Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Madhara ya Kuvaa/ Kuweka Kope Za Bandia

Mapokeo ya urembo wa kisasa katika nchi zinazoendelea ni sehemu ya mchango wa urembo na mvuto tunaouona kwa baadhi ya wasichana na wanawake ambao kwa hakika unaleta hamasa ya kuangalia.
Hata hivyo, urembo huu huja na hatari zake ambazo wengi wanaweza kuzichukulia poa kwa kuwa hazitokei kwa haraka ama katika muda unaoweza kutolewa ushahidi kwa sasa.

Moja kati ya urembo unaofanywa na wanawake wengi wa kisasa ni kuweka kope za bandia juu ya kope halisi, kweli wengi wanakuwa na mvuto wa aina yake wakikuangalia hasa mtoto wa kiume. Lakini hatari inayotokana na urembo huo ni kubwa zaidi ya matokeo ya muda mfupi.

Wataalam wanaeleza kuwa kope za bandia ambazo hugundishwa kwa kutumia gundi ya nywele inayotumika kugundisha nywele bandia kwa wenye vipara inaweza kuwa chanzo cha upofu wa mtumiaji.

Gundi hiyo hupukutika taratibu sana kiasi cha kutoshtukiwa na kuelekea kwenye mboni ya jicho ambayo ndio moyo wa ‘kuona’. Endapo mtumiaji ataendelea kwa muda mrefu kutumia kope hizi bandia anaweza kujikuta anakuwa na tatizo la kuona ama hata upofu wa haraka katika maisha yake ya baadae.

Hata hivyo, hatari kubwa imeelekezwa kwa maduka ama vibanda vinatumia vifaa vya bei nafuu ikiwemo gundi inayotumika. Ukwepaji wa gharama ama kutokuwa na uwezo wa kutumia gharama kubwa kunamuingiza mrembo kwenye hatari zaidi.

Kuwa mwangalifu, urembo usiwe chanzo cha kuhatarisha afya yako. Kumbuka Afya ni uhai wa mwili wako.

Jinsi ya kuandaa Ndizi Mbichi Za Supu Ya Nyama Ng’ombe

Mahitaji

Ndizi mbichi – Kisia

Nyama ng’ombe – ½ kilo

Pilipili ya kusaga – 1 kijiko cha chai

Tangawizi ya kusaga – 2 vijiko vya supu

Thomu (garlic/saumu) – 1 kijiko cha supu

Bizari mchuzi – 1 kijiko cha chai

Nazi ya unga (ukipenda kuongezea) – 2 vijiko cha supu

Chumvi – Kiasi

Ndimu – 1 kamua

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Weka nyama ng’ombe katika sufuria, tia tangawizi, thomu, pilipili mbichi, bizari, chumvi. Roweka kidogo ukipenda kisha ikaushe yenyewe kwa maji yake
Ongezea maji ya kiasi yasizidi mno, kisha funika na chemsha.
Menya ndizi, ukatekate.
Nyama ikikaribia kuiva, weka ndizi uendelee kupika mpaka viive vyote.
Tia nazi ya unga kidogo tu ukipenda. Koleza kwa bizari mchuzi, pilipili, na ndimu
Epua mimina katika chombo cha kupakulia zikiwa tayari.

JITAMBUE : Maisha yako ya kesho hayalingani na maisha yako ya jana, Anza sasa

THERE IS NO FUTURE IN THE PAST.** Ukitaka kufanikiwa usiangalie nyuma yako kunanini na ulishindwa mara ngapi. Siku zote kukaa Chini nakuanza kujuta kwa makosa uliofanya uko nyuma nikupoteza muda, huo muda Utumie kwa kupanga ya kesho.

Bahati nzuri Mungu alitujalia kusahau, ivyo siku zote sahau ya nyuma na waza yale ya mbele yako.

Maisha bora ya mbele hayawezi kuja kama akili yako imebeba kushindwa kwa nyuma.

Binadamu yeyote anayeweza kupoteza muda wake wa leo kwa kulaumu mabaya ya jana, kesho atapoteza muda akilaumu mabaya ya leo.

Tambua ya kuwa, “hakuna awezaye kurudi nyuma na kuanza upya, bali waweza kuanza leo na kutengeneza maisha yako ya kesho”

Kadri unavyofikiria ya nyuma ndivyo unavyochelewa kufika mbele zaidi. Penda zaidi ndoto yako ya kesho kuliko historia yako ya jana,maana hatima yako siku zote iko mbele na sio nyuma.

Siku zote utashindwa kwa kuendekeza mambo yaliopitwa na wakati maana utakuwa unatumia ujuzi uliopitwa na wakati.

“Habari njema ya siku ni leo, na siku nzuri yako ni ya kesho “

Ukiona umesononeka kwa maisha kuwa magumu jua unaumia kwaajili ya maisha yako ya nyuma, maana unawaza jinsi ulivyo shindwa kulipa kodi ya nyumba,ulivyoshindwa kulipa umeme, maji, ada za watoto na ulivyoshindwa kuendesha biashara yako au ulivyoshindwa kuitetea ajira yako. Usipoteze Muda wako kwa kuwaza yaliopita badala yake waza kesho yako itakuwaje.

Waswahili wanasema yaliopita si ndwele, tugange yajayo. Huwezi kubadilisha jana, Bali waweza kubadilisha kesho yako kwa kufanya maamuzi leo.

Usipoteze Muda kwa kugeuza shingo yako kutazama ya nyuma, utajikuta unadumbukia katika shimo la maisha magumu.

“You can’t have a better tomorrow if you are thinking about yesterday all the time “

Maisha yako ya kesho hayalingani na maisha yako ya jana. Anza sasa.

Kilichompata sista duu bishoo wakati akijidai kununua pete

Mwanamke mmoja aliingia duka la vito vya thamani, akaona pete moja ya dhahabu nzuri sana amabayo ilikuwa kwenye shelf ya chini, wakati anainama apate kuitazama vizuri kwa bahati mbaya (au nzuri!), shuzi likamtoka- druuuuuu, soni ikamuingia huku akigeuka haraka kuangalia kama kuna yeyote dukani pale ameliskia shuzi lake, macho yakagongana na mwenye duka ambaye alikuwa karibu huku uso ukiwa umejaa tabasamu zito, mwana mama hakuwa na uhakika kama amesikika au hakusikika, akaona atumie nafasi ile kuyeyusha…Akauliza “Hii pete bei gani?” . Jamaa mwenye duka, huku akiangua kicheko, akajibu “Umeiona tu umejamba, je nikikuambia bei yake si utakunya kabisa?”

Ilinde ndoto yako

Ndoto ni nini?

Ndoto ni zile ndoto za kiuhalisia ambazo mtu anaweza kuwa nazo akiwa macho na anatumia mawazo yake kutengeneza au kuunda picha ya maisha anayotamani kuishi siku zijazo. Hizi si ndoto ambazo mtu anaota usiku akiwa usingizini, bali ni matakwa ya dhati ambayo yanamfanya mtu ajizatiti na kutia bidii katika mambo anayofanya ili kuyafikia malengo yake.

Kila mtu ana ndoto tofauti ambazo anatamani kuzifikia, na mara nyingi ndoto hizi huwa zinaongoza maisha yake na kumpa dira na mtazamo wa maisha yake ya baadaye. Ndoto hizi zinaweza kuwa kubwa au ndogo, na zinaathiri jinsi mtu anavyochagua kuishi maisha yake ya kila siku, jinsi anavyofanya maamuzi, na hata jinsi anavyoingiliana na watu wengine.

Kwa mfano, mtu mwenye ndoto ya kuwa Rais atajituma katika masuala ya uongozi, atajifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na siasa na uongozi wa jamii au nchi. Ataweza pia kujihusisha na harakati mbalimbali za kijamii au kisiasa ili kujenga umaarufu na kuwa na uwezo wa kufikia ndoto yake.

Kwa upande mwingine, mtu anayetamani kuwa mwimbaji bora atajikita katika kuendeleza kipaji chake cha uimbaji, kuhudhuria mashindano ya muziki, na pengine atajitahidi kuwa karibu na watu wengine waliofanikiwa katika tasnia hiyo ili ajifunze mbinu za kufanikiwa.

Wale wenye ndoto za kumiliki vitu kama nyumba za kifahari, magari, au kuwa bilionea, mara nyingi wanajikuta wakihusika katika kufanya kazi kwa juhudi zaidi, kujifunza na kutafuta taarifa juu ya uwekezaji, na kutafuta njia bora za kukuza uchumi wao binafsi.

Ndoto za kutembelea nchi fulani zinaweza kumfanya mtu aweke akiba ya pesa, ajifunze kuhusu tamaduni mbalimbali, na hata kujifunza lugha tofauti ili kujiandaa kwa safari yake. Kwa kufanya hivi, mtu huyo anajiweka katika nafasi nzuri ya kufikia ndoto yake na kuifanya iwe halisi.

Kwa ujumla, ndoto za mchana ni muhimu sana katika kuhamasisha na kutoa motisha kwa mtu kufikia mafanikio makubwa maishani. Zinamfanya mtu kuwa na malengo, azimio la dhati, na muelekeo wa wapi anapenda maisha yake yawe siku za usoni. Ndoto hizi zinapoambatana na mipango mizuri na jitihada za makusudi, mara nyingi huwa na matokeo chanya na kutimia kwa matarajio ya mtu.

Zote hizo ni ndoto ambazo kila mmoja alikua nazo huenda ni kipindi anakua au hata sasa bado anayo.
Kwa bahati mbaya sana watu wengi wamekuwa na ndoto kubwa sana wakiwa wadogo na kuzipoteza walipoanza kuingia kwenye uhalisia wa maisha.

VITU VINAVYOWEZA KUIPOTEZA NDOTO YAKO.

Ugumu wa Maisha.

Maisha yanavyozidi kubadilika na kuwa magumu ndipo baadhi ya watu huanza kuasahu vile vitu ambavyo walikua wanatamani waje kuwa navyo. Maisha yanapokuwa magumu sana wengi huona haiwezekani tena wao kufikia ndoto zao hivyo kukata tamaa kabisa na kuamua kuwa na maisha ya kawaida.
Mtu anaweza kujitazama vile alivyo na kuona yeye hafananii kabisa kuja kuwa Rais wa nchi hii labda kutokana na familia aliyotokea au maisha yanayoendelea sasa hivi.
Nakuomba kama unapitia hali hiyo anza kuikataa kabisa ili usije kupotea.

Marafiki wabaya.

Marafiki na watu unaokuwa nao mara kwa mara wanaweza kuwa sababu kubwa sana kukupoteza kabisa na kukufanya wewe uache kupigania ndoto yako.
Ndoto yako ni ya thamani sana ndio maana inapata upinzani.
Ndio maana utaambiwa haiwezekani. Ndio maana watakucheka ukiwaambia wewe unataka kuwa Rais wa nchi hii au unataka kua Bilionea.
Mara zote watu wanakuhukumu kutokana na hali uliyonayo sasa hivi.
Unaweza kuachwa na Mpenzi wako umpendaye kwa sababu tu yeye anaangalia maisha uliyonayo sasa hivi na hata ukimueleza ndoto zako haamini kutokana na hali yako ya maisha uliyonayo sasa.

Ufanyeje?

Kaa nao mbali wale watu ambao hawana ndoto kama za kwako. Kaa mbali na watu ambao wanafikiri kama kuku. Yaani wao wamejiona kwamba ni maskini na haiwezekani kuwa tajiri labda kuiba tu. Inawezekana ni watu wako wa karibu sana labda kaka, dada, wazazi.
Ufanyeje?
Usikubali kuwasikiliza weka pamba sikioni. Mimi kuna mtu aliniambiaga hizo ni ndoto za mchana haziwezi kutokea kamwe lakini sijakata tamaa naendelea kufanyia kazi ndoto zangu.

UNALINDAJE NDOTO YAKO?

Iandike.

Kama unasema una ndoto lakini bado ipo kichwani bado hujaelewa maana yake. Katafute Notebook nzuri sana ya gharama Huwezi kuandika ndoto ya kuwa Bilionae kwenye note book ya elfu mbili aisee.
Tafuta notebook ya Gharama hata ya 20,000 ili uweze kuitunza vizuri. Andika kila kitu unachokitaka kwenye dunia hii. Hakikisha umeandika kila Kitu na usiache hata kimoja.
Hii ni njia ya kwanza ya kuilinda ndoto yako. Nikikutana na wewe sehemu Uniambie au unionyeshe kilipo kitabu chako cha ndoto. Andika ni Jinsi gani unaweza kupata vile vitu. Ni ujuzi wa namna gani unahitaji ili uweze kufikia ndoto zako. Ni watu wa namna gani unahitaji kuambatana nao ili ufanikiwe kwenye doto zako. Andika ni Baada ya Muda gani utakua umefikia Ndoto zako. Sasa hapa Ni somo jingine kabisa jinsi ya kuandika malengo. Malengo ya muda mfupi na Muda mrefu.

Soma ndoto zako kila siku Asubuhi na kabla ya Kulala.

Soma kila siku namaanisha kila siku asubuhi na jioni. Kwanini usome kila siku ? Unaichora au unaiingiza picha ya ndoto zako ndani ya ubongo wako hii itakufanya chochote utakachokutana nacho kama hakiendani na ndoto yako uweze kukiepuka na kama kinaendana basi uweze kukivuta. Unaposoma inajijenga kwenye akili yako na kutengeneza ukaribu wa wewe kuifikia zaidi.
Soma na tafakari.

Tenga Muda peke yako.

Hakikisha unatenga Muda wa peke yako angalau kila wiki ukiwa peke yako sehemu ambayo haina usumbufu wowote. Sehemu hiyo utakua unaipa akili yako nafasi ya kutafakari juu yako wewe. Jitazame ulivyo sasa halafu jitazame wewe ukiwa umefikia kwenye ile ndoto yako. Kama ni gari basi anza kujiona jinsi unavyoliendesha lile gari la ndoto yako. Kama ni Rais ebu jione ukiwa Ikulu basi Jione ukiongoza majeshi. Kama ni Bilionea anza kuona ukiwa Bilionea utakavyokua. Utakavyoweza kubadilisha maisha ya watu wengi sana Duniani. Ona jinsi dunia inavyofurahia Mungu Kukuumba wewe kwasababu maisha yao yamebadilika. Nashauri hili ufanye angalau lisaa limoja ukiwa peke yako bila simu wala kifaa chochote cha mawasiliano.

Soma Vitabu na Fanyia Kazi ndoto yako Kila siku.

Soma vitabu ambavyo vitakuza ufahamu wako ili wewe uweze kuifkia ndoto yako.
Kama unataka kuwa Rais wa Nchi lazima ujue kua unakwenda kuongoza watu hivyo vitabu gani usome ili ukuze ufahamu wako.
Unataka kuwa Bilionea hutaweza kuwa bilionea na ufahamu ulionao sasa hivi mali zote zinatakiwa ziongozwe na wewe hivyo jijengee tabia ya kujisomea vitu mbalimbali juu ya ile ndoto yako.
Ili ufikie Ubilionea unaanza na hatua moja anza leo kupiga hatua moja moja hadi ufikie kule unakotaka. Usikubali kabisa siku ipite ujafanya chochote juu ya Ndoto yako ni kupoteza fursa.

Kama tunavyojua fursa ya kwanza ni uhai tulionao leo hivyo usitumie vibaya leo siku zote unakuwaga na leo tu. Ukiweza kuipangilia leo vizuri itakufikisha kwenye ndoto yako.

Jipongeze

Kwenye kila hatua unayopiga jipongeze ili kujiongezea hamasa na wewe uweze kusonga mbele. Unaweza kujipa zawadi ndogo ndogo ambazo huwa unazipenda kila unapopiga hatua kuelekea kule unapotaka.

Iseme ndoto yako sehemu yeyote unapokuwa.

Kwanini uiseme kwa sababu una Imani na Imani ni kua na hakika juu ya mambo yasiyoonekana.
Hata Yusuf alianza kuwaambia ndugu zake kwamba anaona ndoto anaona akiwaongoza. Walimkemea lakini hakusita kuendelea kuwaambia.
Hii itakusaidia unapokamilisha iwe ushuhuuda kwamba huyu jamaa alituambiaga anakuja kuwa Rais, Bilionea, Mtu mkuu sana.

Kuwa na ndoto kubwa ni jambo la muhimu sana katika maisha. Mara nyingi, inasemekana kwamba ikiwa una ndoto ambazo hazikutoi usingizi, basi unaelekea katika mwelekeo sahihi. Mara nyingine, watu watakuita mchawi au Freemason wanapoona unafanikiwa. Lakini, kumbuka, maneno hayo hayana msingi kama yanasemwa wakati unapoanza tu kuota ndoto zako kubwa, kama vile kujenga ghorofa au kumiliki gari la kifahari kama BMW, wakati huna chochote.

Watu wanaokatisha tamaa mara nyingi ni wale wale ambao hawawezi kuona mbali kuliko hali yako ya sasa. Hawaelewi kwamba ndoto huenda zaidi ya hali ya sasa. Kama mtoa hamasa Norman Vincent Peale alivyosema, “Panda picha ya mafanikio ya kustaajabisha katika akili yako. Fikiria hili kwa nguvu. Kisha, fanya kazi kwa ujasiri kila siku kufanya picha hiyo kuwa uhalisia.”

Ni muhimu pia kutambua kwamba kuisema ndoto yako, kuiweka wazi mbele ya wengine na kujiamini, kunaweza kukujengea ujasiri. Hiyo ina maana ya kuendelea kutafakari kwa bidii jinsi ya kuifanya ndoto yako iwe kweli. Usemi unasema, “Ujumbe mzito huvunjika moyo pale unapotamkwa.” Hivyo, endelea kuongea kuhusu matarajio yako, mipango yako, na ndoto zako. Hii itakupa nguvu ya kuvumilia nyakati ngumu na kukusaidia kubaki thabiti katika njia yako.

Naamini una kila kitu kinachohitajika kuilinda ndoto yako. Itapasa uwe na nidhamu, uvumilivu, na azma thabiti. Kikubwa zaidi, uwe tayari kujifunza na kukua. Kila hatua unayopiga kuelekea katika ndoto yako, hata ikiwa ni ndogo, ni hatua muhimu.

Kumbuka kwamba hakuna jambo la maana ambalo hutokea usiku mmoja. Mafanikio ya kweli hujengwa kidogokidogo. Kwa hiyo, hata kama unakabiliwa na kejeli au shutuma, usiruhusu hiyo ikuvunje moyo. Kama alivyosema mwanasiasa na mwandishi wa Marekani Adlai Stevenson, “Ni jambo kubwa kuweza kukumbuka wakati umefanikiwa, kwamba kuna wakati pia uliwahi kushindwa, na kwa vipimo vilevile, ukatumia fursa hiyo kukua na kuboresha.”

Hivyo basi, lipokee wazo la mafanikio moyoni mwako, liweke hai katika mazungumzo yako na hatua zako, na kisha, lifanyie kazi kwa ajili ya kesho yenye matumaini. Jitahidi kwa kila njia kuona ndoto yako ikitimia. Jipe moyo na usisahau kusherehekea kila hatua unayopiga kwa mwelekeo chanya.

Mapishi ya Wali, mchicha wa nazi na nyama ya kukaanga

Mahitaji

Mchele (rice 1/2 kilo)
Mchicha uliokatwakatwa (spinach mafungu 2)
Nyama (beef 1/2 ya kilo)
Nyanya (tin tomato 1/2 ya tin)
Nyanya chungu ( garden egg 3)
Kitunguu swaum (garlic cloves 3)
Tangawizi (ginger)
Curry powder
Vitunguu (onion 2)
Limao (lemon 1)
Chumvi
Pilipili (scotch bonnet pepper )
Tui la nazi (coconut milk 1 kikombe cha chai)

Matayarisho

Kaanga kitunguu kikishaiva tia nyanya na chumvi. kaanga mpaka nyanya ziive kisha tia nyanya chungu,curry powder na pilipili 1 nzima, baada ya hapo tia mchicha na uuchanganye vizuri kwa kuugeuzageuza. Mchicha ukishanywea tia tui la nazi na uache lichemke mpaka liive na hapo mchicha utakuwa tayari.
Safisha nyama kisha iweke kwenye sufuria na utie chumvi, tangawizi, limao na kitunguu swaum. Ichemshe mpaka itakapoiva na kuwa laini. Baada ya hapo weka sufuria jikoni na mafuta kidogo yakisha pata moto tia vitunguu na nyama na uvikaange pamoja, kisha tia curry powder na ukaange mpaka nyama na viunguu vya brown. na hapo nyama itakuwa imeiva. Malizia kwa kupika wali kwa kuchemsha maji kisha tia mafuta, chumvi na mchele na upike mpaka uive. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuseviwa.

Jinsi ya Kupika Kalmati

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
Hamira (yeast kijiko 1 cha chai)
Sukari (sugar 2 vikombe vya chai)
Hiliki (cardamon 1/4 ya kijiko cha chai)
Maji kikombe1 na 1/2
Mafuta

Matayarisho

Changanya unga, hamira, maji na mafuta kijiko 1. Koroga vizuri mpaka upate uji mzito usiokuwa na madoge Baada ya hapo uache uumuke kisha zichome kalmati katika moto wa wastani. Baada ya hapo tia sukari, hiliki na maji 1/2 kikombe katika sufuria na ichemshe uku unakoroga mpaka iwe tayari.(ukitaka kujua kama iko tayari chovya mwiko kisha gusa na vidole utaona iko kama nta au gundi) Baada ya hapo tia kalmati na uzichange pamoja mpaka zikolee kisha zitoe na uziache mpaka zipoe tayari kwa kuliwa.

Mapishi ya tambi za mayai

Tambi za mayai ni moja kati ya vyakula ambavyo napenda kuandaa pale ninapokua ninaharaka au sina muda mrefu wakukaa jikoni.pishi hili huchukuca muda mfupi sana na nimlo uliokamilika.

Mahitaji

  1. Tambi ½ paketi
  2. Vitunguu maji 2 vikubwa
  3. Karoti 1
  4. Hoho 1
  5. Vitunguu swaumu(kata vipande vidogo) kijiko 1 cha chakula
  6. Carry powder kijiko 1 cha chai
  7. Njegere zilizochemshwa ½ kikombe
  8. Mafuta kwa kiasi upendacho
  9. Mayai 2
  10. Chumvi kwa ladha upendayo

Njia

1.Chemsha maji yamoto yanayotokota,ongeza chumvi na mafuta kidogo,weka tambi kwenye maji hayo chemsha adi ziive.Chuja maji yote ili kupata tambi kavu
2.Katika bakuli piga mayai kisha weka pembeni
3.Katika kikaango,weka mafuta,vitunguu maji ,vitunguu swaumu,hoho, karoti na carry powder,kaanga kwa pamoja katika moto mdogo kwa muda mfupi kwani mboga hazitakiwi kuiva.
4.Ongeza tambi na njegere katika kikaango,geuza kila mara ili kuchanganya .
5.Ongeza mayai kwenye tambi kisha geuza kwa haraka bila kupumzika adi mayai yaive na tambi ziwe kavu.Tayari kwa kula

Katika hatua hii ongeza moto uwe wa wastani,moto ukiwa mdogo mayai yatafanya tambi zishikane na kufanya mabonge.

Mambo ya kufanya mwezi Disemba

Ikiwa leo ni tarehe **1/12 huwezi amini kuwa hakuna tarehe 1 nyingine tutakayoiona ya mwaka huu hivyo sichelei kusema kuwa mwaka umeisha .Lakini mwaka unaishaje??? pengine hili ndilo swali gumu na la muhimu la kujiuliza .Je, Mwaka unaisha ukiwa umefanya nini cha kujipongeza??? .Je mwaka unakaribia kuisha maarifa yako yakiwa yameongozeka kwa kiasi gani???.Haya ni maswali muhimu sana unavyooanza kufikiria juu ya sherehe za mwisho wa mwaka.

Watu waliopiga hatua katika fikra – yaani, wale waliofanikiwa kutimiza malengo na mipango waliyojiwekea – wanajikuta katika kipindi cha kipekee ifikapo mwezi huu. Ni wakati ambao wanapaswa kuchukua muda na kutafakari kwa kina juu ya safari yao ya mwaka uliopita. Huu si tu wakati wa kuzingatia mafanikio na mafunzo, bali pia ni kipindi cha kulinganisha matarajio yaliyokuwa yamewekwa dhidi ya yale yaliyotimia.

Kurudi kwenye malengo yaliyowekwa hapo awali ni zoezi la muhimu linaloleta tafakuri juu ya uendelevu na ufanisi wa mikakati iliyotumika. Watu hawa wanaweza kujiuliza maswali kama, je, malengo yalikuwa yanatekelezeka? Je, walikutana na changamoto gani, na walizishinda vipi? Changamoto hizi zinaweza kuwa za ndani kama vile kutunza motisha, au za nje kama vile mabadiliko ya kiuchumi na kijamii yaliyokuwa yameshuhudiwa.

Inawezekana pia walikuwa na malengo ambayo hayakutimia. Katika hili, kuna fursa ya kujifunza na kuchukua hatua za marekebisho. Mwisho wa mwaka ni muda mwafaka wa kutathmini upya na kuweka mikakati mipya, kuondoa yaliyopitwa na wakati na kuja na mawazo mapya yatakayowasukuma mbele zaidi. Uchambuzi wa kina utawasaidia kuweka malengo yanayoweza kutekelezeka kwa mwaka unaofuata pamoja na kutengeneza mpango kazi madhubuti ambao utawaongoza katika hatua zao zijazo.

Kwa kuangalia nyuma na kufanya tathmini yenye unyoofu, waliopiga hatua katika fikra wanaweza kupata msingi imara wa kujenga juu yake. Wanaweza kujitathmini na kujipanga upya, kuchukua mwelekeo wenye nguvu na mpya ambao utawawezesha kutimiza malengo yao yaliyosasishwa na yaliyo wazi zaidi. Kila hatua, kila mafanikio, kila funzo, yote huchangia katika safari yao ya kipekee ya maendeleo binafsi na ya kitaaluma.

Leo nataka nikuekeze mambo muhimu ya kufanya mwezi huu pamoja na kuwa unawaza sikukuu na kusafiri kwenda kwenu .Mambo haya unaweza kuwa hujawahi kufanya lakini ni muhimu sana ukafanya mwaka huu ili mwakani tuone mabadiliko .Mambo hayo ni pamoja na ;

1.Fanya Tathimini (Evaluation)

Tathimini ni kipimo kinachoonesha kushindwa kwako na kufanikiwa kwako .Mwezi huu ni mwezi wa kukaa chini na kurejea kwenye malengo na mikakati uliyokuwa umejiwekea na kuona ni kwa jinsi gani umefanikiwa .Ainisha mambo uliyofanikiwa na ambayo hujafanikiwa .Kwa yale uliyofanikiwa jipongeze kwa kufanikiwa kwa yale ambayo hujafanikiwa jiulize kwanini hayajafanikiwa ili yakupe mbinu na hatua mpya mwaka ujao.

Andika kwa mtindo huu;

SEHEMU A:MAMBO NILIYOFANIKIWA HUU

-Mwaka huu nilifanikiwa kuwapata marafiki wazuri wanaounga mkono maono yangu
-Mwaka huu nilifanikiwa kuanzisha biashara ya genge
-Mwaka huu nilifanikiwa kusoma vitabu viwili

*Jitihidi sana kujipongeza kwa yale uliyofanikiwa na hii ni tabia ya watu waliofanikiwa .Usione umefanya madogo lahasha.*

SEHEMU B:MAMBO AMBAYO SIKUFANIKIWA mwaka huu

-Sikufanikiwa kuhudhuria semina hata moja ya ujasiriamali
-Sikufanikiwa kuboresha ofisi

Kwa yale ambayo hukufanikiwa jiulize kwanini hukufanikisha utagundua wewe ndiye sababu kubwa ya kutoyafanikisha .

2.Anza kuandaa malengo ya mwaka ujao (GOAL SETTING)

_Pasipo maono, watu huacha kujizuia_
~(Biblia)

Ndiyo bila malengo hutafika na utafanya kila kitu bila mpangilio .Huu ndio mwezi kwako ambao unapaswa kuandaa malengo ya mwaka ujao haijalishi hukuwahi kuweka malengo toka unazaliwa .Najua malengo yako yalikuwa yanakaa kichwani mwaka huu amua kuandika kwenye notebook Nzuri .Andika kwa ujasiri mkubwa sana .Malengo yako yafuate kanuni za malengo(yapimike,yawe na ukomo,yawe mahususi na yakufikika ).

Andika kwa mfano huu;

-Kufikia Mei  nitakuwa nimefuga kuku watatu hata kama nyumba yangu ni ndogo .

-Kufikia Agosti   nitakuwa nimehudhuria semina 2 za ujasiriamali

Ukiandika kwa mfumo huo itakusaidia kuyafikia malengo yako maana yamefuata kanuni za malengo.

3. Andaa Bajeti ya mwaka  (Budgeting)

Hii ni sehemu ambayo inaleta shida sana .Na hii ni kwa sababu hata wazazi wetu wametulea bila kutufundisha bajeti.Masomo ya darasani wengi hatufundishwi kuishi kwa bajeti .Lakini Tusilaumu sana kutofundishwa maana lawama ni tabia ya kimaskini tuamue mwakani 2017 kuishi na kutembea na bajeti

Mara nyingi tukiulizwa hela zetu zinaenda wapi huwa hatuna majibu sahihi .Hii ni kwasababu hatuna bajeti .Kwanini bajeti??? .Bajeti hutusaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na yaliyo nje ya bajeti .Bila bajeti sehemu ya kutembea kwa mguu utapanda bodaboda .Bila bajeti utanunua simu ya laki saba wakati unasema huna mtaji wa laki sita.Bajeti itaamua uchangie harusi na kitchen party ngapi kwa mwaka.

Ndiyo lazima tubadilike hata mimi nimeamua hivyo mwaka ujao.Kama una familia kaa na mke wako tengeneza bajeti ya mwaka.Kuna vitu vinaweza kujitokeza njiani na hivyo kumbuka kuweka dharura .

Bajeti iliyopangwa kwa mwaka ujao ni kama ramani inayoonesha njia ya malengo na maelekezo ya kifedha ambayo shirika au mtu binafsi anapaswa kufuata. Inatoa muhtasari wa kina kuhusu matarajio ya mapato na matumizi, na hivyo kumwezesha mtu au shirika kupanga kwa ufanisi zaidi juu ya rasilimali zake. Kuweza kwenda sambamba na bajeti hii, mtu au shirika linahitaji kuelewa vizuri vipaumbele vyake na kuweka mipango thabiti kwa kila sehemu ya matumizi au uwekezaji.

Katika kuhakikisha ufanisi, ni muhimu kwa shirika kuwekeza nguvu katika upangaji wa bajeti ulio sahihi, utafiti wa masoko ili kufahamu mwenendo wa kiuchumi unaoweza kuathiri mapato na matumizi, pamoja na uboreshaji wa mbinu za usimamizi wa fedha. Ufuatiliaji wa mara kwa mara wa bajeti na utathminini wa maendeleo halisi ikilinganishwa na yale yaliyopangwa ni muhimu sana. Nguvu katika kufuatilia na kurekebisha mtiririko wa bajeti inaweza kumaanisha tofauti kati ya kufikia malengo ya kifedha au kukabiliana na upungufu.

Kuwekeza nguvu inamaanisha pia kuwa na nidhamu na ufuatiliaji madhubuti wa matumizi ya kila siku, kujifunza kutokana na takwimu na ripoti za awali za fedha, na kujitayarisha kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza. Mwisho, uwekezaji katika mafunzo kwa wafanyakazi wanaoshughulikia fedha na matumizi inaweza kuongeza ufanisi na kuimarisha uzingatiaji wa bajeti iliyowekwa.

Fahamu kuhusu kitambi na uzito uliopitiliza

Mwili wa binadamu umeundwa kwa organs na mifumo mbalimbali ili kuuwezesha kufanya kazi sawia. Mfano,
Moyo
Ini
Figo
Mapafu
Mfumo wa fahamu
Mfumo wa uzazi
Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula.

Vyote hivi hufanya kazi kwa usahihi ikiwa mwili una balance ya
Mafuta
Sukari
Nishati
Protein
Vitamins

Lakini kutokana na mfumo wa maisha kubadilika kwa kiasi kikubwa, watu wengi inasemekana wankumbwa na tatizo la OVERWEIGHT (Uzito uliopitiliza) na OBESITY (Kitambi).

Kwa nini tatizo ni kubwa katika rika zote..!?
1.°° Ulaji wa vyakula vya wanga, kama ugali wa sembe , chapati.
2.°° Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi.
3.°° Ulaji wa nyama nyekundu, kuku wa kisasa na mayai.
4.°° Utumiaji wa beer na soda kwa wingi.
5.°° Mfumo mbaya wa ulaji kwa ujumla.

Madhara yake.

  • Shinikizo la damu (Pressure).
  • Kisukari (Diabetes)
  • Maradhi ya moyo (Heart attack).
  • Maumivu ya mgongo na joints.
  • Kiharusi
  • Maradhi ya mifupa (Osteoporosis)

Nini cha kufanya

  • Mazoezi ya viungo ni muhimu sana.
  • Kuepuka ulaji wa mafuta mengi.

Haya mapenzi jamani! Umewah kumpenda kwa kihivi??

Sijui Kama ushawai fall in love ile haswaa..

yani unampenda mtoto hadi akikupigia ile sauti ilivo tamu unajiskia kutafuna na kuimeza hiyo simu

Akikuita tu “my love”unajiskia tu kuvua nguo mwenywe
..
hicho kiupendo ukiwa nae unajskia unaweza piga wanaume 8 kwa pamoja

Yani ile love mtashinda pamoja kutwa nzima afu usiku unakopa salio umpigie muongee

Yani yale mapenz kiasi ukiona love story za romeo na Juliet unaona hakuna wanachofanya coz mapenz yao hayafikii yenu..

ile true love akikuangalia machoni akuguse mashavu afu akwambie,”I love u”
Unajishikilia kwenye ukuta usizimie..

yani ukimfikiria unaweza kulala chini ya kitanda Ku dilute hiyo feeling coz ni too much..

Umewahi kufeel hivyo??

Kama ushawai experience hivyo?? Basi HIYO SIYO “LOVE” NI “BANGI” PLZ ACHA KUTUMIA!
#ishakua_biashara_kichaa

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini Ya Pilipili Mbichi

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama

Nyama ya ng’ombe vipande vidogo – 2lb

Nyanya – 1

Kitunguu Kilichoktwa katwa – 1

Mafuta – 2 vijiko vya supu

Paprika (bizari ya masala ya rangi) – ½ kijiko cha chai

Kidonge cha supu – 1

Chumvi – Kiasi

Ndimu – Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha nyama kwa chungio ili itoke maji. Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwerangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.
Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.

Vipimo Vya Mboga

Mchicha ulio katwa katwa 400 gm

Nyanya 1

Kitunguu kilicho katwa 1

Nazi ya unga kiasi

Pilipili mbichi 2

Mafuta ½ kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha na Kupika

Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.
Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.
Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji
Tia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa
tayari kuliwa

Vipimo Vya Maharage

Maharage – 1 kopo

Kitunguu – 1

Nazi – 1 mug

Nyanya (itowe maganda) – 1 kiasi

Pilipili mbichi – 2

Mafuta – 1 kijiko cha supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.
kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.
Tia chumvi, maharage na nazi uwachie
moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.

Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi

Pilipili mbichi – 4/5

Kotmiri – 1 Kijiko cha supu

Ndimu – kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 1 chembe

Mafuta ya zaituni – 2 vijiko Vya supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha

Kwenye blender, tia vipimo vyote na sage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Vipimo Vya ugali

Maji – 4 Vikombe kiasi inategemea na unga

Unga wa sembe – 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.

Historia Fupi ya Ibada ya Rozari

Katika Kalenda ya Kanisa Katoliki,
huwa mwezi wa tano na mwezi wa kumi
ni miezi ambayo imewekwa kwa ajili ya
Bikira Maria na Mama Kanisa. Hivyo
hiyo miezi huwa inasaliwa rozari.
Wengi waweza kujiuliza kuwa ni kwa
nini ifanyike miezi hiyo? Yafuatayo nimajibu, mwezi wa tano umewekwa kwa
heshima ya Bikira Maria kutokana na
nini kilitokea katika historia hapo
nyuma.
Mnamo Karne ya 16 mwezi
watano kwa miaka yote ulikuwa ni
mwezi ambao sikukuu nyingi za
kiserikali ndo zilikuwa zikifanyika.
Kanisa kwa kutambua hilo nalo
likahidhinisha pia mwezi wa tano uwe
ni mwezi wa Rozari, na kwa makusudi
zaidi Kanisa lililenga kuwa sherehe hizo
ziendane na taratibu za wakristu, ni
kwa msingi huo sherehe hizo ziliendana
na mwezi wa rozari na kutokea hapo
ikahidhinishwa kuwa mwezi wa tano wa
mwaka ni mwezi wa Bikira Maria. Pia
mwezi wa kumi (October) pia ni mwezi
wa Bikira Maria na pia ni mwezi wa
Kusali Rozari kutokana na historia ya
hapo nyuma pia, na ilikuwa kwamba
baada ya ushindi wakristo walioupata
katika vita baina yao na yule aliyeitwa
Lepanto mnamo 7 October, 1571, Papa
wa wakati ule Papa Pius V aliufanya
huo ushindi kuwa ulitokana na
maombezi ya Bikira Maria, na alisema
kuwa rozari ni silaha kubwa hata kuliko
silaha kubwa za kivita. Ni Kwa msingi
huu tunaona kuanzia hapo mwezi wa
kumi ukawa mwezi uliotengwa na
Mama Kanisa kwa Bikira Maria, na pia
ukaitwa mwezi wa Rozari.

HISTORIA YENYEWE

Ni kwamba sala ya Rozari inasemekana
kuanzishwa na Mt. Dominico
aliyezaliwa mnamo mwaka 1170 na
kufariki mwaka 1221 na hiyo sala Mt.
Dominico aliipata kwa njia ya ufunuo
ambapo Bikira Maria alimtokea na
kumwamuru awe anasali rozari. Bikira
Maria alimwamuru mtakatifu Dominico
kusali rozari kwa kipindi hicho iwe
kama silaha yake ili kupambana na
uzushi uliokuwa umeibuka ukipingana
na mafundisho ya Kanisa, na huo
uzushi uliitwa ‘ Albigensia’ hili ni kundi
lilokuwa na imani kuwa Duniani kuna
nguvu nguvu mbili zenye uwiano sawa
lakini hupingana na kupigana moja
baada ya nyingine, nazo nguvu hizo ni
Mungu na Shetani. Hivyo hawa
waliamini kabisa kuwa Mungu na
Shetani wana nguvu sawa ( Dualistic )
waliamini pia kuwa dunia hii imejaa
uovu kwa kuwa iliumbwa na mwovu. Ni
kwa msingi huu Kanisa liliamua
kupambana na hawa wazushi ambao
pia walionekana kupotosha mafundisho
ya Kanisa. Ndipo tunaona Bikira Maria
anamtokea Mtakatifu Dominico na
kumwambia asali rozari ili kupambana
na mafundisho hayo ya kizushi. Ni Papa
Pio V ambaye mnamo mwaka 1569
alihidhinisha rasmi kusali rozari kwa
kanisa nzima na kuhidhinisha rozari
iwe jinsi tunavyoiona sasa. Katika zile
zama za kati, watawa wamonaki
walizoea kusali zaburi 150, na kwa
upande wa waumini walei ambao kwa
kipindi hicho hawakujua kusoma zaburi
iliwabidi wasali sala ya Baba yetu mara
150 baadala ya zaburi 150 na hizo baba
yetu walizisali kwa kuhesabu punje 150
zilizokuwa zimefungwa kwenye kamba
ndefu ambayo kwa lugha ya kitaalamu
iliitwa “ Corona ” au kwa Kiingereza “
Crown ” kadiri ibada kwa Bikira Maria
ilivyoendelea kushamiri mnamo Karne
ya 12, sala kwa Bikira Maria
ilianzishwa na hivyo kuanza kusali
salamu maria 150 baadala ya baba yetu
150.
Salamu Maria 150 hapo baadaye
zilikuja kugawanywa katika makundi/
mafungu na Mtawa mdominica
aliyeitwa Henry Kalkar ( 1328-1408),
ambapo kila tendo la rozari lilikuwa na
mafungu 50 ya salamu Maria ambapo
pia kila fungu liligusia maisha ya Bikira
Maria na Yesu katika historia ya
wokovu wetu. Zaidi ya hapo, mtawa
mwingine wa mdominican aliyeitwa
Alanus de Rupe aliendelea kugawanya
hiyo historia ya matendo ya wokovu
wetu katika matendo ya furaha ,uchungu,
na utukufu kama tunavyoyaona sasa.
(NB Matendo ya mwanga hayo ni ya
majuzi siyo ya wakati ule). Na
nikuanzia hapo Bikira Maria amepewa
nafasi kubwa katika shirika la watawa
wa Dominican. Hivyo utamaduni wa
kusali rozari umeendelea karne hata
karne, mfano Papa Leo XIII (1878-1903)
aliweka msisitizo mkubwa juu ya ibada
ya rozari kwa Bikira Maria. Kuanzia
September 1, 1883 Baba Mtakatifu Leo
XIII aliandika jumla ya barua za
kichungaji 11 zote zikiwa zinaweka
mkazo juu ya rozari. Hivyo rozari ni
sala inayotokana na maandiko
matakatifu( Biblia). Mafumbo ya rozari
yote yanapatikana katika agano jipya
ambapo ndo tunaona matendo ya Bikira
Maria na Yesu Kristo katika wokovu
wetu.
tunakumbushwa uchungu aliopata
Bikira Maria Katika maisha yake hasa
ule utabiri wa Simeoni kwa Bikira
Maria juu ya mateso na kifo cha
mwanae Yesu, Matendo saba ya furaha
kwa Maria ambapo yaananza na
kupashwa habari kwa Bikira Maria na
Malaika wa Bwana, kupalizwa
mbinguni, na matendo ya huruma ya
Bikira Maria kwa wale ambao
wanaendelea kuteseka hapa duniani.

Mambo ya Msingi Sana Kuhusu Kusali na Kuomba

Rafiki yangu, Omba utafute uso wa Mungu, Aonaye kwa Siri atakujibu kwa wazi.

Mungu ni Mwaminifu Sana hasa kwa wamwombao bila kukoma na kwa matumaini

Mungu yeye anasikia Sala zetu zote na kuzijibu zote.

Mungu hujibu na kutupa kile kilicho muhimu na kizuri kwetu kwa wakati huo.

Ni kama vile Mtoto anapomwomba mzazi wake wembe wa kukata kucha lakini mzazi hampi kwa kuwa anajua utamdhuru.

Vivyo hivyo Mungu hutupa Kile kilicho bora na sio tunachokitaka.

Uwezo wa Mungu ni mkuu na anaweza kutupa chochote tunachoomba.

Lakini kwa Upendo wake usio na mfano anatupa vile vilivyo vizuri kwetu.

Mtumainie Mungu kila wakati.

Rafiki Yangu, Omba Utafute Uso wa Mungu

Rafiki yangu, omba utafute uso wa Mungu, kwa maana yeye aonaye kwa siri atakujibu kwa wazi. Mungu ni mwaminifu sana, hasa kwa wale wanaomwomba bila kukoma na kwa matumaini. Mungu husikia sala zetu zote na kuzijibu kwa hekima na upendo. Tunapomwomba Mungu kwa imani na uvumilivu, anatupa kile kilicho bora kwetu kwa wakati wake mwafaka.

Mungu Anasikia na Kujibu Maombi

Biblia inatufundisha kwamba Mungu husikia na kujibu maombi yetu. Yesu alisema katika Mathayo 6:6:
“Lakini wewe, uombapo, ingia katika chumba chako cha ndani, kisha funga mlango wako, uombe kwa Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujibu kwa dhahiri.” (Mathayo 6:6)

Mungu anapenda tuombe tukiwa na moyo wa unyenyekevu na uaminifu. Sala zetu zinazotoka moyoni humfikia Mungu, na kwa upendo wake mkuu, anatupatia majibu kwa njia ambazo ni bora kwetu.

Mungu Ni Mwaminifu

Mungu ni mwaminifu sana kwa wale wanaomwomba kwa matumaini. Biblia inasema katika 1 Yohana 5:14-15:
“Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kwamba, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Nasi tukijua ya kuwa atusikia katika lolote tuombalo, twaijua kwamba tumevipata vile vitu tulivyomwomba.” (1 Yohana 5:14-15)

Tunapoomba kwa kuzingatia mapenzi ya Mungu, tunakuwa na uhakika kwamba Mungu atasikia na kutujibu.

Mungu Anajibu Kulingana na Hekima Yake

Mungu hujibu maombi yetu kulingana na hekima yake kuu. Wakati mwingine tunapomwomba Mungu vitu fulani, hatupokei majibu tunayotarajia. Hii ni kwa sababu Mungu anajua zaidi kuhusu kile kilicho bora kwetu kuliko tunavyojua sisi wenyewe. Kama vile mzazi anavyomkatalia mtoto wake kitu hatari kwa ajili ya usalama wake, ndivyo Mungu anatupa kile kilicho bora zaidi kwetu. Yesu alisema katika Mathayo 7:9-11:
“Au ni nani miongoni mwenu, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe? Au akimwomba samaki, atampa nyoka? Basi, ikiwa ninyi, mlio wabaya, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba yenu aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa mema wao wamwombao?” (Mathayo 7:9-11)

Mungu, kwa hekima yake isiyo na kipimo, anatupatia kile kilicho bora zaidi kwa maisha yetu. Anajua mahitaji yetu halisi na hutupatia yale yatakayotusaidia kukua kiroho na kufanikisha kusudi lake maishani mwetu.

Uwezo wa Mungu ni Mkuu

Mungu ana uwezo mkuu na anaweza kutupa chochote tunachoomba. Yesu alisema katika Marko 11:24:
“Kwa hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.” (Marko 11:24)

Tunapomwomba Mungu kwa imani, tukiwa na uhakika kwamba atatupatia tunachohitaji, tunaweza kuwa na amani na utulivu tukijua kwamba Mungu anasikia na kujibu maombi yetu.

Mungu Anatupatia Kile Kilicho Bora

Kwa upendo wake usio na mfano, Mungu anatupatia vile vilivyo vizuri kwetu. Warumi 8:28 inasema:
“Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.” (Warumi 8:28)

Mungu anafanya kazi kwa pamoja na sisi ili kutupatia mema. Hata wakati hatuelewi kwa nini maombi yetu hayajajibiwa kama tulivyotaka, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu anafanya kazi kwa ajili yetu, akituandalia mema makubwa zaidi.

Mtumainie Mungu Kila Wakati

Tunapaswa kumtumainia Mungu kila wakati, tukijua kwamba yeye anajua mahitaji yetu na anafanya kazi kwa ajili yetu. Mithali 3:5-6 inasema:
“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.” (Mithali 3:5-6)

Kumtumainia Mungu kwa moyo wetu wote inamaanisha kumwomba, kumtegemea, na kuamini kwamba anafanya kazi kwa ajili yetu kila siku. Mungu ni mwaminifu na anataka tuishi maisha ya furaha na amani, tukijua kwamba anatupatia kila tunachohitaji kwa wakati wake mwafaka.

Rafiki yangu, omba utafute uso wa Mungu, kwa maana yeye aonaye kwa siri atakujibu kwa wazi. Mungu ni mwaminifu sana hasa kwa wale wanaomwomba bila kukoma na kwa matumaini. Mungu husikia sala zetu zote na kuzijibu kwa hekima na upendo. Uwezo wa Mungu ni mkuu na anaweza kutupa chochote tunachoomba. Lakini kwa upendo wake usio na mfano, anatupa kile kilicho bora zaidi kwetu. Mtumainie Mungu kila wakati na utaona mema yake yakitimia katika maisha yako.

Namna ya kutunza kuku na kuwakinga na magonjwa

1. Zingatia chanjo muhimu kwa kuku ili kuzuia magonjwa kama utakavyoshauriwa na mtaalamu wa mifugo.
Chanjo huanza katika wiki ya kwanza (mfano chanjo ya kuzuia sotoka) na inaweza kurudiwa baadaye.

2. Epuka kuweka kuku wengi mahali pamoja.
Ni rahisi magonjwa kuenea kwa haraka kuku wanaporundikana.

3. Kumbuka kutenganisha vifaranga na kuku wakubwa (isipokuwa kutoka kwa mama) kwa sababu vifaranga ni rahisi na wepesi sana kushambuliwa na magonjwa.

4. Hakikisha unaweka mipaka na madaraja ya sehemu za kuku kuzunguka/kucheza.

Shopping Cart
28
    28
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About