Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya

Madhara ya kula yai bichi

Yai bichi linaweza kuwa na vijidudu viitwavyo kwa kitaalamu โ€œSALMONELLAโ€ vinavyoweza kusababisha tumbo kuuma, kichefuchefu na pia kuharisha.
Vijidudu ya โ€œSalmonellaโ€ vinaweza kusababisha madhara makubwa kwa watoto, wazee na wale wenye hali dhaifu ya kimwili kama wagonjwa wa UKIMWI.

Pia yai bichi lililowazi linaweza kuwa zalio zuri la vimelea vya maradhi mbalimbali. Inashauriwa kupika yai mpaka liive kabisa, na kuhakikisha kwamba hakuna ute unaoteleza.

Kama ni yai la kuchemsha, lichemshwe kwa dakika kumi zaidi baada ya maji kuchemka. Pia ni muhimu kuhakikisha kwamba vyombo vilivyotumika k u k o rogea yai bichi vinaoshwa kwa maji na sabuni kabla ya kuvitumia tena kwa matumizi mengine ili kuepuka maradhi.

Mapishi ya choroko

Mahitaji

Choroko kikombe 1 na nusu
Nazi kopo 1
Kitunguu kikubwa 1
Nyanya 1/2 kopo
Swaum 1 kijiko cha chai
Curry powder 1 kijiko cha chai
Chumvi kiasi
Olive oil
Pilipili nzima

Matayarisho

Loweka choroko usiku mzima kisha zichemshe mpaka ziive na ziweke pembeni. Baada ya hapo saga pamoja nyanya, kitunguu, na swaum kisha vipike mpaka maji yote, baada ya hapo tia mafuta na curry powder, pika mpaka nyanya zitoe mafuta kisha tia choroko,tui la nazi, maji nusu kikombe,pilipili na chumvi, kisha koroga vizuri na uache ichemke. Pika mpaka tui la nazi litakapoiva na rojo ibakie kidogo sana, kisha ipua na mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa. Mi huwa napenda kuila na wali ila hata na ugali au chapati inaenda pia.

Jinsi ya kupika Biryani ya mbogamboga

Biriani ni miongoni mwa vyakula ambavyo ni nadra sana kupikwa katika familia nyingi tofauti na vyakula vingine. Inawezekana ni kutokana na watu wengi kutoelewa namna ya kuoika chakula hiki kutokana na kuhitaji viungo vingi ambavyo huwapa usumbufu wapishi.
Kuna aina mbalimbali za upishi wa biriani ambapo mara nyingi hutofautiana kutokana na viungo vinavyotumika katika upishi.
Biriani la mbogamboga ni miongoni mwa aina hizo za upishi. Chakula hiki kinaweza kuliwa na kila mtu hususan wale wasiotumia nyama wala samaki.

Mahitaji:

ยฝ kg mchele wa basmati
Kitunguu maji kikubwa 1
Nyanya 1 kubwa
Karoti 1 kubwa
Njegere robo kikombe
Kiazi ulaya 1 kikubwa
Tangawizi za kusaga kijiko 1
Kitunguu swaumu cha kusaga kijiko 1
Karafuu kijiko 1
Majani ya kotimili fungu 1
Maziwa ya mtingi ยผ kikombe
Chumvi na pilipili kiasi
Unga wa dhani kijiko 1 cha mezani
Juisi ya limao kijiko 1 cha mezani
Mafua ยผ lita

Maandalizi:

Chemsha mchele na kisha weka pembeni
Osha mbogamboga zote isipokuwa vitunguu na nyanya
Changanya mtindi na tangawizi pamoja na kitunguu swaumu viache vikae kwa muda wa saa moja
Chukua sufuria weka mafuta na kisha kaanga vitunguu maji, weka nyanya, chumvi, kotimili na limao halafu weka karafuu na kanga hadi vichanganyike vizuri
Miminia mchanganyiko wa mtindi na baadaye weka pilipili na baadaye weka unga wa dhania
Chukua mchele uliochemshwa changanya na mchanganyiko huo
Palia moto juu ya chakula chako na acha kwa muda wa dakika 30
Baada ya hapo chakula chako cha biriani kitakuwa tayari kwa kuliwa

Mapishi ya Wali Wa Karoti Na Kuku Wa Kukaanga

Vipimo Vya Wali

Mchele wa Basmati/Pishori – 1 kilo moja

Vitunguu maji – 3

Karoti – 2

Siagi – 3 vijiko vya supu

Kidonge cha supu (stock) – 1 kimoja

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

ร“sha mchele uroweke kama saa moja au mbili
Katakata vitunguu vipande vidogodogo (chopped) weka kando.
Kwaruza karoti (grate) weka kando.
Tia siagi katika sufuria ya kupikia wali, weka katika moto iyayuke
Kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi kiasi tu.
Tia maji kiasi ya kupikia wali, changanya na kidonge cha supu.
Yakichemka tia mchele, koroga, funika uweke moto mdogo mdogo.
Kabla ya maji kukauka tia karoti changanya wali kisha funika uive kama unavyopika pilau.

Vipimo Vya Kuku Wa Kukaanga

Kuku alokatwakatwa – 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa – 2 vijiko vya supu

Bizari ya mchanganyiko/garam masala – kijiko cha supu

Mtindi/Yoghurt – 1 kijiko cha supu

Ndimu – 1

Chumvi – kiasi

Mafuta ya kukaangia – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Ukishamuosha kuku, mchuje atoke maji yote.
Changanya viungo vyote katika kibakuli kidogo.
Changanya pamoja na kuku kisha acha akolee viungo (marinate) kwa muda wa masaa mawili takriban.
Weka mafuta katika karai na kaanga kuku, akiwiva yu tayari kuliwa na wali.

Mapishi ya Pilau Ya Adesi Za Brown Karoti Na Mchicha Kwa Samaki Wa Salmon

Vipimo

Mchele vikombe 3

Karoti 1 ikune (grate)

Mchicha katakata kiasi

Adesi za brown

Kitunguu katakata (chopped)

Supu ya kitoweo chochote upendayo au vidonge vya supu 2

Garama masala (bizari mchanganyiko) kijiko 1 cha kulia

Samli ยผ kikombe

Chumvi kiasi

Vipimo Vya Samaki Wa Salmon

Samaki wa Salmon vipande 4 vikubwa

Tangawizi mbichi ilosagwa kijiko 1 cha kulia

Thomu (garlic/saumu) kijiko 1 cha kulia

Chumvi kiasi

Bizari ya mchuzi kijiko 1 cha kulia

Ndimu 1 kamua

Nyanya 2 kata slice kubwa kubwa

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Samaki wa Salmon

Changanya viungo vyote upake katika samaki.
Weka katika treya na panga slice za nyanya juu yake.
Oka (grill/choma) katika oven umgeuze samaki upande wa pili.
Akiwa tayari epua.

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali

Roweka mchele kiasi kutegemea aina ya mchele. Tumia basmati (pishori)
Roweka adesi kisha zichemshe katika maji ya kiasi. Chuja maji adesi na maji yatakayobakia tumia katika kupikia pilau hii.
Kaanga vitunguu katika samli iliyoshika moto kwenye sufuria ya kupikia.
Vikianza kugeuka rangi tia karoti, mchicha, adesi, bizari mchanganyiko kisha kaanga kidogo.
Tia mchele ukaange kidogo kisha tia supu au maji pamoja na kidonge cha supu.
Tia chumvi ukoroge funika upike kama pilau.
Epua upakue katika sahani utolee kwa samaki wa salmon

Jinsi ya kupika Wali wa hoho

Wali wa hoho ni chakula maalum kinachotumika katika hafla au sherehe. Ni chakula chenye ladha nzuri na kina muonekano wa kuvutia kinapokuwa mezani tayari kwa kuliwa.

Mara nyingi huandaliwa kama zawadi katika harusi hususan kwa watu wa pwani. Kwa kuwa zawadi hiyo au maarufu kama kombe huwa kuna vyakula vingi, ikiwamo chakula hiki ambacho hufanya kombe kuwa na muonekano wa kupendeza.

Mbali na kuliwa kama kombe chakula hiki kinaweza kuandaliwa kama mlo wa usiku.

Mahitaji:

โ€ข Mchele ยฝ kg
โ€ข Nyanya 3
โ€ข Mafuta ya kupika ยผ kikombe cha chai
โ€ข Chumvi kiasi
โ€ข Kitunguu swaumu kilichosagwa kijiko 1 cha mezani
โ€ข Kitunguu maji kilichosagwa kijiko 1 cha mezani
โ€ข Hoho 4
โ€ข Nyama ya kusaga ยผ
โ€ข Tangawizi kijiko 1 cha chakula
โ€ข Limao au ndimu kipande

Maadalizi:

โ€ข Chukua mchele uoshe vizuri kasha chuja maji
โ€ข Chukua nyama ya kusaga na kamulia ndimu, weka chumvi na tangawizi, changanya vizuri na weka jikoni.iache ichemke hadi ikauke maji yote.
โ€ข Chukua maji na kiasi cha robo tatu lita chemsha na weka pembeni
โ€ข Chukua sufuria kavu yenye uwezo wa kupika kiasi cha kilo moja
โ€ข Weka mafuta ya kupika kiasi cha vijiko vitatu na acha yapate moto
โ€ข Weka vitunguu maji, menya nyanya na katakata halafu weeka katika sufuria hiyo.
โ€ข Weka chumvi na kanga hadi vilainike kabisa
โ€ข Baada ya kuiva weka vitunguu swaumu na baadaye mchele
โ€ข Koroga hadi uchanganyike na weka nyama. Endelea kukoroga, baada ya hapo weka maji kiasi cha kuivisha mchele huo. Acha vichemke hadi vikaukie.
โ€ข Palia mkaa juu yake au kama unatumia jiko la gesi au umeme weka kwenye oven hadi maji yakauke kabisa.
โ€ข Baada ya hapo chukua hoho na kasha kata upande wa juu kama vifuniko. Kasha ondoa matunda ya ndani yake. Funika na kasha zipange kwenye sufuria yenye maji na chumvi na mafuta kidogo kiasi cha kijiko kimoja. Chemsha jikoni hadi ziive.
โ€ข Baada ya kuiva, chukua hoho zako na kasha chota wali kw akutumia kijiko kasha jaza katika kila hoho na weka kwenye sahani tayari kwa kuliwa.
โ€ข Unaweza kupamba na salad ukipenda.

Mapishi Bora kwa Familia Yote Kupenda

Mapishi Bora kwa Familia Yote Kupenda ๐Ÿฝ๏ธ

Karibu tena kwenye makala ya AckySHINE ambapo leo tutajadili kuhusu mapishi bora ambayo yatapendwa na familia nzima. Tunafahamu kuwa kila familia ina ladha tofauti tofauti linapokuja suala la chakula, lakini tuko hapa kukusaidia kuandaa chakula ambacho kila mtu atakipenda! ๐Ÿฅ˜

  1. Kuku wa Kuchoma ๐Ÿ—
    Kwa wale wapenzi wa nyama ya kuku, hakuna kitu kitakachowafurahisha zaidi kuliko kuku wa kuchoma. Unaweza kuandaa kuku huu kwa kutumia viungo kama vile tangawizi, kitunguu saumu, pilipili manga, na limau kwa ladha ya ziada. Hii ni njia nzuri ya kuhakikisha kuwa wewe na familia yako mnafurahiya chakula pamoja! ๐Ÿ‹

  2. Wali wa Maharage ๐Ÿš
    Wali wa maharage ni chakula ambacho hakina gharama nyingi na ni rahisi kuandaa. Unaweza kutumia mchele wa kawaida na maharage yoyote unayopenda kuandaa wali huu mzuri. Unaweza kuongeza viungo kama vile iliki, bizari na kitunguu saumu ili kuongeza ladha ya wali wako. Hakuna mtu atakayeweza kusimama kwa chakula hiki kitamu! ๐Ÿ›

  3. Chapati za Nyama ๐ŸŒฏ
    Chapati za nyama ni chakula kingine ambacho kitapendwa na familia yote. Unaweza kuandaa chapati hizi kwa kutumia nyama iliyosagwa, vitunguu, pilipili na viungo vingine vya kuchagua. Chapati hizi zinaweza kuliwa pekee yake au kwa kuiandaa na kachumbari na mchuzi wa nyanya. Utapata thawabu nyingi kutoka kwa familia yako! ๐ŸŒฎ

  4. Samaki wa Kukaanga ๐ŸŸ
    Ikiwa familia yako inapenda samaki, basi samaki wa kukaanga ni chaguo bora kwenu. Unaweza kutumia samaki kama vile dagaa, kambale au samaki wengine unaopenda. Tumia unga wa ngano kuwakaanga samaki wako na ongeza viungo kama vile pilipili na chumvi. Hakikisha samaki wako ni mzuri na laini ndani kabisa. Ni uhakika kuwa familia yako italamba vinywa vyao! ๐Ÿ 

  5. Pilau ya Nyama ๐Ÿฒ
    Pilau ya nyama ni chakula kingine kizuri ambacho familia yako itapenda. Unaweza kuandaa pilau hii kwa kutumia nyama iliyokatwa vipande vidogo, mchele, vitunguu, pilipili na viungo vingine kama iliki, mdalasini na mchuzi wa nyanya. Pilau hii itajaza nyumba nzima na harufu nzuri na kumfurahisha kila mtu! ๐Ÿฝ๏ธ

  6. Kachumbari ya Matango na Nyanya ๐Ÿฅ—
    Kachumbari ya matango na nyanya ni sahani ya upande ambayo inawezesha kuongeza ladha kwa chakula chako. Unaweza kukata matango na nyanya vipande vidogo, kisha kuongeza pilipili, kitunguu saumu, chumvi, na limau. Kachumbari hii italeta uwiano na ladha nzuri kwa chakula chako na kufurahishwa na familia yote! ๐Ÿฅ’

  7. Mkate wa Tandoori ๐Ÿฅ–
    Mkate wa tandoori ni sahani inayopendwa sana na watu wengi. Unaweza kutumia unga wa ngano, chachu, maziwa, sukari na chumvi kuandaa mkate huu. Unaweza kuuandaa na mboga za kupenda au nyama na kufurahia kama kitafunio au kwa mlo wa jioni. Hakikisha kuwa unatumia moto wa kutosha kupata mkate uliopendeza! ๐Ÿฅ

  8. Tambi za Nyama ๐Ÿ
    Tambi za nyama ni chakula kingine ambacho kina ladha nzuri na rahisi kuandaa. Unaweza kutumia tambi za aina yoyote, nyama iliyokatwa vipande vidogo, vitunguu, pilipili, na viungo vingine kama iliki, bizari na chumvi. Pika tambi zako kwa muda mfupi ili ziwe laini na uchanganyike na nyama kwa ladha kamili. Hakuna mtu atakayeweza kusimama kwa tambi hizi! ๐Ÿœ

  9. Kuku wa Kienyeji ๐Ÿ”
    Kuku wa kienyeji ni chaguo bora kwa wale wanaopenda ladha ya kiasili na afya. Unaweza kuandaa kuku huu kwa kutumia viungo rahisi kama vile vitunguu, pilipili, bizari, chumvi na tangawizi. Pika kuku wako kwa muda mrefu ili iwe laini na inayeyuka mdomoni. Ukiwa na kuku wa kienyeji, familia yako itafurahia chakula chako kwa uhakika! ๐Ÿ—

  10. Keki ya Chokoleti ๐Ÿฐ
    Keki ya chokoleti ni chakula kizuri cha tamu ambacho kitapendwa na watoto na watu wazima sawa. Unaweza kutumia unga wa ngano, sukari, maziwa, chokoleti na viungo vingine kuandaa keki hii. Unaweza kuiongezea pia glasi ya chokoleti au cream ya chokoleti kwa ladha zaidi. Keki hii itakuwa hit kwenye chakula cha jioni cha familia yako! ๐Ÿซ

Hapa kuna mapishi kadhaa ambayo naamini yatakuwa ya kupendeza kwa familia yako. Njoo na jaribu mapishi haya na angalia jinsi familia yako itakavyofurahia! Je, una mapishi yako bora yanayopendwa na familia yote? Tungependa kusikia kutoka kwako! ๐Ÿฅ˜

Opinion: Je, ungependa kujua mapishi mengine ambayo familia yote itapenda?

Jinsi ya kuandaa Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi

Mahitaji

Nyama Ya Mbuzi – 1 Kilo

Mchele – 4 Magi

Vitunguu – 3

Nyanya – 2

Nyanya kopo – 3 vijiko vya chai

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa – 2 vijiko vya supu

Pilipili mbichi iliyosagwa – 1 kijiko cha supu

Garam Masala (mchanganyiko wa bizari) – 2 vijiko vya supu

Hiliki – 1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Mafuta – ยฝ kikombe

Zaafarani au rangi za biriani za kijani na manjano/orenji

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Sosi Ya Nyama

Changanya nyama na thomu, pilipili, chumvi na nusu ya garam masala. Tia katika treya ya oveni uipike nyama (Bake) hadi iwive. Au iwivishe kwa kuichemsha.
Katika kisufuria kingine, tia mafuta (bakisha kidogo ya wali) kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi, kisha tia nyanya, nyanya kopo, bizari zote nyingine zilizobakia.

Namna Ya Kupika Wali

Mchele – 4 magi

Mdalasini – 1 kijiti

Hiliki – 3 chembe

Kidonge cha supu – 1

Chumvi

Osha na roweka mchele wa basmati.
Tia maji katika sufuria uweke jikoni. Tia kidonge cha supu, mdalasini, hiliki na chumvi .
Yakichemka maji tia mchele, funika upike hadi nusu kiini kisha uchuje kwa kumwaga maji.
Tia mafuta kidogo katika mchele na zaafarani iliyorowekwa au rangi za biriani kisha rudisha mchele katika sufuria ufunike na upike hadi uwive.
Pakua wali katika sahani kisha mwagia sosi ya nyama juu yake, pambia kwa kukatika nyanya, pilipili mboga na figili mwitu (Celery) au mboga yoyote upendayo.

Jinsi ya kupika Biskuti Za Kopa Za Kunyunyuziwa Sukari Za Rangi

MAHITAJI

Unga vikombe 2 ยผ

Siagi 250g

Sukari kukaribia kikombe ยฝ (au takriban vijiko 10 vya kulia)

Baking powder ยฝ kijiko cha chai

Ute wa yai 1

Vanilla 1 kijiko cha chai

Sukari Ya Kunyunyizia na rangi mbali mbali.

MATAYARISHO

Kagawa sukari katika vibakuli utie rangi mbali mbali uweke kando.
Changanya siagi na sukari katika mashine ya kusagia keki upige mpaka ilainike iwe nyororo.
Tia ute wa yai vanilla uhanganye vizuri.
Tia unga na baking powder kidogo kidogo uchanganye upate donge.
Sukuma donge ukate kwa kibati cha shepu ya kopa.
Pakaza siagi katika treya ya kupikia kwenye oveni upange biskuti
Nyunyizia sukari za rangi rangi kisha pika katika oven moto mdogo wa baina 180 โ€“ 190 deg F kwa takriban robo saa.
Epua zikiwa tayari.

Upishi na Karanga na Mbegu: Vyakula vya Virutubishi

Upishi wa vyakula vya virutubishi kama vile karanga na mbegu ni muhimu sana kwa afya yetu. Kwa bahati nzuri, vyakula hivi vina ladha tamu na virutubishi vingi, ambavyo vinaweza kuboresha afya yetu kwa njia nyingi. Kwa hiyo, leo, katika makala hii, nataka kuzungumzia faida za upishi wa vyakula hivi na jinsi unavyoweza kuyatayarisha ili kuwa na chakula bora zaidi.

  1. Mbegu kama vile alizeti, ufuta, na maboga ni matajiri katika asidi ya mafuta muhimu, ambayo ni muhimu kwa afya ya moyo na mishipa ya damu.๐ŸŒป๐ŸŒฐ
  2. Karanga nazo zina protini nyingi, mafuta yenye afya, na nyuzinyuzi, ambazo zinaweza kusaidia kudhibiti kisukari na kukidhi mahitaji ya protini ya mwili.๐Ÿฅœ๐Ÿ’ช
  3. Vyakula hivi vinaweza kuongezwa kwenye sahani za mboga, kachumbari au hata katika smoothies za asubuhi ili kuongeza ladha na virutubishi.๐Ÿ›๐Ÿฅ—๐Ÿฅค
  4. Kwa upande mwingine, unaweza pia kutumia karanga na mbegu kama vitafunio vya afya kati ya milo yako.๐Ÿฟ๐ŸŒฐ
  5. Kwa kuwa karanga na mbegu hazina cholesterol, zinaweza kuwa chaguo bora badala ya vitafunio vingine vyenye mafuta mabaya.๐Ÿšซ๐Ÿ”
  6. Upishi wa vyakula hivi kunaweza kufanywa kwa njia nyingi tofauti. Kwa mfano, unaweza kuchoma karanga kwenye sufuria kavu au kuzipika kwa maji chumvi.๐ŸŒฐ๐Ÿ”ฅ
  7. Kwa mbegu, unaweza kuzikaanga kwenye mafuta kidogo au kuzitumia kama kiungo katika mikate, keki, au saladi.๐Ÿฅ–๐Ÿฅ—
  8. Kumbuka tu kuwa, ili kuhakikisha unapata virutubishi vyote kutoka kwa vyakula hivi, ni muhimu kula kiasi cha kutosha na kupunguza matumizi ya viungo vingine hatari kama vile mafuta ya ziada na sukari.๐Ÿšซ๐Ÿฉ๐ŸŸ
  9. Vyakula vya virutubishi kama vile karanga na mbegu vinafaa kwa watu wa kila umri na wanaweza kusaidia kuboresha afya ya watoto, vijana, watu wazima na wazee.๐Ÿ‘ถ๐Ÿ‘ต
  10. Kwa mfano, watoto wanaweza kula mlo ulio na karanga na mbegu kwa kutengeneza sandwich ya karanga au kuongeza mbegu kwenye tambi au supu.๐Ÿฅช๐Ÿœ
  11. Watu wazima wanaweza kujaribu kuchanganya karanga na mbegu katika sahani za mboga au kwenye saladi ili kuongeza ladha na virutubishi.๐Ÿฅ™๐Ÿฅ—
  12. Na kwa watu wazee, vyakula hivi vinaweza kusaidia kuboresha afya ya akili na kusaidia kuzuia magonjwa ya kuzeeka kama vile ugonjwa wa Alzheimer’s.๐Ÿง ๐Ÿ’ก
  13. Karanga na mbegu pia zinaweza kuwa chaguo bora kwa watu ambao wanahitaji kupata nguvu zaidi, kama vile wanariadha au watu wanaofanya kazi ngumu kimwili.๐Ÿ’ช๐Ÿƒโ€โ™€๏ธ
  14. Kwa kuwa karanga na mbegu zina kiwango cha juu cha kalori, ni muhimu kuzingatia kiasi unachokula ili kuepuka kuongeza uzito kupita kiasi.โš–๏ธ๐Ÿ“‰
  15. Kwa hiyo, kwa kumalizia, nataka kukuhimiza kuongeza vyakula vya virutubishi kama vile karanga na mbegu katika lishe yako ya kila siku. Chakula chako kitakuwa si tu kitamu zaidi, lakini pia kitajaa virutubishi muhimu kwa afya yako. Kumbuka tu kula kwa kiasi na kuzingatia lishe yenye usawa.๐ŸŒฐ๐Ÿฝ๏ธ

Kwa maoni yako, je, wewe hula karanga na mbegu mara ngapi kwa wiki? Je, unapenda kuzipika vipi? Ningependa kusikia kutoka kwako! ๐ŸŒฐ๐Ÿฝ๏ธ๐Ÿค”

Jinsi ya kupika vitumbua inavyotakiwa

Mahitaji

Unga wa mchele ( Vikombe 2 vikubwa)
Sukari (Nusu ya kikombe kikubwa)
Hamira ( Nusu ya kijiko cha chai)
Hiliki (Nusu ya kijiko cha chai)
Tui la nazi ( Kikombe kimoja kikubwa)
Unga wa ngano (Vijiko viwili vya chakula)
Mafuta ya kuchomea (Vegetable oil)

Matayarisho

Unachanga unga, sukari, hamira, hiliki, unga wa ngano na tui la nazi pamoja katika bakuli la plastiki. Kisha unaukoroga mpaka mchanganyiko unakuwa kama uji mzito. Kava bakuli lililokuwa na mchanganyiko kisha hifadhi katika sehemu yenye joto kwa muda wa masaa matatu.

Jinsi ya kupika

Weka chuma cha kuchomea vitumbua katika moto wa wastani, kisha weka mafuta kwenye chuma cha kuchomea ( Kijiko kimoja cha chai) mafuta yakisha pata moto tia uji wako (upawa mmoja) katika kila shimo la chuma cha kuchomea. Acha mpaka kitumbua kikauke kisha geuza na tia mafuta. Acha upande wa pili wa kitumbua mpaka uwe rangi ya kahawia na hapo kitumbua kitakuwa kimeiva utakitoa. Rudia hatua hizo kwa vitumbua vyote vilivyobaki.

Mapishi ya Biskuti Za Mayai

VIAMBAUPISHI

Unga 3 Vikombe

Sukari ya unga (icing sugar) 1 Kikombe

Siagi 250 gm

Mayai 3

Vanilla 2 Vijiko vya chai

Baking powder 1 Kijiko cha chai

JINSI YA KUPIKA

Koroga siagi na sukari katika mashine ya keki (cake mixer) mpaka iwe laini (creamy).
Tia mayai na vanilla koroga mpaka mchanganyiko uwe laini.
Tia unga na baking powder changanya na mwiko.
Tengeneza round upange kwenye tray utie nukta ya rangi.
Nyunyuzia sukari juu ya hizo round ulizotengeneza kabla huja choma.
Pika (bake) katika oven moto wa 350ยฐF kama muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama.

Mapishi ya wali wa hoho nyekundu

Mahitaji

Pilipili hoho (Red pepper 3)
Cougette 1
Kitunguu (onion 1)
Uyoga (mashroom 1 kikombe cha chai)
Carrot 1
Nyanya (fresh tomato 1)
Nyanya ya kopo iliyosagwa (tomato paste 3 vijiko vya chai)
Giligilani (fresh coriander)
Binzari manjano (Turmaric 1/2 ya kijiko cha chai)
Curry powder 1/2 ya kijiko cha chai
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)

Matayarisho

Kata hoho kati na utoe moyo wake kisha ziweke pembeni, Kisha katakata cougette, kitunguu, uyoga, carrot, nyanya katika vipande vidogo vidogo, Weka sufuria jikoni na uanze kupika uyoga kwa muda wa dakika 5, kisha weka curry powder, turmaric na chumvi na kaanga kidogo kisha weka vegetable zilizobakia pamoja na nyanya ya kusaga pamoja na giligilani. Zikaange kwa muda wa dakika 5 kisha zitie kwenye hoho na kisha uzibake kwa muda wa dakika 20 na hapo zitakuwa tayari kuseviwa na wali.
Wali: angalia katika recipe zilizopita

Mapishi ya Mitai

VIAMBAUPISHI

Unga wa ngano – magi 2 (vikombe vikubwa)

Hamira kijiko 1 cha chai

Sukari Vijiko 2 vya supu

Maziwa ยพ Magi

Siagi Vijiko 2 vya supu

Mafuta ya kukaangia kiasi

VIAMBAUPISHI:SHIRA

Sukari ยพ Kikombe

Maji ยพ Kikombe

Illiki ya unga kiasi

Zafarani kiasi

JINSI YA KUPIKA

Katika bakuli, changanya vipimo vyote pamoja na ukande unga usiwe mgumu wala laini sana uwe kiasi.
Kisha fanya donge moja na iache pahali penye joto mpaka iimuke.
Halafu weka mafuta ya kukaangia kwenye moto.
Sukuma donge hadi liwe duara sio nyembamba sana, kisha katakata kama maandazi.
Mafuta ya kisha pata moto choma mittai hukuunazigeuza hadi ziwive na kugeuka rangi.
Katika sufuria tia vipimo vya shira na iache ichemke isiwe nzito sana.
Mimina mitai kwenye shira na uzipepete, kisha weka kwenye sahani na zitakuwa tayari kwa kuliwa.

Jinsi ya kupika Labania Za Maziwa

Viamba upishi

Maziwa ya unga 2 vikombe

Sukari 3 vikombe

Maji 3 vikombe

Unga wa ngano ยฝ kikombe

Mafuta ยฝ kikombe

Iliki kiasi

Jinsi ya kuandaa na kupika

Paka sinia mafuta kabla ya kupika labania
Katika sufuria chemsha maji na sukari pamoja na iliki mpaka inate vizuri
Kisha mimina mafuta koroga
Halafu mimina unga wa ngano na ukoroge haraka haraka
Kisha tia unga wa maziwa, endelea kukoroga usiwe na madonge mpaka uwe rangi ya browni isiokoleza.
Kisha mimina mchanganyiko kweye sinia uliyoipaka mafuta, iwache ipoe na kata kata upendavo na itakuwa tayari.

Mapishi ya chipsi na samaki wa kuchoma

Mahitaji

Viazi ulaya (baking potato 5 vya wastani)
Parprika 1 kijiko cha chai
Pilipili mtama ilyosagwa (ground black pepper 1 kijiko cha chai
Kitunguu swaum cha unga (garlic powder 1 kijiko cha chai)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)
Marination za samaki (angalia kwenye recipe ya samaki ya nyuma)

Matayarisho

Osha viazi na maganda yake kisha vikaushe na uvikate vipande vya wastani. Kwa kila kiazi toa vipande 6. Kisha vitie kwenye bakuli na utie parpika, pilipili mtama ya unga, kitunguu swaum cha unga, chumvi na mafuta kama vijiko 2 vya chakula. Changanya pamoja na kisha uvibake katika oven kwa muda wa dakika 25. Hakikisha vinakuwa rangi ya brown. Vikisha iva vitoe.
Wamarinate samaki, na uwaoke kisha wasevu na potato wedges tayari kwa kuliwa
(Jinsi ya kupika samaki, angalia katika recipe za nyuma)

Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata

Wali Wa Nazi

Mpunga – 4 vikombe

Tui la nazi – 6 vikombe

Chumvi – Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mchele kisha
Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi.
Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.

Mchuzi Wa Samaki Nguru

Samaki – 4

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi – 2 viijiko vya supu

Kitunguu maji kilokatwakawa – 2 slice ndogo

Nyanya/tungule – 4

Nyanya kopo – 3 vijiko vya supu

Pilipili mbichi – 2

Kotmiri ilokatwakatwa – 3 msongo (bunches)

Bizari ya mchuzi (simba 2) – I kijiko cha chai

Ndimu – 1 kamua

Mafuta – ยผ kikombe

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Katakata samaki mkaange kwa kumtia viungo.
Weka mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu. Vinapogeuka rangi thomu na tangawizi mbichi, nyanya, nyanya kopo, kitunguu na bizari ya mchuzi endelea kukaanga.
Tia maji kiasi na ndimu, pilipili mbichi ilosagwa kisha tia kotmiri.
Mwisho tia nusu ya samaki alokaangwa ukiwa tayari

Bilingani Za Kukaanga Na Viazi

Bilingani – 4 madogodogo

Viazi/mbatata – 3

Nyanya – 3

Majani ya mchuzi/mvuje/curry leaves – kiasi 6-7

Nnyanya kopo – 2 vijiko vya supu

Methi/uwatu ulosagwa – 1 kijiko cha chia

Rai/mustard seeds – 1 kijiko cha supu

Bizari ya manjano/haldi/turmeric – 1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Mafuta ya kukaangia – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

1. Weka mafuta ya kukaangia katika karai

2. Katakakata bilingani vipande vipande vya mraba (cubes) kaanga katika mafuta ya moto hadi yageuke rangi. Eupa weka kando.

3. Katakataka viazi/mbatata vipande vidogodogo vya mraba (cubes) Kaanga hadi viive epua weka kando.

4. Ondosha mafuta yote katika karai bakisha kidogo tu kiasi ya vijiko 2 vya supu.

5. Kaanga rai kisha majani ya mchuzi, na methi/uwatu kisha kaanga nyanya.

6. Tia nyanya ya kopo kisha changanya pamoja bilingani na viazi ikiwa tayari.

Mapishi ya Maini ya ng’ombe

Mahitaji

Maini (Cow liver) 1/4 kilo
Vitunguu (chopped onion) 2
Nyanya (chopped tomato) 1
Kitunguu swaum/tangawizi (ginger /garlic paste) 1 kijiko cha chai
Mafuta ya kupikia
Chumvi
Coriander
Curry powder 1 kijiko cha chai
Limao (lemon) 1/4
Pilipili (scotch bonnet ) 1

Matayarisho

Safisha maini na ukate vipande vidogovidogo na uweke pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu kidogo(visiwe vya brown) kisha tia ginger/ garlic paste,carry powder kaanga kidogo kisha tia nyanya. Kaanga nyanya mpaka zitoe mafuta kisha tia chumvi, pilipili na vimaji kidogo. Acha vichemke kidogo kisha tia maini na uyapike mpaka yaive. Malizia kwa kukamulia limao na kutia coriander kisha ipua na hapo yatakuwa tayari kwa kuliwa.

Namna ya kupika Biskuti Za Kuchoveya Chokoleti

VIAMBAUPISHI

Unga 300gm

Siagi 225gm

Icing Sugar 60gm

Chokoleti iliyokoza (Dark Chocolate) – 225gm

Vanilla โ€“ Vijiko 2 vya chai

Yai -1

Baking Powder ยฝ kijiko cha chai

Njugu za vipande ยฝ kikombe cha chai

Njugu zilizosagwa ยผ kikombe cha chai

JINSI YA KUTAYARISHA

Piga sukari na siagi katika mashine ya keki mpaka iwe laini
Kisha mimina yai na vanilla koroga vizuri
Mwisho mimina unga na baking powder polepole mpaka ichanganyike.
Kata kata umbo (shape) lolote unavyopenda (kama nyota, pembetatu,duara, kopa n.k)
Panga kwenye treya na choma kwa moto wa 350ยฐC , vikibadilika rangi kidogo tu vitoe
Yayusha chokoleti tia kwenye bakuli ndogo.
kisha paka kwa kijiko au chovyea upande mmoja mmoja wa biskuti kisha nyunyizia njugu za kipande na njugu ya unga.
Panga kwenye sahani tiyari kunywewa na chai ya maziwa au kahawa.

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About