Ninapoingia kanisani nachovya maji ya baraka na kusema;
“Unitakase Ee Bwana mimi na uovu wangu wote, ili nipate kustahili kushiriki ibada takatifu’ Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu” Amina!
“Unitakase Ee Bwana mimi na uovu wangu wote, ili nipate kustahili kushiriki ibada takatifu’ Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu” Amina!
Ninapiga goti huku nikisema
“Mungu wangu na Bwana wangu”
“Mungu wangu na Bwana wangu”
🙋🏽Nikiinuka nasema
“Nitakusifu na kukuabudu katika Ekaristi takatifu”
🙋🏽Naenda mpaka kwenye bench, napiga magoti au nakaa nikiwa mimeinamisha kichwa (kama mabenchi yameisha nabaki nimejisimamia) huku nikitoa nia yangu ya kusali misa siku hiyo, mfano
“Ee Mungu, ninaungana nawe na jeshi lote la mbinguni, pamoja na Mama Bikira Maria, nikiwa na nia ya kumwombea mama yangu ambaye ni mgonjwa, jirani yangu ambaye mpaka sasa hatuelewani na pia familia yetu ambayo haina amani, Mungu kupitia misa hii rejesha hali ya mama yangu, rejesha uelewano na jirani yangu, na pia rejesha amani ya familia yetu pamoja na familia zote ambazo hazina amani”
🙋🏽Ninaendelea na misa na Kushiriki litrujia kikamilifu
🙋🏽Wakati wa komunyo nikikumbuka kuwa nina dhambi kubwa huwa nakominika kwa sala ya tamaa wala siendi mbele, huwa najikalia tu kwenye bench naangalia wenye moyo safi wanaenda mbele kumpokea Yesu (Kweli huwa najisikia wivu sana, itanibidi katikati ya wiki nifanye kitubio ili nisikae tena)”
🙋🏽Mwisho wakati wa kuondoka nachovya maji ya baraka nikisema
“Unilinde Ee Mwenyezi Mungu, nikapate kuwa mfano katika jamii yangu, na nikushuhudie katika matendo yangu”
(Hapo nachovya maji ya baraka na kufanya ishara ya msalaba) “Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, amina”
(Hapo nachovya maji ya baraka na kufanya ishara ya msalaba) “Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, amina”
Usiku mwema wapendwa. Malaika awalinde
Mwamini Bwana; anajua njia
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Imani inaweza kusogeza milima
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Sifa kwa Bwana!
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Nakuombea 🙏
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu akubariki!
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Rehema zake hudumu milele
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Dumu katika Bwana.
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Baraka kwako na familia yako.
Neema na amani iwe nawe.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Rehema hushinda hukumu
Endelea kuwa na imani!
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Katika imani, yote yanawezekana
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mungu ni mwema, wakati wote!
Tumaini ni nanga ya roho