Kiingereza kinashida kweli, Angalia alichokisema huyu mwalimu
Kiingereza shidaaaa……!
Mwalimu wa chakula alipokuwa anaongea na wapishi akiwaeleza maharage kutoungwa vizur
Kiingereza shidaaaa……!
Mwalimu wa chakula alipokuwa anaongea na wapishi akiwaeleza maharage kutoungwa vizur
Kukoroma ni tatizo linalowapata watu wengi wakati wanapolala ambalo linaweza kuwatokea watu wa kila umri ingawa hutokea mara nyingi kwa wanaume au watu wanene. Kukoroma huzidi kwa kadri umri unavyoongezeka na asilimia 54 ya watu wazima hukoroma baadhi ya wakati huku asilimia 25 ya wengine wakiwa na tabia ya kukoroma kila wakati. Kukoroma baadhi ya wakati kwa kawaida sio tatizo kubwa na mara nyingi huleta tu karaha kwa mtu anayelala karibu na mkoromaji.
Hata hivyo kukoroma huko sio tu kwamba huharibu usingizi wa anayekoroma bali pia huwasumbua na kuwakeresha wanaolala karibu na mkoromaji. Wale wenye tabia ya kukoroma, hukoroma kila wanapolala na mara nyingi huchoka wanapoamka, na watu wa aina hii hushauriwa kumuona daktari na kushauriwa kuhusiana na tatizo hilo. Lakini kabla hatujaendela mbele ni bora tujue kukoroma hasa ni nini au hutokea vipi?
Mtu huwa anakoroma pale kunapokuwa na kitu au sababu yoyote itakayoziba kuingia au kutoka kwa hewa mdomoni na katika pua. Kuta za koo hutikisika wakati wa kupumua na matokeo yake ni sauti inayosikika ya kukoroma. Kuingia au kutoka kwa hewa huweza kuzuiwa na sababu mbalimbali kama vile:
• Kuziba tundu za pua kusiko kamili ambako husababisha nguvu zaidi zitumike katika kupitisha hewa kwenye pua wakati mtu akiwa amelala. Kitendo hicho hupelekea nyama laini za pua na koo zijikusanye na kusababisha mkoromo.
Kuna baadhi ya watu wanakoroma tu kipindi cha allergy (allergy season) au wanapatwa na matatizo ya sinus. Baadhi ya matatizo kama vile kupinda pua (deviated septum) au ukuta unaotenganisha tundu za pua na polyps za pua pia huweza kufanya pua zizibe na kusababisha kukoroma. Watu wengi wanaofanya operesheni za pua pia hupatwa na tatizo la kukoroma.
• Kuwa na misuli dhaifu katika koo na ulimi. Misuli au nyama za koo na ulimi zinapokuwa dhaifu sana hulegea na kuanguka upande wa nyuma wa sehemu inayopita hewa. Suala hilo hutokea pale mtu anapolala fofofo au kuwa na usingizi mzito na kusababisha kukoroma.
• Kuwa na misuli minene ya koo. Hii ni kwa wale watu wanene ambao hata nyama zao za koo pia hunenepa na kupanuka na suala hilo husababisha kukoroma, Pia watoto wenye tonsesi kubwa na adenoids baadhi ya wakati hukoroma.
• Kuwa na kilimi kikubwa ni mojawapo ya sababu zinazosababisha kukoroma. Kilimi kirefu kinaweza kuzuia koo na pale kinapotikisika wakati hewa inapita kwa msukumo husababisha kukoroma.
• Sababu nyinginezo zinazoweza kumsababishia mtu akorome anapolala ni kuwa na umri mkubwa au uzee, imeshuhudiwa kuwa watu wa makamo na wazee hukoroma, kwani misuli na nyama za koo huanza kuzeeka na kulegea kadri umri unayoongezeka. Vilevile wanaume wanakoroma zaidi kuliko wanawake hii ni kutokana na wanaume kuwa na njia nyembamba zaidi ya hewa kuliko wanawake.
Kukoroma pia kunaweza kuwa ni tatizo la kurithi. Pombe, kuvuta sigara na matumizi ya baadhi ya dawa pia husababisha misuli ya koo ilegee na hivyo hupelekea mtu akorome. Kulala vibaya pia husababisha kukoroka kama vile kulala kichalichali, kwani hufanya nyama za koo zilegee na kuziba hewa.
Swali hilo limeulizwa sana na mimi katika kulijibu ningependa kusema kuwa, kujua sababu inayosababisha mtu akorome na kuitatua au kuiondoa sababu hiyo ndiko kunakotibu kukoroma.
Sote tunajua adha inayotokana na kukoroma, na sauti hiyo inavyosumbua hasa iwapo anayekoroma ni mtu wako wa karibu kama vile mumeo, mwenzi wako au yoyote yule inayekubidi ulale naye karibu au katika kitanda kimojana hata chumba kimoja. Kukoroma pia huathiri usingizi wa mkoromaji kwani anayekoroma humbidi aamke mara kadhaa usingizini akijua au bila kujua kutokana njia zake za hewa kufunga kwa sekunde kadhaa ambapo usingizi pia hukatika.
Wanaokoroma pia hushindwa kulala vizuri suala linalopelekea asubuhi wawe wamechoka na kutofanya majukumu yao vyema, na pia wale wanaolala nao karibu hupatwa na matatizo kama hayo. Vilevile tunapaswa kujua kuwa kukoroma kuna athari za kiafya za muda mrefu kwa mtu anayekoroma hivyo si jambo la kufanyia mzaha na ni tatizo ambalo linapaswa kushughulikiwa na kutatuliwa.
Wataalamu wanatuambia kuwa ili kujua kukoroma kwako kunasababishwa na nini ni bora ushirikiane na mwenzi wako au yoyote unayelala naye ili akuchunguze pale unapolala na kujua jinsi mwili wako unavyokuwa pale unapokoroma.
1. Kufunga mdomo na kukoroma kunaonyesha kuwa kuna matatizo ya ulimi.
2. Kufungua mdomo na kukoroma kunaonyesha unaweza kuwa na tatizo katika misuli au nyama za koo.
3. Kukoroma unapolala kichalichali kunaonyesha kuwa pengine kwa kubadilisha namna unavyolala kukoroma nako kunaweza kwisha.
4. Kukoroma wakati unapolala kwa kila mlalo kunaonyesha kwamba tatizo lako ni kubwa na pengine kunahitajia tiba kubwa zaidi.
Iwapo umebadilisha namna unavyolala na haikusaidia, unashauriwa ujaribu yafuatayo:
Kuwa na pua iliyoziba hufanya kupumua kuwe kugumu na kusababisha kukoroma. Unaweza kufanya hivyo kwa kutumia dawa za kusaidia kupumua kwa urahisi (nasal decongestants) zinazopatikana kwa urahisi katika maduka ya dawa.
Kunyanyua kichwa kwa nchi 4 huweza kupunguza kasi ya kupumua na kusaidia ulimi na taya kwenda mbele hali ambayo hupunguza kukoroma. Fanya hilo kwa tumia mito maalum ya kupunguza kukoroma au lala bila mto.
Wataalamu pia wanasema kwamba unaweza kupunguza kukoroma kwa kutokula baadhi ya vyakula au dawa kabla ya kulala ambavyo huongeza kukoroma. Vitu hivyo ni kama vile;
Vilevile wanaokoroma wanashauriwa kufanya mazoezi ya koo ambayo ni pamoja na kuimba, kusoma kwa kurudia rudia voweli (a,e,i,o,u) kwa nguvu kwa dakika tatu mara kadhaa kwa siku, kuweka ncha ya ulimi chini ya meno ya mbele na kurudisha ulimi nyuma kwa dakika 3 kila siku au huku mdomo ukiwa wazi pelekea taya yako upande wa kulia na wacha ibakie katika hali hiyo kwa sekunde 30.
Huku mdomo ukiwa wazi, kaza misuli ya nyuma ya koo na rudia kitendo hicho kwa sekunde thelathini. Unaweza kutizama kwenye kioo na kuona jinsi kilimi kinavyokwenda juu na chini.
Iwapo kukoroma hakutoisha kwa kutumia njia hizo tofauti zilizoelezwa, usife moyo jaribu kumuona
Daktari na akupe ushauri wa kitiba kuhusiana na tatizo hilo. Madakatari wataalamu wa magonjwa ya pua, masikio na koo au ENT wanaweza kukusaidia zaidi kutatua tatizo hilo. Siku hizi kuna vifaa mbalimbali vinavyotumiwa mahospitalini ili kuondoa kukoroma kama vile kifaa kinachowekwa kwenye meno, CPAP, kidude kinachowekwa mdomoni au hata kufanyiwa operesheni ili kuondoa tatizo hilo.
++ TIBA YA MBADALA YA KUACHA KUKOROMA
Dawa ya kukoroma Fanya hivi: Fungua mdomo wako mpaka mwisho, toa ulimi na usukume nje mpaka mwisho, rudisha ulimi ndani mpaka mwisho-rudia mara 20. Ukimaliza utahisi kuna misuli nyuma
na pembeni ya koo umeifanyisha kazi,sasa misuli hii ikilegea ndio inayosababisha kukoroma. Fanya zoezi hili mara 2 mpaka 3 kwa siku na tatizo hili litaisha baada ya siku 10-20 kutegemea mtu hadi mtu.
Siku hizi kuna tangazo moja la kampuni ya simu za mikononi, Tigo, likimuonesha mama akiwa _busy_ na pembeni yupo mwanae mdogo apo akijisemesha na akatamka maneno ambapo mama akaona ni kama ameanza kuongea. Kwa furaha anampigia simu mumewe akimtaka amsikilize mwanae akiongea. Hapo mama anamtaka mwanae aseme “mama” na baba naye anavutia kwake akimtaka aseme “baba”. Kwa maajabu kabisa mtoto anawapotezea wote na kutamka “ni Tigo peesa”. Wazazi wakashikwa na butwaa lakini huku wakitabasamu.
Ukiitazama vizuri kazi ya ubunifu iliyotumika katika tangazo hili unaweza kupata funzo, pamoja na mengine, kwamba mtoto alikua na chaguzi lake ambalo ni tofauti na yale ambayo wazazi walikua wamempa. Lakini zaidi, pamoja na kuwa amekuwa na chaguzi lake binafsi, pasipo kufuata alichoagizwa na baba au mama, bado wazazi wanatabasamu kwani wanaona mwanao kafanya jambo jema.
👉Unaona unavyofanya kazi bila furaha kwa kua ulifanya chaguo la kazi hiyo kwa kusikiliza ndugu au marafiki.
👉Unaona unavyo _struggle_ katika biashara kwani halikua chaguo lako bali ni la ndugu au marafiki
👉Unakumbuka ulivyoshindwa kusomea kile unachopenda kwa kusikiliza ndugu au marafiki
9
👉Unakumbuka ulivyoshindwa kuishi na yule mwenzi uliyempenda na mkapendana naye kwa kusikiliza ndugu na marafiki
Unaweza kushauriwa, na ushauri ukawa ni mzuri kabisaa na ukaona ni vyema uufuate kwa kua hata wewe umeambiwa na ukachanganya na akili yako ukaona inafaa.
Jana nilitoa semina kwa wanafunzi wote wa Shule ya Sekondari Chang’ombe, pamoja na mambo mengine nikawataka kupima sana marafiki walio nao na kuona kama ni washauri wazuri na kama sivyo waachane nao na kuwa na marafiki wapya wenye mawazo chanya ya kuwasaidia kutimiza ndoto zao.
Kuna hii daladala imeandikwa nyuma *_Marafiki wengi mjini hasara_*. 😃. Mie nakuambia sio marafiki tu, hata ndugu pia. Kikubwa ni kuwapima wale ulio nao karibu na kuona kama bado ni wa msaada kwako. Wapime na chukua hatua. Kumbuka Mheshimiwa JK aliwahi kutuasa ” _Akili za kuambiwa, changanya na za kwako_ “.
Unga 2 Viwili
Sukari ya kusaga 1/4 Kikombe
Siagi 250 gms
Jam kisia
Ufuta Kisia
Vanilla 1 kijiko cha chai
1. Tia kwenye mashine ya kusaga (blender) au mashine ya keki, siagi, yai, sukari na vanilla uchanganye hadi ichanganyike vizuri.
2. Tia baking powder, na unga na changanya kwa mkono vizuri.
3. Paka siagi sinia ya kupikia ya oveni.
4. Tengeneza viduara vidogo vidogo.
5. Bonyeza kila kiduara katikati kwa kidole, kisha weka jam, halafu juu yake paka mayai na unynyuzie ufuta.
6. Pika katika moto wa chini 350ºF kwa muda wa dakika 20-25.
7. Tayari kwa kuliwa.
Mchele 3 vikombe
Nyama ya kusaga 1 LB
Mchanganyiko wa Nafaka (upendavyo) 1 kikopo
(maharagwe, njegere, mbaazi, na kadhalika)
Vitunguu maji kata vipande vipande 3 vya kiasi
Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi 2 vijiko vya supu
Mafuta ½ Kikombe
Mchanganyiko wa bizari (Garam Masala) 2 vijiko vya chai
Vipande vya supu (Maggi cubes) 3
Maji (inategemea mchele) 5
Chumvi Kiasi
1) Osha mchele na roweka.
2) Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitunguu mpaka viwe brown.
3) Tia Thomu na tangawizi, kaanga kidogo.
4) Weka nyama ya kusaga, chumvi na garam masala, endelea kukaanga mpaka nyama iwive.
5) Mwaga maji yaliomo katika kopo la nafaka na utie nafaka pekee humo.
6) Tia maji na vipande vya supu (Maggi cubes) huku unavivuruga, koroga kidogo.
7) Tia mchele, koroga kidogo.
8) Funika na pika kwa moto mdogo mpaka karibu na kukauka ukikorogoka kidogo. (kama unavyopika pilau ya kawaida)
9) *Epua uipike katika moto wa oven 350-400 Deg kwa muda wa dakika 15.
*Kama sufuria uliyotumia sio ya kupikia katika oven, mimina katika chombo chochote kinachotumika kwa oven kama bakuli la pyrex au treya za foil.
10) Pakua katika sahani na iko tayari kuliwa.
Rafiki yangu, Omba utafute uso wa Mungu, Aonaye kwa Siri atakujibu kwa wazi.
Mungu hujibu na kutupa kile kilicho muhimu na kizuri kwetu kwa wakati huo.
Vivyo hivyo Mungu hutupa Kile kilicho bora na sio tunachokitaka.
Uwezo wa Mungu ni mkuu na anaweza kutupa chochote tunachoomba.
Mtumainie Mungu kila wakati.
Rafiki yangu, omba utafute uso wa Mungu, kwa maana yeye aonaye kwa siri atakujibu kwa wazi. Mungu ni mwaminifu sana, hasa kwa wale wanaomwomba bila kukoma na kwa matumaini. Mungu husikia sala zetu zote na kuzijibu kwa hekima na upendo. Tunapomwomba Mungu kwa imani na uvumilivu, anatupa kile kilicho bora kwetu kwa wakati wake mwafaka.
Biblia inatufundisha kwamba Mungu husikia na kujibu maombi yetu. Yesu alisema katika Mathayo 6:6:
“Lakini wewe, uombapo, ingia katika chumba chako cha ndani, kisha funga mlango wako, uombe kwa Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujibu kwa dhahiri.” (Mathayo 6:6)
Mungu anapenda tuombe tukiwa na moyo wa unyenyekevu na uaminifu. Sala zetu zinazotoka moyoni humfikia Mungu, na kwa upendo wake mkuu, anatupatia majibu kwa njia ambazo ni bora kwetu.
Mungu ni mwaminifu sana kwa wale wanaomwomba kwa matumaini. Biblia inasema katika 1 Yohana 5:14-15:
“Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kwamba, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Nasi tukijua ya kuwa atusikia katika lolote tuombalo, twaijua kwamba tumevipata vile vitu tulivyomwomba.” (1 Yohana 5:14-15)
Tunapoomba kwa kuzingatia mapenzi ya Mungu, tunakuwa na uhakika kwamba Mungu atasikia na kutujibu.
Mungu hujibu maombi yetu kulingana na hekima yake kuu. Wakati mwingine tunapomwomba Mungu vitu fulani, hatupokei majibu tunayotarajia. Hii ni kwa sababu Mungu anajua zaidi kuhusu kile kilicho bora kwetu kuliko tunavyojua sisi wenyewe. Kama vile mzazi anavyomkatalia mtoto wake kitu hatari kwa ajili ya usalama wake, ndivyo Mungu anatupa kile kilicho bora zaidi kwetu. Yesu alisema katika Mathayo 7:9-11:
“Au ni nani miongoni mwenu, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe? Au akimwomba samaki, atampa nyoka? Basi, ikiwa ninyi, mlio wabaya, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba yenu aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa mema wao wamwombao?” (Mathayo 7:9-11)
Mungu, kwa hekima yake isiyo na kipimo, anatupatia kile kilicho bora zaidi kwa maisha yetu. Anajua mahitaji yetu halisi na hutupatia yale yatakayotusaidia kukua kiroho na kufanikisha kusudi lake maishani mwetu.
Mungu ana uwezo mkuu na anaweza kutupa chochote tunachoomba. Yesu alisema katika Marko 11:24:
“Kwa hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.” (Marko 11:24)
Tunapomwomba Mungu kwa imani, tukiwa na uhakika kwamba atatupatia tunachohitaji, tunaweza kuwa na amani na utulivu tukijua kwamba Mungu anasikia na kujibu maombi yetu.
Kwa upendo wake usio na mfano, Mungu anatupatia vile vilivyo vizuri kwetu. Warumi 8:28 inasema:
“Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.” (Warumi 8:28)
Mungu anafanya kazi kwa pamoja na sisi ili kutupatia mema. Hata wakati hatuelewi kwa nini maombi yetu hayajajibiwa kama tulivyotaka, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu anafanya kazi kwa ajili yetu, akituandalia mema makubwa zaidi.
Tunapaswa kumtumainia Mungu kila wakati, tukijua kwamba yeye anajua mahitaji yetu na anafanya kazi kwa ajili yetu. Mithali 3:5-6 inasema:
“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.” (Mithali 3:5-6)
Kumtumainia Mungu kwa moyo wetu wote inamaanisha kumwomba, kumtegemea, na kuamini kwamba anafanya kazi kwa ajili yetu kila siku. Mungu ni mwaminifu na anataka tuishi maisha ya furaha na amani, tukijua kwamba anatupatia kila tunachohitaji kwa wakati wake mwafaka.
Rafiki yangu, omba utafute uso wa Mungu, kwa maana yeye aonaye kwa siri atakujibu kwa wazi. Mungu ni mwaminifu sana hasa kwa wale wanaomwomba bila kukoma na kwa matumaini. Mungu husikia sala zetu zote na kuzijibu kwa hekima na upendo. Uwezo wa Mungu ni mkuu na anaweza kutupa chochote tunachoomba. Lakini kwa upendo wake usio na mfano, anatupa kile kilicho bora zaidi kwetu. Mtumainie Mungu kila wakati na utaona mema yake yakitimia katika maisha yako.
Tezi dume kila mwanaume anazaliwa nayo ambayo inasaidia kutoa maji maji ambayo yanaweza kusaidia kutengeneza mbegu za kiume.
Maji maji hayo yana alkaline ambayo husaidia Wakati Wa tendo la ndoa asidi (acid) iliyopo Kwa mwanamke isiue mbegu za kiume.
Kwahiyo alkaline ikichanganyika na asidi tunapata neutral na hivyo kusaidia mbegu za kiume zisife zinapoingia Kwa mwanamke.
Kwenye uke kuna asidi ambayo inaua kila bacteria wanaoingia.
Acid+base=salt+water
Tezi dume endapo itakuwa zaidi ndo huweza kuleta madhara ambayo ni kufunga mkojo usitoke kwani hubana mrija unaotoka kwenye kibofu kwenda nje.
Tatizo hilo huwakumba zaidi wanaume zaidi ya miaka 50,60,80 japo sio wote.
Kinga yake.
1. Kunywa maji ya kutosha.
2. Kupunguza kula nyama nyekundu.
3. Kupunguza ulaji wa mafuta.
4. Kula matunda na mbogamboga.
5. Kushiriki tendo la ndoa angalau Mara moja au mbili Kwa wiki ili kupunguza maji maji kwenye tezi dume.
6. Kufanya mazoezi ya viungo.
Kwahiyo tezi dume ni kiungo ambacho wanaume huzaliwa nacho isipokuwa kinaleta madhara endapo kitakuwa kupita kiasi na hutibiwa na kupona.
Matibabu yake ni kufanya upasuaji na kupunguza ukubwa pamoja na kudhibiti homoni za ukuaji wake.
Tiba nzuri ya tezi dume ni kufuata ushauri hapo juu na si vidole
JE WAJUA?
Sungura, panya na Jamii zao huwa na mwendo wa kukimbia na kuruka muda wote na umri wao wa kuishi ni miaka 15. Kobe ni mnyama mwenda pole, asiye na papara wala pilika, muda mwingi hujificha na kupumzika ndani ya jumba lake akikwepa maadui. Umri wa kuishi kobe hufikia hadi miaka 300.
FUNZO: Mazoezi ni kiinimacho na uongo mtupu. Jipumzikie mwaya!!!
🏃🏾🏃🏿
Nimeona leo nitoe darasa kidogo kuhusu mavazi sababu na mimi ni kipaumbele changu katika maisha.
Wakati unamatch mavazi jitahidi kupunguza idadi ya rangi, rangi 3 tu zinatosha kukutoa bomba.
Mtu mjanja anajua kubadilika kulingana na mazingira, sio kuvaa jezi la Man utd lenye jina la Wazza kwenye sherehe
-Marufuku kuvaa oversize/undersize
-Usivae mlegezo
-Hakikisha singlet haionekani
-Usivae mkanda mrefu
-Usivae makubanzi/sandals
-Hakikisha unavaa soksi fupi zisizoonekana
-Piga raba au makubanzi/sandals bila soksi
-Haipendezi kuchemekea
Shati nyeupe ni nzuri kama unaijulia wakati unanunua hakikisha ina urembo wa aina yoyote ile au ni ya kimtindo sio kuvaa shati la shule
Mwanaume yoyote yule wa kijanja anajua umuhimu wa suruali nyeusi sababu inamatch mashati ya rangi nyingi.
-Kama umevaa jeans/kadet unaruhusiwa kuvaa saa ya aina yoyote
-Kama umevaa suti/suruali ya kitambaa epuka kuvaa saa ya mkanda wa plastic.
Duh hapa pagumu kidogo lakini cha msingi zingatia muundo wa kichwa chako pamoja na aina ya macho uliyonayo na aina ya pamba ulizovaa pia.Sio umepiga jeans kali,kichwa kama madenge na macho kama bundi kisha unapiga miwani ndogo ya njano,ni
Kofia pia huongeza mvuto,chagua kofia kulingana na aina ya kichwa na mavazi uliyovaa,haipendezi kuvaa suti na kapelo.Kanzu sharti ivaliwe na barakashia ndo utaeleweka la sivyo ni sawa na kuvaa dera tu
-Usivae mkanda mrefu km vile umefunga nyoka kiunoni
-Mikanda ya vitambaa au madoidoi inafaa kuvaliwa na jeans/kadeti/kaptula
-Jitahidi mkumatch rangi ya mkanda na viatu kama umevaa nguo za kuchomekea
-Zingatia upana wamkanda na rux za nguo yako
Mikufu ya kiume pia huongeza mvuto
-Kama umevaa nguo za kuchomekea au suti itapendeza ukivaa cheni ndogo ambayo haitokezi nje ya shati
-Kama umepiga pamba za kishua mfano T.shirt na jeans hapa tupia cheni kubwa lakini hata cheni ndogo zinakubali
-Vaa kulingana na urefu wako
-Kama wewe mwembamba inapendeza kuvaa tie nyembamba
-Jitahidi kumatch tie na rangi ya shirt/suruali
-Hakikisha tie yako imefungwa vizuri shingoni
Wanaume wajanja wa mjini hupenda kupiga t shirt na jeans na chini kutupia raba Kali…..Vazi hili lina mvuto wa aina yake hasa likivaliwa kitaani na sehemu za mitoko kama vile kwenye Club za starehe.
Hapa pia Kuna changamoto
-Usivaa suruali ya kitambaa na Raba
-Usivae suruali ya kuchomekea na makubanzi
-Ukipiga jeans unaweza kumatch t.shirt/shirt na rangi ya viatu
-Ukivaa suti yakupasa upige kiatu kikali ….ulikosea itakuwa sawa na Toyota Mark X yenye matairi ya Fuso !!!
Safisha vyombo vya kulishia na kunyweshea kila siku. Osha, sugua vizuri, kisha suuza kuondoa utando unaobeba bakteria.
Kuku wanahitaji wapewe chakula cha kutosha na chenye virutubisho vyote. Unaweza kuwaongezea majani, makombo, nafaka, mchanga laini, au maganda ya mayai.
Wapatie kuku maji safi muda wote. Wafugaji wengi wameripoti kuwa na matokeo mazuri baada ya kuchanganya dawa ya kuua vimelea kwenye maji ya kunywa.
Nunua chakula kwa wauzaji wazuri na wanaoaminika ili kuepuka minyoo na sumu hatarishi. Usiwape kuku chakula chochote kinachoonekana kuoza au kunuka uvundo.
Hifadhi chakula cha kuku katika sehemu kavu isiyo na joto na isiwe kwa zaidi ya miezi mitatu ili kuepuka kuharibiwa na fangasi.
Kuna mambo mengi ya kufanya ili tuwe watu wa kuvutia kila wakati.Mpangilio wa mavazi hufanya mtu kuonekana maridadi.
Kama wewe ni mvaaji wa tai unapovaa unazingatia mambo yapi? Na je unafunga tai yako kwa namna inayokubalika?
Wengine huwa hawafahamu jinsi ya kufunga tai na hivyo kuleta mushkeri wakati wa kuvaa tai na kusababisha tai kukaa upande. Unapoamua kuvaa tai na shati ambalo halijanyooshwa ambalo linakuwa kwenye mikunjo au kuvaa tai na ndala unakuwa umeua maananzima na kulivunjia heshima vazi hili.
Tai ni vazi lawatu walio maridadi kama huwezi kuwa maridadi basi vazi hili halikufai kabisa.
Unapovaa taa unatakiwa kuzingatia aina ya umbo lako kama wewe ni mnene vaa tai inayoendana na mtu mnene na kama wewe ni mwembamba basi vaa tai inayoendana na mtu mwembamba.
Kuna wengine huvaa tai zinazofika magotini na kuwa kichekesho anapopita mtaani
Tai ni vazi ambalo huongeza heshima na hadhi ya mvaaji cha muhimu ni jinsi gani unavaa tai yako na ikiwezekana jaribu kumechisha tai na suruali kwa vile ili tai upendeze ni laima iendane na nguo unayovaa.
Ni vyema ukahakikisha kuwa unakuwa na tai zenye rangi tofauti ambazo zitaendana na nguo unazovaa.
Zuzu kaniuliza, “Anko, unajua vitu vinavyoanzia na K ni vitamu sana.”
Nikashtuka, “Astaghafilulah we mtoto! Niondolee wehu wako hapa!”
Zuzu akatabasamu. Akaendelea kuongea kabla sijafanikiwa kumzuia. “Kweli kabisa anko. Vitu vinavyoanza na K ni vitamu sana kwa mfano kuku, kalimati, keki, kabab, katleti, kashata, kisheti na karoti.”
Nikashusha pumzi. “Ahaa! Kumbe ndo hivyo, ni kweli!”
Zuzu akanitupia swali. “Kwani we anko ulidhani nini?”
“MAENEO FLANI ya KISHUA”
-Mshikaji kamwona demu mkali
anakatiza kitaa akamkubali akaamua
amfuate amtemee cheche
MSHIKAJI- mambo dada?
DEMU- pouwa
MSHIKAJI-
umependezaa!!!
DEMU- asante.
MSHIKAJI- unaweza ukanisaidia
namba
yako ya simu……..
maana duh
nmekukubali
kinyama.
Demu baada ya kuambiwa vile
akazama kwenye pochi lake akatoa
noti ya
sh.10000 akaandika namba yake
kwenye
noti akampa mshikaji.
Mshikaji kapokea ile noti kachana
sehem
iliyoandikwa namba halafu
kamrudishia
Demu noti yake..!!!
NANI ANA DHARAU
NA NANI JEURI..
DEMU AU MSHIKAJI??!
Tatizo hili husimama lenyewe kama ugonjwa ingawa pia inaweza kuwa ni dalili kama mwanamke ni mjamzito, ananyonyesha au ametoa mimba au ameharibikiwa na mimba. Kusimama kwake kama ugonjwa ni pale yanapotoka wakati mwanamke hana historia ya dalili hizo hapo juu.
Tatizo hili huwapata wanawake wengi na kwa mujibu wa takwimu huathiri asilimia tano hadi 32 ya wanawake walio katika umri wa kuzaa. Pamoja na kuwapata zaidi wanawake, hali ya kutokwa na majimaji katika matiti pia huweza kuwatokea wanaume watu wazima, vijana walio katika umri wa balehe, wa kike na wa kiume, watoto wachanga wa kike na wa kiume.
Matiti yanaweza kutoa majimaji endapo chuchu zitachezewa au kunyonywa mara kwa mara na kusababisha kuvuruga baadhi ya homoni mwilini.
Homoni zinazohusika zaidi na tatizo hili ni homoni ya ‘prolactine’.
Vilevile katika hali hii ya kutokwa na majimaji asilimia 50 ya matatizo chanzo chake bado hakijulikani.
Mama anayenyonyesha homoni zinazochangizwa na kusababisha matiti yatoe maziwa ni ‘Prolactin’, Estrogen’ na Progesterone.
Dawa nyingine zinazoweza kumfanya mtu atokwe na majimaji katika matiti ni dawa kama Methyldopa, madawa ya kulevya na dawa za magonjwa ya akili.
Pamoja na matatizo katika mfumo wa homoni, hali ya kusuguasugua kifua mara kwa mara, hali ya kuwa na hofu na wasiwasi au shauku f’lani, mfano ya kuhitaji kupata ujauzito husababisha kuamsha homoni za uzalishaji wa maziwa au hayo majimaji.
Vyanzo vingine ni matatizo kichwani kwenye tezi ya ‘pituitary au pituitary adenoma’.
Dawa nyingine zinazoamsha tatizo hili ni kama vile ‘Cimetidine’ ambazo hutibu vidonda vya tumbo.
Pia zipo dawa nyingine za asili ambazo hazijafanyiwa utafiti wa kutosha zinazoweza kusababisha tatizo hili.
Mwanamke mwenye tatizo hili la kutokwa na maziwa kwenye matiti wakati si mjamzito na wala hana historia ya kuwa na mimba, huwa hapati ujauzito.
Mwanaume mwenye tatizo hili hupungukiwa na nguvu za kiume, uzalishaji wa mbegu za kiume huwa mdogo.
Kwa vijana na watoto wa kiume au wa kike ni vema uchunguzi wa kina ufanyike.
Maziwa yanaweza kutoka tu yenyewe au kwa kuminyaminya matiti au chuchu.
Hufanyika hospitalini kwa madaktari wa masuala ya uzazi. Vipimo vya damu kuangalia homoni, matatizo katika matiti, na ikibidi CT-Scan vitafanyika kuangalia matatizo katika tezi ya Pituitary.
Wahi hospitali kwani athari ya tatizo hili ni kupoteza uwezo wa kuzaa.
Epuka kuchezea chuchu ziwe zako mwenyewe au za mpenzi wako au za mtoto kwani unaamsha homoni ambazo katika wakati huo hazitakiwi.
Mchele (rice 1/2 kilo)
Maharage yaliyochemshwa (boiled red kidney beans 1 kikombe cha chai)
Samaki waliokaangwa ( 2 fried fish)
Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2 ya tin)
Vitunguu vilivyokatwa (onion 2)
Kitunguu swaum (garlic 3 cloves)
Tangawizi (ginger kiasi)
Limao (lemon 1/2)
Chumvi (salt)
Pilipili (scotch bonnet pepper 2)
Mafuta (vegetable oil)
Spinach
Tui la nazi (coconut milk 1 kikombe cha chai)
Saga nyanya, kitunguu, tangawizi na kitunguu swaum pamoja. Tia kwenye sufuria na upike mpaka maji yakauke kisha tia curry powder, mafuta na chumvi na upike tena mpaka mchanganyiko uive kisha tia samaki na limao na maji kiasi na uache uchemke kiasi. Na hapo mchizi utakuwa tayari.
Osha na uzikate spinach kisha kaanga kitunguu na mafuta kiasi (hakikisha visiwe vya brown kisha tia spinach na chumvi. zipike kwa muda wa dakika 3-4 na hapo zitakuwa tayari zimeshaiva.
Wali: Chemsha maji kiasi kisha tia, chumvi, pilipili nzima(isikatwe) mafuta na tui la nazi. Baada ya hapo koroga na utie mchele na maharage na ufunike uache uchemke mpaka maji yakauke. Kisha geuza na ufunike tena na uuache mpaka uive. Baada ya hapo chakula chako kitakuwa tayari kwa kuseviwa.
KILA mtu duniani ana ndoto ingawa haijalishi ni ndoto gani uliyonayo.
Ndoto uliyonayo ina thamani kubwa kuliko fedha wala kitu chochote kile. Ndoto uliyonayo ina nguvu kubwa ya kubadilisha maisha yako na kukufikisha sehemu ambayo ulitaka ufike ama zaidi ya pale ulipotarajia kufika.
Ndoto yako inaweza kukupeleka sehemu mbalimbali duniani ukazunguka kufanya mambo yako si kwa sababu una fedha sana, bali ni kwa sababu una ndoto. Ni vyema utambue nguvu ya ndoto uliyonayo ni kubwa kuliko fedha.
Ndoto inaweza kuzaa fedha kwa maana matunda yake yanaweza kuwa fedha, lakini katu fedha haiwezi kuzaa ndoto. Kwa hiyo bais, ndoto ni kubwa kuliko fedha.
Mtu mmoja aliwahi kusema kuwa, mtu maskini kuliko wote duniani ni yule asiyekuwa na ndoto!
Hivyo utakubaliana naye kuwa kila mwenye ndoto ni tajiri na si maskini, maana ana kitu cha thamani, cha pekee na cha tofauti ambacho hakuna mwenye nacho isipokua wewe mwenyewe.
Tatizo kubwa ni kwamba, watu wengi wameua ndoto zao kwa kisingizio cha kukosa fedha lakini wanashindwa kutambua kwamba hakuna fedha inayozidi ndoto isipokuwa ndoto inazidi fedha.
Tatizo lingine ni kwamba, watu wengi hawajui kuwa ndoto zao zina nguvu kubwa kufanikisha maisha yao kijamii, kiuchumi, kisiasa na kila nyanja.
Ndani ya ndoto zako kuna kila kitu unachokitaka ama unachokihitaji – iwe fedha, utajiri, umaarufu, familia nzuri, mume mzuri, mke mzuri, watoto wazuri, kazi nzuri, afya nzuri – hivyo ukiacha kutafuta fedha ukatafuta kutimiza ndoto zako utapata kila kitu ikiwemo utoshelevu na amani ya moyo.
Lakini tatizo lipo kwenye kufanya ndoto zako zitimie na zikuzalie mafanikio. Haijalishi una ndoto kubwa kiasi gani, kama hutaitimiza ikaja kwenye uhalisia tambua kwamba utakufa maskini ukiwa na utajiri wa ndoto, jambo ambalo linaumiza na linatesa maisha ya watu wengi wanaoishi maisha ya chini tofauti na walivyopaswa wawe.
Ndoto yako ndiyo imebeba kusudi la maisha yako. Kama hutaishi katika ndoto yako maana yake utakuwa hujaishi maisha yako ambayo kwa kiasi kikubwa yapo kwenye ndoto zako.
Mtu mmoja aliwahi kusema kuwa, watu wengi duniani hawaishi, bali wapo tu. Kuna tofauti kati ya kuishi na kuwepo. Kuishi ni kutimiza ndoto zako na ndani ya kusudi la maisha yako, lakini kama hutimizi ndoto hizo uko nje ya kusudi la maisha yako. Wewe utakuwa hauishi bali upo upo tu.
Anaamka asubuhi kwa sababu watu wanaamka. Ukimuuliza kwanini umeamka anasema ni kwa sababu watu wameamka! Hana sababu za msingi. Kataa kuishi bila agenda, bila kuwa na ndoto ambayo kila siku unapiga hatua kuifikia ama uko ndani yake sasa katika kuitimiza na kuifanikisha kwa kiwango cha juu.
Kila kitu kipo kwenye ndoto zako, tafuta kutimiza ndoto zako kuliko kutafuta fedha kwa sababu fedha ni moja kati ya bidhaa iliyomo ndani ya ndoto zako.
Sisemi watu wasitafute fedha, la hasha. Wazitafute, tena kwa bidi, ila wasisahau kutafuta kutimiza ndoto zao na kutumia fedha kama moja kati ya nyenzo za kuwawezesha kutimiza ndoto zao.
Ukweli ni kwamba, fedha daima huwa hazitoshi, hata kama ni nyingi kiasi gani. Kama unabisha waulize matajiri kama wamewahi kuridhika. Lakini katika kutimiza ndoto zako kuna utoshelevu kiasi na kuridhika kiasi fulani (satisfaction) hata kama si kwa asilimia 100.
Mwandishi mashuhuri wa vitabu, Myles Munroe, aliwahi kusema kuwa “Watu wenye kusumbuliwa na msongo mkubwa wa mawazo ni wale ambao ndoto zao hazijatokea kwenye uhalisia, zinawasumbua.”
Inawezekana unasumbuka sana kwenye maisha yako kwa sababu hujatimiza ndoto zako, maana ndoto huwa haimwachi mtu akatulia, inampa mahangaiko, mfadhaiko wa kutaifuta.
Kila mtu anapaswa azae, ndoto yako izae, uwezo ulionao uzae. Unaweza kukuzalia mafanikio makubwa, hivyo usikubali kufa na kitu cha thamani kilichoko ndani yako.
Hakuna ndoto kubwa wala ndogo. Fikiria mtu aliyegundua lipstick, leo hii wanawake dunia nzima wanapaka lipstick, si jambo dogo tena.
Hukuja duniani kuwa mtu wa kuhangaikia fedha, inatakiwa fedha ikuhangaikie wewe, ikupende na ikutamani na si wewe utamani fedha.
Tengeneza miundombinu ya fedha na hiyo miundombinu iko kwenye ndoto zako, maono yako, kipaji
“Mkeo amefariki. Rudi nyumbani kwako haraka sana” Hezron alimwambia Daniel katika simu.
“Mke wangu amekufa? Nini kimetokea? Amekufaje?” Daniel aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa vibaya.
“Daktari amesema ni shinikizo la moyo lililosababishwa na stress kali. Daktari na polisi wapo hapa nyumbani kwako. Njoo haraka” Hezron akaongea kidogo na akakata simu.
Muda anapigiwa simu na Hezron, Daniel alikuwa mtoko na mwanamke mwingine mrembo katika moja ya hoteli kubwa iliyoko maeneo ya Kunduchi. Alikuwa akifurahi nae huku wakinywa vinywaji ghali na chakula cha hadhi ya nyota tano. Lakini baada ya kupokea tu ile simu ya taarifa ya kifo cha mkewe, Daniel alichanganyikiwa, uso wake ukabadilika.
Hezron ni rafiki yake wa karibu.
Daniel akainuka na kuondoka katika ile Hotel akimwacha yule mwanake Mrembo.
“Kuna tatizo gani?” Yule mrembo aliuliza.
“Siwezi kuzungumza” Daniel alijibu na kuondoka haraka.
Daniel akaenda alikopaki gari yake, akaingia, akaiwasha na kukanyaga mafuta, akaiondoa kwa kasi ya ajabu.
Akiwa anaendesha, Daniel akakumbuka jinsi yeye na mkewe anaeambiwa amefariki walivoenda pamoja Showroom ya magari na kununua hilo gari pamoja.
Akiwa anakata kona, akakumbuka jinsi alivyokuwa akimfundisha mkewe kuendesha gari. Hizo zilikua nyakati njema kabisa katika maisha yao ya ndoa.
“Mke wangu amekufa! Kweli mke wangu amekufa! Mungu wangu..” alilia sana huku akiendesha.
Akakumbuka siku ya ndoa yao. Agano waliloliweka pamoja. Akiwa anabadilisha gia, akaangalia vidole vyake asiione pete yake ya ndoa. Pete ya ndoa aliitoa ili kudanganya wanawake wengine kwamba hajaoa.
Daniel akakumbuka ni jinsi gani alivyokuwa akimjibu mkewe hovyo, kwamba anayo kila sababu ya kufurahia maisha na kuponda raha. Akakumbuka maneno ya kuchoma aliyokuwa akimwambia mkewe kwamba yeye amezaa na amezeeka!
“Mke wangu amefariki! Kwanini umefariki Lisa! Kwanini Mungu? Alijiuliza maswali lukuki.
Jibu likamjia. Akakumbuka ni nini Hezron alimwambia. Kwamba mkewe yawezekana amekufa kwa shinikizo la damu kutokana ma stress. Kwa hali hiyo Daniel nimemuua mke wangu.
“Nimemuua mke wangu mwenyewe. Mungu nisamehe…” alijutia huku akiendesha gari kwa kasi.
Daniel akakumbuka jinsi mambo yalivyoenda vibaya katika ndoa yake. Jinsi gani upendo ulikimbia katika ndoa yao. Jinsi gani walivyoanza mabishano na ugomvi. Takribani mara nne ameshampiga mkewe vibao. Alikuwa mtu mbaya kwa mkewe na kwa watoto wake wadogo wawili.
Alifikiri aache kuhudumia familia, hitaji lake likaja kuwa kutomheshimu mkewe, kutomheshimu mkewe kukaleta dharau na maneno ya kejeli kwa mkewe, maneno ya kejeli yakasababisha vidonda vya tumbo kwa mke mwema Lisa kutokana na mawazo na kutokula.
Naam, Lisa aliugua vidonda vya tumbo kutokana na maumivu ya mawazo aliyosababishiwa na mumewe. Afya yake ilikongoroka, umbo lake zuri namba nane lilipotea, Lisa alionekana kama mzee, wakati ni mwanamke wa miaka 29 tu. Ila Daniel hakujali, alimzarau. Alijibadili kutoka mume aliyempenda mkewe kuwa mtu msaliti, anayemuumiza mkewe. Lisa amefariki!!?
Akiwa bado anaendesha akakumbuka jinsi alivyomfuata Lisa na kumuomba wafunge ndoa, Lisa alikuwa mzuri, akijitegemea na mwenye furaha na maisha. Yeye kumuoa tu ndio ikawa kumharibu, kumuumiza na mwishowe kumuua kwa stress!
Atakufaje? Hawezi kujua kwa sababu hajarudi nyumbani wiki moja sasa imepita, hajui watoto wanakula nini, wanavaa nini. Mke wake alikuwa akimtumia texts na kumpigia akimsisitizia arudi nyumbani, ila kilio cha mkewe kilitua katika masikio yake ambayo hayasikii. Mkewe alikuwa akilia, akipiga kelele mumewe arudi nyumbani, yote hayo ni kwa ajili ya kuokoa ndoa yake. Lakini mimi Daniel sikusikia. Sasa amefariki!
“Mimi nitafanya nini na watoto wangu?” alifikiria nafsini kwake. Watoto wawili alionao ambao alikuwa hawajali kwa sababu ya kuwa busy na warembo wa jiji la Makonda. Akakubali kwamba kweli mke wake alikuwa na moyo wa ajabu, kuwatunza watoto wale wawili bila msaada wake.
“Nani atanisaidia kuwalea? ” Wanawake ambao amekuwa akila nao bata hawawezi kumsaidia kulea watoto, sio wife material wale, wife material hawezi kuvunja ndoa ya mwanamke mwenzake. Alifikiria nafsini mwake.
Wazazi wa mkewe watafikiri nini?
Watu watafikiri nini? Mungu ananifikiriaje?
Hii ndio inaishaje ishaje? Ndoa yangu ndio imeishia hivi? Mke wangu kafariki?
Daniel akapaki gari, akatoka na kukimbia ndani ya nyumba.
Akafungua geti, akafungua mlango. Akamuona Hezron, rafiki yake akiwa amesimama katika korido ya nyumba yake.
“Kimetokea nini? Haiwezekani kuwa amekufa. Hawezi kufa. Mimi nitafanya nini Hezron?” Daniel aliongea akiwa amekata tamaa.
Hezron akamkumbatia Daniel.
“Uko sawa Daniel?” Hezron aliuliza.
“Nitakuaje sawa wakati mke wangu amekufa? Mama wa watoto wangu! Uko wapi mwili wake?” Daniel aliuliza.
“Upo sebuleni” Hezron alijibu.
Daniel akakimbia kuelekea sebuleni.
Mshangao!!
Akamwona mkewe akiwa hai. Amekaa katika sofa akiwa na mke wa Hezron ambae ni daktari wa saikolojia pembeni.
“Haujafa?!” Daniel aliuliza akiwa na mshangao
“Ndio hajafariki. Ila kama ukiendelea na hii tabia atafariki siku moja. Mkeo hajawa sawa kabisa. Amekuwa akijaribu kukutafuta na kukurudisha nyumbani ila umempuuza. Taarifa za kifo chake zimekufanya ukimbie kama mwehu. Ulitakiwa ukimbie kwa ajili ya maisha yake na si kwa ajili ya kifo.” Mke wa Hezron aliongea.
Daniel akakaa katika kochi mbele ya mkewe na akamshika uso wake. Mkewe akarudishwa kichwa nyuma.
“Natumaini kwamba safari yako ya uchungu kuja hapa ukifikiri mkeo amekufa itakukumbusha ni nini cha muhimu kinachotakiwa kufanywa. Usisubiri mpaka uchelewe ndio ufanye jambo jema. Unayo nafasi ya pili.” Aliongea mke wa Hezron
Daniel akanyanyua mkono wa mkewe machozi yakimtiririka, asiamini juu ya kile anachoshuhudia.
“Ndoa sio lelemama nyie wawili. Acheni kucheza michezo ya kipumbavu na maisha. Kesho sio garantii” aliongeza mke wa Hezron.
“Nyie wawili mna matatizo. Mmeridhika na matatizo ya kuumizana hasa wewe shemeji yangu Daniel. Kesho haiwezi kuwa pale kwa ajili yako kwa ajili ya kuomba msamaha. Mkewe Hezron aliongea.
“Na siku ya kiama tutakapokutana na mwenyezi Mungu, Daniel kitu ambacho Mungu atauliza ulimtendaje mke wako ambae ni ubavu wako? Huyu ni binti wa Mungu. Unavomuumiza yeye na Mungu anaumia pia” Akaongezea Hezron.
Mke wa Daniel akamgeukia Hezron na mkewe akasema “Nashukuruni sana kwa kupanga hii idea ya kumuamsha mume wangu, sio siri nilitamani kufa hata leo. Ninampenda sana ila nimechoka na maumivu. Ninyi ni marafiki bora wa familia yetu.
Daniel akamkumbatia mkewe tightly na akasema “Nisamehe sana Lisa wangu, sitaki kukupoteza. Leo nimeshuhudia familia yangu ikivunjika vipande vipande. Nilikuwa kipofu tena katikati ya giza tororo ila sasa ninaona. Usife tafadhali. Nitafanya yale yaliyo bora kuanzia sasa.
Rafiki yangu Hezron na shemeji yangu Julieth ninyi ni marafiki bora kabisa, rafiki aliye bora hukuondoa katika kiza na kukuweka katika nuru. Mmedhihirisha hilo. Naomba niwaahidi tukio hili limekuwa funzo kubwa kwangu. Naanza sasa kuwa mume na baba bora wa familia. Ila siku nyingine msinitishie kifo, naweza kufa kwa pressure na mimi. Nawashukuruni sana. Mwenyezi Mungu awajazi.
“Hahaaa Okey yaishi maneno yako, Mke wangu na mimi tunawaacha, tuwaache mfanye yale ambayo wanandoa wawili wanaopendana kweli hufanya.” Hezron aliongea.
Na wakaondoka!
Mpende mwanandoa mwenzako, waheshimu wazazi, wabariki watoto wako, wapende rafiki zako, wote wakiwa bado wako hai.
Kabla hujachelewa!
Busara yangu,.
1. Awe na pesa nyingi
2.Siyo lazima awe mzuri wa sura
3. Ajenge ukweni
4.Awe mpole
5.Asimuonee wivu mke wake
6.Awe mwenye upendo wa dhati
7.Asishike simu ya mke wake.
8.Akimkuta na mwanaume apite tu, akitaka kujua ni nani asubiri nyumbani
9.Awe anamskiliza mke wake kwa kika kitu.
10.Asipende mwanamke mwingine zaid yake
UKIMPATA MWANAUME MWENYE SIFA HIZO KAPIME DNA LAZIMA ATAKUWA NI BABA AKO.
😂😂😂😂😂😂😂😂
Recent Comments