SMS Nzuri: Meseji za Vihoja Vya Jumatano

Duh! Tamaa mbaya, cheki kilichompata Huyu

HAHAHAHAHAAAAAA DUH TAMAA MBAYA

Muokota makopo katika uokotaji wake wa makopo akaona chupa ambayo ndani kuna ki2, alipoifungua likatoka jitu la ajabu. Huku akitetemeka lile jitu likamwambia kijana asante sana kwa kuniokoa omba vi2 viwili sasa hivi. Kijana kwa hofu akaomba pesa za kumiliki magari na majumba ya kifahari. Ghafla fuko la hela na pete ya bahati vikadondoka. Akaambiwa ombi la pili,akasema nibadilishe niwe kivutio ili nipendwe sana nakina dada Hapohapo akageuzwa akawa chipsi yai.!!😂🤣🤣🤣

Huyu mtoto kaongea point kweli, angalia anachomwambia baba yake

Mtoto alimwuuliza baba yake,
Mtoto: Baba unaweza kumwachia hilo gari lako house boy/girl akaliendesha?
Baba: siwezi kumwachia gari langu hili aliendeshe ni ghali sana.
Mtoto: je mnaweza kumwachia chumba chenu house boy/girl kikiwa wazi na mkaenda kazini?
Baba: haiwezekani kamwe kuna vitu vya gharama na pia heshima haitakuwepo.

Mtoto: unaweza ukampa house boy/girl ATM CARD yako na namba ya siri ukakuchulie pesa?

Baba: mtoto unatafuta balaa sasa, unataka siku akiiba hii card akachukue pesa zote tuwe maskini, sithubutu.

Mtoto: aahaaaaaa, kumbe hauwezi kumkabidhi chochote chenye thamani house boy/ girl, sasa kwa nini mnanikabidhi mimi kwa house boy/girl na nyie mnaenda kazini mpaka mnarudi kumbe mimi sina thamani kwenu eeeeh!

Je, hii ni kweli kwa wale wasichana wasiojibu meseji WhatsApp!!!?

Ukiona hivyo ujue ndio hivi

Mwanaume mwenzangu ukiona unamtext msg msichana WhatsApp kaisoma hajajibu, umetuma ya pili kasoma hajajibu, ukatuma ya tatu hajajibu mmmmmh😨😨 hapo ujue mwenzio kaangalia kwenye profile yako, kakagua picha weee mwishoni akajisemea tu “Huyu.mkaka hapana kwa kweli”🤣🤣🤣🤣🤣🤣

🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂

Usichokijua kuhusu sungura, panya na jamii yao

JE WAJUA?

Sungura, panya na Jamii zao huwa na mwendo wa kukimbia na kuruka muda wote na umri wao wa kuishi ni miaka 15. Kobe ni mnyama mwenda pole, asiye na papara wala pilika, muda mwingi hujificha na kupumzika ndani ya jumba lake akikwepa maadui. Umri wa kuishi kobe hufikia hadi miaka 300.
FUNZO: Mazoezi ni kiinimacho na uongo mtupu. Jipumzikie mwaya!!!
🏃🏾🏃🏿‍

Sababu ya jamaa kujiita fara ugenini

MZEE:”sasa huyu mgeni sijui alale wap?”
MKE:”saa hizi ni usiku akalale na Bebi.”
jamaa akaona huyo Bebi pengne mtoto anakojoa kitandani au akalia asije msumbua usiku
JAMAA:”msipate tabu mi ntalala hapa kwenye kochi” akalala
asubh wanakunywa chai akaibuka mrembo,jamaa akapigwa bumbuwazi almanusra ajimwagie chai.
BINTI:”Naitwa BEBI,we unaitwa nani?”
Jamaa akasema mimi naitwa Fara…..!

Angalia huyu secretary anavyomjibu bosi wake

Boss mmoja aliingia kazini kwake kasahau kufunga zipu ya suruali yake sasa secretary wake akamfuata na mazungumzo yakawa hivi:

SECRETARY: Boss leo umesahau kufunga geti nyumbani kwako…

Boss akabaki anashangaa… Baadae wakati anakwenda chooni kujisaidia ile anataka kufungua zipu akaikuta iko wazi ndio akajua alichokuwa ameambiwa na Secretary wake.

Akarudi mpaka kwa secretary na mazungumzo yakaendelea:

BOSS: Bibie ulivyoona geti wazi je uliona benz langu lime paki au…?

SECRETARY: Hapana Boss niliona kitoroli kidogo kimepaki kina matairi mawili

Alichojibu dalali baada ya kufumwa na mke wa mtu ndani ya nyumba ya kupanga

Dalali aliwatafutia jamaa chumba Buguruni karibu na reli, nyumba nzuri sana. Jamaa na mkewe wakahamia kwa furaha, lakini furaha yao iliisha walipokuja gudundua nyumba ile iko karibu mno na reli treni ikipita mpaka kitanda kinacheza.

Siku hiyo dalali akapita mke akamwita na kumwambia tatizo wakati treni inapita, wakaanza kubishana, yule mama akamwambia dalali kwa kuwa kuna treni itapita sasa hivi… njoo ndani uone mwenyewe.

Bahati mbaya wakiwa wamejilaza kitandani ili dalali aone adhabu wanayopata, Mzee mwenye mali alirudi ghafla, akauliza,

‘Nyie mnafanya nini hapa?’

Masikini dalali kwa woga mkubwa akajibu’ Tunangoja treni’

Baada ya mwanamke kukataa kufungua mlango angalia kilichomkuta

MUME: Fungua mlango!

MKE: Leo sifungui! Nimechoshwa na ulevi wako.

MUME: kama hufungui najitupa kwenye hili shimo nife kabisa.

MKE. Kufa huna faida yoyote duniani!

MUME kachukua jiwe kubwa kalitupa kwenye shimo chubwiiiiiii!

MKE kajifunga kanga, kafungua mlango. Ghafla mume kaingia ndani na kumfungia mke nje.

MKE: Nifungulie la sivyo nitapiga kelele majirani waje.

MUME: Piga kelele na wakija uwambie unakotoka usiku huu na khanga moja.

Kizungu nacho ni sheeeedeer

Mtalii: Do you have vegetables here.
Mtafsiri: Mnavyo vijimeza hapa.
Waiter: Vijimeza vidogo hatuna.
Mtafsiri: No sir, they don’t have.
Mtalii: OK, fine, do you have hot dogs.
Mtafsiri: Sawa, je mnao mbwa wa moto.
Waiter: Loh! Bwana we, hatupiki mbwa hapa.
Mtafsiri: They don’t cook here
Mtalii: What type of snacks do you have here.
Mtafsiri: Aina ngapi ya nyoka mnao hapa,
Waiter: We bwana we hapa hatupiki aina yeyote
ya nyoka, mwache akale nyumbani kwao.
Mtafsiri: They don’t cook any type of snacks
here,
maybe you can go back and eat at home.
Mtalii: OK, at least give us a cocktail juice.
Mtafsiri: OK, tupatie hata juisi ya mkia wa jogoo.
Waiter: Hebu tokeni na bangi zenu hapa, tena
sasa hivi kabla sijakasirika.
Mtafsiri: Lets get out of here
😝😝😝😂😂😂
Usicheke pekeyako

Kilichotokea baada ya kuzamia sherehe

Pale unapozamia kwenye Dinner Party ya Jumuiya Fulani, sasa Lengo la Jumuiya hiyo ni kupata Fedha za kutunisha Mfuko wa Jumuiya…sasa unakakaa mbele kabisa ili Muda wa Msosi usichelewe na kukuta kwenye Buffee yamebaki maharage!

MC : “Papai zuri kabisa kutoka Newala, Papai Mwendokasi, hili ni Shilingi laki 1..jamani Papai,nipeni ofa!”

MOSHA : “Laki 3 hapaaa!”

“Jamani laki 3 pale kwa Mosha, Papai linaondoka jamani, papai hili ni self contained kabisa….papai jamani”

KIBOLIBO: “Milioni 1 hapaaa”

“Jamani Mambo yanazidi kunoga hapa!…Benedict Kibolibo anataka papai kwa milioni 1 jamani, linaondoka papai!”

RWEYEMAMU : “nitanunua Papai hilo kwa Milioni 5”

Haya sasa jamani Rweyemamu ametoa ofa ya Milioni 5 Jamani, nani mweingineee?”

Kimyaaa…

Haya jamani Papai kama hakuna Ofa basi Papai linakwenda kwa Rweyemamu!……..haya sasa Kuna Kuku hapa Jogoo kabisa, bei yake ni laki 6 jamani Jogoo twitter huyu!”

WEWE “Milioni Mojaaa!”( hapa umejiwahi wa kwanza na wewe uonekane upo huku ukijua kabisa Wakina Mosha na Rweyemamu lazima watampandia Dau Jogoo, tena dau kubwa”

MC: ee sasa Kumekucha Jamani, Kabasele anamtaka Jogoo kwa Milioni 1 jamani!….ofa nyingineeee!”

Kimyaaa…

Jamani Jogoo anakwenda kwa Kabasele jamani!…ofa nyinginee!

Kimyaaa….

Kimyaaa….

😝😝😝…hapa sasa ndio mfukoni kuna Buku jero,..huko kwengineko NMB nill balance…sasa unageuza mimacho kumtazama Mosha kama atapanda dau kwa jogoo👀(mama wee Mosha anachezea Simu!)…..unamtazama Rweyemamu (teh anatafuna Kuku)…..mama weee😝

MC: Haya jamani kama hakuna Mwingine basi zoezi letu liishie hapa na limekwenda kwa Mafanikio, Mpatieni Kabasele Jogoo wake!

Hapa sasa unapokea jogoo wako wa MILIONI kwa Tabasamu la Maiti….kule nyumbani Jogoo wako Mkubwa unauza elfu 20 lakini sasa haka kajogoo kapya Mkononi kanakuwa kazito utadhani umembeba John Cena👀…Mama weee hapa sasa vidari ulivyotafuna unaviona kama vimerudi kwenye Ulimi….Chicken wings zinataka kutokea Masikioni…..Uuuuwiiiii,😝😝😝

Na hapa sasa kabla Dinner haijaisha ndipo unapojikuta Umebuni Cocktail ya Sparetta na Tomato😂😝😝😝😂.
chiel wie okee

Kali za leo: Misemo ya kuchekesha na kuvunja mbavu

1. Ati wee ni m-black mpaka ukiingia kwa dinga(gari), dirisha zinakuwa tinted!

2. Kwenu kuchafu mpaka mende zinatema mate.

3. Vile wewe mfupi, ukipiga picha ya passport inatokea full.

4. Ati(house) yenu ina gate lakini hakuna fence.

5. Baba alienda ku buy ngombe akaona ikikojoa akasema sitaki hiyo imetoboka.

6.Wee mblack mpaka ukikutana na mzungu afternoon anakusalimia: Good evening.

7. Mko wengi kwa house mpaka kuna rush hours na kukinyesha kunakuwa na jam.

8. Paka yenu noma mpaka ikishika panya inaomba chumvi, fork na pilipili.

9. We ni mrefu mpaka ukikunywa maziwa inafika kwa tumbo ikiwa mgando.

10.Wewe ni mweusi ukikanyanga makaa unawacha footprint nyeusi.

11. Kwenyu mkikunywa maji mnaitisha toothpick

12. We ni mbishi hadi ulikataa kuzaliwa uchi

13. Kwenu kuna insecurity ikifika usiku hadi geti mnaingiza ndani

14. Kwenu ni wengi sana hadi mmeweka round about ndani.

15. Wewe ni mlafi hadi maji uliyochemshia mayai unayafanya supu.

16. We ni mjinga sana hadi blood test ulifeli.

17. Una chogo refu hadi ukigeuka haraka unaweza kuliona.

18. Una kichwa kikubwa hadi ukiingia kwenye daladala konda anakwambia “abiria usiingie na mizigo, tunaweka juu kwenye carrier

Shopping Cart
2
    2
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About