Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Mungu ni Mwenye Haki, Mpenda Haki, na Mtenda Haki

Mungu ni mwenye haki, mpenda haki na mtenda haki. Unapoenenda kwa haki na yeye ataipigania haki yako.

Melkisedeck Leon Shine

Mungu ni Mwenye Haki, Mpenda Haki, na Mtenda Haki

Mungu ni mwenye haki, mpenda haki na mtenda haki. Unapoenenda kwa haki, na yeye ataipigania haki yako. Mungu ameweka kanuni na sheria za kiroho ambazo zinaongoza maisha yetu, na ni kupitia haki zake tunaweza kupata baraka na neema zake. Mungu anatuita kuenenda kwa haki, kuwa waaminifu, na kutenda mema katika maisha yetu ya kila siku. Tunapofuata njia zake, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu yupo pamoja nasi na anatupigania.

“Kwa maana Bwana hupenda haki, wala hawaachi watauwa wake; wao watalindwa milele; bali uzao wa wasio haki utakatiliwa mbali.” (Zaburi 37:28)
“Maana mimi, Bwana, ni mpenda haki, nauchukia wizi kwa dhuluma; nami nitawapa thawabu yao kwa kweli, na kufanya agano la milele nao.” (Isaya 61:8)
“Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye fadhili katika kazi zake zote.” (Zaburi 145:17)

Mungu ni Mwenye Haki

Mungu ni mwenye haki. Haki yake inaonekana katika kila kitu anachokifanya na katika jinsi anavyotenda na wanadamu. Mungu anaweka viwango vya haki ambavyo ni kamilifu na bila upendeleo. Kwa haki yake, Mungu anatufundisha njia ya kutenda mema na kuepuka maovu. Haki ya Mungu inatuhakikishia kwamba kila mmoja wetu atapata haki yake katika wakati wake sahihi, na hakuna uovu utakaoponyoka mbele yake.

“Bwana ni mwenye haki; hupenda matendo ya haki; watu wanyoofu watauona uso wake.” (Zaburi 11:7)
“Ee Mungu, njoo uniokoe, Ee Bwana, fanya upesi kunisaidia. Na waaibishwe, wakate tamaa, watafutao roho yangu; warudishe nyuma na kufadhaike, wapendao kunitenda mabaya.” (Zaburi 70:1-2)
“Mimi ni Bwana, ninenaye haki, mwenye kutoa habari za mema.” (Isaya 45:19)

Mungu Mpenda Haki

Mungu anapenda haki. Upendo wake kwa haki una maana kwamba anataka kila mmoja wetu awe mpenda haki pia. Anatuita tuishi maisha yanayolingana na haki zake, tukijiepusha na njia za uovu na dhuluma. Mungu anatamani kuona haki ikitendeka katika kila nyanja ya maisha yetu, kuanzia mahusiano yetu binafsi hadi jinsi tunavyotenda katika jamii. Tunapojitahidi kuwa wanyenyekevu na kutenda haki, tunaonyesha upendo wetu kwa Mungu na kwa jirani zetu.

“Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watashibishwa.” (Mathayo 5:6)
“Enendeni kwa Bwana Mungu wenu, mkaishike njia zake, na kuyashika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, kama ilivyoandikwa katika torati ya Musa, mpate kufanikiwa katika kila jambo mfanyalo, na kila mtazamapo.” (1 Wafalme 2:3)
“Yeye anapenda haki na hukumu; dunia imejaa fadhili za Bwana.” (Zaburi 33:5)

Mungu Mtenda Haki

Mungu ni mtenda haki. Haki yake inadhihirishwa kwa njia ya matendo yake. Tunapomtegemea Mungu na kuenenda kwa haki, tunakuwa chini ya ulinzi wake na upendo wake. Mungu anatenda haki kwa wale wanaomfuata kwa uaminifu, na anahakikisha kwamba haki yao inalindwa. Katika kila hali, Mungu anatafuta kutenda haki, na kupitia nguvu zake, tunaweza kushinda changamoto na dhuluma za maisha.

“Heri wote wamwaminio yeye. Bwana hufanya haki, na hukumu kwa wote wanaoonewa.” (Zaburi 103:6)
“Siku moja hataonewa tena kamwe; maana ni Bwana wa majeshi asemaye, Nitamkomboa na kuwapa watu wasio na lawama amani; nami nitawafanyia haki watu wote wamtumainio jina langu.” (Yeremia 23:5-6)
“Ee Bwana, ujue uovu wao wote na dhambi yao; usiisamehe hatia yao, wala usiifute dhambi yao machoni pako; bali waangamie mbele zako, uwaache chini ya ghadhabu yako.” (Yeremia 18:23)

Hitimisho

Mungu ni mwenye haki, mpenda haki, na mtenda haki. Unapoenenda kwa haki, na yeye ataipigania haki yako. Tunapofuata haki za Mungu, tunakuwa na uhakika wa baraka zake na ulinzi wake. Ni jukumu letu kama Wakristo kuishi kwa haki, kuwa wema na waaminifu, na kutenda mema katika kila jambo tunalofanya. Mungu, katika upendo wake wa haki, atatuonyesha njia ya kutenda haki na kutulinda tunapoishi kulingana na mapenzi yake. Tuishi kwa haki, tukijua kwamba Mungu yupo nasi, akitupigania na kutubariki katika safari yetu ya kiroho.

Mapishi ya tambi za mayai

Tambi za mayai ni moja kati ya vyakula ambavyo napenda kuandaa pale ninapokua ninaharaka au sina muda mrefu wakukaa jikoni.pishi hili huchukuca muda mfupi sana na nimlo uliokamilika.

Mahitaji

  1. Tambi ½ paketi
  2. Vitunguu maji 2 vikubwa
  3. Karoti 1
  4. Hoho 1
  5. Vitunguu swaumu(kata vipande vidogo) kijiko 1 cha chakula
  6. Carry powder kijiko 1 cha chai
  7. Njegere zilizochemshwa ½ kikombe
  8. Mafuta kwa kiasi upendacho
  9. Mayai 2
  10. Chumvi kwa ladha upendayo

Njia

1.Chemsha maji yamoto yanayotokota,ongeza chumvi na mafuta kidogo,weka tambi kwenye maji hayo chemsha adi ziive.Chuja maji yote ili kupata tambi kavu
2.Katika bakuli piga mayai kisha weka pembeni
3.Katika kikaango,weka mafuta,vitunguu maji ,vitunguu swaumu,hoho, karoti na carry powder,kaanga kwa pamoja katika moto mdogo kwa muda mfupi kwani mboga hazitakiwi kuiva.
4.Ongeza tambi na njegere katika kikaango,geuza kila mara ili kuchanganya .
5.Ongeza mayai kwenye tambi kisha geuza kwa haraka bila kupumzika adi mayai yaive na tambi ziwe kavu.Tayari kwa kula

Katika hatua hii ongeza moto uwe wa wastani,moto ukiwa mdogo mayai yatafanya tambi zishikane na kufanya mabonge.

Cheki hawa wachungaji

CHEKA KIDOGO

Wachungaji watatu walikutana kwa siri na kuelezana matatizo yao ili waweze kuombeana.

MCHUNGAJI WA KWANZA: mimi tatizo langu ni wizi, kila nikimaliza ibada lazima niibe pesa za sadaka.

WA PILI: Mimi tatizo langu ni wanawake yani nimeshalala na wana kwaya wote pamoja na mke wa ASKOF.

WA TATU akaanza kulia badala ya kuongea.WENZAKE:

We vp unatatizo gani mbona unalia???

AKAJIBU: jamani mimi tatizo langu ni “umbea” haya yote tuliyoongea lazima nikaseme!

😂😂😂😂😂👆🏻😂😂

Namna ya kutibu chunusi kwa kutumia Binzari, maziwa na asali

Unahitaji vitu vifuatavyo:

a)Binzari ya unga
b)Maziwa fresh
c)Asali
d)Bakuli
e)Kijiko cha chai

Hatua kwa hatua namna ya kutumia:

a)Weka kijiko kidogo kimoja cha binzari ya unga ndani ya bakuli
b)Ongeza kijiko kidogo kimoja cha asali ndani yake
c)Ongeza tena kijiko kidogo kimoja au viwili vya maziwa fresh
d)Changanya vizuri mchanganyiko huu upate uji mzito
e)Pakaa pole pole sehemu yenye chunusi mchanganyiko huu
f)Baada ya dakika 5 au 7 hivi jisafishe uso wako
g)Fanya zoezi hili mara 2 au 3 tu kwa wiki

Status za Whatsapp za Wazungu na Wabongo

STATUS ZA WAZUNGU kwenye Whatsapp vere vere kliaaa…
👉sick
👉at movie
 👉 in a meeting2
👉 kind of happy,, 👉busy,,
👉available
👉Driving
👉sleeping

STATUS ZA WABONGO SASA MBUTA NANGA MBONGO NGAFU

“Akutake nani una shepu la Kitorondo utaishia kumegwa na kuachwa

“Watu tuna nyota za Chips Mayai sio wewe mwenye Nyota ya Punda,halulaaa”

👌Kantangazeee ndo Kwanza naanza na ntakukomesha Mwanaharamu we!

😍 I love yu so much ur my only one,No one lyk yu and I mean it 🎶 Yu ma numba1 ma sweet sweet namba1 roho yangu mama,,

👍 Asante 😍 vimenitoshaaa tena kama ulijua 😘😘😘😘😘,

💪 unajifanya simba kumbe nyau mimi ndo maji kama hujanioga utaninywaa,

🙈 nauza Ubuyu kwa bei nafuuu kama unataka inbox me plz

😔 poleee jaman utapona wangu,,,

💪 utalijua jiji na chuki zako walingia na tako wakati hadi nyani analo kitu sura dada…

😡 usinisemeshe usiniongeleshe tena utaniambia vizur ulikuwa wapi..

😷 mdomo kaumbiwa mwanadamu ongeeni nyie me sijali ya wanafiki nafanya yangu huna hadhi ya kujibiwa na mimi
pamoja na ya kwako uloweka🙈😆😆😆

Jinsi ya kupika mboga ya majani ya mashona nguo

Viamba upishi

Mashonanguo mkono 1
Tui la nazi kikombe 1
Karanga zilizosagwa kikombe ½
Mafuta vijiko vikubwa 4
Kitunguu 1
Nyanya ndogo 2
Chumvi kiasi

Hatua

• Chambua mashona nguo mateke, osha na katakata.
• Menya osha na katakata kitunguu.
• Osha, menya na katakata nyanya.
• Kaanga karanga, ondoa maganda na saga zilainike.
• Kuna nazi na chuja tui.
• Kanga kitunguu, weka nyanya na koroga mpaka zilainike.
• Weka mashona nguo na chumvi kisha koroga sawa sawa,
funikiakwa dakika 5 -10.
• Changanya tui la nazi na karanga, ongeza kwenye hizo mboga
ukikoroga kwa dakika 5, punguza moto ili ziive taratibu.
• Onja chumvi na pakua kama kitoweo.
Uwezekano
Changanya mnavu, mgagani, mashonanguo kidogo ki¬dogo au
mboga nyingme.
Tumia maziwa au krimu badala ya tui la nazi.
Weka nyama au dagaa au samaki au mayai badala ya – karanga.

Tiba mbadala ya chunusi na vipele usoni

Kuna idadi kubwa ya watu wanao kabiliwa na tatizo la vipele vya usoni ( Chunusi ). Kuwa na chunusi ni jambo lenye karaha sana, kwani linakufanya upoteze mvuto wako wa asili na hivyo kukukosesha raha.

Zipo njia mbalimbali za asili zinazo weza kutumika kutibu tatizo la chunusi na vipele vya usoni.

Ifuatayo ni miongoni mwa njia bora kabisa na ya uhakika itakayo kusaidia kuondokana na tatizo la Chunusi au vipele kwenye uso.

Komamanga: Maganda Ya Mkomamanga yaliyosagwa, yakichanganywa na habbat sodah ya unga, hutengeneza dawa nzuri ya asili ya kuondoa tatizo la vipele vya usoni ( chunusi )

Habbat Soda: Hii ni Habbat Sodah Ya Mbegumbegu. Habbat Sodah iliyosagwa ndio inayo hitajika katika kutengeneza dawa ya asili ya kuondoa tatizo la vipele vya usoni ama chunusi.

MAHITAJI:

Habbat Sawdah ya Unga iliyo sagwa.
Nusu kikombe ya maganda ya komamanga yaliyo sagwa.
Nusu kikombe ya siki ya tofaha(apple )

MATAYARISHO NA MATUMIZI

Changanya na pasha moto kwa dakika mbili kikombe kimoja cha Habbat-Sawdaa iliyosagwa, ½ (nusu)
kikombe cha maganda ya komamanga yaliyosagwa, na ½ (nusu) kikombe cha siki ambayo inatokana na juisi ya tofaha (apple).

Paka katika sehemu inayotakiwa kabla ya kwenda kulala kila siku usiku mpaka vipele (chunusi) vitakapoondoka. Mchanganyiko unaweza kukaa mpaka wiki tatu na ni lazima uwekwe katika hali ya ubarid.

Aina ya mazoezi na umuhimu wa mazoezi kwa wamama wajawazito

Leo tutaongelea mazoezi gani ya kawaida ambayo mama mjamzito anaweza kuendelea kuyafanya kila siku ya ujauzito wake na umuhimu wake.

Mazoezi wakati wa ujauzito yanasaidia:

1. Kupata usingizi mzuri usiku.

2. Kuondoa stress.

3. Kulegeza na kunyoosha misuli ya uzazi na kuitayarisha kwa kazi ya kujifungua.

4. Kupunguza kichefu chefu(morning sickness) na kiungulia(heartburn)

KUMBUKA:

Wakati unafanya mazoezi hakikisha kuwa husikii maumivi yoyote na ukipatwa na maumivu hakikisha unaonana na daktari haraka iwezekanavyo. Kumbuka usilalie mgongo wakati wa kufanya mazoezi au usifanye mazoezi aina ya jogging (kukimbia) au kuruka ruka (bouncing) na hakikisha mdundo wa moyo (pulse) na temperature yako ya mwili ziko sawa. Kunwya maji mengi kuzuia dehydration na angalia balance yako iko sawa ili kuzuia kuanguka.

Kama ulikuwa unafanya mazoezi kabla ya ujauzito unaweza kuendelea na mazoezi yafuatayo:

Kuogelea

Uzuri wa zoezi hili ni kwamba halihitaji nguvu nyingi linasaidia kurelax na misuli yote ya mwili inafanya kazi. Unaweza kuogelea kwa dakika 20 hadi 35 lakini uchukue break pale utakapoona umechoka au kuishiwa na nguvu au pumzi. Kuogelea pia kunasaidia kupunguza maumivu yatokanayo na miguu kuvimba.

Kutembea

Ni zoezi zuri sana kwa mwanamke mjamzito. Zoezi hili linaweza kufanywa dakika 20 had 35 kwa siku. Zoezi hili linapunguza stress, linasaidia chakula kushuka vizuri na digestion. Pia linasaidia katika kuweka sawa uti wa mgongo. Tatizo la uti wa mgongo kutokunyooka linasababishwa na tumbo kuongezeka na kukosekana kwa balance kwenye mwili. Hiki ni chanzo cha maumivu ya mgongo. Kumbuka kuchuka break na kupumzika pale utakaposikia uchovu.

Kucheza Muziki

Mama mjamzito anaweza kucheza mziki kama zoezi hasa hasa mziki wa belly dancing wa kunyonga kiuno na miziki aina ya salsa. Hii inasaidia katika kulainisha misuli ya uzazi tayari kwa kujifungua, kusaidia kujifungua kwa urahisi na kupona kwa haraka zaidi baada ya kujifungua, kupunguza michirizi ya tumbo(stretch marks) inayojitokeza kwa ajili ya ngozi ya tumbo kuvutwa, pia inasaidia confidence ya mwanamke kujiona bado ana mvuto, kuondoa stress, kusaidia na balance, kupunguza maumivu ya mgongo na kusaidia kunyoosha uti wa mgongo.

Kuendesha baiskeli.

Pia unaweza kuendesha baiskeli ila uangalie balance usianguke na usiendeshe sehemu zenye msongamano wa watu au traffic ikiwezekana tumia baiskeli special za mazoezi ndani ya gym(stationary bikes).

Cheki tabia za kuandika vimaneno vya ajabuajabu kwenye pikipiki na bodaboda ilivyomponza huyu

Jamaa mmoja dereva wa bajaji alianguka, sasa bajaji ikawa imem’bana akawa anafurukuta bila mafanikio Cha ajabu watu wakawa wanampita bila kumsaidia, Kumbe Nyuma ya Bajaji yake alikua Kaandika “NIACHENI KAMA NILIVYO, HII NDIO STYLE YANGU” 😂😂😂 Mpaka sasa nimemwacha bado yuko hapo *Sipendagi Ujinga mimi* 🚶🏽🚶🏽🚶🏽🚶🏽🚶🏽

JE IMANI AU MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI YANAPATIKANA KATIKA BIBLIA?

Wakatoliki wengi huyumbishwa kwa kuambiwa huamini mambo ambayo hayako au ni kinyume na Biblia. Aya zifuatazo zitakusaidia wewe mkatoliki kuelewa au kujua mistari ya Biblia inayofafanua imani katoliki.
1) KUOMBEA MAREHEMU:
2 Mak. 12:38-46
Hek. 3:1
Tob 4:17
2) MATUMIZI YA SANAMU NA VISAKRAMENTI
2Fal 3:20-21
Hes. 21:8-9
Kut. 25:17-22
Kol. 1:20, 2:14
Yn. 12:32
Mt. 19:11-12
3) USAHIHI WA MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI KAMA CHANZO CHA IMANI
2 The 2:15
2 Kor. 10:10-11
Yn 21-25
2 Yoh. 1:12
3 Yoh. 1:13
4) KUABUDU JUMAPILI BADALA YA JUMAMOSI(SABATO)…. Hasa ni kwa sababu Yesu aliitukuza siku ya kwanza ya juma kwa ufufuko wake na kwa kuwatokea wanafunzi wake siku hiyo.
Ufu 1:10
Mdo 20:7
Mt 28:1-8
Lk. 24:1-7
Lk. 24:13ff
1 Kor. 16:1-2
Yn. 20:1-22
5) MAMLAKA YA PAPA KAMA MFUASI AU MRITHI WA MT. PETRO
Yn. 21:15-17
Mt 16:18-19
W 2:1-14
6) MAPADRI KUITWA BABA WAKATI BABA NI MMOJA ALIYEKO MBINGUNI
Mwa 17:4
Yer. 7:7
Hes. 12:14
Yn. 6:49
Mt 23:30
Lk. 1:73
7) JE BIBLIA INATAMBUA MUUNDO WA UONGOZI WA KANISA?
Efe. 4:11-13
1Tim 5:17-25
1Tim 3:1-7,8-18
8) JE BIBLIA INASEMAJE KUHUSU TOHARANI.
Isa 35:8, 52:1
Zek 13:1-2
1Kor 3:15
Lk 12:47-48, 58-59
Ufu 21:27
Ebr 12:22-23
Ayu 14:13-17
9) KUHUSU MATUMIZI YA UBANI
Kut 30:34-37
Hes 16:6-7
Law 16:12-13
Lk 1:10
Ufu 8:32
10) ROZARI IKO KATIKA BIBLIA?
Lk 1:28
Lk 1:42
11) JE KUTUMIA MAJI YA BARAKA NI MAPENZI YA MUNGU?
2Fal 2:19-22
Yn 5:1-18
Yn 7:37
Hes 19:1-22
12) KWANINI TUNAOMBA WATAKATIFU WATUOMBEE?
Mit 15:8, 15:29
Ayu 42:8
Yak 5:16
Mt 16:19
13)KWANINI TUNATUMIA MEDALI, MISALABA, SCAPURALI NA MIFUPA YA WATAKATIFU?
2Fal 13:20-21
14) KWANINI TUNAUNGAMA DHAMBI ZETU KWA PADRI
Mt 16:19,1-20
Yak 5:15-16
15) UBATIZO WA WATOTO WACHANGA UKO KATIKA BIBLIA
Mdo 16:15-33
Mdo 18:8
Mt 28:19
Mdo 10:47-48
16) KUSIMIKWA KWA UTUME
Kut 28:4-43
17) RANGI ZA KANISA
Kut 27:9-29
18) MATUMIZI YA MISHUMAA
Kut 25:31-40; 27:20-21
Hes 8:1-4
19) MPAKO WA MAFUTA YA KRISMA
Kut 30:22-32
20) MPAKO WA MAFUTA YA WAGONJWA
Yak 5:14-15

Mbinu 9 za kuwavutia na kuwateka wanawake kimapenzi

Kati ya wanawake na wanaume wote wawili wanahitaji kuvutiwa na wenza wao ili wadumu katika mahusiano. Kama mwanaume lazima upate wakati wa kujua unatakiwa kufanya nini kwa ajili ya kulifanya penzi lako lizidi kuchanua.
Hali kadhalika kama bado haupo Kwenye mahusiano kuna mambo ambayo ni ya msingi kufanya au kuwa nayo ili uweze kuwa na mvuto zaidi kwa wanawake.

Yafuatayo ni mambo yakufanya ili kumvutia mwanamke.

1. Kuonyesha kuwa unamjali

Wanawake wanapenda sana wanaume wanaojali wao kama wao, wanaojali kile wanachokifanya na watu wao wa karibu kama ndugu na wazazi. Wanapenda wanaume wanawaona wao ni kila kitu na wanaotoa kipaumbele kwao. Kama huna tabia hiyo, ujue upo katika nafasi kubwa ya kumkwaza mpenzi wako. Mwanamme anatakiwa amjali mpenzi wake kwa kila hali. Kumjulia hali kila wakati na kutaka kujua maendeleo yake, kutakupa nafasi kubwa sana ya kuendelea kudumu katika uhusiano hai. Vile vile kuonyesha kujali mambo yake na watu wake wa karibu kunamvutia mwanamke.

2. Kuonyesha kuwa karibu na kupatikana unapohitajika

Mwanamke huvutiwa sana na mtu ambaye yupo karibu nae na ambaye anapatikana wakati anapohitajika. Kati ya vitu vinavyowapa wapendeza sana wanawake ni pamoja na kusogezwa karibu. Hapa ni kuwa naye katika mambo mengi unayoyafanya kila siku na kushiriki katika mambo yake hata kwa mawazo kama ukishindwa kwa matendo. Ni vizuri kuwa naye au kuwasiliana naye wakati wa kula, ukitaka kujua aina ya chakula alichokula siku hiyo au ikiwezekana mchagulie. Ni mambo madogo sana lakini yanayoongeza nakshi katika mapenzi na ambayo ni muhimu sana kwa wanawake. Yapo mengi sana ambayo kwa kuyafanya utakuwa umemsogeza mpenzi wako karibu yako, mfano kutembea pamoja, kuangalia movie pamoja, nakadhalika. Tumia ubunifu wako ili uweze kuteka hisia za mwenzi wako kisawasawa kwani mwanamke anavutiwa sana na mtu aliye karibu nae.

3. Kumsifia na kumuonyesha kuwa ni bora

Wanawake wanapenda kusifiwa na kuonekana kuwa bora. Mwanamke akisifiwa anahisi kupendwa kupita kiasi. Anajiona kamili, peke yake na mwenye nguvu kwako. Anajiamini na unamfanya azidi kukupenda kwa kuwa anaamini yupo na mwanaume ambaye anajivunia kuwa naye. Vilevile kumsifia mwanamke kwake ni njia ya kuonyesha upendo na Ishara ya kuonyesha kumjali kupita kiasi.

4. Kupewa kipaumbele

Mwanamke anavutiwa zaidi na mtu anayeonyesha kumpa kipaumbele na kupewa nafasi. Kuna wakati wanawake huwa na mambo yao binafsi. Kazini au kifamilia. Inawezekana akatatizika katika eneo fulani ambalo kwa namna moja ama nyingine atahitaji usaidizi wako. Ikitokea mwanamke akawa katika hali hiyo, msikilize.
Mathalani ana tatizo la kifamilia, amekuambia mmoja wa wazazi wake anaumwa, msaidie. Si lazima kifedha, lakini kuonesha kujali kwako tu, kutampa matumani kwamba anaishi na mtu sahihi. Acha kupuuza mambo yake; hata yale madogo, kama ya ‘mtoto wa dada amerudishwa ada shuleni’.
Msikilize, mshauri panapofaa kufanya hivyo na ukiweza msaidie hata kifedha. Katika upande wa pili ni hivyo hivyo. Labda una tatizo binafsi, kazini kwako au kifamilia, mshirikishe.
Unaweza kushangaa jambo ambalo uliamini unaweza kulimaliza peke yako, kwa kumshirikisha likawa jepesi zaidi na mambo yakaendelea vyema. Kipaumbele kwa namna yoyote ile, kunaongeza mapenzi zaidi kwa mwanamke.

5. Usafi binafsi

Wanawake wanapenda mwanamme ambaye ni msafi, hii ni kwa sababu kiasili wamejaliwa kupenda usafi ndio maana ni nadra sana kukutana na mwanamke asiyejipenda. Ndiyo maana wanaitwa mapambo ya nyumba au la nyumba! Ni kwa sababu ya hulka yao ya kupenda sana usafi. Mwanamke anavutiwa sana na mwanaume mtanashati. Usafi wako unamfanya ajiamini kuwa na wewe. Hata nyumbani kwako, lazima uishi katika nyumba safi. Hata anapokuja kukutembelea, anakuta mazingira masafi kuanzia sebuleni hadi chumbani. Anapokukuta katika hali ya usafi, inakuwa rahisi zaidi yeye kuanzia hapo alipokukuta na kuendelea mbele.

6. Anavutiwa na mwanamme anayejiamini

Mwanamke anajisikia salama zaidi akiwa na mwanaume ambaye anajiamini yaani mwenye uwezo wa kutetea hoja zake na kujieleza sawia pale anapotakiwa kufanya hivyo au wakati wowote ule. Siyo anayebabaika na kuyumba yumba. Suala la msimamo binafsi, kwa mwanamke ni kubwa kuliko hata kumnunulia nguo mpya.
Mwanamke anapenda kukuona ukiwa katika hali halisi ya maisha yako, usiyeyumbishwa na mwenye kutoa maamuzi yasiyoyumba.
Wakati mwingine, mwanamke anaweza kukupima hata katika jambo ambalo amekosea yeye, ataangalia unavyotoa maamuzi yako, lakini pia atafuatilia kuona kama utakuwa mwepesi wa kuyabadilisha.
Anataka kuona msimamo wako muda wote. Mwanamke hapendi mtu anayebadilikabadilika Kwenye maamuzi na misimamo yake.

7. Malengo ya maisha

Mwanamke anapenda mwanaume mwenye malengo na anayemshirikisha katika mipango yake. Mwanamke anavutiwa na mwanamke mwenye malengo katika maisha yake. Vilevile anapenda mtu anayemshirikisha katika malengo yake na kumuweka katika mipango yake. Faida ya kumshirikisha katika malengo yako ni pamoja na kunampa nguvu na nafasi ya kujiona mama katika familia yenu. Msaidizi kamili wa nyumba yenu. Mweleze juu ya malengo yako, wakati mwingine anaweza kukusaidia sehemu ambayo hukutarajia.

8. Anayeweza kujitetea

Mwanamke hupenda mwanamme anayeweza kujitetea. Mwanaume aliye ‘fiti’ ni chaguo la wanawake wengi. Si mnyonge. Mpole kupitiliza na aliye tayari kuonewa! Huyu hana nafasi.
Wanawake hawapendi kuwa na wanaume ambao wapo tayari kuonewa. Wanataka wenye uwezo wa kusimama kidete kuona haki zao hazichukuliwi kirahisi. Hili si suala la kutetea tu haki yako pekee kama mwanaume, bali inapobidi kusimamia haki ya mwanamke wako. Nisieleweke vibaya katika hili, lakini mwanaume imara ni yule ambaye ana nguvu – anafanya mazoezi na ambaye yupo tayari kwa lolote! Inapowezekana, uwe na uwezo wa ‘kuzichapa’ ikiwa mtakutana na vibaka au watu wabaya wenye lengo wa kukudhuru/kuwadhuru au kumdhuru mpenzi wako.

9. Anayemtosheleza tendo la ndoa

Mwanamke anavutiwa zaidi na mwanamme anayeweza kumridhisha katika tendo la ndoa. Anataka mwanamme anayeweza kufanya kile anachotaka yeye na kile anachokipenda. Mwanamke hapendi mwanamme anayemkomoa katika tendo la ndoa au anayefanya mambo asiyoyapenda. Mwanamke anataka kuridhishwa na kujaliwa katika tendo la ndoa.

Ili kufahamu mambo Mbalimbali ya muhimu kuhusu wanawake, Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Soma hii Kabla hujafikiria kula nyama ya nguruwe tena

JEE NYAMA YA NGURUWE (KITI MOTO) NI SALAMA KWA BINADAMU???

Hapa huwa kuna mvutano wa kidini sana juu ya nguruwe, Ila Leo napenda kuliweka sawa, kitaalamu kwa mujibu wa MEDICINE (Science)!!

Nguruwe ni mnyama anaeliwa na 38% ya watu wote duniani Na walaji wake ni nchi Magharibi na Kusini mwa Asia, Europe, Sub-Saharan Africa, America ya kaskazini , kusini mwa America, na Oceania.

Nguruwe ni mnyama ambae, Ana umbo la pekee sana, tukiangalia kuhusu madhara yake au faida yake , tunangalia vitu vinavyopatikana ktk mwili wake, tukilinganisha Na Faida.

FAIDA ZA NYAMA YA NGURUWE KITAALAMU

👉🏾Kunapatikna vitamini muhimu ktk mwili Wa binadamu; ambavyo ni B1, B6 and B12
👉🏾Unapata madini ya Chuma, ambayo husaidia kuimarisha mifupa.
👉🏾Nyama ya nguruwe inaimarisha ngozi yako Na kuifanya iwe laini.
👉🏾Nyama ya nguruwe ina magnesium kwa wingi ambayo ina faida ktk mwili Wa binadamu
👉🏾Nyama ya nguruwe ina protein ya kutosha, ambayo husaidia ulinzi wa mwili
👉🏾Nyama ya nguruwe ina mafuta ambayo hutupa nguvu mwilini

HASARA YA NYAMA YA NGURUWE

Licha ya faida tajwa hapo juu, vile vile kuna hasara ya kutumia nyama hii.
👉🏾Nyama ya nguruwe ; ina sumu ya carcinogen ambayo inasababisha kansa; kwa mujibu wa utafiti uliofanyika Na shirika la afya duniani ( WHO), Na The International Agency for Research on Cancer!! Utafiti huo ukaonesha kuwa ukila kila siku 50gms basi uwezekano Wa wewe kupata kansa unaongezeka kwa 18%
👉🏾Anasababisha Swine Flu kwa binadamu; hivi ni virusi vinavyosababisha mafua kwa binaadamu. Kwa mujibu wa utafiti uliofanyika na Centers for Disease Control and Prevention inaonesha influenza virus H1N1 na H3N2 ambaye anatokana Na Nguruwe(kiti moto) imeripotiwa kusababisha maradhi ya mripuko kwa nchi za MAREKANI
👉🏾Nyama ya nguruwe ina minyoo wajulilanao kwa jina la trichinella worm , ambao wadudu hawa ni vigumu sana kuweza kufa kwa joto Hata la 100C , utafiti uliofanyika 1998 Na WHO ukaonesha nyama ya Nguruwe iliopikwa kwa Joto la 104C , Huwa asilimia 52.37% ya trichinella worm wanabaki kuwa hai!! Wadudu hao wakiingia ktk mwili Wa binadamu husababisha ugonjwa ujulikanao kwa jina la trichinosis; ambao huwa Na dalili kama ifuatavyo:
✅Homa kali sana
✅Kichwa kuuma
✅Kukosa nguvu
✅Maumivu ya nyama za mwili
✅Macho kuwa rangi ya pink(conjunctivitis)
✅Kuvimba uso Na kope
✅Kudhuriwa Na mwanga
👉🏾Nyama ya nguruwe ina virus aina ya Hepatitis E virus (HEV); ambaye husababisha homa ya ini aina E
👉🏾Wadudu wengine ni kama;
🥄Nipah virus
🥄Menangle virus
🥄Viruses Ktk kundi Paramyxoviridae
Ambao wote hao; huwa wanaleta madhara kwa mwili Wa binadamu!!
👉🏾Nyama ya nguruwe husababisha Maradhi ambayo Yana resistance(ukinzani) Na ANTIBIOTICS
👉🏾Nyama ya nguruwe ina minyoo aina ya Taenia solium. Kwa mujibu ya shirika la Afya duniani(WHO) – Reference….open_http://www.who.int/news-room/fact-sheets/detail/taeniasis-cysticercosis
Wanasema; minyoo hii huwa;
👉Unaweza kuipata ikiwa hautapika nyama vizuri au Ukila nyama ya kuruwe ilioathirika(infected): Kwa hyo sio kila nyama ya Nguruwe iliopikwa vizuri, huwezi kupata minyoo hii.
👉Minyoo hii ikiingia ktk mwili Wa binadamu husababisha matatizo ya mfumo Wa fahamu (central nervous system) iitwayo neurocysticercosis
Mfano wake ni kifafa
👉30% ya wagonjwa wenye kifafa huwa ni wale ambao hushambuliwa Na minyoo hii ipatikanayo kwenye nguruwe
👉🏾Watu milioni 50 duniani wanaopata kifafa , huwa ni walaji wazuuri Wa Nguruwe.

JEE NG’OMBE, MBUZI, KONDOO NA WANYAMA WENGINE WALIWAO NA WENGI HAWANA MINYOO??

Ukweli ni kwamba Hata wanyama wengine nyama zao huwa zina minyoo aina ya Taenia saginata.
Ila minyoo ya Taenia saginata ni tofauti Na Taenia solium kwa sababu; Saginata wanakufa kwa joto Dogo sana, lakini solium wanahitaji 71C bila Hata kupungua!!
Swali langu kwako wewe msomaji Wa nakala hii;
👉🏾Nani anaepika huku akipima joto limefika au laa???

HITIMISHO

Tahadhari, sana Na nyama ya nguruwe , kwa sababu madhara yake ni makubwa kuliko faida yake!!!

Shared from;
Dr Isack

Namna Biblia inavyomueleza Bikira Maria

Biblia inashuhudia kuwa watu wanatofautiana

Maandiko matakatifu yanawasifu watu mbalimbali kutokana na jinsi walivyomuamini Mungu na kutenda makuu kwa ajili ya taifa lake.
Abrahamu alimuamini Mungu akawa tayari kumtolea sadaka mwanae Isaka, tukio lililomfanya apate baraka ya pekee ya kuwa baba wa waamini (Mwa 22:15-18).
Yosefu, mwana mpenzi wa Yakobo, alikuwa mwaminifu hata akaliokoa taifa lisiangamie kwa njaa (Mwa 50:20).
Musa ndiye mkombozi wa taifa la Mungu katika Agano la Kale: aliongoza Israeli kutoka [[utumwani Misri akalipatia sheria kutoka kwa Mungu katika mlima Sinai. Maandiko ya Agano la Kale yanakiri, “Wala hajainuka kiongozi kama alivyokuwa Musa” (Kumb 34:10-12).
Waliofuata ni Yoshua, Debora, Gideoni, Ruthu, Samweli, wafalme Daudi na Solomoni, manabii Eliya, Isaya, Yeremia, Ezekieli na wengineo.
Mwishoni Yesu Kristo akamsifu Yohane Mbatizaji akisema, “Ni mkuu kati ya uzao wa wanawake” (Lk 7:24-28).
Elizabeti, mama wa Yohane, alijiona hastahili kutembelewa na Bikira Maria, Mama wa Yesu, akamuita, “Mama wa Bwana wangu” (Lk 1:43).
Bikira Maria si mtu wa ziada katika mpango wa Mungu bali ni mshiriki mkuu wa ukombozi wa binadamu. Maria amechangia wokovu kwa kukubali mpango wote wa Mungu aliyetaka amzae Mwanae, amlee na kumfuata kiaminifu hadi msalabani, aliposhiriki kumtoa kama sadaka ya kutuokoa. Msimamo wake ulikuwa mmoja tu: “Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema” (Lk 1:38).
Tukichunguza nafasi yake katika fumbo hilo, tunaweza kukiri pamoja naye kuwa ni Mwenyezi Mungu aliyemtendea makuu (Lk 1:49), kwa kuwa, “Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu” (Yoh 3:27).
Yale yote ambayo Wakristo wengi wanayasadiki kuhusu Bikira Maria, hakujipatia bali alijaliwa na Mwenyezi Mungu huku akiitikia kwa hiari fumbo la mpango wake.

Utabiri kuhusu Bikira Maria kwenye Biblia

Biblia inatupatia utabiri uliotolewa na Mungu mwanzoni mwa historia kuhusu mwanamke atakayemshinda nyoka wa kale (Shetani): “Nitaweka uadui kati yako na huyu mwanamke, kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa chako” (Mwa 3:15). Juu ya [[Eva wa kale, ambaye alidanganywa na kuangushwa na Shetani atende dhambi, imesemwa: “Adamu akamwita mkewe jina lake Hawa, kwa kuwa ndiye aliye Mama wa walio hai” (Mwa 3:20). Hata hivyo Adamu na Eva wa kale wametuletea kifo (Rom 5:12). Mababu wa Kanisa wanamtazama Bikira Maria kama Eva mpya aliyemshinda Ibilisi na kuwa mama wa wote walio hai. Yesu, aliye Adamu mpya, alipokuwa anakamilisha sadaka ya ukombozi pale msalabani alimfanya Mama yake awe Mama wa waliokombolewa kwa kumkabidhi mwanafunzi, tena yule aliyempenda zaidi. “Penye msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mamaye, na umbu la mamaye, Mariamu wa Kleopa, na Mariamu Magdalene. Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, “Mama, tazama, mwanao”. Kisha akamwambia yule mwanafunzi, “Tazama, mama yako”. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake. (Yoh 19:26-27).
Utabiri mwingine ulisema, “Tazama Bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamuita jina lake Emanueli, yaani Mungu pamoja nasi” (Isa 7:14). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:34-35, “Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu akakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli. Kwa sababu hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu”. “Imba, ee binti Sion, piga kelele, ee Israeli, furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, ee binti Yerusalemu. Mfalme wa Israeli, naam, yeye Bwana yu katikati yako” (Sef 3:14-15). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:28: “Malaika akaingia nyumbani mwake akamwambia, ‘Furahi Maria, umejaliwa neema kubwa, Bwana yu pamoja nawe’”. “Umebarikiwa wewe katika kila hema la Yuda na katika kila taifa, nao wanaposikia jina lako watafadhaika. Imani yako haitatoka mioyoni mwa watu wanaoukumbuka uweza wa Mungu milele” (Yudithi 14:7; 15:9). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:42, “Akapaza sauti kwa nguvu akasema, ‘Umebarikiwa wewe kuliko wanawake wote, na yeye utakayemzaa amebarikiwa’”.
Bikira Maria ni fumbo la ajabu alilolifanya Mungu katika mpango wa wokovu kwa ajili yake na kwa ajili yetu. Jamaa yake Elizabeti alimpongeza tena akiongozwa na Roho Mtakatifu, “Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale uliyoambiwa na Bwana” (Lk 1:45).
Hivyo manabii mbalimbali kwa mwanga wa Roho Mtakatifu walimuagua Maria kwa heshima. Mambo yaliyotabiriwa katika Agano la Kale yalitimia katika Agano Jipya: ukombozi ulianza Bikira Maria alipokubali kwa imani fumbo la umwilisho wa Mwana wa Mungu. Bikira Maria hakuwa “chombo” tu kilichotumika bila ya kuelewa, bali alikuwa mshiriki huru wa kazi ya ukombozi ya Mwanae, kwa kuwa alipopashwa habari na malaika alikubali kwa hiari mpango wa Mungu akisema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, na iwe kwangu kama ulivyonena” (Lk 1:38).

Bikira Maria katika maisha ya Yesu

Yesu, kama mtu yeyote mcha Mungu, aliwaheshimu na kuwatii wazee wake: “Basi, akarudi pamoja nao Nazareti, akawa anawatii” (Lk 2:51).
Ishara ya kwanza kwenye maisha ya hadhara ya Yesu iliongozwa na Bikira Maria katika arusi ya Kana ya Galilaya, akisukumwa na huruma kwa wenye shida: kwa ombi lake Yesu aligeuza maji kuwa divai, na wanafunzi wake wakamwamini. Yohane alisimulia hivi, “Siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, ‘Hawana divai’. Yesu akamwambia, ‘Mama tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia’. Mamaye akawaambia watumishi, ‘Lo lote atakalowaambia, fanyeni’. Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. Yesu akawaambia, ‘Jalizeni mabalasi maji’. Nao wakayajaliza hata juu. Akawaambia, ‘Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza’. Wakapelekea. Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maj), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi, akamwambia, ‘Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa’. Mwanzo huo wa ishara Yesu aliufanya huko Kana ya Galilaya, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini. (Yoh 2:1-12).
Bikira Maria anasifiwa kwanza kwa imani yake kuu kabisa, kuliko kwa kumchukua Yesu tumboni tu. Yesu alitaka kuwainua wasikilizaji wake wafuate mambo ya roho kuliko ya mwili. “Basi, mtu mmoja akamwambia, ‘Mama yako na ndugu zako wako nje, wataka kusema nawe’. Lakini Yesu akamjibu huyo mtu aliyemwambia hivyo, ‘Mama yangu ni nani, na ndugu zangu ni akina nani?’ Kisha akanyosha mkono wake juu ya wanafunzi wake akasema, ‘Hawa ndio Mama yangu na ndugu zangu, maana yeyote anayefanya anavyotaka Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye kaka yangu na dada yangu na mama yangu’” (Math 12:46-50). Vilevile, wakati wa utume wake, alimsikia “mwanamke mmoja katika lile kundi la watu akisema, ‘Hongera kwa mwanamke aliyekuzaa na kukunyonyesha’. Yesu akamjibu, ‘Barabara, lakini heri yake zaidi yule anayelisikia Neno la Mungu na kulishika’” (Mk 11:27-28).

Bikira Maria alivyoshiriki Mateso ya Yesu

Katika kumfuata Mwanae Bikira Maria alitabiriwa wazi na mzee Simeoni uchungu kama upanga utakaopenya moyo wake, “Tazama huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa. Nawe mwenyewe uchungu ulio kama upanga utauchoma moyo wako” (Lk 2:34-35).
Bikira Maria alishiriki kwanza mateso ya ukimbizi huko Misri kwa lengo la kumficha Mwanae asiuawe na Herode Mkuu, “Hivyo Yosefu aliamka akamchukua mtoto pamoja na Mama yake akaondoka usiku akaenda Misri akakaa huko mpaka Herode alipokufa” (Math 2:14-15).
Bikira Maria alishuhudia hatua kwa hatua kuteswa kwa Yesu; wanafunzi walipokimbia au kumtazama kwa mbali, yeye alikuwa karibu akaona vema kila teso lililompata Mwanae. Kutokana na fungamano la upendo wa ajabu lililokuwepo kati ya Yesu na Mamaye, alipoyashuhudia yote aliteseka sana katika moyo wake safi, kiasi kwamba Bernardo wa Klervoo akasema, “Msalaba wa Yesu uliwasulubisha wote wawili, Yesu mwilini na Mama yake moyoni”. Uaguzi wa mzee Simeoni ulitimia hivyo.
Kadiri ya mtume Paulo kuteseka ni kutimiliza yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya Kanisa, “Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo” (Kol 1:24). “… maana tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake” (Rom 8:17b).
Pale msalabani Bikira Maria, kwa njia ya mtume Yohane alifanywa Mama wa wote wanaompenda Mwanae; kisha kumzaa pasipo uchungu Bwana wa uzima, pale alituzaa sisi kwa uchungu wa kutisha uliotokana na kumuona Mwanae akifa msalabani. Hata hivyo Bikira Maria aliendelea kumuamini Mwanae aliyeonekana ameshindwa.

Bikira Maria baada ya kifo cha Yesu

Bikira Maria alikuwepo hapo mwanzo wa Kanisa, akilivutia zaidi Roho Mtakatifu kwa sala yake. “Hao wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria Mama yake Yesu na ndugu zake” (Mdo 1:14).
Yesu alisema, “Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili, lakini atakapokuja huyo Roho wa ukweli atawaongoza kwenye ukweli wote” (Yoh 16:12-13). Kwa msaada wa Roho Mtakatifu heshima kwa Bikira Maria ilienea katika Kanisa lote tangu zamani kabisa kadiri ya utabiri wake kuwa ataheshimiwa na vizazi vyote, “Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mdogo, hivyo tangu sasa vizazi vyote wataniita mwenye heri” (Lk 1:48).
Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About