Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Cheki jamaa alivyoumbuka baada ya kuhudhuria semina isiyomuhusu

Jamaa kavamia semina ya wasomi iliyokua inafanyika maeneo ya ubungo plaza bas wakaanza kujitambulisha
1. Naitwa Anna niko SUA mwaka3 nasoma agriculture
2. Naitwa Stella niko UDSM mwaka2 nasoma public relation

3. Naitwa Emmanuel niko UDOM mwaka3 nasoma computer science
bas jamaa nae akainuka kwa kusuasua huku akijishtukia akasema”Naitwa Elisha niko Tanesco mwaka wa 7 nasoma mita”

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nazi Wa Nyanya Chungu/Mshumaa/Ngogwe Na Bamia, Mboga Ya Matembele Na Samaki Wa Kukaanga

Vipimo Vya Ugali

Unga wa mahindi – 4

Maji – 6 kiasi kutegemea na aina ya unga

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Weka maji katika moto.

Tia unga kidogo katika kibakuli, koroga ufanye uji.

Maji yakichemka tia kwenye maji uwe uji.

Ujii ikiiva punguza kidogo tia unga kidogokidogo na usonge ugali. Ikiwa unga ni mgumu utaongeza maji ya ule uji ulopunguza usonge hadi uive ukiwa tayari.

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nazi Kwa Nyanya Chungu/Mshumaa/Ngogwe Na Bamia

Nyanya chungu/mshumaa/Ngogwe – 7

Bamia – 10

Kitunguu maji – 2

Nyanya/tungule – 2

Tui la nazi jepesi – 2 viwili

Tui la nazi zito – 2

Chumvi – kiasi

Ndimu – 2 mbili kamua

Bizari manjano/haldi/turmeric – ½ kijiko cha chai

Pilipili mbuzi – 3

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Katakata kitunguu maji na nyanya vipande vidogodogo sana kisha weka katika sufuria.

Iache ichemke kwa maji yake ya nyanya, ikishachemka tia maji kidogo kama robo kikombe.

Tia nyanya chungu, bamia na koleza ndimu, chumvi.

Iache ichemke. Inapokuwa tayari imeiva tia tui jepesi endelea kuacha katika moto huku unakoroga kidogo kidogo.

Tui jepesi likipungua kiasi chake, tia tui zito, kisha usiachie mkono koroga ikichemka kidog kiasi cha kuiva tui mchuzi tayari.

Vipimo Vya Mboga Ya Matembele

Matembele – 5 mafungu

Mafuta – ¼ kikombe

Kitunguu maji kilokatwakatwa – 1

Nyanya/tungule – 4

Chumvi – 1

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Punguza miche ya matembele kwa kuikata ncha kisha osha majani yake. Acha yachuje maji .
Weka mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji na nyanya hadi viivie.
Tia mboga, Iache ichemke kwa maji yake hadi iive. Ukiona bado haikuiva tia maji kidogo tu.
Ukipenda unatia ndimu kiasi cha kipande kimoja ukamue .

Samaki Wa Nguru Wa Kukaanga

Samaki Wa Nguru – 4 vipande

Kitunguu saumu(thom/galic) na tangawizi ilosagwa – 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi – 4

Ndimu – 2 kamua

Bizari ya samaki – 1 kijiko cha chai

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Mwoshe samaki kisha mtie kitunguu thomu, tangawizi ilosagwa, chumvi, pilipilimbichi ilosagwa, ndimu na bizari ya samaki.
Mwache akolee viungo kwa muda kidogo.
Makaange katika mafuta hadi aive akiwa tayari.

BRAVO 20EC (Imidacloprid 20EC): Dawa nzuri ya wadudu shambani na kwenye majengo. Inaua mchwa, utitiri, kimamba na vipepeo weupe

Ina Imidacloprid 20EC

Hii ni dawa maalumu Kwa ajili ya kuua wadudu shambani na kwenye majengo/majumbani.

Dawa hii inaua wadudu Kama vile kimamba, utitiri mweusi, mabaka meusi chini ya Majani, vipepeo weupe na wadudu wanaofyonza maua.

Dawa hii ina nguvu na uwezo wa kufanya kazi Muda mrefu kuulinda mmea/majengo dhidi ya wadudu waharibifu.

Dawa hii ni Maalumu Kwa kuangamiza mchwa kwenye viota na vichuguu.

Imetengenezwa katika Ubora wa Hali ya Juu Ili kukuhakikishia matokeo mazuri unapotumia dawa hii.

Bidhaa hii inaletwa Kwako na Kampuni ya BareFoot International Limited. Wauzaji na wasambazaji wa bidhaa Bora za Kilimo Tanzania.

Mawasiliano

Simu:

+255 756 914 936

WhatsApp:

+255 756 914 936

Email:

info@bfi.co.tz

NB: Tunapatikana Mikoa Yote Tanzania

Matumizi ya Mrehani (basil) kutibu presha ya kushuka

Hii ni dawa nzuri ya kutibu shinikizo la chini la damu sababu ya kuwa na kiasi kingi cha vitamini C, magnesiamu na potasiamu, vilevile dawa hii husaidia kuweka sawa akili na kuondoa msongo wa mawazo (stress).

Matumizi

  1. Chukua majani 10 mpaka 15 ya mrehani mbichi
  2. Saga au twanga kupata maji maji yake (juisi).
  3. Weka asali kijiko kidogo kimoja ndani yake.
  4. Kunywa mchanganyiko huu kila siku asubuhi ukiamka tu tumbo likiwa tupu.

Vile vile unaweza kutafuna tu moja kwa moja majani kadhaa ya mrehani kila siku asubuhi.

Hii ndio inaitwa mbinu ya biashara

Anakuja Mchina anasema anahitaji Paka🐈,
ananunua mmoja kwa bei ya 20,000/=, basi
wanakijiji wanahaha kusaka Paka🐈,
wanawaleta mchina ananunua wote anasepa
nao. Anarudi tena anasema vipi, naona
wameadimika, sasa ntanunua kwa bei ya
35,000 Paka🐈 mmoja, wanakijiji wanaenda
deep zaidi msituni, kamata Paka🐈, leta kwa
mchina, mchina anasepa nao.

Afu wiki
mnayofuatia Mchina anasema bado anataka
Paka🐈, saivi atanunua kwa Laki. Wanakijiji
macho yamewatoka, hawana tena paka🐈.
Mchina anasema basi ntaftieni kwa Laki na
Nusu. Keshoake inasikika kuwa kuna Mchagga
anauza Paka kijiji cha pili, anauza kwa
100,000/=, wanakijiji wanawahi fasta
wanaenda nunua Paka🐈🐈🐈🐈 wote wa kijiji cha
pili. Wanarudi kijijini hawana pesa ila wana
Mapaka 🐈🐈🐈 wakijua watamuuzia mchina fasta kwa
laki na nusu, Mchina hatokei Ng’oooo!!!!
Infact, yule mchina alikuwa anawakusanya tu
na kuwahifadhi kule kijiji cha pili akijua ataja
wauza kwa 100,000/= kwa hawa hawa wa kijiji
hiki.
This is what called business strategy.😃

Mambo 10 ambayo wanawake wamewazidi wanaume

1. Wana Nguo Nyingi KulikoWanaume.
2. Wanafahamu Nani Ni Baba HalisiWa Watoto Wao.

3. Ni Wepesi Kupenda NaWakipenda Hupenda Kweli.

4.Wanaoga Mara Nyingi Zaidi KwaSiku.

5. Wana Huruma Sana Ingawa MaraNyingi Huwa Inawaponza.

6. Wana Uwezo Wa KubadilishaTabia Ya Mwanaume Muda Wowote.

7.Wana Uwezo Wa Kuishi NaKupendeza Bila Kuwa Na Kazi WalaBiashara Yoyote.

8. Kwao Nywele Na Kucha Ndo Vitu Vya Kwanza Kufikiria WakitakaKutoka.

9. Wana Uwezo Wa Ku-Pretend Kwa Muda Mrefu Zaidi Hasa Kwenye Mapenzi.
10. Hawapendi pesa

Samahanini Jamani. hiyo ya 10 imeniponyoka 🤣😎

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Angalia hawa kina mama, ni shida..!

Mama mdaku alishangaa kila siku mchungaji anaingia nyumba ya jirani yake ambaye hana mume, akawa anajiuliza anakwenda kufanya nini? Uzalendo ukamshinda akamuuliza “Mwenzangu, mbona kila siku mchungaji anakuja kwako, vipi anakuja kukuombea?” Akajibiwa “Nyoo, umbea tu! Mbona kwako kila siku anakuja mwanajeshi kuna vita! chefuuuu 😳😳😳😳😳

😂😂😂😂😂😂😂😂😂

Jinsi ya kupika Pilau Ya Nafaka Na Nyama Ya Kusaga

Viambaupishi

Mchele 3 vikombe

Nyama ya kusaga 1 LB

Mchanganyiko wa Nafaka (upendavyo) 1 kikopo

(maharagwe, njegere, mbaazi, na kadhalika)

Vitunguu maji kata vipande vipande 3 vya kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi 2 vijiko vya supu

Mafuta ½ Kikombe

Mchanganyiko wa bizari (Garam Masala) 2 vijiko vya chai

Vipande vya supu (Maggi cubes) 3

Maji (inategemea mchele) 5

Chumvi Kiasi

Jinsi ya kuandaa na kupika

1) Osha mchele na roweka.

2) Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitunguu mpaka viwe brown.

3) Tia Thomu na tangawizi, kaanga kidogo.

4) Weka nyama ya kusaga, chumvi na garam masala, endelea kukaanga mpaka nyama iwive.

5) Mwaga maji yaliomo katika kopo la nafaka na utie nafaka pekee humo.

6) Tia maji na vipande vya supu (Maggi cubes) huku unavivuruga, koroga kidogo.

7) Tia mchele, koroga kidogo.

8) Funika na pika kwa moto mdogo mpaka karibu na kukauka ukikorogoka kidogo. (kama unavyopika pilau ya kawaida)

9) *Epua uipike katika moto wa oven 350-400 Deg kwa muda wa dakika 15.

*Kama sufuria uliyotumia sio ya kupikia katika oven, mimina katika chombo chochote kinachotumika kwa oven kama bakuli la pyrex au treya za foil.

10) Pakua katika sahani na iko tayari kuliwa.

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia baking soda

Moja ya sababu za kutokea chunusi katika ngozi yako ni kuwepo kwa takataka au uchafu juu ya ngozi yako na njia rahisi ya kusafisha taka hizo ni kwa kutumia baking soda hivyo kuifanya ngozi ipumuwe vizuri.

Kwahiyo ukiwa na chunusi hebu fikiri kuhusu baking soda. Baking Soda husaidia kubandua seli za ngozi zilizokufa na kufanya mafuta yaliyozidi kuondoka.

Ni rahisi zaidi kutumia baking soda kutibu chunusi. Chukua baking soda na uchanganye kidogo na vijiko vinne vidogo vya maji au vya maji maji ya limau na upake uji huo moja kwa moja kwenye chunusi. Subiri kwa dakika 10 na ujisafishe na maji ya moto.

Mapishi – Saladi ya Matunda

Matunda ni mojawapo wa kundi la vyakula, ni muhimu sana kwa afya bora. Matunda yakitengenezwa vizuri yanavutia sana na yanakuwa ni chakula kizuri sana.

Mahitaji

Embe iliyoiva kiasi
Nanasi
Tango
Tikiti maji
Zabibu
Papai

Matayarisho

1. Ondoa maganda kwenye embe, nanasi, tango, papai na tikiti maji kisha kata kata vipande vidogo vidogo vya mraba

2. Changanya vipande vya matunda kwenye bakuli safikisha weka na zabibu zilizotolewa kwenye kikonyo chake.

3. Weka kwenye friji yapate ubaridi kidogo

4. Saladi yako tayari kwa kuliwa

Waweza kula saladi hii kama mlo wa kati au kama mlo kamili wa usiku.

Tofauti ya mke na mchepuko!!!

MKE NA MCHEPUKO.

Mke ni kama Tv na Mchepuko ni kama Simu.
Nyumbani unaangalia Tv lakini ukitoka unatoka na simu.

Mara chache unafurahia Tv lakini Muda mrefu unacheza na simu yako.

Tv ni bure kwa maisha yako yote, lakini Simu kama hujalipia hupati huduma.

Tv ni kubwa nzito na wakati wote ni ya zamani. Lakini simu ni nzuri, nyembamba, na ni rahisi kubeba.

Gharama za huduma za tv ni ndogo sana, Lakini gharama za huduma za Simu ni kubwa na pia ni lazima kuzitimiza.

Tv ina remote lakini Simu haina.

Kitu muhimu zaidi simu ina njia mbili za kuwasiliana unaongea na unasikiliza lakini Tv unalazimika kusikiliza hata kama hutaki au unataka.

Unaweza kununua Tv mara moja na ukatumia kwa kipindi kirefu lakini Simu mara zote unabadilisha inategemea na fasheni.

Ya mwisho na ya kuzingatia

Tv haina Virusi lakini Simu inayo.

KUWA MAKINI.

Mapishi ya Wali Wa Tambi Na Kuku Wa Sosi Ya Mtindi

Vipimo Vya Wali

Mchele – 3 vikombe

Tambi – 2 vikombe

Mafuta – ¼ kikombe

Chumvi

Vipimo Vya Kuku

Kuku kidari (boneless) aliyekatwa katwa vipande – 1 Kilo

Kitunguu maji kilichokatwa katwa – 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa – 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa – 1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Paprika – 1 kijiko cha supu

Masala ya kuku (tanduri au yoyote) – 1 kijiko cha supu

Ndimu – 2 vijiko vya supu

Mtindi (yoghurt) au malai (cream) – 1 kikombe

Mafuta – ¼ kikombe

Majani ya kotmiri (coriander) – ½ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali:

Osha Mchele, uroweke.
Tia mafuta katika sufuria, kaanga tambi zilizokatwakatwa hadi zigeuke rangi kuwa nyekundu.
Tia mchele endelea kukaanga kidogo.
Tia maji kiasi cha wali kupikika kama unavyopika pilau. Kiasi cha maji kinategemea aina ya mchele
Funika katika moto mdogo mdogo hadi uive ukiwa tayari.

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku

Katika bakuli, changanya vitu vyote isipokuwa mtindi na kitunguu.
Tia mafuta katika karai, kisha tia kitunguu ukaange muda mdogo tu, usikiache kugeuka rangi.
Tia kuku na masala yake, endelea kukaanga, kisha tia mtindi au malai ufunike apikike na kuiva vizuri.
Nyunyuzia kotmiri iliyokatwakatwa ikiwa tayari kuliwa na wali wa tambi.

Angalia huyu dada alivyoumbuka, Duh! Alijua haoni!!!

Dem anatoka kuoga akiwa na kanga moja tu anaskia hodi,kufungua mlango akakuta ni jirani yake frank ambaye ni kipofu, akamkaribisha ndani akakaa, dem kavua ile kanga akabaki uchi akainama akaanza kujipaka mafuta akijua frank hamuoni na mazungumzo yakawa ni Haya..

DEM: VIPI FRANK MBONA UMEPOTEA YAANI HUONEKANI SIKU HIZI..?

FRANK: AH NILIENDA INDIA KUFANYIWA OPERESHENI YA MACHO SASA HIVI NAONA VIZURI KABISA!…

😂😂😂

🏃🏻🏃🏻🏃🏻🏃🏻🏃🏻

Unakumbuka hizi enzi za utoto?

Kitambo tukiwa watoto ulikuwa unaitwa uje ule kwa lugha tofauti kulingana na chakula kilichopikwa siku na muda husika

1. UGALI NA KUNDE
Mwitaji : 🗣Joniiiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Uje ukule

2. UGALI NA SAMAKI
Mwitaji: 🗣 we Joniiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Unaitwa na Mama

3. WALI NA NYAMA/KUKU
Mwitaji: 🗣 Joniiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Shauri yako!
😂😂😂😂😂😂

Mambo ya kufanya mwezi Disemba

Ikiwa leo ni tarehe **1/12 huwezi amini kuwa hakuna tarehe 1 nyingine tutakayoiona ya mwaka huu hivyo sichelei kusema kuwa mwaka umeisha .Lakini mwaka unaishaje??? pengine hili ndilo swali gumu na la muhimu la kujiuliza .Je, Mwaka unaisha ukiwa umefanya nini cha kujipongeza??? .Je mwaka unakaribia kuisha maarifa yako yakiwa yameongozeka kwa kiasi gani???.Haya ni maswali muhimu sana unavyooanza kufikiria juu ya sherehe za mwisho wa mwaka.

Watu waliopiga hatua katika fikra – yaani, wale waliofanikiwa kutimiza malengo na mipango waliyojiwekea – wanajikuta katika kipindi cha kipekee ifikapo mwezi huu. Ni wakati ambao wanapaswa kuchukua muda na kutafakari kwa kina juu ya safari yao ya mwaka uliopita. Huu si tu wakati wa kuzingatia mafanikio na mafunzo, bali pia ni kipindi cha kulinganisha matarajio yaliyokuwa yamewekwa dhidi ya yale yaliyotimia.

Kurudi kwenye malengo yaliyowekwa hapo awali ni zoezi la muhimu linaloleta tafakuri juu ya uendelevu na ufanisi wa mikakati iliyotumika. Watu hawa wanaweza kujiuliza maswali kama, je, malengo yalikuwa yanatekelezeka? Je, walikutana na changamoto gani, na walizishinda vipi? Changamoto hizi zinaweza kuwa za ndani kama vile kutunza motisha, au za nje kama vile mabadiliko ya kiuchumi na kijamii yaliyokuwa yameshuhudiwa.

Inawezekana pia walikuwa na malengo ambayo hayakutimia. Katika hili, kuna fursa ya kujifunza na kuchukua hatua za marekebisho. Mwisho wa mwaka ni muda mwafaka wa kutathmini upya na kuweka mikakati mipya, kuondoa yaliyopitwa na wakati na kuja na mawazo mapya yatakayowasukuma mbele zaidi. Uchambuzi wa kina utawasaidia kuweka malengo yanayoweza kutekelezeka kwa mwaka unaofuata pamoja na kutengeneza mpango kazi madhubuti ambao utawaongoza katika hatua zao zijazo.

Kwa kuangalia nyuma na kufanya tathmini yenye unyoofu, waliopiga hatua katika fikra wanaweza kupata msingi imara wa kujenga juu yake. Wanaweza kujitathmini na kujipanga upya, kuchukua mwelekeo wenye nguvu na mpya ambao utawawezesha kutimiza malengo yao yaliyosasishwa na yaliyo wazi zaidi. Kila hatua, kila mafanikio, kila funzo, yote huchangia katika safari yao ya kipekee ya maendeleo binafsi na ya kitaaluma.

Leo nataka nikuekeze mambo muhimu ya kufanya mwezi huu pamoja na kuwa unawaza sikukuu na kusafiri kwenda kwenu .Mambo haya unaweza kuwa hujawahi kufanya lakini ni muhimu sana ukafanya mwaka huu ili mwakani tuone mabadiliko .Mambo hayo ni pamoja na ;

1.Fanya Tathimini (Evaluation)

Tathimini ni kipimo kinachoonesha kushindwa kwako na kufanikiwa kwako .Mwezi huu ni mwezi wa kukaa chini na kurejea kwenye malengo na mikakati uliyokuwa umejiwekea na kuona ni kwa jinsi gani umefanikiwa .Ainisha mambo uliyofanikiwa na ambayo hujafanikiwa .Kwa yale uliyofanikiwa jipongeze kwa kufanikiwa kwa yale ambayo hujafanikiwa jiulize kwanini hayajafanikiwa ili yakupe mbinu na hatua mpya mwaka ujao.

Andika kwa mtindo huu;

SEHEMU A:MAMBO NILIYOFANIKIWA HUU

-Mwaka huu nilifanikiwa kuwapata marafiki wazuri wanaounga mkono maono yangu
-Mwaka huu nilifanikiwa kuanzisha biashara ya genge
-Mwaka huu nilifanikiwa kusoma vitabu viwili

*Jitihidi sana kujipongeza kwa yale uliyofanikiwa na hii ni tabia ya watu waliofanikiwa .Usione umefanya madogo lahasha.*

SEHEMU B:MAMBO AMBAYO SIKUFANIKIWA mwaka huu

-Sikufanikiwa kuhudhuria semina hata moja ya ujasiriamali
-Sikufanikiwa kuboresha ofisi

Kwa yale ambayo hukufanikiwa jiulize kwanini hukufanikisha utagundua wewe ndiye sababu kubwa ya kutoyafanikisha .

2.Anza kuandaa malengo ya mwaka ujao (GOAL SETTING)

_Pasipo maono, watu huacha kujizuia_
~(Biblia)

Ndiyo bila malengo hutafika na utafanya kila kitu bila mpangilio .Huu ndio mwezi kwako ambao unapaswa kuandaa malengo ya mwaka ujao haijalishi hukuwahi kuweka malengo toka unazaliwa .Najua malengo yako yalikuwa yanakaa kichwani mwaka huu amua kuandika kwenye notebook Nzuri .Andika kwa ujasiri mkubwa sana .Malengo yako yafuate kanuni za malengo(yapimike,yawe na ukomo,yawe mahususi na yakufikika ).

Andika kwa mfano huu;

-Kufikia Mei  nitakuwa nimefuga kuku watatu hata kama nyumba yangu ni ndogo .

-Kufikia Agosti   nitakuwa nimehudhuria semina 2 za ujasiriamali

Ukiandika kwa mfumo huo itakusaidia kuyafikia malengo yako maana yamefuata kanuni za malengo.

3. Andaa Bajeti ya mwaka  (Budgeting)

Hii ni sehemu ambayo inaleta shida sana .Na hii ni kwa sababu hata wazazi wetu wametulea bila kutufundisha bajeti.Masomo ya darasani wengi hatufundishwi kuishi kwa bajeti .Lakini Tusilaumu sana kutofundishwa maana lawama ni tabia ya kimaskini tuamue mwakani 2017 kuishi na kutembea na bajeti

Mara nyingi tukiulizwa hela zetu zinaenda wapi huwa hatuna majibu sahihi .Hii ni kwasababu hatuna bajeti .Kwanini bajeti??? .Bajeti hutusaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na yaliyo nje ya bajeti .Bila bajeti sehemu ya kutembea kwa mguu utapanda bodaboda .Bila bajeti utanunua simu ya laki saba wakati unasema huna mtaji wa laki sita.Bajeti itaamua uchangie harusi na kitchen party ngapi kwa mwaka.

Ndiyo lazima tubadilike hata mimi nimeamua hivyo mwaka ujao.Kama una familia kaa na mke wako tengeneza bajeti ya mwaka.Kuna vitu vinaweza kujitokeza njiani na hivyo kumbuka kuweka dharura .

Bajeti iliyopangwa kwa mwaka ujao ni kama ramani inayoonesha njia ya malengo na maelekezo ya kifedha ambayo shirika au mtu binafsi anapaswa kufuata. Inatoa muhtasari wa kina kuhusu matarajio ya mapato na matumizi, na hivyo kumwezesha mtu au shirika kupanga kwa ufanisi zaidi juu ya rasilimali zake. Kuweza kwenda sambamba na bajeti hii, mtu au shirika linahitaji kuelewa vizuri vipaumbele vyake na kuweka mipango thabiti kwa kila sehemu ya matumizi au uwekezaji.

Katika kuhakikisha ufanisi, ni muhimu kwa shirika kuwekeza nguvu katika upangaji wa bajeti ulio sahihi, utafiti wa masoko ili kufahamu mwenendo wa kiuchumi unaoweza kuathiri mapato na matumizi, pamoja na uboreshaji wa mbinu za usimamizi wa fedha. Ufuatiliaji wa mara kwa mara wa bajeti na utathminini wa maendeleo halisi ikilinganishwa na yale yaliyopangwa ni muhimu sana. Nguvu katika kufuatilia na kurekebisha mtiririko wa bajeti inaweza kumaanisha tofauti kati ya kufikia malengo ya kifedha au kukabiliana na upungufu.

Kuwekeza nguvu inamaanisha pia kuwa na nidhamu na ufuatiliaji madhubuti wa matumizi ya kila siku, kujifunza kutokana na takwimu na ripoti za awali za fedha, na kujitayarisha kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza. Mwisho, uwekezaji katika mafunzo kwa wafanyakazi wanaoshughulikia fedha na matumizi inaweza kuongeza ufanisi na kuimarisha uzingatiaji wa bajeti iliyowekwa.

Mkalimani alivyoharibu ibada ya leo

Leo nikaamua niingie misa ya asubuhi kwenye kanisa moja la kilokole kulikua na ugeni wa mchungaji kutoka Bulgaria, Mahubiri yameanza saa 1 asubuhi hali ikawa kama hivi:

MCHUNGAJI: My name is Pastor Livingstone
MKALIMANi: Kwa jina naitwa mchungaji Jiwe linaloishi
MCHUNGAJI: We thank God for All goals we set by our hands
MKALIMANI: Tunamshukuru Mungu kwa Magoli yote tuliyoweka kwa Mkono

Hivi navyoongea kanisa halina viti waumini wote tumekimbia nje naona Mkalimani amebaki na kiatu cha kushoto tu.
Sunday joke

Wewe ni mshindi: Mambo yakuzingatia ili uweze kushinda chochote katika maisha

Mshindi ni mtu aliyeshinda, Hivyo wewe ni mshindi kwa kuwa umeshinda, kuwa hai leo ni ushindi, kuwa na Mungu mpaka sasa huo ni Ushindi, kuweza kujifunza semina na kufuatilia mafundisho kama haya wewe ni mshindi.
Ebu jiulize ni watu wangapi ulikuwa unawafahamu leo hawapo duniani? Wewe umeshinda Mungu kakuweka duniani ili uendelee kushinda.

KWANINI WEWE NI MSHINDI

Wanasayansi wanasema wakati ujauzito wa binadamu unatungwa kunakua na mamilioni ya mbegu za kiume ambazo zinakua zinatoka ili kwenda kurutubisha yai ili azaliwe mtoto. Na kwa kawaida inatakiwa mbegu moja tu kati ya hizo milioni. Hivyo basi wewe ni mmoja wa pekee kati ya mbegu za kiume millioni moja zilizotoka siku ile ulipotungwa tumboni mwa mama yako.

JIPIGIE MAKOFI SEMA MIMI NI MSHINDI

Kabla hujazaliwa ingewezekana ujauzito wako ukaharibika, Ingewezekana labda ujauzito wako ungetolewa, lakini haikuwa hivyo ukatoka salama. Na ulipozaliwa kuna watoto wengi tunasikia wanafariki wakati wa kujifungua lakini hukuwa wewe. Tunasikia pia magonjwa mbalimbali yanaua watoto lakini hukuwa wewe. Umeyashinda yote hayo hivyo wewe ni MSHINDI usijidharau kwa hali uliyonayo sasa wewe ni mshindi. Kuwepo kwako hai leo ni kwa sababu maalumu.

Umekwenda shule, umekua ,wako waliokufa kwa ajali lakini wewe upo hai bado Mungu ana kusudi na wewe.

Usijidharau nipo hapa Leo kukonyesha jinsi wewe ulivyo wa thamani mbele za Mungu. Wako wenzako wamepitia hatari ngumu na mateso hadi wakafikia kujinyonga, kunywa sumu, kujiua, lakini wewe upo hai. Wewe ni mshindi.
Upo duniani sasa ili uendelee kushinda.

Umezaliwa na uwezo wa kipekee sana ndani yako unaokuwezesha wewe kushinda kila siku na ukiweza kuutambua uwezo huo ushindi ni lazima. Kabla ya kutambua uwezo huo lazima utambue kwanini wewe umezaliwa! Ulizaliwa kwa kusudi gani? Ili uelewe kwanini Mungu amekuacha hai mpaka sasa ni ili ulitimize kusudi lake.

Hayo Yote niliyokwambia yanaweza yasiwe na maana sana kwasababu yameshapita sasa nakwenda kuzungumza namna ya kuendelea kutengeneza ushindi mwingine kila siku kupitia kwenye kusudi lako!

UFANYEJE UENDELEE KUSHINDA?

Haijalishi hali gani unapitia sasa upo hai leo kwa sababu maalumu na ni ili uweze kuendelea kua mshindi kwa kuifanya dunia kuwa mahali bora zaidi kuliko ulivyoikuta. Hii dunia haikua hivi miaka 10 iliyopita ni watu wachache wametumia uwezo Mungu aliweka ndani yao na kuvumbua mambo mengi na ya ajabu tunayoyaona sasa. Ni nafasi yako wewe kutumia nafasi hii ya kuwa hai leo kuifanya dunia kuwa sehemu salama ya kuishi naamini wewe una nafasi kubwa sana.

“You were born to win, but to be a winner, you must plan to win, prepare to win, and expect to win.” – Zig Ziglar

Zig Ziglar anasema ulizaliwa kushinda kama tulivyoelezana hapo awali, lakini ili uendelee kua mshindi, lazima ujipange kushinda, ujiandae kushinda, na utarajie kishinda

Timu ya mpira inapochukua kombe sio mwisho wa mchezo wanakwenda kujinoa zaidi ili waweze kushinda tena na tena. Wewe unajiandaa vipi na kuendelea kushinda?
Vipo Vitu vichache vya Muhimu unatakiwa uwe unavifanya ili kushinda kila siku.

(a)Jitambue.

Ili uendelee kushinda kila siku lazima ujitambue wewe ni nani! Najua unatambua kwamba wewe ni jinsia gani. Lakini kujua hivyo tu haitoshi.
Kwanini ulizaliwa mwanamke/mwanaume, mtu mweusi tena Tanzania na sio nchi nyingine?
Ukitambua hivyo lazima ukubali na uanze kufanyia kazi na uendelee kushinda kila siku, Tambua kusudi la wewe kuzaliwa na kwanini ukazaliwa kipindi hiki na sio wakati mwingine.

(b) Usiangalie nyuma.

Haijalishi umepitia maisha ya namna gani umezaliwa kwenye mazingira ya namna gani, wewe jua kusudi la Mungu ndani yako na ulifanyie kazi, haijalishi jana umefanya vibaya kiasi gani, haijalishi pia ulifanya vizuri kiasi gani angalia mbele angalia kule unakokwenda.
Kule unakokwenda kuna maana zaidi ya unakotokea. Pia huwezi kwenda mbele huku umeangalia nyuma utajikwaa. Haijalishi ulikosea mara ngapi, umeua, umeachwa, umefeli, huna kazi, umefukuzwa, una madeni, usiyaangalie hayo.
Kama umeshajitambua liangalie kusudi na songa mbele.
“Adui wa mafanikio yako ya leo ni mafanikio yako ya jana, Adui wa mafanikio yako ya kesho ni mafanikio ya leo”

(c) Jua unapokwenda.

Hakikisha umetambua unapokwenda kama tayari umeshajitambua na umeacha kuangalia nyuma hakikisha sasa unajua unapoelekea. Kuwa na Maono, ndoto kubwa na kua na viongozi wanaokufundisha uelekee kwenye maono yako.Ukijua unapokwenda huwezi kupotea, Ukijua unapokwenda huwezi kufanya mambo ya ajabu ajabu, ukijua unapokwenda huwezi kuchukuliwa na kila mtu hovyo hovyo, Ukijua unapokwenda lazima utajisitiri, Biblia inasema pasipo maono watu huacha kujizuia.
Kama huna maono kulijua kusudi hakuna maana, kama huna maono utadondoka kila siku.

(d)Jifunze Kila Siku.

Umeshajitambua, ukaacha kuangalia nyuma, ukajua unapokwenda kwa kuwa na maono na ndoto kubwa, sasa huwezi kuvifikia vyote hivyo bila kujifunza. Huwezi kwenda kuwa mtu mkuu kwa ufahamu huo ulio nao sasa hivi, Inawezekana umesoma vyuoni una Degree au Masters lakini hiyo haionyeshi vyema kwamba wewe umesoma unajua kila kitu unaweza kuyabeba maono makubwa.
Soma vitabu vya uongozi, vitabu vya kuhamasiha jiendeleze binafsi, Jifunze kwa kupitia watu unaokutana nao kila siku, Jiunge na magroup kama ya whatsapp na ujifunze Makala kama hizi.

USHINDI UTAKUA WAKO KILA SIKU

“adui mkubwa wa kujifunza ni kujua” unapojiona wewe unajua kila kitu umesoma sana huwezi kujifunza kwa mtu mwingine alieko chini yako unakosea sana na hutaweza kufika popote kubali kujifunza kwa kila mtu haijalishi ni nani. Ushindi ni wako Na naamini kabisa kupitia makala hii kutatoka watu wakubwa sana katika Historia ya nchi hii na dunia.

(e) Jitengenezee tabia za Kushinda.

Unajitengenezeaje Tabia za kushinda? Jiambie maneno ya kushinda,huonagi wachezaji huwa wakiwa kwenye mazoezi wanashangilia kama vile tayari wana ushindi?
Jiambie maneno ya kujihamasisha mwenyewe. Mimi ni mshindi nimezaliwa kushinda, Siziogopi changamoto, mimi ni wa thamani, Unaweza kuandika maneno mazuri ya kukuhamasisha ukutani ili unapolala na uamkapo asubuhi uyaone na kuyasoma.
Washindi wana amka mapema. Washindi wanajua ndoto zao vizuri. Hakikisha kile unachokitaka kimekaa kwenye akili yako yaani hata ukishtuliwa usingizini leo unakuwa na uwezo wa kukisema.
Anza kufanyia kazi yale unayojifunza kila siku.

(F) Usiogope Kushindwa.

Usiziangalie changamoto na kukata tamaa. Zitumie changamoto kama shule jifunze kwa kupitia hizo na utaendelea kushinda kila siku.
Changamoto zinakuja kwasababu njia unayoiendea ni nyembamba hujawahi kuipita kabla. Na pia bado uwezo wako haujakuwa vya kutosha tumia changamoto kama njia za kukuza uwezo wako ili siku moja ufikie kule unakotaka ukiwa imara na usitetereke.

(g) Fanya vitu unavyoviogopa.

Usikubali kila siku unafanya vitu vile vile. Hakikisha kila siku kuna kitu kipya umefanya. Hii itakuongezea wewe uwezo wa kushinda na ujasiri wa kupita sehemu za mbele zaidi.
Hakikisha inapokua jioni umeangalia ni vitu gani vipya umefanya. Ni hatua gani umepiga katika malengo yako. Ni kitu gani kipya umejifunza. Usikubali unakutana na mtu anakupita hivi .Hujaongeza kitu chochote kwenye ufahamu wako au yeye hajajifunza kitu kutoka kwako. Wewe una kitu cha pekee sana ndani yako ambacho Mungu kakiweka kwa ajili ya wengine.

(h) Fanya na fuatilia zaidi vitu vinavyoongeza thamani kwako, kwa wengine, kwenye roho yako, kwenye mahusiano yako, kwenye maono na malengo yako na kwenye kusudi lako.

Ukifanya nje ya hapo utakua unapoteza muda bure. usikubali kupoteza siku yako bure. Kumbuka tumepewa masaa 24 tu ya kuishi yatumie vyema masaa hayo.

UKIWEZA KUFUATILIA HAYA USHINDI NI WAKO KILA SIKU, NI MAMBO MADOGO MADOGO UTAPITIA TU NA YANAREKEBIKA.

“Hakuna kiumbe kingine kitakachozaliwa tena kifikiri kama wewe, kitembee kama wewe, kiongee kama wewe, Hakuna tena, wewe ni wa pekee sana usijidharau tumia upekee huo kufanya mambo makubwa katika dunia hii usikubali kuondoka hivi hivi.”

“Hamu Yangu Ni Kuona Unafanikiwa”.

Shopping Cart
1
    1
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About