SMS Nzuri: Meseji za Vituko Vya Kukuparaha

Cheka kidogo, angalia anachosema huyu mchaga

Mchaga baada ya kufa akaulizwa na malaika anayetoa roho: Mangi hapa ni njiapanda kulia ni Mbinguni na kushoto ni Jehanamu, Je unachagua kwenda wapi?

MANGI: Bwashee, mi nabaki hapa hapa njiapanda aisee.
MALAIKA: Kwa nini?
MANGI: Aisee, nikifungua duka hapa si nitapata wateja wa Mbinguni na Jehanam. Yani patakuwa senta ya hatari, supu na nyama choma muda wote. Hata we utafaidi, unavyoenda kuchukua roho unaniletea stock nakupa hela yako cash mkononi. Na kila ukipita hapa unapiga mchemsho wako wa ulimi na bia mbili chap kabla ya kuingia mbinguni.
Kwanza nashangaa Shirima alipitaje hapa bila kushika ploti, au alikufa amelewa sana?

Wanawake wa leo mbele ya hela. Hii ni hatari

MDADA: Baby nikwambie kitu
MKAKA: Yeah Baby Uko huru nambie
MDADA: nilikua naomba hela babyโ˜บ
MKAKA: WW nae kwa kupenda hela jana tu nmekupa hela Leo unaomba ya nn ๐Ÿ˜–
MDADA: hapana๐Ÿ˜Œ Bby sio hivyo nlikua nataka nikashuhudie tetemeko la ardhi BUKOBA nasikia huko linaonekana vizur .
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Wanawake kumbukeni sio vizuri

Huyu jamaa kawaweza wapenda vya bure

Jamaa kaingia mgahawani kwa fujo
JAMAA :ย Nipe soda moja na kila mtu mpe yake maana ninapokunywa soda napenda kila mtu anywe
WATU :ย Ha! Ha! Ha! Haaaa!
JAMAA :ย Nipe mchemsho na kila mtu mpe wa kwake maana ninapokula mchemsho napenda kila mtu ale wake
WATU:ย Watu weweeee! Tena safari hii Na makofi juu..
JAMAA :ย Mhudumu, nipe bili na kila mtu mpe yake maana ninapolipa bili napenda kuona kila mtu analipa yake
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Wale wa kupenda kupewa pewa namba za simu soma hii

Unaomba namba ya simu ya mdada af anakunyima ila unalazimisha akupe anaona kuliko muendelee kuongea bora tu akupe anakutajia 071112016 unafuraahi unaondoka unafika nyumbani unajaribu kuipiga but kabla hujapiga unagundua alikutajia tarehe ya leoย Wadada acheni hizoย ๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿƒ๏ฟฝ๐Ÿƒ๏ฟฝ๐Ÿƒ๏ฟฝ๐Ÿƒ

Angalia sababu ya mke Mtarajiwa kuzimia kabla ya harusi

*Jihadharini* na wachapaji wa kadi za harusi. Hakikisha unasoma maandishi yaliyochapwa kabla ya kadi kuchapwa na kusambazwa!

Mchapaji aliombwa aweke 1 Yohana 4:18 katika kadi ya harusi lakini mchapaji kwa makosa aliweka Yohana 4:18.

1 Yohana 4:18 panasema, “Katika pendo hakuna hofu, lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofuโ€ฆ”

Lakini Yohana 4:18 tunasoma, “Kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako.”

๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚_MKE MTARAJIWA AKAZIMIA HAPA, TUNAMPEPEA_

Darasa lolote lile halikosi watu kama hawa

Darasa lolote lile (hasa vyuoni) lazima liwe na wanafunzi wafuatao:
1. Mrembo wa darasa.
2. Playboy/playgirl. Hawezi kutembea na msichana/mvulana mmoja mara mbili.
3. Group ya marafiki watatu. Kila mara wako pamoja.
4. Mtu mwenye maswali ya kuudhi/kukera.
5. Msongolist kimeo. Huyu huwa anasoma sana bt hana bahati ya kufanya vizuri. Yani msuli tembo, bt matokeo sisimizi.

6. Mlafi. Huyu huwa hakatai offer.
7. Mtoro wa kudumu. Haji darasani hata km hana sababu.
8. Mchelewaji wa kudumu. Anakuja kipindi kiko katikati au kinakaribia kuisha.
9. Miss/Mr.Misifa. kila mara ataeleza the way nyumbani kwao walivyo matajiri.
10. Less talkative bt kiwembe. Jamaa mkimya bt unakuta ametembea na karibu wasichana 15 hapo class.
11. Handsome boy ambaye hana mpango na wanawake.
12.Chips addicted. Hawa wanaweza kula chips asubuhi mchana na jioni. Jumatatu hadi jumatatu.
13. Back benchers. Hawa huwa watundu sana na ni watu wa jokes. Huwa hawajibu swali, but wanasubiri wakati wa kushangilia waongeze bezi.
14. Wambea. Hawapitwi na kitu darasani na washazoea kufeli.
15. Mchungaji/Mtumishi wa Mungu,
16. Waimbaji/Wasanii,
17.Walevi
18.Mabishoo.
19. Team popo. Hawa wewe na hela wasiwe na hela wanakesha club,
20.Mwenye aibu kusimama mbele za watu. Wakati wa Presentation anakimbilia kusimama nyuma ya wenzie,
21. Viherehere. Hawa mara nyingi hutokea kupendwa sana na waalimu.
22. Wanaosoma ili kushindana kwny GPA.
23. Kupe. Huyu boom likitoka atawaganda wenzie hadi ziishe, halafu yeye anaanza kula zake alone.
24. Wise man/woman. Huyu huwa ni mtu anayeaminika na kila mtu darasani. Hutumika sn kushauri pale mambo yanapoenda mrama. Mara nyingi huwa ni mtu mzima.
25.mpenda supu” yeye hata ya nyani atakunywa tu.
26.Fix man. Huyu atakuomba jero, akafuatilie dili la milioni kumi town, kumbe hana hela ya chai.
27. Photocopy machine. Huyu ukimuonesha majibu kwny mtihani anaweza kucopy hadi jina lako.
๐Ÿ’ฅUsposema wewe uko namba ngapi mwngine atakusema๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…

Angalia kilichompata huyu mwanafunzi kilaza anayejiamini

Teacher: Who is a pharmacist?

Shemdoe raised up his hand.

Teacher: So itโ€™s only Shemdoe that can tell who a pharmacist is in this class? So there is no body else to answer the question except Shemdoe? (There was no reply from the students)

Teacher: Ok now Shemdoe, chukua hii fimbo, charaza vilaza hawa wote kila mmoja viboko kumiโ€ฆ. Shemdoe akiwa amevimba kichwa, akawatwanga viboko kumi kumi vya kushiba darasa nzima

Teacher: Now, my dear Shemdoe tell this dumb students who a pharmacist isโ€ฆ

Shemdoe: Yes, sir. A Pharmacist is a farmer who assists people. Shemdoe saiv amelazwa MOI kwa wataalam wa mifupa ๐Ÿƒ

Angalia nilichomfanyia huyu dereva sasa

Tulikua kwa basi tunaelekea arusha,ile namcheki dereva kumbe ni best yangu na basi ilikua kwenye spidi hatari, nikaenda kumziba macho nkamuulizaย otea mi ni nani, kabla hajanijibu nikasikia kishindo kikubwa sana
NA SASA HIVI NIMEZINDUKA NIMEONA ABIRIA WOTE TUPO WODI NAMBA 3 HAPA KCMC MOSHI. ๐Ÿค•๐Ÿค•๐Ÿค•๐Ÿค•
SODA ZA WAGONJWA PLIIIZ!!! ๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ™

Haya mapenzi jamani! Umewah kumpenda kwa kihivi??

Sijui Kama ushawai fall in love ile haswaa..

yani unampenda mtoto hadi akikupigia ile sauti ilivo tamu unajiskia kutafuna na kuimeza hiyo simu

Akikuita tu “my love”unajiskia tu kuvua nguo mwenywe
..
hicho kiupendo ukiwa nae unajskia unaweza piga wanaume 8 kwa pamoja

Yani ile love mtashinda pamoja kutwa nzima afu usiku unakopa salio umpigie muongee

Yani yale mapenz kiasi ukiona love story za romeo na Juliet unaona hakuna wanachofanya coz mapenz yao hayafikii yenu..

ile true love akikuangalia machoni akuguse mashavu afu akwambie,”I love u”
Unajishikilia kwenye ukuta usizimie..

yani ukimfikiria unaweza kulala chini ya kitanda Ku dilute hiyo feeling coz ni too much..

Umewahi kufeel hivyo??

Kama ushawai experience hivyo?? Basi HIYO SIYO “LOVE” NI “BANGI” PLZ ACHA KUTUMIA!
#ishakua_biashara_kichaa

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About