Siri ya kushinda hasira
Siri kuu ya kuishinda hasira yako ni kusubiri kabla ya kutenda unapokuwa na hasira.
Siri kuu ya kuishinda hasira yako ni kusubiri kabla ya kutenda unapokuwa na hasira.
Tunatakiwa tujenge uhodari na uwezo utakaotusaidia kutumia fursa zilizo wazi mbele yetu.
Katika maisha, kinga kuu ya magonjwa na majanga yote ni kujikatalia au kujinyima.
Amini kuwa unashinda na wewe utashinda. Hata vita wanashinda wale wanaoamini katika ushindi. Kutokujiamini ni sawa na kushindwa tayari.
Huwezi kupata maendeleo kwa kusitasita na kuogopaogopa. Hata kobe anayesonga mbele ni yule anayetoa kichwa chake kwenye gamba/nyumba yake.
Ukiweza kutumia vizuri kipaji au uwezo mdogo ulionao itakufanya uwe bora na mwenye sifa nzuri kuliko yule mwenye uwezo mkubwa.
Kukosa mtu, kitu au jambo fulani kunasababila Moyo kujenga upendo kwenye mtu, kitu au jambo ulilolikosa.
Uwe mzuri kwenye kufanya kama ulivyo kwenye kufikiri. Matendo yako yafanane na maneno na maneno na matendo.
Matendo ya mtu ni tafsiri kuu ya mawazo yake.
Kila mtu ni mrithi wake yeye mwenyewe. Mafanikio yako ya baadae ni urithi wako ulioutengeneza hapo awali. Utajiri wako wa sasa unatokana na uliyoyawekeza miaka ya nyuma na utajiri wako ujao ni yale unayoyawekeza sasa.
Huwezi kuona thamani ya kitu ambacho hujakigharamia. Faida haina thamani kama haijagharamiwa.
Usimpe mtu ushauri ambao unahisi ataukubali sana, mpe mtu ushauri wenye manufaa kwake japo ni mgumu kuukubali.
Tamaa ni tabia ya kiasili ya kila mtu, tofauti ya mtu na mtu ni namna ya kukabili tamaa.
Tunatakiwa tujithaminishe wenyewe kwa yale tunayoona tunauwezo wa kuyafanya japokuwa watu wengine wanatuthamanisha kwa yale wanayoyaona tumeshayafanya
Kwenye dunia hii vitu haviwezi kusimama kama havijasimamishwa.
Changamoto na ugumu wa jambo upo kwa wale wanaolifanya. Huwezi kukaa na kutazama jambo bila kulifanya na kisha kujua changamoto zake.
Hakuna uwezo bila fursa. Huwezi kusema unauwezo wa kitu kama hauna fursa ya kukifanya.
Uwezo wa kuwa makini katika jambo bila kuyumbishwa na kitu chochote ni ishara kuu ya mtu mwenye akili na mwenye mafanikio.
Kuacha kitu chochote kabisa moja kwa moja ni rahisi sana kuliko kufanya kitu hicho kidogokidogo kwa wastani. Usijidanganye utafanya kidogo au utaacha kidogo. Acha Kabisa na usifanye tena.
Unapokosa kitu ukipendacho kwa muda mfupi kinapungua thamani, ukikikosa kwa muda mrefu thamani yake yote hupotea.
Recent Comments