Karibu AckySHINE
Karibu AckySHINE
Chagua Unachotaka Kusoma Hapa
Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.
Namna Biblia inavyomueleza Bikira Maria
Biblia inashuhudia kuwa watu wanatofautiana
Maandiko matakatifu yanawasifu watu mbalimbali kutokana na jinsi walivyomuamini Mungu na kutenda makuu kwa ajili ya taifa lake.Abrahamu alimuamini Mungu akawa tayari kumtolea sadaka mwanae Isaka, tukio lililomfanya apate baraka ya pekee ya kuwa baba wa waamini (Mwa 22:15-18).Yosefu, mwana mpenzi wa Yakobo, alikuwa mwaminifu hata akaliokoa taifa lisiangamie kwa njaa (Mwa 50:20).Musa ndiye mkombozi wa taifa la Mungu katika Agano la Kale: aliongoza Israeli kutoka [[utumwani Misri akalipatia sheria kutoka kwa Mungu katika mlima Sinai. Maandiko ya Agano la Kale yanakiri, “Wala hajainuka kiongozi kama alivyokuwa Musa” (Kumb 34:10-12).Waliofuata ni Yoshua, Debora, Gideoni, Ruthu, Samweli, wafalme Daudi na Solomoni, manabii Eliya, Isaya, Yeremia, Ezekieli na wengineo.Mwishoni Yesu Kristo akamsifu Yohane Mbatizaji akisema, “Ni mkuu kati ya uzao wa wanawake” (Lk 7:24-28).Elizabeti, mama wa Yohane, alijiona hastahili kutembelewa na Bikira Maria, Mama wa Yesu, akamuita, “Mama wa Bwana wangu” (Lk 1:43).Bikira Maria si mtu wa ziada katika mpango wa Mungu bali ni mshiriki mkuu wa ukombozi wa binadamu. Maria amechangia wokovu kwa kukubali mpango wote wa Mungu aliyetaka amzae Mwanae, amlee na kumfuata kiaminifu hadi msalabani, aliposhiriki kumtoa kama sadaka ya kutuokoa. Msimamo wake ulikuwa mmoja tu: “Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema” (Lk 1:38).Tukichunguza nafasi yake katika fumbo hilo, tunaweza kukiri pamoja naye kuwa ni Mwenyezi Mungu aliyemtendea makuu (Lk 1:49), kwa kuwa, “Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu” (Yoh 3:27).Yale yote ambayo Wakristo wengi wanayasadiki kuhusu Bikira Maria, hakujipatia bali alijaliwa na Mwenyezi Mungu huku akiitikia kwa hiari fumbo la mpango wake.
Utabiri kuhusu Bikira Maria kwenye Biblia
Biblia inatupatia utabiri uliotolewa na Mungu mwanzoni mwa historia kuhusu mwanamke atakayemshinda nyoka wa kale (Shetani): “Nitaweka uadui kati yako na huyu mwanamke, kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa chako” (Mwa 3:15). Juu ya [[Eva wa kale, ambaye alidanganywa na kuangushwa na Shetani atende dhambi, imesemwa: “Adamu akamwita mkewe jina lake Hawa, kwa kuwa ndiye aliye Mama wa walio hai” (Mwa 3:20). Hata hivyo Adamu na Eva wa kale wametuletea kifo (Rom 5:12). Mababu wa Kanisa wanamtazama Bikira Maria kama Eva mpya aliyemshinda Ibilisi na kuwa mama wa wote walio hai. Yesu, aliye Adamu mpya, alipokuwa anakamilisha sadaka ya ukombozi pale msalabani alimfanya Mama yake awe Mama wa waliokombolewa kwa kumkabidhi mwanafunzi, tena yule aliyempenda zaidi. “Penye msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mamaye, na umbu la mamaye, Mariamu wa Kleopa, na Mariamu Magdalene. Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, “Mama, tazama, mwanao”. Kisha akamwambia yule mwanafunzi, “Tazama, mama yako”. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake. (Yoh 19:26-27).Utabiri mwingine ulisema, “Tazama Bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamuita jina lake Emanueli, yaani Mungu pamoja nasi” (Isa 7:14). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:34-35, “Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu akakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli. Kwa sababu hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu”. “Imba, ee binti Sion, piga kelele, ee Israeli, furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, ee binti Yerusalemu. Mfalme wa Israeli, naam, yeye Bwana yu katikati yako” (Sef 3:14-15). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:28: “Malaika akaingia nyumbani mwake akamwambia, ‘Furahi Maria, umejaliwa neema kubwa, Bwana yu pamoja nawe’”. “Umebarikiwa wewe katika kila hema la Yuda na katika kila taifa, nao wanaposikia jina lako watafadhaika. Imani yako haitatoka mioyoni mwa watu wanaoukumbuka uweza wa Mungu milele” (Yudithi 14:7; 15:9). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:42, “Akapaza sauti kwa nguvu akasema, ‘Umebarikiwa wewe kuliko wanawake wote, na yeye utakayemzaa amebarikiwa’”.Bikira Maria ni fumbo la ajabu alilolifanya Mungu katika mpango wa wokovu kwa ajili yake na kwa ajili yetu. Jamaa yake Elizabeti alimpongeza tena akiongozwa na Roho Mtakatifu, “Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale uliyoambiwa na Bwana” (Lk 1:45).Hivyo manabii mbalimbali kwa mwanga wa Roho Mtakatifu walimuagua Maria kwa heshima. Mambo yaliyotabiriwa katika Agano la Kale yalitimia katika Agano Jipya: ukombozi ulianza Bikira Maria alipokubali kwa imani fumbo la umwilisho wa Mwana wa Mungu. Bikira Maria hakuwa “chombo” tu kilichotumika bila ya kuelewa, bali alikuwa mshiriki huru wa kazi ya ukombozi ya Mwanae, kwa kuwa alipopashwa habari na malaika alikubali kwa hiari mpango wa Mungu akisema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, na iwe kwangu kama ulivyonena” (Lk 1:38).
Bikira Maria katika maisha ya Yesu
Yesu, kama mtu yeyote mcha Mungu, aliwaheshimu na kuwatii wazee wake: “Basi, akarudi pamoja nao Nazareti, akawa anawatii” (Lk 2:51).Ishara ya kwanza kwenye maisha ya hadhara ya Yesu iliongozwa na Bikira Maria katika arusi ya Kana ya Galilaya, akisukumwa na huruma kwa wenye shida: kwa ombi lake Yesu aligeuza maji kuwa divai, na wanafunzi wake wakamwamini. Yohane alisimulia hivi, “Siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, ‘Hawana divai’. Yesu akamwambia, ‘Mama tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia’. Mamaye akawaambia watumishi, ‘Lo lote atakalowaambia, fanyeni’. Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. Yesu akawaambia, ‘Jalizeni mabalasi maji’. Nao wakayajaliza hata juu. Akawaambia, ‘Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza’. Wakapelekea. Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maj), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi, akamwambia, ‘Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa’. Mwanzo huo wa ishara Yesu aliufanya huko Kana ya Galilaya, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini. (Yoh 2:1-12).Bikira Maria anasifiwa kwanza kwa imani yake kuu kabisa, kuliko kwa kumchukua Yesu tumboni tu. Yesu alitaka kuwainua wasikilizaji wake wafuate mambo ya roho kuliko ya mwili. “Basi, mtu mmoja akamwambia, ‘Mama yako na ndugu zako wako nje, wataka kusema nawe’. Lakini Yesu akamjibu huyo mtu aliyemwambia hivyo, ‘Mama yangu ni nani, na ndugu zangu ni akina nani?’ Kisha akanyosha mkono wake juu ya wanafunzi wake akasema, ‘Hawa ndio Mama yangu na ndugu zangu, maana yeyote anayefanya anavyotaka Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye kaka yangu na dada yangu na mama yangu’” (Math 12:46-50). Vilevile, wakati wa utume wake, alimsikia “mwanamke mmoja katika lile kundi la watu akisema, ‘Hongera kwa mwanamke aliyekuzaa na kukunyonyesha’. Yesu akamjibu, ‘Barabara, lakini heri yake zaidi yule anayelisikia Neno la Mungu na kulishika’” (Mk 11:27-28).
Bikira Maria alivyoshiriki Mateso ya Yesu
Katika kumfuata Mwanae Bikira Maria alitabiriwa wazi na mzee Simeoni uchungu kama upanga utakaopenya moyo wake, “Tazama huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa. Nawe mwenyewe uchungu ulio kama upanga utauchoma moyo wako” (Lk 2:34-35).Bikira Maria alishiriki kwanza mateso ya ukimbizi huko Misri kwa lengo la kumficha Mwanae asiuawe na Herode Mkuu, “Hivyo Yosefu aliamka akamchukua mtoto pamoja na Mama yake akaondoka usiku akaenda Misri akakaa huko mpaka Herode alipokufa” (Math 2:14-15).Bikira Maria alishuhudia hatua kwa hatua kuteswa kwa Yesu; wanafunzi walipokimbia au kumtazama kwa mbali, yeye alikuwa karibu akaona vema kila teso lililompata Mwanae. Kutokana na fungamano la upendo wa ajabu lililokuwepo kati ya Yesu na Mamaye, alipoyashuhudia yote aliteseka sana katika moyo wake safi, kiasi kwamba Bernardo wa Klervoo akasema, “Msalaba wa Yesu uliwasulubisha wote wawili, Yesu mwilini na Mama yake moyoni”. Uaguzi wa mzee Simeoni ulitimia hivyo.Kadiri ya mtume Paulo kuteseka ni kutimiliza yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya Kanisa, “Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo” (Kol 1:24). “… maana tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake” (Rom 8:17b).Pale msalabani Bikira Maria, kwa njia ya mtume Yohane alifanywa Mama wa wote wanaompenda Mwanae; kisha kumzaa pasipo uchungu Bwana wa uzima, pale alituzaa sisi kwa uchungu wa kutisha uliotokana na kumuona Mwanae akifa msalabani. Hata hivyo Bikira Maria aliendelea kumuamini Mwanae aliyeonekana ameshindwa.
Bikira Maria baada ya kifo cha Yesu
Bikira Maria alikuwepo hapo mwanzo wa Kanisa, akilivutia zaidi Roho Mtakatifu kwa sala yake. “Hao wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria Mama yake Yesu na ndugu zake” (Mdo 1:14).Yesu alisema, “Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili, lakini atakapokuja huyo Roho wa ukweli atawaongoza kwenye ukweli wote” (Yoh 16:12-13). Kwa msaada wa Roho Mtakatifu heshima kwa Bikira Maria ilienea katika Kanisa lote tangu zamani kabisa kadiri ya utabiri wake kuwa ataheshimiwa na vizazi vyote, “Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mdogo, hivyo tangu sasa vizazi vyote wataniita mwenye heri” (Lk 1:48).
Mapishi ya Pasta za cream na uyoga
Mahitaji
Pasta (2 na 1/2 vikombe vya chai)
Uyoga (mashroom 2 vikombe vya chai)
Cream (1 kikombe cha chai)
Mafuta (vegetable oil)
Kitunguu (onion 1)
Chumvi
Majani ya basil (dried basil leaves 1/2 kijiko cha chai)
Matayarisho
Chemsha maji ya kutosha kisha tia chumvi na mafuta kidogo katika hayo maji na baadae tia pasta na uzichemshe mpaka ziive kisha uzichuje maji na uziweka pembeni. Baada ya hapo weka mafuta kidogo katika sufuria kisha tia uyoga uliokatwa na uupike mpaka uive. Baada ya hapo tia majani ya basil, chumvi na cream kisha acha ichemke kisha weka vitunguu na upike kwa muda wa dakika 4 kisha malizia kwa kutia pasta. Zichanganye vizuri na mchanganyiko wote kisha zipike kwa muda wa dakika 5. Na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Unaweza kupika nyama ya kuku (chiken breast) iliyokatwa vipande vidogo vidogo kama saizi na shape ya pasta. Vizuri kuikaanga pembeni mpaka iwe brown na kuiva alafu kuimix kwenye chakula baada ya uyoga na vitunguu kuiva alafu unamix cream kumalizia mapishi.
Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Mchuzi Wa Kuku wa Tanduri
Vipimo vya Wali:
Mchele basmati – 3 magi (kikombe kikubwa)
Mchanganyiko wa mboga za barafu
(Frozen vegetables) – 1 ½ mug
Chumvi – kiasi
Mafuta – 3 vijiko vya chakula
Kitungu maji (kilichokatwa) – 1
Bizari ya pilau (nzima) – 1 kijiko cha chakula
Namna Ya kutayarisha na kupika:
Osha mchele uroweke kwenye maji muda wa dakika 20.
Chemsha maji kwenye sufuria kama magi 6.
Tia chumvi.
Yakisha kuchemka unatia mchele, chemsha usiive sana, uive nusu kiini. Mwaga maji na kuchuja wali.
Unamimina Yale mafuta kwenye sufuria unakaanga bizari ya pilau kidogo na kitunguu kabla ya kugeuka rangi ya hudhurungi (brown).
Tia mchanganyiko wa mboga za barafu.,
Mimina wali, changanya vizuri, ufunike na uweke katika moto mdogo kwa dakika 20.
Pakua tayari kwa kuliwa.
Vipimo Vya Mchuzi
Kuku – 2 Ratili (LB)
Chumvi – Kiasi
Mafuta – ¼ Kikombe
Nyanya Kata vipande – 4
Nyanya kopo – 2 vijiko wa chakula
Tangawizi – 1 kijiko ya chakula
Kitunguu saumu(thomu/galic) – 1 kijiko ya chakula
Tanduri masala – 1 kijiko cha chakula
Kotmiri liliyokatwa – 3 vijiko vya chakula
Pilipili mbichi – 2
Pili masala – 1 kijiko cha chakula
Garam masala – ½ kijiko cha chakula
Bizari manjano – ½ kijiko cha chakula
Mtindi – 3 vijiko vya chakula
Pilipili boga (kata vipande virefu) – 1
Ndimu – 2 vijiko vya chakula
Namna ya kutayarisha na kupika:
Kwenye bakuli tia kuku na changanya vitu vyote pamoja isipokua mafuta.
Tia mafuta kwenye sufuria yakisha kupata moto mimina kuku umpike kwa muda ½ saa kwa moto kiasi.
Pakua kuku kwenye bakuli au sahani na ukate vitunguu maji duara na umpambie. Tayari kwa kuliwa.
Ulevi noma! Angalia huyu mlevi alichomfanyia huyu jamaa usiku! Ungekua wewe ungefanyaje?
Jamaa alikuwa amelaa na mkewe saa tisa ya usiku akastuka baada ya kusikia mtu anabisha hodi kwenda kufungua mlango
Akamkuta jamaa kalewa sana mlangoni kwao
JAMAA: Nini tena mheshimiwa kuamshana saa hizi?
MLEVI: Naomba uje unisukume.
Jamaa akiamini kuwa pengine kuna gari la huyu mlevi limezima jirani akamwambia subiri nikavae viatu. Baada ya kuvaa viatu akatoka na wakaanza kusindikizana na mlevi. Mlevi akaongoza njia
mpaka kwenye mabembea ya jirani akakaa kwenye bembea moja na kumgeukia jamaa na kumwambia.. Okay nisukume basi.
Sababu ya mke kupewa dawa badala ya mumewe
Dokta: Mama tumemchunguza mumeo kwa makini sana, jopo lote la madaktari tumekubaliana mumeo anahitaji mapumziko japo ya mwezi. Sasa tafadhali chukua hivi vidonge vya usingizi vitasaidia sana.
Mama: Asanteni sana, sasa niwe nampa mara ngapi?
Dokta: Unatakiwa wewe uwe unakunywa vidonge hivi kutwa mara tatu kwa mwezi mzima, mumeo atapona.
Matumizi ya kahawa kutibu presha ya kushuka au shinikizo la chini la damu
Kahawa husaidia kuongeza presha au shinikizo la damu. Unashauriwa Kunywa kikombe kimoja cha kahawa kunaweza pia kusaidia kupandisha shinikizo lako la damu kwa muda.
Kama unapatwa na kushuka kwa shinikizo la damu mara kwa mara basi kunywa kikombe cha kahawa asubuhi au unywe wakati unakula cha mchana na cha jioni.
Usizidishe matumizi ya kahawa kwakuwa kahawa ina madhara mabaya kwa afya ya mwili kwa ujumla.
Kanuni ya fedha ya matumizi na mipango ambayo itakusaidia ukiifuata
Jifunze kanuni za fedha
kama ilivyoainishwa hapo chini.
Fedha inatakiwa uwe na nidhamu nayo katika kutumia
Hii kanuni inatumika kwenye vyanzo vyako vyote vya fedha ili uwe na mafanikio yenye amani
Tuangalie hapa chini hizi kanuni👇👇👇
Fungu la kumi 10%
Akiba 30%
Matumizi 40%
Dharura 10%
Msaada 5%
Sadaka 5%
👆👆hii kanuni inafanya kazi katika kila hela unayopata kama faida
Mfano : mtu mwenye mshahara wa mil 1 unayoipata kila mwezi baada ya makato
Fungu la kumi 10% (Tithe) hii ni mali ya Mungu si yako!!
👉itakuwa ni sh laki 1 unatakiwa uitoe sehemu unayoabudia kila mwezi na kama unabiashara zako faida yake ndani yake toa fungu la kumi
Pia hata kama ni hela unapewa kama zawadi itolee fungu la kumi
👉faida ya hii
🌸inalinda kazi au Biashara unayoifanya zidi ya adui
🌸magonjwa,ajali , ( vitu vitakavyokufanya utumie hela bila mpangilio),etc yanakuwa mbali nawe
Akiba 30%
👉hii unaiweka kwa matumizi yako ya baadae kama kujenga,kusomesha,kulima, investment, etc
👉unatenga laki 3 kwa mtu anaepokea mil 1
Matumizi 40%
👉hii itatumika kwa matumizi ya kila siku ,chakula ,Maji, etc
👉hapa unatenga laki 4 kwa ajili ya matumizi kwa mtu wa mshahara wa mil 1
👉note : hapa ndio hela yako ya kustarehe inatoka
Angalia matumizi yasizidi hela uliyonayo
👉wengi wao hapa watu ndio inamfanya awe na vyanzo vingi vya hela ili aweze kufanya starehe awezavyo
👉pia hii ndio hela unayotoa kwa ajili ya mbegu (sadaka ya gharama) wanaoifahamu
Dharura 10%
👉hii fedha unaitunza kwa ajili ya vitu usivyotarajia kama msiba, ndugu kuumwa au kukwama etc
👉unatunza laki 1 kwa mtu wa mshahara wa mil 1
Msaada 5%
👉hii inawahusu watoto yatima, wajane na wasiojiweza kama vilema
👉unatoa elfu 50 kwa mtu wa mshahara wa mil 1
👉unaigawa kama unamagroup yote hayo
Sadaka 5%
👉hii unatoa elfu 50 kwa mtu wa mshahara wa mil 1
👉igawe mara NNE coz mwezi una jumapili 4 ambayo utapata ni elfu 12500 ivyo basi kila jumapili peleka sadaka elfu 12500
Note:
👉Kitu chochote kinachoitwa sadaka kiombee kabla hujakitoa kama siku 2 au 3 ndio uitoe
sadaka
👉nakama unahitaji kitu mfano Nguo peleka nguo kwa waitaji uone utakavyopata Nguo
Nyingi
👉chukua mfano Bakhresa na Mengi wanavyojitolea mbona hawaishiwi, siri yao iko kwenye nidhamu hii ya pesa!!
Jaribu na wewe anza hata na kidogo kidogo kuwa na nidhamu na fedha uone nayo itakavyokuheshimu
Soma alichokisema mlevi baada ya kukuta watu wakimpiga mwizi
Mlevi mmoja aliona wananchi wakipiga mwizi akawaambia “mwacheni msimpige, hii tabia yenu ya kupiga wezi mtakuja shtukia mnampiga Yesu, maana imeandikwa atakuja kama mwizi!”
Ushauri wangu kwa leo: Zingatia hili, hamasika, badilika
Tupo kwenye dunia ambayo tulikuta watu na tutawaacha watu.
Vyote tulivyovikuta vilianzishwa na binadamu wengine wenye mawazo mema na wenye mawazo mabaya pia. Vitu vingi tunavyovifanya tunaendeleza tulivyovikuta ni mara chache kukuta kitu kipya ambacho hakitegemei mazingira na asili ya tulivyovikuta.
Hivyo basi kwa vyovyote vile unahitaji mtu wa kukuongoza au kuku Coach ili ufanikiwe katika pande zote za maisha.
Nitakwenda kuzungumzia sehemu kuu tatu za muhimu sana ambazo unatakiwa uwe na watu wa kukuongoza ili uweze kukua na kupanda viwango kila wakati.
Ni vitu vya kawaida sana lakini leo nitakwenda kuzungumzia uone ilivyo muhimu sana wewe kua na vitu hivi maana bila vitu hivi mafanikio yatakua magumu sana kufikia. Safari yako itakua ngumu zaidi kama utakosea sehemu hizi tatu.
Nitaomba tuelewane kwamba hapa huendi kuiga au kuwa hawa watu utakua wewe na utatimiza lile kusudi la Mungu ndani yako.
Kwanza kabisa uko hivyo ulivyo kwa sababu ya mazingira uliyokulia na watu ulioishi nao tangu ukiwa mtoto hadi hapo ulipo.
Kuna tabia nyingi sana unazo kutokana na mazingira uliyokulia.
(Hapa ndipo nakutana na kitu ambacho nakipenda sana kujifunza kwa wengine napenda kujifunza kwenye mazingira mapya na kwa watu wapya kwa kua wameishi maisha ambayo mimi siyajui na wanafahamu vitu vingi ambavyo mimi sifahamu. Watu wana utajiri mwingi sana ndani yao ukiweza kukaa na mtu ambaye humjui kabisa unaweza kujifunza mambo mengi ya ajabu kwake. )
Hawa ndio watu wa Muhimu sana kwenye safari yako usiwakose ili uweze kusonga mbele.
Sifa zao kabla hujawachagua ni za muhimu sana pia ili wasije wakakupoteza badala ya kukufikisha kule unakotaka kwenda.
(a)Awe na mafanikio (Amefika Mbali) kwenye hiyo sehemu.
(b)Awe na Tabia njema zinazokubalika na jamii yake na dini yake. (mfano hapa ukikutana na mtu ambaye anakuelekeza kuhusu biashara na ni mlevi na mzinzi hizi tabia lazima atakuambukiza kwasababu atakua mtu wako wa karibu sana)
(c)Awe amekuzidi sana kwenye kile unachotaka akulelee (akuongoze).
Hizo ni sifa za muhimu tu za kuangalia zipo nyingine nyingi sana utajifunza mwenyewe.
1. Mlezi wako wa Kiroho
Huyu ni mtu wa muhimu sana na nimemweka wa kwanza.
Bila roho hakuna mwili.
Bila roho mwili wako unakua umekufa.
Unahitaji ukue kiroho na upande viwango kila wakati ili uweze kuvutia mafanikio ya nje.
Ukishindwa hapa hata ukiwa bilionaire inaweza kuwa kazi bure.
Hutaweza kuzifurahia hizo pesa.
Tafuta mtu wa kukulelea kiroho.
Mtu wa kukufundisha kumcha Mungu.
Kama huna katafute mtu wa kukulea kiroho sifa nimezitaja hapo juu.
Mtu huyu anatakiwa akufahamu vizuri na wewe umfahamu vizuri.
Yaani muwe na mahusiano ya karibu sana.
Mtu huyu awe anafuatilia maendeleo yako ya kiroho kwa karibu sana.
Haijalishi uko Dini gani lazima umpate mlezi wa roho yako.
Dini ndio inahusika kulisha roho zetu.
Ndio maana hatufundishwi biashara kule.
2. Mlezi wa Mahusiano/Uchumba/Ndoa
Hapa ni kwa muhimu sana.
Ukiwa vizuri kiroho mahusiano yakawa na tatizo hutafika mbali.
Ukiwa vizuri kiroho ndoa ikasumbua nayo ni tatizo.
Tafuta mtu wa kukulea kwa upande huu pia mtu aliefika mbele zaidi yako.
Aliefanikiwa zaidi yako.
Kama unatafuta mchumba tafuta mtu aliye kwenye ndoa na amefanikiwa.
Ukimtafuta single mwenzako atakupoteza😀.
Mtu huyu awe karibu yenu kabisa kulea mahusiano/ uchumba au ndoa yenu.
Hakuna aliyezaliwa anajua kila kitu tunajifunza hapa duniani kwa waliotutangulia na waliopo pia.
3. Mlezi wa Maono yako/Ndoto zako/Malengo yako/Biashara Yako/Pesa. (Coacher).
Mtu huyu ni wa muhimu pia katika maisha yako.
Unataka kumiliki utajiri wa dollar billion moja lazima utafute mtu wa kukulelea na kukuwezesha ufikie huko.
Huwezi kwenda mwenyewe.
Unahitaji mtu wa kukuongoza kwenye kila unachotaka kukifanya.
Wengi wanakata tamaa kwa kua hawana watu hawa wa kuwalelea.
Mtu huyu anatakiwa awe anakufuatilia hatua kwa hatua kwenye kile unachokifanya.
Awe anapata taarifa za maendeleo yako kila wakati ikiwezekana hata kila week.
Ukipata mafanikio yeyote ajue pia ukipata changamoto ajue.
Mtu huyu anatakiwa awe amekupita kwenye kile unachokitaka na hapa huendi kuwa Follower,anakwenda kukutengeneza wewe uwe kiongozi.
Uweze kusimama mwenyewe na hatimae uongoze wengine.
Kwa Tanzania wapo watu wanaofanya kazi hizi kwa malipo pia.
Lakini hapa unaweza kuanza na mtu ambaye una mahusiano nae ya karibu awe anakulelea.
Siku hizi teknolojia imekua rahisi sana unaweza kuwa na mawasiliano na mtu yeyote unayemtaka popote alipo duniani.
Unaweza kujifunza pia vitu vingi sana kupitia mitandao hii kama hapa facebook.
Unaweza kusoma vitabu na vitu vingi sana vile unavyovitaka.
Naomba nimalizie kwa kusema kwamba.
Kwa hiki ulichokipata leo ukikifanyia kazi.
Utakua mshindi uliyezaliwa kuwa.
Utafikia Hatma yako kwa kufuata haya, namaanisha wewe uliyesoma hapa.
I will see you at the top!
Utani kwa wadada wembamba
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Wadada wembamba hebu nenepeni basi mnatupa tabu kusoma maneno ya kwenye kanga jamanii ………mnaviringisha kanga mwili mara 3 mpaka maandishii hayaonekanii
🤣🤣🤣🤣
Maswali na Majibu kuhusu Kanisa Katoliki
Sala ya kanisa ni nini?
Vyanzo vya sala za Kikristo
2. Litrujia ya kanisa
3. Fadhila za Kimungu
4. Matukio ya kila siku
Je, ni sahihi kusali sala kwa kurudia rudia mfano Novena?
Je ni makosa kurudia sala maneno yale yale kwa Mfano Rozari?
Sala kwa Mkatoliki ni nini hasa? Tunaposema sala tunamaanisha nini hasa?
Yesu alifundisha tusali vipi?
Ni ipi sala kubwa ya Kanisa?
Ni ipi sala bora kwa Bikira Maria? Kwa nini Tunasali kwa Bikira Maria?
Kwa nini watu wengi wanaomba kwa Bikira Maria?
Bikira Maria anatuombea kwa jina na mamlaka ya nani?
Je ni halali au ni sawa kwa Bikira Maria kutuombea kwa Jina la Yesu? Na Je tunajuaje kuwa Bikira Maria anaushirika na Yesu?
Je ni kweli kwamba Bikira Maria ni Malkia wa Kipepo?
Umwilisho maana yake ni nini?
Kanisa linafafanuaje fumbo la umwilisho?
Kanisa Katoliki ni nini?
Ni nini Msingi wa Imani na Mafundisho ya Kanisa Katoliki?
2. Mapokeo Matakatifu
3. Mamlaka ya Kanisa
Ni nani ameanzisha Kanisa Katoliki?
Yesu aliweka makanisa mangapi? Yesu hakufanya makanisa mengi?
Kwa kusudi gani Yesu alianzisha Kanisa?
Kanisa linatimiza kusudi la Yesu Kristo kwa namna gani?
2. Kwa Ukuhani wake yaani kuwatakasa watu
3. Kwa Uchungaji wake yaani kuwaongoza watu.
Alama za kanisa la kweli ni zipi?
2. Kanisa ni a Takatifu
3. Kanisa ni Katoliki
4. Kanisa ni la Kitume
5. Kanisa ni la Kimisionari
Kanisa ni Moja maana yake ni nini?
Kanisa ni Takatifu maana yake ni nini?
2. Kristo aliye Mtakatifu alijitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake ili kulitakasa
3. Roho Mtakatifu hulihuisha kwa upendo wake
4. Ndani yake wamo Bikira Maria na Watakatifu wengi wanaoliombea
Kanisa ni Katoliki maana yake ni nini?
Kanisa ni la Kitume maana yake ni nini?
Kanisa ni la Kimisionari maana yake ni nini?
Yesu amemweka nani kuwa mkubwa wa Kanisa?
Kanisa Katoliki laweza kudanganya katika mafundisho yake?
Jimbo Katoliki ni nini?
Tuwaonaje Wakristo ambao sio Wakatoliki?
Nje ya Kanisa Katoliki hakuna Wokovu maana yake ni nini?
Taifa la Mungu limeundwa kwa namna gani?
Maklero ni wakina nani?
Watawa ni akina nani?
2. Kwa kuishi masharti ya injili, utii, ufukara na useja mtakatifu.
3. Kwa kufuata mtindo wa maisha uliokubalika na Kanisa
Walei ni wakina nani?
Ushirika wa Watakatifu ni nini?
2. Ni muungano wa Waamini wote katika Ekaristi Takatifu.
Ni kwa nini Bikira Maria anaitwa Mama wa Mungu? Na kwa nini aheshimiwe?
Je, Bikira Maria kuitwa Mama wa Mungu maana yake ni kwamba yeye ndiye chanzo cha Yesu na Bila yeye Yesu asingekuwepo?
Je Bikira Maria anamwonaje Yesu? Bikira Maria Anamchukulia Yesu kama nani Kwake?
Kwa nini Bikira Maria anapewa Heshima kubwa
Je, Bikira Maria anastahili kuabudiwa? Je Tunamwabudu Maria?
Kwa nini tunamuheshimu Bikira maria na kusali kwake?
Ni kwa nini Bikira Maria anaitwa Mama wa Kanisa?
Bikira Maria anafaida yeyote kwa Kanisa?
Nafasi ya Heshima kwa Bikira Maria ni ipi?
Kwa nini wakatoliki wanaweka sanamu Kanisani?
Sanamu au picha sio haramu bali maana ya hiyo sanamu au picha ndio inaiharamisha.
Tofauti ya Sanamu za Kikatoliki na za kipagani ni Kwamba,
Sanamu za Kipagani: Sanamu hizi huchukuliwa kama Mungu na huabudiwa na kutolewa Sadaka kama Mungu Mwenyewe.
Sanamu za Kikatoliki: Sanamu hizi huchukuliwa kama ishara ya kile inachokiwakilisha, haiabudiwi kamwe bali inaheshimiwa tuu.
Jifunze kupitia Sanduku la Agano na Msalaba wa Yesu
Kwa nini tunasali mbele ya Picha/Sanamu na Hasa kufanya Ishara ya msalaba?
Kwa nini watu wanabusu picha na sanamu?
Je, inafaa tushike neno lolote la Agano la Kale kama Wayahudi?
Je, ufunuo wa Mungu unaweza kufafanuliwa rasmi na kila mtu?
Tupokeeje ufunuo wa Mungu?
Tunaweza kusadiki vipi?
Je, miujiza inaweza kutusaidia tusadiki?
Kanisa linahusika vipi na imani?
Je, tukipata mafundisho ya Kanisa tunapaswa kuyasadiki?
Tunapaswa kusadiki hasa nini?
Je, Mungu amegawanyika sehemu tatu?
Kwa nini Maria anastahili kuitwa “Mama wa Mungu”?
Je, Bikira Maria ni kama Bahasha au chombo cha kumleta Yesu tuu Duniani au anayo thamani zaidi?
Kanisa maana yake nini?
Je, Kanisa ni kundi la binadamu tu?
Je, tunaweza kuambatana na Yesu tukilikataa Kanisa?
Je, Kanisa ni muhimu kwa wote?
Wokovu unapatikana wapi?
Mtu akijua Kanisa ni la lazima kwa wokovu asiingie au ajitenge nalo, itakuwaje?
Je, anayejiunga na Kanisa na kudumu ndani yake ana hakika ya kuingia mbinguni?
Sifa kuu za Kanisa ni zipi na zinapatikana wapi?
Kanisa kuwa moja maana yake nini?
Kanisa kuwa takatifu maana yake nini?
Kanisa kuwa katoliki maana yake nini?
Kanisa kuwa la Mitume maana yake nini?
Kanisa limepewa na Yesu muundo gani?
Je, Yesu amejenga Kanisa lake imara juu ya mwamba?
Papa amejaliwa na Mungu mamlaka gani?
Maaskofu wote wamerithi mamlaka gani?
Maaskofu wanasaidiwa na nani?
Bila ya Maaskofu, mapadri na mashemasi, Kanisa lingekuwaje?
Walei wanaitwa na Mungu kufanya nini?
Watawa wanashika mashauri gani ya Kiinjili?
Ushirika wa watakatifu maana yake nini?
Je, Kanisa linaweza kutuondolea dhambi yoyote?
Ekaristi maana yake nini? Je ni kweli Yesu yupo katika Maumbo ya Mkate na Divai?
26Maana kila mnapokula mkate huu na kukinywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja. 27Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana. (1Kor 11:23-27).
Yesu alituambia nini kuhusu Mwili wake na damu yake?
Damu na Mwili aliotupa Yesu ni nini? Ekaristi ni nini hasa?
Fundisho hili la mwili na damu ya Yesu (Ekaristi) lilikua Agizo tunalopaswa kulitii mpaka leo?
Mitume walitii Fundisho la Ekaristi na waliliishi?
Je mkate na divai vilichukuliwa na Mitume kama nini hasa? walichukulia Ekaristi kama nini?
Je ni lazima Kwa Mkristu kupokea Mwili na damu ya Yesu (Ekaristi)?
Je ni kwa nini madhehebu mengine hawakubali mafundisho haya ya Ekaristi Takatifu, Je ni mara ya kwanza watu kukataa?
Hata wakati Yesu akiyasema maneno haya Wafuasi Wengi Walimwacha kama Biblia inavyosema;
Mitume walifundisha nini kuhusu Mwili na Damu ya Kristu (Ekaristi)?
Je Yesu Yupo Mzima katika Ekaristi Takatifu? Na kwa nini Tunaabudu Ekaristi?
Kwa hiyo basi kama tunavyosoma katika Yoh 6:51; na
Je, daraja takatifu zinahitajiwa kabisa na Kanisa?
Je, wenye daraja wanastahili heshima?
Kanisa linaheshimu marehemu kwa namna gani?
Je, Kanisa linahimiza waamini wapokee Ekaristi wakati gani?
Biblia ni nini? Asili, Historia, waandishi na mipaka yake
Je, Biblia ilipatikanaje? Nini chanzo na asili ya Biblia.
Je, Biblia ndicho kitabu pekee cha neno la Mungu?
Je nje ya Biblia hakuna Neno la Mungu au Maandiko matakatifu?
Je Biblia ndiyo mafundisho ya Mungu pekee?
Biblia inatuthibitishia yenyewe kuwa haijakamilika na Si mambo yote yameandikwa Kwenye Biblia
Biblia inatuambia hivi…”Kuna mambo Mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo Kama yangeandikwa yote, moja baada ya jingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.”…Kwa mstari huu Biblia inatuthibitishia kuwa haikuandikwa vitu vyote.
Je Biblia ni mwisho wa Maandiko ya Mungu?
Sababu ya Kanisa katoliki kutumia mapokeo na Maandiko ya Watakatifu
Yesu alituambia nini kuhusu Neno la Mungu na Mwendelezo wa kazi ya Mungu ya kusema na watu?
Mapishi ya Maini ya ng’ombe
Mahitaji
Maini (Cow liver) 1/4 kilo
Vitunguu (chopped onion) 2
Nyanya (chopped tomato) 1
Kitunguu swaum/tangawizi (ginger /garlic paste) 1 kijiko cha chai
Mafuta ya kupikia
Chumvi
Coriander
Curry powder 1 kijiko cha chai
Limao (lemon) 1/4
Pilipili (scotch bonnet ) 1
Matayarisho
Safisha maini na ukate vipande vidogovidogo na uweke pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu kidogo(visiwe vya brown) kisha tia ginger/ garlic paste,carry powder kaanga kidogo kisha tia nyanya. Kaanga nyanya mpaka zitoe mafuta kisha tia chumvi, pilipili na vimaji kidogo. Acha vichemke kidogo kisha tia maini na uyapike mpaka yaive. Malizia kwa kukamulia limao na kutia coriander kisha ipua na hapo yatakuwa tayari kwa kuliwa.
Eti hili nalo ni kweli kwa dada yako?
Oya people hv kwa mfano Dada yako akisomea sheria ndo anaitwa sister in law? au
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Jinsi ya kupika Mchuzi Wa Ngogwe Na Bamia
Viamba upishi
Ngogwe ½ kg
Kitunguu 2
Bamia ¼ kg
Karoti 2
Mafuta vijiko vikubwa 8
Maji vikombe 3 Mayai 2
Nyanya 2
Chumvi
Hatua
• Osha, menya na katakata nyanya na vitunguu.
• Osha, menya na kata karoti virefu virefu.
• Osha, kata ncha za bamia pande zote na kama ndefu sana kata
vipande viwili.
• Osha, kata vikonyo vya ngongwe, kama ni kubwa kata vipande viwili.
• Kaanga vitunguu, ongeza nyanya, korogoa mpaka zilainike.
• Ongeza ngogwe, karoti, bamia na chumvi, koroga mpaka
zionekane kukolea rojo.
• Ongeza maji vikombe 2 koroga na funikia kwa dakika 10-15 au
mpaka ziive. Punguza moto.
• Koroga mayai kwenye maji mpaka iwe kama maziwa, ongeza
kwenye mboga na koroga polepole usiponde ngogwe wala bamia
kwa dakika 5.
• Onya chumvi, pakua za moto kama kitoweo.
Angalia kilichomkuta huyu dada mwenye zarau, mwanae alikufa kwa zarau zake
Dada mmoja akiwa ofisini alipigiwa simu kuwa mwanae amepata ajali wakati anatoka shule, alikuwa ameumia sana. Kwa harakaharaka yule dada aliwasha gari na kuanza safari kuelekea hospitali ili kumuona mwanae.
Akiwa njiani katika mistari ya Zebra huku akiwa na mawazo alitaka kumgonga Kaka mmoja ambaye alikuwa akivuka barabara kwa kukimbia. Katika kumkwepa gari iligonga ukingo wa barabara na kukwaruizika kidogo.
Kwa hasira yule dada alishuka na kuanza kumtukana yule kijana kuwa kamsababishia ajali na kumchelewesha. Alimtukana sana, hali iliyowafanya watu kujaa. Watu walipofika walianza kuuliza nini ndipo yule dada kwa uoga alidanganya kuwa yule kaka alitaka kumuibia.
Watu walianza kumpiga Kaka wa watu kama mwizi, kuona vile yule dada aliingia kwenye gari na kuelekea hospitalini kumuona mwanae. Huku nyuma Polisi walikuja na kumuokoa yule kijana lakini akiwa ameumizwa sana.
Alifika hospitalini na kumkuta binti yake akiwa katika hali mbaya, alikuwa akitakiwa kufanyiwa upasuaji wa haraka ili kuokoa maisha yake, manesi walishamuandaa mtoto na alikuwa akisubiriwa Daktari ambaye alipigiwa simu na alikuwa njiani.
Wakati wakimsubiri Daktari, Nesi alikuja na kuwamabia kuwa, wampeleke hospitali nyingine kwani Daktari waliyekuwa wakimsubiri asingeweza kumfanyia upasuaji mtoto wao kwani alikuwa amepigwa na wananchi wakati akija hospitalini wakimuita mwizi.
Dada na mumewe walichanganyikiwa, mtoto kutokana na hali yake mbaya alichukuliwa harakaharaka na gari la wagonjwa ili kuhamishwiwa hospitalini nyingine. Wakati wanatoka kuelekea kwenye gari kulikuwa na gari ya Polisi inaingia.
Kijana mmoja akiwa hoi alishushwa, yule Dada alimtambua ni yule kijana ambaye alimuitia mwizi kule barabarani. Kwa hasira yule Dada allimuambia Mume wake.
“Huyu Kaka namfahamu ni kibaka tu alitaka kuniibia, ndiyo amenichelewesha kufika huku hospitalini!”
Nesi ambaye alikuwa akimsaidia kumpandisha mtoto katika gari la wagonjwa alimkatisha na kusema.
“Hapana Dada huyu kaka si kibaka, ni Daktari ambaye alipaswa kumfanyia upasuaji mwanao. Amepigwa wakati akikimbia kuja hospitalini, mimi ndiyo nimempigia simu kuja…”
Dada wawatu nguvu zilimuishia ilibidi anyamaze, walifika hospitali nyingine, mtoto alikuwa katika hali mbaya. Aliandaliwa na kuingizwa katika chumba cha upasuaji lakini kabla hajafanyiwa chochote yule mtoto alifariki.
Baada ya uchunguzi ilionekana damu ilishaingia kwenye ubongo. Wangeweza kuokoa maisha yake kama angefanyiwa upasuaji katika hospitali ya mwanzo, kule kusafirishwa tena na kurushwa rushwa barabarani kulisababisha damu kuendelea kuvuja kwa kasi ndani.
Yule dada alizimia baada ya kupata habari zile, maneno yake yalisababisha kuondoa maisha ya mwanae.
FUNZO
Usimdharau mtu kutokana na hali yake kwani hujui ni kitu gani anaweza kukusaidia.
Jinsi ya kupika Mkate
Mahitaji
Unga wa ngano ( self risen flour) kikombe 1 na 1/2
Hamira (yeast) 1 kijiko cha chai
Sukari (sugar) 1 kijiko cha chakula
Chumvi (salt) 1/2 kijiko cha chai
Siagi iliyoyeyushwa (melted butter) 1 kijiko cha chakula
Maji ya uvuguvugu ( warm water) kiasi
Matayarisho
Changanya vitu vyote katika bakuli kubwa kisha aanza kukanda mpaka upate donge laini.Baada ya hapo liweke hilo donge kwenye bakuli la plastic na weke katika sehemu yenye joto ili unga uumuke. Hakikisha unga unaumuka zaidi (yani unaji double size) unaweza kuchukua kama saa 1 na nusu hivi. Baada ya hapo ukande tena na uache uumuke tena kwa mara ya pili, Ukisha umuka pakaza butter katika baking tin (chombo cha kuokea) na upakaze mkate butter kwa juu,kisha uoke katika oven kwa muda wa dakika 30 (katika moto wa 200C) (hakikisha juu na chini unakuwa wa brown Na hapo mkate wako utakuwa tayari
Faida 25 za kutembea kwa Miguu
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili mfumo wa maisha ya watu pamoja na kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanatumia vyombo mbalimbali vya usafiri kwenda karibu kila eneo.
Kwa hakika kutembea kwa miguu kuna manufaa mengi sana kwa ajili ya afya ya mwili, uchumi na maisha yako ya kijamii.
Ikiwa unapenda kuwa bora na mwenye tija zaidi katika nyanja zote, basi fahamu faida za kutembea kwa miguu.
- Hukabili maradhi ya moyo kwa kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu.
- Huimarisha mifupa.
- Huondoa au kupunguza hatari ya kupata kiharusi.
- Husaidia kupunguza uzito.
- Huzuia saratani ya utumbo mpana.
- Hukuwezesha kupata vitamini D kutoka kwenye jua.
- Hukusaidia kuboresha usawa wa mwili wako (balance).
- Hukabili maradhi ya kisukari. Unapotembea unafanya mazoezi yanayoleta uwiano wa urefu na uzito – BMI; jambo litakalokukinga na aina ya pili ya kisukari (Type 2 Diabets).
- Hukabili shinikizo la damu.
- Huondoa msongo wa mawazo.
- Huongeza utayari.
- Hukufanya ujifunze mambo mbalimbali kwa kuona.
- Hukuokolea gharama za nauli au mafuta.
- Hupunguza lehemu mbaya mwilini (cholesterol)
- Huimarisha misuli.
- Husaidia mmeng’enyo wa chakula kwenda vizuri.
- Huwezesha kinga mwili kujiimarisha na kujijenga (kutokana na sababu kuwa kutembea ni aina ya zoezi).
- Huboresha uwezo wa kumbukumbu.
- Hukujengea mahusiano ya kijamii. Unapotembea utakutana na watu mbalimbali.
- Huzuia kuzeeka. Utafiti uliofanyika ulibaini kuwa watu wanaotembea umbali mrefu huishi zaidi.
- Hukuweka katika hali nzuri (mood).
- Hukusaidia kulala vizuri. Kumbuka mazoezi ni chanzo cha usingizi mzuri.
- Huboresha afya ya uzazi hasa kwa wanaume. Kutembea kama zoezi ni njia ya kuwapa wanaume nguvu katika afya ya uzazi.
- Huzuia kuharibika kwa mimba. Mazoezi ni muhimu sana kwa mama mjamzito kwa ajili ya afya yake na mtoto; hivyo zoezi rahisi na jepesi kwake ni kutembea.
- Huboresha mwonekano wa mwili. Mazoezi ni njia moja wapo ya kuufanya mwili wako uonekane katika umbo zuri. Hivyo kutembea kama aina mojawapo ya zoezi kunaweza kukusaidia sana.
Naamini umeona jinsi ambavyo kutembea kwa miguu kuna manufaa makubwa sana kwenye afya, uchumi na hata mahusiano yako ya kijamii.
Inashauriwa kuhakikisha unatembea kwa miguu angalau dakika 30 kila siku. Kwa njia hii utapata manufaa mengi yaliyotajwa hapo juu.
Usiruhusu tabia hii itawale akili yako
Tabia ya kijidharau na kujiona hufai ama huwezi kufanya lolote ukafanikiwa maishani, hakuna mwanadamu aliyeumbwa ili ashindwe,, sote tu washindi zaidi, tunatofautiana njia za kufikia huo ushindi.
Rafiki yawezekana umeshajidharau… na kujitamkia maneno kadha wa kadha ambayo kimsingi yamekukatisha tamaa kabisa ya kufikia lengo fulani maishani… na ukabaki kushuhudia mafanikio ya wengine kila siku maishani.
Embu ondoa dhana ya kushindwa na kujidharau katika kila hatua upitiayo maishani haijalishi umeshindwa mara ngapi, jifunze kuwa na moyo mgumu na wa subila kwa kila hatua upitiayo maishani,, haijalishi upo katika hali gani? Maishani.
Kama ni maskini sana, usijidharau na umaskini wako ukaona wewe ni wa hali hiyo hiyo maisha yako yote,, no.. hapana, haukuumbwa ili uje kuwa maskini. Ila ni juhudi zako mwenyewe ndizo zitakazokutoa katika umaskini ulionao, haijalishi wewe una ulemavu wa aina yeyote ukajidharau na kujiona huwezi fanya lolote mbele ya jamii likakubalika.
Rafiki kuna walemavu kama wewe, wamejitambua na wameamua… hakika wamefikia mafanikio makubwa maishani. Ondoa dharau katika nafsi yako amini unaweza. Kuna walioshindwa kama wewe wakadharauliwa na kutemewa mpaka mate… ila walitambua kusudi la maisha yao na leo hii wamefikia mafanikio makubwa sana maishani, kwa nini?? Wewe ukate tamaa na kujidharau katika hali uliyopo ukajiona hauna maana? Hakika unaweza ukiamua,
PROSTATE GLAND (TEZI DUME) TATIZO SUGU KWA WANAUME
-Hii ni tezi ya wanaume yenye sifa zifuatazo.
~Ina umbo km yai(oval shape)
~Ina ukubwa wenye vipimo hivi, upana 4cm na unene 3cm ingawaje hivi vipimo vinatofautiana kwa kila mwanaume.
~Tezi hii ipo inazunguka shingo ya kibofu cha mkojo na kuzunguka mrija unaopeleka mkojo nje(urethra)
~Tezi hii hua yenye ukubwa wa kawaida lakini huongezeka ukubwa kadri ya umri.
~Tezi hii hutengeneza majimaji yenye rutuba ya mbegu za kiume(shahawa)
SEHEMU KUU ZA TEZI YA KIUME
1.PERIPHERAL ZONE(SEHEMU YA NJE)
~Hii ni sehemu ya nje ya tezi ambayo madakari wengi hutumia hii tezi kubaina kama kuna tatizo kwenye tezi kwani ni virahisi kiugusa km daktari akiingiza ikiingiza index fingure(kidole cha kusontea) kwenye njia ya haja kubwa. Kukua kwa sehemu hii hakuwezi kuathiri utokaji wa mkojo.
2. TRANSITIONAL ZONE(SEHEMU YA KATI)
~ Hii ni sehemu ya tezi ambayo ikikua yani ikiongezeka ukubwa tunasema KUVIMBA KWA TEZI TUME kitalamu BENIGN PROSTATIC HYPERPLASIA (BPH) kuna uwezekano mkubwa wa tezi dume iliyovimba kuzuia njia ya mkojo kupita. Kwani ndio sehemu ya tezi iliyo karibu kabisa na njia ya mkojo. Mara nyingi hii sehemu ikikua ndio inayo sababisha matatizo ya kukojoa(obstructive symptoms). Tezi hii pia daktari anaweza kuibaini kwa kutumia kidole kipomo hiki huitwa DIGITAL RECTAL EXAMINATION(DRE)
hii ni kwa sababu ikikua inasukuma ile sehemu ya pembezoni yani peripheral zone kuelekea njia ya haja kubwa. Hivyo dakatri anaweza kubaini km tezi imekua au laa.
3. CENTRAL ZONE(SEHEMU YA KATI)
~Hii sehemu iko mbele ya transitional zone hivyo uvimbe katika sehemu hii ni vigumu kubaini kipitia kipimo hiki cha haraka cha kutumia kidole hivyo tunatumia vipomo vya picha kinaitwa CYTOSCOPY. Hiki ni kipimo cha picha kinacho angalia kipofu cha mkojo na njia ya mkojo na kutoa majibu katika mfumo ya picha au video.
KUKUA KWA TEZI YA KIUME
~Kukua kwa tezi ya kiume kitalamu tunaita BENIGN PROSTATIC HYPERPLASIA (BPH). Hili tatizo mara nyingi huanza baada ya miaka 40 hivi na dalili huja kujionesha uzeeni. Hivyo tezi inaweza ikawa kubwa sana lakini haina dalili hii ni kutokana na sehemu gani ya tezi iliyovimba au kuongezeka. Tezi inapoonesha dalili jua tatizo hilo ni sugu na liko ktk hali mbaya.
DALILI ZA KUVIMBA KWA TEZI
1. Kukojoa mara kwa mara
2. Kubakiza mkojo kwenye kibofu
3. Kukujoa sana usiku
4. Maumivu wakati wa kukojoa
5.Kupungukiwa nguvu za kiume
6. UTI ya mara kwa mara
7. Mawe kwenye kibofu kutokana na mrundikano wa mkojo.
8. Figo kujaa maji. Hii sababu mkojo huo unarudi nyuma kuelekea figo(hydronephrosis)
9. Kupoteza fahamu(uremia)
HIZI DALILI NIMEZITAJA KULINGANA NA TATIZO LINAVYOKUWA SUGU KWA MGONJWA HIVYO UGONJWA HUU NI HATARI USIPO WAHI.
JINSI YA KUBAINI KUVIMBA KWA TEZI
~Kumbuka BPH sio kansa ni uvimbe tu wa kawaida wa tezi lkn kumbuka tezi hii inaweza kuvimba pia kutokana na kansa ya tezi dume (prostate cancer)
1. Uchunguzi wa kawaida kwa kutumia kidole kupitia njia ya haja kubwa kuangalia kama tezi ina tatizo. Kipimo hiki huitwa DIGITAL RECTAL EXAMINATION. Baada ya kipimo hicho daktari huandika alicho kigusa kama ni ugonjwa au iko kawaida.
2. Hiki ni kipimo cha kupiga picha kibofu cha mkojo kinaitwa CYTOSCOPE. Kumbuka kipimo hiki una ingiziwa waya flani wenye tochi mbele kwenye njia ya mkojo huku huo waya umeunga nishwa kwenye screen. Hivyo chochote huo waya utakacho murika kitaonekana kwenye screen. Ubaya wa hiki kipimo ni kwamba kinaweza kuumiza kuta za njia ya mkojo na baada ya wiki km mbili njia inaweza kuziba mbili jeraha linapo pona. Ila ni kipimo kizuri sana.
3. Kipimo kingine kinaitwa RECTAL UTRASOUND hiki ni kipimo cha kupiga picha kupitia njia ya haja kubwa (rectal) na kutoa picha kwenye jarida gumu kumsaidia daktari kusoma.
4. Kipimo cha kutofautisha kati ya uvimbe wa kawaida(BPH) na kansa ya kipofu(PROSTATE CANCER) Kipimo hiki kinaitwa PROSTATIC SPECIFIC ANTIGEN. Hii ni protein inatolea kwa wingi endapo kuna kansa ya tezi dume. Hivyo damu ya mgonjwa itachukuliwa na kupekwa maabala kuchunguza km ni nyingi kupita kiasi kwenye damu. Kama hii protein ipo kawaida basi uvimbe huo sio kansa ni BPH. Lakini km kiwango ni kingi uvimbe huo ni KANSA. Hivyo uchunguzi zaidi unahitajika kama kuchukua sample ya kinyama kutoka katika tezi na kupeleka maabala.
MATIBABU YA KUKUA KWA TEZI DUME
1. Tezi dume kama haina dalili zozote mara nyingi waga haishighulikiwi sana hospitali lakini dawa za kupunguza kasi anaweza pewa mgonjwa. Lakink ni mara chache.
2. Kama tezi imesha anza kuleta dalili kama usumbufu wakati wa kukojoa siku hizi kuna operation ya bila kukata inaitwa TRANSURETHRAL RECTIONING OF PROSTATE AU CHANNEL TURP.
Hii operation inafanywa kama akiwa anafanya kipimo cha CYSTOSCOPE. Lakini hapa anaweka wire mbele kiko chamviringo kinapitishwa njia ya mkojo kina enda kukata kinyama kinachoziba i mean tezi iliyovimba. Hapa inazibua njia ya mkojo ili mtu akojoe. Ukifanyiwa operation hii vizuri tezi hujirudia baada ya miaka kama 3-5 tangu siku ya operation.
MADHARA YA TIBA HII
1. Kukosa uwezo wa kufikia kishindo yani hutoi shahawa(RETROGRADE EJACULATION) wazee wengi hulalamika sana baada ya hii operation hivyo ushauri nasaha lazima utolewe ili mgonjwa ajue nini madhara yake kabla ya operation.
2. Kuziba kwa njia ya mkojo kutoka na kuumia kwa njia hizo wakati wa kitendo hicho. Panapokua panapona hilo kovu linaziba njia ya mkojo.
3. Operation kubwa ya kuondoa tezi hio hufanyika kwa kufungua kibofu cha mkojo na kutoa hio tezi. Madhara ni mengi sana kuhusu hii bora ile no mbili.
Kama unahisi unatatizo ili nione mapema kabla mambo aya jakuwa makubwa zaidi
Recent Comments