Mke Na Mme Kusaidiana
Inapendeza kweli mke na Mume kusaidiana. Kusaidiana ni Kushirikiana lakini kugawana majukumu ni kupeana mzigo
Inapendeza kweli mke na Mume kusaidiana. Kusaidiana ni Kushirikiana lakini kugawana majukumu ni kupeana mzigo
Jarbu Mambo mengi kadiri uwezavyo kwani kwa kujaribu ndivyo tunajua tunaweza au hatuwezi. Kamwe usiseme huwezi jambo kabla ya kujaribu.
Biashara ya maisha ni kusonga mbele tuu. Maisha hayarudi nyuma wala hayafai kurudisha nyuma. Maisha yanasonga mbele.
Tamaa ni tabia ya kiasili ya kila mtu, tofauti ya mtu na mtu ni namna ya kukabili tamaa.
Changamoto na ugumu wa jambo upo kwa wale wanaolifanya. Huwezi kukaa na kutazama jambo bila kulifanya na kisha kujua changamoto zake.
Tunatakiwa tujithaminishe wenyewe kwa yale tunayoona tunauwezo wa kuyafanya japokuwa watu wengine wanatuthamanisha kwa yale wanayoyaona tumeshayafanya
Matendo ya mtu ni tafsiri kuu ya mawazo yake.
Ukiona unaweza ukakaa siku nzima bila hata kuwa na wazo moja jipya ujue umezeeka akili tayari na kesho unaweza ukawa haupo
Hakuna uwezo bila fursa. Huwezi kusema unauwezo wa kitu kama hauna fursa ya kukifanya.
Sio kila kizuri ni chema, lakini kila chema ni kizuri. Uzuri wa chema ni wema wake.
Siri kuu ya kuishinda hasira yako ni kusubiri kabla ya kutenda unapokuwa na hasira.
Kuacha kitu chochote kabisa moja kwa moja ni rahisi sana kuliko kufanya kitu hicho kidogokidogo kwa wastani. Usijidanganye utafanya kidogo au utaacha kidogo. Acha Kabisa na usifanye tena.
Usimpe mtu ushauri ambao unahisi ataukubali sana, mpe mtu ushauri wenye manufaa kwake japo ni mgumu kuukubali.
Uwezo wa kuwa makini katika jambo bila kuyumbishwa na kitu chochote ni ishara kuu ya mtu mwenye akili na mwenye mafanikio.
Kukosa mtu, kitu au jambo fulani kunasababila Moyo kujenga upendo kwenye mtu, kitu au jambo ulilolikosa.
Unapokosa kitu ukipendacho kwa muda mfupi kinapungua thamani, ukikikosa kwa muda mrefu thamani yake yote hupotea.
Maisha ya ujana ni kufanya mema au mabaya, kushinda au kushindwa. Uzee ni sherehe au majuto ya ujana.
Kwenye dunia hii vitu haviwezi kusimama kama havijasimamishwa.
Huwezi kuona thamani ya kitu ambacho hujakigharamia. Faida haina thamani kama haijagharamiwa.
Kujaribu kufanya jambo kubwa la kipekee ni kushinda hata kama halijafanikiwa.
Recent Comments