Upendo na Matamanio ya Mungu kwa Wanadamu
Kama vile Baba anavyotamani mwanae akue katika maadili na aelekee katika njia nyoofu. Ndivyo na Mungu anavyotamani uachane na dhambi na kumfuata yeye.
Kama vile Baba anavyotamani mwanae akue katika maadili na aelekee katika njia nyoofu. Ndivyo na Mungu anavyotamani uachane na dhambi na kumfuata yeye.
Vile unavyomsogelea Mungu ndivyo na yeye anavyokusogelea. Vile unavyomkubali Mungu katika Maisha yako ndivyo na yeye anavyotenda kazi kwako.
Kama yalivyo maisha ya kimwili, maisha ya kiroho pia yanahitaji mipango. Kila siku panga utafanya nini kiroho, mfano unaweza kupanga sala, kusaidia masikini, kuwa mpole au mwema. Vivyo hivyo kila wiki, kila mwezi na kila mwaka mpya panga cha kufanya kiroho naye Mungu atakubariki na kukupangia zaidi. Huwezi kufanikiwa kiroho kama hujui unafanya nini kiroho.
Kama mtu anasali kila siku katika maisha yake hakuna kitu kitakachokuwa kigumu. Sala ni njia ya kujipatia neema za kuendesha maisha yetu. Usiache kusali kila siku hata kama upo katika hali gani.
Sala ni kama chakula cha Roho, Bila sala roho inakufa. Tusali daima ili roho zetu ziwe hai siku zote.
Mungu haangalii matemdo ya mtu ya nje tuu, bali anaangalia ndani kabisa mawazo ya mtu na nia yake. Nia ya mtu ndiyo inayoonyesha mtu alivyo.
Hakuna sala yeyote itolewayo kwa unyenyekevu wa kweli katika imani, matumaini na mapendo inayopita bure mbele ya Mungu. Mungu hamtupi mwenye unyoofu wa moyo.
Kukosa hata mara moja inahesabika ni kukosea mbele ya Mungu. Kwa kuwa kwa Mungu hakuna kusema, ‘Kukosea mara moja sio kosa bali kurudia kosa ndio kosa’. Mbele ya Mungu kila kosa lina uzito wake haijalishi ni kosa la mara ya kwanza.
Uhuru Na Amani Ya Moyoni hupatikana kwa kusali wala sio kwa kusoma vitabu na kujua sana Mambo mengi.
Jifunze na jijengea tabia ya kumsikiliza Mungu rohoni mwako unaposali. Sala ni mazungumzo ya Mungu na mwanadamu. Mazungumzo yanahusisha kuongea na kusikiliza.
Mawazo ya Mungu ni makuu. Mungu anatuwazia mema daima. Hata unapopitia shida na matatizo katika maisha nia ya Mungu inabaki kuwa njema ya Kukuonyesha ukuu wake na kukuwezesha kumjua yeye. Pengine usingejua matendo ya Mungu bila kupitia shida na changamoto katika maisha. Mungu hapendi upate shida bali anaruhusu hayo ili upate faida ya kumjua na kujua uwezo wake. Hata Yesu ilibidi apitie mateso na kifo ili uwezo wa Mungu udhihirike baada ya kufufuliwa. Amini kuwa kuna mema mbele yako baada ya mateso haya ya sasa.
Mungu ni Mwaminifu Sana na mwenye mipango na subira katika kila kitu hasa Sala na maombi yetu kwake. Tunaposali leo Mungu anatusikia na kujibu leo, kesho au hata miaka kumi ijayo. Inawezekana hata baraka zako za leo ni majibu ya Sala zako miaka kumi iliyopita. Sali bila kuchoka kwani hujui Sala zako zitakusaidia lini. Usitegemee majibu ya Sala zako wakati huo huo, amini katika uaminifu wa Mungu kwani anajua lini ni siku sahii ya kukujibu.
Njia pekee ya Kumrudia Mungu tunapoanguka dhambini ni Njia ya Toba ya kweli ikiambatana na kukiri makosa na kusamehewa. Mara nyingi tunapotubu tunasahau dhambi za mawazo na kukumbuka za matendo tuu. Dhambi ya Mawazo pia ni dhambi yapaswa toba na maondoleo.
Mungu daima ni Mwaminifu na mwenye Huruma. Kinachotakiwa ni kuamini kwamba kipo na kitakuwepo. Kusadiki kwamba kitafanyika na kitafanyika. Hii ndiyo Siri ya Imani.
Upendo wa kweli hauambatani na chuki. Huwezi kusema una Upendo wakati kuna watu wengine unawapenda na wengine unawachukia. Ni sawa na kusema kitambaa ni cheupe lakini kina madoa doa, maana yake sio cheupe.
Ukitaka kupata amani, tumaini katika Ahadi za Mungu. Ahadi ya Mungu ni hii “Hatoacha kutusaidia wala kututupa”.
Sala za kila siku katika maisha ndiyo hazina kubwa na msaada hasa wakati wa kufa. Adumuye katika sala Mungu hatomwacha saa ya mwisho. Tusali, tusali, tusali daima…
Mungu anasubiri sala zako kila siku. Anasubiri sala zako akujibu ili uone utukufu wake. Anasubiri sala zako ili akuze mahusiano yake na wewe. Sali daima kwani Mungu yupo milele kukusikiliza na kukuhudumia.
Huwezi kusema unampenda Mungu usiyemuona kama huwapendi watu wale unaowaona. Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe. Vile unavyotaka akutendee mtendee vivyo hivyo.
Uwe na subira Baada ya kuomba kwa Mungu. Sio kila unachoomba kwa Mungu utakipata kwa wakati huo huo au kwa wakati unaofikiri. Mungu ni Mwaminifu Sana Kwenye kujibu maombi lakini vile vile ni mwenye Hekima Kwenye kukujibu, anajua wakati gani ni sahihi kukujibu maombi yako. Anaweza kukujibu saa hiyo hiyo, kesho, keshokutwa au hata mwakani kwa kuangalia wakati ufaao na kwa manufaa yako. Kwa hiyo unapoona hujajibiwa usife moyo, bali uwe na matumaini. Mungu anajua akujibu lini kwa kuwa anajua ni lini wakati ufaao na ni lini kitu kipi kina kufaa.
Recent Comments