Kuomba na Kushukuru
Unapo mwomba Mungu Usisahau Kushukuru. Kushukuru ni kuomba mara ya pili. Utazidishiwa kile ulichokiomba na kupewa hata usichokiomba kwa shukrani yako.
Unapo mwomba Mungu Usisahau Kushukuru. Kushukuru ni kuomba mara ya pili. Utazidishiwa kile ulichokiomba na kupewa hata usichokiomba kwa shukrani yako.
Viazi ulaya 4 vya wastani
Hoho jekundu 1/2
Hoho la njano 1/2
Hoho la kiajani 1/2
Njegere 1 kikombe cha chai
Carrot 1 kubwa
Broccoli kidogo
Cauliflower kidogo
Kitunguu 1
Nyanya 1/2 kopo
Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chakula
Curry power 1 kijiko cha chakula
Coriander powder 1 kijiko cha chai
Tarmaric 1/2 kijiko cha chai
Olive oil
Chumvi
1/4 ya limao
Katika sufuria isiyoshika chini kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia swaum/tangawizi na spice zote kaanga kwa muda mfupi kisha tia nyanya na chumvi. pika mpaka nyanya ziive kisha tia vegetable zote na vimaji kidogo sana na kisha kamulia limao, baada ya hapo punguza moto na kisha funika na zipike mpaka vegetable zote ziive na rojo ibakie kidogo. Baada ya hapo mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa.
Tupo kwenye dunia ambayo tulikuta watu na tutawaacha watu.
Vyote tulivyovikuta vilianzishwa na binadamu wengine wenye mawazo mema na wenye mawazo mabaya pia. Vitu vingi tunavyovifanya tunaendeleza tulivyovikuta ni mara chache kukuta kitu kipya ambacho hakitegemei mazingira na asili ya tulivyovikuta.
Hivyo basi kwa vyovyote vile unahitaji mtu wa kukuongoza au kuku Coach ili ufanikiwe katika pande zote za maisha.
Nitakwenda kuzungumzia sehemu kuu tatu za muhimu sana ambazo unatakiwa uwe na watu wa kukuongoza ili uweze kukua na kupanda viwango kila wakati.
Ni vitu vya kawaida sana lakini leo nitakwenda kuzungumzia uone ilivyo muhimu sana wewe kua na vitu hivi maana bila vitu hivi mafanikio yatakua magumu sana kufikia. Safari yako itakua ngumu zaidi kama utakosea sehemu hizi tatu.
Nitaomba tuelewane kwamba hapa huendi kuiga au kuwa hawa watu utakua wewe na utatimiza lile kusudi la Mungu ndani yako.
Kwanza kabisa uko hivyo ulivyo kwa sababu ya mazingira uliyokulia na watu ulioishi nao tangu ukiwa mtoto hadi hapo ulipo.
Kuna tabia nyingi sana unazo kutokana na mazingira uliyokulia.
(Hapa ndipo nakutana na kitu ambacho nakipenda sana kujifunza kwa wengine napenda kujifunza kwenye mazingira mapya na kwa watu wapya kwa kua wameishi maisha ambayo mimi siyajui na wanafahamu vitu vingi ambavyo mimi sifahamu. Watu wana utajiri mwingi sana ndani yao ukiweza kukaa na mtu ambaye humjui kabisa unaweza kujifunza mambo mengi ya ajabu kwake. )
Hawa ndio watu wa Muhimu sana kwenye safari yako usiwakose ili uweze kusonga mbele.
Sifa zao kabla hujawachagua ni za muhimu sana pia ili wasije wakakupoteza badala ya kukufikisha kule unakotaka kwenda.
(a)Awe na mafanikio (Amefika Mbali) kwenye hiyo sehemu.
(b)Awe na Tabia njema zinazokubalika na jamii yake na dini yake. (mfano hapa ukikutana na mtu ambaye anakuelekeza kuhusu biashara na ni mlevi na mzinzi hizi tabia lazima atakuambukiza kwasababu atakua mtu wako wa karibu sana)
(c)Awe amekuzidi sana kwenye kile unachotaka akulelee (akuongoze).
Hizo ni sifa za muhimu tu za kuangalia zipo nyingine nyingi sana utajifunza mwenyewe.
1. Mlezi wako wa Kiroho
Huyu ni mtu wa muhimu sana na nimemweka wa kwanza.
Bila roho hakuna mwili.
Bila roho mwili wako unakua umekufa.
Unahitaji ukue kiroho na upande viwango kila wakati ili uweze kuvutia mafanikio ya nje.
Ukishindwa hapa hata ukiwa bilionaire inaweza kuwa kazi bure.
Hutaweza kuzifurahia hizo pesa.
Tafuta mtu wa kukulelea kiroho.
Mtu wa kukufundisha kumcha Mungu.
Kama huna katafute mtu wa kukulea kiroho sifa nimezitaja hapo juu.
Mtu huyu anatakiwa akufahamu vizuri na wewe umfahamu vizuri.
Yaani muwe na mahusiano ya karibu sana.
Mtu huyu awe anafuatilia maendeleo yako ya kiroho kwa karibu sana.
Haijalishi uko Dini gani lazima umpate mlezi wa roho yako.
Dini ndio inahusika kulisha roho zetu.
Ndio maana hatufundishwi biashara kule.
2. Mlezi wa Mahusiano/Uchumba/Ndoa
Hapa ni kwa muhimu sana.
Ukiwa vizuri kiroho mahusiano yakawa na tatizo hutafika mbali.
Ukiwa vizuri kiroho ndoa ikasumbua nayo ni tatizo.
Tafuta mtu wa kukulea kwa upande huu pia mtu aliefika mbele zaidi yako.
Aliefanikiwa zaidi yako.
Kama unatafuta mchumba tafuta mtu aliye kwenye ndoa na amefanikiwa.
Ukimtafuta single mwenzako atakupoteza😀.
Mtu huyu awe karibu yenu kabisa kulea mahusiano/ uchumba au ndoa yenu.
Hakuna aliyezaliwa anajua kila kitu tunajifunza hapa duniani kwa waliotutangulia na waliopo pia.
3. Mlezi wa Maono yako/Ndoto zako/Malengo yako/Biashara Yako/Pesa. (Coacher).
Mtu huyu ni wa muhimu pia katika maisha yako.
Unataka kumiliki utajiri wa dollar billion moja lazima utafute mtu wa kukulelea na kukuwezesha ufikie huko.
Huwezi kwenda mwenyewe.
Unahitaji mtu wa kukuongoza kwenye kila unachotaka kukifanya.
Wengi wanakata tamaa kwa kua hawana watu hawa wa kuwalelea.
Mtu huyu anatakiwa awe anakufuatilia hatua kwa hatua kwenye kile unachokifanya.
Awe anapata taarifa za maendeleo yako kila wakati ikiwezekana hata kila week.
Ukipata mafanikio yeyote ajue pia ukipata changamoto ajue.
Mtu huyu anatakiwa awe amekupita kwenye kile unachokitaka na hapa huendi kuwa Follower,anakwenda kukutengeneza wewe uwe kiongozi.
Uweze kusimama mwenyewe na hatimae uongoze wengine.
Kwa Tanzania wapo watu wanaofanya kazi hizi kwa malipo pia.
Lakini hapa unaweza kuanza na mtu ambaye una mahusiano nae ya karibu awe anakulelea.
Siku hizi teknolojia imekua rahisi sana unaweza kuwa na mawasiliano na mtu yeyote unayemtaka popote alipo duniani.
Unaweza kujifunza pia vitu vingi sana kupitia mitandao hii kama hapa facebook.
Unaweza kusoma vitabu na vitu vingi sana vile unavyovitaka.
Naomba nimalizie kwa kusema kwamba.
Kwa hiki ulichokipata leo ukikifanyia kazi.
Utakua mshindi uliyezaliwa kuwa.
Utafikia Hatma yako kwa kufuata haya, namaanisha wewe uliyesoma hapa.
I will see you at the top!
Kuamka asubuhi na mapema hupunguza uwezekano wa mwanamke kupata saratani ya matiti.
Kulingana na shirika la habari la BBC,wataalamu wa chuo kikuu cha Bristol nchini Uingereza wamewafanyia tathmini wanawake 400,000 na kutambua kuwa sio rahisi kwa mwanamke anaeamka asubuhi na mapema kupata saratani ya matiti.
Utafiti huo umeoneysha kuwa wanawake wanaoamka wamechelewa wana hatari kubwa ya kupata ugonjwa huo ukilinganisha na wale wanaoamka wamechelewa.
Utafiti wa hapo awali ulionyesha kuwa kufanya kazi mpaka usiku wa manane kunaongeza hatari ya kupata saratani.
Matokeo ya utafiti huo yatawasilishwa kwenye Mkutano wa Taifa wa Taasisi ya Utafiti wa Saratani huko Glasgow.
Mtoto wa miaka sita alimuuliza babake:
MTOTO: Baa, eti sisi wanadamu tulikuja vipi
duniani?
BABA: Mungu alimuumba Nabii Adam na Hawa.
Kisha wao wakaanza kuzaa watoto na watoto
wakazaa mpaka tukazaliwa sisi. (Mtoto hakuridhika
akamfuta mamake)
MTOTO: Mma, eti sisi wanadamu tulikuja vipi
duniani?
MAMA: Wanasayansi wamesema sisi tulitokana na
manyani baadae tukawa binadamu. (Mtoto akarudi
kwa baba)
MTOTO: Baa mbona mama ansema sisi tulikuwa
manyani mwanzo?Au wanidanganya?
BABA: Mwanangu, mimi nimekuelezea kuhusu ukoo
wetu. Mamako amekuelezea kuhusu ukoo wao😂😂🚶🏼🚶🏼🚶🏼
Watu wengi tumekuwa hatufahamu utumiaji wa pipilipili, hasa pilipili mbuzi. Naomba leo tuangalie kwa uchache faida hizo za pilipili mbuzi.
1. Pilipili inasaidia sana kusawazisha sukari kwenye damu.
2. Ulaji wa pilipili kunaweza kunawasaidia sana watu wanene (overweight) au wanao ugua ugonjwa wa kisukari.
3. Utafiti huo pia umeonyesha kwamba kawaida ya kula Pilipili kunaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti na kusawazisha insulini kwa 60%. baada ya kula chakula.
4. Pilipili husaidia kupunguza maumivu na uvimbe kwenye tezi na vilevile huwasaidia wagonjwa wa rheumatoid na arthritis kupata nafuu. Vile vile husaidia kuondoa mkusanyiko wa damu sehemu moja ya mwili.
5. Pilipili usaidia kufungua kwa haraka na kwa ufanisi pua zilizoziba kwa mafua, kuruhusu kupumua kwa urahisi zaidi!
6. Pilipili pia husaidia kupunguza upatikanaji wa saratani ya kwenye tumbo (Stomach Cancer)
7. Pilipili usaidia kuongezeka kwa kiwango cha metabolic, ambayo husaidia kuchoma mafuta, ulaji wa pilipili kunaweza kuinua kiwango na metabolic yako hadi 23% ndani ya masaa 3.
8. Kula pilipili usaidia kupunguza cholesterol, na kupunguza kiasi cha fibrin katika damu.
🙄🙄🙄🙄🙄🙄
Jana nimeenda kuazima pasi chumba jirani, ili ninyooshe nguo zangu, Jamaa wakaniambia nichukue nguo nikanyooshe room kwao maana hawataki pasi yao itoke.
Sasa leo amekuja mmoja wao kuazima mopper akasafishe room, nimemwambia aje adekie humu humu…
Jamaa ameondoka nadhani atakua ameenda kuchukua maji
🤒🤒🤒
Siku niliposoma hili andiko kwa mara ya kwanza nakumbuka, kwanza nilipata mshtuko flani baada ya kulisoma, halafu nikajikuta nikitafakari vitu vingi sana.
Hebu kwanza tusome pamoja andiko hili
ZABURI 109
17 Naye alipenda kulaani, nako kukampata.Hakupendezwa na kubariki, kukawa mbali naye
▶Huu mstari wa 17 umenishangaza sana, halafu ukanifungua na kunifundisha vitu vya msingi sana katika haya maisha tunayoishi
Ngoja tuuchambue kidogo hapa ili tuelewane vizuri
_Alipenda kulaani?………………………….Nako (laana/kulaaniwa) kukampata_
_Hakupendezwa na kubariki……………………(Kubarikiwa) kukawa mbali nae_
NET BIBLE inasema hivii
“He loved to curse others, so those curses have come upon him, He had no desire to bless anyone, so he has experienced no blessings” Kumbe the more ninakuwa na shauku ya kuona wengine wakibarikiwa, the more baraka zinanijia mimi and vice versa
Hapa nikajifunza kwamba kumbe yale mabaya tunayowafanyia au kuwawazia watu kuna uwezekano mkubwa sana yakatupata sisi wenyewe
Na tunapotamani kubarikiwa na kuinuliwa wakati hatufurahii kuona wengine wakiinuliwa, kuinuliwa kutakuwa mbali nasi
Huu mstari unaniongezea maarifa na kunifundisha namna ya kuishi katika ulimwengu huu
Nimewaza pia inawezekana wakati mwingine kuna vitu hatupati ni kwasababu tuu hatufurahii wala hatuombi wengine wapate hivyo
Kumbe kubarikiwa kwangu kunategemea na namna ambavyo ninakuwa baraka kwa wengine na kutamani kuona wengine wakibarikiwa
Shauku yangu ya kutamani wengine wabarikiwe na kuinuliwa ndio nyenzo ya kuinuliwa kwangu na moyo mbovu wa kufurahi kuona wengine wakikwama ndio sababu ya kukwama kwangu?
_”Hii ni kanuni ya ajabu”
Ndugu yangu, unajua hapa najifunza kwamba kumbe kuna uwezekano mkubwa kwamba mikwamo mingine tumekuwa tukijikwamisha sisi wenyewe
Ni kweli ninataka kubarikiwa, lakini ni mara ngapi nimefurahi au kuombea wengine ili wabarikiwe?
Unatamani kupandishwa cheo sawa, lakini wengine wakipandishwa vyeo unanuna? Au ukiona ofisini ndio anapewa safari nyingi za nje unakasirika?
Unatamani kuoa/kuolewa halafu wengine wakioa na kuolewa unaona uchungu juu yao, unawanunia, unapunguza ukaribu?
Unatamani kupata gari zuri lakini wengine wakipata unakasirika?
Nikiwa mtoto mdogo nakumbuka mwalimu mmoja aliwahi fundisha kwamba nisipende sana kujiombea mwenyewe, na akasema kama unahitaji kitu, waombee wengine wasionacho wapate, nawe utajibiwa pia, andiko hili limenifanya nielewe kwanini mwalimu yule alifundisha vile
Na wakati mzaburi anaongea maneno haya hapa chini sikumuelewaga, nilijua ni kawaida tuu, nilisoma kikawaida tuu, lakini sasa ndio nimefunguka ufahamu zaidi
*ZABURI 35*
13 Bali mimi, walipougua wao, Nguo yangu ilikuwa gunia. Nalijitesa nafsi yangu kwa kufunga; Maombi yangu yakarejea kifuani mwangu
Bila kujali watu walikuwa wakimuwazia na kumfanyia nini, alipowaombea tuu, maombi yale yalirejea, yalifanya kazi na katika maisha yake. Kumbe kuomba kwaajili ya wengine wafanikiwe, wainuliwe, wabarikiwe na wapandishwe kunarejesha matunda kwetu pia
Ubaya unaomfanyia mwingine si ajabu ukakupata
Kuanguka unakomuombea mwingine kutakujia wewe
Kanuni hii inanifundisha pia kuwa YESU aliposisitiza tupendane alikuwa na maana kuu
Alijua kwamba ukiwa na chuki kwa mwingine chuki ile itakuathiri wewe
Ukiwa na moyo wa kufurahi wengine wanaposhindwa, kushindwa kutakupata wewe
Kwanini sasa tusichague kubariki wengine ili baraka zile zitupate na sisi pia?
Kwanini tusiwaombee mema wengine ili maombi yale ya mema yatutendee mema sisi?
Ni vyema sasa tukachagua kuwa na moyo wa upendo, moyo utakaowawazia na kuwatendea mema wengine kwasababu mema yale tuwafanyiayo wengine yatatuletea mema maishani mwetu pia
Jipime, jiangalie, jichunguze
Waza mema kwaajili ya wengine, mema yaje kwaajili yako
MITHALI 17
13 Yeye arudishaye mabaya badala ya mema,Mabaya hayataondoka nyumbani mwake
If you love to curse others, those curses will come upon you
If you have NO desire to bless others, then you will experience NO blessings
CHOOSE TO BLESS OTHERS,BLESSING WILL FOLLOW YOU
Hakuna Maisha ya Kikristo bila Kusali. Kama kuna Mkristo anaishi bila kusali huyo siyo Mkristo bali Mkristo mfu. Sala ndiyo uhai wa Mkristo. Hakuna Njia nyingine yoyote ya kumfikia Mungu isipokua sala.
Kitunguu swaumu hujulikana kama kitu cha kushangaza katika tiba huko mashariki ya mbali, Kitunguu swaumu ni maajabu ya Mungu mwenyewe.
Kina nguvu za kuua bakteria mbalimbali na kuzuia magonjwa ikiwemo kutibu chunusi. Kuna namna 2 za kutumia kitunguu swaumu kutibu chunusi; namna ya kwanza ni kukitumia kitunguu swaumu kwenye vyakula vyako unavyopika kila siku, namna ya pili ni kukitwangwa kitunguu swaumu na kukipaka moja kwa moja katika sehemu yenye chunusi.
Ukiacha harufu yake isiopendwa na wengi, kitunguu swaumu kinaweza kukupa afya na urembo unaouhitaji.
Kitunguu swaumu husaidia kupunguza ukubwa wa chunusi. Hata hivyo uwe makini kwani kitunguu swaumu kinaweza kuunguza ngozi yako usipokuwa makini na ili kuepuka hili jaribu kuchanganya kidogo na maji baada ya kukitwanga ili kupunguza makali yake.
Tuna (samaki/jodari) – 2 Vikopo
Vitunguu (kata kata) – 4
Nyanya zilizosagwa – 5
Nyanya kopo – 3 Vijiko vya supu
Viazi (vilivyokatwa vipande vidogo – cubes) – 4
Dengu (chick peas) – 1 kikombe
Kitunguu saumu(thomu/galic)&Tangawizi iliyosagwa 1 Kijiko cha supu
Hiliki – 1/4 kijiko cha chai
Mchanganyiko wa bizari – 1 kijiko cha supu
Chumvi – kiasi
Pilipili manga – 1 Kijiko cha chai
Vipande cha Maggi (Cube) – 2
Mchele – 3 Vikombe vikubwa (Mugs)
Mdalasini – 2 Vijiti
Karafuu – chembe 5
Zaafarani – kiasi
Jirsh (Komamanga kavu au zabibu kavu -raisins) – 1/2 Kikombe
Kosha Mchele na roweka.
Kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi (brown) chuja mafuta uweke kando.
Kaanga viazi, epua
Punguza mafuta, kaanga nyanya.
Tia thomu/tangawizi, bizari zote, vipande vya Maggi, nyanya kopo, chumvi.
Mwaga maji ya tuna iwe kavu, changanyisha kwenye sosi.
Tia zaafarani kidogo katika sosi na bakisha ya wali.
Chemsha mchele pamoja na mdalasini na karafuu.
Karibu na kuwiva, chuja maji utie katika chombo cha kupikia katika jiko (oven)
Nyunyizia zaafarani, mwagia vitunguu, viazi, na dengu juu ya wali.
Mwagia sosi ya tuna na pambia jirshi (au zabibu).
Funika wali na upike katika jiko moto wa 450º kwa muda wa kupikika wali. Epua upakue.
1. Wana Nguo Nyingi KulikoWanaume.
2. Wanafahamu Nani Ni Baba HalisiWa Watoto Wao.
3. Ni Wepesi Kupenda NaWakipenda Hupenda Kweli.
4.Wanaoga Mara Nyingi Zaidi KwaSiku.
5. Wana Huruma Sana Ingawa MaraNyingi Huwa Inawaponza.
6. Wana Uwezo Wa KubadilishaTabia Ya Mwanaume Muda Wowote.
7.Wana Uwezo Wa Kuishi NaKupendeza Bila Kuwa Na Kazi WalaBiashara Yoyote.
8. Kwao Nywele Na Kucha Ndo Vitu Vya Kwanza Kufikiria WakitakaKutoka.
9. Wana Uwezo Wa Ku-Pretend Kwa Muda Mrefu Zaidi Hasa Kwenye Mapenzi.
10. Hawapendi pesa
Samahanini Jamani. hiyo ya 10 imeniponyoka 🤣😎
Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke
Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.
Kujua kama mwanamke anakupenda kabla hajakwambia angalia dalili zifuatazo
Mwanamke anayekupenda lakini hawezi kukwa mbia huwa anafanya mambo kukupima kama na wewe unampenda. Mfano wa mambo hayo ni kujifanya anaumwa na kuangalia wewe kiasi gani unamjali na kiasi gani utahangaika kwa ajili yake.
Msichana anayependa haoni aibu kukushika mkono ama kukutomosa au hata kukumbatia. Kwa kufanya hivyo hujua kuwa kwa asilimia kubwa hisia za kushikana kwenu kutamrahisishia kazi ya kuwa na wewe na kutakufanya wewe kujiskia kumpenda pia.
Mwanamke anayetaka ujue anakupenda huwa hucheka unapoongea au kufanya kitu chochote hata kama hakichekeshi. Mara nyingi ataonesha uso wa furaha hata kama si furaha ya kweli. Hii ni kufanya ili umtambue.
Hujisikia wivu anapokuona na wasichana wengine. Ukiwa unaongea nao au ukichati nao na ukiwaita majina ya kimahaba. Hapendi.
Mwanamke anayetaka ujue kuwa anakupenda hukukumbuka siku zako muhimu kama vile siku yako ya kuzaliwa hatoweza kuisahau kufanya ipite bila kukutakia heri ya siku ya kuzaliwa au ukifaulu mtihani au chochote katika maisha yako atakuwa mbele kukupongeza. Hii ni kutaka kuwa karibu na wewe na kukuonyesha kuwa anakupenda.
Mwanamke anayekupenda anapenda kukuangalia machoni muda wote ambao mtakuwa mkizungumza pamoja akidhani kuwa utaelewa ni kiais gani anakupenda kupitia vile ambavyo anakuangalia. Ila wengine huona aibu kuwatazama wavulana wanaowapenda si wote wana ujasiri wa kuwatazama wapenzi wao.
Mwanamke anayekupenda anajisikia furaha kukaa na wewe muda mrefu bila kuchoka. Anaweza akaacha kila kitu anachokifanya ili ajumuike na wewe. Hawezi kupoteza hata sekunde ukimuhitaji kwa mazungumzo.
Kama mwanamke anakupenda yupo tayari kujitoa sadaka. Ni kitu ambacho hakuna mtu ambaye anaweza akafanya kwa mtu mwingine. Yaani yupo tayari yeye akose lakini wewe upate na kwa mwingine anaweza akamwamba hana alichoombwa lakini akakupa wewe kama pesa na vitu vingine. Utaona ni vipi huyo mwanamke alivyo kwako na kwa wengine.
Unapomueleza kuwa ana tatizo anajali tatizo lako kama vile ni lake na hujisikia vibaya sana na kuhuzunika na atafanya lolote ili aweze kukusaidia utoke katika hilo tatizo. Mwanamke kama huyu huwenda anakupenda lakini ameshindwa kukwambia.
Kama mwanamke anakupenda na hamna uhusiano wa kimapenzi mikwaruzano ikitokea katika urafiki wenu hayupo tayari kukupoteza kabla hajakuambia anakupenda. Kwa kuwa anakupenda endapo ikatokea mikwaruzano basi atafanya juu chini kuyaweka mambo sawa ili asikukose.
Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke
Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.
JINSI YA KUONDOKANA NA JANGA HATARI LA UGONJWA WA FIGO:*
*1.Usichelewe kwenda HAJA.* Kutunza mkojo kweye kibofu chako kwa muda mrefu ni wazo baya. Kibofu kikijaa kinaweza kusababisha uharibifu. Mkojo ambao unakaa kwenye kibofu huzidisha bakteria haraka.
Mara mkojo unaporudi nyuma ya njia na Figo, sumu dutu husababisha maambukizi ya figo, pia njia ya mkojo na “nephritis”, pamoja na “uremia”. Wakati wito asili (unahisi mkojo) fanya hivyo haraka iwezekanavyo.
*2. Kula Chumvi kupita kiasi.* Inatupasa kula Chumvi isiyozidi 5.8 gramu kwa siku.
*3. Kula nyama kupita kiasi.*
Protini ikizidi sana katika mlo wako inadhuru figo zako. Mmeng’enyo wa Protini unazalisha amonia- sumu dutu ambayo ina uharibifu mkubwa kwa figo zako. Nyama nyingi inaleta uharibifu zaidi wa figo.
4. *Unywaji mwingi wa “Caffeins”.*
Caffein hutokana na vinywaji vya Soda na vinywaji vingine laini kama Kahawa, Redblue n.k. Hupandisha shinikizo la damu na figo zako kuanza mateso. Unapaswa kupunguza kiwango cha Coke, Pepsi, Red Bull, nk ambavyo hunywa kila siku.
*5. Kutokunywa maji.*
Figo zetu lazima zichakatwe vizuri kutekeleza majukumu yake vizuri. Endapo hatunywi ya kutosha, sumu dutu inaweza kuanza kukusanyika katika damu, kama hakuna kimiminika cha kutosha kutoa kwa njia ya figo. *** Kunywa zaidi ya bilauri 10 za maji kila siku.
Kuna njia rahisi ya kuangalia kama unakunywa maji ya kutosha: Angalia rangi ya mkojo wako; Wepesi wa rangi, ndiyo vzuri.
*6. Kuchelewa matibabu.*
Tibu matatizo yako yote ya kiafya kwa uhakika na uwe unachunguza afya yako mara kwa mara. Wapendwa na wapenzi wangu, hebu tujisaidie wenyewe… Shirikisha wengine, kama unajali. —-
*Pia epuka vidonge hivi, ni hatari sana:*
D- baridi*
Vicks Action- 500*
Actified*
Coldarin*
Cosome*
Nice*
Nimulid*
Cetrizet- D
Hivi vidonge vina Phenyl propanol- amide PPA ambayo husababisha stroke na ni marufuku Marekani.
MWISHO… Tafadhali, kabla ya kufuta, msaidie rafiki yako kwa kumpitishia hii..!
*Inaweza kumsaidia mtu!*
Wasambazie wengi kwa kadiri uwezavyo.
Shirikisha ujumbe huu kwa mpendwa wako.
*Maonyo muhimu ya Afya*
1. Jibu (pokea) simu wito na sikio la kushoto.
2. Usinywe dawa zako kwa maji baridi….
3. Usile milo mizito baada ya saa 11 jioni.
4. Kunywa maji vuguvugu mengi asubuhi na kiasi usiku. Usinywe maji baridi kamwe.
5. Muda bora wa kulala ni kutoka saa 4 usiku hadi saa 10 Alfajiri.
6. Usilale mapema baada ya kumeza dawa au baada ya mlo. Usiku, Kula chakula laini.
7. Usipokee simu yako ikiwa haina chaji. Wakati huo mionzi huwa ina nguvu mara 1000 .
Je, unaweza kuwasambazia watu unao wajali?
Mimi nimeshafanya kwako….!!.
Figisu ya Leo. UMESHAWAHI KUFANYA HILI JARIBIO.?
kadri temperature inavyo ongezeka chura nae huwa ana increase temperature ya mwili wake..
pindi inapokaribia kufika boiling point yaani nyuzi 100 chura atashindwa kuongeza temperature ktk mwili wake na hapo ndipo atataka kutoka ktk maji hayo ya moto na yanayo endelea kuchemka..
kutokana na kutumia nguvu nyingi sana ktk kuongeza temperature ktk mwili wake,pindi anapotaka kuruka atashindwa na atakufa humo ndani ya chombo cha maji yanayochemka..
SWALI; NINI KIMEMUUA CHURA.!??
Najua utaniambia ni maji ya moto…
La hashaa.!
kilichomuua chura ni kushindwa kufanya maamuzi mapema ya kutoka katika chombo cha maji yanayochemka hali ya kuwa bado nguvu anazo..
FUNZO
Fanya maamuzi sahihi sasa kabla nguvu za kutaka kufanya changes hazijakuishia kama yaliyomkuta chura..
NOTE; Kuvumilia jambo usiloliweza ni sifa ya punda.
BADILIKA.
Unga 1 Magi (vikombe vya chai)
Sukari ya browni ½ Magi
Siagi iliyoyayushwa 125 g
Nazi iliyokunwa ½ Magi
Syrup 1/3 kikombe cha chai
Siagi iliyoyayushwa 125 g
Maziwa matamu ya mgando 2 vikopo (condensed milk)
Chokoleti 185 g (dark chocolate)
Mafuta 3 Vijiko vya chai
1. Changanya unga, sukari, siagi na nazi iliyokunwa kwenye bakuli mpaka unga ushikamane.
2. Paka mafuta treya ya kuchomea kisha utandaze kwenye treya ya 20cm kwa 30 cm au (8 in kwa 12 in) unaweza kuweka karatasi ya kuchomea chini ukipenda.
3. Choma kwenye moto 325˚C kwa muda wa dakika 15 mpaka 18 au mpaka ibadilike kuwa rangi ya browni.
4. Kwenye sufuria ndogo tia syrup siagi na maziwa matamu ya mgando na changanya kwa moto mdogo mpaka uwe mzito kasha mimina juu ya keki uliyochoma na choma tena kwa muda wa dakika 20 mpaka karameli iwe rangi ya dhahabu.
5. Kwenye sufuria ndogo nyingine tia vipande vya chokoleti na mafuta na ukoroge kwa moto mdogo mpaka iyayuke kisha wacha ipoe kidogo mimina juu ya mjazo wa karameli kisha weka kwenye friji mpaka ishikamane.
6. Kata vipande weka kwenye sahani tiyari kwa kuliwa
Siyo watu wote wanaokuuliza kwamba watoto hawajambo,wanakuuliza kwa nia nzuri,wengine wanaulizia watoto wao waliozaa na mkeo.duh!! tutafika kwel
🙆🙆🙆🙆🏃🏃🏃
Recent Comments