SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF
Karibu AckySHINE
🤣😃😂
Chagua Unachotaka Kusoma Hapa
Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.
Tabia za kuepuka ili uweze kuwa tajiri
UKIWA NA HIZI TABIA 9, JIANDAE KUFA MASKINI…………
By Kashindi Edson
“Umasikini hauji kwa bahati mbaya kama ubaguzi wa rangi au ukoloni, umaskini hutokana na matendo ya kila siku ya mwanadamu” (Nelson Mandela, R.I.P)
“Kila mtu anataka kufanikiwa, lakini si kila mtu yuko tayari kushika majukumu na wajibu wa kumpeleka kwenye mafanikio”(Mwl Nyerere, R.I.P).
“Kile unahokifanya muda huu ndicho kinachoashiria na kutoa picha kamili ya baadae yako”(Mahatma Gandhi, R.I.P)
“Ukizaliwa maskini sio kosa lako, ila ukifa maskini hilo ni kosa”(Bill Gate, The richest man in the world).
Mwalimu wangu wa chuo aliwahi kuniambia kuwa, “mstari unaomtenganisha maskini na tajiri ni mwembamba sana, kwa hiyo ni rahisi sana kuwa tajiri pia ni rahisi sana kuwa maskini”. Mpaka leo sijaelewa alimaanisha nini.
Watu wote waliofanikiwa katika nyanja mbalimbali za maisha, kwenye uongozi, biashara, kilimo, elimu, siasa, michezo, uandishi, muziki, afya, imani, utangazaji, nk huwa hawana hizi tabia 9 nilizokuandalia leo, kwa hiyo kama una kiu ya mafanikio kwa hicho unachopambania, achana na haya mambo 9 yafuatayo;
1. KUTOKUJARIBU.
Katika kutafuta mafanikio huwa kuna vitu viwili tu vya kuchagua. Tambua kuwa maisha ni vita. “Chagua kufa, au kupambana”. “Siogopi kufa, naogopa kutokujaribu'(Jay Z). Hakuna alie zaliwa anajua, jiamini, jaribu utafanikiwa.
2. KUTOKUJIFUNZA.
Che Guava mpaka anafariki library yake ilikuwa na vitabu zaidi ya 2000, mwenzangu na Mimi sijui hata kama una Biblia au Quran ghetoni kwako. Nkwameh Nkrumah library yake ilikuwa na vitabu zaidia ya 3000, Obama anakuambia kila akiamka asbuhi lazima asome kitu kipya. “JOSEPH=Jifunze, Ona, Soma, Elimika, Pitia, Hamasika.(Prof Jay)
3. WOGA & WASIWASI.
“Tunaweza tukamsamehe mtoto anayeogopa gizani, lakini sio mtu mzima anaeogopa mchana”(Plato, R.I.P). Kitu cha kuogopa katika maisha ni woga wenyewe. Kama hujiamini hutakuja kuwa mshindi katika jambo lolote. Fanya hicho unachofikiria kukifanya kwa moyo wa dhati, kama unaamini ni cha harali na kia manufaa kwako na familia yako, na jamii nzima. Acha tabia ya kuogopa kitu ambacho hakijatokea.
4. KUJILINGANISHA.
Kuna baadhi ya watu, huwa wangetamani kuwa kama watu Fulani. Kuwa wewe pia jiamini. Usitamani kuwa Magufuli, Kassim Majaliwa au Paul Makonda. Kila mtu ni wa pekee na maalumu. Jikubali kwanza afu wengine ndo watakukubali wewe. Weka nguvu kwenye ubora wako na sio kwenye madhaifu yako. Ukijilinganisha sana utakosa furaha ya nafsi maisha yako yote.
*5. KUWEKA VINYONGO.**
“Kuweka chuki na konyongo moyoni ni sawa na kunywa sumu ukidhani atakufa mtu mwingine”. Onesha upendo, sambaza upendo, hayo ndo mafanikio ya kweli.
6. UONGO
“Uongo utakupa ushindi wa siku moja, ukweli utaishi milele”(WEUSI), “Muongo hata akiongoea ukweli usimuamini”(FID Q). Ukiwa muongo huwezi kufanikiwa hata siku moja. “Unaweza ukawadanganya watu, lakini huwezi kuwadanganya watu wote, wakati wote”(Bob Marley). Ukweli kama jua, katika safari ya mafanikio huwezi kuvificha.
7. UVIVU & UZEMBE
“Nyumba yenye njaa ukisizi unapata zero”(Fid Q). Mafanikio huja kwa kupenda unachokifanya. Neno “kazi” katika biblia limeandikwa mara 600. Dangote analala masaa 3 tu kila siku, Mohammed Dewj anaamka saa 11 asbuhi kila siku. We kwepa majukumu tu, kesho utakula magodoro. “Uvivu unalipa muda huu, bidii & juhudi vinalipa baadae”.
8. STAREHE & ANASA KUPINDUKIA
Pombe, sigara, ngono, unga, bange, shisha, cocaine, nk vitu vibaya sana. Ni ngumu sana kufikia mafanikio makubwa kama una tabia kama hizi. “Sisi ni kile tunacho kula”. Mafanikio ya kwanza huanzia kwenye afya yako”. Afya ni utajiri. Pia starehe hupoteza muda sana. “Mavuno ya uzee, ni swaga za ujana, kwa ukila ujana kumbuka kula kiungwana”(Nikki Mbishi,).
9. LAWAMA & UMBEA
“Watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiria hujadili kuhusu mawazo, uwezo wa kati hujadili kuhusu matukio na wale wenye uwezo wa chini, hujadili kuhusu watu” We upo kwenye kundi gani? Bora ukawa kundi la kati kuliko hilo la chini kabisa, hilo ni la “wachawi”. Tusilamike, tupambane,lawama hazisaidii chochote.Ukiweka malengo yako, vizuri na ukaacha hizo tabia hapo juu, muda si mrefu itazifikia ndoto zako
SMS tamu ya kimahaba ya kumuomba mpenzi wako asiende mbali na wewe
Mapigo yangu ya moyo huongezeka pindi nisipokuona japo kwa
dakika plz mpenzi kaa karibu yangu utulize mapigo
Meseji nzuri ya salamu kwa umpendaye
Pokea sms yangu iliyojaa utamu, nimeipamba kwa maneno laini yenye ladha adimu, utamu wake ni kama apple haufanani na ndimu, nimeituma kwako sms hii ikuletee salamu “UHALI GANI MPENZI?”
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Raha ya kuoa kijijini
Kuoa vijijini raha sana Hata ukiulizwa unafanya kazi gani ukiwaambia mimi ni admin basi daaaah wanaona wewe ni bonge la boss😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Alichokijibu chizi baada ya kuanguka ghorofani
Chizi kaanguka toka kwenye gorofa fasta watu wakamfuata kumsaidia wakamuulza VP IMEKUAJE?
Chz akajbu: ”HATA CJUI NA MIE NDO NAFIKA SASA HIVI
Mambo ya msingi kujua kuhusu ugonjwa wa ngiri
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikilia au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiliwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.
Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).
Tatizo la ngiri huweza kumpata mtu yeyote. Miongoni mwa vitu vinavyoweza kumsababisha mtu apate ugonjwa wa ngiri ni: Kuwa na uzito mkubwa wa mwili au kuongezeka uzito kwa ghafla, kazi ya kubeba au kunyanyua vitu vizito, tatizo la kukohoa au kupiga chafya kwa muda mrefu, ujauzito au matatizo yanayojitokeza kwa mwanamke wakati wa kujifungua pia kuharisha au kuvimbiwa (Constipation). Vitu hivyo pamoja na mtu kuwa na misuli au tishu zilizopoteza uimara au uwazi (opening or hole) humfanya mtu apate ngiri (hernia).
Ngiri hutambuliwa kwa kutokea kitu kama uvimbe au kujaa katika eneo husika (baadhi ya maeneo yametajwa hapo juu) na pia kwa kufanyiwa uchunguzi wa mara kwa mara na daktari huwezesha kugundua tatizo hili.
Njia inayoweza kutatua tatizo hili ni kwa mtu mwenye ngiri kufanyiwa upasuaji ili kurekebisha misuli au tishu zilizolegea. Pia kutegemeana na kihatarishi cha tatizo hili, mtu unaweza kuwa unafanya mazoezi ili kupunguza uzito wako na kuweka utaratibu mzuri wa kula chakula kinachojumuisha mboga mboga au matunda yenye nyuzi nyuzi (fibers), hii itasaidia pia mmeng’enyo (digestion) wa chakula tumboni na kuepusha kuvimbiwa. Matunda (Vitamin C) husaidia kuunganisha tishu zilizolegea na pia husaidia kupona haraka kwa sehemu iliyofanyiwa upasuaji (operesheni). Na kama tatizo lako ni la kukohoa kwa muda mrefu kunakosababishwa na uvutaji wa sigara, ni vyema ukasitisha uvutaji ili kupunguza madhara au makali ya ngiri lakini pia kusitisha sigara kwa ajili ya usalama wa afya yako.
Meseji ya pongezi kwa mpenzi wako
pongezi kwako mpenzi kuwa wangu mtetezi kwenye jahazi la
mapenzi,ufundi na ujuzi unao hasa tuwapo wawili
chumbani.penzi lako halichakai daima huzaliwa upya.
Kali za leo: Misemo ya kuchekesha na kuvunja mbavu
1. Ati wee ni m-black mpaka ukiingia kwa dinga(gari), dirisha zinakuwa tinted!
2. Kwenu kuchafu mpaka mende zinatema mate.
3. Vile wewe mfupi, ukipiga picha ya passport inatokea full.
4. Ati(house) yenu ina gate lakini hakuna fence.
5. Baba alienda ku buy ngombe akaona ikikojoa akasema sitaki hiyo imetoboka.
6.Wee mblack mpaka ukikutana na mzungu afternoon anakusalimia: Good evening.
7. Mko wengi kwa house mpaka kuna rush hours na kukinyesha kunakuwa na jam.
8. Paka yenu noma mpaka ikishika panya inaomba chumvi, fork na pilipili.
9. We ni mrefu mpaka ukikunywa maziwa inafika kwa tumbo ikiwa mgando.
10.Wewe ni mweusi ukikanyanga makaa unawacha footprint nyeusi.
11. Kwenyu mkikunywa maji mnaitisha toothpick
12. We ni mbishi hadi ulikataa kuzaliwa uchi
13. Kwenu kuna insecurity ikifika usiku hadi geti mnaingiza ndani
14. Kwenu ni wengi sana hadi mmeweka round about ndani.
15. Wewe ni mlafi hadi maji uliyochemshia mayai unayafanya supu.
16. We ni mjinga sana hadi blood test ulifeli.
17. Una chogo refu hadi ukigeuka haraka unaweza kuliona.
18. Una kichwa kikubwa hadi ukiingia kwenye daladala konda anakwambia “abiria usiingie na mizigo, tunaweka juu kwenye carrier
Je, hili nalo ulilipitia ulipokua Shuleni?
Hakuna Kitu Kilikua Kinaniumizaga Kipindi Nipo Shuleni.
Time Mmetoka Kwenye Mitihani Wa Mathematics Halafu Mpo Kikundi Fulani Either Mnarudi Nyumbani Au Mnapumzika Kwa Ajili Ya Next Exam.
Unasikia Jamaa Wanabishana Pale Jibu Lilikua 4 Mwingine Anasema 5, Na Wewe Ulijaza 80.
Sababu za magonjwa ya figo na jinsi ya kuondokana na janga la magonjwa ya Figo
1.Usichelewe kwenda HAJA. Kutunza mkojo kweye kibofu chako kwa muda mrefu ni wazo baya. Kibofu kikijaa kinaweza kusababisha uharibifu. Mkojo ambao unakaa kwenye kibofu huzidisha bakteria haraka.
Mara mkojo unaporudi nyuma ya njia na Figo, sumu dutu husababisha maambukizi ya figo, pia njia ya mkojo na “nephritis”, pamoja na “uremia”. Wakati wito asili (unahisi mkojo) fanya hivyo haraka iwezekanavyo.
2. Kula Chumvi kupita kiasi.
Inatupasa kula Chumvi isiyozidi 5.8 gramu kwa siku.
3. Kula nyama kupita kiasi.
Protini ikizidi sana katika mlo wako inadhuru figo zako. Mmeng’enyo wa Protini unazalisha amonia- sumu dutu ambayo ina uharibifu mkubwa kwa figo zako. Nyama nyingi inaleta uharibifu zaidi wa figo.
4. Unywaji mwingi wa “Caffeins”.
Caffein hutokana na vinywaji vya Soda na vinywaji vingine laini kama Kahawa, Redblue n.k. Hupandisha shinikizo la damu na figo zako kuanza mateso. Unapaswa kupunguza kiwango cha Coke, Pepsi, Red Bull, nk ambavyo hunywa kila siku.
5. Kutokunywa maji.
Figo zetu lazima zichakatwe vizuri kutekeleza majukumu yake vizuri. Endapo hatunywi ya kutosha, sumu dutu inaweza kuanza kukusanyika katika damu, kama hakuna kimiminika cha kutosha kutoa kwa njia ya figo. * Kunywa zaidi ya bilauri 10 za maji kila siku.
Kuna njia rahisi ya kuangalia kama unakunywa maji ya kutosha: Angalia rangi ya mkojo wako; Wepesi wa rangi, ndiyo vzuri.
6. Kuchelewa matibabu.
Tibu matatizo yako yote ya kiafya kwa uhakika na uwe unachunguza afya yako mara kwa mara. Wapendwa na wapenzi wangu, hebu tujisaidie wenyewe… Shirikisha wengine, kama unajali. —-
Pia epuka vidonge hivi, ni hatari sana:
D- baridi*
Vicks Action- 500*
Actified*
Coldarin*
Cosome*
Nice*
Nimulid*
Cetrizet- D
Hivi vidonge vina Phenyl propanol- amide PPA ambayo husababisha stroke na ni marufuku Marekani.
MWISHO… Tafadhali, kabla ya kufuta, msaidie rafiki yako kwa kumpitishia hii..!
Inaweza kumsaidia mtu!**
Wasambazie wengi kwa kadiri uwezavyo.
Shirikisha ujumbe huu kwa mpendwa wako.
Maonyo muhimu ya Afya
1. Jibu (pokea) simu wito na sikio la kushoto.
2. Usinywe dawa zako kwa maji baridi….
3. Usile milo mizito baada ya saa 11 jioni.
4. Kunywa maji vuguvugu mengi asubuhi na kiasi usiku. Usinywe maji baridi kamwe.
5. Muda bora wa kulala ni kutoka saa 4 usiku hadi saa 10 Alfajiri.
6. Usilale mapema baada ya kumeza dawa au baada ya mlo. Usiku, Kula chakula laini.
7. Usipokee simu yako ikiwa haina chaji. Wakati huo mionzi huwa ina nguvu mara 1000 .
Je, unaweza kuwasambazia watu unao wajali?
Mimi nimeshafanya kwako….!!.
SMS ya kumtumia mpenzi wako kumtakia mahangaiko mema ya kazi
Ukipata tutakula na wala usijali mpenzi wangu.
Ukikosa tutalala na hiyo itabaki siri yanguuuuuuuu.nakupenda mpz
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Chanzo, dalili, aina na matibabu ya ugonjwa wa kifafa
Huu ni ugonjwa ambao unasabababishwa na seli zilizopo katika mishipa ya fahamu zilizopo kwenye ubongo kutoa umeme[impulses] mwingi kuliko kawaida kwenda kwenye misuli na sehemu zingine za mwili, na kusababisha mtu kupata dalili kama vile kuishiwa nguvu, kichwa kuuma, kuchanganyikiwa, mwili kukakamaa na hata kupoteza fahamu. Hali hii hujirudia mara kwa mara.
Ifahamike kuwa, aina ya kifafa inayojulikana sana mitaani ni ile ambayo mtu anakakamaa na kupoteza fahamu, japokuwa kuna aina za kifafa ambazo mtu hakakamai wala kupoteza fahamu, kama tutakavyoona hapo baadae.
Mwaka 2013 ugonjwa huu uliua zaidi ya watu laki moja duniani, 80% wakiwa waafrika.
Mgonjwa huyu huweza kuanguka mara kadhaa kwa mwezi lakini anaweza asianguke kabisa kama anafuata masharti na utaratibu mzuri wa matibabu…
Chanzo cha ugonjwa wa kifafa ni nini?
Chanzo kikuu cha ugonjwa huu kwa watu wengi hua hakifahamiki lakini baadhi ya hiz ni moja ya sababu za kuugua kifafa.
Kurithi; familia na koo zingine zinakua na ugonjwa huu hivyo watoto na wajukuu huzaliwa tayari na ugonjwa huu.
Kuumia kichwa: ajali zinazohusisha kuumia kwa kichwa huweza kusababisha kuumia kwa mishipa ya fahamu na mtu kuugua kifafa.
Magonjwa mengine; kuna magonjwa mtu akiugua maishani mwake baadae huweza kupata kifafa kwasababu magonjwa hayo yanavyoharibu mfumo wa ubongo.. mfano homa ya uti wa mgongo kitaalamu kama meningitis.
Uvimbe kwenye ubongo: matatizo ya uvimbe kwenye ubongo kama kansa huweza kusababisha mtu kuugua kifafa.
Kiharusi; huu ni ugonjwa ambao husababishwa na damu kushindwa kupita vizuri kwenye ubongo au kupasuka kwa mishipa ya damu ya ubongo hali hii husababisha mtu kupooza nusu ya mwili wake na huweza kuugua kifafa baadae.
Matatizo wakati wa kuzaliwa: wakati mwingine mtoto huzaliwa kwa shida sana kwa njia ya kawaida kiasi kwamba kichwa chake hubanwa sana wakati wa kupita na hali hii huweza kumsababishia kifafa kwanzia utotoni.
Matatizo ya utengenezaji wa mtoto tumboni; wakati mwingine ile miezi mitatu ya kwanza ambayo mtoto ndio anapata viungo tumboni huweza kutokea kasoro kwenye mfumo wa fahamu za kwenye ubongo na kumfanya apate kifafa akizaliwa.
Magonjwa ya uzee yanayoathiri ubongo; kuna magonjwa huharibu ubongo wakati wa uzee na magonjwa haya huweza kusababisha kifafa kipindi hicho.
Aina za kifafa
Kuna aina mbili kubwa za kifafa:
1)Primary marygeneralized seizures
Hii ndio aina ya kifafa ambayo inafahamika sana mitaani; na inahusisha mgonjwa kukamaa, na kupoteza fahamu, pamoja na dalili zingine kama vile kutoa povu mdomoni, na kujisaidia haja kubwa na/au ndogo bila kujitambua akishikwa na hali hiyo.
Pia wengine hupatwa kama na wazimu au kuchanganyikiwa kwa muda kabla au baada ya kushikwa na hali hiyo.
2)Partial seizures
Aina hii ya kifafa ni ile ambayo haihusishi muhusika kupoteza fahamu na kukakamaa!! Bali hushikwa na hali fulani kama ya bumbuwazi kwa dakika kadhaa; Wengine huwa na dalili zisizoeleweka za mara kwa mara kama vile kusihiwa nguvu, kizungu zungu, kichwa kuuma sana (bila sababu ya kiafya inayojulikana), na kadhalika. Aina hizi za kifafa ziko nyingi, na dalili hutofautiana kwa kadri ya aina ya kifafa!!
Vipimo vinavyofanyika kugundua kifafa
Ugonjwa huu unaweza kutambulika kwa daktari kuchukua historia ya dalili zinazomkabili muhusika tu(hakuna kipimo ambacho kinaweza kutambua kifafa kwa asilimia 100); Kuna kipimo kinachopima jinsi ubongo unavyotoa taarifa za umeme (ELECTROENCEPHALOGRAM-EEG), ambacho kinaweza kutambua kifafa, lakini kipimo hiki kinaweza kikaonekana kuwa hakina shida, na bado mtu akawa na tatizo hilo la kifafa. Hivyo basi, kifafa ni moja kati ya magonjwa machache ambayo kutambulika kwake kunategemea sana ujuzi na utaalamu wa daktari katika kuunganisha dalili za mgonjwa kuliko vipimo!!
Hata hivyo, mara nyingi nyingi mgonjwa hupimwa vipimo tofauti ili kuweza kujua chanzo cha ugonjwa… mfano
• Uwezo wa kufanya kazi figo
• Uwezo wa kufanya kazi maini
• Kupima maji ya uti wa mgongo
• Kupima Kaswende
• Picha ya ubongo mfano CT SCAN.
Mambo yanayofanya kupata degedege za kifafa mara kwa mara..
• Kukosa usingizi kwa muda mrefu
• Mianga na miale ya disko
• Unywaji wa pombe
• Kuishiwa sukari mwilini wakati wa akisikia njaa kali.
• Kutomeza dawa kama ilivyoelekezwa
Huduma
Matibabu yasiyo ya dawa wakati mgonjwa amekamatwa na kifafa:{non pharmacological treatment}yaani HUDUMA YA KWANZA
• Mzuie mgonjwa asijiumize kwa kuweka kitu laini chini ya kichwa chake, ondoa vitu vikali karibu yake kama kisu, sindano au vyuma.
• Usilazimishe kitu chochote kwenye mdomo wa mgonjwa.
• Usimshike kuzuia mizunguko yake
• Weka kichwa alale anaangalia upande mmoja ili kutoa mate mdomoni.
• Kaa na mgonjwa mpaka degedege ziishe
• Usiweke chochote mdomoni kwa mgonjwa kama dawa au chakula mpaka apate fahamu zake.
Mtu mwenye kifafa hali hii ya kukamatwa na degedege za kifafa sio ya ajabu sana ila ukiona dalili hizi mkimbize hospitali..
• Degedege za kifafa zaidi ya dakika kumi
• Kutapika sana
• Kushindwa kuona vizuri
• Kupoteza fahamu
• Kichwa kuuma sana.
MATIBABU YA UGONJWA
Kama kawaida chanzo cha ugonjwa kikipatikana mgonjwa huanzishiwa matibabu lakini kama mgonjwa alikua tayari ameshapata madhara kwenye ubongo kulingana na chanzo husika ataendelea kua na kifafa.
Ugonjwa wa kifafa hauponi kabisa kwa 100% hospitali, ukishaambiwa una kifafa au mgonjwa wako ana kifafa basi utapewa utaratibu wa matibabu yaani kumeza dawa siku zote za maisha yako na kufuata baadhi ya masharti na utaishi maisha ya kawaida kabisa.
Cheki kilichonipata sasa, ungekua wewe ungefanyaje?
Siku moja katika pitapita zangu nikakutana na mtoto mmoja mkali balaa yaani ni mzuri sanaaaa, moyo ukanituma nimuimbishe mtoto akakubali kwamba nitafute siku tukae tuongee vizuri akasema nimpe namba yangu ya simu.
Ebwana si akatoa simu hiyo inauzwa laki sita mimi hapa nina kisimu cha tochi tena nimefunga na rababendi
Je, wewe ungeendelea kumtajia namba zako!!!
Vipodozi Visivyo Salama/Vilivyopigwa Marufuku Na Madhara Yake
SEHEMU YA KWANZA
1.0 UTANGULIZI
Vipodozi visivyo salama ni vipodozi ambavyo vina kemikali zinadhuru au zinazoweza kuudhuru mwili na kuusababishia matatizo. Maana hii inaweza kuongezewa na kujumuisha vipodozi vyote ambavyo usalama wake unatia mashaka na vinaweza kuleta madhara kwa mtumiaji.
Hivyo hujumuisha :
-Vipodozi ambavyo havijasajiliwa na mamlaka ya chakula na dawa Tanzania (TFDA)
-Vipodozi vyenye viambata (kemikali) vya sumu na vilivyopigwa marufuku na mamlaka ya chakula na dawa Tanzania (TFDA)
-Vipodozi ambavyo muda wake wa matumizi umeisha
-Vipodozi ambavyo havioneshi tarehe ya kuharibika (mwisho wa matumizi)
-Vipodozi ambavyo maelezo yake hayajaandikwa kwa Kiswahili au kiingereza
Vinaweza vikawa ni mafuta, losheni, krimu, pafyumu, poda na kadhalika.
1.1 VIAMBATA (KEMIKALI) VYA SUMU VILIVYOPIGWA MARUFUKU
Vingi vikiwa katika lugha ya kiingereza, hizi ndizo kemikali ambazo huongezewa katika vipodozi ili kufanikisha au kusaidia dhumuni lililolengwa kwa kipodozi husika. Viambato vyenye sumu vilivyopigwa marufuku ni:
- Chloroquinone (Hydroquinone na kemikali zingine)
- Steroids (Mifano ni Betamethasone, Beclomethasone, Hydrocortisone, Clobetasol, na Dexamethasone)
- Mercury (Zebaki) na kemikali zinazotokana nayo
- Chloroform
- Bithionol
- Hexachlorophene
- Mercury (Zebaki) na kemikali zinazotokana nayo
- Vinyl chloride
- Zirconium na kemikali zinazotokana nayo
- Methyelene chloride
- Halogenated salicylanilides (Dimetabromsalan, Trimetabromsalan na Tetrabromsalan)
- Chlorofluorocarbons (Kwenye pafyumu na deodorants)
1.2 JINSI YA KUJUA KAMA KIPODOZI KINA KIAMBATO (KEMIKALI) CHA SUMU KILICHOPIGWA MARUFUKU
Angalia kwenye lebo ya kipodozi chako sehemu waliyoandika Ingredients au Contents au neno jingine lolote lenye maana ya Vitu vilivyomo ndani. Hapo angalia kama kuna kiamabato au kemikali yoyote ambayo nimeiandika hapo juu kuanzia namba 1 mpaka 12.
Kama kuna kiambato au kemikali ambayo imepigwa marufuku basi jua kipodozi chako sio salama. Acha kukitumia mara moja na toa taarifa kwa mamlaka ya chakula na dawa Tanzania (TFDA).
Kama hakuna kiambato cha sumu basi kipodozi chako kinaweza kuwa salama. Tatizo linakuja pale watengenezaji wanapofanya uhuni kwa kudanganya au kuficha na kuacha kuandika baadhi ya viambato vilivyomo ndani. Ambalo pia ni kosa kisheria.
Mifano
- Sabuni ya JARIBU ina kiambato MERCURY. Sabuni hii sio salama, haifai kwa matumizi na imepigwa marufuku.
- Losheni/krimu ya MEKAKO ina kiambato HYDROQUINONE. Losheni/krimu hizi sio salama, hazifai kwa matumizi na zimepigwa marufuku
- Krimu za FAIR & LOVELY SUPER CREAM, VISIBLE DIFFERENCE CREAM, SKIN SUCCESS FADE CREAM, DEMOVATE NA DIPROSON CREAM zina viambata Krimu hizi sio salama kutumika kama vipodozi na zimepigwa marufuku
SEHEMU YA PILI
2.0 MADHARA YA VIPODOZI VISIVYO SALAMA
Vipodozi visivyo salama vina madhara mengi sana kwa afya ya mtumiaji. Na kama mtumiaji ni mjamzito basi madhara hayo yanaweza kumpata na mtoto aliyepo tumboni.
Pia vipodozi hivi vina athari nyingi sana kiuchumi kwani vitapelekea mtu kutumia pesa tena kugharamia matibabu ya matatizo atakayopata. Madhara hayo ni pamoja na:
-Ugonjwa wa saratani (kansa) ya ngozi, maini, ubongo, mapafu, mfumo wa damu, utumbo mpana na kibofu cha mkojo
-Uharibifu wa ngozi, macho, ini, mapafu na figo
-Magonjwa ya moyo na kutopumua vizuri
-Kutokwa na chunusi kubwa kubwa
-Ngozi kuungua, maumivu makali, ngozi kuwa nyekundu na kutokwa na vipele
-Ngozi kuwa nyembamba sana na laini na endapo ngozi itapata jeraha au kufanyiwa upasuaji, kidonda kitachelewa kupona au hakitapona
-Mzio (Allergy) na muwasho wa ngozi
-Kichefuchefu, kutapika, kusikia usingizi na kizunguzungu
-Magonjwa ya akili, mishipa ya fahamu (hasa kichwani)
-Uharibifu wa ubongo na mtindio wa ubongo kwa watoto wachanga na waliopo tumboni
-Ngozi kuwa laini na kusababisha kupata magonjwa kama fangasi kwenye ngozi au maambukizi ya vimelea vya maradhi
-Kuchubuka kwa ngozi
-Ngozi kuwa na mabaka meusi na meupe au rangi mbalimbali
-Upofu, uziwi na upotevu wa fahamu wa mara kwa mara
-Kuumwa kichwa, kusikia kizunguzungu na kupoteza fahamu
2.2 USHAURI
Kama tulivyoona hapo juu mengi ya madhara ya vipodozi visivyo salama ni makubwa na huhatarisha kabisa afya za watumiaji na watoto. Hivyo ni vyema kuvijua na kuviepuka kabisa ili usiweze kupata madhara.
Pili msaidie kumuelimisha ndugu, jamaa na rafiki nay eye ajue na asitumie kabisa vipodozi visivyo salama
Pia ukiona mtu au duka ambalo linauza vipodozi visivyo salama acha kununua vipodozi kutoka kwake na toa taarifa kwa mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa
Epuka kabisa vipodozi visivyo salama. Hata kama vinakuletea matokeo mazuri kiasi gani.
SEHEMU YA TATU
3.0 ORODHA YA VIPODOZI VISIVYO SALAMA NA VILIVYOPIGWA MARUFUKU TANZANIA
Vifuatavyo ni vipodozi visivyo salama na vimepigwa marufuku kutumika. Epuka kabisa kutumia vipodozi hivi hata kama vinakuletea matokeo mazuri kiasi gani.
3.1 Krimu, Losheni na Jeli zenye kiambato cha Hydroquinone
- Mekako Cream
- Rico Complexion Cream
- Princess Cream
- Butone Cream
- Extra Clair Cream
- Mic Cream
- Viva Super Lemon Cream
- Ultra Skin Tone Cream
- Fade-Out Cream
- Palmer’s Skin Success (Pack)
- Fair & White Active Lightening Cream
- Fair & White Lightening Cream
- Fair & White Strong Bleaching Treatment Cream
- Fair & White Body Clearing Milk
- Maxi-Tone Fade Cream
- Nadinola Fade Cream
- Clear Essence Medicated Fade Cream
- Peau Claire Body Lotion
- Reine Clair Rico Super Body Lotion
- Immediate Claire Maxi –Beauty Lotion
- Tura Lotion
- Lkb Medicated Cream
- Crusader Skin Toning Cream
- Tura Bright & Even Cream
- Claire Cream
- Miki Beauty Cream
- Peau Claire Crème Eclaircissante
- Sivoclair Lightening Body Lotion
- Extra Clair Lightening Body Lotion
- Precieux Treatment Beauty Lotion
- Clear Essence Skin Beautifying Milk
- Tura Skin Toning Cream
- Madonna Medicated Beauty Cream
- Mrembo Medicated Beauty Cream
- Shirley Cream
- Kiss – Medicated Beauty Cream
- Uno21 Cream
- Princess Patra Luxury Complexion Cream
- Envi Skin Toner
- Zarina Medicated Skin Lightener
- Ambi Special Complexion
- Lolane Cream
- Glotone Complexion Cream
- Nindola Cream
- Tonight Night Beauty Cream
- Fulani Cream Eclaircissante
- Clere Lemon Cream
- Clere Extra Cream
- Binti Jambo Cream
- Malaika Medicated Beauty Cream
- Dera Heart With Hydroquinone Cream
- Nish Medicated Cream
- Island Beauty Skin Fade Cream
- Malibu Medicated Cream
- Care Plus Fairness Cream
- Topiclear Cream
- Carekako Medicated Cream
- Body Clear Cream
- A3 Skin Lightening Cream
- Ambi American Formula
- Dream Successful
- Symba Crème Skin Lite ‘N’ Smooth
- Cleartone Skin Toning Cream
- Ambi Extra Complexion Cream For Men
- Cleartone Extra Skin Toning Cream
- O’nyi Skin Crème
- A3 Triple Action Cream Pearlight
- Elegance Skin Lightening
- Clere Cream
- Clear Touch Cream
- Crusader Ultra Brand Cream
- Ultime Skin Lightening Cream
- Rico Skin Tone Cream
- Baraka Skin Lightening Cream
- Fairlady Skin Lightening Cream
- Immediate Claire Lightening Body Cream
- Jaribu Skin Lightening Lotion
- Amira Skin Lightening Lotion
- A3 Clear Touch Complexion Lotion
- A3 Lemon Skin Lightening Lotion
- Kiss Lotion
- Princess Lotion
- Clear Touch Lotion
- Super Max-Tone Lotion
- No Mark Cream
- Body Clear
- Top Clear
- Ultra Clear
- Peau Claire Lightening Body Oil
- G &G Dynamiclair Lotion
- G & G Teint Uniforme
- G & G Cream Lightening Beauty Cream
- Dawmy – Lightening Body Lotion
- Maxi White Cream
- Bioclare Lightening Body Lotion
3.2 Vipodozi vingine vyenye Hydroquinone
- Fair & White Powder (Exclusive Whitenizer & Serum)
- New Youth Tinted Vanishing Cream
- Skin Success Fade Cream Regular
- Teint Clair Clear Cpmplexion Body Lotion
- Mareme Cream
- Si Clair Plus Cream
- Clair & White Body Cream
- Body White Lotion
- Bio Claire Cream
- Forever Aloe MSM Gel
- Kroyons Baby Oil
- 3.3 Sabuni zenye kiambato cha Hydroquinone
- Body Clear Medicated Antiseptic Soap
- Blackstar
- Cherie Claire Body Beauty Lightening & Treating Soap
- Immediate Claire Body Beauty Soap
- Lady Claire
- G.C Extra Clear
- Top Clear Beauty Complexion Soap
- Ultra Clear
- 3.4 Vipodozi vyenye Hydroquinone pamoja na Steroid
- Clear Essence Skin Beautifying Milk For Sensitive Skin
- Fair & White Clarifiance Fade Cream
- Fair & White Exclusive Whitenizer Body Lotion
- Fair & White Exclusive Whitenizer Cream
- Fair & White Exclusive Whitenizer Gel
- Fair & White Maxitone Lightening Lotion Sun Block
- Fair & White So White Skin Perfect Gel
3.5 Sabuni zenye kiambato cha Mercury (Zebaki) na michanganyo yake
- Movate Soap
- Miki Soap
- Jaribu Soap
- Binti Jambo Soap
- Amira Soap
- Mekako Soap
- Rico Soap
- Tura Soap
- Acura Soap
- Fair Lady
- Elegance
- Block & White Skin Whitener Germicidal Bath Soap
- Rose Beauty Soap
- Maxi-Tone Soap (Skin Lightening Soap)
- Margostara Soap (New Tannin)
- Rusty – Whitening Soap (New Formula)
- Emani Natural Fair Pearls Soap
3.6 Krimu zenye kiambato cha Mercury na michanganyiko yake
- Pimplex Medicated Cream
- New Shirley Medicated Cream
3.7 Krimu zenye Steroids (Betamethasone, Beclomethasone, Hydrocortisone, Clobetasol,
Dexamethasone nk)
- Amira Cream
- Jaribu Cream
- Fair & Lovely Super Cream
- Neu Clear Cream Plus (Spots Remover)
- Age Renewal Cream
- Visible Difference Cream (Neu Clear Spots Remover)
- Body Clear Cream
- Sivo Clair Fade Cream
- Skin Balance Lemon Cream
- Peau Claire Cream
- Skin Success Cream
- M & C Dynamic Clair Cream
- Skin Success Fade Cream
- Fairly White Cream
- Clear Essence Cream
- Miss Caroline Cream
- Lemonvate Cream
- Movate Cream
- Soft & Lovely Cream
- Mediven Cream
- Body Treatment Cream (Spots Remover)
- Dark & Lovely Cream
- Sivo Clair Cream
- Musk – Clear Cream
- Fair & Beautiful Cream
- Beautiful Beginning Cream
- Diproson Cream
- Demovate Cream
- Top Lemon Plus
- Lemon Cream
- Beta Lemon Cream
- Tenovate Cream
- Unic Clear Super Cream
- Topifram Cream
- First Class Lady Cream
3.8 Vipodozi vingine vyenye kiambato cha Steroid
- Fashion Fair Gel Plus
- Hot Movate Gel
- Hyprogel
- Mova Gel Plus
- Secret Gel
- Secret Cream
- Peau Claire Gel Plus
- Hot Proson Gel
- Skin Success Gel Plus
- Skin Clear Gel Plus
- Soft & Beautiful Gel
- Skin Fade Gel Plus
- Ultra – Gel Plus
- Zarina Plus Top Gel
- Action Demovate Gel Plus
- Prosone Gel
- Skin Balance Gel Wrinkle Remover
- TCB Gel Plus
- Demo – Gel Plus
- Regge Lemon Gel
- Ultimate Lady Gel
- Topifram Gel Plus
- Clai & Lovely Gel
- Fair & White Serum Exclusive Whitenizer
- Maxi White Lightening Body Milk
- Maxitone Cleansing Milk
- Avoderm Cream
- Niomre Cream
- Niomre Lotion
- Nyala Lightening Body Cream
- Si Clair Cream
- Cute Press White Beauty Lotion
- White SPA Rose Lotion
- White SPA UV Lightening Cream
3.9 Vipodozi vya kupunguza unene vilivyopigwa marufuku
- Bio Valley Sliming Gel
3.10 Vipodozi vya nywele vilivyopigwa marufuku
- African Gold Super Glo
- Sofn Free Hair Foodblue Cap Shampoo
- Marhaba Anti-Dandruff Hair Cream
- Blue Cap Spray
- Blue Cap Cream
3.11 Vipodozi vinginevyo vilivyopigwa marufuku
- Bio Light Cream
- Salon Dermaplex Amazon Clay 9Normal To Dry Skin)
- Beauty Secrets Body Cream
- Swiss Soft N White Lightening Gel
- Whitening Complex Mask
3.12 Vipodozi Vinavyosababisha muwasho vikitumika karibu na macho
- Eye Shadow Gel
- Eye Shadow Gel 02
- Eye Shadow Gel 07
- Eye Shadow Gel 08
- Eye Shadow Gel 09
- Eye Shadow Gel 10
TAHADHARI : VIPODOZI VISIVYO SALAMA VIPO VINGI ZAIDI YA HIVYO AMBAVYO VIMEORODHESHWA HAPO JUU NA VINGINE VINGI ZAIDI VINAWEZA VIKAFIKA SOKONI.
Mara zote kuwa makini na vipodozi na pata taarifa, elimu na ushauri kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) na wataalam wa afya, urembo na vipodozi.
Mabinti wengine kwa kupenda hela! cheki huyu anachokifanya
Phone call
gal: hellow
Boy: sweety mambo vipi?
Girl: poa
Boy: utakuwa free weekend? nilikuwa nataka uje nyumbani
Girl: oh sorry ctoweza kuja sababu kuna haruc ya aunt yangu
Boy: kama ni hivyo sawa nilikuwa nataka nikufanyie sapraiz nimekununulia BLACKBERRY.
Girl: oh ucjal ntakuja na hata ntalala huko huko
Boy: na haruc je?
Girl: nilikuwa nakutania
Boy: hata mi nilikuwa nakutania
Nilichokifanya wakati naangalia taarifa ya habari
Jana wakati naangalia taarifa ya habar mtangazaji akasema “mpenz mtazamaji nataka nikupeleke moja kwa moja had marekani” nikazima TV kwa haraka nikaenda kuvaa viatu. Hadi sahv bado nmekaa hapa seblen nahisi bado wanaihangaikia Visa yangu
😂😂😂😂😂😂
Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia mvuke
Mvuke husaidia kusafisha ngozi. Ni rahisi sana kutumia mvuke kutibu chunusi.
Chemsha maji kwenye sufuria jikoni funika na uache nafasi kidgo ya mvuke uwe unatoka, kisha chukua taulo na ujifunike usoni huku ukisogelea karibu na mvuke unapokea na uruhusu mvuke huo ukupate kwa mbali.
Baki hapo kwa dakika 5 mpaka 10 hivi huku ukiwa umetulia (relaxed). Huu mvuke utakusaidia pia kujisikia mtulivu na kukuondolea mfadhaiko wa akili.
Mwishoni mwa zoezi jisafishe uso wako na maji ya baridi.
Endelea kusoma makala hii kujifunza zaidi dawa nyingine za asili za kutibu chunusi.
Kama simu yako ina wifi
Kama simu yako ina Wi-fi ujue uko na mke wa mtu 😂😂😂😂😂😂🙌🏼🙌🏼🙌🏼🙌🏼🙌🏼
Mambo ya kuzingatia kujikinga na chunusi | Jinsi ya kuzuia
Mambo mhimu ya kuzingatia
1. Fanya mazoezi ya viungo kwa saa moja kila siku
2. Kunywa maji mengi kila siku
3. Ondoa mfadhaiko (stress)
4. Weka homoni sawa kama hazipo sawa
5. Kuwa msafi wa mwili wote kila mara
6. Usiziguse chunusi au kuzitoboa na mikono yako au na chochote kuepuka makovu yasiyo ya lazima
7. Epuka vyakula vifuatavyo kama unasumbuliwa na chunusi kila mara, navyo ni pamoja na:
a)Vyakula vyenye mafuta sana
b)Vyakula vinavyopikwa katikati ya mafuta mengi
c)Kahawa
d)Chai ya rangie)
e)Pombe na vilevi vingine
f)Chokoleti
g)Popcorn
h)Maziwa
i)Mapera
j)Vyakula vya kwenye makopo
k)Pizza
Recent Comments