Vichekesho Vya Asubuhi Hii
Hii kazi kweli kweli, Ungekua wewe ungefanyaje?
UNATOKA SEBULENI UNAENDA ZAKO CHOONI UNAINGIA TU HIVI GHAFLA UNAKUTANA NA MZIGO MKUBWA WA MAVI JUU YA CHOO ALAFU UNAAMUA KURUDI ZAKO ILE UNATOKA TU UNAMUONA DEMU MZURI ULIYEMTONGOZA JANA ANAKUJA KUINGIA CHOO ULICHOTOKA WW NA KINA MZIGO WA MAVI JUU NA AMEKUONA WW NDIO UMETOKA MLE NDANI ..unaamua kurudi ili uka flash bahat mby maji hakuna.!!!
😁😁😁HAPO NDIO UTAJUA KWANINI SIKU HIZI HATUPENDI UJINGA😆😆😆😆
Mabinti wengine kwa kupenda hela! cheki huyu anachokifanya
Phone call
gal: hellow
Boy: sweety mambo vipi?
Girl: poa
Boy: utakuwa free weekend? nilikuwa nataka uje nyumbani
Girl: oh sorry ctoweza kuja sababu kuna haruc ya aunt yangu
Boy: kama ni hivyo sawa nilikuwa nataka nikufanyie sapraiz nimekununulia BLACKBERRY.
Girl: oh ucjal ntakuja na hata ntalala huko huko
Boy: na haruc je?
Girl: nilikuwa nakutania
Boy: hata mi nilikuwa nakutania
Angalia huyu house girl wa mzungu alichokifanya na anachokisema
House girl mmoja alipewa kazi na mzungu mara akavunja sahani.
Mzungu aliporejea,kazin akamuuliza ‘what happened to my plate?
House girl akajbu: ‘The dog wow wow friji paaa, mchuzi mwaaaa the vyombo pangalapangala the sahan ngelengenjee……the pasuka paaaaaaaa
😂😂😂😂hadi saiz mzungu bado anasoma dictionary hajui lugha gani imetumika
Sababu ya girlfriend 👧 kuniblock
Nimeblockiwa bila kosa X Girlfriend From no where kanitext eti Hi; Vp na huko kwenu mvua inanyesha …Nimemjibu kwani nimekutumia text ina matope?
sipendangi ujinga mimi
Ikitokea hii kwenye chumba cha mtihani
Upo kwenye chumba cha mtihani,
maswalii yamekupiga kinyama
Unaamua kuchukua smartphone ugoogle kisha ucopy na kupaste kwenye booklet yako,
Ghagfla lecturer aningia na wewe kwa woga wako unaficha calculator na kuweka simu mezani,
Hapo ndo utajua shetani naye alikua anasimamia paper.
😂😂😂😂😂
Sababu za kumuacha mke kama umemchoka
Ukimchoka mkeo, waweza kumtaftia sababu za kumuacha kama hizi
_
1. Missed calls 16? Umeua betri la simu yangu. Kwa hiyo hata mimi unaweza kuniua… It’s Over!!!
_
2. Hata hunieshimu. Mi naongea na wewe lakini we upo bize unavuta pumzi? It’s over!
_
3. Nimekupigia umepokea simu hapohapo. Huna subira. It’s over!!
_
4. Nilikwambia huwa napenda chakula cha moto lakini hujanipashia ice cream. Hunijali. It’s over!
_
5. Nimekupa mayai mawili, moja uchemshe jingine ukaange. We umekaanga ambalo ulitakiwa kuchemsha na umechemsha ulilotakiwa kukaanga. Huniheshimu, It’s over!
_
6. Nimekuita DARLING na wewe ukaniita HONEY. Yani kwa maana nyingine unamuita mama yangu NYUKI. Huheshimu wazazi wangu, fungasha kilicho chako. its over.
😄😂😄😂😄😂😄😂😄
Huyu Jamaa kaona bora afe kuliko mke wake ajue Siri zake
Jamaa Mmoja Alimwambia Mke Wake Wasiliana Na Kitengo Cha Dharura Hospitali, Niko Taabani Nahisi Kama Ninakufa.
Mke Akamwambia Nipe Namba Yako Ya Siri Nifungue Simu Yako.
Mume Akasema👉👉 Basi Acha Tu; Kila Nafsi Itaonja Mauti
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Angalia huyu msichana alichonifanyia
Kuna siku nilichalala kipesa nikaamua kuomba dem wangu aniazime 10,000/= akanipa.
Baada ya siku mbili nikapata pesa zaidi ya laki nne hivi, nikaamua kumpa 100,000/= mpenzi wangu bila yeye kuniomba.
Baada ya siku 3 akaja kuniambia:- “Bae, ile 10,000/- niliyokuazima mwenyewe amekuja kunidai, so kama unayo naomba unipe nimrudishie maana ananisumbua leo siku ya 3.”
SAA HIZI NIPO ZANGU SINGLE NATAFUTA DEM MWINGINE
Mme amemfuma fundi wa kitanda na mke wake, cheki walichokua wanafanya
Kuna mama mmoja ameolewa na wanapendana sana na mmeo. siku moja mme wake alisafiri kikazi (safari ya zaidi ya mwezi) nje ya mkoa. Siku mmeo anarudi, yule mama alimtafuta fundi seremala amrekebishie chaga za kitanda zilikuwa zimeharibika, kwa ajili ya maandalizi ya mechi ya above +18.
Wakati fundi anaendelea na kazi kumbe mmeo huyu dada alishafika. hakutaka kumjulisha mkeo, kwa nia nzuri tu ya kumfanyia suprise, kwani alikuja na mazaga zaga kibao. Hiyo aliingia kwa kunyatia hadi kwenye mlango wa chumbani kwao. Ghafla akasikia mazungumzo ya mkeo na fundi ndani. Mazungumzo yalikuwaje? fuatilia hapa chini
Mama X: Fanya haraka mme wangu amekaribia
Fundi: Nakaribia kumaliza, nisaidie kuchomeka vizuri upande wako (akikusudia chaga)
Mama X: Mbona haiingii
Fundi: Ingiza kwa upande upande
Mama X: Sukuma kwa nguvu
Fundi: Angalia usiumie
Mama X: Hamna shida imeingia
Wakati jamaa akiendelea kusikiliza mlangoni, fundi akaweza godoro juu ya kitanda na mama x akajitupa kitandani kujaribu kama kimetengamaa. mara chaga akachomoka na kuanguaka chini. Nini kilifuata
Mama x: Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii iiiii(miguno) “my God, mbona hivi”
Fundi : Pole sana
Mama X: sasa?
Fundi: Ngoja nichomeke tena
Mama X: Yaan wewe, utaacha mme wangu afike hatujamaliza
Fundi: Usijali namaliza sasa hivi
Baada ya dakika chache, fundi akamuaga mama na kumwambia tayari, sasa naona umefurahi. Kutoka tu mlangoni akakutana uso kwa uso na jamaa amekunja ndita kama matuta ya viatu. Gues what happened?
Kitu gani kitatokea kisia toa maoni yako kama ni ww ungefanyaje?
Ungekua wewe ndio baba wa Huyu mtoto ungemjibu nini?
MTOTO: Hivi Baba wewe umezaliwa wapi?????
BABA: Mbeya
MTOTO: Mama nae kazaliwa wapi????
BABA: Tanga
MTOTO: Mimi jee?????
BABA: Dar
MTOTO: Sasa tulikutanaje????
😂😂 hapo wee kama baba ungemjibuje mwanao😳😳😳
Kilichotokea baada ya bibi na babu kukumbukia mahaba ya ujanani
Mzee wa miaka 60 alimwambia mkewe, leo nataka tukumbukie enzi zetu kutongozana, mke akajibu sawa, inabidi unisubiri mwembeni saa 1 usiku nitapita, mzee akafika saa 1 alikaa hadi saa 5 usiku, aliporudi nyumbani akamuuliza mkewe kwa hasira; sasa tumepanga nin halafu haujatokea ?
Mke; leo mama alinikataza nictoke nyumbani usiku nijisomee ! Babu hoii…
Cheki huyu mwanamke anavyomkomoa mme wake baada ya kumsaliti
MKE: Mbona unanukia pafyumu ya kike?
MUME: Yaa kuna mwanamke tulikuwa tumeminyana ndani ya daladala
MKE: Na lipstiki kwenye shati?
MUME: Tulikumbatiana na wageni toka Zambia walitembelea ofisi yetu
MKE: Na ile kondom iliyotumika kwenye mfuko wa suruali?
MUME: Bwana ee acha maswali ya kijinga mi nalala nina usingizi
MKE: Lazima niulize mie huwa nahakikisha nimeacha kila kitu hukohuko ndio narudi nyumbani
MUME: Umesema nini wewe?
MKE: Bwana ee acha maswali ya kijinga mi nalala nina usingizi. 😄😄
Mwizi kawezwa ki kwelii
Et jana usiku mwiz kavunja mlango kwangu akaanza kutafuta kitu kila kona ikabid na mie niamke namuuliza unatafuta nini ananijibu hela ndipo nilipoanza na mie kutafuta nae maana hta hela ya kula Jana sikua nayo alichoka zaid nilipomuliza una uhakika uliweka humu? sipendagi ujinga🚶🏻 na kitu hela mm!
Hakuna mtu mwenye mbio duniani kama huyu
HAKUNA MTU MWENYE MBIO, KAMA MSICHANA ALIYEPAKA MAKE UP ALAFU MVUA INYESHE….. 😂😂
Huyu jamaa kawaweza wapenda vya bure
Jamaa kaingia mgahawani kwa fujo
JAMAA : Nipe soda moja na kila mtu mpe yake maana ninapokunywa soda napenda kila mtu anywe
WATU : Ha! Ha! Ha! Haaaa!
JAMAA : Nipe mchemsho na kila mtu mpe wa kwake maana ninapokula mchemsho napenda kila mtu ale wake
WATU: Watu weweeee! Tena safari hii Na makofi juu..
JAMAA : Mhudumu, nipe bili na kila mtu mpe yake maana ninapolipa bili napenda kuona kila mtu analipa yake
😂😂😂😂😂😂😂
MAJIBU YA MAKONDA WA DALADALA ZETU GONGOLAMBOTO HUKU
1. wewe Dada unaturingia nini na matiti yako mawili , mbwa pia ana matiti nane na haturingii eboo !!!!
2. Ka wafikiri Una haraka sana Shuka ukimbie.
3. Nauli kulipa lazima ,Chenji ukikumbuka.
4. Kutapika ndani ndani ya Daladala fain 250/= ,ukijamba pia 250/= ,Sasa jamba tukujue viti vina alarm!…
5.Hatujasema wewe ni Mnene ila Ukikalia SITI mbili Lipia….
6. Hio Elfu kumi yako nenda nunua avocado upake alafu uteleze hadi posta ,nauli ya daladala ni 350/=.
7. usifungue dirisha ungetaka upepo ungepanda pikipiki..
8. wewe Dada hebu sogea hukoo, Unaringa nini wakati asubuhi hii umeoga na sabuni ya kuoshea vyombo…
Angalia huyu jamaa alivyomuweza huyu binti wa chuo
😁😁😁😁 .. TABU KUDATE NA MADEMU WA CHUO
Demu ; Baby Safari Hii Nataka Pale Hostel Niwafunike Mashoga Zangu Wote.
Jamaa ; Poa Sweetie Ondoa Shaka Nitakununulia #Turubai Utawafunika Wote…!!!
Demu: Mxiuuuuuuuu Lione Sura Kama Goti La mbuzi Na Namba yangu futa Nakublock Mpaka Sanduku la posta…!!!
😂😂😂😂nmecheka adi nmelazwa
Nilichokifanya wakati naangalia taarifa ya habari
Jana wakati naangalia taarifa ya habar mtangazaji akasema “mpenz mtazamaji nataka nikupeleke moja kwa moja had marekani” nikazima TV kwa haraka nikaenda kuvaa viatu. Hadi sahv bado nmekaa hapa seblen nahisi bado wanaihangaikia Visa yangu
😂😂😂😂😂😂
Alichofanya maasai baada ya kupanda Tax
Baada ya kupanda daladala aina ya DSM kutoka Mbagala chalambe mpaka Mwenge na kulipa sh 500.Masai akachukua tax wakati wa kurudi.walipofika sasa shughuli ilikuwa hivi.
Masai: we dureva? Naulisa Ng’ombe na mbusi ipi ngali?
Dereva: Ni ng’ombe ghali Masai.
Masai: kwanini Ng’ombe ngali?
Dereva: kwa sababu ni mkubwa zaidi ya mbuzi
Masai: umepata..na mbusi na kuku ipi ngali
Dereva: ni mbuzi kwa sababu nae ni mkubwa kuliko kuku.
Masai: Umepata..
Masai: sasa me nimekwenda kule mwenge kwa ngali kubwa nikalitoa sh. 500 hii yko ndogo unasema nikupe 40,000 wewe acha wizi.. Nitakupa 250 Tu..wee acha lbia morani…!!!
Recent Comments