Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

JITAMBUE : Maisha yako ya kesho hayalingani na maisha yako ya jana, Anza sasa

THERE IS NO FUTURE IN THE PAST.** Ukitaka kufanikiwa usiangalie nyuma yako kunanini na ulishindwa mara ngapi. Siku zote kukaa Chini nakuanza kujuta kwa makosa uliofanya uko nyuma nikupoteza muda, huo muda Utumie kwa kupanga ya kesho.

Bahati nzuri Mungu alitujalia kusahau, ivyo siku zote sahau ya nyuma na waza yale ya mbele yako.

Maisha bora ya mbele hayawezi kuja kama akili yako imebeba kushindwa kwa nyuma.

Binadamu yeyote anayeweza kupoteza muda wake wa leo kwa kulaumu mabaya ya jana, kesho atapoteza muda akilaumu mabaya ya leo.

Tambua ya kuwa, “hakuna awezaye kurudi nyuma na kuanza upya, bali waweza kuanza leo na kutengeneza maisha yako ya kesho”

Kadri unavyofikiria ya nyuma ndivyo unavyochelewa kufika mbele zaidi. Penda zaidi ndoto yako ya kesho kuliko historia yako ya jana,maana hatima yako siku zote iko mbele na sio nyuma.

Siku zote utashindwa kwa kuendekeza mambo yaliopitwa na wakati maana utakuwa unatumia ujuzi uliopitwa na wakati.

“Habari njema ya siku ni leo, na siku nzuri yako ni ya kesho “

Ukiona umesononeka kwa maisha kuwa magumu jua unaumia kwaajili ya maisha yako ya nyuma, maana unawaza jinsi ulivyo shindwa kulipa kodi ya nyumba,ulivyoshindwa kulipa umeme, maji, ada za watoto na ulivyoshindwa kuendesha biashara yako au ulivyoshindwa kuitetea ajira yako. Usipoteze Muda wako kwa kuwaza yaliopita badala yake waza kesho yako itakuwaje.

Waswahili wanasema yaliopita si ndwele, tugange yajayo. Huwezi kubadilisha jana, Bali waweza kubadilisha kesho yako kwa kufanya maamuzi leo.

Usipoteze Muda kwa kugeuza shingo yako kutazama ya nyuma, utajikuta unadumbukia katika shimo la maisha magumu.

“You can’t have a better tomorrow if you are thinking about yesterday all the time “

Maisha yako ya kesho hayalingani na maisha yako ya jana. Anza sasa.

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Cornflakes

MAHITAJI

Unga – 1 Kikombe

Sukari ya kusaga – 3/4 Kikombe

Siagi – 125 gms

Yai – 1

Baking powder – 1/2 kijiko cha chai

Zabibu kavu – 1/2 kikombe

Cornflakes iliyovunjwa (crushed) – 2 Vikombe

Vanilla – 1 kijiko cha chai

MAANDALIZI

Tia kwenye mashine ya kusaga (blender) au mashine ya keki, siagi, yai na vanilla uchanganye hadi ichanganyike vizuri.
Tia baking powder, zabibu na unga na changanya vizuri.
Paka siagi sinia ya kupikia ya oveni.
Tengeneza viduara vidogo vidogo.
Weka cornflakes katika sahani ya chali (flat) na zungusha viduara humo kisha upange katika sinia ya oveni.
Pika katika moto wa 350ºF kwa muda wa dakika 20-25 hadi vigeuke rangi na viwive.

AMINI UNA AKILI YENYE UWEZO MKUBWA WA KUBUNI WAZO LA KUWEZA KUKUSAIDIA KUFANIKIWA KIMAISHA

AMINI UNA AKILI YENYE UWEZO MKUBWA WA KUBUNI WAZO LA KUWEZA KUKUSAIDIA KUFANIKIWA KIMAISHA.

Huwa nikikaa na kufikiri ni namna gani binadamu aliweza kubuni ndege, meli kubwa hasa za mizigo, gari na vitu vinginevyo na badae kuja kuwa msaada mkubwa katika dunia yetu ya siku leo hata kurahisisha maisha katika eneo fulani lililokuwa na ugumu kwetu, basi nauona uwezo wa Mungu aliouweka ndani ya binadamu huyu ingawa yeye binafsi kama binadamu wakati mwingine hatulitambui hilo na kama tunalitambua basi ni wachache na wakati mwingine hatujakaa vizuri kuitumia hii fursa ya uwezo huo tuliopewa. Hii inaonyesha ni jinsi gani binadamu alivyo na uwezo mkubwa wa kufanya ubunifu kwa kupitia akili aliyonayo na kuleta mageuzi na mshangao mkubwa katika ulimwengu tunaoishi.

Hebu tazama wengi wa wabunifu waliojitoa kwa kuumiza akili na kubuni vitu vipya katika ulimwengu huu tunaoishi leo hii, ndio tunaowaona matajiri katika dunia hii ya leo kuliko watu wengine waliokataa kutumia uwezo na akili zao walizopewa na Mwenyezi Mungu na zaidi sana kubakia kulalamikia watu wengine wanaofanikiwa. Nataka nikuambie unauwezo mkubwa sana ndani yako unaoweza kuutumia ili kubuni jambo kubwa litakaloleta matokeo chanya na kuwa msaada mkubwa katika jamii yako unayoishi na kwako pia.

Ndio. Una uwezo mkubwa sana tena sana unaoweza kuleta matokeo chanya na makubwa katika ulimwengu wako na ukasahau hata habari ya kuajiriwa na kuanza kujiajiri binafsi kupitia jambo ulilobuni. Tatizo ni kwamba hupendi kutumia akili yako kufikiri kwa upana na kwa kiwango cha juu kwa hofu ya kupoteza muda, kuumiza akili, kutokutaka matatizo (stress), nakadhalika. Kila siku umekuwa ni mtu wa kusema “mimi sitaki kuumiza akili yangu” mara unasema “mimi masuala yanayochosha akili yangu siyataki” unataka kufanya mambo marahisi marahisi ili utoke kimaisha, ni gumu sana kwa namna hiyo rafiki.

“If you do what is easy your life will be hard, but if you do what is hard your life will be easy.” – Les Brown

Nataka nikuambie akili yako inauwezo mkubwa sana, narudia “inauwezo mkubwa sana” tena sana wa kubuni biashara ya kukutoa kimaisha, kutatua matatizo yaliyo magumu kwa jamii iliyokuzunguka, kuleta mbinu na mikakati mipya kwenye kazi au ofisini ili kusaidia kampuni kusimama, nakadhalika. Tatizo unajitetea na kujenga hofu kubwa ndani yako ya kujitoa na kufikiri ili kuhakikisha unaleta matokeo mapya na makubwa mahali ulipo muda huu. Hebu fikiri kama binadamu huyu huyu unayemjua na aliye kama wewe alibuni balbu za umeme anaitwa Thomas Edison kutoka nchini Marekani; na zaidi sana binadamu huyu huyu kama wewe aliweza kugeuza historia ya muonekano wa magari na kuja na kitu kipya zaidi anaitwa Henry Ford, na binadamu huyu huyu aliweza kubuni biashara ya kuuza kuku walioandaliwa kama chakula na hatimaye kuwa na mgahawa mkubwa wa KFC uliosambaa karibu nchi 123 duniani kote anaitwa Harland Sanders. Na wengine wengi sana ambao sitaweza kuwamaliza kwa kuwataja wote mahali hapa siku ya leo.

Naamini wapo watu wanaoweza kujitetea na kusema kwa kuwa hao ni watu weupe yaani wazungu na sijaona mtu mweusi hata mmoja hapo. Hebu fikiri ni watu wangapi wanabiashara ambayo leo hii inawaingizia mabilioni ya pesa na wakati mwingine biashara wanazozifanya ni za kawaida na zilizokuwa zikidharaulika na watu kwenye jamii zao na wapo hapa afrika. Angalia mtu kama Aliko Dangote kwa sasa zaidi ya kujishughulisha na uzalishaji wa cement na bidhaa nyingine za ujenzi na hata biashara zake kubwa nyingine kwa sasa ameenza kuzalisha nyanya na kuuza kwenye nchi yake huko nchini Nigeria. Ulitegemea mtu kama huyu ambaye ni tajiri wa kwanza afrika kuwaza kufanya biashara kama hiyo ya nyaya kwa sasa? Yawezekana wewe ulipoambiwa kuuza nyanya uliona ni biashara kichaa na haina maana ya kuifanya. Ukweli ni kuwa usipende kuanzia pakubwa bali anza na madogo ili kukupeleka kwenye kilele chako cha mafanikio na kutimiliza ndoto yako uliyonayo.

Hivyo hivyo kwa Bakhresa, Mengi, Dewji, Sheria Ngowi na wengine wengi tunaowaona nchini mwetu Tanzania wamefanikiwa kiuchumi, hii yote ni kutokana na kuamua kubuni kitu kipya kilichoweza kuwa msaada mkubwa kwenye jamii yao na kuweza kuwaletea wao mafanikio makubwa katika maisha yao. Sheria Ngowi pamoja na kusomea masuala ya Sheria nchini India lakini alijua bado ana kitu cha ziada ndani yake kinachoweza kumlipa na kumfanya awe na uhuru wa kifedha na maisha mazuri sawa na anavyotaka. Leo hii ni mbunifu wa mavazi Africa nzima inamjua na kumtazama. Jiulize kama asingetumia akili yake kwa kufikiri zaidi na kufuata ndoto yake aliyokuwanayo leo hii ingekuwaje kwake na kwenye jamii yake iliyohitaji mchango wake?

Nataka nikuambie huwezi kutoka kwa siku moja ni lazima uumize kichwa na akili yako leo hii na kujua ni nini cha kufanya kinachoweza kukupa uhuru unaoutaka kesho. Na suala la kuumiza kichwa chako na akili ni sasa na si kesho, narudia tena suala la kuumiza akili yako kwa ajili ya kubuni wazo la kukutoa kimaisha “ni sasa na si kesho” kama unavyofikiri. Usiridhike na maisha yako unayoishi leo, usiridhike na kipato unachokipata huku sema ukweli ndani ya moyo wako na kwa uhalisia hakikutoshelezi kabisa kufikia kwenye kilele cha mafanikio makubwa unayoyataka. Usikubali kuwa mvivu wa kuumiza kichwa na kutumia akili yako kwa ajili ya kuja na kitu kipya kinachoweza kuleta manufaa kwako na kwa jamii yako iliyokuzunguka, anza kuwa mbunifu ili uweze kufikia ndoto yako ya maisha.

Umiza kichwa kuanzia sasa na amini katika wazo (idea) utakayoipata ndani ya moyo na akili yako ili kukusaidia na wewe kuwa miongoni mwa watatuzi wa matatizo katika ulimwengu huu. Unaweza kutumia matatizo yaliyopo kwenye jamii yako kama sehemu ya kukupatia wazo jipya na baada ya hapo kubuni njia na mkakati wa kulitatua tatizo ili kuleta matokeo chanya katikati ya watu waliokuzunguka na kwako pia. Mwombe Mungu akupe mwongozo wa kukusaidia kulitimiza na kulifanya hilo wazo (idea) kuwa wazi katika ulimwengu wa nje ili usibaki na wazo lililo kwenye akili na kichwa tu pasipo kuleta matokeo na mchango wowote makubwa kwa watu wako.

Nakusihi usisubiri kesho. Usione una siku nyingi za kuwaza au kuleta matokeo (ku_implement) ya hilo wazo lako (idea) uliyonayo au ndoto ya siku nyingi unayotembea nayo kila kukicha pasipo kuweka vitendo vya kuifanya izae faida na matunda kwako. Anza leo kuhidhilishia dunia kuwa nawe unauwezo mkubwa aliouweka Mungu ndani yako. Usijikatae wala usiogope kukataliwa na wengine pale utakapofanya uamuzi wa kuja na kitu chako kipya kwenye jamii yako, kumbuka kukataliwa ni sehemu ya kukupeleka katika mafanikio. Kadri unavyoongeza kukataliwa ndio unavyoongeza kufanikiwa.

Kama unahitaji kuwa mbunifu wa mavazi kama sheria ngowi anza kubuni leo hii au ikibidi mtafute na uwe chini yake na afanyike kuwa msaada na mshauri wako (mentor) wa hicho kitu unachotaka kukifanya. Amini inawezekana kwani watu waliofanikiwa si wachoyo unapojishusha na kuonesha uhitaji wa kujifunza kutoka kwao. Kama unataka kuwa mfanyabiashara mkubwa kama Dangote lakini bado huna wazo la biashara. Basi elewa una uwezo mkubwa wa kuumiza kichwa na akili kuanzia sasa na ukapata wazo linaloweza kuishangaza dunia yote hapo badae.

Lakini kumbuka si lazima ukaja na kitu kipya kabisa kwani tambua unauwezo pia wa “kuboresha wazo” au kitu fulani kinachofanyika na watu wengine ila wewe ukaleta ubunifu mpya kwenye hicho kitu na kuleta utofauti mkubwa kwenye eneo (industries) hiyo. Na hii ndio njia inayofanyika kwenye makampuni ya simu, magari, televisheni, nakadhalika. Leo hii samsung akileta simu yenye kamera yenye uwezo wa mega pixel 16 kesho yake utasikia Iphone ametoa simu yake mpya yenye kamera yenye uwezo wa mega pixel 20. Huu ni ubunifu tu ili kuzidi kutawala soko na kuteka wateja wa soko la simu ulimwenguni kote. Nataka nikuambie nawe unauwezo wa kufanya ubunifu mkubwa kwenye jambo lolote lile ili kukuletea mafanikio makubwa na hatimaye ukafanikiwa kufikia katika ndoto yako.

Nataka nikuambie una mawazo milioni na zaidi ndani yako ambayo hadi sasa dunia inayasubiri ili yaweze kuwa msaada kwa watu wengi na kufanyika kuwa faraja kubwa hata kwa watu waliokata tamaa. Ndio. usishangae wala sijakosea kusema ni mawazo “milioni na zaidi” uliyonayo ndani yako. Ni wewe tu umejidharau, ni wewe unajiona huwezi kuwaza na kutoka na kitu kipya au kilichojaa ubunifu, ni wewe tu unajaa hofu ya kukataliwa kisa unaona utaonekana unaiga, huigi kwani hata waandishi wanaoandika kama mimi wanaandika kutokana na walichokipitia kwenye maisha na kujifunza kwa wengine, ni wewe tu unajiona huna lolote na si chochote katika ulimwengu huu hivyo huwezi kufanya mambo makubwa. Unajikosea heshima kwa kujiwiza mawazo hayo ya chini na kumkosea Mwenyezi Mungu yeye aliyekuumba na kukupa akili zote timamu ili uzitumie kwa ajili ya kuwaza na kubuni mambo mapya yanayoweza kuwa msaada mkubwa kwako na kwa jamii yako iliyokuzunguka. Anza kuwaza na kuumiza akili na kichwa chako leo hii, na amini kesho utafanikiwa.

JIAMINI NA AMINI UNAWEZA. ISHI NDOTO YAKO.

Kwa nini Bikira Maria hakuwa anaombwa akiwa hai? Watu na mitume hawakuwa wanasali kumuomba yeye

Kwa hiyo Mitume na wakristu wa mwanzoni hawakuwa kumuomba wakati akiwa hai. Ila Baada ya Kifo chake na kupalizwa kwake Mbinguni walianza ibada kwake.

Kumbuka, Kifo cha Bikira Maria hakijaandikwa kwenye biblia kwa kua wakati anakufa vitabu vya biblia vilikua vimekwishaandikwa

Ndio maana anaitwa Mama wa Wakristu. Mama mbarikiwa

Rejea Ufunuo 12:1-17

Sala ni Hazina

Sala ni Hazina. Kusali ni muhimu sana. Sala unayosali leo inaweza kukusaidia hata miaka kumi ijayo au ikasaidia watoto wa watoto wako. Mungu ni mwenye fadhila na anakumbuka yote. Mwombe Mungu akulinde ukiwa mzima ili uwapo hatarini akukumbuke hata kabla hujamwomba.

Kweli tamaa ni mbaya, mke wa mtu kaponzwa na tamaa, ndio basi tena

Jamaa kaenda kwa mke wa rafiki yake:
JAMAA: Shem nakupenda!
MKE: Hebu toka hapa! Je rafiki
yako akijua? tena koma!
JAMAA: Ntakupa milioni 1!
MKE: Basi njoo kesho mchana
mume wangu akiwa kazini!

Kesho yake Jamaa kaja
na milioni 1 wakamalizana na mke wa rafki yake,
jioni ilipofika
Mume akarudi home na
kumuuliza Mkewe, “Rafki yangu SAM kaleta hela yangu milioni 1?”
MKE akajibu kwa unyonge, “Ndio!”
MUME: Yes! Ndio maana nampenda SAM kanikopa asubuhi jioni karejesha!!!!
Mke hoi……

Soma stori hii, unaweza ukajifunza kitu

Kijana mmoja alisafiri kwa meli na rafiki zake,
wakiwa katikati ya safari yao meli ilianza
kuzama. Watu wengi pamoja na rafiki wa yule
kijana walikufa maji wakati wanajaribu kujiokoa
kwa kuogelea, lakini yule kijana alifanikiwa

kushika ubao ulioelea majini akaanza kuelea nao,
maji yalimpeleka hadi kisiwa cha mbali sana
ambako hakukuwa na watu wala wanyama
isipokuwa wadudu tu! Alifika ufukweni amechoka
sana na asiyeamini tukio lililotokea, akaishi huko
kwa kula matunda. Aliweza kujenga ka-kibanda
kwa shida sana maana hakuwa na shoka wala
panga, hatimaye akaanza maisha mapya.
Aliishi muda mrefu kisiwani na tayari alishazoea
mazingira yale ya shida japo shida haizoeleki.
Mara zote nyakati za jioni aliwasha moto kwa
kupekecha vijiti. Siku moja kama kawaida yake
aliwasha moto nje karibu na kibanda chake, aliota
moto muda mrefu hatimaye akapitiwa na usingizi.
Alilala hapo hapo hadi usiku wa manane
aliposhtushwa na joto kali lisilo la kawaida.
Kumbe moto ulishika nyasi za kibanda chake na
kibanda chote kikaungua moto.Alilia sana na
kumlaani sana Mungu kwa mateso hayo akisema
“Hivi Mungu nimekukosea nini mpaka unitese
hivi? Pamoja na shida zote hizi bado
unaniongezea shida nyingine, umeteketeza makazi
yangu ilhali nimejenga kwa shida, Hukuridhika
kunitenga mbali na familia yangu nilipoishi kwa
raha? Hukuridhika kuwaua rafiki zangu wote
baharini? Kwanini Mungu umekuwa mkatili hivi?
Bora nife tuu maana nimeshachoshwa na hizi
shida!” akaendelea kulalamika na kumlaani Mungu
hadi kukapambazuka.
Ilipofika asubuhi aliiona meli ikija kwa mbali
kuelekea alipo, alishangaa maana hakuna meli
yoyote inayoweza kwenda kisiwa kile labda kama
imepotea njia. Meli ilipofika ufukweni yule kijana
akaifuata, alienda moja kwa moja hadi kwa
kapteni.Kapteni akamwambia “tuliona moto mkali
sana usiku tukahisi ni meli inawaka moto
tukasema tuje ili tutoe msaada..kwa kweli
tumetembea masaa mengi sana hadi kufika hapa,
mshukuru Mungu maana ametumia moto kutuleta
hapa” yule kijana kusikia hivyo alilia sana,
akajilaumu kwa jinsi alivyo mnung’unikia Mungu.
Akaelewa kuwa Mungu ana njia nyingi za kuleta
msaada kwa mtu. Akapiga magoti akatubu huku
akimshukuru Mungu. Safari ya kurudi nyumbani
ikaanza.
FUNDISHO: Wakati mwingine Kuna mambo
mabaya huwa yanatokea katika maisha yetu
yanayotufanya tuone kama Mungu ametusahau.
Tunamnung’unikia na kumlaumu Mungu bila
kujua kuwa Mungu ana njia nyingi sana kutuletea
msaada. Njia za Mungu huwa zinaonekana kama
ujinga fulani, lakini kiukweli ujinga wa Mungu
ndiyo akili kubwa ya mwisho ya mwanadamu.
Tunasahau kuwa mabaya tunayokutana nayo
yanafanya kazi kwa Manufaa ya hatma zetu.
Unaweza fukuzwa kazi usijue kumbe ndio
unaelekea katika kazi bora zaidi, unaweza
kuachwa na mtu uliyempenda sana ukadhani
ndiyo mwisho wa maisha kumbe Mungu
amekuandalia mtu mwingine mwenye mapenzi ya
dhati mtakayefikia malengo ya kujenga familia,
unaweza kukataliwa na kutengwa na ndugu
kumbe Mungu amekuandalia watu-baki
watakaofanikisha ufikie malengo yako pasipo
masimango ya ndugu, hata rafiki wanaweza
kukusaliti kumbe Mungu amewaondoa makusudi
ili kukuepusha na mabaya waliyoyapanga juu
yako. Sasa usimlaumu Mungu ukadhani
anakuzidishia matatizo, hapo anatafuta njia ya
kuyaondoa hayo matatizo.
Mshukuru Mungu kwa Kila Jambo, kwakuwa
hajawahi kukuwazia mabaya. Anakuwazia mema
sikuzote.
Tafadhari Share kama umeipenda na marafiki
zako wajifunze…….

Huu ndio mlolongo wa michepuko kuwahi kutokea kati ya mke, mume mwanafunzi na boss

BOSS anamwambia sekretari wake: Wiki hii tutaenda wote Serena Hotel kwenye mkutano fanya mipango yote.
SEKRETARI (anamuaga mumewe): Tunaenda na bosi Serena hotel kwenye mkutano for 1 week.
MUME (anampigia mpango wa kando): Mambo safi, wife anaenda kikazi Serena, jitayarishe tujipe raha for 1 week
(Mpango wa kando) anamwambia mwanafunzi wake wa tution: wiki hii nina kazi fulani hakuna tution mpaka week ijayo.
MWANAFUNZI anampigia simu sugar daddy wake ambaye ndo (BOSS): Dear hakuna tution wiki hii nakuja kwako…..

BOSS anamwambia sekretari wake: Siendi Serena tena coz mjukuu wangu atanitembelea.
SEKRETARI: Mume wangu hatuendi Serena
MUME (anampigia Mpango): dah! mpenzi, huyu mke wangu haendi tena. Shit! So hadi next time plz
Mpango wa kando a.k.a teacher (anampigia mwanafunzi): Darasa kama kawaida sorry for the earlier message.
MWANAFUNZI: darling tution inaendelea kumbe, so nakuja wiki ijayo!!
BOSS: Sekretari sorry jitayarishe ile safari ya Serena iko palepale……

Jinsi ya kufanya nyuki waingie kwenye mzinga mpya

Ukitaka kuwavutia na kuingiza nyiki kwenye mzinga unatakiwa kufanya yafuatayo;

  1. Tafuta mahali pazuri pa-kuning’iniza mzinga wako.
  2. Weka nta kwenye mizinga yako ili kuwavutia nyuki.
  3. Hakikisha unaweka mizinga yako katika hali ya usafi na kusiwe na wadudu. Nyuki hawapendi kukaa mzinga mchafu.
  4. Hakikisha hakuna siafu wala panya wanaoishi kwenye mzinga.
  5. Ning’iniza mzinga msimu ambao kuna makundi mengi ya nyuki yanayohama. Makundi ya nyuki huama wakati ambao nyuki wamezaliana kwa wingi na kuwepo malikia mwingine kwenye mzinga hivyo kusababisha kuhama ili kuunda kundi jingine. Msimu huo wa mgawanyiko ni rahisi nyuki kufanya makazi katika mzinga wako kwa haraka. Kama haujui msimu wa makundi ya nyuki kuhama waulize wakulima wenzio wanaofuga nyuki katika eneo lako.

Madhara ya soda

Soda ni kiburudisho ambacho si muhimu sana kwa afya.

Aina nyingi za soda zina kafeini ambayo huzuia usharabu (ufyonzwaji) wa madini ya chuma mwilini hasa yatokanayo na vyakula vya mimea Hata hivyo soda zinaweza kutumika kwa kiasi kidogo kama kiburudisho, ila tunapotaka ubora zaidi wa afya zetu inafaa kupunguza matumizi ya soda na badala yake kutumia vinywaji vyenye virutubishi muhimu kama vile maji ya matunda, maziwa, madafu au asusa kama vile matunda, karanga na aina mbalimbali za mboga mfano karoti.

Hii inasaidia pia kutumia fedha kidogo tuliyo nayo kwa vyakula muhimu, hasa ukizingatia badala ya soda moja unaweza kupata mayai matatu au nusu lita hadi lita moja ya maziwa.

Matumizi ya mbaazi kama dawa

Mbaazi ni zao la chakula ambalo linalimwa sehemu nyingi sana hapa nchini, zao hili pia linaweza kutumika kama dawa kwa kutumia majani, mizizi na maua

MAANDALIZI

Chukua majani, maua au mizizi kiasi cha nusu kilo (ni vizuri kama utachanganya vyote) pondaponda na uloweke kwenye maji safi kiasi cha lita 2 kwa muda wa masaa 24.

Chuja na uweke dawa hii mbali na jua/joto, ni vizuri kama ataweka kwenye friji, kunywa kikombe kimoja kutwa mara 3 kwa siku 3

TIBA

Dawa hii inaweza kutibu magonjwa yafuatayo

1-Inauwezo mkubwa wa kushusha homa

2-Husaidia kuponesha vidonda.

3-Husaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi kwa wanawake.

4-Husaidia kupunguza uvimbe

5-Huponyesha kifua na kukohoa.

6-Husafisha kibofu/njia ya mkojo.

7- Huongeza kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbali mbali

Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata

Wali Wa Nazi

Mpunga – 4 vikombe

Tui la nazi – 6 vikombe

Chumvi – Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mchele kisha
Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi.
Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.

Mchuzi Wa Samaki Nguru

Samaki – 4

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi – 2 viijiko vya supu

Kitunguu maji kilokatwakawa – 2 slice ndogo

Nyanya/tungule – 4

Nyanya kopo – 3 vijiko vya supu

Pilipili mbichi – 2

Kotmiri ilokatwakatwa – 3 msongo (bunches)

Bizari ya mchuzi (simba 2) – I kijiko cha chai

Ndimu – 1 kamua

Mafuta – ¼ kikombe

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Katakata samaki mkaange kwa kumtia viungo.
Weka mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu. Vinapogeuka rangi thomu na tangawizi mbichi, nyanya, nyanya kopo, kitunguu na bizari ya mchuzi endelea kukaanga.
Tia maji kiasi na ndimu, pilipili mbichi ilosagwa kisha tia kotmiri.
Mwisho tia nusu ya samaki alokaangwa ukiwa tayari

Bilingani Za Kukaanga Na Viazi

Bilingani – 4 madogodogo

Viazi/mbatata – 3

Nyanya – 3

Majani ya mchuzi/mvuje/curry leaves – kiasi 6-7

Nnyanya kopo – 2 vijiko vya supu

Methi/uwatu ulosagwa – 1 kijiko cha chia

Rai/mustard seeds – 1 kijiko cha supu

Bizari ya manjano/haldi/turmeric – 1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Mafuta ya kukaangia – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

1. Weka mafuta ya kukaangia katika karai

2. Katakakata bilingani vipande vipande vya mraba (cubes) kaanga katika mafuta ya moto hadi yageuke rangi. Eupa weka kando.

3. Katakataka viazi/mbatata vipande vidogodogo vya mraba (cubes) Kaanga hadi viive epua weka kando.

4. Ondosha mafuta yote katika karai bakisha kidogo tu kiasi ya vijiko 2 vya supu.

5. Kaanga rai kisha majani ya mchuzi, na methi/uwatu kisha kaanga nyanya.

6. Tia nyanya ya kopo kisha changanya pamoja bilingani na viazi ikiwa tayari.

Njia 8 za kupata mtaji kwa ajili ya Biashara yako

Njia hizo ni kama ifuatayo!!

1. Mtaji mbadala
Mtaji mbadala unarejelea rasilimali au mbinu ambazo zinaweza kutumika badala ya fedha katika kuendeleza biashara au mradi fulani. Ni muhimu kuelewa kwamba si kila hatua inahitaji matumizi ya fedha taslimu. Kuna nyakati ambapo unaweza kutumia rasilimali zingine ulizonazo ambazo zinaweza kuchukua nafasi ya fedha. Kwa mfano, mtu anaweza kutumia nguvu zake mwenyewe katika kutengeneza kitu kama bidhaa au katika kutoa huduma, hivyo kuokoa gharama ambayo angehitaji kulipa mtu mwingine kufanya kazi hiyo.

Ujasiriamali unahusisha pia kutumia maarifa na uzoefu ambao mtu amepata katika fani au sekta fulani. Maarifa haya yaliyotokana na mafunzo au uzoefu yanaweza kugeuzwa kuwa bidhaa au huduma bila ya gharama za ziada. Halikadhalika, mtaji mbadala unaweza kujumuisha kutumia umaarufu au jina lako kuvutia wateja au wabia bila haja ya matangazo ya gharama.

Kukopa au kuazima ni njia nyingine ya mtaji mbadala. Badala ya kutumia akiba yako ya fedha au kuchukua mkopo wa riba kubwa, unaweza kuazima vifaa au pata mikopo isiyo na riba kutoka kwa marafiki, familia, au taasisi zinazotoa mikopo midogo midogo.

Ubunifu ni sehemu muhimu ya mtaji mbadala. Kwa kutumia ubunifu, mtu anaweza kubuni njia mpya na tofauti za kutekeleza miradi ambazo hazihitaji fedha nyingi. Hii inaweza kujumuisha kufanya biashara kwa njia ya kubadilishana bidhaa na huduma (barter trade) au kuanzisha njia mpya ambazo zinapunguza gharama za uendeshaji.

Kipaji ni rasilimali nyingine ambayo inaweza kutumika kama mtaji mbadala. Kwa mtu mwenye kipaji kikubwa katika sanaa, muziki, riadha, au tasnia nyingine, kipaji hicho kinaweza kuwa njia ya kujipatia kipato bila haja ya kuwekeza fedha nyingi. Uwezo binafsi uliojengwa kama vile uongozi, mawasiliano na uwezo wa kushawishi watu, pia ni mali ambazo zinaweza kutumika kama mtaji mbadala.

Kwa ujumla, dhana ya mtaji mbadala inasisitiza umuhimu wa kuchangamkia rasilimali na vipawa tulivyonavyo, na kutafuta njia mbadala za kufanikisha malengo bila kutegemea fedha taslimu pekee.

2. Kupata mtaji kwa ndugu, jamaa na marafiki

Watu wengi wanakuwa kwenye umaskini wakati wamezungukwa na ndugu matajiri kisa wanaona aibu kuomba msaada, lakini amini usiamini watu wengi wametajirika kupitia ndugu, jamaa na marafiki, mfano mtu tajiri kuliko wote barani Afrika kutoka Nigeria ndugu Dangote yeye alivyotaka kuanza ujasiriamali aliomba msaada toka kwa mjomba wake ambaye alimuazima kama milioni 3 hiv , kwa kuwa aliona fursa kwenye mambo ya ujenzi (cement) yeye akaanza kununua cement na kuuza leo hii ndugu Dangote amekuwa bilionea ambaye amewekeza sana barani Afrika anauza cement, unga , mchele, mafuta, sukari na saa hivi anauza mafuta kule Africa Magharibi hata hapa Tanzania tuna kiwanda chake kule Mtwara,

Kuomba msaada sio ishara ua udhaifu bali ni ishara ya nguvu kwamba unajiamini ndio maana unaomba msaada. kumbuka kwenye neno UJASIRIAMALI kuna neno Jasiri pia, huwezi kuwa na mali bila kuwa jasiri.Umezungukwa na watu waliobarikiwa usisite kuwaambia wakusaidie ,.

3. Kwa kujiwekea akiba.

Watu wengi sana hapa kwetu Tanzania ukiwaambia weka akiba wanakwambia mimi siwezi kuweka akiba, sina utamaduni wa kuweka akiba, hivyo mi nakushauri anza leo kujifunza kuweka akiba, ni ngumu sana kufika juu bila kuweka akiba kwa mfano kama umeajiriwa na unajua biashara fulani inataka milioni 2 ili kuifanya na wewe mshahara wako ni laki 4, kwa nini basi kila mwezi usiweke laki 1 pembeni, ndan ya miaka miwili utakuwa na milioni 2.4 huo ni mtaji wako wewe mwenyewe.

Usisite kuanza kidogo kwa kuweka akiba polepole mpaka ufike huko unakoenda.

4. Pata kazi ya ziada
Kama kipato unachopata hakitoshi unaweza kujitafutia kazi ya ziada kwa muda wako wa jioni au weekend ili uweze kupata ziada ya akiba kwa ajili ya mtaji.

Watu wengi wanatumia muda vibaya, Je baada ya kazi yako unafanya nini? ile saa 10 hadi saa 4 usiku unatumiaje muda wako? Jinsi unavyotumia muda huu itakupelekea kuwa tajiri au maskini

5. Pata Mtaji kwa njia ya kudunduliza
Hii njia ya kudunduliza ndio njia ambayo ni nyepesi kabisa ambayo watu wengi hawaioni, ukiamua kutumia njia hii kamwe huwezi kukosa mtaji, hii ina maana unaanza katika hali ya chini kabisa ya kufanya kitu chochote halafu ile faida unayoipata hauitumii bali unaiwekeza kwenye biashara yako.Tuone mfano wa dada Christine ambaye ni mfano mzuri wa mtaji wa kudunduliza

Christine Momburi alikuwa amejifungua na mume wake walikuwa wamemuachisha kazi kwa hivyo maisha hayakuwa mazuri sana,

Sasa siku moja walitembelewa na mgeni nyumbani kwao yule mgeni alipotaka kuondoka alimpa Christina shilingi 700 ili anunue maziwa ya mtoto, baada ya yule mgeni kuondoka Christina alijiuliza Je aitumie ile sh 700 kununua maziwa au afanyie nini hasa ili iweze kubadili maisha yake? kwa hiyo alijiuliza sana baadae akaamua kuichukua ile hela aende sehemu akanunue nyanya chungu na mboga mboga kwa bei ya jumla. Akazinunua akaenda kuuza, kwa siku ya kwanza ikatoka sh 700 kwenda 1500 akaongeza mtaji wake, ilikufupisha stori baada ya wiki moja Christina akawa na mtaji wa sh 25000/=.

Siku moja akasikia kuna mahali wanajenga wanataka mama lishe wa kuwapelekea chakula akachukua ile tenda akawa anawapelekea chakula, baadae akasikia kuna sehemu wanataka mtu wa kuwapelekea sare za shule. akawa anazidi kukua na kukua na hivi sasa Christina amekuwa ni mjasiriamali mkubwa pale Moshi ana maduka makubwa sana na amehojiwa na vyombo vya habari mbalimbali na yeye amekiri kwamba kudunduliza ndio kuliko mtoa.

Sasa swali la msingi nalotaka nikuulize ni swali lifuatalo:

Swali, Ni je ni Sh 700 ngapi zimepita mikononi mwako? Je ni Sh 7000 ngapi zimepita mikononi mwako? Je ni Sh 70000 zimepita mikononi mwako? vipi kuhusu laki 7 au milioni 7 ngap zimepita mikononi mwako? mara nyingi tumeidharau fedha na kuona ni ndogo lakini kumbuka nilishasema siku za nyuma kuwa kila shilingi inayopita mikononi mwako ni itazame kwa jicho la kimilionea.

Nikukumbushe kuwa tajiri kuna maumivu ambayo utayapitia, watu wengi hawataki kupitia maumivu ndio maana watu wachache sana wanakuwa matajiri., watu wengi wanapenda utukufu lakini hawataki kubeba msalaba.

Hivyo usidharau pesa bali fikiria kwa ubunifu jinsi ya kuizalisha fedha hiyo.

6. Pata Mtaji mdogo kupitia wawekezaji

Wakati mwingine kutokana na mazingira uliyonayo unaweza ukagundua kwamba una wazo zuri sana la biashara lakini hauna mtaji, hapa jambo la msingi ni kuangalia unaweza kumpata vipi muwekezaji ambaye atataka faida, ni afadhali ukawa na wazo ukawashirikisha wengine wakakupa mtaji halafu mkagawana faida kuliko kufa na wazo lako zuri,.

Sisi watanzania tupo nyuma sana katika suala la kufanya biashara pamoja ( Partinership) tofauti na wakenya.
mfano mzuri ni rafiki yangu anaitwa Elisha Edson yuko Iringa, yeye aliwaza kuanzisha kiwanda cha mbao hizi nguzo za umeme, bahati mbaya hakuwa na mtaji wa kutosha akaamua kuongea na marafiki zake zaidi ya 10 akamshawishi kila rafiki yake awekeze kiasi kadhaa cha fedha na kumpatia hisa kwenye kile kiwanda chake, rafiki zake walikusanyika waktoa fedha na sasa kiwanda kimeanzishwa na kinakaribia kutoa nguzo wakati wowote kuanzia sasa.

Je wewe una weza ukatumia njia hii? je una wazo ambalo unajua kabisa hili wazo nikipata wawekezaji wa nanmna hii? masharti yake yanaweza kuwa magumu sababu unaweza kuambiwa uandike mchanganuo wa biashara unao eleweka, na wazo lako la biashara lionekane limetulia kabisa.

Lakini ni afadhali ukapitia mchakato huu kuliko kuwa na wazo zuri halafu wewe huna fedha. na kumbe ungeweza kutoa ajira na kulipa kodi kwa nchi hii na kufanya wenzako wakanufaika na wazo ulilonalo.

7. Mtaji kwa njia ya Mgavi ( Supplier Financing)

Hii ni njia ya uhakika ya kupata mtaji wako. Naomba nitoe stori halisi , Miaka mingi iliyopita kijana mmoja anayeitwa Reginald alikuwa anatafuta kalamu za kuandikia mtaani kwake, lakin bahati mbaya baada ya kutafuta sana kwa muda mrefu alikosa kalamu pale mtaani kwake, jambo hilo lilimfanya aweze kushangaa sana na kujiuliza hivi kweli inawezekana vipi hakuna kalamu hapa mtaani? kwa hyo hilo likamfanya aanze kutafuta mbinu na maarifa ya yeye kuwa mtu ambaye analeta kalamu Tanzania. baada kufanya uchunguzi kwa marafiki mbalimbali wakati huo yeye alikuwa muhasibu tu, akaambiwa Mombasa kuna mtu ana kiwanda cha kalamu na baada ya kufanya mazungumzo na yule ndugu ikaonekana bwana Reginald angeweza kuwa anaingiza kalamu hapa Tanzania lakini hakuwa na mtaji, ndipo hapo ilibidi atumie mali kauli yaani awshawishi wale watu wampatie zile kalamu azilete hapa, aziuze halafu aweze kurejesha fedha na kuchukua faida yake.

Hivyo akaanza hiyo biashara kwenye chumba chake kidogo sebuleni akisaidiwa na familia yake baadae wahamia nje wakatengeneza banda la mabati tayari ikawa ndio kiwanda kwa ajili ya kupaki zile kalamu kwa pamoja. mwaka huo huo wa kwanza bwana Reginald alipata faida kubwa sana takriban bilion ya shilingi

8.Kupitia Taasisi za kifedha
Mada hii ni ndefu sana lakini tutajifunza huko mbele mada inayoitwa Jinsi ya kuishawishi benki ikukopeshe hata kama hukopesheki. hii mada tutaiongelea zaidi huko mbele , lakini nataka tu ujue ili benki ikukope inahitaji uwe na biashara ambayo imeshakuwepo kwa takribani miezi 6 au zaidi, pia watahitaji uwe na mzunguko mzuri wa fedha unaoeleweka, uwe na dhamana ambayo unaiweka ili kama unashindwa kulipa waweze kuichukua ile dhamana, watahitaji uwe umefanya usajili rasmi wa biashara yako., uwe na account ya benk n.k

Sasa basi kwa kuwa watu wanaogopa kwenda benki kutokana na yote haya ndipo unaweza kujaribu kutumia microfinances, hizi ni taasis za kifedha ambazo hutoa mikopo midogo midogo, kwa hiyo angalia kama huko ndiko unapoweza ukaponea. Zaidi ya hayo, taasisi hizi za kifedha zinajulikana kwa kutoa huduma zilizobinafsishwa zaidi, ambazo zinaweza kuwa na manufaa hasa kwa wajasiriamali wadogo na wa kati, watu binafsi, na biashara ndogo ndogo ambazo zinatafuta fursa za kukuza mitaji.

Microfinance institutions (MFI) zina sifa ya kuwa na mifumo inayoweza kufikiwa kwa urahisi, kwani mara nyingi hawana vikwazo vikali vya kielimu au kiuchumi kama vile benki kubwa. Wanaweza kutoa mikopo kwa riba nafuu na wakati huo huo kutoa mafunzo na ushauri wa kibiashara, ambayo yanaweza kuwa na manufaa makubwa kwa wakopaji.

Pia ni muhimu kufahamu kwamba MFI zinaweza kuwa na mitandao mikubwa inayowezesha huduma kufika hata vijijini ambako benki kubwa haziwezi kufika. Hii ina maana kwamba watu wanaoishi maeneo ya vijijini wanaweza kupata huduma za kifedha bila ya kuwa na ulazima wa kusafiri masafa marefu kwenda kwenye miji mikubwa.

Kwa kutumia huduma za microfinance, unaweza kupata fursa ya kuongeza mtaji, kuboresha biashara yako, na hata kupata elimu ya kifedha ambayo inaweza kusaidia katika kufanya maamuzi bora ya kibiashara na kifedha. Ni muhimu kuchunguza chaguzi zilizopo, kulinganisha tofauti za riba na masharti ya mkopo kabla ya kuchukua uamuzi wa kutumia taasisi fulani ya microfinance.

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Wali Wa Mpunga

Mchele wa mpunga – 4 Vikombe

Tui la nazi – 6 vikombe

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mchele kisha

Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi.

Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.

Mchuzi wa nyama Ng’ombe

Nyama – 1 kilo

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa -2 viijiko vya supu

Viazi/mbatata – 2

Kitunguu maji kilokatwakawa (slice ndogo) – 2

Nyanya/tungule – 4

Nyanya kopo – 3 vijiko vya supu

Majani ya mchuzi/mvu – 3 msongo (bunches)

Bizari ya mchuzi (simba 2) – I kijiko cha chai

Ndimu – 1 kamua

Mafuta – ¼ kikombe

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Weka nyama katika sufuri, tia kijiko kimoja cha kitunguu thomu na tangawizi, chumvi, ndimu na chemsha nyama hadi iwive na ibakie supu yake kidogo.
Weka mafuta katika sufuri nyingine, kaanga kitunguu. Vinapogeuka rangi tia majani ya mchuzi endelea kukaanga hadi vigeuke rangi ya hudhurungi (golden brown)
Tia nyanya/tungule, viazi/mbatata, endelea kukaanga mpaka nyanya ziive.
Tia nyama na supu yake kisha tia nyanya ya kopo, kotmiri, bizari ya mchuzi, chumvi uache mchuzi kidogo katika moto hadi viazi viive vikiwa tayari.

Mboga Mchicha

Mchicha – 4 michano/vifungu

Kitunguu – 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 3

Nyanya/tungule – 2

Tui la nazi zito – 1 kikombe cha chai

Chumvi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mboga iache ichuje maji.
Ikatekate kisha weka katika sufuria.
Katika kitunguu maji, kitunguu thomu kisage au kikatekate kidogodogo (chopped), nyanya.
Weka jikoni ipikike kwa maji yake na mvuke.
Tia tui endelea kuweka katika moto mdogomdogo hadi ikaribie kukauka ikiwa tayari.

Angalia hawa wadada walivyoumbuliwa, Huyu kasuku jeuri kweli

Kasuku alisimama mlango wa kuingia supermarket wakapita wanawake watatu akasema nyeupe, nyekundu, kijani. Wale wanawake wakatatizika baada ya mda wakajua ni chupi walizovaa. Wakasema basi kesho tubadilisheni. Siku ya pili wakapita tena kasuku akasema nyeusi, manjano, zambarau. Loh! Wanawake wakastaajabu sana. Wakasema lazima wamshinde yule kasuku kwa hekima. Wakaambiana basi kesho tusivae chupi tuone kama ni kweli anaona mpaka ndani. Siku ilipowadia wakapita mbele ya kasuku akasema- kipilipili, kipara, rasta…

Namna ya Kuifanya ngozi yako kuwa laini bila Madoa

Ili kufanya ngozi yako kuwa laini bila madoa zingatia mambo haya yafuatayo;

1.TUMIA ANTIOXIDANT SERUM.

Sio kila mtu ana bahati ya kupata ngozi laini na nyororo bila kuifanyia kazi. Kwa wengine it a must to work hard ili kupata that perfect skin you have always wanted.

So Ladies you have to change your beauty routine, unatakiwa uanze asubuhi yako in a healthy way. Jinsi unavyoanza siku yako itaonesha kwenye uso wako.

Antioxidants kama vile Vitamin C&E hulinda ngozi yako ili isi dehydrate na pia zile aging radicals zitalindwa from UV-ray pollution na bad dietary habits(kula vibaya). Paka antioxidant serum baada tu ya kutoka kuoga, subiri dakika chache then paka moisturizer yako.

2.KULA PROTEIN YA KUTOSHA.

Kula breakfast ambayo ipo high in protein, husisha mayai, karanga, yogurt nk. Hivi husaidia kujenga collagen ambayo ndio kitu kikubwa ambacho hukusaidia ngozi yako isizeeke mapema. Ngozi yako haitokuwa na mikunjo wala kutepeta. Watu ambao hula protein for breakfast hula kidogo for the rest of the day, na pia protein husaidia kukuza nywele zako.

3.TUMIA SPF.

SPF ni lazima. Kila mmoja weto anapaswa kutumia SPF, hata kama wewe ni mweusi. Na kama hutumii kisa tu unaona kuwa makeup yako na moisturizer yako ina SPF, hiyo haitoshi. Paka SPF usoni, kwenye shingo, juu ya macho, kwenye lips, nyuma ya mikono, yani paka sehemu zote ambazo huwahi kuanza kuzeeka.

4. HYDRATE! KUNYWA MAJI YA KUTOSHA.

Maji ni part kubwa sana ya urembo wa kila mtu. Kila asubuhi baada tu ya kuamka chukua maji ya uvuguvugu kamulia ndimu nusu kisha kunywa. Hii itasaidia kujenga more collagen..na ku-replenish ngozi yako.

5. MOVE YOUR BODY! EXERCISE

Si lazima kufanya yale mazoezi ya kufa mtu, No. Lakini ni lazima angalau uufanyishe mwili wako kazi kidogo. Unaweza hata ukaanza tu na mazoezi ya dakika 10-15 kila siku hadi utakapozoea.

Unaweza ukachagua kufanya Yoga. Kwa kifupi ni fanya kitu chochote ili kufanya heart rate yako ipande asubuhi, kunyoosha viungo vyako, ku-sweat kidogo. Lakini kama unajiweza si mbaya kufanya mazoeze haswa.

Mazoezi yatakupa nguvu for the rest of the day, pumps your blood na kukupa a glow kwa uso wako.

6. KUNYWA GREEN TEA

Yes Loves, green tea sio kwa ajili ya kukufanya upungue tu, bali husaidia pia ngozi yako. Ina-slowdown ageing process ya ngozi yako na kuifanya ionekane bado nzuri.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About