Mapishi yetu leo ni kisamvu cha kuchanganya na karanga. Karibu.
Mahitaji
Majani ya kisamvu
Karanga nusu kikombe
kitunguu kimoja
nyanya mbili
karoti moja
mafuta na chumvi kiasi
Matayarisho
1. Osha kisamvu chako vizuri kisha katakata vipande vidogo vidogo
2. Unaweza kutwanga kwa kutumia kinu au kuchemsha kidogo na kisha kusaga kwa kutumia mashine. Ukitumia mashine uwe makini usije ukasaga sana ukaharibu.
3. Kaanga karanga kidogo na kisha zisage ziwe unga unga.
4. Chemsha kisamvu chako hadi kiive.
5. Katakata kitunguu, karoti na na nyanya
6. Anza kuunga kisamvu kwa kukaanga vitunguu, weka karoti na kisha nyanya na vikishaiva weka kisamvu na koroga pamoja kisha weka karanga. Acha vichemke kwa muda na unaweza pia weka na nazi tui la kwanza.
7. Baada ya muda mfupi epua na kitakiwa tayari. Waweza kula kwa ugali, wali, chapati, makande n.k
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Jinsi ya kupika mboga ya majani ya mashona nguo
Jinsi ya kupika Keki Ya Maboga
Mapishi ya Samaki wa kuokwa
Nguvu ya Nafaka Zote: Chaguzi za Upishi Zenye Afya
Jinsi ya Kupika skonzi
Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha
Mapishi ya Tende Ya Kusonga Ya Lozi Na Cornflakes
Mapishi ya Samaki wa kupaka