Mahitaji
Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
Hamira (yeast kijiko 1 cha chai)
Sukari (sugar 2 vikombe vya chai)
Hiliki (cardamon 1/4 ya kijiko cha chai)
Maji kikombe1 na 1/2
Mafuta
Matayarisho
Changanya unga, hamira, maji na mafuta kijiko 1. Koroga vizuri mpaka upate uji mzito usiokuwa na madoge Baada ya hapo uache uumuke kisha zichome kalmati katika moto wa wastani. Baada ya hapo tia sukari, hiliki na maji 1/2 kikombe katika sufuria na ichemshe uku unakoroga mpaka iwe tayari.(ukitaka kujua kama iko tayari chovya mwiko kisha gusa na vidole utaona iko kama nta au gundi) Baada ya hapo tia kalmati na uzichange pamoja mpaka zikolee kisha zitoe na uziache mpaka zipoe tayari kwa kuliwa.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Mapishi ya Ugali na dagaa
Mapishi ya Chicken Curry
Upishi wa Afya na Vitoweo vya Hewa: Vinywaji vya Kukoroga na Visivyo na Hatia
Vitafunio vya Afya kwa Kutosheleza Hamu Zako
Tofauti kati ya yai la kuku wa kienyeji na la kuku wa kisasa
Jinsi ya kupika Visheti Vya Kastadi Vya Shepu Ya Kombe
Mapishi ya Kabichi
Jinsi ya kuandaa Pilau ya sosi ya soya, nyama na mboga