Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Siri ya mafanikio katika maisha Ni Kutoangalia Watu

Baada ya kusoma makala kuhusu hofu zinazotugharimu katika safari ya mafanikio, Leo nimekuandalia Makala hii ya Siri ya mafanikio.

Katika safari ya mafanikio, watu wanaweza kuwa kikwazo kikubwa kinachosababisha ugumu wa kuendelea mbele. Wanaweza kuleta upinzani, kukosa imani, au hata kuzua vikwazo visivyo na msingi. Hata hivyo, ni muhimu kuelewa kuwa changamoto hizi zilizoletwa na watu ni sehemu ya mchakato wa kufikia mafanikio. Ingawa inaweza kuwa ngumu kukabiliana na watu wenye upinzani au wasioamini katika safari yetu ya kufikia malengo yetu, tunapaswa kuzingatia kuwa hakuna mafanikio ya kweli ambayo hayakuja na changamoto. Naam, inaweza kuwa rahisi kufanya kazi peke yetu na kuepuka kukabiliana na watu wasioamini au wenye upinzani, lakini hiyo haitatupeleka mbali sana.

Tunahitaji kushughulikia changamoto hizi na kuona jinsi tunaweza kuzishinda. Kukutana na watu ambao hawana imani na malengo yetu inaweza kuwa kama mtihani mkubwa kwetu. Wanaweza kutushawishi kuacha au kuanza kutilia shaka uwezo wetu. Lakini ni muhimu kukumbuka kuwa imani yetu ndio itakayotuendesha mbele. Tunapaswa kujikumbusha kuwa mafanikio hayangeweza kupatikana ikiwa tungekuwa na imani ndogo ndani yetu wenyewe. Mbali na hilo, tunapaswa pia kutambua kuwa vikwazo visivyo na msingi vinaweza kuwepo katika safari yetu ya mafanikio. Watu wanaweza kuzua vikwazo hivi kwa sababu ya wivu, woga, au tu kutokuelewa malengo yetu. Ni muhimu kutambua kuwa hatuwezi kudhibiti tabia au mitazamo ya watu wengine, lakini tunaweza kujifunza kuweka mipaka na kuendelea kufuata malengo yetu licha ya vikwazo hivyo. Katika safari yetu ya mafanikio, tunapaswa kuwa na uvumilivu na subira.

Tunapaswa kutambua kuwa kila changamoto tunayokutana nayo inatupa fursa ya kukua na kujifunza. Tunapaswa kutumia changamoto hizi kama nguvu ya kuendelea mbele badala ya kutuacha tukata tamaa. Kwa kumalizia, ingawa watu wanaweza kuwa kikwazo katika safari yetu ya mafanikio, tunapaswa kuona changamoto hizi kama sehemu ya mchakato wa kufikia malengo yetu. Tunapaswa kuwa na imani thabiti ndani yetu wenyewe, kuweka mipaka na kuendelea kusonga mbele licha ya vikwazo vinavyoweza kuzuka. Kwa kufanya hivyo, tutapata mafanikio kamili na kuwa bora zaidi katika safari yetu ya kuelekea mafanikio.

Wakati mwingine, tunaweza kukutana na watu ambao hawana imani na uwezo wetu au wanajaribu kutuweka chini kwa sababu ya wivu au tamaa. Ni muhimu kujifunza kuweka mipaka na kuendelea kusonga mbele, kujiamini katika uwezo wetu na kuendelea kufanya kazi kwa bidii kuelekea malengo yetu.

Watu wanaweza pia kuwa vikwazo kwa kuwa na maoni tofauti au kutokuwa na uelewa kamili wa malengo yetu. Katika hali hizi, ni muhimu kuwa na uvumilivu na kuwasiliana kwa wazi ili kuelezea malengo yetu na kutafuta njia za kuwashawishi au kuwashirikisha katika safari yetu ya mafanikio.

Hakikisha pia kuwa unazungukwa na watu wenye mawazo chanya ambao wanakuunga mkono na kukusaidia kufikia malengo yako. Kuwa na timu ambayo inakusaidia na kukutia moyo ni muhimu sana katika safari ya mafanikio.

Kwa hiyo, tunapokabiliana na vikwazo kutoka kwa watu katika safari yetu ya mafanikio, ni muhimu kujifunza kutokana na hilo, kuweka mipaka, kuwasiliana kwa wazi, na kuwa na timu yenye msaada karibu nasi. Hatimaye, tunapaswa kuendelea kuamini katika uwezo wetu wenyewe na kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yetu.

Waziri mkuu wa zamani wa uingereza Sir Wiston Churchill aliwahi kusema;

“huwezi kufika mwisho wa safari yako kama utakuwa unasimama kila mahali kumtupia jiwe kila mbwa anaye kubwekea”

Sir Wiston Churchill

Kauli hii ina maana kwamba kama una picha kichwani ya kule unakokwenda au umekusudia kufikia na kutimiza lengo fulani katika maisha hupaswi kusikiliza, kupambana au kushindana nakila mtu.

Unapokuwa njiani kutimiza lengo lako lazima utakutana na watu wa aina hizi;

  1. Watakaokurudisha nyuma kwa kukuharibia mipango na juhudi zako
  2. Watakaokuvunja moyo na kukukatisha tamaa
  3. Watakaokusema vibaya hata kwa mazuri yako na kukuzushia uongo
  4. Watakaokuchukia kwa sababu ya bidii yako

Unaweza kushawishika kutaka kumjibu kila mtu anayekusema vibaya, kukuchukia au kukukatisha tamaa (hapo ndo unakuwa sawa na yule anayesimama kumtupia jiwe kila mbwa anayebweka).

Unaweza ashawishika kutaka kuona kila mtu anakukubali na kukuunga mkono, kitu ambacho hakiwezekani.
Kuna Msemo usemao “siri kubwa ya kufeli katika maisha ni kujaribu kumpendeza kila mtu”.

Hapa duniani huwezi kumpendeza kila mtu hata ufanye jambo zuri kiasi gani “hata ukichezea maji utaambiwa unatimua vumbi”. Mara nyingi tunajitahidi kufanya mambo mema na kuwa na nia njema, lakini bado kuna watu ambao hawatafurahia jitihada zetu na watatupinga tu. Hii inaweza kuwa changamoto kubwa kwetu kihisia na kijamii, kwani tunatamani kukubalika na kupendwa na kila mtu.

Lakini kumbuka, haifai kuchukulia kila upinzani kibinafsi au kuathiri thamani yako. Watu wana mitazamo tofauti na uzoefu wao binafsi, na huenda hawana ufahamu kamili wa hali yako au malengo yako. Badala yake, ni muhimu kuwa na imani katika nia zako na kuendelea kufanya mambo mema bila kujali jinsi watu wengine watakavyokuona au kukupinga.

Njia bora ya kushughulikia upinzani ni kujielewa na kuweka mipaka. Jifunze kuamini kwamba wewe ni wa thamani na una uwezo mkubwa wa kuathiri mazingira yako. Wacha maadili yako yaongoze vitendo vyako na usiruhusu maneno au maoni ya wengine kukufanya ujisikie vibaya au kupoteza lengo lako.

Kumbuka pia kuwa hakuna mtu aliyeweza kufanya kila mtu awe radhi. Hata watu mashuhuri na viongozi wa kiroho hawakuepuka upinzani. Kina Mandela, Mahatma Gandhi, au Martin Luther King Jr., walikabiliana na upinzani mkubwa, lakini waliendelea kusimama imara kwa imani zao na kufanikisha mabadiliko makubwa.

Ili kufanya mabadiliko katika jamii au ulimwengu, ni muhimu kuwa tayari kukabiliana na upinzani. Upinzani unaweza kukusaidia kukua kibinafsi na kitaaluma, kurekebisha njia zako, na kukuza uvumilivu wako. Ni nafasi ya kujifunza na kujenga hoja zako kwa msingi thabiti.

Hivyo, jinsi unavyokabili upinzani ina athari kubwa kwa maendeleo yako na mtazamo wako kwa maisha. Usikate tamaa na usiruhusu upinzani ukuzuie kufuata ndoto zako na kufanya mambo makubwa. Jiamini, thamini uwezo wako, na endelea kusonga mbele bila kujali kile ambacho wengine wanaweza kusema au kufikiria. Hakuna kitu kikubwa kilichofanyika bila ya upinzani, kwa hiyo endelea na safari yako na uhakikishe kuwa unaamini kwamba una nguvu ya kufanya tofauti.

Wewe fwatilia Mipango yako huku ukitazame hatima yako. Soma hapa mbinu hizi za kukunufaisha maishani.

Lakini haimaanishi uwachukie watu na kuwatendea mabaya ili ufanikiwe mwenyewe. Chuki na Mapambano hayanufaishi bali yanakufanya kuwa dhaifu.

Vivyo hivyo, Sio watu wote ni kikwazo. Kuna watu wa aina nyingine ambao wanaweza kukusaidia kufanikiwa. Unapaswa kuwa makini na kutumia Busara yako kuweza kuwatambua watu unaokuwa nao katika safari ya Mafanikio.

Kwa nini watu wanapenda pesa

Watu wengi tunapenda sana Pesa lakini hatuko tayari kuzifanyia Pesa kazi nikiwa na maana kutumia njia sahihi kuzipata na tunapozipata hatuna Akili ya kuweza kuwa nazo muda mrefu zisiondoke.
Kama tujuavyo katika maisha yetu haya Pesa ndio kila kitu,tunahitaji Pesa ili tuweze kufanya mambo mengi mazuri na makubwa.Kitu kinachotukwamisha hatujui tufanye nini ili tuweze kuzipata hizi Pesa na tunapozipata tunakosea tena cha kuzifanyia ili zisipotee tena au zisiishe.

Kitu kikubwa kinachotugharimu ni kwamba hatuna elimu ya Pesa.Wengi wetu tumesoma tena sana lakini huko shuleni na vyuoni hatufundishwi jinsi gani ya kuzitafuta Pesa,uzifanyie nini,na nini kifanyike ili zisiishe.
Elimu hii kuhusu Pesa haitolewi shuleni zaidi ni ya kujifunza kutoka mtaani hasa kwa watu wanaomiliki Pesa nyingi au ambao wamefanikiwa ndio watakupa utaalam halisi na elimu kuhusu Pesa.

Kuna watu wengi sana tumeshawahi kuwasikia wamepata Pesa nyingi sana lakini sasaivi hawana kitu.Wengi tumewasikia kwenye bahati nasibu wamejishindia Pesa nyingi,wengine kwenye mashindano mbalimbali wamejishindia Pesa kibao lakini cha kujiuliza hao watu mpaka sasa wapo wapi?hela zao ziko wapi?wamezifanyia kitu gani?bado wanazo??Jibu rahisi ni hapana na hii ni kutokana na kwamba hawakupata elimu ya Pesa ndio maana.

Inatakiwa kabla ya kuwapa watu Pesa lazima wapate elimu kuhusiana na Pesa hapo ndipo watakapokuwa na ujuzi Wa kuweza kuzifanyia kazi na kuziongeza.
Matajiri wote unaowafahamu wana elimu juu ya Pesa ndio maana Pesa zinazidi kuwafuata wao na sisi ambao hatuna elimu ya Pesa tunazidi kuhangaika kuzitafuta.

Lakini sifa nyingine ya Pesa kadiri unavyotoa ndivyo unavyozidi kuzipata yaani ni kama vile unabarikiwa….kama unajua au unavyoona matajiri wengi sana ni watoaji Wa hela kusaidia sehemu mbalimbali hasa kwa wasiojiweza au miradi ya kimaendeleo ndio maana unaona wanazidi kufanikiwa.

Watu wengi tunazifanyia Pesa kazi badala ya Pesa kutufanyia sisi kazi. Hii ni kutokana na kwamba hatujaelewa au hatujui jinsi gani ya kutengeneza mfumo utakaokuwa unakuingizia tu Pesa hata kama haupo.Umeshawahi kujiuliza hicho unachokifanya kama ukipumzika kwa muda Wa kama miezi sita utaendelea kupata kiasi kilekile cha Pesa ulichokuwa unakipata kabla ya kupumzika?Kama huwezi hivyo basi wewe unazifanyia Pesa kazi.

Kwa muajiriwa ukipumzika miezi sita utaendelea kulipwa mshahara wako?
Kwa mfanyabiashara labda Wa duka ukipumzika wiki moja bila kufungua duka lako utapata kipato kile kile unachokitengeneza kila siku?Kama hauwezi basi ujue unazifanyia Pesa kazi.

Tukiangalia kwa upande mwingine wafanyabiashara wakubwa wanaweza kupumzika hata mwaka mzima na wakaendelea kupata hela zilezile kwani wameshatengeneza mfumo ambao sisi wengi hatunao na ndio watu ambao Pesa zinawafanyia kazi.Ana uwezo Wa kwenda kupumzika Marekani mwaka mzima na Pesa zikaendelea kuingia huu ndio Uhuru Wa Pesa.

Jiulize wewe unazifanyia Pesa kazi au Pesa zinakufanyia wewe kazi?
Unaufanyia mfumo kazi au mfumo unakufanyia wewe kazi?
Kipato chako ni endelevu au sio endelevu?
Ukipumzika mwaka mzima bila kufanya au kugusa chochote utaendelea kupata kipato hichohicho?

Kama jibu ni hapana basi ni muda muafaka Wa kubadilika na kubadilisha unachokifanya.

……Shtuka na changamkia fursa……

Maswali ya kijinga yakijibiwa vizuri

Haya ndiyo majibu mazuri😁😁👇👇👇👇👇👇👇👇

Q: Umenyoa nywele?

A: *Hapana, nimebadilisha kichwa.*

Q: Hiyo simu umenunua?

A: *Hapana nimeitengeneza mwenyewe.*

Q: Utakula mboga na nini?

A: *Mdomo*

(Simu inaita usiku,then aliyepiga anauliza) Q: Nimekuamsha?

A: *Hapana nilikuwa naota jua hapa nje.*

Q: Gazeti la leo linasemaje?

A: *Sijaongea nalo.*

Q: Gari limejaa, nitakaa wapi?

A: *Usijali dereva anashuka kituo kinachofata utapata kiti.*

Q: Hiyo ni ajali?

A: *Hapana ni driver ameamua kupark gari upside down* .

Q: Umepause movie?

A: *Hapana wamechoka kuact wanarest.*
😂😂😂😂😂😂

🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂

Maswali na majibu kuhusu Mpako wa wagonjwa au Mpako wa Mwisho

Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu gani?
Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu alijua udhaifu wa binadamu hauishi mara anapopokea uzima wa Mungu kwa sakramenti tatu za kuingizwa katika Ukristo. Hivyo alipanga kusaidia mpaka mwisho wa dunia waamini wake watakaopatwa na dhambi na ugonjwa, kama alivyowasaidia wengi aliokutana nao katika maisha yake.
“Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, ‘Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako’… ‘Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi’ – amwambia yule mwenye kupooza – ‘Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako’. Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake. Makutano walipomwona, walishikwa na hofu, wakamtukuza Mungu, aliyewapa watu amri ya namna hii” (Math 9:2,6-8).


Mpako wa Wagonjwa ulianzishwa na nani?
Mpako wa Wagonjwa ulianzishwa na Yesu, kama sakramenti zote. Maandiko yanasimulia huruma yake iliyomfanya awaponye wengi kwa namna mbalimbali na kuwapa Mitume uwezo wa kufanya vilevile kwa “kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina” (Math 10:1). Nao
“wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza” (Mk 6:13).
“Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa, nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa” (Yak 5:14-15).


Mafuta ya mpako wa wagonjwa yanamaanisha nini?
Mafuta ya wagonjwa yanamaanisha lengo la kuwaponya na kuwarudishia nguvu na uzuri.
Kama kawaida, maneno yanaweka wazi zaidi kuwa lengo si kuponya mwili tu, bali hasa roho kwa kuitia msamaha na faraja katika mateso ambayo huenda yakaendelea. Kwa kuwa Mungu haponyi mwili kila mara, isipokuwa kwa faida na wokovu wa mgonjwa na wa wengine. Kama ndiyo mapenzi yake, kila mmoja ajifunze kufaidika vilevile na ugonjwa:
“Makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, ‘Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu’. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu” (2Kor 12:7-9).
“Sasa nayafurahia mateso niliyo nayo kwa ajili yenu, tena nayatimiliza katika mwili wangu yale yaliyopungua ya mateso ya Kristo, kwa ajili ya mwili wake, yaani, kanisa lake” (Kol 1:24).


Sakramenti ya Mpako wa wagonjwa ni nini?
Ni Sakramenti ambayo Padri humuombea neema ya Mungu na kumpaka Mafuta Matakatifu mgonjwa aliye katika hatari ya kifo kwa ajili ya neema ya roho na mwili. (Yak 5:14-15, Mk 6:13)
Sakramenti ya Mpako wa wagonjwa ilianza lini? Je, wakati wa Yesu kulikuwa na sakramenti hii?
Sakramenti ya mpako wa wagonjwa ilikuwepo tangu wakati Yesu akiwa hai. Tunaweza kuiona Kwenye Biblia tunaposoma Yesu alivyowatuma wanafunzi wake waliwapaka watu mafuta. “Waliwatoa pepo wengi Wabaya, wakawapaka wagonjwa wengi mafuta wakawaponya. (Marko 6:13)


Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa inaadhimishwaje?
Inaadhimishwa kwa Padre kumuombea mgonjwa, kumuwekea mikono na kumpaka mafuta katika panda la uso na viganja vya mikono; kwa kutumia mafuta aliyobariki Askofu siku ya Alhamisi kuu.


Sakramenti ya Mpako Wa Wagonjwa inamanufaa gani rohoni mwa mtu?
Manufaa ya Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa ni
1. Nguvu ya kuvumilia mateso na kuyaunganisha na mateso ya Yesu Kristo
2. Maondoleo ya dhambi zote asizoweza kuziungama
3. Nafuu ya mwili, hata uzima ikifaa kwa wokovu wa roho yake
4. Neema ya kujiandaa kuaga dunia na kuingia katika uzima wa milele


Ni nani anayetoa Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa?
Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa hutolewa na kuhani tuu yaani Askofu au Padri


Padri aitwe kwa mgonjwa lini?
Padri aitwe kwa mgonjwa mara inapoonekana Hatari ya Kifo na kamwe isisubiriwe mpaka mgonjwa apoteze fahamu.


Ni nani aweza kupokea Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa?
Ni kila Mkatoliki aliyefikia umri wa kufikiri na aliye katika hatari ya kufa kwa ugonjwa au uzee aweza kupokea Sakramenti hii.


Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa yaweza kupokelewa mara ngapi?
Sakramenti hii yaweza kupokelewa mara nyingi ugonjwa ukizidi au akipatwa na ugonjwa mwingine mkubwa


Alama wazi ya Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa ni nini?
Alama wazi ya Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa ni tendo la kupaka Mafuta Matakatifu wagonjwa na kutamka maneno
“Kwa mpako huu Mtakatifu na kwa pendo lake kuu, Bwana Akujaze na nguvu ya Roho Mtakatifu. Amina Akuondoe katika enzi ya dhambi, akuweke huru. Kwa wema wake akupe nafuu katika mateso yako na kukujalia neema. Amina”


Kama padri hatapatika na mgonjwa afanye nini?
Kama padri hatapatikana mgonjwa aweke nia ya kuungama na afanye majuto kamili


Komunyo pamba ndio nini?
Komunyo pamba ndio Ekaristi inayopokelewa na wale wanaokaribia kuaga maisha ya duniani na wanaojiandaa kuvukia uzima wa milele

Angalia jinsi muda wako unavyopotea

Kila mtu ambaye ni hai amepewa muda Wa masaa 24 kila siku,168 kwa wiki,672 kwa mwezi,8064 kwa miezi 12 au kwa mwaka.

Katika hayo masaa 24 unayoyapata kila siku unayatumiaje katika suala zima la kukufikisha katika ndoto na malengo au mafanikio yako?

Kwa nini kuna matajiri na maskini na wote tunapewa masaa 24???
Tucheki mgawanyo Wa masaa 24 ulivyo….katika masaa 24 unayopewa kwa siku masaa 8 ni ya kazi,masaa 8 ni ya kulala na masaa 8 ni ya kufanya mambo yako mengine.

Tuseme katika Masaa 8 kwa ajili ya mambo yako mengine labda masaa manne yanapotea katika foleni au purukushani za maisha kama kula nk.
Je haya mengine manne yanaenda wapi?Tunayapotezea wapi?
Kwenye mpira?kwenye movie?kwenye TV?kwenye mitandao ya kijamii?kukaa na kuwajadili wengine na mashosti?

Hivi unajua kwa siku una wastani Wa kupoteza masaa manne kwenye masaa yako 24??
Kwa wiki unapoteza masaa 28 hali kadhalika masaa 112 kwa mwezi hupotea.
Kwa mwaka mmoja wenye masaa 8760 una wastani Wa kupoteza masaa 1344 ambayo ni sawa na siku 56 kwa mwaka kwa makadirio ya haraka haraka.

Kwa maana nyingine kwa kutumia hii “concept” kila miezi 12 ya mwaka mzima unapoteza miezi miwili kwa mambo ambayo sio “productive”.
Hii ni sawasawa na kupoteza mwaka mmoja ndani ya miaka 6…kwa maana nyingine kwa “the same concept” ya masaa 4 kwa siku kupotea ni kwamba unapoteza mwaka mmoja kwa mambo ambayo hayakusaidii chochote.

Hebu jiulize hapo ulipo una umri gani?umeshapoteza miaka mingapi kwa mambo ambayo sio productive??
Kama wewe ni mfanyakazi au muajiriwa ukifanya kazi kwa muda Wa miaka 40 au kwa muda Wa miaka 40 unapoteza miaka 6.6.

Je hebu jiulize muda wote huo unaoupoteza kwenye mambo ambayo sio “productive” ungekuwa ni muda ulioutumia vizuri kwa mambo ya uzalishaji mfano kuanza kidogo kidogo kujenga biashara yako sasaivi tungekuwa na mamilionea na mabilionea wangapi?
Ili uweze kujenga biashara ambayo ni “strong” inakuhitaji angalau uijenge kwa muda Wa miaka mitano kwa maana nyingine kwa kutumia masaa manne tu kwa siku ndani ya miaka 40 utakuta tayari wewe ni milionea na baada ya kustaafu ajira usingeanza kuangaishana na pensheni (kwanza ni shilingi ngapi) au kuanza kubembeleza kuomba uongezewe mkataba au kwenda kufanya tena part time employment…..kwa concept hiyo ni mamilionea wangapi tumewapoteza??

Ndio maana katika hii dunia yetu tunayoishi matajiri wote ni 3% na 97% ya watu waliobakia wanawafanyia kazi matajiri.
Matajiri waliweza kuiona hii concept kwa jicho la Tatu na wakaanza kuifanyia kazi and the rest is history.
Huwezi kumkuta tajiri anapoteza muda wake kwa mambo ya kizembe yasiyomuingizia chochote ndio maana matajiri wanazidi kuwa matajiri na maskini wanaendelea kuwa maskini.

Lakini bado muda na nafasi unayo sasa ukiamua na ukianza kuutumia muda wako ulio nao kwa ajili ya kuyatengeneza maisha yako.
Watu wengi hawako tayari kuumia na kujifunza biashara na kuielewa ndani ya miaka mitano itakayowapelekea kuwa matajiri na kuweza kuyafikia malengo na ndoto zao lakini wapo tayari kuajiriwa na kufa maskini ndani ya miaka 40.

Muda mzuri ndio sasa Wa kufanya maamuzi sahihi Wa kuyawekeza masaa manne kwenye biashara ili uje upate matokeo chanya.

Namna ya kuondokana na tatizo la kunuka Kikwapa

Harafu ya jasho inakera, kibaya zaidi ni kuwa wewe mwenyewe husikii harufu hiyo ila wale walio karibu yako. Kwa upande mwingine kujaribu kuzuia kutoka jasho ni hatari kwa afya yako na kujaribu kuondoa harufu kwa kutumia pafyumu husababisha madhara mengine ya kiafya na kwa bahati mbaya perfume zina jaribu poteza harufu kwa mda mfupi tu na sio kutokomeza tatizo hilo.

Dawa rahisi ya kuondoa harufu kwenye kwapa o ni kutunza mwili wako ikiwa ni pamoja kuoga mara kwa mara hata ikibidi mara tatu kwa siku kwa kuanzia, kwani harufu mbaya ya kwapa inatokana na kuwepo kwa bakteria katika kwapa hasa kukiwa na unyevu au maji maji kwapani.

Ili kukomesha tatizo hili ni lazima kuoga mara nyingi pia wakati unaoga mkazo utiliwe kwenye kwapa tumia dodoki na sabauni unaposafisha kwapa lako, pili ni lazima ukaushe kwapa barabara ili kuondoa unyevu ambao unakaribisha bakteria ambao wanajaribu kuvunja vunja jasho lako na ndiyo maana linatoa harufu kali.

Vile unashauriwa mara baada ya kuoga tumia potassium alum au sulphur.

Vile vile jitahidi kuepuka nguo za polista (polyster) vaa nguo za pamba 100%

Punguza kula vyakula vyenye viungo vikali kama vitunguu swaumu nk.

BADILIKA : huu ni mwaka mpya

**Badilika huu mwaka. Kipenga kimeshapulizwa wenye mbio zao wameshatoka, wewe bado uko kitandani unaandika happy new year kwenye mitandao ya kijamii
Kipenga kimeshapulizwa wewe maliza bajet yote leo kwenye starehe alafu uanze kulalamika eti Mwezi wa kwanza Mgumu utadhani umeubonyeza

Kipenga kimeshapulizwa wenzako wanaenda na kasi ya Magufuli, wewe bado unapiga vibomu alafu unalalamika uchumi mbovu

Kipenga kimeshapulizwa wenzako wanaenda porini kutafuta pesa na kuja kuzitumia mjini wanaenzi ule msemo wa Mali utaipata shambani /porini wewe unatafuta pesa kati kati ya mji, my friend utapata nauli tu

Kipenga kimeshapulizwa wanasiasa wenzako wanaleta matokeo chanya kwenye jamii, wewe umekwama na siasa zako za Maigizo, utaisoma namba vizuri

Kipenga kimeshapulizwa wenzako wanatengeneza ajira na kulipa mishahara, wewe umeajiriwa mwaka wa 10 unasubiri bonus, increment na kubagain ongezeko la mshahara alafu bado unataka kuwa celebrity, my friend labda celebrity wa mikopo

Kipenga kimeshapulizwa wenzako wanatafuta matatizo ili yawe fursa kwao, wewe ukiona changamoto unakimbia na kuilalamikia serikali, utasubiri sana

Kipenga kimeshapulizwa wenzako wanatafuta kazi kwa kufanya kazi za kujitolea kujenga nchi, wewe unasubiri interview, hiyo experience utaipata ndotoni

Kipenga kimeshapulizwa wakati wenzako wanahojiwa na forbes magazine wamewezaje kuleta impact Africa nzima, we unakazana kujisifu unafollowers wengi instagram alafu Huna hata mmoja ambae ni rafiki wa kusaidiana.

Kipenga kimeshapulizwa wakati wenzako wakipost kwenye mitandao yao ya kijamii wanalipwa, wewe kazi yako ni kuretweet/kurepost na kulike siku nzima bila kupata faida yoyote

Kipenga kimeshapulizwa wenzako wanaoipenda nchi yao wanachangia matembezi ya tembo na faru yatakayofanyika Morogoro kwa kununua tshirt, wewe bado unazungusha bia na nyama choma alafu unalalamika watalii wamepungua, unataka waje wakuangalie wewe?

BADILIKA my friend.
😹😹😹😹😹

Mchemsho wa samaki na viazi

Mahitaji

Samaki mbichi (1)
Viazi mbatata (3)
Nyanya (1)
Kitunguu maji
Limao
Kitunguu saumu
Tangawizi
Chumvi
Pilipili
Vegetable oil

Matayarisho

Safisha samaki kisha mmarinate na tangawizi, kitunguu swaum, chumvi na limao kwa muda wa masaa mawili. Baada ya hapo menya viazi na uvikate vipande vidogo kisha vioshe na viweke kwenye sufuria yenye maji kiasi kwa ajili ya kuvichemsha. Viinjike jikoni na uviache vichemke kwa dakika 7. Vikisha chemka tia samaki, katia kitunguu,pilipili, chumvi, limao, vegetable oil na nyanya na uache supu ichemke mpaka samaki na viazi vitakapoiva. baada ya hapo supu itakuwa tayari kwa kuliwa.

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini Ya Pilipili Mbichi

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama

Nyama ya ng’ombe vipande vidogo – 2lb

Nyanya – 1

Kitunguu Kilichoktwa katwa – 1

Mafuta – 2 vijiko vya supu

Paprika (bizari ya masala ya rangi) – ½ kijiko cha chai

Kidonge cha supu – 1

Chumvi – Kiasi

Ndimu – Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha nyama kwa chungio ili itoke maji. Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwerangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.
Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.

Vipimo Vya Mboga

Mchicha ulio katwa katwa 400 gm

Nyanya 1

Kitunguu kilicho katwa 1

Nazi ya unga kiasi

Pilipili mbichi 2

Mafuta ½ kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha na Kupika

Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.
Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.
Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji
Tia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa
tayari kuliwa

Vipimo Vya Maharage

Maharage – 1 kopo

Kitunguu – 1

Nazi – 1 mug

Nyanya (itowe maganda) – 1 kiasi

Pilipili mbichi – 2

Mafuta – 1 kijiko cha supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.
kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.
Tia chumvi, maharage na nazi uwachie
moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.

Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi

Pilipili mbichi – 4/5

Kotmiri – 1 Kijiko cha supu

Ndimu – kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 1 chembe

Mafuta ya zaituni – 2 vijiko Vya supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha

Kwenye blender, tia vipimo vyote na sage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Vipimo Vya ugali

Maji – 4 Vikombe kiasi inategemea na unga

Unga wa sembe – 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.

Faida 10 za kulala mapema kiafya

Mapera ni matunda yanayo patikana kwa wingi lakini mara nyingi huwa hayapendelewi sana kutokana na ugumu wake wakati wa kuyatafuna pamoja na kuwa na mbegu mbegu nyingi. Hata hivyo matunda haya yana faida kubwa sana kwa afya ya mwili wa mwanadamu.

Zifuatazo ni faida kumi za mapera:

1. Utajiri wa Vitamin C.

Mapera yana utajiri mkubwa wa Vitamin C ambayo ni muhimu sana katika mwili wa mwanadamu.

2. Ni kinga nzuri ya kisukari.

Ulaji wa watu wengi unawaweka katika hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari lakini matumizi ya mapera yatakupunguzia hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari Hii ni kwa sababu mapera yana utajiri mkubwa sana wa Fibre.

Fibre ni muhimu sana katika kupunguza kiasi cha sukari kwenye damu. Vilevile ni muhimu sana katika kuusafisha mfumo wa usahihi.

3. Kuimarisha Uwezo Wa Kuona

Mapera yana utajiri mkubwa sana wa Vitamin A au Retinol ambayo ni muhimu sana katika kusaidia kuona vizuri. Hivyo basi kama ilivyo kwa karoti, mapera yanasaidia sana katika kuongeza na kuimarisha uwezo w a mtu kuona.

4. Kusaidia katika Uzazi

Mapera yana madini yaitwayo Folate ambayo husaidia katika kurutubisha mayai ya uzazi.

5. Kurekebisha Kiwango Cha Shinikizo La Damu

Madini ya Potassium yaliyomo ndani ya mapera yanasaidia katika ku-normalise shinikizo la damu ( Blood Pressure )
Ndizi na mapera vina kiwango cha potassium sawa.

6. Utajiri mkubwa wa Madini Ya Shaba

Mapera yana madini ya shaba ( Trace element copper ) ambayo ni mazuri sana katika ku- maintain ufanyaji kazi wa tezi ziitwazo thyroid.
Tezi za thyroid zisipo fanya kazi vizuri zinaweza kusababisha matatizo mengi ya kiafya kwa mwanadamu.

7. Utajiri wa Madini Ya Manganese

Mapera yana utajiri mkubwa wa madini ya manganese ambayo yanausaidia mwili katika kunyonya ama kupata virutubisho muhimu kutoka kwenye vyakula tunavyo kula.

Chakula tunacho tumia kikitumika vizuri mwilini, tunapata virutubisho vyote muhimu kama vile biotini, vitamin nakadhalika.

8. Kuusadia mwili na akili katika ku-relax.

Mapeara yana utajiri mkubwa wa madini ya magnesium ambayo hufanya kazi ya kuvifanya akili na mwili wa mwanadamu viweze ku relax. Unashauriwa kutumia mapera baada ya kazi nzito. Hii itasaidia katika kuufanya mwili na akili yako kutumika.

9. Mapera ni muhimu katika afya ya akili ya mwanadamu.

Vitamin B3, Vitamin B6 ambazo zinapatikana ndani ya tunda la mpera muhimu katika kuimarisha afya ya akili ya mwanadamu. Mapera yatasaidia kuufanya ubongo wako u relax.

10. Ni muhimu sana katika ngozi ya mwanadamu

Vitamin C, viondoa sumu na karotini ambavyo vyote vinapatikana ndani ya tunda la mpera ni muhimu sana katika kuimarisha afya ya ngozi.

Kama hiyo haitoshi, kokwa la mpera huwa linatumika katika kutengeneza vipodozi na losheni kwa ajili ya matumizi ya mwanadamu.

JE UNAFAHAMU NINI KUHUSU KUJAMBA?

Kwanini tunajamba? kwanini “ushuzi” unanuka?
Kujamba inaweza kuwa kitendo cha aibu kwa wengi wetu,lakini
inaweza kukufanya ujisikie vizuri kujua kwamba ni tendo
la kawaida sana kwa mwili wa binadamu kutenda.Kila
mtu anajamba,hata Halle Berry nae hujamba.

1.Kujamba ni nini hasa?
Kujamba kunasababishwa na kubanwa kwa hewa,ambayo
inaweza kutoka mwilini kwa njia nyingi.Baadhi ni hewa
tuliyoimeza wakati wa kula au kunywa.Hewa ingine
husababishwa na gesi kuingia kwenye utumbo wetu
kutoka kwenye damu,na baadhi ya gesi huzalishwa na
kemikali katika utumbo au bakteria.Kwa kawaida
“ushuzi” unakua na asilimia 59 ya gesi ya
nitrogen,asilimia 21 ni hydrogen,asilimia 9 ni carbon
dioxide,asilimia 7 methane na asilimia 4 ni oygen.
Asilimia moja tu ya “ushuzi” inaweza kuwa hydrogen
sulfide na mercaptans,ambayo ndio ina sulfur ndani
yake,sulfur ndo hufanya “ushuzi” utoe harufu mbaya
Kujamba huambatana na sauti,hii ni kutokana na
“vibration” katika njia ya haja kubwa.Ukubwa wa mlio wa
kujamba hutegemea “presha” inayosukuma gesi itoke nje
na pia ugumu wa misuli ya njia ya haja kubwa.

2.Kwa nini Ushuzi hutoa Harufu mbaya?
Harufu mbaya ya ushuzi hutegemea na ulaji wa
mtu,vyakula vyenye sulfur kwa wingi ndio husababisha
hili.Vyakula vyenye sulfur kwa wingi ni kama
maharage,kabichi,soda na mayai.

3.Watu hujamba hadi mara 14 kwa siku
Mtu wa kawaida hutoa hata nusu lita ya ushuzi kwa
siku.Inasemekana mtu akijamba mfululizo kwa kipindi
cha miaka 6,anaweza kuzalisha nishati ya kutosha
kutengeneza bomu la atomiki.

4.Ushuzi husafiri kwa mwendo wa futi 10 kwa sekunde.
Harufu ya ushuzi huanza kusikika sekunde 10-15 baada
ya mtu kujamba,hiyo ni kwa sababu inachukua muda
mrefu kwa harufu kufikia pua.

5.Kujizuia Kujamba Inaweza Kuhatarisha Afya Yako
Madaktari hawajakubaliana moja kwa moja kama kujizuia
kujamba ni hatari kiafya.Baadhi ya wataalam wanafikiri
kujamba ni sehemu muhimu katika mfumo wa
mmeng’enyo wa chakula,hivyo kujizuia kujamba
haitakuletea madhara.Wengine wanadhani kwamba
kujizuia kujamba kunaweza kusababisha tumbo kujaa
gesi,na pia inaweza sababisha bawasili (hemorrhoids).

6.Kwa Baadhi ya Tamaduni,Kujamba Sio Ishu
Wakati tamaduni nyingi zikichukulia tendo la kujamba
lifanywe kistaarabu,kuna baadhi ya tamaduni hawaoni
haya kujamba hadharani,na pia hufurahia tendo
hilo.Mfano kabila la Yanomami huko America ya
Kusini,kwao husalimiana kwa kujamba,na China
unaweza kupata kazi ya kunusa ushuzi! Katika Roma ya
zamani,Mfalme Claudius akihofia kwamba kujizuia
kujamba inaweza kuwa hatari kiafya,alipitisha sheria
kwamba ni ruhusa kujamba kwenye “banquets”.

7.Ushuzi Unawasha Moto
Kama ilivyoandikwa hapo juu,methane na hydrogen
inayozalishwa na ushuzi inaweza sababisha moto.

8.Mchwa Hujamba Kuliko Wanyama Aina Zote
Ni ngumu kuamini kuwa mchwa ndo anawajibika na
matatizo yetu ya “Global Warming”.Mchwa huongoza kwa
kujamba kwa wanyama,na hiyo huzalisha gesi ya
methane.

9.Ukiubana Ushuzi,Utakutoka Usingizini
Hata ujitahidi kuubana vipi,ushuzi utatoka mara
utapokua umepumzika,hasa ukiwa umelala.

10. Watu Hujamba Hata Baada ya Mauti Kuwafika
Maiti huendelea kutoa gesi hadi masaa matatu baada ya
mtu kufariki dunia,hii huambatana na milio ya
kujamba.Hali hii husababishwa na misuli kusinyaa.

UKIPATA NAFASI JAMBA MWANANGU

Sababu, dalili na jinsi ya kujikinga na tatizo la kiungulia kwa wanawake wajawazito

Hii ni hali inayowakumba mama wajawazito walio wengi. Inaweza kutokea kipindi chochote cha ujauzito ila mara nyingi hutokea katika umri wa mimba kuanzia miezi mitatu.

Kiungulia ni nini?

Kiungulia ni maumivu mithili ya moto yanayotokea kifuani sehemu ya katikat ya kifua. Maumivu haya hayana uhusiano na moyo.Yanatokea pale asidi ya kwenye tumbo inapopanda na kurudi kwenye koo la chakula.

Asidi hii ikiwa tumboni haisababishi madhara wala maumivu kwani inazalishwa muda wote na kuta za tumbo kumeng’enya chakula. Seli za kuta za tumbo haziathiriki na asidi hii ndio maana inapokuwa tumboni haileti shida yoyote.
Ila seli za kuta za koo la chakula haziwez kustahimili asidi hii ndiyo maana inapopanda kwenye koo la chakula unapata maumivu ya kiungulia.

Dalili ya kiungulia

Kiungulia mara nyingi hutokea wakati unakula au baada ya kula na kinaweza kuzidi makali wakati umelala.

Dalili ni kama, Kuhisi maumivu kama ya kuungua kwenye kifua au chembe moyopamoja na kujisikia radha ya uchachu mdomoni.

Saabu za kiungulia kwa wajawazito.

Sehemu mbali mbali za mwili hupata mabadiliko wakati wa ujauzito. Wakati wa ujauzito mwili hutengeneza kwa wingi hormone ya progesterone na relaxin ambazo huathiri mfumo wa chakula.

Progesterone hormone hii hufanya chakula kutembea na kufyonzwa kwa taratibu sana.
Relaxin hormone hufanya misuli laini ya mwili kulegea ikiwemo misuli inayobana sehemu ya juu ya tumbo (sphincter) inayozuia chakula au vitu vya tumboni visirudi kwenye koo la chakula .
Mabadiliko haya hufanya kuwa rahisi asidi na chakula vilivyomo tumboni kurudi kwenye koo la chakula na kusababisha kiungulia.

Vitu vingine vinavyoweza kusababisha kiungulia kwa mama mjauzito ni;

  1. Kula chakula kingi sana
  2. Vyakula vyenye viungo
  3. Vyakula vyenye mafuta mengi
  4. Matunda jamii ya limao na machungwa
  5. Chocolate
  6. Soda
  7. Kahawa
  8. Sigara
  9. Pombe
  10. Baadhi ya madawa
  11. Stress
  12. Uzito uliopitiliza.

Jinsi ya kujikinga na kiungulia kwa wajawazito.

  1. Kuwa na uzito unaowiana na urefu wako
  2. Epuka vyakula vinavyosababisha kiungulia kama nilivyoainisha hapo juu
  3. Epuka kula chakula kingi kwa wakati mmoja. Bali kula chakula kidogo kila baada ya muda.
  4. Kunywa maji ya kutosha. Angalau lita moja na zaidi kwa siku
  5. Epuka kuvaa nguo zinazobana sana tumbo na kiuno
  6. Usilale muda mfupi baada ya kula.
  7. Epuka kuwa na msongo wa mawazo /stress
  8. Onana na Daktari kupata ushauri wa dawa za kupunguza makali ya asidi hii ambazo ni salama kwa wajawazito

Bisikuti Za Kokoa (Cocoa Biscuits)

Viambaupishi

Siagi 100gm

Unga wa kaukau (cocoa powder) 2 Vijiko vya supu

Maziwa mazito (condensed milk) Moja kikopo (397gm)

Bisikuti za Mary 2 Pakiti

Njugu ½ Kikombe

Karatasi la plastiki

Jinsi ya kuandaa na kupika

1. Vunjavunja bisikuti zote packet mbili ziwe vipande vidogo vidogo.

2. Pasha moto siagi mpaka ipate.

3. Tia kwenya siagi imoto maziwa mazito na cocoa koroga vizuri.

4. Kisha tia kwenye mchanganyiko bisikuti zilizovunjwa na njugu na uchanganye kisha epua motoni.

5. Paka karatasi la plastiki mafuta kidogo halafu tia mchanganyiko kisha kunja (roll).

6. Tia kwenye freeza muda wa saa.

7. Halafu toa karatasi na ukate kate na panga kwenye sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Mapishi ya Boga La Nazi

Vipimo

Boga la kiasi – nusu yake

Tui zito la nazi 1 ½ gilasi

Sukari ½ kikombe

Hiliki ½ kijiko cha chai

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Menya boga kisha katakata vipande vya kiasi.
Weka katika sufuri tia maji kiasi ya kuchemshia na kuwiva bila ya kubakia maji mengi.
Changanya tui na sukari na hiliki kisha mimina juu ya boga wacha katika moto dakika chache tu bila ya kufunika.
Epua mimina katika chombo likiwa tayari.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About