.
BABA:- Unasemaje we mwanamke.. nakwambia nikukute nyumban ndani ya dk 15
Baada ya dk 15 Baba kafika nyumban.
MAMA:- Haya umefkaje kutoka morogoro?
BABA:- Nimepewa lift na helkopta ya Mbowe..

Kama umeipenda shea na rfiki zakooo…..

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About