Anachokiangalia Mungu
Mungu haangalii matemdo ya mtu ya nje tuu, bali anaangalia ndani kabisa mawazo ya mtu na nia yake. Nia ya mtu ndiyo inayoonyesha mtu alivyo.
Mungu haangalii matemdo ya mtu ya nje tuu, bali anaangalia ndani kabisa mawazo ya mtu na nia yake. Nia ya mtu ndiyo inayoonyesha mtu alivyo.
Hakuna Binadamu anayemchukia Mungu kama hajichukii yeye mwenyewe na wale wanaomzunguka. Huwezi kusema humtaki Mungu kama hujichukii mwenyewe na wale waliokuzunguka vivyo hivyo huwezi kusema Unampenda Mungu kama hupendi wengine waliokuzunguka.
Usiogope wala usisite kutubu na kuomba msamaha kwa Mungu. Uwe na Amani na Matumaini katika Huruma ya Mungu itokayo katika Upendo wake wa Mfano wa baba awapendavyo wanawe. Mungu anasubiri kukupokea kwenye mikono yake Ili akutunze kama mtoto wake kama utatubu na kumrudia yeye. Amua kumwendea leo! Anakungoja ni wewe tuu…
Mungu anasubiri sala zako kila siku. Anasubiri sala zako akujibu ili uone utukufu wake. Anasubiri sala zako ili akuze mahusiano yake na wewe. Sali daima kwani Mungu yupo milele kukusikiliza na kukuhudumia.
Hakuna Maisha ya Kikristo bila Kusali. Kama kuna Mkristo anaishi bila kusali huyo siyo Mkristo bali Mkristo mfu. Sala ndiyo uhai wa Mkristo. Hakuna Njia nyingine yoyote ya kumfikia Mungu isipokua sala.
Sala ni Hazina. Kusali ni muhimu sana. Sala unayosali leo inaweza kukusaidia hata miaka kumi ijayo au ikasaidia watoto wa watoto wako. Mungu ni mwenye fadhila na anakumbuka yote. Mwombe Mungu akulinde ukiwa mzima ili uwapo hatarini akukumbuke hata kabla hujamwomba.
Uhuru Na Amani Ya Moyoni hupatikana kwa kusali wala sio kwa kusoma vitabu na kujua sana Mambo mengi.
Upendo hauandamani na ubinafsi. Huwezi kusema una upendo wa kweli kama huwezi kujinyima vile unavyovipenda kwa ajili ya yule au wale unaowapenda. Upendo wa kweli ni kujitoa.
Mungu ni mwenye haki, mpenda haki na mtenda haki. Unapoenenda kwa haki na yeye ataipigania haki yako.
Melkisedeck Leon Shine
Mungu ni mwenye haki, mpenda haki na mtenda haki. Unapoenenda kwa haki, na yeye ataipigania haki yako. Mungu ameweka kanuni na sheria za kiroho ambazo zinaongoza maisha yetu, na ni kupitia haki zake tunaweza kupata baraka na neema zake. Mungu anatuita kuenenda kwa haki, kuwa waaminifu, na kutenda mema katika maisha yetu ya kila siku. Tunapofuata njia zake, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu yupo pamoja nasi na anatupigania.
“Kwa maana Bwana hupenda haki, wala hawaachi watauwa wake; wao watalindwa milele; bali uzao wa wasio haki utakatiliwa mbali.” (Zaburi 37:28)
“Maana mimi, Bwana, ni mpenda haki, nauchukia wizi kwa dhuluma; nami nitawapa thawabu yao kwa kweli, na kufanya agano la milele nao.” (Isaya 61:8)
“Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye fadhili katika kazi zake zote.” (Zaburi 145:17)
Mungu ni mwenye haki. Haki yake inaonekana katika kila kitu anachokifanya na katika jinsi anavyotenda na wanadamu. Mungu anaweka viwango vya haki ambavyo ni kamilifu na bila upendeleo. Kwa haki yake, Mungu anatufundisha njia ya kutenda mema na kuepuka maovu. Haki ya Mungu inatuhakikishia kwamba kila mmoja wetu atapata haki yake katika wakati wake sahihi, na hakuna uovu utakaoponyoka mbele yake.
“Bwana ni mwenye haki; hupenda matendo ya haki; watu wanyoofu watauona uso wake.” (Zaburi 11:7)
“Ee Mungu, njoo uniokoe, Ee Bwana, fanya upesi kunisaidia. Na waaibishwe, wakate tamaa, watafutao roho yangu; warudishe nyuma na kufadhaike, wapendao kunitenda mabaya.” (Zaburi 70:1-2)
“Mimi ni Bwana, ninenaye haki, mwenye kutoa habari za mema.” (Isaya 45:19)
Mungu anapenda haki. Upendo wake kwa haki una maana kwamba anataka kila mmoja wetu awe mpenda haki pia. Anatuita tuishi maisha yanayolingana na haki zake, tukijiepusha na njia za uovu na dhuluma. Mungu anatamani kuona haki ikitendeka katika kila nyanja ya maisha yetu, kuanzia mahusiano yetu binafsi hadi jinsi tunavyotenda katika jamii. Tunapojitahidi kuwa wanyenyekevu na kutenda haki, tunaonyesha upendo wetu kwa Mungu na kwa jirani zetu.
“Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watashibishwa.” (Mathayo 5:6)
“Enendeni kwa Bwana Mungu wenu, mkaishike njia zake, na kuyashika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, kama ilivyoandikwa katika torati ya Musa, mpate kufanikiwa katika kila jambo mfanyalo, na kila mtazamapo.” (1 Wafalme 2:3)
“Yeye anapenda haki na hukumu; dunia imejaa fadhili za Bwana.” (Zaburi 33:5)
Mungu ni mtenda haki. Haki yake inadhihirishwa kwa njia ya matendo yake. Tunapomtegemea Mungu na kuenenda kwa haki, tunakuwa chini ya ulinzi wake na upendo wake. Mungu anatenda haki kwa wale wanaomfuata kwa uaminifu, na anahakikisha kwamba haki yao inalindwa. Katika kila hali, Mungu anatafuta kutenda haki, na kupitia nguvu zake, tunaweza kushinda changamoto na dhuluma za maisha.
“Heri wote wamwaminio yeye. Bwana hufanya haki, na hukumu kwa wote wanaoonewa.” (Zaburi 103:6)
“Siku moja hataonewa tena kamwe; maana ni Bwana wa majeshi asemaye, Nitamkomboa na kuwapa watu wasio na lawama amani; nami nitawafanyia haki watu wote wamtumainio jina langu.” (Yeremia 23:5-6)
“Ee Bwana, ujue uovu wao wote na dhambi yao; usiisamehe hatia yao, wala usiifute dhambi yao machoni pako; bali waangamie mbele zako, uwaache chini ya ghadhabu yako.” (Yeremia 18:23)
Mungu ni mwenye haki, mpenda haki, na mtenda haki. Unapoenenda kwa haki, na yeye ataipigania haki yako. Tunapofuata haki za Mungu, tunakuwa na uhakika wa baraka zake na ulinzi wake. Ni jukumu letu kama Wakristo kuishi kwa haki, kuwa wema na waaminifu, na kutenda mema katika kila jambo tunalofanya. Mungu, katika upendo wake wa haki, atatuonyesha njia ya kutenda haki na kutulinda tunapoishi kulingana na mapenzi yake. Tuishi kwa haki, tukijua kwamba Mungu yupo nasi, akitupigania na kutubariki katika safari yetu ya kiroho.
Ukitaka kupata amani, tumaini katika Ahadi za Mungu. Ahadi ya Mungu ni hii “Hatoacha kutusaidia wala kututupa”.
Uzuri wa Mungu ni kwamba anasamehe na kisha anasahau. Unapotubu dhambi zako na kutaka huruma zake yeye anakufutia uovu wote na kukufanya mpya.
Hakuna kitu cha Muhimu zaidi Duniani kama kumjua Mungu na kumuishi Mungu. Kila binadamu ameumbwa kwa ajili hii. Na Mungu anachotaka ndicho hichi, kumjua na kumuishi. Mengine yote ni maziada. Ukimuishi Mungu atakufanikisha katika yote.
Sala siyo maneno mazuri, bali sala ni NIA ya Upendo iliyobebwa na maneno mazuri. Tusali kwa kunuia kutoka moyoni na sio kwa kunena maneno tuu mdomoni.
Njia pekee ya Kumrudia Mungu tunapoanguka dhambini ni Njia ya Toba ya kweli ikiambatana na kukiri makosa na kusamehewa. Mara nyingi tunapotubu tunasahau dhambi za mawazo na kukumbuka za matendo tuu. Dhambi ya Mawazo pia ni dhambi yapaswa toba na maondoleo.
Sala sio maneno mengi au maneno ya kurudiarudia. Sala ni maneno au hata neno moja la kimapendo litamkwalo kwa imani na kwa nia thabiti.
Upendo wa Mungu hauna mwisho. Mtu anaweza akaacha kukupenda na kukusahau kabisa lakini kamwe Mungu haachi kumpenda Mtu wala hamsahau Mtu.
Wakati wazazi waliweza kuaamua kuzaa mtoto tuu, Mungu yeye alikuchagua wewe utungwe mimba na kukulinda ungali tumboni mwa mama yako….Wakati wazazi wanasubiri kwa shauku kuona muonekano wako wewe, Mungu anawaweka wajukuu wa wazazi wako/ watoto wako ndani mwako…. Wakati wazazi wakitafuta chakula kwa ajili yako, Mungu yeye aliwawezesha kukipata…. Wakati wazazi wakingoja kuona unavyoendelea kukua huku wakiwaza hatima ya maisha yako Mungu anakuendeleza na alishapanga maisha yako tangu alipokuchagua uwe mtu ukiwa tumboni mwa mama yako…. Wazazi wanaweza kukuombea kwa Mungu lakini Mungu ndiye anayeamua akufanyie nini maana Wewe ni wa kwake….Wewe na wazazi wako ni watoto wa Baba mmoja ambaye ndiye Mungu.
Uwe na subira Baada ya kuomba kwa Mungu. Sio kila unachoomba kwa Mungu utakipata kwa wakati huo huo au kwa wakati unaofikiri. Mungu ni Mwaminifu Sana Kwenye kujibu maombi lakini vile vile ni mwenye Hekima Kwenye kukujibu, anajua wakati gani ni sahihi kukujibu maombi yako. Anaweza kukujibu saa hiyo hiyo, kesho, keshokutwa au hata mwakani kwa kuangalia wakati ufaao na kwa manufaa yako. Kwa hiyo unapoona hujajibiwa usife moyo, bali uwe na matumaini. Mungu anajua akujibu lini kwa kuwa anajua ni lini wakati ufaao na ni lini kitu kipi kina kufaa.
Mungu ni mwema sana tunapokua wadhambi anapotuadhibu haimaanishi kuwa anatuchukia. Inamaanisha kuwa anatuonya na hapendi turudie makosa.
Kufanya Mambo mema ndipo kunaleta furaha ya kweli kwa Binadamu yeyote yule. Hakuna Binadamu anayefurahia kufanya maovu. Mema hayaambatani na majuto lakini uovu wowote unamajuto. Hata waovu wanafanyiana mema ili wapate furaha.
Recent Comments