Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Jinsi ya kutengeneza Wali Wa Dengu Kwa Samaki Wa Kukaanga

Mahitaji

Mchele wa basmati – 3 Vikombe

Dengu – 2 vikombe

Viazi – 3 vikubwa

Kitunguu – 2 kubwa

Nyanya – 2

Pilipili mbichi kubwa – 3

Pilipilimanga – ½ kijiko cha chai

Garama Masala (bizari mchanganyiko) -1 kijiko cha chai

Supu ya vidonge (stock cubes) – 2 vidonge

Chumvi – kiasi

Mafuta – ¼ kikombe

Zaafarani – 1 kijiko cha chai

Samaki wa kukaanga

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Dengu kama sio za tayari kwenye kopo, roweka na zichemshe hadi ziwive

Maandalizi ya Masala Ya Dengu:

Zaafarani – iroweke katika maji ya dafu dafu (warm) ya chini ya robo kikombe weka kando.
Osha mchele, roweka.
Menya viazi na vitunguu, katakata vitunguu, na nyanya , weka kando.
Katakata viazi vipande vidogo vidogo kwa umbo la mchemraba (cubes).
Katika sufuria tia mafuta yakipata moto, tia viazi ukaange kidogo kwa moto mdogo mdogo hadi kukaribia kuwiva, toa weka kando.
Kaanga vitunguu hadi vigeuka rangi ya hudhurungi isiyokoza (light brown) kisha tia nyanya ukaange kidogo.
Tia vidonge vya supu (stock cubes) uvivuruge katika mchanganyiko, katakata pilipili mbichi kwa urefu tia, uendelee kukakaanga. Tia bizari, chumvi.
Zima moto, changanya dengu na viazi katika mchanganyiko huo.

Mapishi ya Wali:

Chemsha mchele kama kawaida ya kupika wali mweupe, kiini kiwe kimewiva nusu yake.
Chuja maji kisha changanya katika mchanganyiko wa dengu.
Nyunyizia zaafarani, uchanganye wali na mchanganyiko kidogo tu.
Funika acha uive katika mtoto mdogo mdogo au tia katika oveni hadi uive kama kawaida ya kupika wali.
Pakua katiha sahani na tolea na samaki yoyote wa kukaanga.

Matumizi ya maji kutibu shinikizo la chini la damu

Matumizi ya maji ya kunywa ni moja ya dawa rahisi kabisa ya shinikizo la chini la damu.

Hii ni kwa sababu Maji ni mhimu kwa kila ogani ndani ya mwili iweze kufanya kazi zake sawa.

Kwa hiyo sababu kuu ya mtu kuwa na shinikizo la chini au hata la juu ni matokeo ya mishipa ya damu kutokuwa na vimiminika vya kutosha.

Mishipa ya damu imeundwa kwa maji maji ya damu (serum) na seli za damu.

Maji yanapopungua kwenye mwili hata vipenyo vya mishipa yako navyo hupungua ukubwa wake jambo linaloleta kushuka kwa shinikizo la damu.

Matatizo yote haya ni matokeo ya kutokunywa maji ya kutosha kila siku.

Kwa sababu hii, ili kupandisha juu shinikizo la damu unahitaji kunywa zaidi maji sambamba na juisi nyingine za matunda au za mboga mboga kila siku.

Hii inasaidia kuongeza vimiminika katika mishipa ya damu.

Huyu jamaa bonge la bwege, ungekua wewe ndiyo rafiki ake ungemwambiaje?

RAFIKI: Vipi mbona leo huna uchangamfu
JAMAA: Wanawake bwana, mwanamke hata umpendeje atakugeuka tu
RAFIKI: Nini tena ndugu yangu? Mbona shemeji mtu fresh sana
JAMAA: Hata mimi nilikuwa najua hivyo, leo nimegundua kumbe ana siri kubwa sana
ananificha, mi naita huu ni usaliti wa ndoa.
RAFIKI: Nini tena?

JAMAA:Nimegundua mke wangu kumbe anafanya biashara ya kitimoto na hajawahi hata kuniambia
RAFIKI: Kitimoto? We umejuaje?
JAMAA: Leo asubuhi nilichelewa kuamka niliamua nijipumzishe kidogo kabla ya kwenda kazini, simu ya mke wangu ikalia, nikaamua kuipokea, kabla hata sijafungua mdomo, nikasikia sauti ya mwanaume mmoja akauliza, “Huyo nguruwe umeshamuondoa?’ Hebu we fikiria nilivyoshtuka, yaani mpaka sasa nashindwa kuamini kuwa mke wangu ananizunguka anafanya biashara ya nguruwe hajaniambia hata siku moja

Jinsi ya kupika Wali Wa Kichina wa mboga mboga Na Mayai

Viambaupishi

  1. Mchele (Basmati) – 3 vikombe
  2. Mbogamboga za barafu (karot, njegere, spring beans na mahindi) – 1 kikombe
  3. Kuku Kidari – 1 LB (ratili)
  4. Mayai – 2 mayai
  5. Vitunguu (vikubwa) – 2 au 3 vidogo
  6. Pili pili manga – 1 kijiko cha chai
  7. Paprika – 1 kijiko cha chai
  8. Chumvi – Kiasi
  9. Mafuta – 1/3 kikombe cha chai
  10. Kitunguu saumu(thomu/galic) – 1 kijiko cha supu
  11. Tangawizi – 1 kijiko cha chai
  12. Kidonge cha supu – 1
  13. Soy sauce – 2 vijiko vya supu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku

Kata kidari cha kuku vipande vidogo vidogo vya kiasi.

Tia mafuta kidogo katika wok (karai ya kichina)

Kisha mtie kuku, thomu, tangawizi, soy sauce, pilipilimanga, paprika chumvi.

Tia mboga za barafu, kidonge cha supu, kaanga kuku na mboga viwive yitu vyote na mchanganyiko ukauke.

Namna Ya Kutayarisha Na kupika Wali

Roweka mchele wa basmati kwa muda wa saa au zaidi.

Halafu chemsha mchele pamoja na chumvi

Wacha uchemke asilimia 70%

Chuja maji na weka kando

Katika sufuria, tia mafuta kidogo tu

Kisha tia mayai mawili ukaange haraka haraka (crumbled egg)

Changanya mchanganyiko wa kuku na mboga

Kisha tia wali changanye vizuri

Rudisha katika moto, funika upikike kidogo hadi uive

Kisha pakua katika sahani na tolea na mayai ya kuchemsha ukipenda.

Umakini katika kuwaza

Kuwa makini sana na mawazo yako, Yanaweza kukupeleka Mbinguni au motoni.


Kumbuka vile unavyowaza ndivyo utakavyovitenda.


Amua kuwaza mema kutoka ndani ya moyo wako kisha utatenda mema katika maisha yako


Kumbuka Mungu humhukumu mtu kwa mawazo yake maana mawazo ya mtu ndiyo mtu mwenyewe


Tuwaze mema wapenzi ili tuwe wema

Kuwa Makini na Mawazo Yako

Kuwa makini sana na mawazo yako, yanaweza kukupeleka Mbinguni au motoni. Mawazo ni nguvu inayoweza kuelekeza maisha yako kwa njia ya heri au shari, na ni muhimu kuyadhibiti na kuyatumia kwa njia inayofaa.

“Ndivyo aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.” (Mithali 23:7)
“Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema; na mtu mwovu katika hazina mbaya hutoa yaliyo mabaya; kwa kuwa wingi wa moyo huongea kinywa chake.” (Luka 6:45)
“Tena mkiwaza hayo, yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema, ikiwepo wema wowote, ikiwa na sifa njema yoyote, mawazeni hayo.” (Wafilipi 4:8)

Mawazo Yanaelekeza Matendo

Kumbuka vile unavyowaza ndivyo utakavyovitenda. Mawazo yako yanaathiri moja kwa moja matendo yako. Unapowaza mema, utatenda mema; unapowaza mabaya, utatenda mabaya. Hivyo, ni muhimu kuzingatia na kuimarisha mawazo yako kuwa chanya na yenye kujenga.

“Kwa maana nimemwita Bwana siku zote; heshima na utukufu una mpata.” (Zaburi 19:14) “Mkishika maagizo yangu, mtapata uzima; tena msifanye mfano wa matendo ya nchi ya Misri mliyokaa, wala msifanye mfano wa matendo ya nchi ya Kanaani niliyowaleta; wala msizifuate sheria zao.”_ (Mambo ya Walawi 18:3-4)
“Jishughulisheni na mawazo yaliyo juu, wala siyo ya chini.” (Wakolosai 3:2)

Amua Kuwaza Mema

Amua kuwaza mema kutoka ndani ya moyo wako kisha utatenda mema katika maisha yako. Uamuzi wa kuwaza mema unatokana na kujitolea kuwa na moyo safi na mwenye nia njema. Jenga tabia ya kusoma na kutafakari Neno la Mungu ili moyo wako uweze kujazwa na mawazo mema yanayokuza tabia njema.

“Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.” (Zaburi 119:105)
“Nitalificha neno lako moyoni mwangu, nisije nikakutenda dhambi.” (Zaburi 119:11)
“Mwenye hekima ana moyo wa busara, neno la Mungu ni ngao kwake.” (Mithali 14:33)

Hukumu ya Mungu kwa Mawazo

Kumbuka Mungu humhukumu mtu kwa mawazo yake maana mawazo ya mtu ndiyo mtu mwenyewe. Mungu anaangalia moyo wa mtu na mawazo yanayotoka ndani yake. Ni muhimu kujitahidi kuwa na mawazo yanayoendana na mapenzi ya Mungu ili tuweze kumpendeza.

“Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina makali kuliko upanga wowote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake, tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” (Waebrania 4:12)
“Kila njia ya mtu ni safi machoni pake mwenyewe, lakini Bwana huzipima roho.” (Mithali 16:2)
“Kwa maana mimi, Bwana, nachunguza mioyo, nakijaribu viuno, nimpe kila mtu kwa kadiri ya njia zake, kwa kadiri ya matunda ya matendo yake.” (Yeremia 17:10)

Mawazo Mema Yanaweza Kutupeleka Kwa Wema

Tuwaze mema wapenzi ili tuwe wema. Mawazo mema hujenga tabia nzuri na matendo mema. Ni jukumu letu kujitahidi kuwaza na kutenda mema kila wakati, kwani kwa kufanya hivyo, tunakuwa vyombo vya amani na upendo wa Mungu duniani.

“Wenye amani hawatafutwa kwa bure, bali watapata furaha ya Bwana.” (Isaya 32:17)
“Kwa hiyo, wote mnaoamini, muwe na nia moja, wenye huruma, wenye kupendana kama ndugu, wenye huruma nyingi, wanyenyekevu.” (1 Petro 3:8)
“Na Bwana mwenyewe awafanye ninyi mzidi sana na kuongezeka katika upendo ninyi kwa ninyi na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu.” (1 Wathesalonike 3:12)

Kwa hivyo, tuwe makini na mawazo yetu, tuwe na nia ya kuwaza mema, na tuishi kwa kutenda matendo mema yanayotokana na mawazo hayo. Mungu anapenda watu wenye moyo safi na wenye nia njema, na atawabariki kwa wingi wa rehema na neema zake.

Kweli tamaa ni mbaya, mke wa mtu kaponzwa na tamaa, ndio basi tena

Jamaa kaenda kwa mke wa rafiki yake:
JAMAA: Shem nakupenda!
MKE: Hebu toka hapa! Je rafiki
yako akijua? tena koma!
JAMAA: Ntakupa milioni 1!
MKE: Basi njoo kesho mchana
mume wangu akiwa kazini!

Kesho yake Jamaa kaja
na milioni 1 wakamalizana na mke wa rafki yake,
jioni ilipofika
Mume akarudi home na
kumuuliza Mkewe, “Rafki yangu SAM kaleta hela yangu milioni 1?”
MKE akajibu kwa unyonge, “Ndio!”
MUME: Yes! Ndio maana nampenda SAM kanikopa asubuhi jioni karejesha!!!!
Mke hoi……

MAPISHI YA LADU

VIAMBAUPISHI

Unga – 6 vikombe

Samli – ½kikombe

Baking Powder – ½kijiko cha chai

Maziwa- 1 kikombe

Maji -Kisia kiasi kama unga bado mzito

VIAMBAUPISHI VYA SHIRA

Sukari – 5 vikombe

Maji – 2 1/2 vikombe

Vanilla – 2 vijiko vya chai

Rangi ya orange – 1 kijiko cha chai

Iliki ya unga – 1 Kijiko cha chai

MAANDALIZI

Changanya unga wa dengu, samli, baking powder pamoja na maziwa katika mashine ya keki (cake mixer).
Ukisha changanya angalia kama mchanganyiko wako umekua mwepesi kidogo kuliko wa keki, kama bado mzito basi ongeza maji kiasi.
Kisha weka mafuta kiasi kwenye karai,weka na samli kikombe kimoja, weka kwenye moto wa kiasi.
Mafuta yakisha pata moto, chukua kijiko kikubwa cha matundu chota mchanganyiko wako na kijiko cha kawaida tia kwenye kijiko cha matundu. Hakikisha kijiko cha matundu kiwe juu ya karai ili mchanganyiko wako uchuruzike ndani ya mafuta yalio pata moto.
Pika ndani ya mafuta mpaka iwive, ila usiache ikawa brown.
Toa mchanganyiko ulowiva tia ndani ya shira uliyo pika. Hakikisha shira iwe imepoa kabla ya kutia mchanganyiko huo.
Endelea kupika mchanganyiko wako mpaka uishe, kila ukitoa katika mafuta hakikisha unatia ndani ya shira.
Ukishamaliza wote kanda huo mchanganyiko ulokua ndani ya shira mpaka uone shira yote imekauka (yaani iwe imeingia ndani ya mchanganyiko).
Tupia zabibu kavu na lozi zilizo katwa, changanya na mkono.
Wacha mchanganyiko katika bakuli, funika na foil mpaka siku ya pili.
Siku ya pili chukua mchanganyiko kiasi katika mkono tengeneza mviringo (round).

MAANDALIZI YA SHIRA

Katika sufuria, tia sukari, maji, iliki, vanilla na rangi.
weka kwenye moto wacha ichemke mpaka itowe povu (bubbles) juu.
Kisha toa povu, wacha shira kwenye moto kama dakika 3.
Hakikisha shira yako iwe inanata kiasi kwenye vidole, lakini iwe nyepesi kidogo kuliko shira ya kaimati.

Usichokijua kuhusu sungura, panya na jamii yao

JE WAJUA?

Sungura, panya na Jamii zao huwa na mwendo wa kukimbia na kuruka muda wote na umri wao wa kuishi ni miaka 15. Kobe ni mnyama mwenda pole, asiye na papara wala pilika, muda mwingi hujificha na kupumzika ndani ya jumba lake akikwepa maadui. Umri wa kuishi kobe hufikia hadi miaka 300.
FUNZO: Mazoezi ni kiinimacho na uongo mtupu. Jipumzikie mwaya!!!
🏃🏾🏃🏿‍

Wachaga wana mambo mbele ya hela, angalia hii bili ilivyomchanganya MASSAWE

MASSAWE alienda na marafiki zake bar kunywa, baada ya kumaliza kutumia akaletewa bili kama ifuatavyo:
Manka 35,000
Marieta 20,000
Kekuu 30,000

Kitime 15,000
Kinabo 10,000
TOTAL 110,000/=
MASSAWE akaicheki akasema “Wote nitawalipia lakini huyo “TOTAL” Yesuu simlipii.
Kwansa anamiliki sheli kibao sa mafuta hapa bongo. Shensi taip ! Na amekunywa nyingi kuliko wote alipe mwenyewe…

Usiyoyajua kuhusu pesa haya hapa

Habari za Leo Rafiki yangu wa Muhimu sana. Ni furaha yangu kujua unaendelea vyema sana na majukumu yako.

Ni wakati mwingine tena tunaenda kujifunza pamoja juu ya mambo mbalimbali ili tuweze kufikia mafanikio kila siku. Leo tunakwenda kujifunza kuhusu pesa na utajua mambo mengi sana juu ya pesa.

Ni siri gani ipo ndani ya fedha na wengi hawaijui?

Kwanini watu wengi wanakua matajiri halafu wanapoteza utajiri wao wote na kuwa maskini tena?

Ulishawahi kuona watu maarufu wamekua na pesa nyingi lakini baada ya muda wanapotea na pesa zao zinapotea na kurudi kuwa watu wa kawaida kabisa?

Hujawahi kuona watu wakiuza mashamba ya urithi kwa mamilioni ya pesa na wakabadilisha aina ya maisha wanayoishi lakini baada ya muda pesa zinapotea na wanarudia hali yao ya zamani?

Hujakutana na vijana waliochimba madini wakajikuta wamepata mawe wakawa milionea lakini ghafla baada ya muda Fulani wanarudi kule kule walipokua?

Wengi wakiona hayo utawasikia wanasema pesa za mashamba hazika! Pesa za madini zina mashetani! Ni siri gani ipo kwenye hii pesa?

Inawezekana umeshajiuliza sana maswali haya na hata kuogopa kuwa nayo. Ukaamua kuwa mtu wa kawaida tu kwasababu ya hofu hizi zinazokujia unapofikiri kuwa tajiri kisha uje upoteze pesa zako zote!

Watu wengi wamekuwa na fikra kwamba pesa ni mbaya, zinaharibu watu, zinawafanya watu kuwa wachoyo, zinawafanya watu kuwa na tamaa pamoja na mengine mengi unayoyafahamu.

Ukweli ni kwamba pesa haina tatizo lolote pesa haina shetani wala pepo lolote linaloifanya imharibu mtu anapokuwa nayo nyingi. Pesa sio kiumbe hai. Pesa tunaitumia kununua bidhaa mbalimbali au kulipia huduma tunazozihitaji katika maisha yetu ya kila siku.

Ukweli kuhusu pesa ni huu hapa. Kwanza pesa haimbadilishi mtu bali inamfanya awe Zaidi ya vile alivyokuwa mwanzo yaani kama mtu alikuwa ni mchoyo akipata pesa atakuwa mchoyo maradufu, kama alikua mlevi akipata pesa anazidisha kuwa mlevi Zaidi.

Na wengine wakiwa hawana pesa kuna tabia nyingi wanakuwa nazo ndani zimejificha hawazionyeshi wakishapata pesa zile tabia zinafunguka na kuwa wazi.

Kama mtu alikuwa Malaya akipata pesa ndio utaona anaanza kubadilisha wanawake. Pesa zinabaki kuwa pesa na tabia za mtu zinabakia kuwa tabia za mtu.

Kama mtu alikua mtoaji akipata pesa atakuwa mtoaji Zaidi.
Kama alikua mcha Mungu akipata pesa atakwenda kuabudu Zaidi.
Hivyo pesa sio tatizo watu ndio wenye matatizo ndani yetu.

“Having more money won’t change you as a person. It will, however, magnify
the person you already are.” – Bob Proctor

Huwa napenda kuutumia mfano wa chombo. Watu wengi wanaopata pesa nyingi ghafla na kuzipoteza zote ni kama maji yaliyojaa kwenye ndoo utake kuyaweka yote kwenye kikombe cha chai.

Ukweli ni kwamba kikombe kitajaa lakini yale yaliyobaki yatamwagika yote chini hivyo hivyo na pesa zinazopatikana ghafla ni sawa na kuziweka kwenye kikombe ambacho ni uwezo wa akili yako.

Kama Akili yako bado haijaweza kupangilia milioni ishirini hivyo hata ukipewa leo zote zitapotea na zitabaki kile kiwango ambacho akili yako inaweza kutawala na kuendesha. Hivyo njia sahihi ya wewe kuweza kumiliki mamilioni ya shilingi na kubakia nayo ni kuanza kubadili ufahamu wako. Kuza ufahamu wako kidogo kidogo ili uweze kuendesha utajiri mkubwa. Na hili halitokei ndani ya siku moja ni kadiri unavyojifunza kila siku. Kwa kusoma vitabu na kufanyia kazi yale unayojifunza.

Jambo moja na muhimu la kufanya ni kutokuweka akili yako yote kwenye pesa. Usiweke malengo yako kwenye pesa unapofanya biashara unafanya ili upate pesa lakini siku zote pesa hazikai huwa zinaisha hivyo badala ya wewe kuweka nguvu zako na mawazo yako kwenye pesa weka Zaidi katika kuwasaidia watu kama unauza nguo kazana Zaidi katika kuwafanya watu wafurahie huduma yako pesa zitakuja.

Kama unatoa huduma hakikisha unatoa huduma bora ili kuvutia wateja Zaidi kila siku. Pesa utaziona kwako na zitaongezeka kila wakati.

Wekeza pia muda wako kwenye kutengeneza mifumo mbalimbali ambayo itakuwa inakuingizia pesa bila kuwa na kikomo. Unapotegemea mfereji mmoja wa kipato lazima utabakia pale pale siku zote.

Jambo la muhimu la kufanya ili uweze kubakia juu kwenye mafanikio siku zote ni kujifunza na kujijengea misingi ambayo itakuwezesha wewe usiyumbe na ubakie na utajiri wako.

Kuwa mwaminifu, kua mtoaji, wapende wengine, kuwa muadilifu, usidhulumu mtu, kabla hujafanya lolote angalia lina manufaa gani kwako na kwa wengine.

Nikutakie wakati mwema Asante sana kwa kusoma Makala hii.

Angalia kilichomkuta huyu dada mwenye zarau, mwanae alikufa kwa zarau zake

Dada mmoja akiwa ofisini alipigiwa simu kuwa mwanae amepata ajali wakati anatoka shule, alikuwa ameumia sana. Kwa harakaharaka yule dada aliwasha gari na kuanza safari kuelekea hospitali ili kumuona mwanae.

Akiwa njiani katika mistari ya Zebra huku akiwa na mawazo alitaka kumgonga Kaka mmoja ambaye alikuwa akivuka barabara kwa kukimbia. Katika kumkwepa gari iligonga ukingo wa barabara na kukwaruizika kidogo.

Kwa hasira yule dada alishuka na kuanza kumtukana yule kijana kuwa kamsababishia ajali na kumchelewesha. Alimtukana sana, hali iliyowafanya watu kujaa. Watu walipofika walianza kuuliza nini ndipo yule dada kwa uoga alidanganya kuwa yule kaka alitaka kumuibia.

Watu walianza kumpiga Kaka wa watu kama mwizi, kuona vile yule dada aliingia kwenye gari na kuelekea hospitalini kumuona mwanae. Huku nyuma Polisi walikuja na kumuokoa yule kijana lakini akiwa ameumizwa sana.

Alifika hospitalini na kumkuta binti yake akiwa katika hali mbaya, alikuwa akitakiwa kufanyiwa upasuaji wa haraka ili kuokoa maisha yake, manesi walishamuandaa mtoto na alikuwa akisubiriwa Daktari ambaye alipigiwa simu na alikuwa njiani.

Wakati wakimsubiri Daktari, Nesi alikuja na kuwamabia kuwa, wampeleke hospitali nyingine kwani Daktari waliyekuwa wakimsubiri asingeweza kumfanyia upasuaji mtoto wao kwani alikuwa amepigwa na wananchi wakati akija hospitalini wakimuita mwizi.

Dada na mumewe walichanganyikiwa, mtoto kutokana na hali yake mbaya alichukuliwa harakaharaka na gari la wagonjwa ili kuhamishwiwa hospitalini nyingine. Wakati wanatoka kuelekea kwenye gari kulikuwa na gari ya Polisi inaingia.

Kijana mmoja akiwa hoi alishushwa, yule Dada alimtambua ni yule kijana ambaye alimuitia mwizi kule barabarani. Kwa hasira yule Dada allimuambia Mume wake.
“Huyu Kaka namfahamu ni kibaka tu alitaka kuniibia, ndiyo amenichelewesha kufika huku hospitalini!”
Nesi ambaye alikuwa akimsaidia kumpandisha mtoto katika gari la wagonjwa alimkatisha na kusema.
“Hapana Dada huyu kaka si kibaka, ni Daktari ambaye alipaswa kumfanyia upasuaji mwanao. Amepigwa wakati akikimbia kuja hospitalini, mimi ndiyo nimempigia simu kuja…”

Dada wawatu nguvu zilimuishia ilibidi anyamaze, walifika hospitali nyingine, mtoto alikuwa katika hali mbaya. Aliandaliwa na kuingizwa katika chumba cha upasuaji lakini kabla hajafanyiwa chochote yule mtoto alifariki.

Baada ya uchunguzi ilionekana damu ilishaingia kwenye ubongo. Wangeweza kuokoa maisha yake kama angefanyiwa upasuaji katika hospitali ya mwanzo, kule kusafirishwa tena na kurushwa rushwa barabarani kulisababisha damu kuendelea kuvuja kwa kasi ndani.

Yule dada alizimia baada ya kupata habari zile, maneno yake yalisababisha kuondoa maisha ya mwanae.

FUNZO

Usimdharau mtu kutokana na hali yake kwani hujui ni kitu gani anaweza kukusaidia.

Mungu ni mwenye upendo, Huruma na Rehema hasa kwa Wenye dhambi

Mungu ni mwenye upendo Huruma na Rehema hasa kwa Wenye dhambi.
Mungu yupo tayari kumsikiliza mtu yeyote mwenye dhambi kama ameutambua, amekiri na Kutubu makosa yake.

Mungu akishamsamehe mtu uovu wake anambariki.

Hakuna mtu ambaye hatasamehewa na Mungu kama Ametubu, amekiri na Kuomba msamaha wa makosa yake.

Mungu wakati wote yupo akisubiri wenye dhambi waende kwake kwa Toba ili awasemehe.

Lakini tatizo ni la watu wengi wanazani kua wakati wakiwa dhambini Mungu anakua amewakasirikia, Ukweli ni kwamba unapokua dhambini Mungu anakuonea Huruma na anatamani umrudie yeye.

Unaweza ukawa umetenda dhambi lakini hujamuasi Mungu, Kumuasi Mungu ni pale Unapoona kuwa Mungu hana nafasi katika maisha yako tena. Lakini ukiwa dhambini huku unamtumaini Yeye basi bado upo katika njia yake kwa kuwa yeye ni sawa na Baba kwako na kumkosea Baba yako sio kumuasi kama tuu utarudi Kuomba msamaha na Kuheshimu nafasi yake katika maisha yako.

Upendo wa Mungu Kwa Wenye Dhambi

Mungu ni mwenye upendo, huruma, na rehema hasa kwa wenye dhambi. Biblia inatufundisha kwamba Mungu hachoki kuwakaribisha wenye dhambi wanaotubu kwa dhati. Mungu yupo tayari kumsikiliza mtu yeyote mwenye dhambi ambaye ameutambua, amekiri, na kutubu makosa yake. Huruma na rehema zake haziishi kamwe, na anasubiri kwa shauku kubwa kuona wanae wakirudi kwake kwa toba.

“Basi, Bwana, Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli.” (Kutoka 34:6)
“Acha waovu na watu wanaodharau sheria wamrudie Bwana, naye atawahurumia. Warudi kwa Mungu wetu, maana atawasamehe kabisa.” (Isaya 55:7)
“Wote wanaokuja kwangu sitawatupa nje kamwe.” (Yohana 6:37)

Msamaha na Baraka za Mungu

Mungu akishamsamehe mtu uovu wake, anambariki. Hakuna mtu ambaye hatasamehewa na Mungu kama ametubu, amekiri, na kuomba msamaha wa makosa yake. Hii inaonyesha upendo wa ajabu wa Mungu kwa wanadamu wake, upendo ambao haujali ukubwa wa dhambi, bali ukubwa wa toba ya mtu.

“Tubu basi, geuka ili dhambi zako zifutwe.” (Matendo 3:19)
“Na dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kamwe.” (Waebrania 10:17)
“Maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitakumbuka tena.” (Yeremia 31:34)

Mungu Anasubiri Wenye Dhambi Warudi Kwake

Mungu wakati wote yupo akisubiri wenye dhambi waende kwake kwa toba ili awasamehe. Huu ni ujumbe wa matumaini kwa kila mtu anayehisi ameanguka mbali na neema ya Mungu. Mungu ni kama baba anayesubiri mwanae mpendwa arudi nyumbani. Ana shauku ya kumsamehe na kumrejesha kwenye familia ya kiroho.

“Bwana si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili, husamehe uovu na makosa, lakini hatahesabu kuwa hana hatia mwenye hatia.” (Hesabu 14:18)
“Mkiungama dhambi zenu, yeye ni mwaminifu na mwenye haki, atasamehe dhambi zenu na kuwasafisha na udhalimu wote.” (1 Yohana 1:9)
“Furahini pamoja nami, kwa sababu mwana wangu alikuwa amekufa, naye amerudi tena kuwa hai; alikuwa amepotea, naye ameonekana.” (Luka 15:24)

Wakati wa Dhambi: Huruma ya Mungu

Tatizo ni kwamba watu wengi wanadhani kuwa wakati wakiwa dhambini Mungu anakua amewakasirikia. Ukweli ni kwamba unapokuwa dhambini, Mungu anakuonea huruma na anatamani umrudie yeye. Unaweza ukawa umetenda dhambi lakini hujamuasi Mungu, Kumuasi Mungu ni pale unapomkataa kabisa na kuona kuwa hana nafasi katika maisha yako tena.

“Nanyi mtarudi, na kuona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.” (Malaki 3:18)
“Hata kama dhambi zenu ni nyekundu sana zitakuwa nyeupe kama theluji.” (Isaya 1:18)
“Bwana ni mwingi wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, ana wingi wa fadhili. Hata mshika hasira yake daima, wala hatawakemea milele.” (Zaburi 103:8-9)

Kurejea kwa Mungu kwa Toba

Ukiwa dhambini huku unamtumaini Mungu, basi bado upo katika njia yake kwa kuwa yeye ni sawa na baba kwako. Kumkosea Baba yako sio kumuasi kama tu utarudi kuomba msamaha na kuheshimu nafasi yake katika maisha yako. Toba ya kweli inarejesha uhusiano wetu na Mungu, na anatupokea kwa mikono miwili.

“Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao.” (Zaburi 103:13)
“Nikaribieni mimi, nami nitawakaribia ninyi, asema Bwana.” (Yakobo 4:8)
“Heri wenye huruma, maana hao watapata rehema.” (Mathayo 5:7)

Kwa hivyo, tunapokuwa dhambini, tunapaswa kukumbuka kwamba Mungu anatuona kwa macho ya huruma na upendo. Yupo tayari kutusamehe na kutubariki, mradi tu tutambue dhambi zetu, tukiri, na kutubu kwa dhati. Tunapomrudia Mungu kwa toba, tunapokea huruma na neema zake zisizo na kipimo.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About