Chema na kizuri
Sio kila kizuri ni chema, lakini kila chema ni kizuri. Uzuri wa chema ni wema wake.
Sio kila kizuri ni chema, lakini kila chema ni kizuri. Uzuri wa chema ni wema wake.
Kitu chochote kinapofanywa vizuri mwanzoni ni sawa na kimefanywa nusu tayari.
Tunatakiwa tujenge uhodari na uwezo utakaotusaidia kutumia fursa zilizo wazi mbele yetu.
Uwe mzuri kwenye kufanya kama ulivyo kwenye kufikiri. Matendo yako yafanane na maneno na maneno na matendo.
Kushindwa jambo sio Makosa, bali kuacha kufanya jambo kabisa ni makosa makubwa.
Siri kuu ya kuishinda hasira yako ni kusubiri kabla ya kutenda unapokuwa na hasira.
Jarbu Mambo mengi kadiri uwezavyo kwani kwa kujaribu ndivyo tunajua tunaweza au hatuwezi. Kamwe usiseme huwezi jambo kabla ya kujaribu.
Amini kuwa unashinda na wewe utashinda. Hata vita wanashinda wale wanaoamini katika ushindi. Kutokujiamini ni sawa na kushindwa tayari.
Ukitaka kufanya biashara kwa ufanisi; wakati wa kununua nunua ukiwa na mtazamo wa muuzaji kwa kufikiri kama wewe ungekua ndio unauza ungeuzaje, na Wakati wa kuuza uza ukiwa na mtazamo wa mnunuzi kwa kufikiri kama ungekua wewe ndiye mnunuzi ungenunuaje.
Uwezo wa kuwa makini katika jambo bila kuyumbishwa na kitu chochote ni ishara kuu ya mtu mwenye akili na mwenye mafanikio.
Hakuna uwezo bila fursa. Huwezi kusema unauwezo wa kitu kama hauna fursa ya kukifanya.
Changamoto na ugumu wa jambo upo kwa wale wanaolifanya. Huwezi kukaa na kutazama jambo bila kulifanya na kisha kujua changamoto zake.
Kujaribu kufanya jambo kubwa la kipekee ni kushinda hata kama halijafanikiwa.
Tunatakiwa tujithaminishe wenyewe kwa yale tunayoona tunauwezo wa kuyafanya japokuwa watu wengine wanatuthamanisha kwa yale wanayoyaona tumeshayafanya
Ukiweza kutumia vizuri kipaji au uwezo mdogo ulionao itakufanya uwe bora na mwenye sifa nzuri kuliko yule mwenye uwezo mkubwa.
Maisha ya ujana ni kufanya mema au mabaya, kushinda au kushindwa. Uzee ni sherehe au majuto ya ujana.
Huwezi kupata maendeleo kwa kusitasita na kuogopaogopa. Hata kobe anayesonga mbele ni yule anayetoa kichwa chake kwenye gamba/nyumba yake.
UMAKINI ni siri kuu ambayo wenye akili wote, wasomi na wanasayansi wanaitegemea.
Unapokosa kitu ukipendacho kwa muda mfupi kinapungua thamani, ukikikosa kwa muda mrefu thamani yake yote hupotea.
Huwezi kuona thamani ya kitu ambacho hujakigharamia. Faida haina thamani kama haijagharamiwa.
Recent Comments