Mungu ni nani? Sifa za Mungu
Mungu ni Muumba wa vyote maana yake amefanya vitu vyote kwa kutaka tuu pasipokutumia kitu chochote (Yoh. 1:3)
Mungu ni Roho kamili na ukamilifu wake hauna mpaka na haonekani wala hashikiki. (Yoh. 4:24, Kut 3:13-15, Zb 144:3, Lk: 24:39)
Mungu anaweza kufanya kila anachokitaka. (Zab. 135:6)
Hii ina maana Mungu hana mwanzo wala mwisho, amekuwepo kabla ya nyakati, yupo na atakuwepo baada ya nyakati. Yeye ndiye anazifanya nyakati, Yupo daima. (1 Tim, 1:17)
Maana yake anavipenda na kuvitunza viumbe vyake hasa wanadamu na anavitakia mema tuu (Zab: 25:8-10)
Kila mtu hupata kwa Mungu Haki yake kadiri na anavyostahili.
Anawasamehe watu dhambi zao wakitubu
Recent Comments